SOMA VITENDAWILI VYA KISWAHILI NA MAJIBU YAKE HAPA

VITENDAWILI VYA KISWAHILI NA MAJIBU YAKE

A

1. Adui lakini po pote uendako yuko nawe. Inzi

2. Afahamu kuchora lakini hajui achoracho. Konokono

3. Afuma hana mshale. Nungunungu

4. Ajenga ingawa hana mikono. Ndege

5. Ajifungua na kujifunika. Mwavuli

6. Akitokea watu wote humwona. Jua

7. Akitokea watu wote hunungunika na kuwa na huzuni. Ugonjwa

8. Akivaa nguo hapendezi, akiwa uchi apendeza. Mgomba

9. Alipita mtu ana bunda la mshale. Mkindu

10. Alipita mtu mwenye kibandiko cha nguo. Inzi

11. Aliwa, yuala; ala, aliwa. Papa

12. Amchukuapo hamrudishi. Kaburi

13. Amefunika kote kwa blanketi lake jeusi. Giza

14. Amefunua jicho jekundu. Jua

15. Ameingia shimoni akiwa uchi, akatoka amevaa nguo nzuri. Mbegu

16. Amejitwika mzigo mkubwa kuliko yeye mwenyewe. Konokono/Koa

17. Amekaa kimya na watoto wamemzunguka pande zote. Mgomba

18. Amekula ncha mbili. Wali

19. Amevaa joho kubwa kuliko yeye mwenyewe. Kaburi

20. Anakuangalia tu wala halali au kutembea. Picha

21. Anakula kila siku lakini hashibi na hatashiba. Mchanga

22. Anakula lakini hajashiba na hatashiba milele. Ardhi

23. Anakula lakini hashibi. Mauti

24. Anapendwa sana ingawaje ni mkali sana. Moto

25. Anatoka kutembea, anakuja nyumbani anamwambia mama, ‘Nieleke’. Kitanda

26. Ashona mikeka wala hailali. Maboga

27. Askari wangu wote wamevaa kofia upande. Majani

28. Askari wangu wote wamevaa mavazi meusi. Chunguchungu

29. Asubuhi atembea kwa miguu mine, adhuhuri kwa miwili. Fedha

30. Atapanya mbegu nyingi sana lakini hazioti. Mvua

31. Atolewapo nje hufa. Samaki

B

32. Baba alinipa mfupa, nikautunza ukawa fahali. Muwa

33. Baba ameweka mkuki nje nikashindwa kuukwea, mdogo wangu akaukwea. Sisimizi

34. Babako akojoapo hunung’unika. Mawingu

35. Babu amefunga ushanga shingoni. Mtama/Nazi

36. Babu anakula ng’ombe, analea fupa linakuwa ng’ombe. Muwa

37. Babu hupiga kelele akojoapo. Mvua

38. Babu mkubwa ameangushwa na babu mdogo. Mti na shoka

39. Babu, nyanya, mjomba, mama, baba na watoto, mna safari ya wapi? Siafu

40. Bak bandika, bak bandua. Nyayo

41. Bawabu mmoja tu asiyeogopa chochote duniani. Mlango

42. Bibi kikongwe apepesa ufuta. Kope za macho

43. Bibi yake hutandikwa kila siku, lakini hatoroMoyoKinu cha kutwangia

C

44. Chakula kikuu cha mtoto. Usingizi

45. Cha ndani hakitoki nje, cha nje hakiingii ndani. Nyama na mfupa

46. Chang’aa chapendeza, lakini hakifikiwi. Jua

47. Chatembea na hakijapata kupumzika hata nukta moja. Mwezi/Jua

48. Cheupe chavunjika manjano yatokea. Yai

49. Chumba change kina ukuta niondoa na kuusimika nitakapo. Pazia

50. Chungu change cha udongo hakipasuki kikianguka. Mjusi/Panya

51. Chungu kikubwa sana chenye kifuniko kikubwa sana. Dunia na mbingu

D

52. Dada yangu akitoka kwao harudi kamwe. Jani likwanyukapo

53. Dada yangu kaoga nusu. Jiwe mtoni

54. Drrrrrh1 Ng’ambo. Daraja la buibui

55. Dume wangu amelilia machungani. Radi

F

56. Fahali wa ng’ombe na mbuzi wadogo machungani. Mwezi na nyota angani

57. Fika umwone umpendaye. Kioo

58. Fuko kajifukia, mkia kaacha nje. Kata mtungini

59. Funga mizigo twende Kongo. Mikia ya mbwa

H

60. Hachelewi wala hakosei safari zake. Jua

61. Haina miguu wala mikono, lakini, yabeba magogo. Maji

62. Hakihitaji maji, wala udongo, wala chakula; lakini chamea. Nywele

63. Hakionekani wala hakishikiki. Hewa

64. Hakisimami, na kikisimama msiba. Moyo

65. Hakuchi wala hakuchwi. Kula

66. Halemewi wala hachoki kubeba. Ardhi

67. Hamwogopi mtu yeyote. Njaa

68. Hana mizizi, nimemkata mara nyingi lakini haachi kukua. Ukucha

69. Haoni kinyaa. Mvua

70. Hapo nje panapita mtu mwenye miguu mirefu. Mvua

71. Hasemi, na akisema hatasahaulika. Kalamu

72. Hasimamishwi akiwa na ghadhabu. Upepo

73. Hata inyeshe namna gani haifiki humu. Kwapani

74. Hata jua likiwaka namna gani hakauki wala kupata joto. Pua ya mbwa

75. Hata Mzungu ameshindwa. Mauti

76. Hauchagui chifu wala jumbe. Utelezi

77. Hausimiki hausimami. Mkufu

78. Hawa wanaingia hawa wanatoka. Nyuki mzingani

79. Hesabu haihesabiki. Nyota

80. Huitumia kila siku lakini haiishi. Miguu

81. Huku kutamu, huku kutamu, katikati uchungu. Jua

82. Huku unasikia ‘pa’ Huku unasikia ‘pa! Mkia wa kondoo

83. Hula lakini hashibi. Sindano

84. Hulala tulalapo, huamka tuamkapo. Jua

85. Humu mwetu tuko wanne tu, ukimwona wa tano mwue. Matendegu ya kitanda

86. Huna macho lakini wakamata wanyama. Ndoana

87. Hupanda mtini na mwenye kichaa wake. Kivuli

88. Hutembea watatu. Mafiga

89. Hutoka upesi sana lakini hasalimu. Kuku

90. Huwafanya watu wote walie. Moshi

91. Huwezi kukalia alipokalia msichana wangu mweusi. Chungu jikoni

92. Huzikwa mmoja, hufufuka mmoja, huzeeka wengi. Mbegu na matunda

I

93. Inaonekana mara mbili katika dakika moja na mara moja tu katika mwaka. Herufi "K"

94. Ini la ng’ombe huliwa hata na walioko mbali. Kifo

J

95. Jembe la Wangoni haliishi. Miguu/Nyayo

96. Je, unaweza, kukua ukampita mzee wako? Nywele kichwani

97. Jiwe litoalo maji. Macho

K

98. Kaburi la mfalme lina milango miwili. Kata ya kuchukulia Maji kichwani

99. Kaka yangu anapanda darini na fimbo nyuma. Paka na mkia wake

100. Kama kingekuwa mkuki, ungekuta kimekwisha kuua wote. Kizingiti cha mlango

101. Kama unapenda, mbona usile? Ulimi

102. Kanipa ngozi nikapikia, kanipa nyama nikala, kanipa mchuzi nikanywa, kanipa mfupa nikautumia. Nazi

103. Kapanda mti pamoja na uchawi wake. Tumbaku inaponuswa puani

104. Kidimbwi kimezungukwa na majani. Macho

105. Kikioza hutumiwa, kikiwa kichungu hakitumiwa. Maziwa

106. Kila linapofika kwetu hutanguliza makelele. Mvua

107. Kila mtu atapitia malango huo. Kifo

108. Kila mtu hata mfalme huheshimu akipita. Mlango

109. Kila siku hupita njia hiyo hiyo bali arudipo hatumwoni. Jua

110. Kileee! Hiki hapa. Kivuli

111. Kilimsimamisha chifu njiani. Chawa

112. Kina mikono na uso lakini hakina uhai. Saa

113. Kinaniita lakini sikioni. Mwangwi

114. Kisima cha Bimpai kina nyoka muwai, ndiye fisadi wa maji. Taa ya utambi

115. Kisima kidogo kimejaa changarawe. Kinywa na meno

116. Kitendawili change ukikitambua nitakupa hirizi. Mimba

117. Kiti cha dhahabu hakikaliwi na watu. Moto

118. Kiti cha Sulatni hukaliwa na mwenyewe. Kuku aatamiapo mayai

119. Kiti nyikani. Uyoga

120. Kitu changu asubuhi chatembea kwa miguu mine, saa sita kwa miguu miwili, jioni kwa miguu mitatu. Maisha ya binadamu

121. Kiwanja kizuri lakini hakifai kuweka mguu. Kipara

122. Kombe ya Sultani Ii wazi. Kisima

123. Kondoo wangu amezaa kwa paja. Mhindi

124. Kondoo wangu mnene kachafua njia nzima. Konokono

125. Kondoo za mtoto zamaliza mavuno. Jiwe la kusagia

126. Kufanya kwa ridhaa mojamoja. Kusuka mkeka

127. Kuku wangu aliangua mayai jana, lakini si kuku wala ndege. Nyoka au samaki

128. Kuku wangu amezalia miibani. Nanasi au chungwa

129. Kuku wetu hutagia mayai mikiani. Matunda

130. Kuna mlima mmoja usio pandika. Nafasi kati mdomo na pua

131. Kuna mtu mwenye tumbo kubwa aliyesimama nje. Ghala

132. Kuna ziwa kubwa ambalo limekauka na limebakiza mizizi. Chongo

133. Kunguru akilia hulilia mirambo. Mtoto akililia maziwa

134. Kwenye msitu mkubwa Napata mti mmoja tu, lakini kwenye msitu mdogo naweza kupata miwili. Watoto wa ng'ombe na mbuzi

135. Kwetu mishale na kwenu mishale. Mikia ya panya

136. Kwetu twalala tumesimama. Nguzo za nyumba

L

137. La mgambo limelia wakatoka weusi tu. Chunguchungu

138. Likienda hulia, likirudi halilii. Debe aka buyu

139. Likitoka halirudi. Neno

140. Liwali amekonda lakini hana mgaga. Sindano

M

141. Mama ametengeneza chakula lakini hakula. Chungu cha kupikia

142. Mbona kinakumeza lakini hakikuli? Nyumba

143. Mbona mwakunjiana ngumi bila kupigana? Mafiga

144. Mbona mwasimama na mikuki, mwapigana na nani? Katani

145. Mchana ‘ti’ usiku ‘ti’. Mlango

146. Mdogo lakini humaliza gogo. Mchwa

147. Mfalme amesimika mkuki wake hapa name nikausimika wangu kando yake, baadaye

hatukuitambulisha tena. Kohozi

148. Mfalme hushuka kwa kelele. Mvua

149. Mfalme katikati lakini watumishi pembeni. Moto na mafiga

150. Mfalme wetu hupendwa sana, lakini wakati wa kumwona lazima umtoe nguo zote kwanza. Hindi

151. Mhuni wa ulimwengu. Inzi

152. Mkanda mrefu wafka mpaka pwani. Njia

153. Mke wangu mfupi, lakini huvaa nguo nyingi. Hindi

154. Mlango wa nyumba yangu uko juu. Shimo la mchwa

155. Mlima mkubwa wapandwa kuanzia juu. Sima/Ugali

156. Mlimani sipandi. Maji

157. Mlima umezuia kutazama kwa mjomba. Kisogo

158. Mlima wa kupanda kwa mikono. Mlima

159. Mlima wa kwetu hupandwa na mfalme. Nafasi kati ya mdomo na pua ya ngombe

160. Mlima wa mwenyewe hupandwa na mwenyewe. Buibui na utando wake

161. Mpini mmoja tu lakini majembe hayahesabiki. Mkungu wa ndizi

162. Msitu ambao haulii hondohondo. Mimba

163. Mti mkubwa, lakini una matawi mawili tu. Kichwa na masikio

164. Mti mnyanya mti kerekeche mti ah mti ah!. Ngoma na upatu

165. Mti wangu una matawi kumi na mawili na kila tawi lina majani kadiri ya thelathini. Mwaka

166. Mtoto asemea pangoni. Ulimi mdomoni

167. Mtu mdogo mwenye miguu mirefu ambaye aweza kutembea dunia nzima kwa dakika tano. Mawazo

168. Mvua hema na jua hema. Kobe

169. Mvua kidogo ng’ombe kaoga kichwa. Jiwe

170. Mwadhani naenda lakini siendi. Jua

171. Mwalimu analala na mwanafunzi wanamsomea. Kinyesi na inzi

172. Mwanamke mfupi hupiga kelele njiani. Kunguru

173. Mwanamke mfupi hutengeneza pombe nzuri. Nyuki

174. Mwanang’ang’a hulia mwituni. Shoka

175. Mwepesi, lakini aweza kuvunja nyumba za mji wote. Tufani

176. Mwezi wangu umepasuka. Kweme

177. Mzee Kombe akitoa machozi wote hufurahi. Mvua

178. Mzee Kombe akilia watu hufurahi. Mvua

179. Mzizi wa miti hutokea mbali. Siafu

180. Mzungu yuko ndani na ndevu ziko nje. Hindi

N

181. Naitumia ngazi hiyo kwa kupandia na kushukia. Mwiba

182. Nakikimbilia lakini sikikuti. Njia

183. Nakupa lakini mbona huachi kudai. Tumbo

184. Nakwenda msituni na mdogo wangu, lakini yeye namwacha huko.

185. Nameza lakini sishibi. Mate

186. Namkimbiza lakini simkuti. Kivuli

187. Namlalia lakini halii. Kitanda

188. Namwomba atangulie lakini hukataa kabisa. Kigino

189. Nanywa supu na nyama naitupa. Muwa

190. Napigwa na mvua na nyumba ipo. Matunda ya pua/Kwapa

191. Natembea juu ya miiba lakini hainichomi. Miiba

192. Natembea juu ya miiba lakini sichomwi. Ulimi

193. Natembea na wenzangu lakini tukifika kwenye nyumba mimi hukaa mlangoni. Mbwa

194. Natengeneza mafuta lakini nimepauka sana. Mzinga was nyuki kwa nje

195. Natengeneza mbono lakini alama hazionekani. Mzinga wa nyuki

196. Ndege wengi baharini. Nyota

197. Ndugu wawili wafanana sana, lakini hawatembeleani. Macho

198. Ngoja nikumbuke. Boga changa

199. Ng’ombe wa baba watelemka mtoni. Mawe mtoni

200. Ng’ombe wa babu huchezea miambani. Mijusi

201. Ng’ombe za babu zikienda machungani hulia, zikirudi hazilii. Vbuyu

202. Ng’ombe za babu zinalala na mkia nje.Viazi vitamu udongoni

203. Ng’ombe wamechanganyika nikakosa wa kwangu. Pesa/Nyayo

204. Ng’ombe wangu ni weupe kwatoni. Katani

205. Ng’ombe wangu wote hunywa maji isipokuwa mmoja. Fimbo ya kuchunga

206. Ngozi ndani nyama juu. Firigisi

207. Nguo ivaliwayo kila siku isiyoingiwa na chawa. Nyusi

208. Nikicheka kinacheka, nikinuna kinanuna. Kioo

209. Nikienda arudi, nikirudi aenda. Kivuli majini

210. Niiita ‘baba’ huitika ‘baba’. Mwangwi

211. Nikija kwenye ndege wananifukuza, na nikienda kwenye wanyama hawanitaki. Popo

212. Nikimpiga huyu huyu alia. Utomvu wa papai

213. Nikimpiga mambusu. Puliza kidole wakati unapojikwaa

214. Nikimwita hunijibu nani. Mwangwi

215. Nikipewa chakula nala bali natema. Shoka

216. Nikitembea walio wafu huniamkia na walio hai hukaa kimya. Majani makavu na mabichi

217. Nikitembea yuko, nikikimbia yuko, nikiingia ndani hayupo. Kivuli

218. Ni kitu gani ambacho kutoa ni kuongeza? Shimo

219. Nikitupa mshale wangu mchana huenda mbali sana, lakini niutupapo usiku hauendi mbali. Jicho

220. Nikiwaambia ondokeni hukataa, lakini mjomba akitokea wote hukimbia. Umande na jua

221. Nilijenga nyumba yangu nikaiacha bila kuiezeka majani; lakini niliporudi nilikuta imekwisha ezekwa majani. Mahindi machanga

222. Nilijenga nyumba yangu yenye mlango mmoja. Jani la mgomba la nchani

223. Nilimkata alafu nikamridhia. Kupanda mbegu

224. Nilimtuma askari vitani akaniletea kondoo mweusi. Fuko

225. Nilipandia majanini nikashukia majanini. Mwiba

226. Nilipigwa na tonge la ugali la moto nilipopita msituni. Manyigu

227. Nilipitisha mkono wangu chini la ardhi, nikamshika beberu mkubwa sana. Kiazi kikuu

228. Nilipoangalia kwenye magereza ya Wazungu, nikaona wameketi juu ya mabati. Pelele

229. Nilipofika msituni nilikuta chungu cha pure kinachemka. Mzinga wa nyuki

230. Nilipoingia Rumi, alitoka mtu na wake kumi; kila mke na tundu kumi, kila tundu na kuku

kumi; kila kuku na mayai kumi. Mayai, kuku, tundu, wake, kumi kumi kumi. Wangapi

walikwenda Rumi? Hakuna

231. Nilipo, juu kuna miiba na chini vivyo hivyo; lakini sichomwi. Ulimi kinywani

232. Nilipokuwa mchanga nilikuwa na kijikia lakini sasa sinacho. Chura

233. Nilitembea na mwezangu naye hupita vichakani. Kivuli

234. Nimechoma fimbo yangu pakabaki pa kushikia tu. Njia

235. Nimefyeka mitende yote kiungani isipokuwa minazi miwili tu. Masikio

236. Nimejenga nyumba babu akaihamia kabla mimi sijahamia. Mjusi

237. Nimekata mti, akaja samba mwekundu akaukalia. Utomvu

238. Nimekata mti bara ukaangusha matawi pwani. Nzige

239. Nimekwenda na rafiki yangu kwa jirani, yeye akafika kabla yangu. Sauti ya nziga

240. Nimemtahiri binti wangu akatoa damu mchana kutwa. Kivuli

241. Nimempeleka kondoo wangu akatoa damu mchana kutwa. Mgomba

242. Nimemtuma mtu kumwamkua mtu, yeye amekuja, Yule aliyetumwa hajaja. Kuangua tunda Ana nazi

243. Nimemwacha mzee kikongwe mtoni anangojea mgeni kulaki. Mtego

244. Nimempandikiza mti wangu ukapeleka matawi ng’ambo ya mto. Kivuli

245. Nimesimama mbali nyikani lakini naonekani. Moto

246. Nimetembea kitambo, kukumbuka sikufunga nyumba. Dirisha Ana ufa

247. Nimetoka kutembea kutembea, nikashika ng’ombe mkia. Kata

248. Nimetupa mshale angani wala sitambui utateremsha ndege wa namna gani. Mimba

249. Nimeweka ndizi yangu, asubuhi siioni. Nyota

250. Nimezaliwa na mguu mmoja. Uyoga

251. Nimezungukwa na adui wengi, lakini siumizwi. Ulimi na meno

252. Nina kijiti change, nizidivyo kukikata ndivyo kizidivyo kuwa kirefu. Maisha

253. Nina kitu changu kitumiwacho na wengine kuliko mimi. Jina

254. Nina kitu kizuri sana nyumbani, lakini siwezi kukichukua. Dada

255. Nina kitu nipendacho ambacho hata baba, mama, dada, kaka hata na mgeni nimpendaye sana siwezi kumwazima. Mke

256. Nina mwezi ndani ya bakuli. Maziwa

257. Nina ng’ombe wangu nisipomshika mkia hali majani. Jembe

258. Nina nyumba yangu imezungukwa na mifupa. Mdomo

259. Nina pango langu lilojaa mawe. Kinywa

260. Nina watoto wangu hamsini na wote nimewavisha visibau vyeupe. Kunguru

261. Nina watoto watatu, mmoja akitoka kazi haifanyiki. Mafiga

262. Nina badilika umbo langu baada ya kila muda mfupi. Kivuli

263. Ninachimba mizizi ya mti usio na mizizi. Jiwe

264. Ninacho, nakitumia, lakini kila nikitumiapo, sikiharibu ila nakipa rangi. Maji na mkojo

265. Ninakula vitu vyote vinono lakini sikui wala sinenepi. Chungu cha kupikia

266. Ninakwenda naye na kurudi naye. Kivuli

267. Ninao mlima ambao una msitu kileleleni tu. Kichwa

268. Nitokeapo kila mmoja asema namtazama yeye tu. Jua au mwezi

269. Njia yapitwa siku zote lakini haina alama. Njia ya jua au mwezi

270. Njoo hapa nije hapo. Kiraka

271. Nne nne mpaka pwani. Matendegu

272. Nusu mfu nusu hai. Sungura alalapo

273. Nyama ndogo imewashibisha wengi wala isiishe. Kinoo

274. Nyama ya Reale haijai kikombe. Mkufu

275. Nyanya yako ana huruma kukubeba ulalapo. Kitanda

276. Nyumba yangu ina makuti tele, lakini mvua ikinyesha huvuja. Mwembe

277. Nyumba yangu ina milango mingi. Kichuguu

278. Nyumba yangu ina nguzo moja. Uyoga

279. Nyumba yangu kubwa, haina mlango. Yai

280. Nyumba yangu kubwa, haina taa. Kaburi

281. Nyumba yangu kubwa hutembelewa mgongoni. Konokono

O

282. Oh! Mwanamke aliyevunja chungu mshangao wake

283. Ondoka nikae. Maji ya mfereji

P

284. Paa alipenga hata pua ikapasuka. Mbarika

285. Palikuwepo watu watatu wakivuka mto. Mmoja alivuka pasipo kukanyaga maji wala kuyaona; wa pili aliyaona maji lakini alivuka bila kuyakanyaga; wa tatu aliyaona na kuyakanyaga alipovuka.

Ni nani hawa? Was kwanza in Mtoto tumboni mwa mamake, was pili ni Mtoto aliyebebwa mgongoni, was tatu ni mama mwenyewe

286. Panda ngazi polepole. Sima ya ugali

287. Para hata Maka. Utelezi

288. Pete ya mfalme ina tundu katikati. Kata ya kuchukulia mizigo

289. Poopoo mbili zavuka mto. Macho

290. Po pote niendako anifuata. Kivuli

R

291. Rafiki yangu ana mguu mmoja. Uyoga

292. Reli yangu hutandika ardhini. Siafu

293. Ruka Riba. Maiti

S

294. Shamba langu kubwa lakini mavuno hayajazi kiganja. Nywele kichwani

295. Shamba langu miti mitano tu. Mkono wa vidole

296. Shangazi yangu ni mrefu sana lakini hafikii tumbo la kondoo. Njia

297. Sijui aendako wala atokako. Upepo

298. Sijui afanyavyo. Nyoka apandavyo mtini

299. Sina dada wala kaka, lakini baba wa huyu jamaa ni mtoto wa babangu. Ni nani huyo? Mtoto wangu

300. Subiri kidogo! Miiba

301. Sultani alipiga mbiu watu waje kufanya kazi yake lakini wakashindwa. Maji

T

302. Taa ya bure. Jua au mwezi

303. Taa ya Mwarabu inapepea. Kilemba

304. Tajiri aniweka mfukoni na maskini anitupa. Makamasi

305. Tandika kitanga tule kunazi. Nyota

306. Tangu kuzaliwa kwake sijamwona asimame wala kukimbia. Mkufu

307. Tatarata mpaka ng’ambo ya mto. Utando wa baibui

308. Tatu tatu mpaka pwani. Mafiga

309. Tega nikutegue. Mwiba

310. Teke teke huzaa gumugumu, na gumugumu huzaa teke teke. Mahindi ama yai

311. Tengeneza kiwanja kikubwa kabila Fulani lije kupigania. Mbono

312. Tonge la ugali lanifikisha pwani. Jicho

313. Tukate kwa visu ambacho hakitakatika. Maji

314. Tulikaribishwa mahali na mdogo wangu, yeye akaanza kushiba kabla yangu. Kucha

315. Tuliua ng’ombe na babu, kila ajaye hukata. Kinoo

316. Tuliua ng’ombe wawili ngozi ni sawasawa. Mbingu na nchi

317. Tumvike mwanamke huyu nguo. Kuezeka nyumba

318. Tunajengajenga matiti juu. Mapapai

319. Twamsikia lakini hatumwoni. Sauti

U

320. Ukimcheka atakucheka, ukimwomba atakuomba. Mwangwi

321. Ukimwita kwa nguvu hasikii, lakini ukimwita polepole husikia. Fisi

322. Ukimwona anakuona. Jua

323. Ukitaka kufahamu ana mbio, mwonyeshe moto. Kinyonga

324. Ukitembea ulimwengu wote utakosa nyayo. Mwamba

325. Ukiukata haukatiki, ukiushika haushikiki. Moshi

326. Ukiwa mbali waweza kumwona Fulani umatini. Tundu LA sindano

327. Ukoo wa liwali hauna haya. Wanyama

328. Ule usile mamoja. Kifo

329. Umempiga sungura akatoa unga. Funds LA mbuyu

330. Unatembea naye wote umjiao atakuona. Bakora

331. Upande wote umjiao atakuona. Kinyonga

332. Ushuru wa njia wKujikwaa Kujikwaa

333. Utahesabu mchana na usiku na hutamaliza kuhesabu. Nywele

V

334. Viti kumi nyumbani, tisa vyakalika lakini kimoja hakikaliki. Moto

W

335. Wake wa mjomba kimo kimoja. Vipande vya kweme

336. Wako karibu lakini hawasalimiani. Nyumba ama kuta zinazoelekeana

337. Wanakuja mmoja mmoja na kujiunga kuwa kitu kimoja. Matone ya mvua

338. Wanameza watu jua linapokuchwa. Nyumba

339. Wanamwua nyoka. Watu wanaotwanga

340. Wanangu wawili hugombana mchana, usiku hupatana. Mlango

341. Wanao wakati wao wa kuringa, nao ni weupe kama barafu. Nyota

342. Wanapanda mlima kwa makoti mazuri meusi na meupe. Vipepeo

343. Wanastarehe darini. Panya

344. Wanatembea lakini hawatembelewi. Macho

345. Watoto wa mtu mmoja hulala chini kila mwaka. Maboga

346. Watoto wangu wana vilemba, asio kilemba si mwanangu. Fuu

347. Watoto wangu wote nimewavika kofia nyekundu. Jogoo

348. Watoto wangu wote wamebeba vifurushi. Vitovu

349. Watu ishirini walipanda juu ya mti, wawili wakaona chungwa, watano wakalichuma, kumi wakalimenya, wote wakaridhirika mtu mmoja alile. Je, ni watu gani hao? Waliopanda ni vidole vya miguu na mikono, walioona ni macho mawili, waliochuma ni vidole vitano vya mikono, waliomenya ni vidole vya mikono yote miwili, na aliyelila ni mdomo

350. Watu waliokaa na kuvaa kofia nyekundu. Kuku, katani au mahindi

351. Watu wamehama askari wekundu wakazidi nyikani. Viroboto

352. Watu wawili hupendana sana; kati ya mchana hufuatana ingawa mmoja ni dhaifu. Usiku mdhaifu

haonekani tena. Kivuli

353. Watu wote ketini tumfinye mchawi. Kula ugali

354. Wewe kipofu unaenda wapi huko juu? Mkweme

Y

355. Yaenda mbali lakini haiondoki ilipo. Njia

Z

356. Zilitazamana na mpaka sasa hazijakutana. Kingo za mto

357. Ziwa dogo linarusha mchanga. Chungu jikoni

358. Ziwa kubwa, lakini naogelea ukingoni tu. Moto

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256