STD VII SAYANSI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2007

SAYANSI 2007

SEHEMU A

Chagua jibu sahihi kisha andika herufi inayohusika mbele ya namba ya kila swali katika karatasi ya kujibia.

1. Umuhimu wa vyakula vya kabohaidreti mwili ni

  1. Kujenga mwili
  2. Kulinda mwili 
  3. Kutia nguvu 
  4. Kuweza kufikiri 
  5. Kuongeza joto
Chagua Jibu


2. Ukiwa katika chumba chenye giza na ghafla taa ikawashwa kitatokea nini kuhusu jicho?

  1. Mboni ya jicho itaongezeka ukubwa
  2. Mbona ya jicho itabaki vilevile
  3. Lenzi ya jicho itabinuka
  4. Mboni ya jicho itapungua ukubwa
  5. Kelele za nguvu zitasikika
Chagua Jibu


3. Kikohozi kikavu, homa, kutoka jasho usiku na kukohoa damu ni dalili za . . . . . .

  1. Kifua kikuu 
  2. Tetekuwanga 
  3. Pepopunda
  4. Homa ya matumbo 
  5. Kifaduro
Chagua Jibu


4. Michoro katika kielelezo namba 1 inawakilisha seli katika mwili wa binadamu ambazo kazi zake ni:

 Kielelezo Na. 1
  1. Kuzuia na kukinda mwili
  2. Kusafirisha oksijeni
  3. Kugandisha damu 
  4. Kurekebisha joto 
  5. Kusafirirsha taka mwilini
Chagua Jibu


5. Mtu mwenye kiribatumboni ni rahisi zaidi kupata ugonjwa gani?

  1. Moyo na msukumo mkubwa wa damu
  2. Kansa 
  3. Unyafuzi
  4. Kuvia kwa ukuaji wa akili 
  5. Kwashakoo
Chagua Jibu


6. Vinyesi na vitu vya wanyama na mimea vilivyooza

  1. Huufanya udongo usifae kwa kilimo
  2. Vinakaribisha wadudu wengine wanaoharibu mazao
  3. Vinaongeza mbolea ya mboji kwenye udongo 
  4. Havina umuhimu katika udongo
  5. Vinatumika kama chombo kwa wavuvi.
Chagua Jibu


7. Mwanga na sauti vina tabia moja tu. Je tabia hiyo ni ipi?

  1. Kupinda
  2. Kuakisi 
  3. Kusharabiwa
  4. Kupita kwenye vakyumu 
  5. Kusambaa
Chagua Jibu


8. Kuhifadhi vyakula katika jokofu ni njia ambayo ..

  1. Hufanya vyakula vikae muda mrefu bila kuharibika
  2. Inapunguza kazi ya kupika mara kwa mara
  3. Inapoteza ladha na kuvifanya vioze iwapo vitakaa siku nyingi 
  4. kugeuza chakula kuwa barafu
  5. inapunguza gharama ya kwenda sokoni.
Chagua Jibu


9. Ukiweka sarafu ya shilingi 20 katika beseni lenye maji, sarafu hiyo inaonekana mepansa juu. Hali hiyo hutokea kwa sababu .........

  1. Sarafu hiyo ni nyepesi
  2. Macho yanamatatizo
  3. Mwanga umenyooka 
  4. Maji ni kidogo
  5. Mwali wa mwanga hupinda unapoingia katika maji
Chagua Jibu


10. Kwa nini chupa za soda na bia hazijazwi hadi pomoni?

  1. Kwa ajili ya nafasi ya gesi
  2. Husaidia kufungwa chupa kwa urahisi
  3. Kuruhusu kutanuka wakati ya joto
  4. Kupunguza gharama
  5. Ikijazwa huweza kumwagikia mnywaji
Chagua Jibu


11. Volkano hai hutoa kimiminika kizito katika uso wa dunia kiitwacho:

  1. Lava 
  2. Kreta 
  3. Gesi 
  4. Volcano 
  5. Maji
Chagua Jibu


12. Kwa nini kwa kawaida mwanga unaonekana kwanza kabla ya muungurumo wa radi ingawa vyote vinatokea pamoja?

  1. Mwanga unamawimbi makubwa kuliko sauti
  2. Mishipa ya fahamu ya macho inafanya kazi haraka kuliko mishipa ya fahamu ya kusikia
  3. Mwendokasi wa mwanga ni wa haraka kuliko sauti
  4. Mwanga na sauti kwa kawaida husafiri wima 
  5. Mawimbi ya sauti hayasafiri katika hewa
Chagua Jibu


13. Vipi kati ya Vitu vifuatavyo vinaweza kusababisha uchafuzi wa hewa?

  1. Maji machafu ya viwandani, spiriti na ujenzi wa biashara
  2. Moshi, Majivu na mbolea
  3. Moshi wa viwandani na matokeo ya kuungua kwa petrol
  4. Misitu asili, viwanda na mbolea
  5. Mbolea, mboji na maji machafu ya viwandani

Chagua Jibu


14. Ni kiumbe kipi kati ya vifuatavyo huishi kwenye maji?

  1. Inzi 
  2. Buibui 
  3. kaa 
  4. Panzi 
  5. Mende
Chagua Jibu


15. Ukuaji wa mbu hupitia katika hatua/kuu nne. Mtiririko sahihi wa ukuaji huo ni  . . . . . . . . .

  1. Yai, pupa, lava, mbu 
  2. Pupa, yai, lava, mbu
  3. Yai, lava, pupa, mbu 
  4. Lava, yai, pupa, mbu
  5.  Pupa, lava, yai mbu
Chagua Jibu


16. Kitendo cha mmea kufuata mwanga katika kielelezo na 2 huitwa .........

Kielelezo Na. 2
  1. Kutembelea
  2. Kukua
  3. Kujongea
  4. Kuitikia kichocheo
  5. Kuhisi
Chagua Jibu


17, Chanzo cha chakula kwa wanyama ni .........

  1. Mmea
  2. Mimea na nyama
  3. Mimea kwa hebivora na nyama kwa canivora
  4. Maziwa 
  5. Maharage
Chagua Jibu


18. Vyombo vya kupikia Vina mikono iliyotengenezwa kwa mbao na plastiki kwa sababu ...m

  1. Haipitishi joto haraka
  2. Haipitishi joto
  3. Husharabu joto
  4. Huakisi joto 
  5. Hutunza joto kwa muda mrefu
Chagua Jibu


19. Kuta, sarafu na dari ya nymba ya utangazaji vimewekewa Vitu Iaini ili.

  1. Kupunguza sauti 
  2. kuakisi
  3. Kuongeza sauti na nguvu
  4. kufanya sauti kuwa Iaini na safi
  5. Kupunguza mwamgwi
Chagua Jibu


20. Kuna uhusiano gani kati ya sumaku na umeme.

  1. Zote ni nishati za kemikali
  2. Zote ni sakiti za umeme
  3. Kuliko na sumaku lazima kuwe na umeme
  4. Kuliko na umeme lazima kuwe na sumaku
  5. Zote zinatoa nishati ya mwanga
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256