STD VII KISWAHILI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2007

KISWAHILI 2007

SEHEMU A

SARUFI

Katika swali Ia 1-15 andika herufiyajibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia.

1. Mvutano kati ya wanakijiji na viongozi wao ulikuwa haujapatiwa neno lipi linakamilisha sentensi hii?

  1. Ugunduzi 
  2. Ufunguzi 
  3. Ufumbuzi
  4. Uvumbuzi 
  5. Uchunguzi
Chagua Jibu


2. Maneno "mrefu, mweusi, mwerevu na mpole" yakitumika pamoja na majina hufanya kazi gani?

  1. Kivumishi 
  2. Kielezi 
  3. Kitenzi
  4. Nomino 
  5. Kiswahili
Chagua Jibu


3. Sentensi ipi kati ya zifuatazo ni umoja wa sentensi "Bakari amehamisha mizinga ya nyuki kutoka shambani mwake"?

  1. Bakari amehamisha mizinga ya nyuki shambani
  2. Bakari amehamisha mzinga wa nyuki shambani mwake
  3. Alihamisha kimzinga cha nyuki shambani mwake
  4. Amehamisha kamzinga ka shambani mwake
  5. Bakari ameamishia mzinga wa nyuki shambani mwake
Chagua Jibu


4. Katika sentensi ifuatayo ni neno lipi limetumika kama kiwakilishi "Yule ni mnene kupita kiasi".

  1. Yule
  2. Ni
  3. Mnene 
  4. Kupita 
  5. Kiasi
Chagua Jibu


5. Kinyume cha neno ughaibuni ni kipi?

  1. Nchi jirani 
  2. Magharibi
  3. Nchi za mbali 
  4. Mashariki
  5. Nyumbani
Chagua Jibu


6. Sentensi ipi kati ya hizi zifuatazo ipo katika kauli taarifa?

  1. Rafiki yetu yule kachoka kusubiri
  2. Amechoka kusubiri rafiki yetu yule
  3. Rafiki yetu amesema kwamba amechoka kusubiri
  4. Rafiki yetu vipi, umesema umechoka kusubiri? 
  5. Amesema hajachoka kusubiri
Chagua Jibu


7. Kipi ni kinyume cha neno gwiji?

  1. Mwerevu 
  2. Asiye hodari
  3. Mwanamuziki 
  4. Mwimbaji 
  5. Hodari
Chagua Jibu


8. Katika neno "sitakuwepo" kiambishi kinachoonyesha ni kipi?

  1. -ta- 
  2. -we- 
  3. -ku- 
  4. -po- 
  5. -si-
Chagua Jibu


9. "Mvvanafunzi aliyefaulu vizuri atapewa tuzo". Kishazi tegemezi katika sentensi hii ni kipi?

  1. Atapewa tunzo
  2. Aliyefaulu tunzo
  3. Mwanafunzi aliyefaulu vizuri
  4. Mwanafunzi vizuri atapewa
  5. Aliyefaulu vizuri atapewa
Chagua Jibu


10. Neno lipi limekosekana kuikamilisha sentensi ifuatayo kwa usahihi? "Mtoto haandiki . . . . . . . . . . . hasomi".

  1. Ila
  2. bali
  3. kama 
  4. wala 
  5. hata
Chagua Jibu


11. "Ukifanya vizuri utapongezwa". Sentensi hii ni ya aina gani?

  1. Sahili 
  2. Shurutia 
  3. Changamano 
  4. Tegemezi 
  5. Ambatano
Chagua Jibu


12. "Nyumba ya Amini imejengeka vizuri". Sentensi hiyo ipo katika kauli gani?

  1. Kutenda 
  2. Shurutia
  3. Kutendeka
  4. Kutendeana 
  5. Kutendwa
Chagua Jibu


13. Unaponyumbulisha neno apiza unapata nomino ipi?

  1. Apizo 
  2. Pizo
  3. Apizika
  4. Waapizo 
  5. Apizana
Chagua Jibu


14. Neno lipi ni tofauti na maneno mengine kati ya yafuatayo?

  1. Senge'nge 
  2. Wigo
  3. Barabara
  4. Ukuta 
  5. Ukingo
Chagua Jibu


15. "Uji huu una sukari na maziwa". Ukanushi wa kauli hii ni upi?

  1. Uji huo hauna sukari ila maziwa
  2. Uji huu hauna sukari wala maziwa
  3. Uji huo hauna sukari bila maziwa
  4. Uji huu sukari bila maziwa
  5. Uji huu hauna lakini una maziwa
Chagua Jibu


SEHEMU B

MSAMIATI

Katika swali 16 - 25, andika herufiya jibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia.

16. Neno lenye maana sawa na neno "mawio" ni lipi kati ya yafuatayo?

  1. Macheo 
  2. Magharibi 
  3. Mchana
  4. Jioni 
  5. Machweo
Chagua Jibu


17. Watu waliokusanyika kwa pamoja ili kuabudu huitwaje?

  1. Wafuasi 
  2. Waabudu
  3. Waumini
  4. Waswalishwa 
  5. Wakereketwa
Chagua Jibu


18. Selina alitumwa sokoni kununua mbuzi ya kukuna nazi. Neno "mbuzi" limetumika kwa maana ipi?

  1. Mnyama anayekuna nazi
  2. Kinu cha kutwangia nazi
  3. Kibao chenye kipande cha chuma cha kukunia nazi
  4. Kitu cha kukalia ambacho hutumika kukunia nazi 
  5. Kitu chenye kibao cha kukunia nazi
Chagua Jibu


19. Neno lipi kati ya maneno yafuatayo lina maana sawa na neno "shaghalabaghala"?

  1. Mpangilio
  2. Ovyo ovyo 
  3. Vizuri
  4. Viovu
  5. Faragha
Chagua Jibu


20. Neno lipi kati ya maneno yafuatayo halilandani na mengine?

  1. Kuona 
  2. Kunusa
  3. Kuonja
  4. Kusikia 
  5. Kutoa jasho
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256