SAYANSI 2013
Chaguajibu sahihi kisha andika herufiyake kwa kila swali.
1. Ni sehemu zipi za mwili zinahusika na utoaji wa takamwili?
2. Kundi lipi limeainisha wanyama wenye uti wa mgongo?
3. Endapo mito na mabwawa yatakauka, ni viumbe hai Vipi kati ya vifuatavyo vitaathirika zaidi?
3. Endapo mito na mabwawa yatakauka, ni viumbe hai Vipi kati ya vifuatavyo vitaathirika zaidi?
5. Ni sehemu ipi ya ua hupokea mbegu za kiume?
6. Uhusiano uliopo kati ya viumbe hai na visivyo hai katika mazingira unaitwa
7. Ni Vipi kati ya viumbe hai vifuatavyo hujitengenezea chakula chao kwa kutumia klorofili?
8. Tezi inayodhibiti matendo ya ukuaji wa mwili na kulinda mwili dhidi ya magonjwa huitwa
9. Wanyama wenye uwezo wa kuishi majini na nchi kavu ni wale wa kundi la
10. Maji safi na salama ni maji ambayo
11. Ugonjwa wa kipindupindu ni hatari sana kwa binadamu kwa kuwa
12. Mwanafunzi wa Darasa la Sita alipumulia hewa ndani ya neli jaribio yenye myeyuko usiokuwa na rangi, kisha akatikisa neli jaribio hiyo. Baada ya kuitikisa myeyuko ulionekana kuwa na rangi nyeupe. Je, kemikali gani ilikuwa kwenye myeyuko usiokuwa na rangi?
13. Homoni inayodhibiti sukari katika mwili wa binadamu huitwa.
14. Himoglobini katika chembe chembe nyekundu za damu inafanya kazi gani?
15. Ili kuimarisha mifupa na meno, mtoto anahitaji
16. Ugonjwa unaosababishwa na bakteria aina ya basili ambao hushambulia mapafu huitwa
17. Ni magojwa yapi kati ya yafuatayo huitwa magojwa ya kuambukiza?
18. Kemikali inayotumika kubaini uwepo wa chakula aina ya wanga inaitwa.
19. Ingawa wanyama huvuta hewa ya oksijeni na kutoa hewa ya kabondayoksaidi, hewa hizi hazipungui wala kuongezeka kwenye mizazi kwa kuwa.
20. Vyakula vyenye mafuta vina umuhimu gani mwilini?
21. Vyakula vinavyosababisha kukua kwa miili ya wanyama huitwa
22. Huduma ya kwanza hutolewa kwa lengo gani?
23. Huduma ipi ya kwanza kati ya zifuatazo hutolewa kwa mtu aliyekazwa na misuli?
24. Mtu anayeharisha na kutapika anapoteza
25. Kifaa kifuatacho siyo muhimu kuwemo katika sanduku Ia huduma ya kwanza
26. Magonjwa yapi kati ya yafuatayo yanazuilika kwa chanjo?
27. Kuvimba miguu, kula sana na kuhisi njaa mara kwa mara ni dalili za ugonjwa wa
28. Jeki, parafujo, mkasi na patasi ni aina za mashine rahisi ziitwazo
29. Chunguza mlinganyo wa kikemikali ufuatao kisha jibu swali linalofuata.
Herufi Y inawakilisha Kemikali ipi?
30. Tendo lipi kati ya yafuatayo linasababisha maada mpya kutokea?
31. Madhara gani yatatokea endapo vyanzo vya maji havitalindwa?
32. Mchakato wa usafirishaji wa myeyuko wa chumvichumvi katika mimea huitwa.
33. Atomi mbili za haidrojeni zikiungana kikemikali na atomi moja ya oksijeni kampaundi inayotengenezwa huitwa
34. Gesi inayosaidia vitu kuwaka ni
36. Maji ambayo ukitumia sabuni hubadilika rangi kuwa meupe mithili ya maziwa huitwa
36. Mwangwi humaanish sauti...
37. Kwa nini sauti za watangazaji wa radio na televisheni hazisikiki nje ya vyumba vya kutangazia kupitia kuta za vyumba hivyo?
38.Kiasi cha mkondo wa umeme katika sakiti hupimwa kwa kutumia
39. Kielelezo Na 1 kinawakilisha tendo la kusumakisha.
Iwapo ncha ya sumaku ya kaskazini (N) itatumika kusumakisha ncha X ya kipande cha chuma chenye ncha X — Y, ncha Y ya kipande cha chuma itakuwa sawa na ncha ipi ya sumaku?
40. Ipi kati ya rangi zifuatazo ina uwezo wa kuakisi miale ya mwanga lakini sio kusafirisha miale hiyo?
41. Mshipi na ndoano ya kuvua samaki ni mifano ya nyenzo daraja la ngapi?
42. Chunguza sakiti ya umeme iliyooneshwa katika kielelezo Na 2 kisha jibu swali lifuatalo
Sakiti iliyooneshwa katika kielelezo Na 2 huitwa
43. Mkulima aligundua kuwa jembe lake lililotengenezwa kwa chuma limepata kutu. HaE imesababishwa na jembe kugusana na
44. Mtu mwenye WU anaweza kutambulika kutokana na
45. Mgonjwa wa UKIMWI anastahili kupata mlo maalumu ili
46. Unyafuzi ni ugonjwa unaosababishwa na ukosefu wa
47. Dalili mojawapo ya ugonjwa wa UKIMWI ni
48. Katika uchunguzi wa kisayansi hatua ipi hutumika kukubali au kukataa dhanio?
49. Kazi ya chembe nyekundu za damu katika mwili wa binadamu ni
50. Chunguza kielelezo Na. 3 kinachoonesha mzunguko rahisi wa damu katika mwili wa binadamu kisha jibu swali linalofuata.
Herufi zinazowakilisha mishipa ya damu inayosafirisha damu isiyokuwa na oksijeni ni
MTIHANI WA SAYANSI DARASA LA IV 2013
SEHEMU A
Jibu sali namba 1 hadi 10 kwa kuchagua jibu sahihi na kisha kuandika herufi yake pembeni ya namva ya swali.
1. Mimea haiwezi kuendelea kukua bila hewa, maji na . . . . .
2. Jasho hutoka mwilini kwa . . . . . . vilivyoko kwenye ngozi
3.Chumvi katika maji inaweza kutenganishwa na maji kwa . . . . . . .
4. Fagio na sepetu ni mifano ya nyenzo daraja la . . . . . . . . .
5. Jotoridi la kuganda kwa maji(maji kuwa barafu) ni . . . . . .
6. Kutembea, kusimama na kukimbia kwa muda mrefu husababisha . . . . . . kukaza
7. Mzunguko kamili wa . . . . . . huitwa sakiti
8. Vitu vilivyoundwa kwa . . . . . . huweza kuvutwa na sumaku
9, Joto husambaa katika kimiminika kwa njia ya . . . . . .
10. Mwanga husafiri katika mstari. . . . . .
SEHEMU C
Jibu swali la 11 hadi la 17 kwa kujaza nafasi zilizoachwa wazi.
11. . . . . . . ni kifaa kinachotumika kuangalia vitu vidogo ambavyo haviwezi kuonekana kwa macho yetu.
Fungua Jibu12. Maji katika hali yabisi huitwa. . . . . .
Fungua Jibu13.. . . . . . ni kifaa kinachotumika kunyoosha mguao na kuzifanya zionenkane nadhifu.
Fungua Jibu14. Katika sakiti ya umeme, alama huwakilisha . . . . . .
15. . . . . . . husababishwa na kukojoa na kujisaidia haja kubwa katika maji na huenezwa na konono wa majini..
Fungua Jibu16. Sauti iliyoakisiwa huitwa . . . . . .
Fungua Jibu17. Maji yakichemshwa hubadilika na kuwa . . . . . .
Fungua JibuSEHEMU C
Jibu swali la 18 hadi la 20 kwa kuandika "Ndio" au "Hapana"
18. Selihai nyeupe za damu hulinda miili yetu dhidi ya magonjwa . . . . . .
Fungua Jibu19. Inafaa kumtenga mgonjwa wa UKIMWI na watu wengine . . . . . .
Fungua Jibu20. Nyenzo daraja la tatu, jitihada huwa kati ya egemeo na mzigo. . . . . .
Fungua JibuSEHEMU D
Jibu swali la 21 hadi la 25 kwa kuoanisha maneno toka "Fungu A" na sentensi zilizoendana nayo kutoka "Fungu B"
FUNGU A | FUNGU B |
21. Kipimajoto 22. Mwangwi 23. Kwashakoo 24. Sepali 25. Ufagio |
|