STD VII SAYANSI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2016

201 6 - SAYANSI

SEHEMU A

Chaguajibu sahihi kisha andika herufiyake kwenye karatariya kujibia.

1. Ili mbegu ichipue inahitaji: 

  1. Maji, udongo na hewa
  2. Mvua, hewa na udongo
  3. Unyevu, udongo na jotoridi
  4. Maji, hewa na jotoridi
  5. Maji, mwanga na upepo
Chagua Jibu


2. Wadudu wanapohama toka ua moja kwenda lingine wanfanya hivyo ili:

  1. kuzalisha mimea  
  2. kuepuka maadui
  3. kutafuta nekta 
  4. kutafuta harufu 
  5. kusambaza mbegu
Chagua Jibu


3. Hali ya mtu kuzimia hutokana na ukosefu wa damu katika .......

  1. Tumbo
  2. Figo
  3. Mapafu
  4. Moyo
  5. Ubongo
Chagua Jibu


4.  Aina kuu mbili za mashine ni:

  1. ngumu na laini
  2.  rahisi na tata
  3. za kumenya na kutwanga 
  4. puli na roda
  5. roda na katapila
Chagua Jibu


5. Mojawapo ya njia za kuondoa takamwili katika mwili ni:

  1.  kutema mate 
  2.  kukojoa
  3. kuoga 
  4. kunawa mikono 
  5. kutoa machozi
Chagua Jibu


6. Mbegu ya kike ambayo haijarutubishwa huitwa:

  1.  kondo 
  2.  yai
  3. uterasi 
  4. ovari    
  5. mrija wa falopio
Chagua Jibu


7.  Angalia kielelezo namba 1 ambapo jotoridi lioneshwa kwa nyuzi za sentigredi kisha jibu maswali yanayofuata.

Mbegu itakayoota ni ya chombo kipi?

  1.  Chombo A    
  2.  Chombo B
  3.  Chombo C    
  4.  Chombo D  
  5.  Chombo A na D
Chagua Jibu


8. Sehemu zinazounda mfumo wa upumuaji katika mwanadamu ni:

  1.  pua, mdomo na tumbo
  2. mapafu, pua na ini
  3. pua, mapafu na masikio 
  4. koromeo, mapafu na kongosho
  5. mapafu, pua na mdomo
Chagua Jibu


9.  Mdudu yupi kati ya wafuatao huleta hasara kwa mkulima akiwa katika hatua ya pili ya ukuaji?

  1. Inzi                                                         
  2. Kipepeo
  3. Panzi                                                    
  4. Mbungo
  5. Mbu
Chagua Jibu


10. Usafirishaji wa chakula mwilini hufanywa na: 

  1. moyo     
  2. damu
  3. misuli                                     
  4. mapafu
  5. maji
Chagua Jibu


11. Tazama kwa makini kielelezo namba 2 kisha jibu maswali yanayofuata:

Alama Y inawakilisha sehemu iitwayo:

  1.  petali
  2.  filamenti
  3.  chavulio
  4.  pistili
  5.  ovari
Chagua Jibu


12.  Mbegu za mimea uhifadhi chakula katika:

  1.  mizizi 
  2. majani      
  3. shina
  4. kotiledoni 
  5. tunda
Chagua Jibu


13. Lipi kati ya magonjwa yafuatayo huambukizwa kwa njia ya kujamiiana?

  1.  Polio  
  2.  Kipindupindu         
  3.  Pepopunda
  4.  Kaswende                            
  5.  Tetekuwanga
Chagua Jibu


14. Nini kitatokea iwapo idadi ya wanyama wanaokula nyama katika eneo ni kubwa kulikc idadi ya wanaokula majani?

  1. Majani yatapungua
  2. Majani yatabakia kama yalivyokuwa awali
  3. Majani yatanyauka
  4. Majani yataongezeka
  5. Majani yataliwa
Chagua Jibu


15. Lipi kati ya mafungu yafuatayo ya vyakula hulinda mwili?

  1.  Samaki na maziwa          
  2.  Ugali na ndizi
  3.  Maharagwe na karanga 
  4.  Mayai na kabichi 
  5.  Matunda na mboga za majani
Chagua Jibu


16. Umuhimu wa asidi ya haidrokloric katika tumbo ni:

  1.  kubadili hali ya besi katika tumbo
  2.  kulainisha mafuta tumboni
  3.  kuongeza uchachu tumboni
  4.  kumengenya vyakula vya sukari tumboni 
  5.  kuua wadudu wanaoingia tumboni na chakula.
Chagua Jibu


17. Nini tofauti kati ya malaria na homa ya matumbo?

  1.  Malaria hushambulia mishipa ya damu, homa ya matumbo hushambulia neva za fahamu.
  2.  Malaria husababishwa na mbu, homa ya matumbo husababishwa na inzi.
  3.  Malaria hutibiwa kwa siku nne, homa ya matumbo hutibiwa kwa siku saba.
  4.  Malaria husababishwa na plasmodiam, homa ya matumbo husababishwa na bakteria.
  5.  Malaria huambatana na maumivu ya kichwa, homa ya matumbo huambatana na maumivu ya uti wa mgongo.
Chagua Jibu


18. Kipi kati ya vifuatavyo vinapaswa kudumishwa? 

  1. Kutumia kikombe kimoja wakati wa kunywa maji. 
  2. Kunawa mikono kabla ya mlo katika karai moja. 
  3. Kupika mboga za majani na nyama kwa muda mrefu.
  4. Kuchemsha na kuchuja maji ya kunywa. 
  5. Kuogelea katika mito na mabwawa.
Chagua Jibu


19. Viungo vinavyohusika katika kutoa takamwili mwilini ni:

  1.  figo, ini na moyo            
  2.  ini, ngozi na figo 
  3.  mapafu, moyo na figo              
  4.  moyo, figo na ngozi 
  5.  Ngozi, Ini na Moyo 
Chagua Jibu


20. Mbungo husababisha ugonjwa uitwao ....

  1.  homa ya matumbo     
  2.  nagana
  3. malale                                           
  4. matende                
  5. homa ya ini
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256