STD VII SAYANSI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2008
SAYANSI 2008

SEHEMU A

Chagua jibu sahihi kisha andika herufi inayohusika mbeleya kila swali katika karatasi yakoya kujibia.

1.  Licha ya kusaidia kujenga misuli michezo huimarisha nini?

  1. Miguu 
  2. Viungo vya mwili
  3. Viungo vya kichwa 
  4. Mikono 
  5. Viungo vya sehemu ya juu ya mwili
Chagua Jibu


2.  Faida kubwa ya uzazi wa mpango kwa familia ni .........

  1. kuwapa watoto elimu
  2. kufanya idadi ya watoto kuwa kubwa
  3.  kuweza kujenga nyumba imara kwa ajili ya familia
  4.  kuepuka matatizo
  5. kuwa na uwezo wa kutoa huduma zote muhimu kwa familia
Chagua Jibu


3. Ni kundi lipi kati ya makundi yafuatayo hutoa mafunzo ya Huduma ya kwanza pamoja na huduma yenyewe?

  1.  Msalaba mwekundu
  2. Angaza 
  3. Askari wa zimamoto 
  4. Wasamaria wema 
  5. Askari wa usalama barabarani
Chagua Jibu


4. Chakula kinachoupatia mwili virutubisho vyote katika uwiano sahihi ni:

  1.  mlo wenye protini 
  2. mlo wenye protini na kabohaidreti
  3. mlo kamili 
  4. chakula kilichopikwa vizuri
  5. chakula kinachonukia vizuri
Chagua Jibu


5. Namanji anaonekana kupinda miguu. Unafikiri anakosa madini gani?

  1. Kalsiamu
  2. Sodiamu
  3. Magnesiamu 
  4. Chuma 
  5. Aluminiamu
Chagua Jibu


6.  Yafuatayo ni magonjwa yanayoweza kuzuiwa kwa njia ya chanjo kwa watoto:

  1. Kifaduro, polio, pepopunda na surua
  2. Kuhara, tetekuwanga, surua na homa ya matumbo
  3. Polio, unyafuzi, pepopunda na kifaduro
  4. Tetekuwanga, utapia mlo, surua na polio
  5. UKIMWI, kifua kikuu, pepopunda na kuhara damu
Chagua Jibu


7.  Degedege husababishwa na:

  1.  ugonjwa wa mafua ya ndege
  2. kikohozi kikali
  3. homa kali 
  4. kipindupindu
  5. UKIMVVI
Chagua Jibu


8.  Mama Katu ameingia chumbani na kumkuta mumewe ameanguka chini baada ya kushituliwa na umeme. Mama Katu atamsaidia mumewe kwa:

  1.  kumpa maji safi ya kunywa 
  2. kumpa maziwa
  3. kumtikisa kwa nguvu 
  4. kumpulizia hewa
  5. kumwogesha
Chagua Jibu


9.  Hewa ni mchanganyiko wa:

  1.  Oksijeni 
  2. kabondayoksaidi
  3. gesi 
  4. mvuke 
  5. maji na oksijeni
Chagua Jibu


10.  Maji katika hali ya mvuke ni:

  1.  Mawingu 
  2. mvua 
  3. barafu 
  4. umande 
  5. unyevu
Chagua Jibu


11.  Moja kati ya hatua ziifuatazo huzuia mmomonyoko wa udongo:

  1.  Kupunguza wingi wa miti 
  2. Kuchoma misitu
  3. Kupanda miti 
  4. Kukwatua nyasi
  5. Kuongeza idadi ya mifugo
Chagua Jibu


12 Kiwavi ni lava wa

  1. panzi 
  2. mende 
  3. chura 
  4. kipepeo 
  5. mbu
Chagua Jibu


13.Jambo lipi linaweza kusababisha kutokea kwa "badiliko chanya" katika maliasili ya mazingira?

  1.  Kuvua samaki kwa kutumia sumu
  2.  Kulima holela kwenye miinuko
  3.  Kukata miti ovyo karibu na vyanzo vya maji
  4. Kuvua samaki kwa kutumia baruti E. Kupanda miti na nyasi
Chagua Jibu


14.Zifuatazo ni sifa muhimu zinazotambulisha viumbe hai. Unafikiri ni sifa ipi haihusiki?

  1.  Kupumua 
  2. Kukua
  3. Kujitengenezea chakula
  4. Kujongea 
  5. Kuzaliana
Chagua Jibu


15.Sehemu ya mbegu inayotunza chakula cha mbegu inayoota ni:

  1. ghala
  2. ganda 
  3. embryo
  4. kijusi 
  5. kikonyo
Chagua Jibu


16. Chunguza jani la mmea lililooneshwa kwenye kielelezo kisha jibu swali linalofuata.

Jani hilo unaweza kulifananisha na jani la mmea upi kati ya ifuatayo?

  1.  Mpunga
  2.  Mtama
  3.  Kunde
  4.  Mahindi
  5. Mnazi
Chagua Jibu


17. Nta hutengenezwa kutoka katika ......... ya nyuki.

  1. Matezi 
  2. Mabawa 
  3. Macho
  4. Miguu
  5. Mafumbatio
Chagua Jibu


18.Sehemu ya ua inayovutia wadudu wanaokuja katika mmea na kusaidia uchavushaji na uchukuaji wa poleni inaitwaje?

  1. Petali 
  2. Sepali 
  3. Stigma 
  4. Kikonyo
  5. Pistili
Chagua Jibu


19. Mgongo wa chura ni mfupi ili kumwezesha .........

  1. kukimbia 
  2. kulala 
  3. kupaa
  4. kuruka na kutua 
  5. kugeuka
Chagua Jibu


20.Kipi kati a Vitu vifuata  husafirisha •oto kwa haraka zaidi?

  1. A
  2. B
  3. C
  4. D
  5. E
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256