STD VII KISWAHILI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2018

1. Neno lipi kati ya haya lina maaana sawa na shari?

  1.  Ubunifu
  2. Umaarufu
  3. Uzembe
  4. Ugomvi
  5. Uzushi
Chagua Jibu


2.      Shida alivaa nguo za kijeshi wakati wa mkutano.Neno "za kijeshi" ni aina gani ya neno?

  1. Kivumishi
  2. Kielezi
  3. Kitenzi
  4. Kiwakilishi 
  5.  Nomino
Chagua Jibu


3.      Hicho ulichopata sikupata lakini nimepata hiki" katika sentensi hii, maneno "hicho na hiki"ni aina gani ya maneno?

  1. Vivumishi 
  2. Viwakilishi
  3. Vielezi    
  4. Vitenzi
  5. Nomino
Chagua Jibu


4.      Ni sentensi ipi iliyo sahihi kimuundo  kati ya zifuatazo?

  1.  Amenunua gari mashaka
  2. Mashaka gari amenunua 
  3. Amenunua mashaka gari 
  4. Mashaka amenunua gari
  5.  Gari amenunua mashaka.
Chagua Jibu


5.      Maana ya neno "faraghani" ni ipi kati ya hizi?

  1. Wazi wazi
  2. Kivulini
  3. Pembejeo
  4. Mafichoni
  5. Hadharani
Chagua Jibu


6.      Wingi wa sentensi "Mbuzi wamepotea" ni upi?

  1. Mbuzi zetu zimepotea
  2. Mbuzi yetu zimepotea
  3. Mbuzi wetu wamepotea 
  4.  Mbuzi zetu wamepotea
  5. Mbuzi yetu wamepotea.
Chagua Jibu


7.      "Wanafunzi kenda walikwenda ziara nchini Kenya".neno wa ni aina gani ya neno?

  1. Kivumishi
  2. Kiwakilishi
  3. Kielezi 
  4.  Kitenzi
  5. Nomino.
Chagua Jibu


8.      Ashura anacheza mpira wa miguu vizuri.katika sentensi hii,neno lipi limetumika kama kielezi?

  1. Anacheza
  2.  Mpira
  3. Vizuri
  4. Ashura
  5. Wa mguu.
Chagua Jibu


9. Mtu anayetafsiri ana kwa ana katika lugha moja kwenda lungha huitwaje?

  1. Msuluhishi
  2. Mpatanishi
  3. Mkalimani
  4.  Mfafanuzi
  5. Mhubiri
Chagua Jibu


10. "Sote tunafanya mtihani darasani". "darasani" limetumika kama aina gani ya neno?

  1. Kielezi
  2. Kivumishi
  3. Kitenzi
  4. Kiwakilishi 
  5.  Nomino
Chagua Jibu


I l. Baraka aliona --------- kuwa miongoni mwa waliofaulu. Ni neno i:zn linakamilisha sentensi hii kwa usahihi  ya maneno yafuatayo?

  1. Fadhili
  2. Fahari
  3. Fahiri
  4. Fadhaa
  5. Fadhila
Chagua Jibu


12. Mwanamke yule alikaa baada ya kufiwa na mume wake. Ni neno lipi linakamilisha sentensi hii kati ya maneno yafuatayo?

  1. eda 
  2.  heda 
  3. arobaini 
  4.  fungate 
  5. edaha.
Chagua Jibu


13. Kitenzi "piga"kikiwa katika kauli ya kutendeka kitakuwa neno lipi kati ya maneno yafuatayo?

A  Pigia             

B  Pigwa

C  Pigika

D  Pigiwa

E   Pigana.

Chagua Jibu


14. Wewe unasoma kwa bidii"wingi wa sentensi hii ni upi?

  1.  Sisi tunasoma kwa bidii 
  2.  Wale wanasoma kwa bidii
  3. Nyinyi mnasoma kwa bidii 
  4.  Ninyi tunasoma kwa bidii 
  5. Wao wanasoma kwa bidii
Chagua Jibu


15."Wanafunzi wale ni hodari sana" neno "wale" ni aina gani ya neno?

  1. Kitenzi 
  2.  Kivumishi 
  3. Nomino 
  4.  Kielezi
  5. Kiwakilishi
Chagua Jibu


16. "Wasichana saba wamechaguliwa kujiunga na kozi ya uhandisi." Neno na ni aina gani ya neno?

  1. Kitenzi
  2. Nomino
  3. Kiwakilishi 
  4.  Kielezi
  5.  Kiunganishi.
Chagua Jibu


17. Ni neno lipi lina maana sawa na neno kumzonga mtu kwa maneno makali kwa lengo la kumkasirisha?

  1. Kumhukumu
  2. Kumwinda
  3.  Kumwadhibu 
  4.  Kumaskama
  5. Kumzoea.
Chagua Jibu


18. Katika vitenzi "sitafyeka" na "hupendi" ni silabi zipi zinazoonesha ukanushi?

  1. ta na hu
  2. ta na pe
  3. ka na ndi 
  4.  si na hu
  5. fye na pe.
Chagua Jibu


19. Neno lipi kati ya haya halilandani na mengine?

  1. Cheka
  2. Tabasamu
  3. Furaha 
  4.  Sherehe 
  5.  Shere.
Chagua Jibu


20. Mnyama huyu anafanana na ngombe. Wingi wa sentensi hii ni ipi?

  1. Wanyama anayefanan na ngoombe 
  2.  Mnyama anayefanana na ngombe
  3. Wanyama wanaofanana na ngombe 
  4. Wanyama wanaofanana na mango mbe 
  5. Mnyama wanaofanana na ngombe.
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256