STD VII KISWAHILI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2014

2014: KISWAHILI

 SEHEMU A: SARUFI

 Katika swali la 1 - 20, andika herufi ya jibu lililo sahihi katika karatasi yaka ya kujibia.

 1. "Yeye amefaulu mitihani yake vizuri." katika sentensi hii neno lipi limetumika kama kielezi? 

  1.  amefaulu
  2.  yeye
  3.  vizuri 
  4.  mitihani
  5.  yake 
Chagua Jibu


2. "Dada ameandika barua kwa baba." Sentensi hii iko katika kauli gani? 

  1.  kutendea
  2.  kutenda
  3.  kutendwa 
  4.  kutendeana
  5.  kutendeka
Chagua Jibu


3. Katika sentensi zifuatazo ipi ni sahihi?

  1. Nimekuja hapa tangia asubuhi 
  2. Nimekuja hapa tangiapo asubuhi 
  3. Nimekuja hapa tanguapo asubuhi 
  4. Nimekuja hapa tangu asubuhi 
  5. Nimekuja hapa tangiepo asubuhi 
Chagua Jibu


4. Neno lipi ni tofauti na maneno mengine kati ya maneno yafuatayo?

  1.  viwakilishi
  2.  vivumishi
  3.  vielezi 
  4. vitenzi
  5. visaidizi 
Chagua Jibu


5. "Tunu angalisoma ..... mtihani wake." Neno lipi linakamilisha sentensi hiyo kwa usahihi? 

  1.  angefaulu
  2.  angalifaulu
  3. asingefeli 
  4.  angelifaulu
  5. asingalifaulu 
Chagua Jibu


6. "Mnyama mkali amekamatwa leo." Katika sentensi hii neno "mkali" limetumika kama aina gani ya neno? 

  1. kielezi
  2. kiwakilishi
  3. kitenzi 
  4. kivumishi
  5. kiunganishi 
Chagua Jibu


7. "juma amefika na hatacheza mpira" Kitenzi "hatacheza" kipo katika half gani? 

  1.  Ukanushi
  2.  Titnilifu
  3.  Mazoea 
  4.  Ujao
  5.  Shurutia 
Chagua Jibu


8. "Alisema hanywi dawa tena." Kauli halisi ya sentensi hii ni ipi? 

  1. "Hanywi dawa"
  2. "Hatakunywa dawa" 
  3. "Sinywi dawa" 
  4.  "Sitakunywa tena dawa"
  5. ."Sinywi tena" 
Chagua Jibu


9. "Walikotoka kuna mvua." Sentensi hii ipo katika wakati gani? 

  1. Mazoea
  2. Shurutia
  3. Uliopo 
  4. UliopitaE.Ujao
Chagua Jibu


10. "Hamisa na Hanifa ni mapacha walioungana." Katika sentensi hii neno "na" limetumikakama aina gani ya neno?

  1. Kihisishi
  2. Kiunganishi 
  3. Kimilikishi
  4. Kivumishi 
  5. Kiwakilishi
Chagua Jibu


11. Panya huyu anakula unga wangu. Wingi wa sentensi hii ni upi?

  1. Panya hawa wanakula unga wangu.
  2. Mapanya hawa wanakula unga wetu.
  3. Panya hizi zinakula unga wangu.
  4. Panya hizi zinakula unga wetu.
  5. Panya hawa wanakula unga wetu.
Chagua Jibu


12. Siku ile ya maandamano kulikuwa na...........wa pikipiki. Ni neno lipi linakamilisha sentensi hii?

  1.  msururu 
  2.  msuluru 
  3.  msurulu
  4.  Msululu 
  5.  musururu
Chagua Jibu


13. "Mpira wetu umechanika vibaya" Sentensi hii ipo katika kauli gani?

  1.  Kutenda 
  2.  Kutendeka 
  3.  Kutendeana
  4.  Kutendwa 
  5.  Kutendewa
Chagua Jibu


14. Neno mchwa lina silabi ngapi?

  1.  Mbili 
  2.  Tana 
  3.  Moja
  4.  Nne 
  5.  Tatu
Chagua Jibu


15. "Hapa ...............alipoishi chifu Mirambo." Ni neno lipi linakamilisha sentensi hii kwa usahihi?

  1.  ndiko 
  2.  ndimo 
  3.  ndiyo
  4.  ndipo 
  5.  ndio
Chagua Jibu


16. Atakapomnyonyoa yule hata ......... kwenye moto. Kitenzi kipi kinakamilisha tungo hii?

  1.  atambanika 
  2.  anambanika 
  3.  humbanika
  4.  amembanika 
  5.  alimbanika
Chagua Jibu


17. "Kitabu changu ni cheusi, chako ni cheupe." Neno "chako" ni aina gani ya neno?

  1.  Kivumishi 
  2.  Kiwakilishi 
  3.  Kielezi
  4.  Kihusishi 
  5.  Kiunganishi
Chagua Jibu


18. Yeye ni kijana mdogo. Neno "yeye" lipo katika nafsi gani?

  1.  Ya kwanza umoja 
  2.  Ya tatu umoja 
  3.  Ya pill umoja
  4.  Ya tatu wingi 
  5.  Ya pill wingi
Chagua Jibu


19. Kinyume cha kitenzi "paa" ni kipi?

  1.  Toweka 
  2.  Potea 
  3.  Elea
  4.  Shuka 
  5.  Tua
Chagua Jibu


20. Mwalimu J. K. Nyerere ni mwasisi wa chama cha TANU. Neno "ni" limetumika kama ainaipi ya kitenzi?

  1.  Kitenzi kikuu 
  2.  Kitenzi kisaidizi
  3.  Kitenzi kishirikishi 
  4. Kitenzi kikamilifu
  5.  Kitenzi kitegemezi
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256