Katika swali la 1 — 20, weka kivuli katika herufiyajibu lililo sahihi.
1. "Ramadhani anacheza mpira uwanjani." Sentensi hii ikiwa katika hali ya mazoea itakuwa ipi kati ya hizi zifuatazo?.....
2. "Bura yangu sibadili na rehani." Kitenzi "sibadili" kipo katika hali ipi?.......
3. "Babu alikuwa analima shambani." Neno "alikuwa" ni aina ipi ya kitenzi? .
4. Katika sentensi zifuatazo ipi ina maana sahihi?..
5. Ni neno lipi kati ya yafuatayo ni kisawe cha neno "hifadhi"? .
6. Lahaula! Loo! La hasha! Masalale! Ni maneno ya aina gani?
7. "Ingawa walipata matatizo mengi safarini walifika salama." Neno lipi linakamilisha sentensi hiyo kwa usahihi?
8. "Mjukuu wangu hupenda kuniamkia kila mara." Sentensi hiyo ipo katika kauli gani?
9. "Wawili wameshindwa kupanda mlima Kilimanjaro." Kiwakilishi katika sentensi hiyo ni kipi?
10. ”Vita ilipoanza nchini Kenya watu wote . . Kitenzi kipi kinakamilisha sentens hiyo?
11. "Tulicheza ngoma na kuimba usiku kucha.” Katika sentensi hii watenda ni nafsi ipi?
12. ”Utundu wake ulimfanya ajulikane shuleni.” Neno "Utundu” limetumika kama aina gani
neno?
13. "Mwanamuziki hodari aliimba nyimbo vizuri.” Kielezi katika sentensi hii ni kipi? ........
14. "Mgeni aliondoka alikofikia.............kuaga.” Kifungu kipi cha maneno kinachokamilishE sentensi hiyo kwa usahihi?
15. Neno moja linalojumuisha herufi "a, e, i, o na u” ni lipi?
16. "Kaka anapenda kujisomea chumbani mwake.” Katika sentensi hiyo kitenzi kisaidizi ni kipi? ........
17. ”Mchezo mkali ni ule tuliocheza ......... ya Timu ya Majengo.” Neno lipi linakamilisha tungc hiyo kwa usahihi?
18. Mama Ntilie akiondoka, uondoke naye. Sentensi hii ipo katika wakati gani? ........
19. Mpira umegonga mwamba nusura goli liingie. Neno lipi linaonesha kitendwa? ........
20. Ni neno lipi kati ya haya yafuatayo ni tofauti na mengine? ........
Katika swali la 21 — 30, weka kivuli katika herufiya jibu lililo sahihi.
21. Nahau isemayo, "Mtu mwenye ndimi mbili" ina maana ipi kati ya zifutazo? ...... .
22. Wanafunzi walipotoka safari walilala usingizi wa pono. Msemo usemao, "Usingizi wa pono" una maana gani?
23. Kitendawili kisemacho: "Kamba yangu ndefu lakini haiwezi kufunga kuni," kina maana ipi kati ya hizi zifuatazo?
24. Methali isemayo: "Mgaagaa na upwa hali wali mkavu," inatoa funzo gani
25. Usingelitia chumvi kwenye kile kikao wajumbe wasingeligombana. "Kutia chumvi" ni usemi wenye maana gani?
26 "........... hufa maskini." Kifungu kipi hukamilisha methali hiyo kwa usahihi? .
27. Nahau ipi kati ya hizi zifuatazo hutumika kwa watu ambao matendo yao si ya kupendana?
28. Methali ipi kati ya hizi zifuatazo inapingana na hii, "Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu."
29. Methali ipi kati ya hizi zifuatazo inapingana na hii, "Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu”.
30. "Mchelea mwana kulia hulia yeye mwenyewe”. Methali hii inatoa funzo gani?
SEHEMU C
Soma kwa makini habari ifuatayo kisha jibu maswali 31 — 40 kwa kuweka kivuli katika herufi ya jibu lililo sahihi.
Matunda kama yalivyo mazao mengine ya kilimo yanatokana na mimea mbalimbali. Kwa mfano fenesi ni tunda litokanalo na mfenesi na chungwa hutokana na mchungwa. Maembe, mapapai, mananasi na mapera ni matunda matamu. Ubuyu, ukwaju na limau ni matunda machachu. Hata hivyo, karibu matunda mengi huwa machachu yakiwa mabichi, yakiiva huwa matamu.
Miaka ya hivi karibuni watu wengi wamepanda mimea ya matunda kwenye maeneo ya nyumba zao, hivyo kujipatia matunda kwa njia rahisi. Baadhi ya watu wanaoishi katika mikoa kama vile Tanga na Morogoro wamelima mashamba ya matunda na wameshaona faida ya kilimo hicho na kupanua mashamba yao. Licha ya watu hao kujipatia chakula bora, wameuza na kuwa na pato kubwa.
Matunda yana umuhimu mkubwa sana katika miili yetu. Matunda tunayokula yanaikinga miili yetu isipatwe na maradhi. Pia matunda yanaongeza damu mwilini, husaidia kuponyesha vidonda haraka na macho kuona vizuri katika mwanga hafifu. Watu wasiokula matunda hupata udhaifu wa fizi ambao husababisha fizi kutoa damu.
Aidha matunda ni kiburudisho wakati wa joto. Watu wengi wamekuwa wakisindika matunda ili kupata juisi kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na biashara.
MASWALI
31. Kichwa cha habari hii kinachofaa zaidi ni kipi?
32. "Watu wanaokula matunda huepuka magonjwa mengi,” ni methali ipi inaendana na kauli hii?
33. Maji ya matunda yaliyokamuliwa huitwaje? .
34.
"Matunda yaliyoiva” ina maana sawa na ipi kati ya zifuatazo? ........
35."Kilimo cha matunda kimekuwa cha faida kubwa kwao.” Methali ipi ambayo inaendana na maelezo hayo?
36. Ni kwanini wakulima wa matunda hupanua mashamba yao?
37. Matunda ya ubuyu na ukwaju yakiwa yameiva huwa na ladha gani?
38. Kazi kubwa ya matunda mwilini ni ipi?
39. "Kusindika matunda” ina maana sawa na kifungu kipi kati ya vifuatavyo?
40. Umepata funzo gani kutokana na kifungu hiki cha habari?
SEHEMU D
Soma kwa makini shairi lifuatalo kisha jibu maswali 41 - 46 kwa Kuweka kivuli katika herufi ya jibu.
Mtu kujitegemea, huwajambo Ia lazima,
Usipende subiria, kusaidiwa daima,
Huwezi kuendelea, ndugu usipojituma,
Kamwe hupati heshima, usipojitegemea.
Kama Mungu kakuumba, mzima huna kilema, Fedheha kuombaomba, takuwa mtu wa nyuma, Hutakuja kujigamba, ukikudharau umma. Kamwe hupati heshima, usipojitegemea.
Kazi mtu usidhani, sharti niya kusoma,
Ya kuleta ofisini, na kuhesabu ndarama,
Waweza kwenda shambani, ushikejembe kulima, Kamwe hupati heshima, usipojitegemea.
Utaambiwa doezi, mtu uso taadhima,
Pengine uitwe mwizi, umezoea dhuluma, Wajapo wapelelezi, ndiwe watakuandama, Kamwe hupati heshima, usipojitegemea.
41. Katika shairi ulilosoma neno "ndarama" lina maana ipi?
42. Kisawe cha neno "taadhima" ni kipi?
43. Ujumbe unaopatikana katika shairi hili unaweza kuwasilishwa kwa methali ipi kati ya zifutazo? ........
44. Katika shairi ulilosoma kituo bahari ni kipi?
45. Katika shairi ulilosoma nusu mstari una mizani ngapi?
46. Neno "fedheha" kama lilivyotumika katika shairi hili lina maana gani?
Umepewa habari yenye sentensi nne(4) zilizoandikwa bila mtiririko sahihi wa mawazo katika swali 47 — 50. Zipange sentensi hizo ili ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi A, B, C, na D weka kivuli katika herufi ya jibu sahihi.
47. Ukataji wa miti kwa wingi kwa ajili ya ujenzi na shughuli zingine huweza kuisababisha nchi yetu ya Tanzania kuwa jangwa.
Chagua Jibu48. Kutokana na miti watu hujenga nyumba nzuri za kila namna, zinazopendeza na za kudumu.
Chagua Jibu49. Hivyo ni muhimu kwa kila mtu kupanda mti kila anapokata mti kwani nchi isiyo na miti ni sawa na mtu ambaye amevuliwa nguo.
Chagua Jibu50. Miti ina faida nyingi sana kwa binadamu.
Chagua Jibu