MAARIFA YA JAMII - 2018
SEHEMU A
URAIA
Chagua jibu sahihi kisha weka kivuli kwenye herufi ya jibuhullosahihi katika fornu maaLkujibia.
1. Mtu anayedhibiti mwenendo wa wanafunzi shuleni ni..
- Mwenyekiti wa kamati ya shule
- Mwalimu wa nidhamu
- Mwalimu mkuu msaidizi
- Mwalimu wa taaluma
- Mwalimu wa somo
Chagua Jibu
2. Chombo cha juu katika maamuzi kwenye serikali ya kijiji ni ..................
- Serikali ya kijiji
- Kamati ya ulinzi na usalama
- Mkutano mkuu wa kijiji
- Afisa Mtendaji wa kijiji
- Kamati ya Maendeleo ya kijiji
Chagua Jibu
3. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya huchaguliwa na...................
- Mkurugenzi mtendaji wa wilaya
- Baraza la madiwani
- Waziri katika ofisi ya Rais
- Afisa Mtendaji wa Kata
- Wenyeviti wa vijiji
Chagua Jibu
4. Ipi kati ya sarafu zifuatazo ina picha ya Rais wa kwanza wa Zanzibar?.................
- Sarafu ya shilingi mia moja
- Sarafu ya shilingi mia mbili
- Sarafu ya shilingi hamsini
- Sarafu ya silingi ishirini
- Sarafu ya shilingi kumi
Chagua Jibu
5. Maliasili zinazovutia watalii na kuchangia katika kukuza uchumi wa Tanzania ni..................
- ardhi
- mito
- mifugo
- madini
- mbuga za wanyama
Chagua Jibu
6. Wajibu wa serikali katika kujenga maadili ya viongozi ni....................
- Kuwakopesha magari viongozi wote
- Kuimarisha mfumo wa chama kimoja cha siasa
- Kusimamia sheria za utumishi wa umma
- Kuhamisha watumishi wasio waadilifu
- Kuajiri watumishi wenye elimu ya juu to
Chagua Jibu
7.Tofauti kati ya mila na desturi ni....
- Mila hubadilika mara kwa mara kuliko desturi
- Desturi hubadilika mara kwa mara kuliko mila
- Mila ni mazoea wakati desturi ni vitendo
- Mila ni mazoea na huweza kubadilika na kuwa desturi
- Desturi hubadilika mara kwa mara kuliko mazoea
Chagua Jibu
8. Matumizi ya ofisi ya umma kwa manufaa binafsi huitwa.................
- takrima
- rushwa
- uzalendo
- ubinafsi
- ujasiriamali
Chagua Jibu
9. Zipi kati ya nchi zifuatazo ni wanachama wa Jumuiya ya Madola?................
- Botswana na Burundi
- Botswana na Zambia
- Kenya na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
- Malawi na Burundi
- Zambia na Jamhuri ya Kidemkrasia ya Kongo
Chagua Jibu
10. Moja ya matukio yanayokiuka Haki za Binadamu nchini Tanzania ni.............
- Mauaji ya vikongwe na maalbino
- Ukataji na upandaji mid
- kuwafungulia mashtaka wahalifu
- kufukuzwa kazi viongozi wasio waadilifu
- Serikali kusimamia ukusanyaji kodi
Chagua Jibu
11. Mojawapo ya njia ambazo wananchi wanaweza kushiriki katika ulinzi na usalama ni...............
- kupiga wahalifu
- kufanya mazoezi ya viungo
- kuwaua wahalifu
- kuwafichua wahalifu
- kuwa rafiki na wahalifu
Chagua Jibu
12.Viashiria vya utandawazi ni pamoja na...............
- kupungua kwa tofauti ya kipato
- uchumi wa soko huria
- kupungua kwa umaskini
- kuwepo kwa ushindani wa kutengeneza silaha
- kuwepo kwa bidhaa nyingi toka viwanda vya ndani
Chagua Jibu
SEHEMU B
HISTORIA
:hagua jibu sahihi kisha weka kivuli kwenye herufi ya jibu h u b sahihi katika karatasi ya kujibia.
13. Baba wa baba yako anaitwa
- baba
- mjukuu
- mjomba
- babu
- mpwa
Chagua Jibu
14.Ni Taifa lipi la kibepari liliitawala Tanganyika kuanzia mwaka 1891 hadi 1918?
- Ujerumani
- Uingereza
- China
- Ureno
- Ufaransa
Chagua Jibu
15. Kwa nini Berlin ni miongoni mwa miji maarufu katika historia?
- Ni Makao Makuu wa Umoja wa Mataifa
- Ni Makao Makuu wa Jumuiya ya Madola
- Ni mji uliokuwa kitovu cha biashara ya utumwa
- Ni mji wa Ufaransa ambao uliendesha utawala wa kulisha kasumba
- Ni mji ambao mgawanyo wa Bara la Afrika ulifanyika
Chagua Jibu
16.Mataifa makubwa ya kibepari yaliyogombania Bara la Afrika yalikuwa
- Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Ubelgiji, Italia na Ureno
- Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Uchina, Uhispania na Marekani
- Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Japani, Uhispania na Ubelgiji
- Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Urusi, Uchina na Japani
- Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Ubelgiji, Italia na Uchina
Chagua Jibu
17. Mwanzilishi wa Kampuni wa Kibiashara ya Kiingereza ya Afrika Mashariki anaitwa
- David Livingstone
- Karl Peters
- Mungo Park
- William Mackinnon
- Seyyid Said
Chagua Jibu
18. Julius Von Soden alikuwa nani?................
- Gavana wa kwanza wa kiingereza katika Tanganyika
- Gavana wa kwanza wa kijerumani katika Tanganyika
- Gavana wa mwisho wa kijerumani katika Tanganyika
- Gavana wa mwisho wa Kiingereza katika Tanganyika
- Gavana aliyeanzisha utawala wa moja kwa moja katika Tanganyika
Chagua Jibu
19. Mtaalamu wa mambo wa kale aliyevumbua fuvu la binadamu wa kwanza Olduvai aliitwa
- Charles Darwin
- Zinjathropus
- Homo Habilis
- David Livingstone
- Louis Leakey
Chagua Jibu
20. Ni lini binadamu alianza kuchoma misitu iii kuwafukuza wanyama wakali?.................
- Wakati wa Zama za Chuma
- Wakati wa Zama za Mwanzo za Mawe
- Wakati wa Zama za Kale za Mawe
- Wakati wa Zama za Mwisho za Mawe
- Wakati wa Zama za Kati za Mawe
Chagua Jibu
21. Ni katika mfumo upi wa kiuchumi ambamo njia kuu za uzalishaji maliwanajamii wote?
- Utumwa
- Ukabaila
- Ubepari
- Ujima
- UjarnEd.
Chagua Jibu
22. Kama Juma na Hawa ni watoto wa Masanja Muntete, je, Hawa anamwitaje Juma?..........
- Binamu
- Mjomba
- Shemeji
- Mpwa
- Kaka
Chagua Jibu
23. Binti wa shangazi yako huitwa................
- Mpwa
- Binamu
- Mama mkwe
- Shemeji
- Dada
Chagua Jibu
24. Kwa nini vita vya Maji Maji vilitokea?..............
- Wareno waliwapeleka Watanganyika utumwani.
- Kinjekitile alikasirisha na uhasama wa Wajerumani na Waarabu.
- Watanganyika walipigwa mijeledi na Waingereza.
- Wajerumani waliwalazimisha watu kufanya kazi katika mashamba ya pamba.
- Sultani Seyyid Said aliwatesa na kuwatumikisha Waafrika.
Chagua Jibu
25. Rais Julius Kambarage Nyerere na Kwame Nkurumah walikuwa
- waanzilishi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
- waanzilishi wa Umoja wa Mataifa.
- waanzilishi wa Jumuiya ya Mataifa.
- waanzilishi wa Umoja wa Nchi Huru za Kiafrika.
- waanzilishi wa Jumuia ya Madola.
Chagua Jibu
26. Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia elimu na utamaduni linaitwa
- WHO
- UNICEF
- UNESCO
- UNHCR
- UNDP
Chagua Jibu
SEHEMU C
)10GRAFIA
Thagua jibu sahihi kisha weka kivuli kwenye herufi ya jibu sahihi katika fomu ya kujibia
27. Wakati wa mvua kubwa inayoambatana na radi, watu hawaruhusiwi
- kuvaa nguo nyekundu.......
- kutumia miavuli
- kufungua milango na madirisha
- kujificha chini ya mti
- kufunga luninga na redio
Chagua Jibu
28. Janga la kimazingira linalosababishwa na nguvu za asili pekee linaitwa
- Ukame
- Tetemeko la ardhi
- Mmomonyoko wa udongo
- Njaa
- Uchafuzi wa mazingira
Chagua Jibu
29. Uchafuzi wa maji unaweza kuepukwa kwa...............
- utupaji hovyo taka za kemikali
- utupaji sahihi wa majitaka
- matumizi ya mbolea ya chumvichumvi
- kuvua samaki kwa kutumia sumu
- kuosha magari katika mita
Chagua Jibu
30. Upi ni mlingano sahihi wa viumbe hai?.................
- swala —> simba --> nyasi
- ngombe —> swala —> nyasi
- nyasi —>simba —>swala
- swala —>nyasi —> simba
- simba —>swala —> nyasi
Chagua Jibu
31. Zifuatazo ni njia bora za kutunza mazingira isipokuwa................
- kudhibiti uchafuzi wa hewa
- kilimo cha kuhamahama
- kudhibiti takataka za viwandani
- kupanda miti
- kutunza vyanzo vya mail
Chagua Jibu
32. Kipi kati ya vipimo vya ramani vifuatavyo kinawakilisha eneo dogo?................
- 1:50
- 1:500,000
- 1:50,000
- 1:5,000
- 1:500
Chagua Jibu
33. Milima mikunjo hutokea katika maeneo yenye...............
- miamba tabaka
- miamba ya volkano na moto
- miamba geu
- miamba mato
- miamba volcano
Chagua Jibu
34. Angahewa lina sehemu kuu ngapi?................
- Nne
- Nane
- Mbili
- Tatu
- Tano
Chagua Jibu
35. Vifuatavyo ni vipengele vinavyounda hall ya hewa isipokuwa................
- mvua
- unyevu
- upepo
- mwanga wa jua
- udongo
Chagua Jibu
36. Ipi ni athari ya ongezeko kubwa la watu?.................
- Kupungua kwa uhalifu
- Ongezeko la ajira
- Kupungua kwa maji
- Kupungua kwa biashara ndogondogo
- Kutotosheleza kwa huduma za jamii
Chagua Jibu
37. Tatizo kubwa linalowakabili wakulima wengi wa Afrika Mashariki ni pamoja na................
- uwepo wa mvua nyingi mwaka mzima •
- mvua zisizoaminika
- uwepo wa masoko ya uhakika
- uhaba wa maeneo ya kulima
- matumizi ya mbolea za chumvi
Chagua Jibu
38. Shughuli inayohusisha kununua, kuuza au kubadilisha na bidhaa huitwa..................
- uwekezaji
- ujasiriamali
- biashara
- mitaji
- utajiri
Chagua Jibu
39. Biashara ya kimataifa inahusisha...............
- uingizaji na usafirishaji wa bidhaa nje ya nchi
- uingizaji bidhaa kutoka nje ya nchi tu
- usafirishaji bidhaa kwenda nje ya nchi tu
- kufanya biashara kwa kutumia pesa
- kukopa fedha kutoka nje ya nchi
Chagua Jibu
40. Ni mikoa ipi inahusika na usafirishaji kupitia bahari ya Hindi?..................
- Mwanza, Pemba, Zanzibar na Mtwara
- Tanga, Mtwara, Kigoma na Pwani
- Zanzibar, Pemba, Mwanza na Kigoma
- Kilimanjaro, Kigoma, Tanga, na Zanzibar
- Dar es Salaam, Tanga, Mtwara na Zanzibar
Chagua Jibu
Try Another Test |