KISWAHILI DARASA LA 4
SURA YA PILI
VITENDAWILI, NAHAU NA METHALI
Katika sura hii utajifunza namna ya kutega na kutegua vitendawili. Pia, kueleza maana ya nahau. Kisha, utaweza kukamilisha methali, kuelezea maana zake na kufafanua ujumbe uliomo. Vilevile, utaweza kueleza umuhimu wa vitendawili, nahau na methali.
Kuna tofauti gani kati ya Kiswahili na methali? Eleza kama hizi ni methali au kitendawili
Ufahamu
Soma habari ifuatayo kisha jibu maswali.
Doto mshindi
Siku ya Jumamosi ni siku ya mapumziko. Mimi na wadogo zangu Ngwila na Aisha hatuendi shule. Tunafua nguo zetu za nyumbani na sare za shule. Pia tunawasaidia wazazi kazi za nyumbani.
Siku hiyo nilitembelewa na marafiki zangu Kulwa na Doto. Walipofika nyumbani kwetu walifurahia mazingira ya nyumba yetu.
Doto alisema, "Rafiki yangu Tumaini, nyumba yenu ni safi na inapendeza sana. Maua yamepandwa kwa mpangilio mzuri." Kulwa naye aliongeza, "Rangi mbalimbali zilizopakwa zinaifanya nyumba yenu ipendeze zaidi." Niliwaeleza kuwa siku za mapumziko tunawasaidia wazazi wetu kufanya usafi wa mazingira. Vilevile, tunamwagilia bustani ya maua. Doto naye alisema, "Kweli ninyi ni mfano bora wa kuigwa. Mazingira safi ni muhimu kwa afya zetu."
Siku hiyo baba alinunua matunda na mama alitupikia chakula kizuri. Baada ya chakula cha mchana tulikaa barazani na kutega vitendawili. Tulimkaribisha kaka iii aweze kusikiliza jinsi tunavyotega na kutegua vitendawili. Kaka alituambia yeye ataandika alama za kila mmoja wetu. Alitueleza kuwa atakayetega kitendawili na wengine wakashindwa kutegua, atakuwa amepata alama. Hivyo mshindi atakuwa ni yule aliyepata alama nyingi.
Mazungumzo yetu katika kutega vitendawili yalikuwa kama ifuatavyo:
Mimi: Kitendawili?
Wote: Tega.
Mimi: Ukoo wetu hauishiwi na safari.
Kulwa: Gari.
Mimi: Umekosa.
Aisha: Pikipiki.
Mimi: Umekosa. Nipeni mji.
Doto: Nenda Dodoma.
Mimi: Sawa naenda Dodoma nikirudi nitawaletea zabibu. Ukoo wetu hauishiwi na safari jibu lake ni siafu.
Kulwa: Sasa ni zamu yangu. Kitendawili?
Wote: Tega.
Kulwa: Ubwabwa wa mwana mtamu.
Aisha: Mahindi.
Kulwa Umekosa
Doto: Usingizi.
Kulwa: Umepata.
Tulishindana kutega vitendawili kwa saa moja. Mimi nilitegua kitendawili kimoja. Aisha alitegua vitendawili viwili na Doto aliweza kutegua vitendawili vitatu. Kaka alimtangaza Doto kuwa ndiye mshindi. Wote tulimpigia makofi ya kumsha' ngilia. Kaka alituambia, "Ninyi ni hodari wa kutega vitendawili." Baada ya kuona usiku umeingia, kaka aliwaambia Kulwa na Doto warudi nyumbani. Wote tulisimama na kuwasindikiza rafiki zetu.
Zoezi La Kwanza
Ufahamu.
A. Tegua vitendawili vifuatavyo.
B. Tegua vitendawili vifuatavyo:
6. Kamba yangu ndefu lakini haiwezi kufunga mzigo wa kuni.
C. Andika vitendawili vyenye majibu yafuatayo:
Mfano: Macho Popoo mbili zavuka mto.
Zoezi la Tatu
Lugha.
Andika KWELI au SI KWELI.
ZOEZILA NNE
Tumia nahau zifuatazo kukamilisha maelezo uliyopewa.
Kwa mfano:
Sanga ni mkulima wa mahindi. Mafuriko yalipotokea mazao yake yote yalizolewa na maji. Baada ya mwezi mmoja mvua ilikatika. Sanga hakutaka tena kurudia kupanda mahindi. Je, Sanga alifanya nini? Sanga alikata tamaa.
Maelezo:
A. Soma hadithi ifuatayo kisha andika methali zilizomo na maana zake.
Umoja ni nguvu
"Ama kweli kuishi kwingi, ni kuona mengi."Nilimsikia bibi
akiongea maneno hayo peke yake. Sikusita kumkaribia na kumuuliza, "Bibi unaongea na nani?" Bibi alijibu, "Nimekumbuka habari ya kijana aitwaye Besao. Ngoja nikusimulie mjukuu wangu."
Besao ni mtoto wa kwanza kuzaliwa katika familia yenye watoto wanne. Besao hakupenda kushirikiana na wadogo zake katika mambo mbalimbali. Alikuwa mbinafsi na alifanya kila kitu peke yake. Aliamini kuwa wingi si, hoja.Mama yake alimwambia kuwa, kidole kimoja, hakivunji chawa.
Siku moja Besao aliumia mguu. Ndugu zake walishirikiana kumuuguza hadi alipopona. Baada ya kupona mguu Besao aliona aibu sana. Aliwaomba radhi wazazi na wadogo zake.
Besao aliwaambia kwamba ameamini kuwa, umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu.Kuanzia hapo Besao alianza kushirikiana na wadogo zake.
B. Tumia methali zifuatazo kujaza nafasi zilizoachwa wazi katika maelezo uliyopewa 1 - 4.
Methali
Maelezo
C. Kamilisha methali zifuatazo.
D. Andika methali methali zitakazo tumika kuwaonya watu wenye tabia zifuatazo
ZOEZI LA SITA
MAZOEZI YA LUGHA.
A. Badili sentensi zifuatazo kuwa katika wakati ujao
B. Andika sentensi zifuatazo katika hali timilifu
C. Oanisha methali zinazofanana kutoka sehemu ya A na B
Sehemu A | Sehemu B |
|
|
D. Andika sentensi zifuatazo katika hali ya ukanushi
E. Tegua vitendawili vifuatavyo tumia viteguzi ulivyopewa.
F. Tumia viteuzi hivi kutegua vitendawili vifuatavyo
www.learninghubtz.co.tz