KISWAHILI
SURA YA PILI
SHAIRI
Soma na ghani shairi lifuatalo kisha jibu maswali.
1. Elimu kwa wanadamu, ndio silaha imara,
Imekuwepo dawamu, hata kwa wale sonara,
Tajua wake utamu, ukipitishwa kwa sura,
Usilikose darasa, kwa kufuata mkumbo.
2. Nakupatia nudhumu, taona nayo tijara,
Ujifunze na elimu, ya kuucheza mpira,
Uione yako timu, kisha kuanza ziara,
Usilikose darasa, kwa kufuata mkumbo.
3. Na ving’ora vya kudumu, adui kuteka nyara,
Kwa yote yalo magumu, ni shime kuyazingira,
Kukazania elimu, kuuzika ufukara,
Usilikose darasa, kwa kufuata mkumbo.
4. Kusoma kunawakimu, vijana kuwa imara,
Kupambana na magumu, kwenye uwanja wa dura,
Watu kushika hatamu, huwa na nyingi fikira,
Usilikose darasa, kwa kufuata mkumbo.
5. Rafiki yangu Adamu, kwepa ya ujinga nira,
Usijekosa fahamu, kupata ari na ghera,
Mkumbo ni kama sumu, atakukosesha dira,
Usilikose darasa, kwa kufuata mkumbo.
6. Liyotukuka elimu, hufunza na biashara,
Yafaa kuwa timamu, kujipatia ajira,
Maisha hana karimu, ukikosa ubora,
Usilikose darasa, kwa kufuata mkumbo.
7. Sheria ni msumeno, hukosa huku na huku,
Elimu nayo ni meno, pia ni kama sumaku,
Yaweza leta unono, mithili ngoma chiriku,
Usilikose darasa, kwa kufuata mkumbo.
8. Aliye moyo mgumu, hatimi katia fora,
Kaitunga na hukumu, ya kuhimiza fikira,
Kaupata ufahamu, na kung’amua taswira,
Usilikose darasa, kwa kufuata mkumbo.
9. Ukiwepo darasani, mwalimu msikilize,
Kisichotiwa mizani, angalia usimeze,
Kilopita kipimoni, ndicho ukitekeleze,
Usilikose darasa, kwa kufuata mkumbo.
10. Mazoezi darasani, yatakufanya uweze,
La kufanya akilini, kuchagua ipendeze,
Ujuzio ubaini, jamii isipumbaze,
Usilikose darasa, kwa kufuata mkumbo.
11. Utakuwa hatiani, masomo kuyapuuza,
Kuishi kama kunguni, hakika inaumiza,
Bora uishi porini, na majini kama pweza,
Usilikose darasa, kwa kufuata mkumbo.
12. Kwa walimu na wazazi, nidhamu uidumishe,
Na mambo yalo azizi, pekee jishughulishe,
Tabia ya uchokozi, kamwe usijifundishe,
Usilikose darasa, kwa kufuata mkumbo.
13. Tabia mbaya ya wizi, elimu iikomeshe,
Madhara ya udokozi, jamii uifundishe,
Mwenendo kama wa mbuzi, daima jiepushe,
Usilikose darasa, kwa kufuata mkumbo.
14. Fanikiwa hatimaye, ni mfano maishani,
Tegemea cha nduguye, hufa hali masikini,
Mwanafunzi asomaye, apaswa awe kifani,
Usilikose darasa, kwa kufuata mkumbo.
15. Kijana nakuusia, usiachie na hisa,
Masomo kung’ang’ania, nakupatia hamasa,
Ndani ya historia, jinalo lipate nasa,
Usilikose darasa, kwa kufuata mkumbo.
16. Ya viwandani elimu, lazima uzingatie,
Wanafunzi wahitimu, ujuzi washikirie,
Wa viwanda ufahamu, hakika wakumbatie,
Usilikose darasa, kwa kufuata mkumbo.
17. Naweka chini kalamu, tamati nimefikia,
Labaki lako jukumu, nasaha, kucharukia,
Usiache ufahamu, sukari kukimbilia,
Usilikose darasa, kwa kufuata mkumbo.
ZOEZI LA 1: UFAHAMU.
ZOEZI LA PILI. MSAMIATI:
Tunga sentensi kwa kutumia misamiati ifuatayo:
ZOEZI LA TATU. METHALI:
Kamilisha methali zifuatazi:
ZOEZI LA NNE. MAZOEZI YA LUGHA:
A: Pigia msitari neno lenye maana tofauti na mengine: -
B: Chagua jibu sahihi katika maswali haya: -
(i) Mtu anayetunga mashairi anaitwa?
(ii) Shairi huweza kuimbwa au?
(iii) Kituo ni mstari wa _____ unaojirudiarudia katika kila ubeti wa shairi.
(iv) Katika shairi la kimapokeo _______ vya kati na vya mwisho hufanana.
(v) Idadi ya silabi katika mshororo huitwa?
(vi) Kila ubeti wa shairi lazima ubebe angalau wazo _____ muhimu.
(vii) Ubeti wa shairi wenye mistari minne huitwa?
(viii) Mistari katika ubeti wa shairi inaweza pia kuitwa?
(ix) Ni nini maana ya kughani shairi?
(x) Utungo wa kifasihi unaotumia lugha ya mkato kuwasilisha ujumbe kwa hadhira huitwa?
C: Eleza maana ya taswira zilizotumika katika shairi ulilolisoma.
D: Kanusha sentensi zifuatazo:
E: Tumia maneno uliyopewa kwa kula sentensi kujaza nafasi zilizoachwa wazi.
www.learninghubtz.co.tz