STD VII MAARIFA_JAMII ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2022

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA 
 MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI

03 MAARIFA YA JAMII NA STADI ZA KAZI

Muda: Saa 1:30 Mwaka: 2022

Maelekezo

1. Karatasi hii ina sehemu A na zenye jumla ya maswali arobaini na tano (45).

2. Jibu maswali yote.

3. Soma maelekezo yote yaliyoko katika fomu maalumu ya kujibia (OMR).

4. Jaza taarifa zote katika fomu ya OMR.

5. Weka kivuli katika kila tarakimu ya Namba yako ya Mtihani kwenye nafasi husika katika fomu ya OMR.

6. Weka kivuli katika herufi ya jibu sahihi kwa swali la hadi 40 katika fomu yako ya kujibia uliyopewa. Kwa mfano, kama jibu sahihi ni A weka kivuli kama ifuatavyo:

7. Ukigundua kuwa herufi uliyowekea kivuli si jibu sahihi, futa kivuli hicho kwa umakini kwa
kutumia kifutio safi kabla ya kuweka kivuli katika herufi mpya.

8. Tumia penseli ya HB to katika kujibu swali la hadi 40 na kalamu ya wino wa bluu au mweusi kujibu swali la 41 hadi 45.

9. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi ndani ya chumba cha mtihani.

SEHEMU A (Alama 40) 
Jibu maswali yote katika sehemu hii.

Chagua jibu sahihi kisha weka kivuli kwenye herufi ya jibu lililo sahihi katika fomu maalum (OMR) uliyopewa.

1. Ubunifu ni kipengele muhimu katika ujasiriamali. Je, nini kitatokea endapo ubunifu utakosekana?

  1. Wajasiriamali kukosa motisha 
  2. Polisi kuingilia kati biashara
  3. Wajasiriamali kupoteza wateja 
  4. Wajasiriamali kuongeza wateja
  5. Serikali kutunga sheria
Chagua Jibu


2. Je, mjasiriamali ni mtu wa namna gani?

  1. Mwenye kukata tamaa upesi
  2. Mwenye kutegemea mawazo ya wengine 
  3. Mwenye matumaini ya kuwa tajiri kwa haraka
  4. Mwenye kukasirika haraka apatapo hasara
  5. Mwenye kutumia fursa vizuri
Chagua Jibu


3. Amani ni mjasiriamali ambaye ameajiri watu wanne kwenye biashara zake. Je, huo ni aina gani ya ujasiriamali?

  1. Kati 
  2. Mdogomdogo 
  3. Mdogo 
  4. Mkubwa 
  5. Makini
Chagua Jibu


4. Ardhi ni rasilimali ambayo isipotunzwa vizuri inaweza kusababisha hatari katika maisha ya viumbe hai na rasilimali nyingine. Ipi ni njia bora itakayotumika kutunza rasilimali hiyo? 

  1. Kuongeza idadi ya wakulima mashambani
  2. Kutoa elimu juu ya uhifadhi na utunzaji wa ardhi
  3. Wananchi kuhimizwa kutumia mbolea za viwandani
  4. Kuacha kupanda miti katika maeneo ya wazi
  5. Kuhimiza wafugaji kuongeza idadi ya mifugo
Chagua Jibu


5. Tanzania imebahatika kuwa na rasilimali nyingi, mojawapo imebeba nyinginezo katika mazingira. Rasilimali hiyo ni ipi?

  1. Madini 
  2. Misitu 
  3. Mifugo
  4. Mbuga za wanyama
  5. Ardhi
Chagua Jibu


6. Mwalimu Kasese aliwaambia wanafunzi wake wataje madini na mikoa yanapopatikana nchini Tanzania. Je, walitaja mkoa gani makaa ya mawe yanapatikana?

  1. Manyara 
  2. Mbeya 
  3. Kagera 
  4. Morogoro 
  5. Mara
Chagua Jibu


7. Wakati wa kipindi, mwalimu aliwataka wanafunzi wataje fursa za kibiashara zinazoweza kupatikana pembezoni mwa bahari ya Hindi. Lipi kati ya yafuatayo lingekuwa jibu lao? 

  1. Kutengeneza mikanda ya ngozi 
  2. Kuzalisha maziwa 
  3. Kuuza madawa ya mifugo
  4. Kuuza ngozi za wanyama 
  5. Utalii
Chagua Jibu


 8. Mwalimu Timamu alifundisha kuhusu kilimo cha mazao ya biashara kilichofanywa Tanganyika kabla ya uhuru. Je wanafunzi walifundishwa mazao yapi?

  1. Zabibu, kahawa, chai na maharage 
  2. Mahindi, kahawa, chai na pareto
  3. Kahawa, pareto, mkonge na chai 
  4. Pareto, korosho, chai na mahindi
  5. Korosho, maharage, mkonge na pareto
Chagua Jibu


 9. Inapendekezwa kuwa shughuli za kibinadamu ziwe rafiki kwa mazingira iii kuzuia kuharibika

kwa tabaka la ozoni. Ni shughuli ipi sahihi katika kulinda tabaka hilo?

A Kufuga mifugo mingi katika eneo dogo B Kuvua kwa kutumia baruti

C Uchimbaji wa madini D Upandaji wa miti

  1. Kutumia mbolea za viwandani kwa wingi
Chagua Jibu


10. Mwalimu alifundisha umuhimu wa tabaka la ozoni kwa maisha ya viumbe hai na vitu vinavyoathiri uimara wa tabaka la ozoni. Je mwalimu alitaja kitu gani kinachoathiri uimara wa tabaka la ozoni?

  1. Upepo 
  2. Hewa ya oksijeni 
  3. Radi
  4. Mvua 
  5. Gesi ya kloroflorokaboni
Chagua Jibu


11. Meli ya mizigo iliyoko mji wa Brasilia 450 Magharibi huanza safari siku ya Jumatatu saa 4:00 usiku. Muda huo utakuwa ni saa ngapi katika mji wa Kabul ulioko 75° Mashariki?

  1. Jumatatu 6:00 usiku 
  2. Jumanne 5:00 usiku 
  3. Jumanne 12:00 asubuhi
  4. Jumatatu 6:00 mchana 
  5. Jumanne 12:00 jinni
Chagua Jibu


12. Mwalimu Kulwa aliwafundisha wanafunzi wake kuhusu mistari ya kufikirika inayochorwa katika ramani. Je, ni mistari ipi aliwafundisha kuwa huchorwa kutoka upande wa Kaskazini kuelekea Kusini?

  1. Tropiki 
  2. Latitudo 
  3. Mstarihi 
  4. Longitudo 
  5. Ikweta
Chagua Jibu


13. Jasiri anayeishi katika mji wa Handani, alianza kuangalia mechi katika televisheni saa 9:00 alasiri na rafiki yake Juhudi anayeishi katika mji wa Mikoko uliopo longitudo 40° Mashariki, alianza kuangalia mechi hiyo saa 7:00 mchana. Je, mji wa Handani upo longitudo ngapi?

  1. 70° Magharibi
  2. 30° Magharibi
  3. 90° Mashariki
  4. 70° Mashariki
  5. 30° Mashariki
Chagua Jibu


14. Bara la Afrika lina mashujaa wengi ambao walipinga ukoloni mamboleo. Mashujaa gani wa Afrika Mashariki waliopinga ukoloni huo?

  1. Jomo Kenyatta, Patrice Lumumba na Samora Machel
  2. Julius K. Nyerere, Kwame Nkrumah na Nelson Mandela
  3. Jomo Kenyatta, Julius. K. Nyerere na Milton Obote
  4. Patrice Lumumba, Julius. K. Nyerere na Kwame Nkrumah
  5. Jomo Kenyatta, Kamuzu Banda na Samora Machel
Chagua Jibu


15. Tanzania imeongozwa na Mawaziri wakuu wengi tangu uhuru. Je, Mawaziri wapi walishika nyazifa wakati wa Mwalimu Nyerere?

  1. Rashid Mfaume Kawawa na Joseph Sinde Warioba
  2. Rashid Mfaume Kawawa na Edward Moringe Sokoine
  3. John Samweti Malecela na Mizengo Kayanza Pinda
  4. Edward Ngoyai Lowassa na Cleopa David Msuya
  5. Edward Moringe Sokoine na Fredrick Sumaye
Chagua Jibu


16. Ni kwa jinsi gani Uganda ilipata uhuru wake?

  1. Kupitia vita vya msituni 
  2. Kupitia mapinduzi
  3. Kupitia vita
  4. Kupitia njia ya Katiba 
  5. Kupitia ushirikiano
Chagua Jibu


17. Kiongozi yupi aliongoza mapambano ya kudai uhuru wa watu weusi nchini Afika ya Kusini?

  1. Julius Kambarage Nyerere
  2. De Clerk 
  3. Keneth Kaunda
  4. Nelson Mandela 
  5. Kwame Nkurumah
Chagua Jibu


18. Katika karne ya 19, Pwani ya Afrika Mashariki ilitembelewa na wageni wengi kutoka Sara la Asia. Nini lilikuwa lengo lao kuu?

  1. Shughuli za kijeshi
  2. Shughuli za kisiasa 
  3. Shughuli za kiutamaduni
  4. Shughuli za kiuchumi 
  5. Shughuli za kijamii
Chagua Jibu


19. Kwa nini Wareno walijenga ngome nyingi maeneo ya Pwani? 

  1. Kuwalinda Waafrika dhidi ya Waarabu
  2. Kulinda maslahi yao ya kibiashara
  3. Kuwalinda Waarabu wasivamiwe na Waafrika
  4. Kuonyesha nguvu zao za kijeshi kwa Waafrika
  5. Kuwafundisha Waafrika mbinu za kijeshi
Chagua Jibu


20. Fatuma ni binti wa kaka yangu, Casmir ni mtoto wa kiume wa dada wa baba yake Fatuma. Je, Fatuma atamwitaje Casmir?

  1. Binamu 
  2. Mpwa wa kiume 
  3. Mpwa wa kike 
  4. Mjomba 
  5. Kaka
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256