MTIHANI WA KUJIPIMA WA MADA

SAYANSI DARASA LA SABA

ALAMA ZA USALAMA KATIKA MAZINGIRA

Sehemu A

  1. Makundi ya alama za usalama ni………..
  1. Alama za kuzuia, alama za onyo, alama za lazima na alama za dharura
  2. Alama za dharura, alama za binafsi na alama hatarishi
  3. Alama za amri, alama za kuzuia na alama za kukubali
  4. Alama za hospitali, alama za onyo, alama za barabarani na alama za angani
Choose Answer


  1. Alama za lazima au amri huoneshwa kwa rangi gani?
  1. Njano
  2. Nyekundu
  3. Bluu
  4. Kijani
Choose Answer


  1. Alama hii inawakilisha nini?

 

  1. Sumu
  2. Inashika moto
  3. Inamomonyoa na kuunguza
  4. Inadhuru
Choose Answer


  1. Mojawapo kati ya maneno yafuatayo, hayawekwi kwenye viuatilifu vya kuua wadudu.
  1. Inashika moto
  2. Sumu au hatari
  3. Maji yasiyo salama
  4. Inakereketa
Choose Answer


  1. Unapotumia vitu vinavyohatarisha macho, unapaswa kuchukua tahadhari gani?
  1. Kuvaa barakoa
  2. Kufunga kitambaa usoni
  3. Kuvaa kofia
  4. Kuvaa miwani
Choose Answer


Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256