STD VII KISWAHILI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2020

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA

MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI

01 KISWAHILI

Muda: Saa 1:30 Mwaka: 2020

Maelekezo

l. Karatasi hii ina sehemu A, B, C, D na E zenye maswali arobaini na tano (45).

2. Jibu maswali yote katika kila sehemu.

3. Soma maelekezo yote yaliyoko katika fomu maalum ya kujibia (OMR).

4. Jaza taarifa zote katika fomu ya OMR na katika ukurasa wenye swali Ia 41 hadi 45 kwenye karatasi ya maswali.

5. Andika Namba yako ya Mtihani kisha weka kivuli kwenye tarakimu za namba hiyo mahali panapohusika kwenye karatasi yako ya kujibia.

6. Weka kivuli kwenye herufi yajibu lililo sahihi kwa swali I - 40. Kwa mfano, kamajibu sahihi ni A weka kivuli kama ifuatavyo:

7. Ukigundua kuwa herufi uliyowekea kivuli si jibu sahihi futa kivuli hicho kwa umakini kwa kutumia kifutio safi kabla ya kuweka kivuli katika herufi mpya.

8. Tumia penseli ya HB tu katika kujibu swali Ia 1 — 40; na kalamu ya wino wa bluu au mweusi kwa swali Ia 41 hadi 45.

9. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi ndani ya chumba cha mtihani.

SEHEMU A (Alama 20)

SARUFI

Katika swali la 1 - 20, weka kivuli katika herufi ya jibu lililo sahihi katika fomu yako ya kujibia.

l . "Amevaa kichina mimi nimevaa kihindi." Maneno "Kichina na Kihindi" ni aina gani za maneno?

  1. Vielezi
  2. Vivumishi
  3. Viwakilishi
  4. Vihusishi
  5. Nomino.
Chagua Jibu


2. "Wewe ni mtoto mzuri sana." Neno lililotumika kama kiwakilishi ni lipi?

  1. mtoto
  2. ni
  3. mzuri
  4. sana
  5. wewe.
Chagua Jibu


3. "Walimu wanafundisha lakini wanafunzi hawajisomei." Neno "lakini" ni aina gani ya neno?

  1. Kivumishi
  2. Kiunganishi
  3. Kitenzi
  4. Kielezi
  5. Kihisishi.
Chagua Jibu


4. "Amenunua bidhaa kadhaa na kuzipeleka nyumbani."Neno 'kadhaa" ni aina gani ya neno?

  1. Kielezi
  2. Kitenzi
  3. Nomino
  4. Kiwakilishi
  5. Kivumishi.
Chagua Jibu


5. "Madaktari walifanya kila njia ili kunusuru maisha yake." Neno "ili" ni aina gani ya neno?

  1. kihisishi
  2. kihusishi
  3. kiunganishi
  4. kielezi
  5. kiwakilishi
Chagua Jibu


6. "Watoto wawili waliimba wimbo vizuri sana." Neno "wawili" ni aina gani ya neno?

  1. Kiunganishi
  2. Kiwakilishi
  3. Kivumishi
  4. Kielezi
  5. Kitenzi.
Chagua Jibu


7. Neno lipi halihusiani na maneno mengine kati ya haya yafuatayo?

  1. Wali
  2. Ugali
  3. Ndizi
  4. Viazi
  5. Mchicha.
Chagua Jibu


8. Kuku, bata, mwewe. kunguru na kanga kwa neno moja wanaitwaje?

  1. Wanyama
  2. Ndege
  3. Wadudu
  4. Wanyamapori
  5. Ndegepori.
Chagua Jibu


9. Neno lipi halilandani na mengine kati ya yafuatayo?

  1. Mchungwa
  2. Embe
  3. Ndizi
  4. Papai
  5. Pera.
Chagua Jibu


10. Mtu hodari asiyeogopa huitwaje?

  1. Jambazi
  2. Jangili
  3. Jasiri
  4. Jeuri
  5. Njemba.
Chagua Jibu


SEHEMU B (Alama 10)

LUGHA YA K?FASIHI

Katika swali la 21 - 30, weka kivuli katika herufi ya jibu lililo sahihi katika fomu yako ya kujibia.

21 . Kamilisha methali hii, "Udongo upate . . . . . . . . . . . ."

  1. ungali mfinyanzi
  2. ungali kichanga
  3. ungali maji
  4. ingali mapema
  5. ukiwa na mbolea
Chagua Jibu


22. . . . . . . . . . . . . . ila siku ya idi.” Kifingu kipi cha maneno kinakamilisha methali hii?

  1. Anafunga mchana
  2. Hatasali
  3. Hatafaidi pilau
  4. Mkaidi hafaidi
  5. Hapati zawadi
Chagua Jibu


23. 'Mia nawe hafi nawe ila mzaliwa nawe.” Methali hii inahusiana na ipi kati ya zifuatazo?

  1. Jembe halimtupi mtu
  2. Baada ya dhiki faraja
  3. Damu ni nzito kuliko maji
  4. Penye urembo ndipo penye ulimbo
  5. Kila mtoto na koja lake
Chagua Jibu


24. Hana adabu wala staha kwa watu.” Jibu la kitendawili hiki ni lipi?

  1. Kinyesi
  2. Kamasi
  3. Jasho
  4. Utelezi
  5. Pombe
Chagua Jibu


25. 'Mwavuli 'tva nyikani haukingi mvua." Jibu la kitendawili hiki ni lipi?

  1. Mgomba
  2. Mpapai
  3. Uyoga
  4. Mnyonyo
  5. Mfenesi
Chagua Jibu


26. "Akibeba watoto wake hawezi kuwashusha." Jibu la kitendawili hiki ni lipi?

  1. Mzaituni
  2. Mhindi
  3. Mchundwa
  4. Mwembe
  5. Mpera
Chagua Jibu


27. "Babu huanika sembe usiku,asubuhi huiondoa."Jibu la kitendawili hiki ni lipi?

  1. Mvua
  2. Giza
  3. Mwezi
  4. Umande
  5. Mawingu
Chagua Jibu


28. "Unga mkono." Maana ya nahau hii ni ipi?

  1. Kushikana mkono
  2. Ongozana
  3. Kubaliana
  4. Fuatana
  5. Tembeleana
Chagua Jibu


29. Ni nahau ipi kati ya zifuatazo inadhihirisha hali ya kumsema mtu kwa mafumbo ili asitambue?

  1. Kumpiga vijembe
  2. Kumpiga kinagaubaga
  3. Kumsema kimasomaso
  4. Kumsema kisiasa
  5. Kumsema kwa kumjuza
Chagua Jibu


30. 'Nikipata wasaa nitajitahidi kukutupia jicho."Usemi "kukutupia jicho" una maana gani?

  1. Kukusikiliza
  2. Kukuletea fedha
  3. Kukupa miwani
  4. Kukuona
  5. Kukupima macho.
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256