KISWAHILI 2006
 SEHEMU A
 SARUFI
 Katika swali la 1-15 andika herufi yajibu lililo sahihi katika karatasiya kujibia.
 1. Huyu ......... mtoto aliyekuwa amepotea.
  - ndio 
- ndiyo 
- ndiye
- ndiyo
- ndivyo
Chagua Jibu    
2. Neno lipi ni kinyume cha neno 'Adili"? .
  - wema 
- uovu 
- ujasiri
- ujanja
- ujinga
Chagua Jibu    
3. "Ala kumbe! Ameondoka leo asubuhi”. Kihisishi ni kipi kati ya maneno haya?
  - Ala kumbe
- leo
- Ala
- kumbe
- ameondoka
Chagua Jibu    
4. Kisawe cha neno shaibu ni .
  - barabara
- baneti
- buda 
- ajuza 
- kigori
Chagua Jibu    
5. Neno "MBWA” lina silabi ngapi?
  - nne
- mbili
- moja 
- tatu 
- sifuri
Chagua Jibu    
6. Kipi kinyume cha neno aghalabu? ......
  - mara nyingi
- mara kwa mara
- nadra
- muda wote
- kila wakati
Chagua Jibu    
7. Kitoto hiki kinacheza kitQtQ. Neno lililopigiwa mstari limetumika kama ...
  - Nomino 
- Kitenzi 
- Kielezi 
- Kivumishi 
- Kielelezi
Chagua Jibu    
8. Shule ile imeendelea ingawa haina umeme. Sentensi hii iko katika aina ipi ya tungo?
  - Tungo tegemezi 
- Tungo sahihi
- Tungo shurutia 
- Tungo ambatano 
- Tungo huria
Chagua Jibu    
9. Sikuweza kutambua ni nani amelala kitandani kwa sababu alijifunika shuka  . . . . . . .
  - Lote 
- Gubigubi
- Zima
- Nzima 
- Zama
Chagua Jibu    
10.Neno "Vibaya” katika sentensi isemayo "Vibaya pia vinanunuliwa” limetumika kama aina ipi ya maneno?
  - Kivumishi 
- Kiwakilishi 
- Kielezi
- Kisifa 
- Nomino
Chagua Jibu    
11. Mkutano kati ya Viongozi wa DECI na Serikali ulikuwa haujapatiwaNeno lipi linalokamilisha sentensi hii?
  - Uchunguzi 
- Ufumbuzi 
- Ufunguzi
- Kutendwa
- Kutendea
Chagua Jibu    
12. 'Salama na Samina wanapendana sana". Sentensi hii ipo katika kauli ipi?
  - Kutendwa 
- Kutendana 
- Kutenda
- Kutendwa 
- Kutendea
Chagua Jibu    
13. Katika neno "tutakuja” kiambishi cha wakati ni .........
  - tu- 
- -ku 
- -ja-
- u
- -ta-
Chagua Jibu    
14. Neno ”MWALIMU” lipo katika upatanisho wa ngeli ya aina gani?
  - A-WA
- I-ZI
- LI-YA 
- U-YA
- U-ZI
Chagua Jibu    
15. Wingi wa sentensi ifuatayo ni ipi? mti huu unaharibu mazingira
  - Miti hizi zinaharibu mazingira
- Miti hiyo inaharibu mazingira
- Miti hii itaharibu mazingira
- Miti hii inaharibu mazingira
- Miti hii imeharibu mazingira
Chagua Jibu    
SEHEMU B
 MSAMIATI
 16. Mzee Mwendapole aliwapa wanaemawaidha juu ya maisha ya baadaye. Neno lililopigiwa mstari lina maana gani?
  - Hotuba 
- Maonyo 
- Urithi
- Mawazo 
- Mahubiri
Chagua Jibu    
17. Neno lenye maana sawa na "mawio” ni lipi kati ya yafuatayo?
  - Asubuhi 
- Maonyo
- Mawazo
- Urithi
- Mahubiri
Chagua Jibu    
18. Mwl. Juma alinunua shati dukani. Neno lililopigiwa mstari lilmetumika kama aina gani ya maneno?
  - Kivumishi 
- Kiwakilishi
- Kielezi 
- Kihisishi
Chagua Jibu    
19. Mtu anayesimamia kazi za shambani anaitwaje?
  - Kiongozi 
- Msimamizi
- Mkuu
- Nokoa 
- Mnyapara
Chagua Jibu    
20. Jina analotumia mjomba kumwita mtoto wa dada yake ni:
  - Mtoto 
- Mjomba
- Binamu
- Shangazi 
- Mpwa
Chagua Jibu    
        BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB  
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA   
Try Another Test |