MTIHANI WA KUJIPIMA WA MADA

MAARIFA YA JAMII  DARASA LA SABA

ATHARI ZA NJIA ZILIZOTUMIKA KUDAI UHURU AFRIKA

 

Chagua jibu sahihi

1.     Vita vya Maji Maji vilisababishwa na:

  1.  maji na dawa toka mto Rufiji     
  2.  tamaa na ushawishi wa waganga wa kienyeji
  3. unyonyaji wa Wajerumani  
  4.  ukatili wa Wamatumbi wa Songea 
  5.  majaribio ya silaha za jadi
Choose Answer


2.     Tanganyika ilipata Uhuru wake kwa njia ya:

  1.  matumizi ya bunduki  
  2.  vita vya msituni
  3.  mikataba ya kilaghai 
  4.  kikatiba 
  5.  matumizi ya Veto
Choose Answer



 3.Utawala waWaingereza nchini Tanganyika uliisha mnamo .....

  1. karne ya 15 
  2. karne ya 19 
  3. karne ya 20 
  4. karne ya 18 
  5. karne y 17
Choose Answer



 4. Mataifa ya Ulaya yaliyokuwa yakipigania Mto Nile yalikuwa:

  1.  Ufaransa na Ubelgiji
  2.  Uingereza na Ujerumani
  3.  Ufaransa na Ureno
  4.  Uingereza na Ufaransa 
  5.  Ubelgiji na Ureno
Choose Answer



 5. Mapambano ya kudai Uhuru katika bara la Afrika yalianza baada ya:

  1.  Kuundwa kwa Umoja wa Mataifa
  2.  Kusambaratika kwa Umoja wa Kisovieti
  3.  Vita Kuü ya Pili ya Dunia
  4.  Kupigwa marufuku biashara ya watumwa
  5.  Kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi
Choose Answer


6. Mojawapo ya athari ya utawala wa Waingereza katika visiwa vya Unguja ilikuwa ....

  1.  kukomesha biashara ya utumwa. 
  2. kuanzishwa kwa dini ya kikristu.
  3.  kuondoa umaskini.
  4.  kuanzisha kilimo cha karafuu. 
  5. kuanzisha vyama vya siasa.
Choose Answer


7. Makoloni ya Ujerumani katika Afrika yalikuwa ..

  1.  Naijeria, Namibia na Togo.
  2.  Gambia, Togo na Namibia. 
  3. Kameruni, Togo na Namibia. 
  4. Namibia, Tanganyika na Naijeria.
  5. Kameruni, Tanganyika na Senegal.
Choose Answer


 8.  Moja ya mbinu iliyotumika kudhoofisha teknolojia ya Waafrika wakati wa ukolono ni 

  1.  kufundisha masomo ya sayansi.
  2.  kuanzisha viwanda vya kisasa katika Afrika.
  3.  kubinafsisha viwanda vya Afrika.
  4.  kuleta bidhaa za viwandani kutoka ulaya. 
  5.  kufundisha Waafrika teknolojia ya Ulaya.
Choose Answer



 9.  Mkutano wa Berlin wa mwaka 1884-1885 uliitishwa na ..

  1. Carl Peters 
  2. Johann Krapf 
  3. Henry Stanley 
  4. David Livingstone
  5. Otto Von Bismarck.
Choose Answer


10. Mwanzilishi wa mfumo wa utawala wa mlango wa nyuma katika Afrika alikuwa ...

  1. Horace Byatt
  2. Friedrick Lugard
  3. Richard Turnbull
  4. Donald Cameroon
  5. Edward Twinning
Choose Answer


11.Ni Taifa lipi la kibepari liliitawala Tanganyika kuanzia mwaka 1891 hadi 1918?

  1.  Ujerumani 
  2.  Uingereza
  3.  China 
  4.  Ureno 
  5.  Ufaransa
Choose Answer


12. Kwa nini Berlin ni miongoni mwa miji maarufu katika historia?

  1. Ni Makao Makuu wa Umoja wa Mataifa
  2. Ni Makao Makuu wa Jumuiya ya Madola
  3. Ni mji uliokuwa kitovu cha biashara ya utumwa
  4. Ni mji wa Ufaransa ambao uliendesha utawala wa kulisha kasumba
  5. Ni mji ambao mgawanyo wa Bara la Afrika ulifanyika
Choose Answer


13.Mataifa makubwa ya kibepari yaliyogombania Bara la Afrika yalikuwa

  1. Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Ubelgiji, Italia na Ureno
  2. Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Uchina, Uhispania na Marekani
  3. Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Japani, Uhispania na Ubelgiji
  4. Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Urusi, Uchina na Japani
  5. Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Ubelgiji, Italia na Uchina
Choose Answer


Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256