STD VII KISWAHILI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2021


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI

01 KISWAHILI

 Muda: Saa 1:40 Mwaka: 2021

Maelekezo

l . Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali arobaini na tano (45).

2. Jibu maswali yote katika kila sehemu.

3. Soma maelekezo yote yaliyoko katika fomu maalum ya kujibia (OMR).

4. Jaza taarifa zote katika fomu ya OMR.

5. Andika Namba yako ya Mtihani kisha weka kivuli kwenye tarakimu za namba hiyo mahali panapohusika kwenye karatasi yako ya kujibia.

6. Weka kivuli kwenye herufi ya jibu lililo sahihi kwa swali 1 — 40. Kwa mfano, kama jibu sahihi ni A weka kivuli kama ifuatavyo:

7. Ukigundua kuwa herufi uliyowekea kivuli si jibu sahihi futa kivuli hicho kwa umakini kwa kutumia kifutio safi kabla ya kuweka kivuli katika herufi mpya.

8. Tumia penseli ya HB tu katika kujibu swali la 1— 40; na kalamu ya Wino wa bluu au mweusi kwa swali la 41 hadi 45.

9. Simu za mkononi na Vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi ndani ya chumba cha mtihani.

SEHEMU A (Alama 35)

Sikiliza kwa makini hadithi utakayosomewa na msimamizi, kisha jibu swali la 1 - 5, kwa kuweka katika herufi ya jibu lililo sahihi katika fomu yako ya kujibia.

Bofya Hapa Kusikiliza Hadithi

Maswali

1. Malkia wa nyuki alikuwa analindwa na nani?

  1. Vibaraka
  2. Askari hodari
  3. Wanakijiji
  4. Nyuki Hohehahe
  5. Wafanyakazi.
Chagua Jibu


2. Ni kitu gani ambacho malkia wa nyuki hakukipenda?

  1. Wanakijiji hohehahe
  2. Mafundi wa masega
  3. Ushirikiano wa nyuki
  4. Vibaraka wa malkia
  5. Kuwalipa vibarua
Chagua Jibu


3. Nani alijishughulisha kutafuta nekta kwenye maua?

  1. Nyaki wote
  2. Vibarua
  3. Wafanyakazi
  4. Vibaraka
  5. Wanakijiji
Chagua Jibu


4. Utajiri katika kijiji cha nyuki ulitokana na nini?

  1. Kuuza asali
  2. Kuuza nta
  3. Kuuza masega
  4. Kuuza maua
  5. Kuuza mizinga
Chagua Jibu


5. Nani walitumika kupeleka habari mbalimbali katika vijiji vya jirani?

  1. Vibarua
  2. Wafanyakazi
  3. Vibaraka
  4. Wanakijiji
  5. Nyuki
Chagua Jibu


Katika swali la 6 - 35, weka kivuli katika herufi ya jibu lililo sahihi katika fomu yako ya kujibia.

6. Wanakijiji walifanya juu Chini ili kuleta maendeleo katika kijiji Chao. Nahau "fanya juu chini" inafafanuliwa na kifungu kipi cha maneno kati ya vifuatavyo?

  1. Walijitahidi kwa kila njia.
  2. Walishirikiana kwa pamoja.
  3. Walijituma kwa ujasiri.
  4. Walijituma kwa uzalendo.
  5. Walitumia nguvu.
Chagua Jibu


7. Nahau ipi yenye maana ya "kunywa pombe?"

  1. Piga mbizi
  2. Piga chenga
  3. Piga yowe
  4. Piga soga
  5. Piga maji
Chagua Jibu


8. Katika sentensi "Dada alimwambia kuwa atakapopata muda atakuja nyumbani ," mzungumzaji ametumia nafsi gani kati ya hizi?

  1. Nafsi ya pili wingi
  2. Nafsi ya tatu wingi
  3. Nafsi ya tatu umoja
  4. Nafsi ya pili umoja
  5. Nafsi ya kwanza wingi
Chagua Jibu


6. "Sisi ni wanafunzi hodari wa somo la kiswahili". Kauli hiyo inawakilisha nafsi ipi kati ya hizi zifuatazo?

  1. Nafsi ya kwanza umoja
  2. Nafsi ya tatu wingi
  3. Nafsi ya tatu umoja
  4. Nafsi ya kwanza wingi
  5. Nafsi ya pili wingi
Chagua Jibu


10. Daktati alisema kwamba mgojwa wetu amepata ahueni" Hiyo ni aina gani ya kauli kati ya zifuatazo?

  1. Tata
  2. Mazoea
  3. Halisi
  4. Taarifa
  5. Kutenda
Chagua Jibu


11. Masumbuko aliwaambia kuwa, hataingia darasani tena. Kauli halisi ya sentesi hii ni ipi kati ya zifuatazo??

  1. Masumbuko aliwaambia kuwa. "haingii darasani tena."
  2. Masumbuko aliwaambia. "hataingia darasani tena".
  3. Masumbuko aliwaambia. "sitaingia darasani tena."
  4. Masumbuko aliwaambia. "hakuingia darasani tena.'
  5. Masumbuko aliwaambia "kamwe haingii darasani i'
Chagua Jibu


12. "Nyamante alikata shauri na kuwaambia wenzake, kweli elimu ndiyo mkombozi wa mtoto wa kike." Nahau "kata shauri" katika sentensi hii ina maana ipi kati ya zifuatazo?

  1. Kuamua
  2. Kuwatahadharisha
  3. Kuwaasa
  4. Kuonya
  5. Kufundisha
Chagua Jibu


13. Chekacheka anapenda watoto wake wawe na tabia njema hadi ukubwani. Methali ipi kati ya zifuatazo inahimiza tabia ya aina hiyo?

  1. Zimwi likujualo halikuli likakwisha.
  2. Asiyesikia la mkuu huvujika guu.
  3. Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.
  4. Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu.
  5. Tabia hupamba kuliko libasi.
Chagua Jibu


14. "Nikitembea walio wafu huamka na walio hai hukaa kimya." Jibu la kitendawili hiki ni lipi kati ya yafuatayo?

  1. Nyuki ndani na nje ya mzinga
  2. Yai na kifaranga chake
  3. Majani makavu na mabichi
  4. Kulala usingizi na kuamka
  5. Tumbo na chakula
Chagua Jibu


15, Ni methali ipi kati ya zifuatazo inamaana sawa na methali "akufaaye kwa dhiki ndio rafiki"?

  1. Baniani mbaya kiatu chake dawa,
  2. Damu nzito kuliko maji,
  3. Undugu kufaana si kufanana,
  4. Shukrnni ya punda njateke,
  5. Sikio la kufa halisikii dawa,
Chagua Jibu


16. Neno lipi kati ya yafuatayo ni jumuishi kwa maneno haya "nyanya, vitunguu, pilipili na tangawizi'?"

  1. Nafaka
  2. Matunda
  3. Vinywaji
  4. Vitoweo
  5. Viungo
Chagua Jibu


17. Mwaka 1985 Mwalimu Julius Kambaragc Nyerere aliamua kung'atuka madarakaní na kumwachia Mheshimiwa, Ali Hassan Mwinyi, Kitcndo cha Mwalimu Julias Kambarage Nyerere kung'atuka kinamaanisha nini?

  1. Kuaga wafanyakazi
  2. Kuwaachia wafanyakazí
  3. Kustaafu kazi
  4. Kujiuzulu madaraka
  5. Kupumzika kazi kidogo
Chagua Jibu


18. Neno lipi kati ya yafuatayo ni jumuishi kwa maneno haya "almasí, dhahabu, Tanzanaiti na lulu" ?

  1. Shaba
  2. Vyuma
  3. Marumaru
  4. Mgodi
  5. Madini
Chagua Jibu


19. Katika neno "ninakula" kiambishi cha wakati uliopo ni kipi kati ya vifuatavyo?

  1. -ni-
  2. -ku-
  3. -na-
  4. -la-
  5. -kul-
Chagua Jibu


20. "Muda ulipowadia wanafunzi wote tulisimama foleni.' Neno "wadia" linashabihiana na neno lipi kati ya yafuatayo?

  1. fika
  2. kwisha
  3. patikana
  4. pungua
  5. ongezeka
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256