STD VII MAARIFA_JAMII ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2020

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA

MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI

03 MAARIFA YA JAMII

Muda: Saa 1:30 Mwaka: 2020

Maelekezo

l . Karatasi hii ina sehemu A na B zenye jumla ya maswali arobaini na tano (45).

2. Jibu maswali yote katika kila sehemu.

3. Soma maelekezo yote yaliyoko katika romu maalumu ya kujibia (OMR).

4. Jaza taarifa zote katika (omu ya OMR na katika ukurasa wenye swali la 41 hadi 45.

5. Weka kivuli katika kila tarakimu ya Namba yako ya Mtihani kwenye nafasi husika katika fomu ya OMR.

6. Weka kivuli katika herufi ya jibu sahihi ksva swali la I hadi 40 katika fomu yako ya kujibia uliyopewa. K?va mfano, kama jibu sahihi ni A weka kivuli kama ifuatavyo: 

7. Ukigundua kuwa herufi uliyoweka kivuli si jibu sahihi, futa kivuli hicho kwa umakini kwa kutumia kifutio safi kabla ya kuweka kivuli katika herufi mpya.

8. Tumia penseli ya HB tu katika kujibu swali la I hadi 40, na kalamu ya wino wa bluu au ?nweusi kujibu swali la 41 hadi 45.

9. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi ndani ya chumba cha mtihani.

SEHEMU A (Alama 40)

KIPENGELE 1: URAIA

Chagua jibu sahihi kisha weka kivuli kwenye herufi ya jibu lililo sahihi katika fomu maalum (OMR) ya kujibia uliyopewa.

1. Ni nani anahusika kumchagua mwenyekiti wa kjiji?

  1. Wananchi wote katika kijiji 
  2. Wajumbe wa kamati za kijiji
  3. Halmashauri ya kijiji 
  4. Baraza la madiwani
  5. Wakuu sva idara za serikali katika kijiji
Chagua Jibu


2. Lipi kati ya yafuatayo ni jukumu la Baraza la Madiwani katika Manispaa?

  1. Kukusanya kodi katika Manispaa husika 
  2. Kutunga sheria ndogondogo katika eneo lao 
  3. Kuajiri mkurugenzi mtendaji wa Manispaa 
  4. Kusimamia shughuli za uchaguzi wa mitaa
  5. Kuajiri wakuu wa idara katika Manispaa
Chagua Jibu


3. Ipi kati ya zifuatazo ni faida za mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini Tanzania'?kisiasa nchini 

  1.  Kuongezeka kwa ajira serikalini 
  2. Kutokuwepo kwa tofauti za
  3. Vyama vyote vya siasa kupokea ruzuku 
  4. Kuongezeka kwa uwajibikaji serikalini 
  5. Kuongezeka kwa wawekezaji toka nje
Chagua Jibu


4. Ni mwaka gani Umoja wa Mataifa (UN) ulipitisha Azimio D kuhusu Haki za Binadamu?

  1. 1964
  2. 1945
  3. 1948
  4. 1961
  5. 1984
Chagua Jibu


5. Kwa nini tarehe 7 Aprili ya kila mwaka inakumbukwa nchini Tanzania? 

  1. Ni siku ya kifo cha Rais wa kwanza wa Zanzibar Abeid Karume.
  2. Ni siku ya kifo cha Rais wa kwanza v,va Tanzania Julius K. Nyerere. 
  3. Ni siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
  4. Ni siku ya kuzaliwa TANU.
  5. Ni siku ya uhuru wa Zanzibar.
Chagua Jibu


6. Ni vyombo gani vya kitamaduni hutumika kupikia chakula?

  1. Chungu na ngao 
  2. Chungtl na mwiko 
  3. Ngao na kikapu 
  4. Kinu na chungu 
  5. Mtungi na kinu
Chagua Jibu


7. Yupi kati ya wafuatao huendesha vikao vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Spika na Naibu spika wanapokuwa hawapo Bungeni?

  1. Mwanasheria Mkuu wa Serikali 
  2. Wenyeviti wa Bunge
  3. Waziri Mkuu 
  4. Katibu wa Bunge
  5. Wenyeviti wa Kamati za Bunge
Chagua Jibu


8. Ipi kati ya zifuatazo ni faida ya kiuchumi ya kuwekeza katika elimu ya rasilimali watu Tanzania'?

  1. Ufanisi katika kusimamia rasilimali za taifa. 
  2. Uwepo wa sekta iliyo rasmi tu.
  3. Watu wote kupata kipato sawa. 
  4. Kutoweka kwa utandawazi. 
  5. Kupungua kwa bidhaa kutoka nchi za nje.
Chagua Jibu


9. Upi kati ya ujumbe ufuatao hutolewa kwa madereva na watumiaji wengine wa barabara kwa kutumia rangi nyekundu katika taa za barabani'?

  1. Ongeza mwendo 
  2. Punguza mwendo 
  3. Simama
  4. Kuna hatari mbele 
  5. Kuna reli inapita mbele
Chagua Jibu


10. Makao Makuu ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) yapo katika mji gani?

  1. Pretoria. 
  2. Lusaka. 
  3. Harare. 
  4. Maputo. 
  5. Gaboroni.
Chagua Jibu


ll . Yupi kati ya wanyama watUatao anaweza kulinda maisha na mali zetu?

  1. Farasi 
  2. Punda 
  3. Ngamia
  4. Palea 
  5. Mbwa
Chagua Jibu


12. Ni kwa namna gani Tanzania inaweza kunufaika na utandawazi'?

  1. Kuwa na uwezo •wa kupanga bei za bidhaa zake katika soko la kimataifa.
  2. Kupata fursa ya kuwekeza katika nchi tajiri duniani.
  3. Kuwa na uwezo wa kuwa na kura ya turufu katika Umoja wa Mataifa.
  4. Kupata fursa ya kutangaza vivutio vyake vya utalii.
  5. Vijana wengi kupata fursa za ajira katika nchi tajiri.
Chagua Jibu


KIPENGELE 11: HISTORIA

Chagua jibu sahihi kisha weka kivuli kwenye herufi ya jibu lililo sahihi katika fomu maalum (OMR) ya kujibia uliyopewa.

13. Ni nani aliyegundua moto katika Zama za Kati za Mawe'?

  1. Primeti 
  2. Homo Habilisi 
  3. Homo Erectus 
  4. Australopithikasi 
  5. Homo Sapiensi
Chagua Jibu


14. Vipi vilikuwa vyama maarufu vya siasa vilivyopigania uhuru "'a Zimbabwe'?

  1. KANU na UNIP 
  2. UNITA na ZANU 
  3. ZANU na MPLA
  4. ZNP ZANU 
  5. ZAPU na ZANU
Chagua Jibu


15. Ni jamii ipi ilipinga uvamizi wa Kiingereza kwa njia ya vita katika Afrika ya Kati?

  1. Wamatumbi 
  2. Wamandika 
  3. Wakhoisa
  4. Wandehele 
  5. Waasante
Chagua Jibu


16. Ni taifa gani la Ulaya lililosaini makubaliano ya Buganda yaliyompa Kabaka madaraka ya kisiasa mwaka 1900?

  1. Ubelgiji 
  2. Marekani 
  3. Ujerumani 
  4. Ufaransa 
  5. Uingereza
Chagua Jibu


17. Ni nchi gani mfumo wa kulisha kasumba ulianzishwa kwa mara ya kwanza?

  1. Naijeria 
  2. Msumbiji 
  3. Uganda
  4. Angola 
  5. Senegali
Chagua Jibu


18. Ni karne ya ngapi mataifa ya Ulaya yalilivamia Bara la Afrika?

  1. Karne ya 15 
  2. Karne ya 20 
  3. Karne ya 18 
  4. Karne ya 9 
  5. Karne ya 19
Chagua Jibu


19. Nani alikuwa binadamu wa kwanza kutcngeneza zana na ambaye alikuwa na ubongo mkubwa kuliko wa Zinjanthropasi?

  1. Homo Erectus
  2. Homo Sapiensi
  3. Homo Habilisi
  4. Australopithikasi
  5. Primeti
Chagua Jibu


20. Ni katika zama gani mwanadamu alianza kuzalisha chakula zaidi?

  1. Zama za Mwisho za Mawe
  2. Zama za Mwanzo za Mawe
  3. Zama za Kati za Mawe 
  4. Zama za Kale za Mawe 
  5. Miaka milioni 30 kabla ya Kristo
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256