STD VII MAARIFA_JAMII ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2014

2014 - MAARIFA YA JAMII

SEHEMU A

URAIA

Chagua jibu lililo sahihi kisha andika herufi yake mkabala na namba ya swali kwenye karatasi ya kujibia.

1.  Kazi ya kamati ya shule ni:

  1. Kusimamia maendeleo ya taaluma
  2. Kutoa ushauri juu ya maambukizi ya UKIMWI
  3. Kuidhinisha uteuzi wa waalimu 
  4. Kusimamia nidhamu ya waalimu
  5. Kusimamia ujenzi na maendeleo ya shule.
Chagua Jibu


2.  Vyanzo vya mapato ya serikali za mitaani pamoja na:

  1. kodi ya kichwa na kodi ya rasilimali
  2. ruzuku, kodi na michango mingine
  3. kodi ya ardhi, na kodi ya rasilimali
  4. tozo katika mazao ya mali asili 
  5. tozo za leseni za biashara
Chagua Jibu


3.  Katika muundo wa kiutawala wa serikali za mitaa, wilaya na manispaa zinaongozwa na:

  1. Chama tawala    
  2. Mkurugenzi mtendaji
  3. Mkuu wa wilaya   
  4. Kamati yenyewe 
  5. Afisa utawala wa wilaya
Chagua Jibu


4.  Rangi nyeusi katika bendera yetu huwakilisha:

  1.  Mimea      
  2.  Madini
  3.  Watu   
  4.  Ardhi 
  5.  Mbuga za wanyama
Chagua Jibu


5.  Ngaoya taifa inawakilisha:

  1. umoja, uhuru, uwezo na mamlaka ya taifa
  2. uhuru, umoja na rasilimali za taifa
  3. uwezo, uhuru, uoto wa asili na mamlaka ya taifa
  4. uhuru, umoja na mamlaka ya taifa 
  5. uhuru na umoja
Chagua Jibu


6.  Sababu kubwa ya kuruhusu mfumo wa vyama vingi Tanzania ni:

  1.  kutekeleza matakwa ya wahisani
  2.  kulinda haki za makundi maalumu katika jamii
  3.  kuvutia wawekezaji wa nje
  4.  kutekeleza maelekezo ya Umoja wa Mataifa
  5.  kupanua demokrasia
Chagua Jibu


7.  Chombo chenye mamlaka ya kusimamia uchaguzi wa rais, wabunge na madiwani Tanzania ni:

  1.  Jeshi la polisi 
  2. Tume ya Taifa ya Uchaguzi
  3. Mahakama Kuu 
  4. Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa
  5. Ofisi ya Waziri Mkuu
Chagua Jibu


8.  Haki ya kumiliki mali iko katika kipengele kipi cha haki za binadamu?

  1.  Kijamii na kiuchumi   
  2.  Kisiasa na kiuchumi
  3.  Kikatiba na kisiasa               
  4.  Kijamii na Kisiasa 
  5.  Kijamii na Kiutamaduni
Chagua Jibu


9.  Ulinzi na usalama wa taifa letu ni jukumu la:

  1.  Jeshi Wananchi wa Tanzania 
  2.  kitengo cha Usalama wa Taifa
  3.  Jeshi la Polisi
  4.  mgambo
  5.  kila mwananchi
Chagua Jibu


10.Mojawapo ya kazi za mgamboni:

  1.  kukamata wahalifu na kuwapeleka kwenye kituo cha polisi
  2.  kuadhibu wanaovunja sheria mijini
  3.  kuzuia ajali za moto
  4. kukusanya kodi ya maendeleo mijini 
  5. kuzuia na kupambana na rushwa
Chagua Jibu


11. Utandawazi ni mfumo unao hamasisha:

  1. teknolojia ya habari na mawasiliano katika nchi zinazoendelea
  2. haki sawa kwa kila mmoja duniani
  3. mfumo wa vyama vingi katika nchi zinazoendelea
  4. biashara huria baina ya mataifa
  5. sekta binafsi katika nchi zinazoendelea .    
Chagua Jibu


12.Nini maana ya ujasiriamali?

  1.  Bishara yoyote yenye faida
  2.  Uwekezaji kwenye biashara
  3.  Biashara ndogondogo
  4.   Sekta binafsi
  5.  Ujasiri wa kumiliki mali
Chagua Jibu


13.Mojawapo ya udhaifu wa Umoja wa Mataifa ni:

  1.  kushindwa kuzuia kuenea kwa Utandawazi
  2.  Waafrika hawajawahi kupata nafasi katika uongozi wa juu katika Umoja wa Mataifa
  3.  baadhi ya watu tu ndio wenye kura ya turufu
  4.  kushindwa kupitisha maazimio ya haki za binadamu
  5.  kutokushirikishwa kwa Waafrika katika vikao vya baraza la usalama
Chagua Jibu


14.Jaji Mkuu waTanzania huteuliwa na:

  1.  Bunge 
  2.  Waziri Mkuu        
  3.  Rais
  4.  Makamu wa rais     
  5.  Mwanasheria Mkuu
Chagua Jibu


SEHEMU B

HISTORIA

15. Wafanyabiashara kutoka bara la Asia walifika Tanganyika kwa mara ya kwanza mnamo

  1.  Karne ya 15 
  2.  Karne ya 19 
  3.  Karne ya 8 
  4.  Karne ya 9 
  5.  Karne ya 12
Chagua Jibu


16. Kabla ya ukoloni majukumu ya kiongozi wa ukoo yalikuwa ni pamoja na:

  1.   kutatua migogoro   
  2.  kusaini mikataba na wakoloni
  3.  kuongeza idadi ya mifugo 
  4.  kujenga nyumba 
  5.  kuanzisha vijiji vya ujamaa
Chagua Jibu


17. Mkutano wa kuligawa bara la Afrika ulifanyika:

  1. Berlin
  2. London
  3. Roma
  4. Paris
  5. New York
Chagua Jibu


18. Azimio la Arusha lililenga zaidi:

  1. uhuru na kazi 
  2. siasa na kilimo
  3. elimu kwa wo?e
  4. ujamaa na kujitegemea
  5.  mfumo wa vyama vingi
Chagua Jibu


19. Katika zama za mawe za mwisho ugawanyaji majukumu katika jamii ulifanyika kwa misingi ya:

  1. hekima na utajiri
  2. hekima na umri
  3. uzoefu na hekima 
  4. umri na jinsia 
  5. utajiri na umri
Chagua Jibu


20.Mwanadamu alianza kutembea kwa miguu miwili katika hatua gani ya mabadiliko?

  1.  Primate 
  2.  Homo sapiens
  3.  Homo habilis 
  4.  Zinjanthropus 
  5.  Homo erectus
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256