STD VII SAYANSI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2016
201 6 - SAYANSI
SEHEMU A
Chaguajibu sahihi kisha andika herufiyake kwenye karatariya kujibia.
1. Ili mbegu ichipue inahitaji:
Maji, udongo na hewa
Mvua, hewa na udongo
Unyevu, udongo na jotoridi
Maji, hewa na jotoridi
Maji, mwanga na upepo
Chagua Jibu
2.Wadudu wanapohama toka ua moja kwenda lingine wanfanya hivyo ili:
kuzalisha mimea
kuepuka maadui
kutafuta nekta
kutafuta harufu
kusambaza mbegu
Chagua Jibu
3.Hali ya mtu kuzimia hutokana na ukosefu wa damu katika .......
Tumbo
Figo
Mapafu
Moyo
Ubongo
Chagua Jibu
4. Aina kuu mbili za mashine ni:
ngumu na laini
rahisi na tata
za kumenya na kutwanga
puli na roda
roda na katapila
Chagua Jibu
5.Mojawapo ya njia za kuondoa takamwili katika mwili ni:
kutema mate
kukojoa
kuoga
kunawa mikono
kutoa machozi
Chagua Jibu
6.Mbegu ya kike ambayo haijarutubishwa huitwa:
kondo
yai
uterasi
ovari
mrija wa falopio
Chagua Jibu
7.Angalia kielelezo namba 1 ambapo jotoridi lioneshwa kwa nyuzi za sentigredi kisha jibu maswali yanayofuata.
Mbegu itakayoota ni ya chombo kipi?
Chombo A
Chombo B
Chombo C
Chombo D
Chombo A na D
Chagua Jibu
8.Sehemu zinazounda mfumo wa upumuaji katika mwanadamu ni:
pua, mdomo na tumbo
mapafu, pua na ini
pua, mapafu na masikio
koromeo, mapafu na kongosho
mapafu, pua na mdomo
Chagua Jibu
9.Mdudu yupi kati ya wafuatao huleta hasara kwa mkulima akiwa katika hatua ya pili ya ukuaji?
Inzi
Kipepeo
Panzi
Mbungo
Mbu
Chagua Jibu
10. Usafirishaji wa chakula mwilini hufanywa na:
moyo
damu
misuli
mapafu
maji
Chagua Jibu
11.Tazama kwa makini kielelezo namba 2 kisha jibu maswali yanayofuata:
Alama Y inawakilisha sehemu iitwayo:
petali
filamenti
chavulio
pistili
ovari
Chagua Jibu
12. Mbegu za mimea uhifadhi chakula katika:
mizizi
majani
shina
kotiledoni
tunda
Chagua Jibu
13. Lipi kati ya magonjwa yafuatayo huambukizwa kwa njia ya kujamiiana?
Polio
Kipindupindu
Pepopunda
Kaswende
Tetekuwanga
Chagua Jibu
14.Nini kitatokea iwapo idadi ya wanyama wanaokula nyama katika eneo ni kubwa kulikc idadi ya wanaokula majani?
Majani yatapungua
Majani yatabakia kama yalivyokuwa awali
Majani yatanyauka
Majani yataongezeka
Majani yataliwa
Chagua Jibu
15.Lipi kati ya mafungu yafuatayo ya vyakula hulinda mwili?
Samaki na maziwa
Ugali na ndizi
Maharagwe na karanga
Mayai na kabichi
Matunda na mboga za majani
Chagua Jibu
16.Umuhimu wa asidi ya haidrokloric katika tumbo ni:
kubadili hali ya besi katika tumbo
kulainisha mafuta tumboni
kuongeza uchachu tumboni
kumengenya vyakula vya sukari tumboni
kuua wadudu wanaoingia tumboni na chakula.
Chagua Jibu
17. Nini tofauti kati ya malaria na homa ya matumbo?
Malaria hushambulia mishipa ya damu, homa ya matumbo hushambulia neva za fahamu.
Malaria husababishwa na mbu, homa ya matumbo husababishwa na inzi.
Malaria hutibiwa kwa siku nne, homa ya matumbo hutibiwa kwa siku saba.
Malaria husababishwa na plasmodiam, homa ya matumbo husababishwa na bakteria.
Malaria huambatana na maumivu ya kichwa, homa ya matumbo huambatana na maumivu ya uti wa mgongo.
Chagua Jibu
18. Kipi kati ya vifuatavyo vinapaswa kudumishwa?
Kutumia kikombe kimoja wakati wa kunywa maji.
Kunawa mikono kabla ya mlo katika karai moja.
Kupika mboga za majani na nyama kwa muda mrefu.
Kuchemsha na kuchuja maji ya kunywa.
Kuogelea katika mito na mabwawa.
Chagua Jibu
19. Viungo vinavyohusika katika kutoa takamwili mwilini ni:
figo, ini na moyo
ini, ngozi na figo
mapafu, moyo na figo
moyo, figo na ngozi
Ngozi, Ini na Moyo
Chagua Jibu
20. Mbungo husababisha ugonjwa uitwao ....
homa ya matumbo
nagana
malale
matende
homa ya ini
Chagua Jibu
21. Tunaweza kujikinga na magonjwa ya moyo kwa kufanya yafuatayo: .......
Kula chakula na kufanya mazoezi mara kwa mara
Kufanya mazoezi ya mwili, kuepuka kuvuta sigara na kuepuka kunywa pombe
Kula chakula chenye chumvi na kunywa pombe
Kufanya mazoezi ya mwili na kuvuta sigara
Kula vyakula vyenye mafuta na kunywa pombe
Chagua Jibu
22. Wanawake wajawazito wanashauriwa kula kiwango kikubwa cha vyakula vifuatavyo:
Wanga, mafuta na hamirojo
Mafuta, vitamini na protini
Protini, vitamini na madini ya chumvichumvi
Madini ya chumvichumvi na vitamini pekee
Protini, hamirojo na udongo pekee
Chagua Jibu
23. Ili kujikinga dhidi ya malaria ni muhimu .........
kumeza mchanganyiko wa madawa
kutumia dawa za mitishamba
kutumia vyandarua vilivyowekwa dawa
kujifunika na blanketi Zito lililowekwa dawa
kufanya mazoezi kila mara
Chagua Jibu
24. Kongosho hutoa homoni inayothibiti kiasi cha:
damu mwilini
sukari mwilini
takamwili
hamu ya chakula
oksijeni
Chagua Jibu
25.Mojawapo ya kazi za misuli katika mwili ni:
kuwezesha kujongea
kuruhusu damu kupita
kuruhusu maji kupita
kuruhusu hewa kupita
kuimarisha mwili
Chagua Jibu
26. Lipi kati ya mambo yafuatayo si sahihi kumfanyia mtu aliyebanwa misuli?
Kuchua eneo lililoathirika kwa kiganja
Kuchua kwa kukandamiza eneo lililoathirika hadi misuli ilegee
Kuuchua msuli kwa kitambaa na maji baridi
Kuweka kemikali zitakazowezesha misuli kulegea
Kulala juu chini na kuchua msuli ulioathirika kvva maji moto.
Chagua Jibu
27.Mtu anayetapika na kuharisha anapaswa kupewa:
asidi, maziwa na maji
maziwa, besi na sukari
maji, besi na maziwa
chumvi, sukari na maji
sukari, asidi na besi
Chagua Jibu
28. Huduma ya kwanza anayopewa mtu aliyezimia ni:
kumpa hewa ya oksijeni
kumpa juisi ya nazi mbichi
kumlaza juu chini na kumbonyeza tumbo
kumpa maji yaliyochanganywa na glukosi
kumpa juisi ya malimao, sukari na chumvi
Chagua Jibu
29.Mtandao wa watu wenye virusi vya UKIMWI unatanuka kwa kuwa
matumizi ya kondom na simu za mkononi yameongezeka
matangazo kuhusu UKIMWI yameboreshwa
kuna ongezeko la mahusiano ya kingono yasiyo salama
elimu ya UKIMWI inatolewa kwa watu wachache
watu wenye UKIMWI wanazingatia kanuni za kujikinga na UKIMWI
Chagua Jibu
30.UKIMWI husambazwa kwa kupitia:
kusalimiana kwa kushikana mikono na mgonjwa wa UKIMWI
kulala chumba kimoja na mgonjwa wa UKIMWI
kuongea na mwathirika wa UKIMWI
kuwekewa damu
kuosha nguo za mwathirika wa UKIMWI.
Chagua Jibu
31. Ili kuepuka kupata maambukizi mapya ya UKIMWI tunashauriwa:
kumeza dawa na kufanya mazoezi
kuwa mwaminifu na kuepuka ngono zembe
kuepuka kushirikiana na waathirika
kuepuka kula pamoja na kubadilishana nguo na waathirika
kupata chanjo ya UKIMWI na Kifua Kikuu.
Chagua Jibu
32. Nini kati ya vifuatavyo husababisha chupa ya plastiki kusinyaa hewa inapoondoleua ndani?
Hewa ndani ya chupa kuwa na mgandamizo mkubwa zaidi ya hewa nje ya chupa
Hewa nje ya chupa kuwa na mgandamizo mkubwa kuliko hewa ndani ya chupa
Mgandamizo wa nje na ndani ya chupa kulingana
Mgandamizo wa hewa ndani ya chupa kuwa pungufu ya mngandamizo wa kutoa hewa nje ya chupa
Mgandamizo nje ya chupa kuwa sawa na ujazo wa hewa mdomoni.
Chagua Jibu
33.Chembe ndogo kabisa za maada zinazounda elementi na zinazohusika katika kutengenezz bondi za kikemikali huitwa:
molekyuli
elektroni
protoni
atomi
nyutroni
Chagua Jibu
34. Mwanga hupinda unapopita kutoka
Ncha ya Kaskazini kwenda Kusini
media moja kwenda nyingine
Ncha ya Kaskazini kwenda Mashariki
Magharibi kwenda Mashariki
Kaskazini kwenda Magharibi
Chagua Jibu
35.Tazama kielelezo namba 3 kinachoonesha muundo wa atomi.
Je, ni herufi gani inayowakilisha elektroni?
T
S
R
Q
P
Chagua Jibu
36.Msuguano baina ya kifaa cha plastiki kama chana na nywele huzalisha:
oksijeni
chaji za umeme
sumaku
mfereji
molekyuli za mafuta
Chagua Jibu
37.Ipi kati ya alama zifuatazo inawakilisha atomi ya klorini?
K
P
Na
CI
H
Chagua Jibu
38. Hewa ya kabonidaiyoksidi hutumika kuzima moto kwasababu:
haichochei uwakaji
ni nzito kuliko hewa
haiwaki
hunyonya joto
huungana na oksijeni
Chagua Jibu
39.Ipi kati ya zifuatazo ni kazi za sumaku?
Kutengeneza uga sumaku na kunyanyua mizigo
Kuzalisha umeme na kuunda dira
Hutumika katika vipaza sauti na hutengeneza uga sumaku
Kuvuta ncha ya kaskazini na kuzalisha umeme
Kuonesha mwelekeo na kuundia spika.
Chagua Jibu
40.Tafuta umbali kati ya mzigo na egemeo katika wenzo iwapo mzigo wa gramu 50, utanyanyuliwa kwa jitihadi ya Nyutoni 100 iliyo katika umbali wa sm 40 kutoka katika egemeo.
sm75
1500
sm 140
sm 80
sm 12.5
Chagua Jibu
41. Aina kuu mbili za sakiti za umeme ni:
mkondo geu na mnyoofu
sambamba na mfuatano
mkondo geu na sambamba
mkondo mnyoofu na mkondo geu
mkondo mnyoofu na sambamba
Chagua Jibu
42. Mifupa imeundwa kwa madini ya:
Sodiamu na kalsiamu
Kalsiamu na oksijeni
Fosforasi na kalsiamu
Salfa na fosforasi
Kalsiamu na chuma
Chagua Jibu
43. Asidi ikiungana na besi huunda:
chumvi na maji
kaboneti ya sodiamu
chumvi na besi
maji na asidi
chumvi na oksijeni
Chagua Jibu
44. Iwapo mashine yenye mzigo wa kgf 90 huhitaji jitihadi ya kgf 15, ni nini manufaa ya kimakanika?
15
10
8
6
5
Chagua Jibu
45. Sumaku inaweza kuvuta vitu vyenye asili ya:
mpira
udongo
madini
karatasi
chuma
Chagua Jibu
46.Kitendo cha bakteria kuozesha kinyesi cha wanyama kwenye shimo pasipokuwa na hewa ya oksijeni husababisha:
joto kali
gesivunde/biogesi
asidi kali
alkali kali
haidrojeni
Chagua Jibu
47.Je ni sehemu ipi ya jicho ambamo taswira hutengenezwa?
Irisi
Lenzi
Kano
Filim
Retina
Chagua Jibu
48.Katika kurunzi, nishati ya umeme inayotoka kwenye betri hubadilishwa na kuwa:
nishati ya kikemikali
nishati ya joto
nishati ya kimakaniki
nishati ya mwanga
Nishati ya moto
Chagua Jibu
49.Nini maana ya dhanio katika utafiti wa kisayansi?
ni wazo tu
ni utabiri wa matokeo ya kubuni
utabiri wa matokeo ya jaribio
wazo la kina
mawazo yaliyojengwa kabla ya utafiti
Chagua Jibu
50.Mojawapo ya hatua za kufuata unapoandaa jaribio la kisayansi ni: