Katika swali la 1 — 20, weka kivuli katika herufiyajibu lililo sahihi.
1. "Wachache wamehamia Boro". Katika sentensi hiyo "Wachache" limetumika kama aina gani ya neno?
2. Alimwita nyumbani kwake kwa dhamira ya kumpa karo ya shule. Neno "dhamira" lina maana ipi?
3. Kauli ipi inaonesha hali ya kutendewa?
4. Katika vifungu vya maneno vifuatavyo, kifungu kipi kipo katika kauli taarifa?
5. Mwenyekiti hakufika mkutanoni leo. Kitenzi "hakufika" kipo katika hali gani?
6. "Wapiganaji wetu walipowasili visiwa vya Comoro walishangiliwa kwa Ni neno lipi linakamilisha sentensi hiyo?
7. Mawaziri wote wa Baraza la Mapinduzi waliapishwa. Neno "wote" limetumika kama aina gani ya neno?
8. Babu amemhamishia yule mbuguma kwenye zizi kubwa. Neno "mbuguma" lina maana
9. "Chama kimeteka nyara sera ya serikali." Wingi wa sentensi hiyo ni upi?
10. Nyumba ya ndege huitwaje?
11. "Wanafunzi hodari watapewa zawadi". Sentensi hiyo ipo katika wakati gani?
12. Maji yamejaa "pomoni" Neno "pomoni" ni aina ipi ya neno?
13. Kati ya maneno "Sherehi, Sherehe, Shamrashamra, Hafla, Tafrija" neno lipi halihusiani na mengine?
14. Neno lipi kati ya maneno yafuatayo lina maana sawa na "thubutu"?
15."Kuzua kizaazaa" ni msemo wenye maana gani?
16. Mtu anayetafuta kujua jambo fulani kwa kuuliza maswali huitwaje?
17. Neno Mchakato lina maana ya mfululizo wa................
18. Neno lipi kati ya yafuatayo lina maana sawa na neno shehena
19. Mtu aliyezaliwa na wazazi wa rangi mbalimbali huitwaje?
20. Baada ya miaka minne Kalunde ... ...... mafunzo yake ya udaktari. Ni neno lipi linakamilisha sentensi hiyo?
Katika swali la 21 — 30, weka kivuli katika herufiyajibu lililo sahihi.
21. Methali isemayo, "Katika msafara wa mamba na kenge wamo" iko sawa na methali ipi kati ya zifuatazo?
22. Diengi anapenda kuwarairai watu. "l<urairai watu" ni msemo wenye maana ipi?
23. Msemo "kubarizi" maana yake ni kukusanyika kwa ajili ya .
24. Methali isemayo "Kila mtoto na koja lake" ina maana gani?
25. Nahau isemayo "kuvishwa kilemba cha ukoka" ina maana gani?
26. Tegua kitendawili kifuatacho: "Nyumbani kwangu kuna jini mnywa maji."
27. "Wakulima wa kahawa wa wilaya ya Mbinga wamepewa heko kwa kuzalisha kahawa bora".
Msemo "wamepewa heko" hufanana na msemo gani kati ya ifuatayo?
28. Methali isemayo, "Mwenda pole hajikwai" inafanana na methali ipi kati ya zifuatazo?
29. Methali ipi kati ya hizi zifuatazo haifanani na zingine?
30. Mwamba ngoma .. Kifungu kipi cha maneno kinakamilisha methali hiyo?
SEHEMU C
UFAHAMU
Soma kwa makini habari ifuatayo kisha jibu maswali 31 — 40 kwa kuweka kivuli katika herufi ya jibu lililo sahihi.
Mpendwa kaka Yohana,
Natumani hujambo na unaendelea vizuri na masomo yako. Nimefurahi kusikia kwamba umechaguliwa kujiunga na masomo ya Sekondari. Ndugu wote wanakupongeza na kukutakia kila la kheri katika masomo yako. Soma kwa bidii zaidi kwani elimu ni bahari na haina mwisho.
Baba na mama walifurahi sana baada ya kupata taarifa za kuchaguliwa kwako kwa-njia ya simu kutoka kwa shangazi. Wanamshukuru sana shangazi kwa kukuwezesha na misaada yake mingi kwako ya hali na mali. Baba ameahidi kumtembelea shangazi tarehe ishirini mwezi wa kumi na moja mwaka huu ili kumkabidhi zawadi aliyomwandalia kutokana na ukarimu wake kwako.
Rafiki yako Juma alifika hapa nyumbani akasema kwamba ataniletea picha nikutumie. Hamisi amekuandalia zawadi ambayo atakukabidhi utakapokuja nyumbani wakati wa likizo yako ya mwisho wa muhula. Tunu amesema atakutembelea, lakini uwe mwangalifu unapoongea naye asije akakuchezea shere. Siku hizi ni msanii.
Nisalimie sana shangazi na wanae wote, yaani Amani, Anasitazia na Asia. Sisi sote tunakutakia kila la kheri katika masomo yako.
Akupendaye daima, Mdogo wako, Tumaini.
31. Neno "ukarimu” lina maana sawa na lipi kati ya maneno yafuatayo?
32. Mwandishi wa barua hii ametumia msemo "kuchezea shere” Msemo huo una maana ipi?
33. Ushindi wa Yohana na mafanikio yake katika masomo umetokana na nini?
34. Wazazi na ndugu zake Yohana walipata taarifa ya kufaulu kwake kwa njia gani?
35. Uhusiano wa Yohana na watoto wa shangazi yake ni upi?
36. Katika barua hii mwandishi anafananisha elimu na nini?
37. Unafikiri ni sababu ipi ilimfanya baba yake Yohana kumwandalia dada yake zawadi?
38. Lengo la Tumaini kumwandikia kaka yake barua lilikuwa lipi?
39. Kifungu hiki cha habari ni aina gani ya barua?
40. Ni methali ipi inatoa fundisho kutokana na ushindi wa Yohana?
Soma kwa makini shairi lifuatalo kisha jibu maswali 41 - 46 kwa kuweka kivuli katika herufiya jibu.
Nimekwisha peleleza, karibu kila mahali,
Mule wanamotangaza, matangazo lugha mbili, Juu kuwa Kingereza, Chini kuwa Kiswahili, Juu kiwe Kiswahili, Chini kiwe Kingereza.
Kitangazwe Kingereza, baada ya Kiswahili
Hivi tutapotimiza, lugha itakuwa ghali,
Hivi mnavyofanyiza, sana mnaidhalili,
Juu kiwe Kiswahili, Chini kiwe Kingereza
Serikali bembeleza, tafakari tafadhali,
Jambo hili kueleza, kwa zingine serikali Kiswahili kutangaza, kuwa Chini twakidhili Juu kiwe Kiswahili, Chini kiwe Kingereza.
Tuache kukipumbaza, kwa andiko au kauli, Kwa nyuma kukisogeza, kukipa kisulisuli,
Lazima kuyafukuza, yawezayo kikatili,
Juu kiwe Kiswahili, Chini kiwe Kingereza
Na wenyewe kujikaza, kwa bidii za kimwili kiswahili kutukuza, tukivalie bangili,
Ngomani kutumbuiza, waume na wanawali Juu kiwe Kiswahili, Chini kiwe Kingereza.
41. Katika shairi hilo mstari wa pili katika ubeti wa pili una mizani mingapi?
42. Katika ubeti wa nne, vina ni vipi?
43. Kituo ni kipi katika shairi hili?
44. Shairi hili linahimiza kuhusu nini?
45. Ujumbe unaopatokana katika shairi hili unafanana na methali ipi?
46. Kutokana na shairi ulilosoma neno "kutukuza” lina maana ipi?
SEHEMU E
UTUNGAJI
Umepewa habari yenye sentensi nne(4) zilizoandikwa bila mtiririko sahihi wa mawazo katika swali 47 — 50. Zipange sentensi hizo ili ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi A, B, C, na D. Weka kivuli katika herufi yajibu sahihi.
47. Hivyo mazoezi huleta afya, kwa hiyo ni muhimu kwa kila mmoja wetu kufanya mazoezi.
Chagua Jibu48. Mtu asiyefanya mazoezi anapata maradhi ya moyo; atanenepa kupita kiasi, kwa hiyo atapata ugonjwa wa kuumwa mgongo na magoti.
Chagua Jibu49. Mazoezi ya viungo yanachangamsha misuli ya mwili, mifupa na ubongo.
Chagua Jibu50. Lakini mtu anayefanya mazoezi anaepuka magonjwa ya moyo na msukumo wa damu.
Chagua Jibu