STD VII SAYANSI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2017

SAYANSI 2017 

Chagua jibu sahihi kisha andika herufi yake kwenye karatasi ya kujibia.

1. Ipi kati ya tabia zifuatazo humwezesha ndege kuruka hewani?

  1. Mifupa milaini iliyo na manyoya.
  2. Miili iliyochongoka na mifupa iliyo wazi ndani.
  3. Mfupa iliyoungana.
  4. Uwepo wa mifupa mingi.
  5. Mifupa imara ya mabawa iliyo imara.
Chagua Jibu


2. Makundi makuu ya viumbe hai ni:

  1.  Mimea na ndege 
  2.  Mimea na mijusi
  3.  Wanyama na majani 
  4.  Mimea na wanyama
  5.  Wanyama na bakteria
Chagua Jibu


3. Ipi kati ya aina zifuatazo za mbegu hujisambaza zenyewe?.................

  1.  Nazi na pamba 
  2. Kunde na mbaazi
  3.  Kunde na papal 
  4.  Embe na pera
  5.  Chungwa na mbaazi
Chagua Jibu


4. Chunguza Kielelezo Namba 1, kisha chagua jibu lenye mpangilio sahihi wa zilizoonyeshwa kwa alama A - D.

Kielelezo Na. 1

  1. Nyuzi, uboho njano, uboho nyekundu, gegedu.
  2. Uboho nyekundu, gegedu, uboho njano, kano.
  3. Gegedu, kano, uboho njano, uboho nyekundu.
  4. Kano, njano, gegedu, uboho njano, uboho nyekur.: _
  5. Uboho njano, gegedu, kano, uboho nyekundu.
Chagua Jibu


5. Chunguza Kielelezo Namba 2 kisha jibu swali linalofuata

Kielelezo Na. 2

Kifaa katika Kielelezo Namba 2 hutumia tabia ipi ya mwanga?..............

  1.  Kuakisiwa 
  2.  Mpitisho 
  3.  Mwachano
  4.  Mgeuzo 
  5.  Mtawanyiko
Chagua Jibu


6. Magonjwa yapi kati ya yafuatayo huzuiliwa kwa chanjo?................

  1.  Surua na kifaduro 
  2.  Kichocho na malaria
  3.  Kuhara na mkamba 
  4.  Ukimwi na kisukari
  5.  Kifua kikuu na tetekuwanga
Chagua Jibu


7. Kitu gani muhimu mwanamke mjamzito anapaswa kuzingatia?...............

  1. Kula chakula kingi cha wanga anapokaribia muda wa kujifungua
  2. Kufanya kazi ngumu ili awe mkakamavu.
  3. Kuhudhuria kliniki na kula mlo kamili.
  4. Kulala mara kwa mara.
  5. Kutumia sabuni zenye manukato wakati wote.
Chagua Jibu


8. Ugonjwa unaotokana na tatizo la upumuaji ni 

  1.  pumu 
  2.  malaria kali 
  3.  kuzimia
  4.  kifafa 
  5.  kisukari
Chagua Jibu


9. Kitu gani kitatokea endapo mfumo wa fahamu utasimama kufanya kazi?.............

  1. Mtu ataanza kutetemeka.
  2. Mtu ataanza kuhisi udhaifu.
  3. Mtu ataanza kuhisi maumivu makali mwilini.
  4. Kukosekana kwa mawasiliano ndani ya mwili.
  5. Mtu ataanza kupungua uzito.
Chagua Jibu


10. Mojawapo ya dalili za unyafuzi ni.....................

  1. uso kufanana na wa mzee
  2. macho meupe na mafua 
  3. tezi ya shingo kuvimba
  4. kuhisi baridi na kutapika 
  5. tumbo kubwa na kuvimba miguu
Chagua Jibu


11. Njia za uzazi wa mpango ambazo ni salama kwa afya ya mama ni.............

  1. kitanzi na sindano 
  2. njia ya asili
  3. sindano na vidonge 
  4. vidonge na kondomu
  5.  kondomu na sindano
Chagua Jibu


12. Njia bora ya kuepuka utapiamlo ni ..............

  1. kutumia dawa za kinga mara kwa mara.
  2. kuelimisha jamii juu ya matumizi ya mlo kamili.
  3. kula mboga za majani kwa wingi.
  4. kutumia madawa ya kuongeza virutubisho mwilini.
  5. kuongeza idadi ya milo kwa siku.
Chagua Jibu


13. Mtu aliyepigwa na shoti ya umeme anaweza kusaidiwa kwa kutumia ..................

  1.  miguu 
  2.  kipande cha chuma 
  3.  ubao mkavu
  4. mikono 
  5. ubao mbichi
Chagua Jibu


14. Vipande viwili vya ubao safi vilivyofungwa kwenye sehemu mfupa ulipovunjika husaidia

  1. kuzuia kutokwa damu
  2. kukipa joto kidonda. 
  3. kuimarisha sehemu iliyovunjika.
  4. kutibu sehemu iliyovunjika. 
  5. kuunganisha sehemu iliyovunjika
Chagua Jibu


15. Gesi inayotumika kuzima moto ni ................

  1.  haidrogeni 
  2.  kabondayoksaidi 
  3.  naitrojen
  4.  kaboni 
  5.  oksijeni
Chagua Jibu


16. HIV haienezwi kwa ......

  1.  kujamiiana 
  2.  kuchangia sindano 
  3.  kuumwa na mbu
  4.  kuchangia nyembe 
  5.  kuwekewa damu
Chagua Jibu


17. Uhusiano kati ya magonjwa yanayoambukizwa kwa kujamiiana na UKIMWI ni kwamhz

  1. Ni rahisi kupata maambukizi ya UKIMWI kama umeambukizwa magonjwa yato-,na kujamiiana.
  2. Magonjwa yanayoenezwa kwa kujamiiana ni sawa na UKIMWI.
  3. Dawa za kutibu magonjwa yanayoenezwa kwa kujamiiana zinaweza kutumik,aUKIMWI.
  4. Magonjwa yanayoambukizwa kwa kujamiiana na UKIMWI yanaenezwa -- kujamiiana pekee.
  5. Majongwa yanayoambukizwa kwa kujamiiana na UKIMWI yanatibika.
Chagua Jibu


18. Ipi kati ya sentensi zifuatazo ina maana sahihi ya UKIMWI?...............

  1.  Kupoteza kinga ya mwili,
  2.  Kinga kubwa ya mwili.
  3.  Kukosekana kwa kinga mwilini 
  4.  Upungufu wa kinga mwilini.
  5.  Uwezo wa kinga ya mwili.
Chagua Jibu


19. Mbinu mojawapo ya kupunguza maambukizi ya virusi vya UKIMWI ni...............

  1. kutenga eneo la watu wenye virus! vya UKIMWI.
  2. kuepuka kushirikiana vifaa vya chakula na watu wenye virusi vya UKIMWI.
  3. kula chakula bora na kunywa mail safi.
  4. kubadili tabia na kuepuka ngono zembe.
  5. kufanya mazoezi ya mwili.
Chagua Jibu


20. Vitu vilivyorushwa angani hurudi chini.............

  1.  kwa sababu ya uzito 
  2.  kwa sababu ya nguvu ya msuguano
  3.  kwa sababu ya nguvu ya hewa 
  4.  kwa sababu ya nguvu ya sayari
  5.  kwa sababu ya nguvu ya uvutano
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256