STD VII SAYANSI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2009

SAYANSI 2009

SEHEMU A

Chagua jibu sahihi na andika herufi inayohusika mbeleya nambaya kila swali katika karatasi ya kujibia.

1. Unaweza kumhudumia mtu aliyezirai kwa:

  1. kumpa hewa safi 
  2. kumtingisha kwa nguvu
  3. kumlaza kifudifudi 
  4. kumbonyeza tumboni polepole
  5. kumwekea kitambaa cha maji baridi usoni
Chagua Jibu


2. . . . . . . . .. husababishwa na upungufu wa virutubisho vya vitamin A.

  1. Utapiamlo 
  2. Ukavu macho 
  3. Matege
  4. Kiribatumbo 
  5. Unyafuzi
Chagua Jibu


3. Umuhimu wa kadi ya kliniki kwa watoto ni kuwezesha wahusika

  1. kujua tarehe ambayo mtoto alizaliwa
  2. kuhakikisha kuwa mtoto alizaliwa
  3. kufahamu maendeleo ya ukuaji wa mtoto
  4. kupata huduma za kiafya kiurahisi 
  5. kwenda na wakati
Chagua Jibu


4. Mgonjwa anayeharisha anatakiwa kupatiwa huduma gani ya kwanza?

  1. kumpeleka kwa daktari mapema
  2. kumpa vidonge kupunguza maumivu
  3. kumpa maji yaliyochanganywa limau, sukari na chumvi
  4. kumpeleka kwa mganga wa kienyeji 
  5. kumpa chakula cha kutosha
Chagua Jibu


5. Njia kuu inayoongoza kueneza virusi vya UKIMWI kwa watu ni:

  1. kutoboa masikio na pua 
  2. kuwekewa damu
  3. kujamiiana 
  4. ajali
  5. kudunga sindano
Chagua Jibu


6. Panda alikatazwa na mama yake kuchezea konokono. Unafikiria mama yake alikuwa anamwepusha na ugonjwa upi?

  1. kichocho 
  2. kuhara
  3. malaria
  4. malale 
  5. UKIMWI
Chagua Jibu


7. Todi alifungulia gesi toka kwenye mtungi na kuielekeza kwenye moto. Moto uliwaka zaidi. Je, mtungi ulikuwa na gesi gani?

  1. oksijeni 
  2. kabondayoksaidi 
  3. monoksaidi 
  4. Haidroksaidi
  5. gesi ya upepo
Chagua Jibu


8. Baadhi ya majanga ya asili ambayo huweza kuhatarisha mimea na misitu ni:

  1. mvua zinazoambatana na tufani, ukame na volcano
  2. moto, ukame na volcano
  3. mvua zilizoambatana na tufani, moto na volcano
  4. moto, ukame na mvua zilizoambatana na tufani
  5. moto, kemikali za mimea na mifugo mingi kupita kiasi
Chagua Jibu


9. Wakati wa mchana mimea ya kijani hupunguza gesi gani kwenye anga?

  1. kabonidayoksaidi 
  2. naitrojeni 
  3. haidrojeni 
  4. oksijeni 
  5. naitret
Chagua Jibu


10. Inashauriwa mahali pa kujenga Choo cha shimo pawe:

  1. bondeni karibu na mto
  2. ndani ya nyumba ya kuishi 
  3. mbali kidogo na nyumba ya kuishi
  4. tambarare sana 
  5. karibu sana na nyumba ya kuishi
Chagua Jibu


11. Iwapo swala katika mlishano ufuatao wataongezeka, lipi litajitokeza kwa haraka? MAJANI → SWALA → SIMBA

  1. majani yatapungua 
  2. simba watakufa
  3. idadi ya simba haitabadilika
  4.  kiasi cha majani hakitabadilika
  5. majani yataongezeka
Chagua Jibu


12. Baada ya utungisho, kitoto chura huitwa:

  1. lava 
  2. buu 
  3. tunutu 
  4. tedipoli
  5. yai
Chagua Jibu


13. Sehemu mbili za ua zinazoungana na kuwa stameni ni:

  1. mbegu na pistili 
  2. staili na kikonyo
  3. ovari na sepali 
  4. petali na sepali
  5. filamenti na kichavua
Chagua Jibu


14. Hatua ya pili katika ukuaji wa mende ni:

  1. lava 
  2. tunutu
  3. buu 
  4. mende kamili
  5. yai
Chagua Jibu


15. Kwa kawaida mimea hukua kuelekea wapi?

  1. kwenye maji
  2. kwenye mwanga
  3. mwelekeo wa upepo
  4. kwenye rutuba
  5. gizani
Chagua Jibu


16. Sehemu ya ua ambayo hupokea chavua au poleni huitwa:

  1. staili 
  2. stigma 
  3. ovari 
  4. stameni
  5. ovuli
Chagua Jibu


17. Mchoro ufuatao unaonesha kiumbe anayeishi majini.

Kielelezo 1

Ni sehemu ipi ya mwili wake humsaidia kuogelea?

  1. U
  2. R
  3. T
  4. V
  5. S
Chagua Jibu


18. Ni ogani ipi inayohusika kubadili seli hai nyekundu za damu kuwa chembechembe za nyongo katika mwili wa binadamu?

  1. ini 
  2. figo 
  3. moyo 
  4. mapafu 
  5. wengu
Chagua Jibu


19. Vifuatavyo ni vyanzo vya kuzalisha nishati ya umeme isipokuwa:

  1. maporomoko ya maji 
  2. nishati ya jua
  3. ngurumo ya mvua 
  4. fueli 
  5. upepo
Chagua Jibu


20. Eleza mabadiliko ya nishati yanayotokea katika Kielelezo kifuatacho wakati mvuke unapotumika kuzungusha kata upepo:

Kielelezo 2
  1. umeme kuwa sauti
  2. sauti kuwa joto
  3. joto kuwa kimakanika
  4. sauti kuwa umeme
  5. umeme kuwa sumaku
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256