STD VII KISWAHILI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2009

KISWAHILI 2009

SEHEMU A

SARUFI

Etika swali la 1 - 15 andika herufi yajibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia.

1. Angeliamka mapema asingeliachwa na ndege. Kiambishi cha masharti katika sentensi hiyo ni kipi?

  1. -a- 
  2. -nge- 
  3. -ngeli- 
  4. angeli- 
  5. -ili-
Chagua Jibu


2. Neno lipi kati ya haya yafuatayo halina uhusiano na mengine?

  1. Masika 
  2. Mavunde 
  3. Kipupwe
  4. Kiangazi 
  5. Kifuku
Chagua Jibu


3. Alisema hajisikii vizuri. Kauli halisi ya sentensi hii ni ipi?

  1. "Hajisikii vizuri” 
  2. "Anajisikia vizuri”
  3. "Najisikia vizuri”
  4. "Nilijisikia vizuri” 
  5. "Sijisikii vizuri”
Chagua Jibu


4. Neno lipi linakamilisha sentensi ifuatayo:

Kama kazi hii ingalifanywa na mtu mmoJa ... ... ... kumaliza.

  1. asingeweza 
  2. asingaliweza
  3. angaliweza
  4. asingeliweza 
  5. asingeweza
Chagua Jibu


5. Chakula hiki si kibayahakina viungo. Neno linalokosekana katika sentensi hii ni lipi?

  1. kama 
  2. ila
  3. wala
  4. alimurudia 
  5. kwa kuwa
Chagua Jibu


6. "Shule imefunguliwa” ukanushi wa sentensi hii ni ipi?

  1. Shule haitafunguliwa 
  2. Shule aijafunguliwa
  3. Shule haijafunguliwa 
  4. Shule haikufunguliwa
  5. Shule aikufunguliwa
Chagua Jibu


7. Kiranja mkuu wa shule . . . . . . . . mawazo ya wanafunzi wenzake katika kikao cha uongozi wa shule. Neno lipi linakamilisha sentensi hiyo?

  1. aliwakilisha
  2. ariwasilisha
  3. aliwasirisha
  4. aliwasilisha
  5. ariwasirisha
Chagua Jibu


8. Wingi wa neno "kuku” ni upi?

  1. Kuku
  2. Vikuku
  3. Makuku
  4. Makuku 
  5. Vijikuku
Chagua Jibu


9. Kayumba na Neema wanaosha vyombo. Neno "vyombo” limetumika kama aina gani ya neno?

  1. Kitenzi 
  2. Nomino 
  3. Kivumishi
  4. Kielezi 
  5. Kiwakilishi
Chagua Jibu


10. "Padri Joni anapenda sana kucheza mpira wa kikapu." Sentensi hii ipo katika nafasi ipi?

  1. Nafsi ya kwanza - umoja
  2. Nafsi ya tatu - wingi
  3. Nafsi ya pili - umoja 
  4. Nafsi ya tatu - umoja 
  5. Nafsi ya kwanza — wingi
Chagua Jibu


11. Sentensi ipi kati ya zifuatazo ipo katika kauli taarifa?

  1. Anakwenda mjini, Joti alisema
  2. Joti alisema, ninakwenda mjini
  3. Joti alisema, nitakwenda mjini
  4. Joti alitaka kujua kama atakwenda mjini
  5. Joti alisema kuwa amekwenda mjini
Chagua Jibu


12. Buibui, inzi, mbu, papasi na tandu kwa neno moja huwa wanaitwaje?

  1. Wanyama 
  2. Warukao 
  3. Wadudu 
  4. Ndege 
  5. Viroboto
Chagua Jibu


13. "Mzee Masanja amempa binti yake mume." Sentensi hii ina maana ipi?

  1. Mzee Masanja amemwolesha binti yake
  2. Mzee Masanja ameozesheana na binti yake
  3. Mzee Masanja amemwozesha binti yake
  4. Mzee Masanja amemwoza binti yake
  5. Mzee Masanja amemchukua mume na kumpa binti yake
Chagua Jibu


14. Katika sentensi zifuatazo ni ipi iliyo sahihi kimuundo?

  1. Nilikwenda kituo cha afya nilimkuta daktari hayupo
  2. Nilikwenda kituo cha afya lakini nilimkuta daftari hayupo
  3. Nilikwenda kituo cha afya lakini sikumkuta daktari
  4. Nilipokwenda kituo cha afya nikamkuta daktari hayupo
  5. Nilipokwenda nikamkuta hayupo
Chagua Jibu


15. Ni kipi kinyume cha neno "kaditama?"

  1. Kati 
  2. Mwanzo
  3. China
  4. Juu 
  5. Mwisho
Chagua Jibu


SEHEMU B

MSAMIATI

Katika swali la 16 - 25 andika herufiyajibu lililo sahihi latika karatasiyakoya kujibia.

16. Wakati akiendesha baiskeli yake, magurudumu yalimrushia tope kwa kuwa hayajakuwz na . . . . . . la kuzuia. Sentensi hii inakamilishwa na neno lipi?

  1. mbago 
  2. zuio
  3. bati
  4. jiwe 
  5. bano
Chagua Jibu


17. Mtu mwenye elimu ya mienendo ya nyota anaitwaje?

  1. Mnadhimu 
  2. Mnajimu
  3. Mnandi
  4. Mwananyota 
  5. Shauku
Chagua Jibu


18. "Mnyamavu" ni neno lenye maana sawa na kifungu kipi cha maneno kati ya vifuatavyo?

  1. Mwenye kupenda wanyama
  2. Mwenye kuchukia wanyama
  3. Mwenye tabia ya kuongea sana
  4. Mwenye tabia ya kukaa kimya
  5. Mwenye tabia ya ucheshi
Chagua Jibu


19. Kifungu cha maneno chenye maana sawa na neno "mwafaka" ni kipi?

  1. Mapatano baina ya watu
  2. Mafarakano baina ya watu
  3. Utengano baina ya watu
  4. Matatizo baina ya watu
  5. Ushirikiano baina ya watu
Chagua Jibu


20. Wanakijiji wa Songambele walifanya kazi zao kikoa. Neno "kikoa" lina maana gani?

  1. Kiukoo 
  2. Kwa ushirika
  3. Kwa ubinafsi 
  4. Kwa bidii 
  5. Kwa utengano
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256