STD VII KISWAHILI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2015

Katika swali la 1 — 20, weka kivuli katika herufiyajibu lililo sahihi.

1.  "Ramadhani anacheza mpira uwanjani." Sentensi hii ikiwa katika hali ya mazoea itakuwa ipi kati ya hizi zifuatazo?.....

  1. Ramadhani hucheza mpira uwanjani.
  2. Ramadhani atacheza mpira uwanjani. 
  3. Ramadhani alicheza mpira uwanjani. 
  4. Ramadhani amecheza mpira uwanjani 
  5. Ramadhani anacheza mpira uwanjani.
Chagua Jibu


2.          "Bura yangu sibadili na rehani." Kitenzi "sibadili" kipo katika hali ipi?.......

  1. Mazoea 
  2. Timilifu 
  3. Ukanushi 
  4. Kuendelea
  5.  Shurutia
Chagua Jibu


3.          "Babu alikuwa analima shambani." Neno "alikuwa" ni aina ipi ya kitenzi? .

  1. Kitenzi kikuu 
  2.  Kitenzi kitegemezi 
  3. Kitenzi jina
  4. Kitenzi kishirikishi 
  5. Kitenzi kisaidizi
Chagua Jibu


4.          Katika sentensi zifuatazo ipi ina maana sahihi?..

  1. Sikuwa najua Halima ni dada yako.
  2. Sikujua kuwa Halima ni dada yako. 
  3. Sikuwa ninajua Halima ni dada yako.
  4. Sikuwa ninajua kwamba Halima ni dada yako.
Chagua Jibu


5.          Ni neno lipi kati ya yafuatayo ni kisawe cha neno "hifadhi"? .

  1. Weka 
  2.  Panga    
  3. Tunza 
  4.  Ficha  E.
  5.  Funga
Chagua Jibu


6.          Lahaula! Loo! La hasha! Masalale! Ni maneno ya aina gani? 

  1. Vitenzi 
  2. Vihisishi 
  3. Viwakilishi
  4.  Vivumishi 
  5.  Viunganishi
Chagua Jibu


7.          "Ingawa walipata matatizo mengi safarini walifika salama." Neno lipi linakamilisha sentensi hiyo kwa usahihi?

  1. vilevile
  2. kwa hiyo
  3.  halikadhalika D. 
  4. hivyo 
  5. hatimaye
Chagua Jibu


8.          "Mjukuu wangu hupenda kuniamkia kila mara." Sentensi hiyo ipo katika kauli gani? 

  1. Kutendwa  
  2. Kutenda  
  3. Kutendeka
  4. Kutendana  
  5.  Kutendewa
Chagua Jibu


9.          "Wawili wameshindwa kupanda mlima Kilimanjaro." Kiwakilishi katika sentensi hiyo ni kipi? 

  1. Mlima 
  2.  Kupanda 
  3.  Wameshindwa
  4. Kilimanjaro 
  5. Wawili
Chagua Jibu


10.      ”Vita ilipoanza nchini Kenya watu wote . . Kitenzi kipi kinakamilisha sentens hiyo?

  1. walitweta 
  2.  walitaharuki 
  3. walitunukiwa 
  4. walinusurika  
  5.  walitahamaki
Chagua Jibu


11.      "Tulicheza ngoma na kuimba usiku kucha.” Katika sentensi hii watenda ni nafsi ipi?

  1. Ya tatu wingi 
  2. Ya pili wingi
  3.  Yapili umoja
  4. Ya tatu umoja 
  5. Ya kwanza wingi.
Chagua Jibu


12.      ”Utundu wake ulimfanya ajulikane shuleni.” Neno "Utundu” limetumika kama aina gani

neno? 

  1. Kivumishi  
  2.  Nomino
  3.  Kiwakilishi
  4.  Kitenzi  
  5. Kielezi.
Chagua Jibu


13.      "Mwanamuziki hodari aliimba nyimbo vizuri.” Kielezi katika sentensi hii ni kipi? ........

  1. Hodari 
  2.  Aliimba 
  3. Mwanamuziki
  4. Nyimbo  
  5. Vizuri
Chagua Jibu


14.      "Mgeni aliondoka alikofikia.............kuaga.” Kifungu kipi cha maneno kinachokamilishE sentensi hiyo kwa usahihi?

  1. licha ya 
  2. pasi ya 
  3. bila kwa 
  4.  bila ya   
  5.  bila na
Chagua Jibu


15.      Neno moja linalojumuisha herufi "a, e, i, o na u” ni lipi? 

  1. Silabi   
  2.  Konsonanti   
  3. Mwambatano
  4.  Kiambishi 
  5. Irabu.
Chagua Jibu


16.      "Kaka anapenda kujisomea chumbani mwake.” Katika sentensi hiyo kitenzi kisaidizi ni kipi? ........

  1. Anapenda   
  2. . Chumbani 
  3.  Kujisomea
  4. Kaka  
  5.  Kwake.
Chagua Jibu


17.      ”Mchezo mkali ni ule tuliocheza ......... ya Timu ya Majengo.” Neno lipi linakamilisha tungc hiyo kwa usahihi?

  1. zidi
  2. zaidi
  3. kabla
  4. thidi
  5. dhidi
Chagua Jibu


18.      Mama Ntilie akiondoka, uondoke naye. Sentensi hii ipo katika wakati gani? ........

  1. Ujao 
  2.  Timilifu 
  3.  Shurutia 
  4.  Uliopo 
  5.  Mazoea.
Chagua Jibu


19.      Mpira umegonga mwamba nusura goli liingie. Neno lipi linaonesha kitendwa? ........

  1. Nusura 
  2.  Goli C. 
  3. Mpira D.
  4.  Mwamba 
  5. Liingie.
Chagua Jibu


20.      Ni neno lipi kati ya haya yafuatayo ni tofauti na mengine? ........

  1. Sahibu 
  2.  Ajuza 
  3. Msiri
  4. Mwandani 
  5.  Mwenzi
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256