SURA YA KWANZA

MAZINGIRA

Msamiati

  • Hatari- hali ya kutokuwa katika usalama
  • Jongea- sogea karibu toka au nenda
  • Vitu- chochote kisichokuwa na sifa ya viumbe hai
  • Uchunguzi- namna ya kudadisi jambo lisilojulikana kwa kutumia njia mbalimbali

Mazingira ni jurata ya vitu vyote vinavyotuzunguka. Vitu hivyo ni kama vile udongo, mimeo, majengo, wanyama, hewa na maji. Tunachunguza mazingira kwa kutumia viungo mbatimbati vya mwili. Viungo hivyo ni macho, pua, masikio, ngozi na Mimi. Macho hutumika kuona na kutambua vitu. Tunaona vitu vyenye rangi mbatimbati kama vile maua na mavazi..

Pia, tunagundua eneo safi au chafu kwa kuona.

Pua ni kiungo kinachotumika kunusa. Unaweza kutambua mazingira yenye harufu nzuri au mbaya kwa kutumia pua.

Masikio hutumika kutambua na kutofautisha sauti za vitu mbalimbali. Mfano, sauti ya mngurumo wa gari, sauti ya ndege na sauti ya ngoma.

Ngozi hutumika kuhisi vitu mbalimbai katika mazingira. Unapokuwa karibu na kitu chrenye joto, ngozi ya mwiti huhisi hati ya joto. Ukiwa karibu na kitu cha baridi ngozi ya mwi[i kuhisi baridi. ukigusa kitu, n.gozi yahuhisi kuwa kitu hicho ni kigumu, kitaini au kinakwaruza.

Utimi hutumika kuonja vitu mbalimbali kama chakula, matunda na vinywaji. Hairuhusiwi kuonja vitu tusivyovifahamu wakati wa kufanya uchunguzi.Vitu vingine ni sumu.

Viungo mbalimbali

Vitu na viumbe hai

Tazama picha hizi, kisha jibe swab.


Kielelezo Baadhi ya viumbe hai na vituvinavyopatikana katika mazingira

Picha unazoziona zinaonesha ng'ombe, nyasi, mwembe, meza na mkate. Vilevile, zinaonesha chupa ya chai, kalamu, sahani na mpira wa miguu. Katika

picha hizo vitu ni meza, mkate, chupa ya chai na sahani. Vitu vingine ni kalamu na mpira wa miguu.

Vilevile, katika picha hizo viumbe hai ni ng’ombe, nyasi na mwembe

Kuchunguza tofauti kati ya panzi, mende na jiwe kwenye chupa

Mahitaji;

  1. Chupa tatu zenye mifuniko yenye matundu madogo
  2. Jiwe
  3. Panzi na mende walio hai

Hatua

  1. Weka mende, panzi na jiwe kila kimoja katika chupa yake
  2. Funika chupa hizo
  3. Chukua chupa zote ziwekejuu ya meza
  4. Angalia kwa makini tofauti unazoziona
  5. Andika unachokiona

Panzi akiwa ndani ya chupa ataonekana anaruka na mende atakuwa anatambaa. Kuruka kwa panzi. Na Kutambaa kwa mende ni kujongea. Kujongea huwasaidia viumbe hai kutafuta mahitaji muhimu kama chakula na sehemu salama. Matundu yaliyopo kwenye chupa yanawasaidia kupata, hewa. Viumbe hai wakikosa. Hewa hufa. Jiwe halioneshi kitendo chochote ndani ya chupa kwa kuwa halina uhai.

Viumbe hai hukua na kuongezeka kimo na uzito. Mfano, binadamu hukua kwa kupitia hatua mbalimbali za ukuaji. Hatua hizo ni kama vile, utoto, ujana, utu

uzima hadi uzee.

Kielelezo Hatua za ukuaji wa binadamu

Pia, mimea hukua kwa kuongezeka kimo.

Kielelezo : Hatua za ukuaji katika mimea.


Vilevile viumbe hai huzaliana. Kwa mfano, mimeo huzaliana kwa kutoa mbegu. Wanyama huzaliana kwa kuzaa watoto au kutaga mayai.

Tazama picha hii, kisha soma maetezo yanayofuata.

Kielelezo: Mbuzi akita majani

Kula ni mojawapo ya sifa za viumbe hai. ili viumbe hai viishi vinahitaji chakula Bila chakula. Bila chakula viumbe hai hufa.

Kwa hiyo, viumbe hai wana sifa za kujongea, kula, Kupumua, kukua na kuzaLiana. ViLeviLe, sifa nyingine za viumbe hai ni kuhisi na kutoa taka mwili.


Kuthamini vitu na viumbe hai

Viumbe hai huthaminiwa kwa kulindwa, kupewa chakula, maji na kuhifadhiwa katika mazingira salama. Hivyo, tunapaswa kutunza mazingira ili kuwezesha viumbe hai kuzaliana, kukua na kuishi.

Kutunza mazingira


Vitu na viumbe hai hatari

Ni muhimu kuchukua tahadhari unapofanya uchunguzi katika mazingira. Hii ni kwa sababu baadhi ya viumbe hai wanauma na wana sumu kali. Vilevile, baadhi ya vitu vinachoma, vinaunguza na hutoa harufu kali.

Kielezo: vitu na viumbe hai hatari

www.learninghubtz.co.tz

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256