JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI
01 KISWAHILI
Muda: Saa 1:40 Mwaka: 2021
Maelekezo
l . Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali arobaini na tano (45).
2. Jibu maswali yote katika kila sehemu.
3. Soma maelekezo yote yaliyoko katika fomu maalum ya kujibia (OMR).
4. Jaza taarifa zote katika fomu ya OMR.
5. Andika Namba yako ya Mtihani kisha weka kivuli kwenye tarakimu za namba hiyo mahali panapohusika kwenye karatasi yako ya kujibia.
6. Weka kivuli kwenye herufi ya jibu lililo sahihi kwa swali 1 — 40. Kwa mfano, kama jibu sahihi ni A weka kivuli kama ifuatavyo:
7. Ukigundua kuwa herufi uliyowekea kivuli si jibu sahihi futa kivuli hicho kwa umakini kwa kutumia kifutio safi kabla ya kuweka kivuli katika herufi mpya.
8. Tumia penseli ya HB tu katika kujibu swali la 1— 40; na kalamu ya Wino wa bluu au mweusi kwa swali la 41 hadi 45.
9. Simu za mkononi na Vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi ndani ya chumba cha mtihani.
SEHEMU A (Alama 35)
Sikiliza kwa makini hadithi utakayosomewa na msimamizi, kisha jibu swali la 1 - 5, kwa kuweka katika herufi ya jibu lililo sahihi katika fomu yako ya kujibia.
Bofya Hapa Kusikiliza Hadithi
Maswali
1. Malkia wa nyuki alikuwa analindwa na nani?
2. Ni kitu gani ambacho malkia wa nyuki hakukipenda?
3. Nani alijishughulisha kutafuta nekta kwenye maua?
4. Utajiri katika kijiji cha nyuki ulitokana na nini?
5. Nani walitumika kupeleka habari mbalimbali katika vijiji vya jirani?
Katika swali la 6 - 35, weka kivuli katika herufi ya jibu lililo sahihi katika fomu yako ya kujibia.
6. Wanakijiji walifanya juu Chini ili kuleta maendeleo katika kijiji Chao. Nahau "fanya juu chini" inafafanuliwa na kifungu kipi cha maneno kati ya vifuatavyo?
7. Nahau ipi yenye maana ya "kunywa pombe?"
8. Katika sentensi "Dada alimwambia kuwa atakapopata muda atakuja nyumbani ," mzungumzaji ametumia nafsi gani kati ya hizi?
6. "Sisi ni wanafunzi hodari wa somo la kiswahili". Kauli hiyo inawakilisha nafsi ipi kati ya hizi zifuatazo?
10. Daktati alisema kwamba mgojwa wetu amepata ahueni" Hiyo ni aina gani ya kauli kati ya zifuatazo?
11. Masumbuko aliwaambia kuwa, hataingia darasani tena. Kauli halisi ya sentesi hii ni ipi kati ya zifuatazo??
12. "Nyamante alikata shauri na kuwaambia wenzake, kweli elimu ndiyo mkombozi wa mtoto wa kike." Nahau "kata shauri" katika sentensi hii ina maana ipi kati ya zifuatazo?
13. Chekacheka anapenda watoto wake wawe na tabia njema hadi ukubwani. Methali ipi kati ya zifuatazo inahimiza tabia ya aina hiyo?
14. "Nikitembea walio wafu huamka na walio hai hukaa kimya." Jibu la kitendawili hiki ni lipi kati ya yafuatayo?
15, Ni methali ipi kati ya zifuatazo inamaana sawa na methali "akufaaye kwa dhiki ndio rafiki"?
16. Neno lipi kati ya yafuatayo ni jumuishi kwa maneno haya "nyanya, vitunguu, pilipili na tangawizi'?"
17. Mwaka 1985 Mwalimu Julius Kambaragc Nyerere aliamua kung'atuka madarakaní na kumwachia Mheshimiwa, Ali Hassan Mwinyi, Kitcndo cha Mwalimu Julias Kambarage Nyerere kung'atuka kinamaanisha nini?
18. Neno lipi kati ya yafuatayo ni jumuishi kwa maneno haya "almasí, dhahabu, Tanzanaiti na lulu" ?
19. Katika neno "ninakula" kiambishi cha wakati uliopo ni kipi kati ya vifuatavyo?
20. "Muda ulipowadia wanafunzi wote tulisimama foleni.' Neno "wadia" linashabihiana na neno lipi kati ya yafuatayo?
21. Katika sentensi "Wimbo wa Taifa umeimbwa kwa ustadi." Neno lipi kati ya yafuatayo limesimama kama kitenzi?
22. Neno lipi halilandani na mengine kati ya maneno yafuatayo?
23. "Mtoto mzuri anajua kupangilia ratiba." Katika sentensi hii, neno lipi kati ya yafuatayo limetumika kama kivumishi?
24. "Hawa ndio wapole darasani mwetu." Katika sentensi hii, neno lipi kati ya yafuatayo limetumika kama kiwakilishi?
25 Ni neno lipi kati ya yafuatayo linakamilisha sentensi hii kwa usahihi? "Nikisoma kwa bidii . . . . . . . mtihani wangu."
26. "Nitakula uji wangu kesho asubuhi." Sentensi hii imekosewa. Sentensi sahihi ni ipi kati ya zifuatazo?
27. "Kijiji Chetu kina maendeleo duni lakini mwaka ujao itakua kinyume chake." Je, mwaka ujao kijiji Chetu kitakuwa na maendeleo gani?
28. Maneno yapi kati ya yafuatayo yapo katika mpangilio sahihi kwa kuzingatia matumizi ya kamusi?
29. Kitenzi kipi kati ya vifuatavyo kinatokana na nomino "mchemsho?"
30. Ni nomino ipi inaundwa kutokana na neno "chunga'?"
31. "Polepole ndio mwendo." Methali hii inahusiana na methali ipi kati ya hizi zifuatazo?
32. Charubuma alionywa na wazazi wake kuacha tabia ya wizi, lakini hakuwasikiliza hatimaye alifungwa jela. Methali gani kati ya zifuatazo inakemea tabia hiyo isiyofaa katika jamii'?
33. ”Hakuna msiba . . . . . . . . . . . . . . ". Kifungu kipi cha maneno kati ya vifuatavyo kinakamilisha methali hii?
34. Kirefu cha neno BAKITA ni kipi kati ya maneno yafuatayo?
35. Katika uandishi wa kumbukumbu za mkutano saini ya mwenyekiti hukaa sehemu gani?
11. Mahali panapochimbwa madini ya chumvi. makaa ya mawe, dhahabu na almasi panaitwaje?
12. Neno lipi kati ya yafuatayo ni kinyume cha neno 'kinai" ?
13. Neno lipi linakosekana katika sentensi ifuatayo? "Humo . . . . . . . . . . . alimopita mbunge wakati wa kuomba kura".
14. Abdi . . . . . . . . . . mtoto wa jirani yangu. Neno linalokamilisha sentensi hii ni lipi?
15. Hawa . . . . . . . . . . walioalikwa katika sherehe hii. Neno lipi linakamilisha sentensi hii kwa usahihi?
16. "Baba atam kanya mjomba ili aache ulevi.” Sentensi hii ipo katika wakati gani?
17. 'Sitakubafi kuonewa”. Neno "sitakubali” liko katika hali gani?
18. Mti unakatwa na Ali. Neno "unakakatwa" liko katika kauli ipi?
19. "Mtoto alinunuliwa zawadi."Kitenzi 'alinunuliwa” kipo katika kauli gani?
20. "Ndizi yake imeliwa na Ngedere” . Wingi wa sentensi hii ni upi?
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI
01 KISWAHILI
Muda: Saa 1:30 Mwaka: 2020
Maelekezo
l. Karatasi hii ina sehemu A, B, C, D na E zenye maswali arobaini na tano (45).
2. Jibu maswali yote katika kila sehemu.
3. Soma maelekezo yote yaliyoko katika fomu maalum ya kujibia (OMR).
4. Jaza taarifa zote katika fomu ya OMR na katika ukurasa wenye swali Ia 41 hadi 45 kwenye karatasi ya maswali.
5. Andika Namba yako ya Mtihani kisha weka kivuli kwenye tarakimu za namba hiyo mahali panapohusika kwenye karatasi yako ya kujibia.
6. Weka kivuli kwenye herufi yajibu lililo sahihi kwa swali I - 40. Kwa mfano, kamajibu sahihi ni A weka kivuli kama ifuatavyo:
7. Ukigundua kuwa herufi uliyowekea kivuli si jibu sahihi futa kivuli hicho kwa umakini kwa kutumia kifutio safi kabla ya kuweka kivuli katika herufi mpya.
8. Tumia penseli ya HB tu katika kujibu swali Ia 1 — 40; na kalamu ya wino wa bluu au mweusi kwa swali Ia 41 hadi 45.
9. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi ndani ya chumba cha mtihani.
SEHEMU A (Alama 20)
SARUFI
Katika swali la 1 - 20, weka kivuli katika herufi ya jibu lililo sahihi katika fomu yako ya kujibia.
l . "Amevaa kichina mimi nimevaa kihindi." Maneno "Kichina na Kihindi" ni aina gani za maneno?
2. "Wewe ni mtoto mzuri sana." Neno lililotumika kama kiwakilishi ni lipi?
3. "Walimu wanafundisha lakini wanafunzi hawajisomei." Neno "lakini" ni aina gani ya neno?
4. "Amenunua bidhaa kadhaa na kuzipeleka nyumbani."Neno 'kadhaa" ni aina gani ya neno?
5. "Madaktari walifanya kila njia ili kunusuru maisha yake." Neno "ili" ni aina gani ya neno?
6. "Watoto wawili waliimba wimbo vizuri sana." Neno "wawili" ni aina gani ya neno?
7. Neno lipi halihusiani na maneno mengine kati ya haya yafuatayo?
8. Kuku, bata, mwewe. kunguru na kanga kwa neno moja wanaitwaje?
9. Neno lipi halilandani na mengine kati ya yafuatayo?
10. Mtu hodari asiyeogopa huitwaje?
SEHEMU B (Alama 10)
LUGHA YA K?FASIHI
Katika swali la 21 - 30, weka kivuli katika herufi ya jibu lililo sahihi katika fomu yako ya kujibia.
21 . Kamilisha methali hii, "Udongo upate . . . . . . . . . . . ."
22. . . . . . . . . . . . . . ila siku ya idi.” Kifingu kipi cha maneno kinakamilisha methali hii?
23. 'Mia nawe hafi nawe ila mzaliwa nawe.” Methali hii inahusiana na ipi kati ya zifuatazo?
24. Hana adabu wala staha kwa watu.” Jibu la kitendawili hiki ni lipi?
25. 'Mwavuli 'tva nyikani haukingi mvua." Jibu la kitendawili hiki ni lipi?
26. "Akibeba watoto wake hawezi kuwashusha." Jibu la kitendawili hiki ni lipi?
27. "Babu huanika sembe usiku,asubuhi huiondoa."Jibu la kitendawili hiki ni lipi?
28. "Unga mkono." Maana ya nahau hii ni ipi?
29. Ni nahau ipi kati ya zifuatazo inadhihirisha hali ya kumsema mtu kwa mafumbo ili asitambue?
30. 'Nikipata wasaa nitajitahidi kukutupia jicho."Usemi "kukutupia jicho" una maana gani?
SEHEMU C ( Alama 06)
USHAIRI
Soma kwa makini shairi lifuatalo kisha jibu swali la 31 - 36 kwa kuweka kivuli katika herufi ya jibu lililo sahihi katika fomu yako ya kujibia.
Kuwaza na kuwazua, matukio mbalimbali,
Ndivyo akili yakua, pungufu kuwa kamili,
Asojua akajua, kwa lile ama kwa hili,
Lau ukipuuzia, katu hutofika mbali.
Kusoma na kuchambua, vitabu na mafaili,
Mambo ukapambanua, ya uwongo na ukweli,
Hapo hatokusumbua, kila aliye jahili,
Lau ukipuuzia, katu hutofika mbali.
Kupanga na kupangua, mikakati ya halali,
Utaweza kubagua, lilo jema na batili,
Jema utalichukua, baya utaweka mbali,
Lau ukipuuzia, katu hutofika mbali.
31. Kichwa kinachofaa kwa shairi hili ni kipi?
32. Vina vya kati na vya mwisho katika mistari ya ubeti wa tatu ni vipi?
33. Jumla ya silabi kumi na sita katika kila mstari wa shairi huitwaje?
34. Shairi hili lina mizani ngapi?
35. Kituo kilichotumika katika shairi hili ni kipi?
36. Neno "jahili" kama lilivyotumika katika ubeti wa pili lina maana gani?
1. Neno lipi kati ya haya lina maaana sawa na shari?
2. Shida alivaa nguo za kijeshi wakati wa mkutano.Neno "za kijeshi" ni aina gani ya neno?
3. Hicho ulichopata sikupata lakini nimepata hiki" katika sentensi hii, maneno "hicho na hiki"ni aina gani ya maneno?
4. Ni sentensi ipi iliyo sahihi kimuundo kati ya zifuatazo?
5. Maana ya neno "faraghani" ni ipi kati ya hizi?
6. Wingi wa sentensi "Mbuzi wamepotea" ni upi?
7. "Wanafunzi kenda walikwenda ziara nchini Kenya".neno wa ni aina gani ya neno?
8. Ashura anacheza mpira wa miguu vizuri.katika sentensi hii,neno lipi limetumika kama kielezi?
9. Mtu anayetafsiri ana kwa ana katika lugha moja kwenda lungha huitwaje?
10. "Sote tunafanya mtihani darasani". "darasani" limetumika kama aina gani ya neno?
I l. Baraka aliona --------- kuwa miongoni mwa waliofaulu. Ni neno i:zn linakamilisha sentensi hii kwa usahihi ya maneno yafuatayo?
12. Mwanamke yule alikaa baada ya kufiwa na mume wake. Ni neno lipi linakamilisha sentensi hii kati ya maneno yafuatayo?
13. Kitenzi "piga"kikiwa katika kauli ya kutendeka kitakuwa neno lipi kati ya maneno yafuatayo?
A Pigia
B Pigwa
C Pigika
D Pigiwa
E Pigana.
14. Wewe unasoma kwa bidii"wingi wa sentensi hii ni upi?
15."Wanafunzi wale ni hodari sana" neno "wale" ni aina gani ya neno?
16. "Wasichana saba wamechaguliwa kujiunga na kozi ya uhandisi." Neno na ni aina gani ya neno?
17. Ni neno lipi lina maana sawa na neno kumzonga mtu kwa maneno makali kwa lengo la kumkasirisha?
18. Katika vitenzi "sitafyeka" na "hupendi" ni silabi zipi zinazoonesha ukanushi?
19. Neno lipi kati ya haya halilandani na mengine?
20. Mnyama huyu anafanana na ngombe. Wingi wa sentensi hii ni ipi?
21. Ni methali ipi kati ya zifuatazo inahimiza ushirikiano katika jamii?
22. "Watoto wa mfalme ni rahisi kujificha" Jibu la kitendawili hiki ni kipi?
23. "Uzururaji umepigwa marufuku".Nahau umepigwa marufuku ina maaña gani?
24. "Amenisahau kwa moyo mweupe" Nahau"moyo mweupe" ina maana ipi"?
25. "Mwenye nguvu Neno linakamilisha methali hii?
26. "Asiyefunzwa na mamaye hufunzwa ulimwengu." Ni methali ipi inafanana na methali hii?
27. "Haba na haba hujaza kibaba" Methali hii inatoa funzo gani?
28. "Heri kufa macho kuliko "Methali hii UKAMILISHWA na kifungu kipi cha maneno?
29. "Maji yakimwagika hayazoolekl hii ina maana gani kati ya zifuatayo?
30. "Amani haiji kifung•z cha maneno kinakamilisha methali usahihi?
USHAIRI Soma kwa makini shairi lifuatalo kisha jibu maswali 31-36 kwa kuweka kivuli katika herufi ya jibu sahihi katika fomu yako ya kujibia
Kazi ifanye kwa nia,itakupatia
Ifanye kwa kupania,iwe kwako ni daraja
Kazi ni kuibobea, ili ilete faraja.
Juhudi katika kazi,ni zawadi maridhawa
Ni zawadi maridhawa juhudi katika kazi
Ifanye uwe mzawa,uonekane wazi,
Uoneshe uelewa,nchini mwako azizi
Tufanye kazi kwa dhati,itatupa manufaa
Itatupa manufaa ,tufanye kazi kwa dhati,
Tuoneshe yanofaa,kwa moyo ulo thabiti
Kazi ndiyo mhimili,popote utapokuwa.
Popote utapokuwa,kazi ndio mhimili, Kama gari huendeshwa,vile inastahili, Mafunzo uliyopewa,vile inastahili,
Mafuzo uliyopewa iwe kwako ni kivuli,
Kwako ni muhimu maisha kuendelea,
31. Kichwa kinachofaa kwa shahiri hili ni
32. Mwandishi "anasema kazi ni kuibobea" ana maana gani?
33. Vina vya kati na mwisho katika ubeti wa pili ni vipi?
34. Shairi hili linatoa funzo gani?
35. Neno "thabiti" katika shairi hili lina maana gani?
UTUNGAJI
Umepewa habari yenye sentensi nne(4)zilizoandikwa bila mtiririko wa mawazo katika swali la 37-40 zipange sentensi hizi ili ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi weka kivuli katika herufi ya jibu sahihi katika fomu yako ya kujibia.
37. Kwa mfano,wavulana walipofikia umri wa kuoa iliwalazimu kujijengea nyumba ya kuishi na kuwa na mazao ya chakula.
38. Elimu hiyo ilitolewa na walimu maalum wa jadi na ilihusisha na vitendo.
39. Wakati wa ukoloni elimu hiyo ilipigwa vita na kuonekana kuwa haifai hivyo uliletwa mfumo mpya wa Elimu.
40. Kabla ya kuja kwa wakoloni Waafrika walikuwa na mfumo wao wa elimu ya jadi.
SEHEMU A: SARUFI Katika swali la 1 — 20, weka kivuli katika herufl ya jibu lililo sahihi katika karatasi yako ya kujibia
1. Neno lipi ni tofauti na maneno mengine kati ya haya
2. Mto Ruvu umefurika mwaka huu. Katika sentensi hii, maneno "mwaka huu" ni ya aina gani?
3."Mimi sitakuja" Sentensi hii iko katika kauli gani?
4.Mama mdogo amepika ugali mwingi". Maneno gani ni vivumishia sentensi hii?
5. "Wakulima wamehamisha mizinga ya nyuki kutoka mashambani mwao. "Umoja wa sentensi hii ni upi?
6. "Mwajuma amemwibia Mwanahamisi kalamu yake". Katika sentensi hii. "Mwajuma ni nani?
7. Kinyume cha neno "duwaa" ni kipi?
8. "Uvumilivu ulimfanya Pendo apate zawadi. "Uvumilivu ni aina gani ya neno?
9. Yupi kati ya wafuatao ni lazima awe mwanaume?
IO. "Walimu watafundisha masomo yao vizuri". Sentensi hii ipo katika wakati gani?
11. "Wanafunzi wenzake walimnyanyapaa. Neno walimnyanyapaa lina maana gani kati ya hizi zifuatazo?
12. Neno nimerudi lipo katika nafsi ipi?
13. Kiwanda hutoa ajira kwa wananchi "kiwanda" ni aina gani ya neno?
14. Mashine nyingi hupatikana" kiwandani" ni aina gani ya neno
15.Kisawe cha neno "ndovu" ni kipi kati ya maneno yafuatayo?
16, "Mlima meru unafuka moshi" Ukanusha wa sentensi hii ni upi?
17. Panga maneno yafuatayo kwa kuanzia na neno ambalo katika familia hiyo linaonesha aliyetangulia kuzaliwa hadi wa mwisho kuzaliwa: Baba, kitukuu, babu, kilembwe,
mjukuu, kilembwekeza.
18. Kisawe cha neno ”kinyinginya” ni kipi katika maneno yafuatayo?
19.Kisawe cha neno ”mviringo” ni kipi?
20.Mtu anayechonga vinyago anaitwaje?akaokota,
21. Alipomwona Yule Chui, Juma akapiga moyo konde na kuanza kumshambulia kwa mpini wa jembe. Maana ya msemo kupiga moyo konde ni ipi?
22. Nimeugua kwa kipindi kirefu sana, lakini sasa ni wa afya. Neno lipi linakamilisha sentensi hii?
23. Wakikua mama yao huwatupa mbali kwa kishindo.Jibula kitendawili hiki ni lipi?
24.Kati ya methali zifuatazo ni ipi haitoi msisitizo wa kufanya juhudi katika jambo?
26 sihimili kishindo"kifungu kipi cha maneno kinakamilisha methali hii?
27. "Asiyeuliza" maneno yapi yanakamilisha methali hii kwa usahihi
28." Gari langu halitumii mafuta jibu la kitendawili hiki ni lipi?
29. "Anatengeneza mchuzi mtamu sana lakini hapiki jikoni" kitendawili hiki jibu lake ni lipi?
30. "Ukiona vyaelea vimeundwa" methali hii ina maana gani?
UFAHAMU.
Soma kwa makini habari ifuatayo kisha jibu maswali 31-40 kwa kuweka kivuli katika herufi ya jibu lililo sahihi katika karatasi yako ya kujibia.
Jua lilikuwa linaunguza mithili ya moto. Hapakuwa na nyasi wala miti iliyokuwa na majani ya rangi ya kijani.Kila uoto ulikuwa wa rangi ya kahawia kavu! Aidha kupata tone la maji ya kunywa ilikuwa ndoto kwani mito na visima vyote vilikauka kau.Baada kuhangaika kwa njaa na kiu, ndipo wanyama waliamua waitishe mkutano ili wajadili hatua ya kuchukua. Makundi • ya wanyama wa aina mbalimbali walikutana chini ya mbuyu. Swala, nyani, mbawa na tembo wote walikuwepo.
"Kama mjuavyo mimi ndimi mfalme wa wanyama wote.Niungurumapo hapana achezae kwa hiyo bila shaka mtakubali kuwa mimi ndiye mwenyekiti wa mkutano huu."alitangaza simba.Wanyama wote walitazamana na kutikisa vichwa kwa ishara ya kuafiki. Kisha alisimama na kusema "Mheshimiwa mwenyekiú, jana nilisikia mlindimo toka upande wa magharibi. Hivyo ninashauri sote tuhame na kuelekea upande huo ili tuokoe maisha yetu kwani huko kuna dalili ya mvua."Wanyama wote waliunga mkono hoja hiyo,isipokuwa kobe ambaye alisema, "mheshimiwa mwenyekiti, endapo kweli tumeazimia kuhama, sisi akina kobe tunaomba mtubebe kwani kasi yetu ya kutembea ni ndogo mno."
Baada ya kila mnyama kutoa rai yake ,Mwenyekiti alisimama na kusema, "Nimesikia yote mliyosema, kabla ya kuanza kuhama nakutuma wewe ngombe upeleke ujumbe wetu kwa binadamu ili waache kuharibu mazingira, kwani hicho ndicho kiini cha matatizo yanayotusibu.Wewe ni kiungo baina yetu na binadamu." ngombe alikubali.
Baada ya kufika ujumbe ule, binadamu alijibu kuwa alikwishaelewa tatizo Ia mazingira na tayari alikuwa na mpango kabambe wa kuchinja mifugo yote ili kutekeleza ushauri wa wataalamu wa mazingira wa kuiokoa dunia na janga Ia jangwa. Kusikia hivyo ngombe alichanja mbuga kuelekea kwa wanyama wengine.
31. Kwa mujibu wa habari uliyo soma, mkutano wa wanyama ulifanyika wapi?
32. Mwenyekiti wa mkutano wa wanyama alikuwa nani?
33. Hali ya kukauka kwa mito,visima nyasi na miti kunakutokana na ukosefu wa mvua inaitwaje?
34. Jina lingine Ia mnyama aliye washauri wanyama wote kuhamia upande ambako kulikuwa na dalili ya mvua ni lipi kati ya yafuatayo.
35.Katika habari uliyo soma sababu iliyomfanya kobe kutoafiki moja kwa moja hoja ya kuhama ni ipi?
36. kwa mujibu wa habari hii ,uharibifu mkubwa wa mazingira hufanywa na nani?
37. Neno lipi kati ya yafuatayo lina maana sawa na neno janga?
38. Kifungu cha maneno "alichanjambuga"kinamaana gani?
39. Binadamu alikusudia kuchinja wanyama wa aina gani
40. Kichwa cha somo uliyosoma kingefaa kiwe kipi?
41. Kituo cha shairi hili ni kipi?
42. Katika shairi hili vina vya kati na mwisho ni vipi?
43. Shairi hili lina mizani ngapi?
44. Shairi hili lina beti ngapi?
45. Neno "kuangua" kama lilivyotumika katika shairi hili lina maana ipi?
46. Neno "Mizozo" kama lilivyotumika katika shairi hili lina maana gani?
SEHEMU E:
UTUNGAJI
Panga sentensi nne (4) zifuatazo ili ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi
A, B, C na D.
47. Zizi hilo limegawanywa katika sehemu mbili
48. Baba yangu anafuga ngombe, mbuzi na kondoo.
49. Nje ya nyumba yetu kuna zizi kubwa.
50. Sehemu moja ni ya ngombe na nyingine ni ya mbuzi na kondoo.
Katika swali la 1 — 20, weka kivuli katika herufiyajibu lililo sahihi.
1. "Wachache wamehamia Boro". Katika sentensi hiyo "Wachache" limetumika kama aina gani ya neno?
2. Alimwita nyumbani kwake kwa dhamira ya kumpa karo ya shule. Neno "dhamira" lina maana ipi?
3. Kauli ipi inaonesha hali ya kutendewa?
4. Katika vifungu vya maneno vifuatavyo, kifungu kipi kipo katika kauli taarifa?
5. Mwenyekiti hakufika mkutanoni leo. Kitenzi "hakufika" kipo katika hali gani?
6. "Wapiganaji wetu walipowasili visiwa vya Comoro walishangiliwa kwa Ni neno lipi linakamilisha sentensi hiyo?
7. Mawaziri wote wa Baraza la Mapinduzi waliapishwa. Neno "wote" limetumika kama aina gani ya neno?
8. Babu amemhamishia yule mbuguma kwenye zizi kubwa. Neno "mbuguma" lina maana
9. "Chama kimeteka nyara sera ya serikali." Wingi wa sentensi hiyo ni upi?
10. Nyumba ya ndege huitwaje?
11. "Wanafunzi hodari watapewa zawadi". Sentensi hiyo ipo katika wakati gani?
12. Maji yamejaa "pomoni" Neno "pomoni" ni aina ipi ya neno?
13. Kati ya maneno "Sherehi, Sherehe, Shamrashamra, Hafla, Tafrija" neno lipi halihusiani na mengine?
14. Neno lipi kati ya maneno yafuatayo lina maana sawa na "thubutu"?
15."Kuzua kizaazaa" ni msemo wenye maana gani?
16. Mtu anayetafuta kujua jambo fulani kwa kuuliza maswali huitwaje?
17. Neno Mchakato lina maana ya mfululizo wa................
18. Neno lipi kati ya yafuatayo lina maana sawa na neno shehena
19. Mtu aliyezaliwa na wazazi wa rangi mbalimbali huitwaje?
20. Baada ya miaka minne Kalunde ... ...... mafunzo yake ya udaktari. Ni neno lipi linakamilisha sentensi hiyo?
Katika swali la 21 — 30, weka kivuli katika herufiyajibu lililo sahihi.
21. Methali isemayo, "Katika msafara wa mamba na kenge wamo" iko sawa na methali ipi kati ya zifuatazo?
22. Diengi anapenda kuwarairai watu. "l<urairai watu" ni msemo wenye maana ipi?
23. Msemo "kubarizi" maana yake ni kukusanyika kwa ajili ya .
24. Methali isemayo "Kila mtoto na koja lake" ina maana gani?
25. Nahau isemayo "kuvishwa kilemba cha ukoka" ina maana gani?
26. Tegua kitendawili kifuatacho: "Nyumbani kwangu kuna jini mnywa maji."
27. "Wakulima wa kahawa wa wilaya ya Mbinga wamepewa heko kwa kuzalisha kahawa bora".
Msemo "wamepewa heko" hufanana na msemo gani kati ya ifuatayo?
28. Methali isemayo, "Mwenda pole hajikwai" inafanana na methali ipi kati ya zifuatazo?
29. Methali ipi kati ya hizi zifuatazo haifanani na zingine?
30. Mwamba ngoma .. Kifungu kipi cha maneno kinakamilisha methali hiyo?
SEHEMU C
UFAHAMU
Soma kwa makini habari ifuatayo kisha jibu maswali 31 — 40 kwa kuweka kivuli katika herufi ya jibu lililo sahihi.
Mpendwa kaka Yohana,
Natumani hujambo na unaendelea vizuri na masomo yako. Nimefurahi kusikia kwamba umechaguliwa kujiunga na masomo ya Sekondari. Ndugu wote wanakupongeza na kukutakia kila la kheri katika masomo yako. Soma kwa bidii zaidi kwani elimu ni bahari na haina mwisho.
Baba na mama walifurahi sana baada ya kupata taarifa za kuchaguliwa kwako kwa-njia ya simu kutoka kwa shangazi. Wanamshukuru sana shangazi kwa kukuwezesha na misaada yake mingi kwako ya hali na mali. Baba ameahidi kumtembelea shangazi tarehe ishirini mwezi wa kumi na moja mwaka huu ili kumkabidhi zawadi aliyomwandalia kutokana na ukarimu wake kwako.
Rafiki yako Juma alifika hapa nyumbani akasema kwamba ataniletea picha nikutumie. Hamisi amekuandalia zawadi ambayo atakukabidhi utakapokuja nyumbani wakati wa likizo yako ya mwisho wa muhula. Tunu amesema atakutembelea, lakini uwe mwangalifu unapoongea naye asije akakuchezea shere. Siku hizi ni msanii.
Nisalimie sana shangazi na wanae wote, yaani Amani, Anasitazia na Asia. Sisi sote tunakutakia kila la kheri katika masomo yako.
Akupendaye daima, Mdogo wako, Tumaini.
31. Neno "ukarimu” lina maana sawa na lipi kati ya maneno yafuatayo?
32. Mwandishi wa barua hii ametumia msemo "kuchezea shere” Msemo huo una maana ipi?
33. Ushindi wa Yohana na mafanikio yake katika masomo umetokana na nini?
34. Wazazi na ndugu zake Yohana walipata taarifa ya kufaulu kwake kwa njia gani?
35. Uhusiano wa Yohana na watoto wa shangazi yake ni upi?
36. Katika barua hii mwandishi anafananisha elimu na nini?
37. Unafikiri ni sababu ipi ilimfanya baba yake Yohana kumwandalia dada yake zawadi?
38. Lengo la Tumaini kumwandikia kaka yake barua lilikuwa lipi?
39. Kifungu hiki cha habari ni aina gani ya barua?
40. Ni methali ipi inatoa fundisho kutokana na ushindi wa Yohana?
Soma kwa makini shairi lifuatalo kisha jibu maswali 41 - 46 kwa kuweka kivuli katika herufiya jibu.
Nimekwisha peleleza, karibu kila mahali,
Mule wanamotangaza, matangazo lugha mbili, Juu kuwa Kingereza, Chini kuwa Kiswahili, Juu kiwe Kiswahili, Chini kiwe Kingereza.
Kitangazwe Kingereza, baada ya Kiswahili
Hivi tutapotimiza, lugha itakuwa ghali,
Hivi mnavyofanyiza, sana mnaidhalili,
Juu kiwe Kiswahili, Chini kiwe Kingereza
Serikali bembeleza, tafakari tafadhali,
Jambo hili kueleza, kwa zingine serikali Kiswahili kutangaza, kuwa Chini twakidhili Juu kiwe Kiswahili, Chini kiwe Kingereza.
Tuache kukipumbaza, kwa andiko au kauli, Kwa nyuma kukisogeza, kukipa kisulisuli,
Lazima kuyafukuza, yawezayo kikatili,
Juu kiwe Kiswahili, Chini kiwe Kingereza
Na wenyewe kujikaza, kwa bidii za kimwili kiswahili kutukuza, tukivalie bangili,
Ngomani kutumbuiza, waume na wanawali Juu kiwe Kiswahili, Chini kiwe Kingereza.
41. Katika shairi hilo mstari wa pili katika ubeti wa pili una mizani mingapi?
42. Katika ubeti wa nne, vina ni vipi?
43. Kituo ni kipi katika shairi hili?
44. Shairi hili linahimiza kuhusu nini?
45. Ujumbe unaopatokana katika shairi hili unafanana na methali ipi?
46. Kutokana na shairi ulilosoma neno "kutukuza” lina maana ipi?
SEHEMU E
UTUNGAJI
Umepewa habari yenye sentensi nne(4) zilizoandikwa bila mtiririko sahihi wa mawazo katika swali 47 — 50. Zipange sentensi hizo ili ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi A, B, C, na D. Weka kivuli katika herufi yajibu sahihi.
47. Hivyo mazoezi huleta afya, kwa hiyo ni muhimu kwa kila mmoja wetu kufanya mazoezi.
48. Mtu asiyefanya mazoezi anapata maradhi ya moyo; atanenepa kupita kiasi, kwa hiyo atapata ugonjwa wa kuumwa mgongo na magoti.
49. Mazoezi ya viungo yanachangamsha misuli ya mwili, mifupa na ubongo.
50. Lakini mtu anayefanya mazoezi anaepuka magonjwa ya moyo na msukumo wa damu.
Katika swali la 1 — 20, weka kivuli katika herufiyajibu lililo sahihi.
1. "Ramadhani anacheza mpira uwanjani." Sentensi hii ikiwa katika hali ya mazoea itakuwa ipi kati ya hizi zifuatazo?.....
2. "Bura yangu sibadili na rehani." Kitenzi "sibadili" kipo katika hali ipi?.......
3. "Babu alikuwa analima shambani." Neno "alikuwa" ni aina ipi ya kitenzi? .
4. Katika sentensi zifuatazo ipi ina maana sahihi?..
5. Ni neno lipi kati ya yafuatayo ni kisawe cha neno "hifadhi"? .
6. Lahaula! Loo! La hasha! Masalale! Ni maneno ya aina gani?
7. "Ingawa walipata matatizo mengi safarini walifika salama." Neno lipi linakamilisha sentensi hiyo kwa usahihi?
8. "Mjukuu wangu hupenda kuniamkia kila mara." Sentensi hiyo ipo katika kauli gani?
9. "Wawili wameshindwa kupanda mlima Kilimanjaro." Kiwakilishi katika sentensi hiyo ni kipi?
10. ”Vita ilipoanza nchini Kenya watu wote . . Kitenzi kipi kinakamilisha sentens hiyo?
11. "Tulicheza ngoma na kuimba usiku kucha.” Katika sentensi hii watenda ni nafsi ipi?
12. ”Utundu wake ulimfanya ajulikane shuleni.” Neno "Utundu” limetumika kama aina gani
neno?
13. "Mwanamuziki hodari aliimba nyimbo vizuri.” Kielezi katika sentensi hii ni kipi? ........
14. "Mgeni aliondoka alikofikia.............kuaga.” Kifungu kipi cha maneno kinachokamilishE sentensi hiyo kwa usahihi?
15. Neno moja linalojumuisha herufi "a, e, i, o na u” ni lipi?
16. "Kaka anapenda kujisomea chumbani mwake.” Katika sentensi hiyo kitenzi kisaidizi ni kipi? ........
17. ”Mchezo mkali ni ule tuliocheza ......... ya Timu ya Majengo.” Neno lipi linakamilisha tungc hiyo kwa usahihi?
18. Mama Ntilie akiondoka, uondoke naye. Sentensi hii ipo katika wakati gani? ........
19. Mpira umegonga mwamba nusura goli liingie. Neno lipi linaonesha kitendwa? ........
20. Ni neno lipi kati ya haya yafuatayo ni tofauti na mengine? ........
Katika swali la 21 — 30, weka kivuli katika herufiya jibu lililo sahihi.
21. Nahau isemayo, "Mtu mwenye ndimi mbili" ina maana ipi kati ya zifutazo? ...... .
22. Wanafunzi walipotoka safari walilala usingizi wa pono. Msemo usemao, "Usingizi wa pono" una maana gani?
23. Kitendawili kisemacho: "Kamba yangu ndefu lakini haiwezi kufunga kuni," kina maana ipi kati ya hizi zifuatazo?
24. Methali isemayo: "Mgaagaa na upwa hali wali mkavu," inatoa funzo gani
25. Usingelitia chumvi kwenye kile kikao wajumbe wasingeligombana. "Kutia chumvi" ni usemi wenye maana gani?
26 "........... hufa maskini." Kifungu kipi hukamilisha methali hiyo kwa usahihi? .
27. Nahau ipi kati ya hizi zifuatazo hutumika kwa watu ambao matendo yao si ya kupendana?
28. Methali ipi kati ya hizi zifuatazo inapingana na hii, "Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu."
29. Methali ipi kati ya hizi zifuatazo inapingana na hii, "Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu”.
30. "Mchelea mwana kulia hulia yeye mwenyewe”. Methali hii inatoa funzo gani?
SEHEMU C
Soma kwa makini habari ifuatayo kisha jibu maswali 31 — 40 kwa kuweka kivuli katika herufi ya jibu lililo sahihi.
Matunda kama yalivyo mazao mengine ya kilimo yanatokana na mimea mbalimbali. Kwa mfano fenesi ni tunda litokanalo na mfenesi na chungwa hutokana na mchungwa. Maembe, mapapai, mananasi na mapera ni matunda matamu. Ubuyu, ukwaju na limau ni matunda machachu. Hata hivyo, karibu matunda mengi huwa machachu yakiwa mabichi, yakiiva huwa matamu.
Miaka ya hivi karibuni watu wengi wamepanda mimea ya matunda kwenye maeneo ya nyumba zao, hivyo kujipatia matunda kwa njia rahisi. Baadhi ya watu wanaoishi katika mikoa kama vile Tanga na Morogoro wamelima mashamba ya matunda na wameshaona faida ya kilimo hicho na kupanua mashamba yao. Licha ya watu hao kujipatia chakula bora, wameuza na kuwa na pato kubwa.
Matunda yana umuhimu mkubwa sana katika miili yetu. Matunda tunayokula yanaikinga miili yetu isipatwe na maradhi. Pia matunda yanaongeza damu mwilini, husaidia kuponyesha vidonda haraka na macho kuona vizuri katika mwanga hafifu. Watu wasiokula matunda hupata udhaifu wa fizi ambao husababisha fizi kutoa damu.
Aidha matunda ni kiburudisho wakati wa joto. Watu wengi wamekuwa wakisindika matunda ili kupata juisi kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na biashara.
MASWALI
31. Kichwa cha habari hii kinachofaa zaidi ni kipi?
32. "Watu wanaokula matunda huepuka magonjwa mengi,” ni methali ipi inaendana na kauli hii?
33. Maji ya matunda yaliyokamuliwa huitwaje? .
34.
"Matunda yaliyoiva” ina maana sawa na ipi kati ya zifuatazo? ........
35."Kilimo cha matunda kimekuwa cha faida kubwa kwao.” Methali ipi ambayo inaendana na maelezo hayo?
36. Ni kwanini wakulima wa matunda hupanua mashamba yao?
37. Matunda ya ubuyu na ukwaju yakiwa yameiva huwa na ladha gani?
38. Kazi kubwa ya matunda mwilini ni ipi?
39. "Kusindika matunda” ina maana sawa na kifungu kipi kati ya vifuatavyo?
40. Umepata funzo gani kutokana na kifungu hiki cha habari?
SEHEMU D
Soma kwa makini shairi lifuatalo kisha jibu maswali 41 - 46 kwa Kuweka kivuli katika herufi ya jibu.
Mtu kujitegemea, huwajambo Ia lazima,
Usipende subiria, kusaidiwa daima,
Huwezi kuendelea, ndugu usipojituma,
Kamwe hupati heshima, usipojitegemea.
Kama Mungu kakuumba, mzima huna kilema, Fedheha kuombaomba, takuwa mtu wa nyuma, Hutakuja kujigamba, ukikudharau umma. Kamwe hupati heshima, usipojitegemea.
Kazi mtu usidhani, sharti niya kusoma,
Ya kuleta ofisini, na kuhesabu ndarama,
Waweza kwenda shambani, ushikejembe kulima, Kamwe hupati heshima, usipojitegemea.
Utaambiwa doezi, mtu uso taadhima,
Pengine uitwe mwizi, umezoea dhuluma, Wajapo wapelelezi, ndiwe watakuandama, Kamwe hupati heshima, usipojitegemea.
41. Katika shairi ulilosoma neno "ndarama" lina maana ipi?
42. Kisawe cha neno "taadhima" ni kipi?
43. Ujumbe unaopatikana katika shairi hili unaweza kuwasilishwa kwa methali ipi kati ya zifutazo? ........
44. Katika shairi ulilosoma kituo bahari ni kipi?
45. Katika shairi ulilosoma nusu mstari una mizani ngapi?
46. Neno "fedheha" kama lilivyotumika katika shairi hili lina maana gani?
Umepewa habari yenye sentensi nne(4) zilizoandikwa bila mtiririko sahihi wa mawazo katika swali 47 — 50. Zipange sentensi hizo ili ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi A, B, C, na D weka kivuli katika herufi ya jibu sahihi.
47. Ukataji wa miti kwa wingi kwa ajili ya ujenzi na shughuli zingine huweza kuisababisha nchi yetu ya Tanzania kuwa jangwa.
48. Kutokana na miti watu hujenga nyumba nzuri za kila namna, zinazopendeza na za kudumu.
49. Hivyo ni muhimu kwa kila mtu kupanda mti kila anapokata mti kwani nchi isiyo na miti ni sawa na mtu ambaye amevuliwa nguo.
50. Miti ina faida nyingi sana kwa binadamu.
2014: KISWAHILI
SEHEMU A: SARUFI
Katika swali la 1 - 20, andika herufi ya jibu lililo sahihi katika karatasi yaka ya kujibia.
1. "Yeye amefaulu mitihani yake vizuri." katika sentensi hii neno lipi limetumika kama kielezi?
2. "Dada ameandika barua kwa baba." Sentensi hii iko katika kauli gani?
3. Katika sentensi zifuatazo ipi ni sahihi?
4. Neno lipi ni tofauti na maneno mengine kati ya maneno yafuatayo?
5. "Tunu angalisoma ..... mtihani wake." Neno lipi linakamilisha sentensi hiyo kwa usahihi?
6. "Mnyama mkali amekamatwa leo." Katika sentensi hii neno "mkali" limetumika kama aina gani ya neno?
7. "juma amefika na hatacheza mpira" Kitenzi "hatacheza" kipo katika half gani?
8. "Alisema hanywi dawa tena." Kauli halisi ya sentensi hii ni ipi?
9. "Walikotoka kuna mvua." Sentensi hii ipo katika wakati gani?
10. "Hamisa na Hanifa ni mapacha walioungana." Katika sentensi hii neno "na" limetumikakama aina gani ya neno?
11. Panya huyu anakula unga wangu. Wingi wa sentensi hii ni upi?
12. Siku ile ya maandamano kulikuwa na...........wa pikipiki. Ni neno lipi linakamilisha sentensi hii?
13. "Mpira wetu umechanika vibaya" Sentensi hii ipo katika kauli gani?
14. Neno mchwa lina silabi ngapi?
15. "Hapa ...............alipoishi chifu Mirambo." Ni neno lipi linakamilisha sentensi hii kwa usahihi?
16. Atakapomnyonyoa yule hata ......... kwenye moto. Kitenzi kipi kinakamilisha tungo hii?
17. "Kitabu changu ni cheusi, chako ni cheupe." Neno "chako" ni aina gani ya neno?
18. Yeye ni kijana mdogo. Neno "yeye" lipo katika nafsi gani?
19. Kinyume cha kitenzi "paa" ni kipi?
20. Mwalimu J. K. Nyerere ni mwasisi wa chama cha TANU. Neno "ni" limetumika kama ainaipi ya kitenzi?
SEHEMU B
LUGHA YA KIFASIHI
Katika swali la 21- 30 chagua herufi ya jibu lililo sahihi kisha andika kwenye karatasiya majibu.
21. "Ulichokitupa pwani ................" Kifungu kipi cha maneno hukamilisha methali hiyo?
22. "Mkiweza..............katika kazi hiyo, hatimaye mtafanikiwa." Nahau ipi inakamilisha tungo hii?
23. Methali isemayo, "Ngoma ikilia sana hupasuka" hulingana kimaana na methali ipi kati yahizi zifuatazo?
24. "Ukukuu wa kamba si upya wa ukambaa." Methali hii ina maana sawa na methali ipi?
25. "Hamadi kibindoni." Kati ya tafsiri zifuatazo ni ipi inayotoa maana sahihi ya msemo huo?
26. "Samaki mkunje angali mbichi." Methali ipi kati ya zifuatazo ina maana sawa na hii?
27. Methali isemayo. "Chanda chema huvikwa pete" inatoa funzo gani?
28. "Ukitaka kuruka agana na nyonga" Methali hii inaasa kuhusu jambo gani?
29. Methali isemayo. "Mpofuka ukongweni.................. " hukamilishwa na kifungu kipi cha maneno kati ya hivi vifuatavyo?
30. Nikikutana na adui yangu nanyongea. Jibu la kitendawili hiki ni lipi?
SEHEMU C
UFAHAMU
Soma kwa makini habari ifuatayo kisha jibu maswali 31 - 40 kwa kuandika herufi ya jibu lililo sahihi katika karatasi ya majibu.
Mabadiliko ya hali ya hewa yamekuwa makubwa kiasi cha kutisha. Zamani mababu wetu walitabiri mvua wao wenyewe pasi na kuwa na vyombo vya kisasa. Suala linalozungumziwa sana siku hizi ni mabadiliko ya hali ya hewa na athari zake kwa jamii nzima. Kila mtu ana wasiwasi kuhusu mvua ambazo huchukua muda mrefu bila kunyesha.
Ukosefu wa mvua ambao mwishowe huleta ukame na njaa umechangiwa kwa kiasi kikubwa na shughuli za binadamu ambazo zinaongezeka kwa haraka siku hadi siku. Shughuli hizo mbalimbali ambazo kwa upande mmoja zimeonekana kama za kimaendeleo ni kuongezeka kwa matumizi ya maliasili. Mifano mbalimbali ambayo inaonesha matumizi hayo ni pamoja na ujenzi wa nyumba nyingi zaidi, kupata nishati ya kutosha kwa ajili ya kupikia na upatikanaji wa mbao na magogo kwa wingi kwa matumizi ya ndani na hata ya nje ya nchi.
Hata hivyo, iii maendeleo hayo yawe na mwelekeo chanya jamii inalazimika kupanda miti kwa wingi iii kukidhi mahitaji hayo. Aidha ni vema kuzingatia kuwa ukataji miti ni chanzo kikubwa cha mito na vijito kuwa na maji haba au kukauka kabisa.
MASWALI
31. Kichwa cha habari kinachofaa habari hii ni kipi?
32. Tatizo kubwa zaidi ambalo husababishwa na ukosefu wa mvua kwa muda mrefu ni lipi kati ya haya yafuatayo?
33. Mwandishi anayaelezea mabadiliko ya hali ya hewa kuwa yalikuwa.
34. Neno "haba" kama lilivyotumika katika kifungu cha habari lina maana gani?
35. Dalili mojawapo kubwa ya maendeleo ni ipi kama ilivyoelezwa katika kifungu cha habari?
36. Mabadiliko ya hali ya hewa yana maana sawa na ipi kati ya hizi zifuatazo?
37. Kisawe cha neno "mwishowe" kama kilivyotumika katika habari hii ni kipi?
38. Watu wa zamani waliweza kutabiri mvua kwa kutumia:
39. Mito na vijito huwa na maji haba au kukauka kutokana na nini?
40. Nishati ni neno lenye maana sawa na lipi?
SEHEMU D
USHAIRI
Soma kwa makini shairi lifuatalo kisha jibu maswali 41 - 46 kwa kuandika herufi ya jibulililosahihi kwenye karatasi ya majibu.
Msituni nikakuta, nyuki wamo mzingani,Kwa juhudi wanakita, mara nje mara ndani,Husuda wameikata, hata hawasengenyani,
Nyuki ni wadudu duni, wanashinda kwa umoja,
Mchwa nao nikaona, wamejenga maskani,Wafanya bidii sana, uvivu hawatamani, Wao husaidiana, tena hawadanganyani,
Mchwa wadudu wa chini, wanaishi kwa umoja.
Nalojeshi la siafu, hutandawaa njiani, Laenda bila ya hofu, maana lajiamini,Silaha zao dhaifu, menu tena hawaoni,Wa kuwatania nani, kwani wanao umoja
Nao chungu wachukuzi, nyamarima wa njiani,Maskani wapagazi, mizi,go yao kichwani,Ingawa si wachokozi, wakali ukiwahini,
Katu hawafarakani, wanadumu kwa umoja
41. Mwandishi wa shairi hili anasisitiza kuhusu nini?
42. Shairi hili lina mizani mingapi kwa kila mstari?
43. Neno "husuda" kama lilivyotumika katika shairi hili lina maana gani?
44. Kisawe cha neno "Tadi" ni kipi?
45. Kina cha kati katika ubeti wa pili ni kipi?
46. Kichwa cha habari kinachofaa kwa shairi hill ni kipi?
SEHEMU E
UTUNGAJI
Umepewa habari yenye sentensi nne (4) zilizoandikwa bila mtiririko sahihi wa mawazo katikaswali la 47 - 50. Zipange sentensi hizo iii ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi A,B,C na D. Andika herufi ya jibu sahihi katika karatasi ya kujibia.
47. Kwa njia hii, vizazi vilivyofuata viliweza kujua uvumbuzi uliofanywa kabla yao.
48. Jambo muhimu lililofanywa na mababu zetu ni kuhifadhi kumbukumbu za uvumbuzi waokwa kuchora kila kifaa walichovumbua.
49. Kwa kutumia vizazi vilivyotangulia nasi pia tunaweza kuvumbua vitu vipya ambavyovitaweza kutuletea maendeleo zaidi.
50. Hivyo maisha ya binadamu yakaendelea kuwa bora na yenye manufaa kila siku. 11. Sentensi ipi kati ya hizi ipo katika hali timilifu? 12. Neno lipi ni tofauti na maneno mengine kati ya yafuatayo? 13. "Kitabu chako ni kizuri, ukienda dukani nami uninunulie ... ......” Ni kifungu kipi cha maneno hukamilisha sentensi hiyo? 15. Mkutano haukufanyika kwa sababu mwenyekiti na katibu hawakufika. Kifungu kipi cha maneno kati ya vifuatavyo kinasadifu sentensi hiyo? 16. Mlinzi wa mlangoni huitwaje? 17. Joshua yuko jikoni anapaa samaki. Neno "anapaa” kama lilivyotumika katika sentensi hii lina maana ipi? 18. "Mtoto wa ngombe anaitwa ndama, watoto wa kuku, bata, kanga wanaitwa vifaranga, kimatu ni mtoto wa nani? 19. Kisawe cha neno ”eupe” ni kipi? 20. Siku ya nne baada ya leo huitwaje? SEHEMU C Soma kifungu cha habari na kishajibu maswaliyanayofuata: Maji ni moja kati ya vitu vitatu muhimu sana vinavyotuwezesha kuishi. Vitu vingine ni hewa na chakula. Hewa ndiyo yenye umuhimu wa kwanza, ikifuatiwa na chakula. Kusingelikuwa na maji maisha ya binadamu na ya viumbe wengine yasingewezekana. Kila mtu anaelewa umuhimu wa maji katika maisha. Maji yanatawala maisha kwa kiasi kikubwa sana. Baadhi ya viumbe kama vile samaki, mamba, kasa, konokono, nyangumi na wengineo maskani yao ni majini, hivyo maji yakikosekana viumbe hao huweza kuaga dunia. Binadamu anatumia maji kwa shughuli mbalimbali. Shughuli hizo ni pamoja na kupikia, kufulia, kusafishia vyombo, kuoga na kunywa. Katika sehemu nyingi za nchi yetu watu hutumia maji kwa kumwagilia bustani za mboga, maua na miti. Katika maeneo yenye mito mikubwa na maziwa maji yake hutumika kwa kumwagilia mashamba kama yale ya mpunga na mahindi. Kilimo cha umwagiliaji kinafaa kwa sababu mkulima anakuwa na uhakika wa kuvuna. Maji ya mvua huwezesha watu kulima na kupanda mazao ya chakula na ya biashara. Hivyo zipo sehemu ambazo wakulima hulima kilimo cha umwagiliaji lakini sehemu kubwa ya wakulima hutegemea kilimo cha mvua. Kwa ujumla maji yawe ya mvua au yanayotokana na mito au maziwa yana umuhimu mkubwa mno kwa binadamu kama walivyosema wahenga maji ni uhai, hivyo inashauriwa kwamba ni muhimu kwa kila mtu kunyvva maji safi na salama ili kulinda siha zetu. MASWALI 31.Vitu vitatu muhimu vinavyomwezesha binadamu kuishi ni vipi? 32.Wakulima wengi kama ilivyoelezwa katika habari hii hulima kilimo kinachotegemea nini? 33. Kiumbe yupi kati ya wafuatao halandani na wenzie? 34.Kilimo cha umwagiliaji kina sifa gani kubwa? 35.Neno "siha" kama lilivyotumika katika kifungu hiki cha habari lina maana gani? 36. "Kuaga dunia" ni msemo wenye maana gani? 37. Ni kwanini mtunzi wa habari hii anashauri watu kunywa maji safi na salama? 38.Neno "maskani" kama lilivyotumika katika kifungu cha habari lina maana gani? 39.Kichwa cha habari kinachofaa kwa kifungu hiki ni kipi? SEHEMU D USHAIRI Soma shairi lifuatalo kisha jibu maswali yanayofuata Nyumbani kwako kuzuri,japokuwa ni pangoni, Nyumba yako nijohari,ya mwenzako sitamani, Hata pawe pa tajiri, hapafai maishani, Nyumbani kwakojohari, kwingine usitamani. Kwingine usitamani, nyumbani kwakojohari, Unaishi kwa amani, na pia kwa ujasiri, Hiyo kweli abadani, nyumbani kunasetiri, Nyumbani kwakojohari, kwingine usitamani, Uipende nyumbayako, utaona raha yake, Kisha penda nduguyako, kwako apaone kwake, Dunia mahangaiko, usipende pekepeke, Nyumbani kwakojohari, kwingine usitamani. Usichaguejirani, bali chagua rafiki, Usitenge asilani, shauri pia afiki, Palipo na burudani, kaa nao marafiki, Nyumbani kwakojohari, kwingine usitamani MASWALI 41. Kichwa cha shairi kinachofaa ni kipi? 42. Kituo katika shairi hili ni kipi? 43. Neno "johari" kama lilivyotumiwa na mtunzi lina maana gani? 44. Neno "pekepeke" kama lilivyotumiwa na mshairi lina maama gani? 44. Neno "pekepeke" kama lilivyotumiwa na mshairi lina maama gani? 45. Vina vya kati na vya mwisho katika ubeti wa tatu ni vipi? 46. Funzo linalopatikana katika shairi hilo linawakilishwa na methali ipi kati ya zifuatazo? SEHEMU E UTUNCAJI Katika Sehemu hii kuna habariyenye sentensi nne (4) zilizoandikwa bila mtiririko sahihi unatakiwa kuzipanga sentensi hizo ili ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi A, B, C, na D 47. Vile vile matunda huongeza damu mwilini 48. Hivyo matunda yana umuhimu mkubwa katika miili yetu. 49. Lakini watu wasiokula matunda hupata maradhi kama vile ugonjwa wa fizi, macho na ngozi. 50. Kula matunda kunasaidia kuponyesha magonjwa na vidonda haraka, pia husaidia macho kuona vizuri katika mwanga hafifu. SEHEMU B Jibu swali la 6 - 10 kwa kuchagua herufi ya jibu sahihi na kuiandika katika kisanduku pembeni ya kilo swali. 6. Mtu anayeongoza meli huitwa 7. Nimepatwa na. . . . . . . . . . . kutokana na msiba wa mjomba. 8. Usipoziba . . . . . . . . . . . utajenga ukuta 9. Mkoa wa Iringa ni mojawapo ya mikoa iliyoko nyanda za juu ...... 10. Ili kupika ugali unahitaji maji na KISWAHILI-2012 SEHEMU A SARUFI Chagua herufiyajibu lililo sahihi kisha andika katika karatasiyakoya kujibia. 1. Katika maneno yafuatayo ni lipi ambalo ni nomino dhahania? 2. Wingi wa neno "paka" ni upi? 3."Akiondoka Sulubu kazi zote zitalala." Neno "sulubu" ni la aina ipi? 4."Ili tuendelee.... ..... kufanya kazi kvva bidii." Neno lipi limekosekana kukamilisha sentensi hiyo? 5."Mvua ilinyesha jana usiku kucha. " Katika sentensi hiyo kikundi kielezi ni kipi? 6."Baba alilimiwa shamba." Sentensi hii ipo katika kauli gani? 7."Adili alikuwa anaimba tangu ujana wake." Neno "alikuwa" ni aina gani ya kitenzi? 8."Mchungaji alivaa suti maridadi sana."Katika sentensi hii neno lipi limetumika kama kivumishi? 9.Kitenzi " anapigwa" kipo katika kauli gani? 10.Kisawe cha neno "bahati" ni kipi kati ya maneno yafuatayo? 11."Maandishi yanasomeka vizuri." Sentensi hii ipo katika wakati gani? 12. "Makubi ni mtoto wa mjukuu wangu." Makubi ni nani kwangu? 13."Sipendi uongo." Sentensi hii ipo katika nafsi ipi? 14.Neno "poni" lina maana sawa na neno lipi kati ya maneno? 15. "Shuleni kwetu kuna upungufuwa . Ni neno lipi hukamilisha tungo hiyo kwa usahihi? 16. "Mtoto ametengeneza toroli Ia mti." Wingi wa sentensi hii ni upi? 17. "Muda mfupi atakuwa anaingia uwanjani." Sentensi hii ipo katika wakati gani? 18. Ni neno lipi kati ya haya yafuatayo halilandani na mengine? 19. Juma aliondoka hivi punde. Maneno "hivi punde" yana maana ipi? 20. Neno lipi ni kisawe cha neno adili? SEHEMU B LUCHA YA KIFASIHI Katika swali la 21 — 30 andika katika herufiyajibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia. 21. "Mwanzo wa ngoma ni lele.” Methali inayofanana na hii kati ya hizi zifutazo ni ipi? 22. "Akutendaye mtende usimche akutendaye.” Methali hii inatoa funzo gani? 23. "Uzuri wa mkakasi ndani .........” Ni kifungu kipi kati ya vifuatavyo kinakamilisha methali hiyo? 24. Msemo upi kati ya ifuatayo unakamilisha sentensi, "Kinjekitile alijaribu lakini baadaye hakuitekeleza.” 25. Tegua kitendawili kisemacho, " Atembeapo kila mara huringa hata kama kuna adui.” 26. "Siku hizi siri za mafisadi zimeanikwa juani.” Usemi "kuanikwa juani” una maana ipi kati ya hizi zifuatazo? 27. Methali ipi kati ya zifuatazo ina maana sawa na hii isemayo "Meno ya mbwa hayaumani.” 28. "Tatizo la ufisadi limeota mizizi katika nchi yetu.” Usemi "kuota mizizi” una maana gani? 29. Tegua kitendawili kifuatacho "Kondoo wangu kachafua njia nzima.” 30. "Ntandu alikuwa na kichwa cha panzi." Msemo "kichwa cha panzi" una maana gani? SEHEMU C UFAHAMU Soma kwa makini habari ifuatayo kishajibu maswali 31 - 40 kwa kuchagua herufiyajibu sahihi na kuandika katika karatasi yakoya kujibia. Uuzaji wa mazao ni tendo la kubadilisha mazao kwa fedha. Mkulima anampa mtu mwingine mazao yake ili yeye apewe fedha. Uuzaji huu unaweza kufanywa na mkulima mwenyewe au dalali. Kituo kibubwa cha kuuzia mazao haya ni soko au gulio. Serikali huwa inawashauri wakulima kuanzisha vyama vya ushirika. Vyama hivi vitakuwa na kazi ya kununua mazao ya wakulima na kuyauza ndani na nje ya nchi. Tatizo kubwa la vyama vya ushirika ni ile tabia ya kukopa mazao kwa wakulima halafu kuyauza ndipo ipatikane fedha ya kuwalipa wakulima. Mfumo huu unatakiwa uwe unaratibiwa vizuri na wakulima, kwani mali bila daftari hupotea bila habari. Siku hizi kuna soko huria. Watu binafsi hujitokeza kununua mazao kwa bei nzuri na hulipa fedha kwa wakati huo huo. Kwa njia hii huwasaidia wakulima kupata soko ka mazao yao. Hata hivyo, wakulima wanapaswa kuwa makini kwa kuwa wanunuzi wengine ni matapeli. Mashambega hawa hufanya hila kwa kutumia mizani zisizo sahihi na hivyo wakulima huambulia fedha kichele tu. Hali hii huwaletea simanzi wakulima, lakini pamoja na masononeko hayo kwa kuwa walanguzi hutoa pesa papo kwa papo, wakulima wengi huona bora kuwauzia walanguzi kuliko kuikopesha serikali. Wahenga walisema heri kenda kisha kuliko kumi nenda uje. MASWALI 31. Kichwa cha habari kinachofaa kwa habari uliyosoma ni kipi? 32. Neno "simanzi" kama lilivyotumika katika habari hii lina maana tofauti na lipi? 33. Vyama vya ushirika vinahitaji kuwa na nini? 34. "Fedha kichele." Nahau hii ina maana ipi? 35.Kisawe cha neno tapeli ni kipi? 36.Methali "Heri kenda shika kuliko kumi nenda uje" inatoa funzo gani? 37.Katika habari uliyoisoma jamii inaaswa kuhusu nini? 38.Neno lipi kati ya yafuatayo ni kinyume cha neno "hili?" 39.Neno "dalali" kama lilivyotumika katika habari hii lina maana gani? 40.Funzo muhimu zaidi ulilolipata katika habari uliyosoma linawakilishwa na methali ipi? SEHEMU D USHAIRI Soma kwa makini shairi lifuatalo kishajibu maswali 41 - 46 kwa herufiyajibu lililo sahihi katika karatasiya kujibia. Wanafunzi sikiliza, nawapa huu wasia, Nataka kuwaeleza, mambo muhimu sikia, Kwanza ninawapongeza, hapa mlipofikia, Hongereni hongereni, hongereni kuhitimu. Hapa mlipofikia, kamwe msije bweteka, Malenga kuyafikia, huu ni mwanzo hakika, Usije kuvizikia, vitabuvyo kwenye taka, Hongereni hongereni, hongereni kuhitimu. Shuleni mmejifunza, masomo kwa uhakika, Kiswahili ni cha kwanza, lugha hamkuichoka, Kwa ari mkijifunza, mbele kitawapeleka, Hongereni hongereni, hongereni kuhitimu. Safari miaka saba,yenye raha na karaha, Mlichopata si haba, mwende nacho kwa furaha, Hicho kidogo kibaba, kisilete majeraha, Hongereni hongereni, hongereni kuhitimu. MASWALI 41. Mshairi anaposema "mlichokipata si haba" ana maana gani? 42. Vina katika ubeti wa pili ni vipi? 43. Wazo kuu katika shairi hili ni lipi? 44. Kichwa kinachofaa kwa shairi hili ni kipi? 45. Kinyume cha neno "karaha" ni kipi? 46. Neno "bweteka" kama lilivyotumika kwenye shairi hilo lina maana ipi? SEHEMU E UTUNGAJI Umepewa habari yenye sentensi nne (4) zilizoandikwa bila mtiririko sahihi wa mawazo katika swali la 47 - 50. Zipange sentensi hizo ili ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi A, B, C na D. Weka kivuli katika herufiyajibu sahihi katika karatasiyakoya kujibia. 47.Dakika chache baadaye, tuliona msafara wa magari ukiingia. 48.Gari hilo lilifuatwa na gari lingine lililojaa askari wa kuzuia fujo, kisha lilifuata gari la Rais. 49.Mnamo saa saba hivi tuliona pikipiki ya askari wa usalama barabarani ikija mbio kama mshale. 50.Mbele ya msafara huo kulikuwa na pikipiki nne zilizofuatiwa na gari la polisi lenye kingora. KISWAHILI 2013 SEHEMU A SARUFI 1. Sweta langu limeshonwa na fundi mzoefu? "Mzoefu" ni aina gani ya neno? 2. "Ningejua ukweli wa mambo kabla ......... hapa bure saa hizi." Neno gani Iinakamilisha sentensi hiyo? 3. "UKIMWI unaua." Mbunge alisema. Ipi ni kauli taarifa ya sentensi hiyo kati ya hizi zifuatazo? 4. "Anna anatembea polepole twiga." Kifungu kipi cha maneno kinakamilisha sentensi hiyo? 5. Neno lipi halilandani na maneno yafuatayo? 6. Sentensi ipi kati ya hizi zifuatazo ni kauli ya kutendea? 7. "Tumejifunza . kujikinga na VVU na UKIMWI." Kifungu kipi cha maneno kati ya vifuatavyo kinakamilisha sentensi hiyo? 8. Sehemu ambayo ngombe huogeshwa ili kuwaepusha na magonjwa huitwaje? 9. ”Mboga haina chumvi ya kutosha.” Wingi wa sentensi hiyo ni upi? 10. Nywele zinazoota kuanzia karibu na masikio mpaka kwenye mashavu huitwaje? SEHEMU B LUCHA YA KIFASIHI 21. Tegua kitendawili kisemacho: "Mwenye kuitwa amefika lakini mjumbe bado hajarudi.” 22. Wakoloni walitunyanyasa lakini hatimaye unyanyasaji huo ulifika ukingoni kwani .........” Ni methali ipi kati ya zifuatazo inakamilisha sentensi hiyo? 23. ”Kidagaa kimemwozea.” Msemo huu una maana gani? 24. "Kukubali kwa ulimi” ni msemo wenye maana ipi? 25. Nahau isemayo, "amevimba kichwa” ina maana ipi? 26. "Kitanda usichokilalia hujui kunguni wake." Methali ipi kati ya zifuatazo ina maana save na hiyo? 27. "Nina mwanangu mweupe nikimtia maji hufa." Kitendawili hicho kina maana ipi? 28 Bwana mkubwa amelala ndani lakini ndevu zipo nje zapepea." Jibu sahihi la kitendawili hiki ni lipi? 29. "Kazi mbaya si mchezo mwema." Methali inayofanana na methali hiyo ni ipi? 30. Msemo usemao, "kushikwa sikio" una maana ipi? KISWAHILI 2011 SEHEMU A SARUFI Katika swali la (1 - 20) andika herufi ya jibu sahihi katika karatasi yako ya kujibia. 1. Neno "jenga" likinyumbulishwa katika kauli ya kutendeka litakuwa neno lipi? 2. Neno "wamewalisha" linadokeza hali gani ya kitenzi? 3. "Yeye hupenda sana kusoma Kiswahili". Katika sentensi hii ni neno lipi limetumika kama kiwakilishi? 4. Katika sentensi zifuatazo ni ipi ipo katika hali ya mazoea 3. Sara alimwambia Heri kwamba hakusafiri bali alikuwepo pale pale. Kauli halisi itakuwa ipi? 6. "Alikuwa anajibu kihuni". Neno "kihuni" limetumika kama aina gani ya neno? 7. "Mtu anayetaka msaada wa aina nitampa". Neno linalofaa kukamilisha tungo hiyo ni lipi? 8. "Wanafunzi wanaendelea kusoma Kiswahili ingawa hawana mwalimu". Neno "wanaendelea" limetumika kama aina gani ya kitenzi? 9. Mahali pale panatisha. Neno "pale" ni aina gani ya neno 10. "Kinyonga anatembea". Ukanushi wa sentensi hii ni upi? 11. "Mama anapika lakini baba abapangamawe". Neno lakini limetumika kama aina gani ya neno? 12. "Kiburi si maungwana". Neno "si" limetumika kama aina gani ya kitenzi 13. "Baba yangu ni mwenyekiti wa lopp". Neno "mwenyekiti ni nomino ya aina gani? 14. Wingi wa neno chuma ni upi kati ya maneno yafuatayo? 15. "Wanafunzi walitumiana salamu". Sentensi hii ipo katika kauli gani? 16. Kinyume cha neno "elea" ni kipi? 17. "Huyu mwanangu mpendwa". Neno lipi ni sahihi iii kukamilisha sentensi hiyo. 18. "Mbwa ameonekana". Neno lipi ni sahihi kukamilisha tungo hiyo? 19. Hall ya kuwa na fedha au mall nyingi huitwaje? 20. Ni sentensi ipi inawakilisha kauli ya kutendwa? SEHEMU B LUGHA VA KIFASIH1 21. "Uzi mwembamba unafunga dume kubwa". Kitendawili hiki kina maana gani? 22. "Usisahau ubaharia kwa sababu ya unahodha". Methali ambayo ina uhusiano na hii ni ipi kati ya hizi zifuatazo? 23. "Watoto wangu wote wamevaa hirizi nyeupe" Kitendawili hiki kina maana gani 24. Hali ya kumfanya mtu atii kila analoambiwa ina maana sawa na nahau ipi kati ya zifuatazo? 25. Ni muhimu kwa kila mtu kuwa mwangalifu kwa wanaojitangazia kutibu kisukari. Ni usemi upi kati ya ifuatayo ina maana sawa na "kuwa mwangalifu"? 26. "Mambo mema na mabaya hayafungamani", kifungu hiki cha maneno kinatoa maana ya methali ipi kati ya zifuatazo? 27. Tegua kitendawili kisemacho "Gari langu halitumii mafuta ya waarabu" 28. "Umejuaje kuwa mimi ni mgeni hapa?" methali ipi kati ya zifuatazo inawajibu swali hilo? 29. Juma alipumzika chini ya mti, alipoulizwa anafanya nini pale alijibu kuwa, "Navinjari to mwalimu". Jibu sahihi alilotakiwa kutoa ni lipi? 30. "Babu kafa kaniachia pete". Kitendawili hiki kina maana gani? SEHEMU C UFAHAMU Soma kwa makini habari ifuatayo kisha jibu maswali 31 - 40 kwa kuchagua herufi ya jibu lililo sahihi na kuandika katika karatasiyakoya kujibia. Umewahi kusikia viumbe wanaoitwa dinozo? Hawa ni wanyama ambao walikuwepo duniani zaidi ya miaka milioni 65 iliyopita. Wanasayansi wamegundua mabaki ya mafuvu na mifupa yao ardhini. Wanasayansi wamechunguza sana sababu za kutokomea kwa dinozo. Mpaka leo hii haijapatikana sababu rasmi ya tukio hilo. Hata hivyo, bado uchunguzi unaendelea kufanywa katika kutafuta sababu za kupotea kwa wanyama hao. Tanzania ni miongoni mwa nchi chache duniani zenye wanyama wa aina nyingi. Watalii wengi kutoka kila pembe ya dunia huja kuwaangalia wanyama hawa. Hali hiyo huongeza pato Ia taifa. Aidha, vitendo mbalimbali vinahatarisha usalama wa viumbe hao; kwa mfano makazi ya wanyama yanaharibiwa kwa kuchomwa misitu na kukata miti ovyo. Hali hii husababisha misitu kubaki vichaka tu, hivyo wanyama hukosa makazi na mwishowe hupotea. Vile vile binadamu huwinda wanyama kama tembo kwa ajili ya pembe zao. Sasa umefika wakati kwa kila mmoja wetu kukemea vitendo hivi. Wanyama na mimea ni urithi wa taifa letu. Ni fahari iliyoje kwetu kuwa navyo. Tusipokuwa waangalifu wanyama hao na mimea adimu kama mianzi vitatoweka kabisa. Vizazi vijavyo vitabaki kusimuliwa kama tunavyosikia kuhusu dinozo. MASWALI 31. Dinozo ni wanyama wenye sifa ipi kati ya hizi zifuatazo? 32. Kwa kuzingatia habari uliyosoma mambo mawili yanayoathiri ustawi wa wanyama ni yepi? 33. Sababu kubwa ya watu kuwinda na kuwaua ndovu ni ipi? 34. Kutokana na habari hii ni sababu ipi inayowafanya watalii kuja Tanzania? 35. Tanzania hupata faida gani kubwa kutokana na sekta ya utalii? 36. Mwandishi anatoa wito gani kwa jamii kuhusiana na usalama wa viumbe hai? 37. Athari zipi zinapatikana kutokana na kuchoma misitu? 38. Mwandishi anadai kuwa fahari ya taifa letu bi kuwa na vitu gani? 39. Kuna tofauti gani kati ya msitu na kichaka? 40. Kwa ujumla habari hii inahusu nini? SEHEMU D USHAIRI Soma shairi lifuatalo kisha jibu maswali 41 - 46 kwa kuandika herufi ya jibu lililo sahihi katika karatasi ya kujibia. Kasimama kizimbani, popo anatetemeka, Kuitwa mahakamani, popo kujibu shitaka, Atakiwa abaini, kwa ulimi kutamka, Ajitetee bayana, ni mnyama au ndege. Hakimu nashukuru, shitaka kunisomea, Sina jadi na kunguru, ila na Pundamilia, Mimi ni mnyama huru, amini ninakwambia, Tukidaiwa ushuru, kwa wanyama nalipia. Ni kweli popo napaa, na mabawa nimepata, Lakini mimi nazaa, hilo halina utata Kuwa ndege nakataa, sina undugu na bata Nakataa katakata, mimi si ndege nasema. Hakimu nathibitisha, kwa moyo wangu thabiti, Nazaa na kunyonyesha, vipi niwe msaliti, Wale wanaopotosha, niwaonyeshe matiti, Hakimu simama kati, nipatie kaki. MASWALI 41. Popo anakataa kuwa si ndege kwa sababu gani? 42. Katika ubeti wa pill popo anasema "sina jadi na kunguru", usemi "sina jadi" una maana gani? 43. Popo alitakiwa kujitetea bayana. Usemi "Kujitetea bayana" una maana gani? 44. Mstari wa mwisho katika kila ubeti wa shairi hill huitwaje? 45. "Kitendo cha kuzaa na kunyonyesha hufanywa na viumbe ambao ni " Neno linalokamilisha sentensi hiyo ni lipi? 46. Kichwa cha shairi hill chafaa kiwe kipi? SEHEMU E UTUNGAJI Umepewa habari yenye sentensi nne (4) zilizoaandikwa bila mtiririko sahihi wa mawazo katika swali la 47 - 50. Zipange sentensi hizo iii ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi A, B, C, na D. 47. Alipomaliza kusema hayo Mzee komba akauliza, "Tupande miti wakati inaota kwa uwezo wa Mungu?" 48. Mkutano ulipomalizika kila mtu alirejea nyumbani kwake akiwa na dhamira ya kupanda miti. 49. Bwana miti akasema "Yapasa kupanda miti kwa sababu matumizi yake yameongezeka sana siku hizi". 50. "Tusipopanda miti mipya tutaishiwa miti kabisa". Bwana miti alijibu. KISWAHILI 2010 SEHEMU A SARUFI Katika swali la 1-5 andika herufiya jibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia. 1. "Ukitaka cha mvunguni inama". Hii ni sentensi ya aina gani? 2. Katika neno "hatutakamilisha", kiambishi kinachoonesha nafsi ni kipi? 3. "Kampeni ya upandaji miti wilayani Kishapu ilifanikiwa sana na wananchi." Sentensi hii ipo katika kauli gani? 4. Kisawe cha neno "beseni" ni kipi? 5. Wingi wa sentensi isemayo, "Ubao umetumika" ni ipi? 6. Katika sentensi ifuatayo, ni neno lipi limetumika kama kiwakilishi? "Huu ni wa maziwa." 7. Ubegete ameshinda kondeni akiamia ndege. Kielezi katika sentensi hii ni kipi? 8. Mwalimu alikuwa anatunga mtihani. N eno "anatunga" limetumika kama aina ipi ya kitenzi? 9. Alfajiri na mapema tuliondoka ukumbini. Mzizi katika neno lililopigiwa mstari ni upi? 10. Kinyume cha neno "Tandika" ni kipi? 11. Umoja wa sentensi "Machungwa mabichi yana ladha ya uchachu” ni... 12. Fundi atengenezaye herein, pete an mikufu huitwaje? 13. "Zena amemnunulia mwanae kizibao” limetumika kwa maana ipi? 14. Neno "kindumbwendumbwe” lina silabi ngapi? 15. Watalii wengi hufika Tanzania ili .mlima Kilimanjaro. Ni neno lipi linalokosekana kukamilisha sentensi hiyo? SEHEMU B MSAMIATI Katika swali la 16 - 25 andika herufiyajibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia. 16. Baada ya mshenga kutoa wageni waliondoka na kurudi makwao. Chagua neno sahihi kati ya maneno yafuatayo ili ukamilishe sentensi hiyo. 17. Neno "msimu” lina maana gani? 18. Yule bwana amelima kwa bidii na amevuna . . mwingi sana. 19. Kisawe cha neno ”hitimisho” ni kipi? 20. Katika vifungu vya maneno vifuatavyo ni kifungu kipi chenye maneno yanayoshabihiana? 21. Kinyume cha neno "shaibu" ni kipi? 22. Ng'ombe dume aliyeachishwa ambaye hutumika kwa kufanya kazi kama vile kuvuta mkokoteni au plau huitwaje? 23. "Mfanyabiashara alipatwa na nuksi kubwa baada ya bidhaa zake kuungua moto". Ni neno lipi linalandana na neno "nuksi" kati ya yafuatayo? 24. Kisawe cha neno "runinga" ni kipi? 25. Kinyume cha neno "kunyanyapaa" ni kipi? SEHEMU C METHALI, NAHAU NA VITENDAWILI Katika swali la 26 - 30 Andika herufiyajibu lililo sahihi katika karatasi yakoya kujibia. 26. Wanafunzi wa darasa la tano wanafanya kazi zote bega kwa bega. Neno lililopigiwa mstari lina maana gani? 27. Kifungu cha maneno kisemacho, "Anayefanya juhudi katika masomo au jambo Iolote hufanikiwa" kinashabihiana na methali ipi kati ya zifuatazo? 28. Baada ya John kupanda cheo, alimtilia Sara kitumbua chake mchanga. Maana ya msemo "kutilia kitumbua mchanga" ni upi? 29. Wanafunzi wa darasa Ia saba wamesoma kwa makini hadi wamehitimu masomo yao. Ni methali ipi kati ya zifuatazo inasadifu sentensi hiyo? 30. "Mwana wa ndugu kirungu, mjukuu mwanangwa." Methali ambayo haifanani na mehtali hii kati ya hizi zifuatazo ni ipi? 31. Kifungu kipi cha maneno kinakamilisha methali ifuatayo? "Ikiwa kilemba kimelowa..." 32. Aisatu hujulikana sana kwa "majina ya lakabu". "Majina ya lakabu" maana yake ni ipi? 33. Binetuu anawachukua wazazi wake. "Kuwachukua" lina maana gani? 34. Mama Chakupewa alipotokeza tu sebuleni, wapangaji wenzake wote yyaliangua-kichelo Msemo uliopigiwa mstari una maana gani? 35. Kasanga alitegewa kitendawili na babu yake na akakitegua kwa kusema "Mwangwi". Kitendawili hicho ni kipi? SEHEMU D UFAHAMU Soma kwa makini kifungu cha habari kifuatacho kashajibu swali la 36 - 45 kwa kuandika herufi yajibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia. Hapo kale watu walikuwa wakila vyakula vibichi. Kadri miaka ilivyokwenda mbele watu igundua matumizi ya moto kwa njia ya kupekecha vijiti. Ugunduzi huu uliwasaidia kuanza kuchoma nyama na kupika vyakula. Kadri miaka ilivyoendelea ndivyo maendeleo yalivyopatikana. Baada ya watu kupata moto kwa kupekecha vijiti, waligundua pia njia nyingine. Njia iliyotumiwa na watu wengi ni ile ya kutumia viberiti. Hivyo waliweza kutumia majiko ya aina mbalimbali kama jiko la mafuta ya taa, jiko la mkaa, jiko la gesi na waliweza kupika kwa kutumia kuni. Kazi ya kupika ilikuwa rahisi baada ya ugunduzi huu, walianza kula vyakula vya mchanganyiko. Walitambua kwamba vyakula vinavyopikwa kwa mchanganyiko kama mseto na vinginevyo vina manufaa makubwa. Vyakula hivi hujulikana kama mlo kamili. MIO kamili huimarisha siha ya mlaji. Matumizi ya viberiti hayakuishia katika kuwasha majiko. Viberiti hadi leo vinatumika kuwashia kandili, karabai, vibatari na mishumaa ili kuweza kupata mwanga katika nyumba zetu. Tunatumia viberiti kupata moto tunaoutumia kuchoma mabiwi na takataka nyingine ili kuondoa uchafu katika mazingira yetu. Moto pia huweza kupatikana kwa njia ya umeme ambao aghalabu hutumika katika sehemu za miji. Ugunduzi wa umeme umesaidia katika shughuli za upishi. Huwawezesha akina mama kupika vyakula kwa kutumia majiko ya umeme. Hupika vyakula vingi kwa urahisi na kwa haraka zaidi. Hali hii imeleta uwezekano wa kupika vyakula vya mchanganyiko yaani mlo kamili. Vyakula hivi huwa na mchanganyiko wote, yaani vyakula vinavyotia nguvu na joto mwilini, vyakula vya kulinda mwili na kujenga mwili. Watu walao mlo kamili kwa nadra huwa goigoi. Moto pia huweza kupatikana kwa kutumia lensi, kwani lensi ikielekezwa kwenye mwanga wa jua kwa muda mrefu basi karatasi itakayowekwa chini yake hushika moto. Faida za moto ni nyingi. Hutupa mwanga wakati wa usiku, hutumika katika kuendesha mashine na mitambo mbalimbali. Kama moto usingegunduliwa, maisha ya watu yangekuwa duni. Aidha, moto una madhara mbalimbali usipotumika vema. Madhara haya hutukumbusha kwamba "uzuri wa mkakasi, ndani kipande cha mti". Athari zake ni kama kuunguza majengo na mitambo, majengo yanapoungua wakati mwingine husababisha maafa ya watu kuungulia ndani ya majengo na mali zao. Kuepuka madhara na hasara zitokanazo na moto hatuna budi kuwa waangalifu. Tuweke viberiti, mishumaa na taa mbali na watoto; tuunganishe nyaya za umeme kwa kutumia wataalamu, warina asali kufuata njia za kisasa kwa kutumia mavazi ya kitaalamu, kulima kwa kuepuka kuchoma mapori na mashamba. Tusipochukua tahadhari hiyo tutajuta, kwani "Hamna! Hamna! Ndimo mliwamo". MASWALI 36. Kichwa cha habari hapo juu ni kipi? 37. Neno "Mseto" lina maana sawa na kifungu kipi cha maneno kati ya vifuatavyo? 38. "Watu walao mlo kamili kwa nadra huwa goigoi". Sentensi hii ina maana ipi? 39. "Hamna! Hamna! Ndimo mliwamo". Methali hii ina maana gani? 40. Neno "siha" kama lilivyotumika katika kifungu cha habari Ilina maana gani? 41. Kwanini watu wa kale walikula vyakula vibichi? 42. MIO kamili huwa na mchanganyiko wa vyakula vyenye virutubisho mwilini. Vyakula hivyo ni vipi? 43. Moto una faida nyingi katika maisha ya kila siku. Taja faida tatu za moto. 44. kama ilivyotumiwa na mwandishi, methali inayosema "Uzuri wa mkakasi ndani kipande cha mti" ina maana gani? 45. Madhara yasababishwayo na moto kama yalivyoelezwa kwenye kifungu cha habari ni yapi? SEHEMU E UTUNGAJI Umepewa insha yenye sentesi tano (5) zilizoandikwa bila mtiririko sahihi wa mawazo. Zipange sentensi hizi ili ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi A, B, C, D na E ili ujibu maswali 46 - 50. 46. Ili mpate kuyajua ni lazima mjifunze kwa bidii na maarifa muweze kufaulu mitihani yenu. 47. Ninyi ni vijana wadogo bado wenye matumaini ya kupata maendeleo katika maisha yenu ya baadaye. 48. Endeleeni kusoma na kujifunza kwa bidii kwani Elimu ni bahari, haina mwisho. 49. Elimu ndiyo itakayoweza kuwafungulia njia za kupata maendeleo hayo, katika safari hii ya kuelimika zaidi. 50. Katika safari hiyo ya kuelimika zaidi, utagundua kuwa yapo mambo mengi muhimu ambayo hamyajui. KISWAHILI 2009 SEHEMU A SARUFI Etika swali la 1 - 15 andika herufi yajibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia. 1. Angeliamka mapema asingeliachwa na ndege. Kiambishi cha masharti katika sentensi hiyo ni kipi? 2. Neno lipi kati ya haya yafuatayo halina uhusiano na mengine? 3. Alisema hajisikii vizuri. Kauli halisi ya sentensi hii ni ipi? 4. Neno lipi linakamilisha sentensi ifuatayo: Kama kazi hii ingalifanywa na mtu mmoJa ... ... ... kumaliza. 5. Chakula hiki si kibayahakina viungo. Neno linalokosekana katika sentensi hii ni lipi? 6. "Shule imefunguliwa” ukanushi wa sentensi hii ni ipi? 7. Kiranja mkuu wa shule . . . . . . . . mawazo ya wanafunzi wenzake katika kikao cha uongozi wa shule. Neno lipi linakamilisha sentensi hiyo? 8. Wingi wa neno "kuku” ni upi? 9. Kayumba na Neema wanaosha vyombo. Neno "vyombo” limetumika kama aina gani ya neno? 10. "Padri Joni anapenda sana kucheza mpira wa kikapu." Sentensi hii ipo katika nafasi ipi? 11. Sentensi ipi kati ya zifuatazo ipo katika kauli taarifa? 12. Buibui, inzi, mbu, papasi na tandu kwa neno moja huwa wanaitwaje? 13. "Mzee Masanja amempa binti yake mume." Sentensi hii ina maana ipi? 14. Katika sentensi zifuatazo ni ipi iliyo sahihi kimuundo? 15. Ni kipi kinyume cha neno "kaditama?" SEHEMU B MSAMIATI Katika swali la 16 - 25 andika herufiyajibu lililo sahihi latika karatasiyakoya kujibia. 16. Wakati akiendesha baiskeli yake, magurudumu yalimrushia tope kwa kuwa hayajakuwz na . . . . . . la kuzuia. Sentensi hii inakamilishwa na neno lipi? 17. Mtu mwenye elimu ya mienendo ya nyota anaitwaje? 18. "Mnyamavu" ni neno lenye maana sawa na kifungu kipi cha maneno kati ya vifuatavyo? 19. Kifungu cha maneno chenye maana sawa na neno "mwafaka" ni kipi? 20. Wanakijiji wa Songambele walifanya kazi zao kikoa. Neno "kikoa" lina maana gani? 21. Siku hizi bei ya mafuta imekithiri. Neno "kithiri" limetumika kwa maana ipi? 22. Mtu anayefanya kazi ya kuhifadhi vitabu katika maktaba na kuviazimisha kwa wasomaji anaitwaje? 23. Alionesha ......... kuwa Diengi ndiye aliyehusika na uuzaji wa madawa ya kulevya. Neno linalokamilisha sentensi hii kwa usahihi ni lipi? 24. Kifungu cha maneno kati ya vifuatavyo chenye maana sawa na neno "nishati" ni kipi? 25. Neno "kuengua" lina maana gani? SEHEMU C METHALI, NARAU NA VITENDAWILI Katika swali la 26 - 35 andika herufi ya jibu sahihi katika karatasiyakoya kujibia. 26. Methali isemayo, "Mti hawendi ila kwa nyenzo” iko sawa na methali ipi kati ya hizi zifuatazo? 27. Wanakijiji walimtaka yule mwizi asalimu amri.” Kusalimu amri” ni usemi wenye maana ipi? 28. Kitendawili kisemacho. "Mbwa mwitu wamezunguka kumlinda” hutenguliwa kwa jibu lipi? 29. Methali inayopingana na methali isemayo, "Haraka haraka haina Baraka” ni ipi? 30. Wanafunzi wengi wamepigwa na butwaa baada ya kuyaona matokeo yao ya mtihani wa Darasa la Saba. "Kupigwa butwaa” ni msemo wenye maana ipi? 31. Mwita anataka mtoto wake awe na "maadili mema” hadi ukubwani. Methali ipi ataitumia kuhimiza tabia hiyo? 32. Kiangazi chote hulala usingizi; yakija masika nakesha. Maana ya kitendawili hiki ni ipi? 33. Moto alioniachia babu yangu huzima ninapokwenda kulala na huwaka tena mara ninapoamka. Kitendawili hiki kina maana gani? 34. ”Chemsha bongo.” Usemi huu una maana gani? 35. Methali isemayo, "Avumaye baharini papa kumbe wengine wapo”, ina onyo gani? SEHEMU D UFAHAMU Soma kwa makini shairi lifuatalo kisha jibu maswali (36 - 45) kwa kuandika herufi ya jibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia. Leo ninawasilisha, haya utakayosikia, Wazazi mmetuchosha, haki zetu mwafukia, Kwa kweliyametuchosha, tumekwisha shitukia, Twaomba mtukidhie, haki hizi za watoto. Asubuhi twaondoka, shuleni kujisomea, Na shuleni tukifika, usafi ni mazoea, Vinywa vyetu vinanuka, njaa kwetu mazoea, Twaomba mtukidhie, haki hizi za watoto. Mtazame mama yangu, anang'ara kwa mapambo, Tazama mavaziyangu, maduaraya matobo, Kupendeza baba yangu, utadhani ni mgambo, Twaomba mtukidhie, haki hizi za watoto, Amanda wa kijijji, sareya shule hadithi, Matekenya miguuni, elimu kwake hadithi, Baadayeya kilabuni,jana njaa kalalia, Hana mbele wala nyuma, haki atapata lini? Walimu nao shuieni, sare wasisitizia, Usafi nao mwilini, kwa hakika wakazia, Tupate wapi sabuni,jana njaa kalalia, Wazazi muwajibike, haki zetu tupatiwe. Shuleni nako kifika, elimu wapulizia, Viboko navyo kulika, matakoni vyatulia, Nyumbani nako kufika, mama hataki tulia, Twaomba kupumzika, hakiyetu ya msingi. Mwalimu acha viboko, nikanye takusikia, Adhabu bila viboko, ukijali takufaa, Vifaa liwe tamko, shuleni kujisomea, Elimu ni haki kwetu, tupate iliyo bora. Haki kwa wote sikia, wakubwa nao watoto, Chakula bora sikia, afya zetu kuwa moto, Ubaguzi kususia, wasichana ni watoto, Haki msizitoweshe, kwetu taifa la kesho. Njaa inatusumbua, ajira twazitafuta, Waajiri wasumbua, kwao utu wamefuta, Jamani watuumbua, kwa nini kututafuta, Chungulia kwajirani, haki zetu hatupati. Mwishoni nimefikia, badoo ninawakumbusha, Heri ninawatakia, huduma kuimarisha, Unapopata rupia, umgawie na ngosha, Ukijalifamilia, mungu atakubariki. MASWALI 36. Kichwa kinachofaa kwa shairi hili ni kipi? 37. Neno "kizingiti" kama lilivyotumiwa na mshairi lina maana sawa na neno lipi kati ya yafuatayo? 38. Vina katika ubeti wa Sita ni: 39. Haki wanazozidai watoto katika shairi hili ni zipi? 40. Neno "kuwasilisha" kama lilivyotumiwa na mwandishi lina maana gani? 41. Mshairi anaposema, "elimu kwake hadithi" ana maana gani? 42. Mtunzi anaposema "hana mbele wala nyuma”, msemo huo una maana ipi? 43. Katika ubeti wa nane, mwandishi anashauri nini kuhusu elimu kwa jinsia zote? 44. Kuna mizani mingapi katika kila mstari wa shairi? 45. Kwa ujumla shairi hili linamshauri kila mtu afanye nini? SEHEMU E UTUNCAJI Umepewa insha yenye sentensi tano (5) zilizoandikwa bila mtiririko sahihi wa mawazo. Zipange sentensi hizo ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi A, B, C, D na E ili kujibu swali 46 - 50. 46. Baadhi ya mambo yanayochangia kuenea kwa gonjwa hatari la UKIMWI ni kuchangia vifaa vya kutogea masikio, vifaa vya kutahiri, ngono isiyo salama na kutoka kwa mama mjamzito kwenda kwa mtoto wakati wa kujifungua na kunyonyesha. 47. Dalili za gonjwa hili ni homa za mara kwa mara, kupungua uzito, upungufu wa damu mwilini, ukurutu, kuvimba matezi na kuharisha. 48. Ili kuzuia gonjwa hili la hatari lisienee hatuna budi kuepuka kuchoma sindano za mitaani zisizochemshwa, kutochangia vifaa vya kutogea masikio na kutahiria, kuwa mwaminifu na kusubiri, hivyo Tanzania bila UKIMWI itawezekana. 49. UKIMWI ni ugonjwa hatari usiokuwa na tiba wala kinga. 50. Madhara yatokanayo na ugonjwa huu ni kudidimia kwa uchumi kwa sababu ya kupoteza nguvu kazi ya taifa, umasikini na kuongezeka kwa watoto yatima. KISWAHILI 2008 SEHEMU A SARUFI Katika swali la 1 - 15 andika herufiyajibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia. 1. Neno lipi linakamilisha sentensi isemayo, "Humu . . alimoingia yule nyoka" 2. Badala ya kusema, "mimi sijambo". Ninaweza kusema, "mimi .. kamilisha sentensi hiyo kwa neno sahihi. 3. Ala kumbe! Kihisishi ni kipi kati ya yafuaatayo? 4. Kisawe cha neno kati ya yafuatayo? 5. Mtoto aliyepotea amepatikana. Hii ni aina ipi ya sentensi? 6. Yule msichana anaimba vizuri. Neno lililopigiwa mstari limetumika kama aina ipi ya maneno? 7. Sentensi ipi kati ya zifuatazo ipo katika kauli halisi? 8. Nomino inayotokana na kitenzi "Vaa" ni ipi? 9. Neno lipi linakamilisha sentensi isemayo, Timu ya Taifa ingalicheza vizuri . mchezo A. ingelishinda B. ingeshinda C. ingashinda D. ingalishinda E. itashinda 10. Siku ya Mei Mosi wafanyakazi walipita mbele ya Waziri Mkuu wakishikilia ......... yenye maneno ya kuhimiza kazi. Neno lipi linakamilisha sentensi hiyo? 11- "Nguo yangu imechafuka sana.” Wingi wa sentensi hii ni upi? 12. Lipi kati ya maneno yafuatayo halina uhusiano na mengine? 13. Samaki, dagaa na nyama. Kwa neno moja huitwaje? 14. Sentensi isemayo, ”ltakapofika mchana .... kuondoka” inakamilishwa kwa usahihi na neno lipi kati ya yafuatayo? 15. Kinyume cha neno "duni” ni kipi? SEHEMU B MSAMIATI Katika swali la 16 - 25 andika herufiyajibu lililo sahihi katika karatasi yakoya kujibia. 16. Mzee Jumbe aliwapa wanae mavvaidha juu ya maisha yao. Neno lilipogiwa mstari lina maana gani? 17. Mtu anayesimamia kazi za shambani huitwaje? 18. Pondamali ni kijana mwenye hila sana. Kisawe cha neno ”hila l'ni kipi? 19. "Jioni bahari ilikuwa . kwa hiyo wavivu walivua samaki bila wasiwasi. Neno lipi linakamilisha sentensi hiyo kwa usahihi? 20. Mama alijifunza kuendesha gari lakini bado hajafuzu. Neno "Hajafuzu” lina maana ipi kati ya zifuatazo? 21. Mchanganyiko wa mboga au matunda unaoliwa bila kupikwa huitwaje? 22. Kabwela alimsihi baba yake ampe nauli akatembelee mbuga za wanyama. Neno sihi kama lilivyotumika katika sentensi hiyo lina maana gani? 23. Neno lipi linakamilisha sentensi isemayo, "Anapenda kukaa bure ... ...... ana nguvu nyingi”. 24. Kijana yule anafanya kazi zake kwa makini. Badala ya kutumia neno "makini” ungeweza kutumia neno lipi kati ya yafuatayo? 25. "Timu ya mieleka ya mkoa wa Rukwa ilikuwa na pambano ......... ya timu ya mieleka ya mkoa wa Mtwara”. Kamilisha sentensi hiyo kwa neno mojawapo kati ya yafuatayo: SEHEMU C METHALI, NAHAU NA VITENDAWILI 26. "Kidole kimoja hakivunji chawa”. Methali hii ina maana sawa na methali ipi kati ya zifuatazo? 27. Kifungu kipi cha maneno hukamilisha kitendawili kifuatacho kwa usahihi? 'Watoto wa binadamu . . . . . . 28. "Sina hali”. Nahau hii ina maana gani? 29. "Udongo uwahi ungali maji". Methali hii ina maana gani? 30. Tatizo la ufisadi limeota mizizi katika nchi yetu. "Kuota mizizi" ni usemi wenye maana gani? 31. "Mgonjwa aendapo hospitalini na kutopata matibabu hadi atoe chochote kwa mhudumu wa afya." Nahau ipi inasaidia hali hiyo? 32. Katika methali zifuatazo ni methali ipi ambayo haifanani na zingine? 33. Neno lipi linakamilisha methali isemayo: Ndugu chungu jirani ? 34. Tegua kitendawili kisemacho "Ajihami bila silaha" kwa kuchagua neno sahihi kati ya yafuatayo: 35. Tegua kitendawili kisemachö "Maskini huyu hata umchangie namna gani haridhiki", kwa kuchagua neno moja kati ya yafuatayo: SEHEMU D UFAHAMU Soma habari ifuatayo halafu jibu maswali (36 - 45) kwa kuandika herufi sahihi katika karatasi yakoya kujibia. Kijana Makubwa alikuja juu katika kushikilia tabia yake ya ufedhuli na maringo. Kwa kuwa alikuwa msomi, hakudiriki kufumbata jembe na kulima shambani pamoja na wazazi wake. Yeye katika mawazo yake aliona kuwa alihusika na kwenda mjini kutafuta kazi ya ukarani. Aidha Makubwa alikuwa akiwaudhi wengi kijijini, alipozungumza nao aliwamung'unyia Kiswahili kwa majivuno na ukaidi sana. Matendo na mwenendo wake vilionesha kuwa alijiona mtu wa maana sana kuliko wengine na alijawa na mawazo kemkem ya ukubwa wa madaraka. Shuleni kwake, kama kijijini, Makubwa alipenda maisha ya huria, kutenda Iolote alilotaka akilini mwake. Mara nyingi alikuwa kiguu na njia, hakupenda kutulia mahali pamoja. Alikuwa hajali sheria, aliamka, alisomea alipopataka na kujivalia alivyotaka. Yeye kila wakati alipenda starehe. Kazi alikuwa hafanyi, hata akazoea kusingizia mvua kwa kila wajibu ambao hakuutimiza. Lakini siku zake arobaini ziliwadia, shule haikuweza kuvumilia tena kijana Mkubwa aliyependa huria kuliko nidhamu iliyokubalika na wengi. Shuleni kwake alipigwa kalamu nyekundu. Bila shaka kijijini walianza kusema. "Aliye juu mngoje chini". Wengine walisema "msiba wa kujitakia hauna kilio". MASWALI 36.Makubwa hakuweza shughuli za kilimo kwa sababu 37.Makubwa alikuwa na tabia gani ambayo haikupendeza huko shuleni? 38. Mwandishi anasema, "alijawa na mawazo kemkem ya ukubwa wa madaraka." Maana ya neno kemkem ni ipi? 39.Kutenda mambo kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa. Neno gani kati ya yafuatayo linasadifu sentensi hiyo? 40. Ni kipi kilichomsibu Makubwa baada ya shule kushindwa kuvumilia tabia yake? 41. Mwandishi anazungumzia nini juu ya wanafunzi kutimiza wajibu wao? 42. Kwa maoni yako kichwa cha habari hii kinaweza kuwa kipi? 43. 'Msiba wa kujitakia hauna kilio". Usemi huu una maana gani? 44. Fundisho unalolipata katika habari hii ni "wanafunzi tuwe na: 45. Kifungu kipi cha habari hukamilisha sentensi isemayo "Makosa ya kutotimiza wajibu shuleni yakijitokeza mara nyingi ... ... ... " SEHEMU E UTUNGAJI Umepewa insha yenye sentensi tano (5) zilizoandikwa bila mtiririko sahihi wa mawazo. Zipange sentensi hizo ili ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa A, B, C, D na E ili kujibu maswali 46 - 50. 46. Tutaendelea kusaidiana na kushirikiana katika mambo mbalimbali hasa katika shughuli za kiuchumi, kielimu na kijamii. 47. Kumekuwa na mwingiliano wa tamaduni za kigeni katika nchi zetu mfano mavazi, lugha, ngoma, nyimbo, mila, na desturi. 48. Lakini katika kijiji chetu cha Tupendane tumeamua kudumisha upendo na ushirikiano miongoni mwetu. 49. Baadhi ya misingi mizuri ya maisha imevurugwa. 50. Mambo mengi yaliyotokea na yanayoendelea kutokea yameathiri sehemu ya utamaduni wetu. KISWAHILI 2007 SEHEMU A SARUFI Katika swali Ia 1-15 andika herufiyajibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia. 1. Mvutano kati ya wanakijiji na viongozi wao ulikuwa haujapatiwa neno lipi linakamilisha sentensi hii? 2. Maneno "mrefu, mweusi, mwerevu na mpole" yakitumika pamoja na majina hufanya kazi gani? 3. Sentensi ipi kati ya zifuatazo ni umoja wa sentensi "Bakari amehamisha mizinga ya nyuki kutoka shambani mwake"? 4. Katika sentensi ifuatayo ni neno lipi limetumika kama kiwakilishi "Yule ni mnene kupita kiasi". 5. Kinyume cha neno ughaibuni ni kipi? 6. Sentensi ipi kati ya hizi zifuatazo ipo katika kauli taarifa? 7. Kipi ni kinyume cha neno gwiji? 8. Katika neno "sitakuwepo" kiambishi kinachoonyesha ni kipi? 9. "Mvvanafunzi aliyefaulu vizuri atapewa tuzo". Kishazi tegemezi katika sentensi hii ni kipi? 10. Neno lipi limekosekana kuikamilisha sentensi ifuatayo kwa usahihi? "Mtoto haandiki . . . . . . . . . . . hasomi". 11. "Ukifanya vizuri utapongezwa". Sentensi hii ni ya aina gani? 12. "Nyumba ya Amini imejengeka vizuri". Sentensi hiyo ipo katika kauli gani? 13. Unaponyumbulisha neno apiza unapata nomino ipi? 14. Neno lipi ni tofauti na maneno mengine kati ya yafuatayo? 15. "Uji huu una sukari na maziwa". Ukanushi wa kauli hii ni upi? SEHEMU B MSAMIATI Katika swali 16 - 25, andika herufiya jibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia. 16. Neno lenye maana sawa na neno "mawio" ni lipi kati ya yafuatayo? 17. Watu waliokusanyika kwa pamoja ili kuabudu huitwaje? 18. Selina alitumwa sokoni kununua mbuzi ya kukuna nazi. Neno "mbuzi" limetumika kwa maana ipi? 19. Neno lipi kati ya maneno yafuatayo lina maana sawa na neno "shaghalabaghala"? 20. Neno lipi kati ya maneno yafuatayo halilandani na mengine? 21. "Elimu maalumu inayohusiana na matukio na mambo yaliyopita". Neno lipi kati ya maneno yafuatayo lina maana sawa na kauli hii? 22. Mtu anayeacha kazi ya ajira baada ya kutimiza umri uliowekwa kutokana na kanuni anaitwaje? 23. Ni kipi kinyume cha neno "barubaru"? 24. Neno lipi kati ya maneno yafuatayo lina maana sawa na neno "zuzu"? 25. Mahindi, maharage, ufuta, michungwa, migomba na mihogo. kwa neno moja ni SEHEMU C METHALI, NAHAU NA VITENDAWILI 26. Maneno yapi yanakamilisha methali ifuatayo kwa usahihi? Tamu ya sukari . . . . . . . . . 27. Methali isemayo "kila mwamba ngoma, ngozi huvutia kwake" ina maana gani? 28. Kibarua chake kimeota nyasi. Maana ya maneno "kuota nyasi" ni ipi? 29. Babu huanika sembe usiku, asubuhi huiondoa. Kitendawili hiki kina maana ipi? 30. Mtoto huyu anamlanda baba yake. "Anamlanda baba yake" ni usemi wenye maana gani? 31. Ni kifungu kipi cha maneno hukamilisha methali ifuatayo kwa usahihi? Mtafunwa na nyoka akiona . . . . . . . 32. Mtoto umleavyo, ndivyo akuavyo". Methali hii ina maana sawa na methali ipi kati ya zifuatazo? 33. Wageni walipofika nyumbani kwake aliwapokea kwa mikono miwili. "Kupokea kwa mikono miwili" ni usemi wenye maana gani? 34. Akitembea huringa hata akiwa hatarini. Kitendawili hiki kina maana gani? 35. Kitendawili kisemacho "wana wa mfalme ni wepesi sana kujificha" kina maana gani? SEHEMU D UFAHAMU Soma kwa makini kifungu cha habari kishajibu maswali 36 — 45 kwa kuandika herufiyajibu lililo sahihi katika karatasi yakoya kujibia. Lugha iwe ya mazungumzo au ya maandishi ni chombo cha mawasiliano. Katika mawasiliano kuna pande mbili. Chanzo na kikomo. Chanzo niyule anayeandika na kusema pamoja nayote atakayoandika au atakayosema. Kikomo ni msemaji au msikilizaji, mtu ambaye anaandikiwa au kusemeshwa. Kwa msomaji au msikilizaji inatakiwa apate maana na ujumbe muda mfupi iwezekanavyo, achague, azingatie na hatimaye aweze kuitumia katika kuyajadili maisha yanayomzunguka. Hivyo katika uwanja wa uandishi, ni wajibu wa kila mwandishi kuwafikiria wale awaandikiao. Ni vema kuelewa kuwa tunawaandikia binadamu. Kila binadamu amezaliwa pekee na kujaliwa kukubaliana na mazingira tofauti. Katika kuwatambua wasomaji wa vitabu tutakavyoandika ni lazima kufikiria mazingira waliyo nayo, yaani vitabu vyetu vya kiada vioneshe uhalisi wa maisha ya wasomaji. Kwa maneno mengine vitabu hivyo vifikirie mahitaji na matakwa ya wasomaji wake. Ingawaje katika somo Iolote lile, maarifa na stadi zaweza kuwa zilezile kwa aina moja ya wanafunzi. Lakini kiwango na Nyanja za kutolea maudhui hayo, misimamo na tathimini zake zitatofautiana kufuatana na hali ya kisiasa, kijamii na kiuchumi ya nchi ambazo mwanafunzi huyo anaishi. Kwa hiyo mwandishi, lazima afikirie hayo yote wakati anapotarajia kuandika kitabu cha kiada. MASWALI 36. Pande kuu za mawasialiano ni 37. Msomaji asomapo kitabu cha kiada azingatie nini? 38. Neno "hatimae" kama lilivyotumika katika kifungu hiki lina maana sawa na neno lipi kati ya yafuatayo? 39. Katika kifungu cha habari ulichosoma maneno "uwanja wa mwandishi" yametumika kwa maana ipi? 40. Wajibu mkubwa wa mwandishi ni upi? 41. Madhumuni ya kitabu cha kiada ni muhimu kwa msomaji kwa sababu gani? 42. Vitabu vinatakiwa vioneshe uhalisi wa msomaji. Sentensi hii ina maana gani? 43. Mambo ambayo ni muhimu kuzingatia katika uandishi ni yapi? 44. Kitabu cha kiada. Hiki ni kitabu gani? 45. Kichwa cha habari hii kinachofaa ni kipi? SEHEMU E UTUNGAJI Umepewa insha yenye sentensi tano (5) zilizoandikwa bila mtiririko sahihi wa mawazo. Zipange sentensi hizo ili ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi A, B, C, D na E ili ujibu maswali 46 - 50. 46. Baada ya kusubiri kwa nusu saa, basi liliwasili na nikapanda kwenda Bunda. 47. Abiria wo?e walishuka kutoka kwenye gari moshi. 48. Lilipowasili mjini Mwaza, gari moshi lilisimama taratibu na kutangaza kuwa hapo ndipo ulikuwa mwisho wa safari yake. 49. Nami nilishuka na kwenda moja kwa moja hadi kwenye kituo cha mabasi. 50. Mimi na abiria wenzangu tulisafiri kwa amani na kufika Bunda salama jioni. KISWAHILI 2006 SEHEMU A SARUFI Katika swali la 1-15 andika herufi yajibu lililo sahihi katika karatasiya kujibia. 1. Huyu ......... mtoto aliyekuwa amepotea. 2. Neno lipi ni kinyume cha neno 'Adili"? . 3. "Ala kumbe! Ameondoka leo asubuhi”. Kihisishi ni kipi kati ya maneno haya? 4. Kisawe cha neno shaibu ni . 5. Neno "MBWA” lina silabi ngapi? 6. Kipi kinyume cha neno aghalabu? ...... 7. Kitoto hiki kinacheza kitQtQ. Neno lililopigiwa mstari limetumika kama ... 8. Shule ile imeendelea ingawa haina umeme. Sentensi hii iko katika aina ipi ya tungo? 9. Sikuweza kutambua ni nani amelala kitandani kwa sababu alijifunika shuka . . . . . . . 10.Neno "Vibaya” katika sentensi isemayo "Vibaya pia vinanunuliwa” limetumika kama aina ipi ya maneno? 11. Mkutano kati ya Viongozi wa DECI na Serikali ulikuwa haujapatiwaNeno lipi linalokamilisha sentensi hii? 12. 'Salama na Samina wanapendana sana". Sentensi hii ipo katika kauli ipi? 13. Katika neno "tutakuja” kiambishi cha wakati ni ......... 14. Neno ”MWALIMU” lipo katika upatanisho wa ngeli ya aina gani? 15. Wingi wa sentensi ifuatayo ni ipi? mti huu unaharibu mazingira SEHEMU B MSAMIATI 16. Mzee Mwendapole aliwapa wanaemawaidha juu ya maisha ya baadaye. Neno lililopigiwa mstari lina maana gani? 17. Neno lenye maana sawa na "mawio” ni lipi kati ya yafuatayo? 18. Mwl. Juma alinunua shati dukani. Neno lililopigiwa mstari lilmetumika kama aina gani ya maneno? 19. Mtu anayesimamia kazi za shambani anaitwaje? 20. Jina analotumia mjomba kumwita mtoto wa dada yake ni: 21. Kipindi cha muda wa mika mia huitwaje? . 22. Kutembea kwa matao ni kutembea kwa ......... 23. Nimetumwa ujumbe lakini sijapata mwitiko wowote. Neno mwitiko lina maana sawa na 24. Maelezo gani kati ya haya yanatoa maana ya neno "Mseja . 25. Neno lipi linakamilisha sentensi isemayo, "Anapenda kukaa bure ......... ana nguvu nyingi?". SEHEMU C METHALI, NARAU NA VITENDAWILI 26. Moja kati ya Methali zifuatazo haihimizi watu kujiendeleza kielimu. Methali hiyo ni ipi? 27. Kinyume cha nahau "Kata tamaa ni 28. Ana mkono wa birika 29. Kitendawili kipi kati ya hivi jibu lake siyo kinyonga? 30. ”Chungu cha mwitu hakipikiwi wapishi wake wakaiva” jibu la kitendawili hiki ni ... ... ... 31. "Mtu akifanya kazi yake bila umakini mambo hayatakuwa mazuri, itamlazimu apokee matokeo mabaya ya mambo hayo". Maelezo hayo ni sawa na maana ya methali isemayo 32. Kifungu kipi kinafaa kumalizia methali? Jina jema ......... 33. Nini maanaya Nahau "Ku iga chuku" 34. Tegua kitendawiYhiki. Nina kitand changu cha Mkangashale mwana wa halali aende akalale: 35. Walipofika mahakami kusikiliza kesi-ya ufisadi walitulia sana ili wasikie vizuri na kuelewa zaidi. Maneno yaliyopogiwa mstari yanawakilisha nahau isemayo: 37. Mstari wa pili katika kila ubeti wa kwanza una jumla ya mizani 38. Mstari wa nne katika kila ubeti wa shairi huitwa: 39. Katika ubeti.wa pili Msanii anasema "Waliosoma vyuoni, hawachoki kuuliza." Maneno haya yanatuaSä kuwa . 40. Neno "adhiri" kama lilivyotumiwa na mtunzi lina maana ya . 41. Neno "Misuli" katika ubeti wa tatu lina maana ya: 42. Katika ubeti wa tatu tunajifunza kuwa ni aibu .. 43. Jambo muhimu linalozungumzwa na msanii katika shairi hili ni: 44. "EIimu pana ajabu” maneno haya yana maana kuwa elimu 45. Pendekeza kichwa cha habari cha shairi kutoka katika nahau hizi: SEHEMU E UTUNGAJI Panga sentensi hizi Ili ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi A, B, C, D na E ili ujibu maswali 46 - 50. 46. Anko alikuwa ndiye aliyetawala ukoo ule kwa muda mrefu kuliko viongozi wengine waliopita. [ ] 47. Ukoo huo ulikuwa na mjamii wapatao elfu moja na mia tano hivi wote wakiongozwa na mjamii Mzee aliyeitwa Anko. [ ] 48. Kutokana na uongozi wake mzuri. mara tatu alipotaka kujiuzulu, mjamii wenzake walimkatalia ?sijiuzulu. [ ] 49. Ukoo mkubwa wa mjamii ulikuwa ukiishi katika msitu mmoja karibu na kijiji cha Namtumbo mkoani Ruvuma. [ ] 50. Anko alikuwa Mzee kuliko mjamii wote wa ukoo wake. [ ] KISWAHILI 2005 SEHEMU A SARUFI Katika swali 1 - 15 andika herufiyajibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia 1. Sudi na Celina "wanapigana". Neno lililopigiwa mstari liko katika kauli ipi? 2. Kamilisha sentensi ifuatayo kwa kutumia neno moja kati ya uliyopewa: "Ingawa walipata shida nyingi njiani . walifika salama 3. Sentensi isemayo, . Jumatatu tulipoanza mtihani" inakamilishwa kwa usahihi na neno lipi kati ya yafuatayo? 4. Neno haiba lina maana sawa na neno lipi kati ya haya yafuatayo? 5. Tumia neno mojawapo kati ya haya yafuatayo ili ukamilishe sentensi isemayo "Tukitaka kupata mazao mengi ......... tutumie mbolea". 6. Ni neno lipi linalokamilisha sentensi isemayo "Kiranja wetu wa darasa alikwenda dukani . . . . . . . alikatazwa na mwalimu"? 7. "Kitabu ulichonipa kina kurasa chache". Katika sentensi hii maneno yaliyokolezwa wino yanawakilisha nini? 8. "Kobe anatembea taratibu". Neno "taratibu" ni aina ipi ya maneno? 9. Neno "vibaya" katika sentensi isemayo "vibaya pia vimenunuliwa" limetumika kama aina ipi ya maneno? 10. Katika sentensi: "Mama anaendesha gari," herufi a-katika neno anaendesha inawakilisha kiambishi cha aina ipi? 11. Neno shule limetolewa kutoka katika lugha ipi? 12. Sentensi isemayo "Shangazi mkubwa alikuwa analima shambani" ni aina ipi ya sentensi? 13. Kinyume cha neno adimu ni kipi? 14. Sentensi isemayo "Ukinisaidia nitakusadia" ni aina ipi ya sentesi? 15. "Huyu si ndugu yangu". Katika sentensi hii, neno si ni aina ipi ya maneno? SEHEMU B MSAMIATI Katika swali 16 — 25 andika herufi yajibu lililo sahihi katika karatasi yakoya kujibia. 16. Mahali panapochimbwa madini panaitwaje? 17. "Furaha alishikwa na fadhaa alipobaini ameuziwa mali ya wizi" Neno ' fadhaa" katika sentensi hii lina maana ipi? 18. Ni kiumbe kipi kisichokuwa na uhusiano baina ya hivi vifuatavyo? 19. Neno "tamati" lina maana sawa na neno lipi? 20. Kinyume cha neno tapanya ni kipi? 21. "Seremala alinihadaa aliponiambia angenipa kabati juzi". Neno alinihadaa limetumika kwa maana ipi? 22, "Matona alioa msichana wa hirimu yake." Neno "hirimu" lina maana ipi katika sentensi hii? 23.Kinyume cha nuka ni kipi? 24. Kifungu cha maneno chenye maana sawa na samani ni kipi? 25. Kinyume cha neno okota ni kipi? SEHEMU C METHALI, NAHAU NA VITENDAWILI Katika maswali 26 - 35 chaguajibu lililo sahihi kwa kuandika herufiyake katika karatasiyakoya kujibia. Kwa swali la 35 andikajibu kwa NENO moja tu. 26. Methali isemayo "jifya moja haliinjiki chungu" ina maana ipi? 28.Methali isemayo "Ukipewa shubiri usichukue pima" ina maana ipi? 29.Methali inayofanana na methali isemayo "Ajali haina kinga” ni ipi? 30."Mzigo wa mwenzio ni ... ... ...” ni methali inayokamilishwa na sehemu ipi kati hizi zifuatazo? 31."Kazi ya Daudi ni ya kijungujiko”. Kazi ya kijungujiko ni kazi ya aina ipi? 32.M?u asemapo 'Ashakum si matusi” ana maana ipi? 33.Katika kilimo cha pareto mkoa wetu umetia fora. "Umetia fora" maana yake ni ipi? 34.Kitendawili kisemacho "Babu apiga mbizi; akiibuka ndevu zimekuwa nyeupe” huteguliwa kwa jibu lipi? SEHEMU D UFAHAMU Soma kwa makini kifungu cha habari kifuatacho kishajibu maswali 36 - 45 kwa kuandika herufi ya jibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia. Mpendwa Shangazi, Shikamoo. Asante sana kwa kututhibitishia kwamba ndugu Yangu, binti yako Sekelo, ataolewa tarehe 10 Oktoba 2005 huko mjini. Tarehe hiyo, hasa kwa mimi, ni nzuri sana kwani sitakuwa na pingamizi la kuhudhuria kwani nitakuwa nimemaliza kufanya mtihani wangu. Naingoja siku hiyo kwa shauku kubwa ili nimwone Sekero akiwa amevaa shela kama ishara ya kuingia katika hatua ya utu-uzima. Shangazi, baba anasikitika sana kwa kukosa kuhudhuria kwenye harusi ya mpwawe. Hivi sasa mzee Musa hajiwezi kutokana na nyonda ya shinikizo la damu tangu pale alipoibiwa ng'ombe wake sita wa maziwa. Hata hivyo, mimi na mama tutakuja. Kwa vile tutakuwa na mizigo mingi, tunaomba watu watatu waje kwenye kituo cha mabasi watupokee siku tatu kabla ya tarehe harusi. Huku nyumbani mwaka huu hakukuwa na masika ya kutosha, mazao mengi yamenyauka mashambani. Watu wengi wameanza kukata tamaa kwa jinsi njaa inavyonyemelea bila kuikaribisha. Kwa upande mwingine, ukame umeleta neema kwa baadhi ya watu. Huwezi kuamini shangazi, mbuzi sasa anauzwa kwa shilingi elfu tatu! Watu wanafanya hivyo ili wapate pesa za kununulia chakula. Sisi tumepata bahati ya kuwa na shamba la bonde. Ndiyo maana tuna chakula cha kutosha hata cha watu watakaokuwa harusini. Shangazi, nisalimie sana Sekelo na mdogo Wake, Rehema. Mungu akipenda tutaonana ili nije niwape visa vya Tongoni ya sasa; siyo ile waliyoiacha miaka saba iliyopita. Tongoni sasa kumekucha! Wasalaam, Mwanao, Hawa MASWALI 36. Barua uliyoisoma hapo juu ni: 37. Anayeolewa tarehe 10/10/2005 ana uhusiano upi na mwandishi wa barua hii? 38. Maradhi ya Mzee Musa yametokana na sababu ipi? 39. Neno "nyonda" kwa mujibu wa barua hii lina maana ipi? 40. Ni tarehe ipi ya mwezi Oktoba 2005 ambayo Hawa na mama yake watawasili Tongoni? 41. Hawa na mama yake watakwenda kijijini na mizigo mingi kwa sababu ipi? 42. Kwa nini mwandishi anasema . njaa inavyowanyemelea bila kuikaribisha”? 43. Methali inayoeleza hali ya ukame na matokeo yake ni ipi? 44. Kwa nini familia ya Mzee Musa haikuathirika kwa njaa? 45. Hawa ana maana ipi asemapo ”Tongoni sasa kumekucha”? SEHEMU E UTUNCAJI Umepewa insha yenye sentensi tano (5) zilizoandikwa bila mtiririko sahihi wa mawazo. Zipange sentensi hizo ili ziwe na mtririko wenye mantinki kwa kuzipa herufi A, B, C, D na E ili ujibu maswali 46-50. 46. ”Tusipopanda misitu mipya tutaishiwa na miti kabisa.” Bwana Miti alijibu. 47. Alipomaliza kusema hayo, Mzee Komba akauliza: ”Kwa nini tupande miti ilihali inaota kwa uwezo wa Mungu?” 48. Bwana Miti akajibu tena, ”Yatupasa kupanda miti kwa sababu matumizi yake yameongezeka sana siku hizi.” 49. Mkutano ulipomalizika, kila mtu alirejea nyumbani kwake, akiwa na dhamiri ya kupanda miti. 50. "Tena tutafanana na mtu anayekula chakula chote alichonacho kabla ya kuzalisha kingine". Bwana Miti alihitimisha.
UFAHAMU