11. Sentensi ipi kati ya hizi ipo katika hali timilifu?
12. Neno lipi ni tofauti na maneno mengine kati ya yafuatayo?
13. "Kitabu chako ni kizuri, ukienda dukani nami uninunulie ... ......” Ni kifungu kipi cha maneno hukamilisha sentensi hiyo?
15. Mkutano haukufanyika kwa sababu mwenyekiti na katibu hawakufika. Kifungu kipi cha maneno kati ya vifuatavyo kinasadifu sentensi hiyo?
16. Mlinzi wa mlangoni huitwaje?
17. Joshua yuko jikoni anapaa samaki. Neno "anapaa” kama lilivyotumika katika sentensi hii lina maana ipi?
18. "Mtoto wa ngombe anaitwa ndama, watoto wa kuku, bata, kanga wanaitwa vifaranga, kimatu ni mtoto wa nani?
19. Kisawe cha neno ”eupe” ni kipi?
20. Siku ya nne baada ya leo huitwaje?
SEHEMU C
Soma kifungu cha habari na kishajibu maswaliyanayofuata:
Maji ni moja kati ya vitu vitatu muhimu sana vinavyotuwezesha kuishi. Vitu vingine ni hewa na chakula. Hewa ndiyo yenye umuhimu wa kwanza, ikifuatiwa na chakula. Kusingelikuwa na maji maisha ya binadamu na ya viumbe wengine yasingewezekana. Kila mtu anaelewa umuhimu wa maji katika maisha. Maji yanatawala maisha kwa kiasi kikubwa sana. Baadhi ya viumbe kama vile samaki, mamba, kasa, konokono, nyangumi na wengineo maskani yao ni majini, hivyo maji yakikosekana viumbe hao huweza kuaga dunia.
Binadamu anatumia maji kwa shughuli mbalimbali. Shughuli hizo ni pamoja na kupikia, kufulia, kusafishia vyombo, kuoga na kunywa. Katika sehemu nyingi za nchi yetu watu hutumia maji kwa kumwagilia bustani za mboga, maua na miti. Katika maeneo yenye mito mikubwa na maziwa maji yake hutumika kwa kumwagilia mashamba kama yale ya mpunga na mahindi. Kilimo cha umwagiliaji kinafaa kwa sababu mkulima anakuwa na uhakika wa kuvuna.
Maji ya mvua huwezesha watu kulima na kupanda mazao ya chakula na ya biashara. Hivyo zipo sehemu ambazo wakulima hulima kilimo cha umwagiliaji lakini sehemu kubwa ya wakulima hutegemea kilimo cha mvua.
Kwa ujumla maji yawe ya mvua au yanayotokana na mito au maziwa yana umuhimu mkubwa mno kwa binadamu kama walivyosema wahenga maji ni uhai, hivyo inashauriwa kwamba ni muhimu kwa kila mtu kunyvva maji safi na salama ili kulinda siha zetu.
MASWALI
31.Vitu vitatu muhimu vinavyomwezesha binadamu kuishi ni vipi?
32.Wakulima wengi kama ilivyoelezwa katika habari hii hulima kilimo kinachotegemea nini?
33. Kiumbe yupi kati ya wafuatao halandani na wenzie?
34.Kilimo cha umwagiliaji kina sifa gani kubwa?
35.Neno "siha" kama lilivyotumika katika kifungu hiki cha habari lina maana gani?
36. "Kuaga dunia" ni msemo wenye maana gani?
37. Ni kwanini mtunzi wa habari hii anashauri watu kunywa maji safi na salama?
38.Neno "maskani" kama lilivyotumika katika kifungu cha habari lina maana gani?
39.Kichwa cha habari kinachofaa kwa kifungu hiki ni kipi?
39.Kichwa cha habari kinachofaa kwa kifungu hiki ni kipi?
SEHEMU D
USHAIRI
Soma shairi lifuatalo kisha jibu maswali yanayofuata
Nyumbani kwako kuzuri,japokuwa ni pangoni,
Nyumba yako nijohari,ya mwenzako sitamani, Hata pawe pa tajiri, hapafai maishani,
Nyumbani kwakojohari, kwingine usitamani.
Kwingine usitamani, nyumbani kwakojohari,
Unaishi kwa amani, na pia kwa ujasiri,
Hiyo kweli abadani, nyumbani kunasetiri,
Nyumbani kwakojohari, kwingine usitamani,
Uipende nyumbayako, utaona raha yake,
Kisha penda nduguyako, kwako apaone kwake, Dunia mahangaiko, usipende pekepeke,
Nyumbani kwakojohari, kwingine usitamani.
Usichaguejirani, bali chagua rafiki,
Usitenge asilani, shauri pia afiki,
Palipo na burudani, kaa nao marafiki,
Nyumbani kwakojohari, kwingine usitamani
MASWALI
41. Kichwa cha shairi kinachofaa ni kipi?
42. Kituo katika shairi hili ni kipi?
43. Neno "johari" kama lilivyotumiwa na mtunzi lina maana gani?
44. Neno "pekepeke" kama lilivyotumiwa na mshairi lina maama gani?
44. Neno "pekepeke" kama lilivyotumiwa na mshairi lina maama gani?
45. Vina vya kati na vya mwisho katika ubeti wa tatu ni vipi?
46. Funzo linalopatikana katika shairi hilo linawakilishwa na methali ipi kati ya zifuatazo?
SEHEMU E
UTUNCAJI
Katika Sehemu hii kuna habariyenye sentensi nne (4) zilizoandikwa bila mtiririko sahihi unatakiwa kuzipanga sentensi hizo ili ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi A, B, C, na D
47. Vile vile matunda huongeza damu mwilini
Chagua Jibu48. Hivyo matunda yana umuhimu mkubwa katika miili yetu.
Chagua Jibu49. Lakini watu wasiokula matunda hupata maradhi kama vile ugonjwa wa fizi, macho na ngozi.
Chagua Jibu50. Kula matunda kunasaidia kuponyesha magonjwa na vidonda haraka, pia husaidia macho kuona vizuri katika mwanga hafifu.
Chagua JibuKISWAHILI DARASA LA IV 2013
SEHEMU A
Sikiliza sentensi zinazomwa kisha uziandike.
SEHEMU B
Jibu swali la 6 - 10 kwa kuchagua herufi ya jibu sahihi na kuiandika katika kisanduku pembeni ya kilo swali.
6. Mtu anayeongoza meli huitwa
7. Nimepatwa na. . . . . . . . . . . kutokana na msiba wa mjomba.
8. Usipoziba . . . . . . . . . . . utajenga ukuta
9. Mkoa wa Iringa ni mojawapo ya mikoa iliyoko nyanda za juu ......
10. Ili kupika ugali unahitaji maji na
SEHEMU C
Jibu swali la 11 - 15 kwu kukamilisha methali zifuatazo.
11. Mchelea mwana kulia . . . . . . . . . . .
Fungua Jibu12. Leo ni leo . . . . . . . . . . .
Fungua Jibu13. Macho hayana. . . . . . . . . . .
Fungua Jibu14. Hasira . . . . . . . . . . .
Fungua Jibu15. Kusikia. . . . . . . . . . .
Fungua JibuSEHEMU D
Katika swali la 16 - 20 umepewa methali na vitendawili. Chagua jibu sahihi kutoka sehemu B na kuandika herufi ya jibu sahihi.
SEHEMU A | SEHEMU B |
16. Bibi hatui mzigo wake. . . . . . . . . . 17. Kulia kwake ni kicheko kwetu. . . . . . . 18. Jungu kuu halikosi. . . . . . . . . 19. Akiba . . . . . . . . . . 20. Mjomba hataki tuonane. . . . . . . . . . |
|
SEHEMU E
UFAHAMU
Soma habari ifuatayo kisha jibu swali la 21 hadi 25.
Gulio ni soko linalofanyika siku maalumu iliyochaguliwa na watu wa eneo husika. Kwa kawaida huwa mara moja kwa juma. Watu huuza na pia hununua bidhaa za aina mbalimbali. Katika magulio mengi, bidhaa zinazouzwa ni zile zinazopatikana katika eneo haio na vijiji vya jirani. Watu wa mijini pia hupeleka na kuuza bidhaa mbalimbali kwenye magulio ya vijijini.
Bidhaa zinazouzwa kwa wingi katika magulio mengi ni mazao ya shambani kama mahindi, maharagwe, mihogo, matunda na mboga za majani. Watu wa mijini huuza nguo na vyombo vya nyumbani. Mara nyingi huuza sahani, bakuli. sufuna na vikombe. Wengme huuza chumvi, vinu, visu, vyungu mikeka na vikapu.
Maswali
21. Andika kichwa cha haban uliyoisoma
Fungua Jibu22. Gulio ni nini?
Fungua Jibu23. Gulio hufanyika mara ngapi kwa juma?
Fungua Jibu24. Ni shughuli zipi hufanyika gulioni?
Fungua Jibu25. Kutokana na haban uliyo soma matunda na mboga mboga huuzwa na watu kutoka wapi?
Fungua Jibu