MTIHANI WA KUJIPIMA WA MADA

SAYANSI DARASA LA SITA

HUDUMA YA KWANZA

Sehemu A

Chagua Jibu Sahihi

1. Hali ya mtu kuzimia hutokana na ukosefu wa damu katika .......

  1. Tumbo
  2. Figo
  3. Mapafu
  4. Moyo
  5. Ubongo
Choose Answer



2. Huduma ya kwanza anayopewa mtu aliyezimia ni:

  1.  kumpa hewa ya oksijeni
  2.  kumpa juisi ya nazi mbichi
  3.  kumlaza juu chini na kumbonyeza tumbo
  4.  kumpa maji yaliyochanganywa na glukosi
  5.  kumpa juisi ya malimao, sukari na chumvi
Choose Answer


3. Huduma ya kwanza ni nini?

  1. Msaada wa dharura apewao mgonjwa na daktari.
  2. Msaadawa awali apewao mgonjwa kabla ya kupelekwa hospitali.
  3. Msaada kwa ajili ya mtu aliyeungua moto. 
  4. Msaada kwa ajili ya mtu aliyeumwa na nyoka. 
  5. Msaada kwa ajili ya mtu aliyevunjika mfupa.
Choose Answer


4. Mojawapo ya huduma ya huduma muhimu ya kumpa mtu aliye ungua moto ni;-

  1. kummwagia maji
  2. kumfunika nguo
  3. kumwagia asidi
  4. kumfunika blanketi
  5. kumpaka asali
Choose Answer


5. Mojawapo ya athari za kupaka mafuta kwenye jeraha la moto ni:

  1. kuongeza joto kwenye jeraha
  2. kuongeza maumivu kwenye jeraha
  3. kuruhusu hewa kupita kwenye jeraha 
  4. kusababisha vijidudu kuingia kwenye jeraha 
  5. kuongeza malengelenge.
Choose Answer


6. Huduma ya kwanza hutolewa kwa lengo gani?

  1. Kushusha gharama za matibabu
  2. Kuonesha umahiri wa kitabibu
  3. Kuokoa maisha ya wagonjwa 
  4. Kurahisisha matibabu
  5. Kupunguza idadi ya madaktari.
Choose Answer



7. Huduma ipi ya kwanza kati ya zifuatazo hutolewa kwa mtu aliyekazwa na misuli?

  1. Kumfanyisha mazoezi ya viungo
  2. Kumpumzisha kitandani
  3. Kufunga misuli kwa bandeji
  4. Kumpa dawa ya kutuliza maumivu
  5.  Kuchua polepole misuli husika
Choose Answer


8. Kifaa kifuatacho siyo muhimu kuwemo katika sanduku Ia huduma ya kwanza

  1. Wembe 
  2. Pimajoto 
  3. Mkasi 
  4. Kijiko 
  5. Kibanio
Choose Answer


9. Ipi kati ya sentensi zifuatazo inatoa maana ya huduma ya kwanza?.............

  1. Msaada wa haraka anaopewa mtu kabla ya kwenda hospitali.
  2. Msaada wa haraka anaopewa mtu baada ya kufika hospitali.
  3. Msaada wa haraka unaotolewa kwa mtu na mtaalamu wa afya.
  4. Msaada unaotolewa kwa mtu aliyezirai.
  5. Msaada unaotolewa kwa mtu aliyeumwa na nyoka.
Choose Answer


10. Je nini utakachokifanya ikiwa utaona nguo alizovaa rafiki yako zinaungua kwa moto?..........

  1. Kumpaka mafuta
  2. Kumweka maji kwenye jeraha
  3. Kumfunika kwa blanketi au nguo nzito
  4. Kumpulizia hewa ya oksijeni
  5. Kumvua nguo zilizokwisha ungua
Choose Answer


Andika NDIYO kwa sentensi iliyo sahihi na HAPANA kwa sentensi isiyo sahihi.

  1. Unatakiwa kuikata au kuichanjaa sehemu iliyoumwa na nyoka na kufyonza sumu………
  2. View Answer


  3. Unatakiwa kugandamiza tumbo la mtu aliyezama kwenye maji akiwa amelala kifudifudi………..
  4. View Answer


  5. Usijaribu kurudisha  ndani mfupa uliovunjika wakati wa kutoa huduma ya kwanza…………..
  6. View Answer


  7. Tangawizi na limau husaidia kuondoa kichefuchefu kwa mtu anayetapika………….
  8. View Answer


  9. Msaidie mtu aliyezama kwenye maji kupumua kwa kupiliza pumzi kwa nguvu kwa kutumia mdomo kwa mdomo………..
View Answer


Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256