MTIHANI WA KUJIPIMA WA MADA
 MAARIFA YA JAMII DARASA LA SABA
 UJASIRIAMALI
 Chagua jibu sahihi
 1.Aina kuu mbili za biashara ni:
  - biashara ya mkopo na ya malipo
  - biashara ya mkopo na kubadilishana
  - biashara ya mtaji na fedha
  - Biashara ya hisa na ya mitaji
  - biashara ya ndani na ya nje
  
Choose Answer    
2.Nini maana ya ujasiriamali?
  - Bishara yoyote yenye faida
  - Uwekezaji kwenye biashara
  - Biashara ndogondogo
  -  Sekta binafsi
  - Ujasiri wa kumiliki mali
  
Choose Answer    
3. Zipo aina tatu za mipango ya uchumi ambayo ni mipango ya ...
  - miaka kumi, kumi na tano na ishirini na tano
  - Taifa, Mkoa na Wilaya
  - kilimo, biashara na viwanda
  - muda mrefu, dharura na muda mfupi
  - muda mfupi, muda wa kati na muda mrefu
  
Choose Answer    
4. Ufugaji wa kisasa wa wanyama huzingatia nini? ..
  - Utamaduni wa jamii
  - Ubora wa wanyama na mazao yao.
  - Kuwepo kwa ardhi ya kutosha.
  - Mbuga za asili za kulishia mifugo.
  - Hali ya hewa.
  
Choose Answer    
5. Ni katika mfumo upi wa kiuchumi ambamo njia kuu za uzalishaji mali wanajamii wote?
  - Utumwa
  - Ukabaila
  - Ubepari
  - Ujima
  - Ujamaa
  
Choose Answer    
 6. Ipi kati ya fursa hizi za kibiashara haipatikani mijini?
  - Ufugaji
  - Kushona nguo
  - Usafirishaji
  - Kuuza vyakula
  
Choose Answer    
7. Faida ya ubunifu ni hizi isipokuwa;
  - Kuvutia wateja
  - Kukabiliana na ushindani
  - Kuiga kazi za wengine
  - Kuongeza faida
  
Choose Answer    
8. Ipi sio aina ya wajasiriamali?
  - Wajasiriamali wabunifu
  - Wajasiriamali wafanyabiashara
  - Wajasiriamali watumishi
  - Wajasiriamali jamii
  
Choose Answer    
9. Tabia hizi zinaweza kukwamisha biashara yako isipokuwa
  - Kujituma
  - Uvivu
  - Kuwa na visingizio
  - Kupoteza muda
  
Choose Answer    
10. Ipi sio tabia ya mjasiriamali?
  - Uthubutu
  - Uaminifu na uadilifu
  - Kukata tama
  - Ubunifu
  
Choose Answer    
11. Fursa ya ujasiriamali inayopatikana vijijini pamoja na
  - Ukulima
  - Ufugaji
  - Uchimbaji madini
  - Zote hizo
  
Choose Answer    
 Andika KWELI kwa sentensi ya kweli na SI KWELI kwa sentensi isiyo ya kweli katika nafasi uliyopewa.
  - Kufanya biashara haramu ni njia halali inayotumiwa na baadhi ya wajasiriamali ili kujiongeza kipato............
 View Answer 
- Wajasiriamali wanashauriwa kuepuka kujiingiza kwenye biashara haramu kama vile biashara ya kuuza vipodozi vyenye viambato vyenye sumu.............
 View Answer 
- Ukwepaji wa kodi kwa baadhi ya wajasiriamali hukosesha taifa mapato...........
 View Answer 
- Ubora wa bidhaa za wajasiriamali huthibitishwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)..........
 View Answer 
- Namna ya kudhibiti njia zisizohalali katika ujasiriamali ni kutoa elimu kwa wajasiriamali na wananchi kwa ujumla..............