STD VII URAIA_MAADILI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2022

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI

06 URAIA NA MAADILI

Muda: Saa 1:30 Mwaka: 2022

Maelekezo

1. Karatasi hii ina sehemu A na B zenye jumla ya maswali arobaini na tano (45).

2. Jibu maswali yote.

3. Soma maelekezo yote yaliyoko katika fomu maalumu ya kujibia (OMR).

4. Jaza taarifa zote katika fomu ya OMR.

5. Weka kivuli katika kila tarakimu ya Namba yako ya Mtihani kwenye nafasi husika katika fomu ya OMR.

6. Weka kivuli katika herufi ya jibu sahihi kwa swali la 1 hadi 40 katika fomu yako ya kujibia uliyopewa. Kwa mfano, kama jibu sahihi ni A weka kivuli kama ifuatavyo:

7. Ukigundua kuwa herufi uliyoweka kivuli si jibu sahihi, futa kivuli hicho kwa umakini kwa kutumia kifutio safi kabla ya kuweka kivuli katika herufi mpya.

8. Tumia penseli ya HB to katika kujibu swali la 1 hadi 40, na kalamu ya wino wa bluu au mweusi kujibu swali la 41 hadi 45.

9. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi ndani ya chumba cha mtihani.

SEHEMU A (Mama 40)

Katika swali la 1- 40, chagua jibu sahihi kisha weka kivuli kwenye herufi ya jibu lililo sahihi katika fomu maalum (OMR) ya kujibia uliyopewa.

1. Misaada inayotolewa kwa wahitaji ni ya aina mbalimbali kulingana na uhitaji wa watu. Ni kundi lipi sio la wahitaji katika jamii?

  1. Watoto yatima
  2. Wanafunzi wa elimu ya juu
  3. Watu wenye ulemavu
  4. Wanaoishi katika mazingira hatarishi
  5. Waathirika wa majanga
Chagua Jibu


2. Ofisa mtendaji wa kata hupatikanaje?

  1. Huchaguliwa na madiwani 
  2. B Huchaguliwa na wananchi
  3. C Huteuliwa na Halmashauri 
  4. D Huajiriwa na serikali
  5. Huchaguliwa na wenyeviti wa mitaa
Chagua Jibu


3. Ni kipi kati ya vifuatavyo hakiwezi kuitambulisha shule?

  1. Madarasa ya shule
  2. Mipaka ya shule
  3. Kaulimbiu ya shule
  4. Nembo ya shule
  5. Wimbo wa shule
Chagua Jibu


4. Mwanafunzi mwenye tabia nzuri ni lazima awe mwenye kujipenda. Nini maana ya kujipenda?

  1. Kujisifia mara tote 
  2. Kuwakubali wengine
  3. Kustahimili na kujikubali 
  4. Kujitegemea katika masomo
  5. Kujithamini na kujikubali
Chagua Jibu


5. Ni kitendo gani kati ya hivi vifuatavyo kinaweza kutumika katika kutokomeza ukandamizaji wa kijinsia katika jamii?

  1. Kutoa elimu kwa wote
  2. Kutoa elimu kwa wanaume
  3. Kutoa elimu kwa watu wazima
  4. Kutoa elimu kwa watoto
  5. Kutoa elimu kwa vijana
Chagua Jibu


6. Jambo lipi sio huduma inayoweza kutolewa kwa watu wenye ulemavu?

  1. Ushauri
  2. Uadilifu
  3. Makazi
  4. Msaada wa kiafya
  5. Msaada wa kisheria
Chagua Jibu


7. Ni madhara gani hutokea kutokana na ukandamizwaji wa wanawake katika jamii? 

  1. Kuongezeka kwa vifo katika jamii
  2. Kujengeka kwa matabaka katika jamii
  3. Kuongezeka kwa ufahamu wa haki za binadamu
  4. Kuongezeka kwa ndoa halali katika jamii
  5. Kuongezeka kwa asasi za kiraia
Chagua Jibu


8. Kila raia wa Tanzania ana wajibu wa kulinda amani ya nchi. Ni kwa vipi utatimiza wajibu huu?

  1. Kwa kutii sheria za nchi
  2. Kwa kutii maelekezo ya wataalamu
  3. Kwa kutoa taarifa kwa wafadhili
  4. Kwa kutoa elimu kwa wazee
  5. Kwa kutenda haki kwa watu wachache
Chagua Jibu


9. Katika jamii iliyostaarabika watu hujiheshimu na hujikinga na mambo yanayowaletea madhara. Je, kitendo hicho huitwaje?

  1. Kujijali 
  2. Kuwajali wengine 
  3. Kujipenda
  4. Kuwapenda wengine 
  5. Kujiamini
Chagua Jibu


10. Mahusiano mabaya baina ya wanajamii huleta athari gani?

  1. Vurugu na upendo 
  2. Chuki na upendo 
  3. Umaskini na ujinga
  4. Migogoro na mapigano 
  5. Umbea na umaskini
Chagua Jibu


11. Ni njia ipi bora zaidi ya kufikisha taarifa au maoni kwa uongozi wa shule kuhusu vitendo visivyofaa shuleni?

  1. Kutumia sanduku la maoni 
  2. Kutumia mkutano wa wazazi
  3. Kutumia wazazi ili kutoa malalamiko 
  4. Kutumia ubao wa matangazo
  5. Kutumia Sanduku la Posta
Chagua Jibu


12. Mwalimu mkuu wa Shule ya Msingi Mapinduzi ameanzisha kitengo cha ushauri nasaha katika shule yake. Kitengo hicho kina umuhimu gani?

  1. Kutoa mwongozo wa kutatua changamoto
  2. Kueleza mipango ya shule kwa undani
  3. Kudhibiti nidhamu za wanafunzi
  4. Kuandaa mipango ya usafi shuleni
  5. Kuandaa orodha ya wanafunzi wahitaji
Chagua Jibu


13. Ni kitendo gani hakihusiki katika kuchafua vyanzo vya maji?

  1. Kuoga mtoni 
  2. Kufua nguo mtoni
  3. Kukojoa pembezoni mwa mto 
  4. Kulima kandokando ya mto
  5. Kutumia njia salama za uvuvi
Chagua Jibu


14. Kuna umuhimu gani wa elimu ya afya ya uzazi kwa vijana? 

  1. Huwasaidia kuhimili mihemko ya milli yao
  2. Huwasaidia kujiepusha na magonjwa ya mlipuko 
  3. Huwasaidia kuhimili ndoa za ukubwani
  4. Huwasaidia kujenga ari ya kuwapenda wengine
  5. Huwasaidia kufanya maamuzi kwa wachumba watarajiwa
Chagua Jibu


15. Riziki alielezwa umuhimu wa kushirikiana na wengine katika kutekeleza majukumu yake ya nyumbani na shuleni. Ni mambo yapi kati ya yafuatayo ni majukumu ya nyumbani?

  1. Kufagia, kucheza na kumwagilia bustani
  2. Kumwagilia bustani, kudeki na kuwa kiongozi
  3. Kufagia, kudeki na kumwagilia bustani
  4. Kupiga kura, kufagia na kudeki
  5. Kudeki, kusafisha zahanati ya na kufagia
Chagua Jibu


16. Barabara, majengo ya shule na zahanati ni miundombinu ya jamii katika kijiji. Nani ana jukumu la kuilinda?

  1. Kamati ya maendeleo ya kijiji 
  2. Afisa maendeleo wa kijiji
  3. Wanakijiji wote 
  4. Jeshi la polisi
  5. Walimu na wazazi
Chagua Jibu


17. Rasimali za taifa ni tunu zinazotakiwa kulindwa na kuhifadhiwa. Ni kundi lipi Tina wajibu wa kulinda na kuhifadhi rasilimali za Taifa?

  1. Maafisa wa polisi 
  2. Maafisa wa jeshi 
  3. Wananchi wote
  4. Serikali ya kijijt 
  5. Viongozi wa serikali
Chagua Jibu


18. Ni mbinu ipi utaitumia kuwafanya wanafunzi wenzako wajitolee kufanya kazi za shuleni na nyumbani?

  1. Kuwafundisha namna ya kufanya kazi 
  2. Kuwaadabisha iii wafanye kazi
  3. Kuwahamasisha kufanya kazi 
  4. Kuwaonya ili wafanye kazi
  5. Kuwaombea kwa Mungu
Chagua Jibu


19. Mwongozo unaohusu mbinu za kupanga mipango ya maendeleo ya shule hutumiwa na nani?

  1. Mwalimu mkuu 
  2. Mwalimu mkuu msaidizi
  3. Uongozi wa shule 
  4. Kamati ya shule
  5. Serikali ya kijui
Chagua Jibu


20. Ni njia ipi haiwezi kuchochea maendeleo ya sekta mbalimbali?

  1. Usimamizi wa biashara 
  2. Uchambuzi wa sera za uchumi
  3. Usimamizi mzuri wa fedha 
  4. Uimarishwaji wa mazao ya chakula
  5. Kuimarisha stadi za viwandani
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256