STD VII SAYANSI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2012

SAYANSI - 2012

Chagua jibu sahihi kisha andika herufi yake kwa kila swali.

1. Ili kudumisha afya ya mwili, tunapaswa:

  1. kufanya mazoezi, kula chakula bora na kupumzika.
  2. kulala sana, kula chakula bora na kucheza.
  3. kutofanya kazi ngumu, kufanya mazoezi na kulala.
  4. kufanya mazoezi na kushiriki michezo
  5. kula vizuri na kufanya mazoezi muda wote.
Chagua Jibu


2.Ni kipi kati ya virutubisho vifuatavyo ni muhimu kwa mama mjamzito kupata kwa wingi?

  1. Protini.
  2. Kabohaidreti.
  3. Mafuta.
  4. Chumvichumvi.
  5. Vitamini.
Chagua Jibu


3.Kukojoa mara kwa mara, kutoa mkojo mwingi na kupata kiu mara kwa mara ni dalili za ugonjwa upi?

  1. Kansa.
  2. Kisukari.
  3. Kwashakoo.
  4. Kifaduro.
  5. Upungufu wa damu.
Chagua Jibu


4.Ni njia gani kati ya zifuatazo inafaa kumsaidia mtu aliyepata mshtuko uliotokana na kunaswa na waya wenye umeme?

  1. Kumsukuma kwa mikono haraka.
  2. Kuuvuta waya wa umeme uliomshtua. 
  3. Kutumia maji kuuzima umeme.
  4. Kumvuta kwa kutumia kifaa kisichopitisha umeme.
  5. Kumwacha mpaka umeme ukatike wenyewe.
Chagua Jibu


4.Ni njia gani kati ya zifuatazo inafaa kumsaidia mtu aliyepata mshtuko uliotokana na kunaswa na waya wenye umeme?

  1. Kumsukuma kwa mikono haraka.
  2. Kuuvuta waya wa umeme uliomshtua. 
  3. Kutumia maji kuuzima umeme.
  4. Kumvuta kwa kutumia kifaa kisichopitisha umeme.
  5. Kumwacha mpaka umeme ukatike wenyewe.
Chagua Jibu


6.  Ipi kati ya zifuatazo siyo dalili ya UKIMWI?

  1. Kuvimba kwa matezi
  2. Kupoteza uzito 
  3. Kuharisha kusikokoma
  4. Kikohozi cha muda mrefu kisicho cha kawaida.
  5. Kutoa jasho kusiko kwa kawaida wakati wa usiku.
Chagua Jibu


7.  Zifuatazo ni njia za kujikinga na majanga mbalimbali katika mazingira isipokuwa:

  1. kuchimba mahandaki
  2. kujenga nyumba mbali na milima ya volcano
  3. kuweka akiba ya chakula
  4. kuishi maisha ya kuhamahama
  5. kudumisha usafi katika mazingira
Chagua Jibu


8.  Ni ipi kati ya zifuatazo ni mchanganyiko wa gesi mbalimbali?

  1. Mwanga 
  2. Hewa
  3. Mafuta ya taa 
  4. Kabondayoksaidi 
  5. Mvuke
Chagua Jibu


9.  Ni lipi kati ya matendo yafuatayo siyo sababu ya uharibifu wa mazingira?

  1. Uchomaji wa karatasi
  2. Maendeleo ya viwanda
  3. Kuoga ziwani
  4. Kutumia mbolea ya samadi
  5. Kuoshea magari mtoni.
Chagua Jibu


10.  Mfalme wa porini aliamuru wanyama wote walao nyama wauawe. Unafikiri ni nini kitatokea porini baada ya miaka mingi?

  1. Mimea itaota kwa wingi
  2. Idadi ya wadudu haitabadilika 
  3. Mimea itapungua 
  4. Wanyama walao majani watapungua 
  5. Mazingira yatabaki katika hali nzuri ya kuvutia.
Chagua Jibu


11.  Kani za asili husababisha moja kati ya mambo yafuatayo katika mazingira:

  1. Kutoonekana kwa samaki
  2. Tetemeko la ardhi 
  3. Ongezeko la mimea 
  4. Upungufu wa umeme 
  5. Kukauka kwa mito.
Chagua Jibu


12.  Ipi kati ya zifuatazo siyo njia sahihi ya kuhifadhi rutuba ya udongo katika shamba?

  1. Kubadilisha mazao 
  2. Kupanda mimea jamii ya kunde. 
  3. Kupumzisha shamba. 
  4. Kutumia mbolea 
  5. Kupanda zao la aina moja mfululizo.
Chagua Jibu


13.  Chura hupitia hatua kuu ngapi katika kukua kwake?

  1. Moja 
  2. Saba 
  3. Sita 
  4. Tano 
  5. Nane.
Chagua Jibu


14.  Mdudu yupi kati ya hawa wafuatao hupitia metamofosisi isiyokamilika?

  1. Mbu 
  2. Kipepeo 
  3. Inzi 
  4. Nyuki 
  5. Mende
Chagua Jibu


15.     Panya aliyekuwa amefungiwa kwenye kisanduku kilichokuwa na kipande cha nyama alikufa baada ya siku mbili. Ni kitu gani kilisababisha panya huyo kufa?

  1. Alikula nyama iliyooza
  2. Alikosa hewa ya kabondayoksaidi 
  3. Alikosa hewa ya oksijeni.
  4. Alikosa maji ya kutosha baada ya kula nyama.
  5. Alikosa mwanga ambao ni muhimu kwa ukuaji wa wanyama.
Chagua Jibu


16.  Ni kiumbe yupi kati ya hawa wafuatao ni amfibia?

  1. Chura 
  2. Panya 
  3. Mjusi 
  4. Kobe 
  5. Kinyonga.
Chagua Jibu


17.  Wanyama kama mamba, viboko, vyura wanaishi katika maskani gani?

  1. Angani na ardhini
  2. Ardhini na majini. 
  3. Mazingira yoyote ilimradi chakula kiwepo
  4. Ardhini na mapangoni 
  5. Kwenye misitu.
Chagua Jibu


17.  Wanyama kama mamba, viboko, vyura wanaishi katika maskani gani?

  1. Angani na ardhini
  2. Ardhini na majini. 
  3. Mazingira yoyote ilimradi chakula kiwepo
  4. Ardhini na mapangoni 
  5. Kwenye misitu.
Chagua Jibu


19.  Kuna aina kuu mbili za mbegu za mimea ambazo ni:

  1. ghalambegu kuu na ghalambegu ndogo
  2.  monokotiledoni na daikotiledoni 
  3. daikotiledoni na kikonyo kikuu
  4. mbegu zenye mizizi na zisizo na mizizi.
  5. mbegu za asili na za porini.
Chagua Jibu


20.  Miale ya mwanga wa radi inaonekana kabla ya kusikia mngurumo wa radi kwa kuwa:

  1. miale ya mwanga haizuiwi na chochote 
  2. sauti husharabiwa kwanza na mawingu 
  3. mwanga husafiri haraka kuliko sauti.
  4. sauti husafiri haraka kuliko mwanga
  5. mawingu yanayotoa sauti husafiri polepole.
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256