MTIHANI WA KUJIPIMA WA MADA

URAIA NA MAADILI A SITA

KUAMINIKA KATIKA JAMII

MADA YA KUMI NA NNE

 

Zoezi

  1. Lipi kati ya yafuatayo si wajibu wa mtoto?
  1. Kuwasaidia wazazi shughuli za nyumbani
  2. Kuwasaidia wadogo wake
  3. Kulipa karo ya shule
  4. Kufua nguo zake
Choose Answer


  1. Kufanya kazi kwa bidii kuna faida nyingi. Lipi kati ya yafuatayo si mojawapo ya faida hizo?
  1. Kuongeza kipato cha familia
  2. Kuchoka kutokana na kazi nyingi
  3. Kuheshimika katika jamii
  4. Kuburudika kimwili na kiakili
Choose Answer


  1. Lipi kati ya matendo yafuatayo huharibu uhusiano wa watu?
  1. Kuwa mkweli na mwaminifu
  2. Kuwaheshimu watu wanaokuzunguka
  3. Kutosaidia jirani wakati wa shida
  4. Kuwajali watu wengine
Choose Answer


  1. Lipi kati ya majukumu yafuatayo si jukumu la mwanafunzi awapo shuleni?
  1. Kupika chakula cha wanafunzi wenzake
  2. Kufanya usafi darasani
  3. Kuhudhuria paredi
  4. Kufanya bidii masomoni
Choose Answer


  1. Kipi kati ya vifuatavyo ni kitendo kinachoharibu uhusiano baina ya watu?
  1. Kutothamini wengine
  2. Kuwaonya wengine
  3. Kufanya kazi kwa bidii
  4. Kusema ukweli
Choose Answer


6.  Majukumu ya kiongozi wa wanafunzi katika shule ni pamoja na:

  1.  kusimamia maendeleo ya taaluma katika shule
  2.  kuandaa ripoti za maendeleo ya wanafunzi
  3.  kuwa kiungo kati ya wanafunzi na walimu
  4.  kusimamia nidhamu ya walimu
  5. kuadhibu wanafunzi wanaovunja sheria za shule 
Choose Answer


7. Chombo cha juu katika maamuzi kwenye serikali ya kijiji ni ..................

  1.  Serikali ya kijiji 
  2.  Kamati ya ulinzi na usalama
  3.  Mkutano mkuu wa kijiji 
  4.  Afisa Mtendaji wa kijiji
  5.  Kamati ya Maendeleo ya kijiji
Choose Answer


8. Matumizi ya ofisi ya umma kwa manufaa binafsi huitwa.................

  1.  takrima 
  2.  rushwa
  3. uzalendo
  4.  ubinafsi 
  5.  ujasiriamali
Choose Answer


9. Mojawapo ya njia ambazo wananchi wanaweza kushiriki katika ulinzi na usalama ni...............

  1.  kupiga wahalifu 
  2.  kufanya mazoezi ya viungo
  3.  kuwaua wahalifu 
  4.  kuwafichua wahalifu
  5.  kuwa rafiki na wahalifu
Choose Answer


10. Kuna aina mbili za uongozi katika Serikali za Mitaa ambao ni uongozi wa:

  1. kulipwa na kujitolea.
  2. kuchaguliwa na kuteuliwa.
  3. kidemokrasia na kidikteta.
  4. kuteuliwa na kujitolea.
  5. kuteuliwa na kulipwa.
Choose Answer


Andika KWELI kwa sentensi iliyo sahihi na SI KWELI kwa sentensi isiyo sahihi.

  1. Unaweza kubadili mwenendo mbaya kuwa mzuri utakapoweza kujitathmini............
  2. View Answer


  3. Ili kutoharibu uhusiano wa watu inakupasa kuwa na upendo...............
  4. View Answer


  5. Ili kupata mahitaji muhimu katika maisha si lazima kufanya kazi kwa bidii..............
  6. View Answer


  7. Majukumu ya nyumbani na ya shuleni hayatofautiani.................
  8. View Answer


  9. Tunaweza kumsaidia mtu mwenye tabia ya ugomvi kwa kumtenga..............
View Answer


Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256