STD VII SAYANSI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2014
2014 - SAYANSI
Chagua herufi ya jibu lililo sahihi, kisha andika katika karatasi ya majibu/kujibia
1. Lipi kati ya magonjwa yafuatayo husambazwa na inzi na mende?
Tetekuwanga
Kuhara
Kifaduro
Utapia mlo
Homa ya matumbo
Chagua Jibu
2.?pi kati ya yafuatayo sio sehemu ya mfumo wa damu?
Bronchiole
Valvu
Auriko
Capillari
Ateri
Chagua Jibu
3.Lipi kati ya yafuatayo linapaswa kuzingatiwa kabla ya kumhudumia mgonjwa wa UKIMWI?
Vaa nguo safi
Nawa kwa sabuni
Vaa glovu
Sali
Mruhusu apumzike
Chagua Jibu
4.?pi kati ya yafuatayo ni ?ifa ya maji safi na salama?
Yametekwa kwenye kisima.
Yamehifadhiwa na kupoozwa kwenye mtungi wa maji
Yamechujwa na kuhifadhiwa kwenye chombo safi
Yamechemshwa, yamechujwa na kuhifadhiwa kwenye chombo safi
Yasiwe na magadi mengi
Chagua Jibu
5. Upi kati ya magonjwa yafuatayo hauna chanjo?
Kifua kikuu
Pepopunda
Surua
Kifaduro
Trakoma
Chagua Jibu
6. Gesi inayotumiwa na mimea kutengeneza protini ni:
carbondayoksaidi
haidrojen
oksijen
naitrojen
gesi asilia
Chagua Jibu
7.Kiwango cha maji kinachopotezwa na mmea huathiriwa na hali za hewa zifuatazo...
joto na unyevu
unyevu na mwanga
upepo na mwanga wa jua
mawingu na upepo
unyevu na upepo
Chagua Jibu
8.Tunaweza kusababisha mmomonyoko wa ardhi kwa kufanya mojawapo ya mambo yafuatayo:
Kukata miti
Kuongeza mbolea kwenye udongo
Kuotesha nyasi
Kuweka matuta lavenye maeneo ya mteremko
Kupanda miti
Chagua Jibu
9.Shughuli za mwanadamu kama kilimo, ufugaji wa wanyama na uchimbaji madini vyote hutegemea:
mito
chemchemi
ardhi
umwagiliaji
upepo
Chagua Jibu
10. Kinyonga hujibadili rangi yake ili:
kutafuta chakula
kupumua
kuzaliana
kutafuta maadui
kujilinda dhidi ya maadui
Chagua Jibu
11. Mende hupitia hatua kuu ......... katika ukuaji wake?
mbili
tatu
nne
tano
sita
Chagua Jibu
12. Yupi kati ya wanyama wafuatao hana uti wa mgongo?
Buibui
Popo
Paka
Mwanadamu
Kuku
Chagua Jibu
13.Mojawapo ya kazi ya misuli katika mwili ni:
kuzuia kutokwa damu
kuwezesha mwendo
kutengeneza selihai nyeupe
kushikilia meno mahali pake
kuiwezesha kunyooka
Chagua Jibu
14.Viungo katika mifupa huwezesha .........
kuzuia mifupa kuvunjika
mifupa iwe ya sawa
kurahisisha kujongea
kuupa mwili umbo
mifupa kunyooka
Chagua Jibu
15. ..... hupinda unapopita kutoka maada ya aina moja kwenda nyingine.
Upinde wa mvua
Mistari sambamba
Miale ya mwanga
Lenzi
Mwale na lenzi
Chagua Jibu
16.Mionzi ambayo hupinda zaidi mwanga unapopinda ni ile ya . ....
rangi nyekundu
njano
bluu iliyoiva
bluu
zambarau
Chagua Jibu
17.Tazama mchoro ufuatao unaoonesha sehemu za ndani za mbegu ya haragwe....
Ni sehemu ipi inayohusika na kuilinda mbegu isiharibiwe na wadudu waharibifu mabadiliko ya jotoridi?
2
3
5
4
1
Chagua Jibu
18. Anga huonekana la rangi ya bluu kwasababu .
hewa na maji ny vya rangi ya bluu
rangi nyekundu inatawanywa zaidi kuliko rangi ya bluu
uwezo wa kuona hupungua
rangi ya bluu hutawanywa zaidi ya rangi nyingine
wakati wa mawio jua huonekna kama la manjano
Chagua Jibu
19. Kipi kati ya vifuatavyo hakitumii sumaku?
Kipaza sauti
Simu ya mezani
Redio
Simu ya mkono
Pasi
Chagua Jibu
20. Kipimio cha kazi ni:
kilogramu
Newton
Tani
Joule
Gramu
Chagua Jibu
21. Hatua ya kwanza ya utafiti wa kisayansi ni
kuanza jaribio
kukusanya data
kutambua tatizo
kuchanganua data
kutafsiri matokeo
Chagua Jibu
22.Hatua ya tatu ya utafiti wa kisayansi ni .........
kuchambua data
kutafsiri matokeo
kuandaa na kuanza jaribio
ukusanyaji wa data
kutambua tatizo
Chagua Jibu
23.Bahati aliweka karatasi nyekundu ya litmus kwenye myeyuko asioutambua. Rangi ya karatasi ya litmas ilibadilika na kuwa bluu.Hii inaonesha kuwa myeyuko ule ulikuwa .........
asidi
besi
maji
mafuta
spiriti
Chagua Jibu
24. Matokeo ya jaribio yanaweza kuwa mojawapo ya yafuatayo:
Kweli au uongo
Yaliyochambuliwa au yasiyochambuliwa
Yenye maswali au yasiyo na maswali
Ya awali au ya kati
Ya awali au ya mwisho
Chagua Jibu
25.Nini kitatokea iwapo ncha mbili za KASKAZINI za sumaku zitaletwa pamoja?
Zitavutana kwa nguvu
Zitavutana kuelekea upande mmoja
Zitasukumana
Hakuna kitakachotokea
Zitavunjika
Chagua Jibu
26.PQ ni rula ya urefu wa nusu meta. Mzigo wa gram 20 umewekwa kwenye sehemu P umbali wa meta 0.1 kutoka kwenye egemeo. lwapo mzigo M utawekwa sehemu Q umbali wa meta 0.4 kutoka kwenye egemeo, nini uzito wa M?
4g
10g
5g
2.5g
25g
Chagua Jibu
27. Dhana ya kuakisiwa kwa mwanga inadhihirika katika moja ya vifaa vifuatavyo:
Hadubini
Televisheni
Saa
Balbu
Miwani
Chagua Jibu
28.Tazama kielelezo namba 2 kinachoonesha sakiti ya umeme yenye balbu zilizounganishwa sambamba na kisha jibu maswali yafuatayo:
Iwapo balbu namba 2 itaungua, balbu namba ......
3 pekee itabaki ikiwaka
1 na 3 zitabaki zikiwaka
1 pekee itabaki ikiwaka
1 na 3 zitaungua
3 itaungua
Chagua Jibu
29.Uwepo wa viumbehai, maji na hewa ni sifa ya sayari ipi?
Zebaki
Mihiri
Utaridi
Dunia
Sarateni
Chagua Jibu
30. Mhimili wa dunia umeinama katika nyuzi ...
60
18 1/2
32 1/2
25 1/2
23 1/2
Chagua Jibu
31.Ipi kati ya vifuatavyo huzunguka dunia toka magharibi kwenda mashariki?
Jua
Nyota
Mwezi
Kimondo
Sayari
Chagua Jibu
32. Mtu mwenye goita ana upungufu wa ...
madini ya kalsium
madini joto
madini ya potasiam
madini ya fosforas
madini ya chaki
Chagua Jibu
33. Tazama mchoro ufuatao kwa umakini kisha jibu maswali yafuatayo
Herufi gani inaonyesha uterasi?
C
D
E
A
B
Chagua Jibu
34.Mojawapo ya kazi za mifupa ni kutengeneza:
seli visahani
plasma
selihai nyeupe
selihai nyekundu
selihai za kugandisha damu
Chagua Jibu
35.Uhuru ana tatizo la meno yanayovunjika na miguu dhaifu. Ni virutubisho gani utamshaufi atumie ili kutatua tatizo lake hili?
Madini ya chuma
Madini ya fosforasi
Madini ya kasiamu
Madini joto
Vitamini K
Chagua Jibu
36.Mwalimu alipomwuliza Ahadi swali juu ya mfumo wa jua alifikiri kwa muda kisha akatoa jibu sahihi kwa mwalimu. Je ahadi alitumia sehemu gani ya ubongo kujibu swali?
Ubongo wa mbele
Ubongo wa nyuma
Ubongo wa kati
Ubongo wa mbele na nyuma
Ubongo wa kati na wa nyuma
Chagua Jibu
37.Kazi ya uta mgongo katika mfumo wa fahamu wa mwanadamu ni
Kuongoza matendo ya hiari
kuongoza matendo yasiyo ya hiari
Kuongoza miondoko ya mwili
kudumisha umbo la mwili
kupeleka taarifa katika mfumo mkuu wa fahamu.
Chagua Jibu
38. Kupwa na kujaa kwa maji katika bahari na maziwa makubwa husababishwa na ...
dunia kuzunguka jua
dunia kuzunguka katika mhimili wake
kupatwa kwa mwezi
kupatwa kwa jua
uvutano kati ya dunia na mwezi
Chagua Jibu
39.Katika hali ya kawaida, kutu ni matokeo ya mjibizo wa athari za kikemikali kati ya:
shaba, maji na oksijeni
sodiamu, maji na oksijeni
kalsiamu, maji na oksijeni
chuma, oksijeni na maji
maji, oksijeni na potasiamu
Chagua Jibu
40.Mboga za majani na matunda huwezesha utengenezwaji wa:
selihai nyekundu
selihai nyeupe
chembe visahani
plasma
uboho
Chagua Jibu
41. Njia zifuatazo huweza kutumiwa kuhifadhi vyakula na mazao ili visiharibike ISIPOKUWA:
kuoka
kutumia asali
kukausha
kutumia chumvi
kutumia maji
Chagua Jibu
42. Yafuatayo ni makundi ya vyakula isipokuwa:
madini ya chumvi chumvi
vitamini
Maji
protini
hamirojo
Chagua Jibu
43.Vipi kati ya vyakula vifuatavyo vinaweza kuhifadhiwa kwa kugandisha kwa baridi?
Matunda na mbogamboga
Mbogamboga na nafaka
Samaki na matunda
Nyama na samaki
Nyama na nafaka
Chagua Jibu
44.Ugonjwa utokanao na ukosefu wa madini ya chuma kwenye mlo ni: