MAARIFA YA JAMII 2010
URAIA, JOGRAFIA NA HISTORIA
SEHEMU A
Chagu jibe hullo sahihi kisha andika herufi inayohusika mbele ya kilo swali katika karatasi ya kujibia uhyopewa.
1. Ukoo ni muungano wa:
- familia zinazokaa karibu
- familia nyingi zenye asili moja
- familia nyingi zilizo rafiki
- baba, mama na watoto.
- familia zilizoungana kufanya kazi pamoja.
Chagua Jibu
2. Utamaduni maana yake ni
- imani, desturi, mila na miiko ya jamii ya watu
- kuimba na kucheza kwa pamoja
- namna ya kufanya matambiko katika jamii
- desturi na mila za jamii Fulani
- utaratibu wa kuishi
Chagua Jibu
3. Kiongozi wa serikali ngazi ya kata ni
- Diwani
- Afisa mtendaji wa kata
- Mwenyekiti wa kata
- Katibu kata
- Afisa mifugo wa kata
Chagua Jibu
4. Ili Afrika ijitegemee kiuchumi inahitaji
- misaada toka nje
- Ongezeko kubwa la watu
- sayansi na teknolojia
- mikopo ya masharti nafuu
- wawekezaji wa kiafrika.
Chagua Jibu
5. Lengo kuu la kuanzishwa kwa Jumuiya ya Madola lilikuwa
- kupata makoloni zaidi barani Afrika
- kuimarisha uhusiano baina ya Uingereza na nchi ilizozitawala
- kuoongeza kiasi cha malighafi zilizokuwa zinahitajiwa na wazungu.
- kuwaachia watumwa ambao bado walikuwa hawajawa huru
- kumfanya malkia wa Uingereza aogopwe na ulimwengu mzima.
Chagua Jibu
6. Mahakama inayotoa hukumu ya kesi za mauaji ni
- Mahakama ya mwanzo
- Mahakama ya wilaya
- Mahakama kuu
- Mahakama ya hakimu mkazi
- Mahakama ya Rufaa
Chagua Jibu
7. Nchi zinazopakana na Tanzania upande wa kusini ni
- Msumbiji na Malawi
- Msumbiji na Zimbabwe
- Jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo na Malawi
- Burundi na Malawi
- Rwanda na Malawi
Chagua Jibu
8. Nini tofauti kati ya nyota na sayari?
- Nyota humweka wakati sayari hazimweki
- Nyota zinatoa mwanga mweupe, wakati sayari hutoa mwanga wa rangi ya njano.
- Sayari huonekana mchana lakini nyota huonekana usiku tu.
- Nyota hazina mwanga wakati sayari zina mwanga
- Sayari zote zina viumbe hai wakati nyota hazina viumbe hai
Chagua Jibu
9. Bonde la ufa limegawanyika sehemu ya Mashariki na Magharibi katika nchi gani?
- Kenya
- Uganda
- Tanzania
- Burundi
- Ethiopia
Chagua Jibu
10. Vifuatavyo vilikuwa ni vyama vya ukombozi kusini mwa Afrika isipokuwa
- ANC
- PAC
- SWAPO
- KANU
- UNITA
Chagua Jibu
11. Mkusanyiko wa shughuli zinazohusisha wafanyabiashara na walaji au watumiaji huitwa
- Soko
- duka
- Bidhaa
- mteja
- fedha
Chagua Jibu
12. Bara la pili kwa ukubwa ulimwenguni ni
- Asia
- Afrika
- Australia
- Amerika ya Kaskazini
- Amerika ya kusini
Chagua Jibu
13. Rais wa kwanza wa Bunge la Umoja wa Afrika lililoanzishwa Machi 2004 ni
- Dr. Salim Salim
- Dr. Emek Anyauko
- Mh. Getrude Mongela
- William Erek
- Peter Omu
Chagua Jibu
14. Mtanzania anaruhusiwa kupiga kura katika uchaguzi mkuu anapofikia umri wa miaka
- 15
- 25
- 40
- 21
- 18
Chagua Jibu
15. Hapo awali mabara yote yalikuwa yameshikana na kuwa bara moja lililojulikana kama
- Andes
- Pangaea
- Australia
- Eurasia
- Antaktika
Chagua Jibu
16. Tabaka la ozone huweza kuharibiwa na
- kuongezeka kwa gesi ya oksijeni
- Kuongezeka kwa gesi ya haidrojeni kwenye anga
- moshi wenye kemikali unaotoka viwandani na kwenye magari
- kupungua kwa gesi ya kaboni daioksaidi kwenye anga
- vumbi linalosambaa angani kutokana na shughuli za uchimbaji wa madini
Chagua Jibu
17. Rhoda anachemsha maji ya kunywa kila siku kwa sababu maji yaliyochemshwa
- ni safi na salama
- yana ladha nzuri
- hukata kiu haraka
- huua wadudu walioko katika matumbo yetu
- huwa na virutubisho vingi
Chagua Jibu
18. Lengo mojawapo la michezo shuleni ni
- kutumia viwanja vya shule vizuri
- kuleta umoja na ushirikiano
- kuwapa zawadi washiriki
- kutambua shule zisizo na viwanja vya michezo
- kupata wachezaji wa kulipwa
Chagua Jibu
19. Serikali za mitaa zina aina ......za Halmashauri
- moja
- nne
- tano
- tatu
- sita
Chagua Jibu
20. Idadi kubwa ya wakimbizi katika bara la Afrika inasababishwa na
- umaskini katika nchi nyingi za Afrika
- migogoro ya kifamilia
- miundo mbinu duni
- upungufu wa ajira
- machafuko ya kisiasa
Chagua Jibu
21. Vituo vikuu vya misafara ya watumwa Tanganyika vilikuwa
- Ujiji, Kilwa na Tanga
- Tabora, Mpwapwa na Tanga
- Tabora, Ujiji na Bagamoyo
- Pangani, Mpwapwa na Dodoma
- Kilwa, Bagamoyo na Dodoma
Chagua Jibu
22. Vyama vingi vya kisiasa nchini Tanzania viliruhusiwa kisheria kwa mara ya pili mnamo mwaka .........
- 1995
- 2000
- 1992
- 1990
- 1964
Chagua Jibu
23. Tanzania ipo kusini mwa
- lkweta
- Tropiki ya kaprikoni
- Greenwich
- Ncha ya kaskazini
- Muhimili wa dunia
Chagua Jibu
24. Ikiwa kwenye longitude 0° ni saa 4 asubuhi, je itakuwa saa ngapi Afrika Mashariki nyuz: 45° Mashariki?
- saa 6 mchana.
- saa 12 jioni
- saa 4 usiku
- saa 7 mchana
- saa 2 asubuhi
Chagua Jibu
25. Yafuatayo ni mambo yalisababishwa na uharibifu wa uoto isipokuwa:
- Kimbunga na tufani
- upungufu wa maji na nusu jangwa
- mmomonyoko wa udongo na kupotea kwa viumbe hai
- njaa na mifugo mingi ku fa
- Uchimbaji madini na utengenezaji barabara
Chagua Jibu
26. Miinuko ya mlima Mlanje nchini Malawi ni maarufu kwa kilimo cha
- pamba
- Kahawa
- katani
- chai
- pareto
Chagua Jibu
27. Nini maana ya biashara ya rejareja?
- Kuuza bidhaa kidogo kidogo
- Kingiza bidhaa za kutoka nje
- Kuuza bidha ya aina moja tu.
- Kuuza bidhaa bila kuwa mwangalifu.
- Kuuza bidha za vitu vinavyotumika majumbani
Chagua Jibu
28. Bahari ya Shamu na bahari ya Mediterranean zimeunganishwa na
- mfereji wa Suez
- mfereji wa panama
- Mto wa Nile
- Mlango bahari wa Gibraltar
- milima ya Atlas
Chagua Jibu
29. Zifuatazo ni sababu za kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa (UNO) isipokuwa:
- kuepusha vita kuu ya Dunia
- kudumisha amani na usalama
- kukuza na kuendeleza uchumi
- kutatua migogoro sehemu mbalimbali
- kutoa upendeleo kwa mataifa makubwa
Chagua Jibu
30. Sera ambazo hutuongoza katika kutekeleza mambo ya maendeleo ya uma hutokana na
- Chama tawala
- Vyama vya upinzani
- baraza la mawaziri
- Vyombo vya dola
- kamati za serikali
Chagua Jibu
31. Ukanda wa kitropiki hupatikana kati ya latitude
- 0° - 5° kaskazini na kusini ya Ikweta
- 0°- 15° kaskazini na kusini ya Ikweta
- 0° - 30° kaskazini na kusini ya lkweta
- 35° - 65° kaskazini na kusini ya lkweta
- 30° - 60° kaskazini na kusini ya lkweta
Chagua Jibu
32. Kwanini mito mingi ya Afrika haitumiki kwa usafirishaji
- Ina maporomoko
- Ina magugu mengi
- Ina mamba wengi
- Haina bandari kubwa
- Mingi ni mifupi
Chagua Jibu
33. Mtu akiugua UKIMWI ni muhimu
- kumtengea chumba
- kumtengea chombo cha chakula
- kumpa upendo na huduma
- kumkabidhi kwa wazee
- Kutocheza nae
Chagua Jibu
34. Aina kuu madawa ya kulevya ni pamoja
- Bangi, kokeini na heroini
- Gongo, Kokeini na bangi
- Tumbaku, bangi na mihadarati
- Sigara, valiamna gongo
- Bangi, Sigara na gongo
Chagua Jibu
35. Mahali penye genge huoneshwa namna gani kwa mistari ya kontua kwenye ramani?
- Kwa alama ya U au V
- Kukaribiana kwa mistari ya kontua
- Kutengana kwa misitari ya kontua
- Mistari ya kontua huonekana kama imekutana
- Mistari ya kontua iliyonyooka
Chagua Jibu
36. Zao kuu la biashara linalolimwa wilaya ya mbinga mkoani Ruvuma ni
- Korosho
- Karafuu
- Chai
- Kahawa
- Pamba
Chagua Jibu
37. Nani huwateua Mawaziri na Manaibu mawaziri katika serikali ya Tanzania
- Spika wa bunge
- Rais
- Katibu wa bunge
- Makamu wa Rais
- Waziri Mkuu.
Chagua Jibu
38. Sababu kubwa zinazochangia idadi ya vifo barani Africa ni pamoja na
- maisha ya starehe na michezo ya hatari
- njaa, maradhi na milipuko ya vita
- ukeketaji na mimba za utotoni
- mila potofu na makazi yasiyo na uhakika
- Rushwa, udikteta na ukuaji wa miti.
Chagua Jibu
39. Yapi ni madhara ya ukataji wa miti katika maeneo jirani na ziwa Victoria?
- kupunguza idadi ya samaki
- kuharibu vyanzo vya maji vinavyoleta maji ziwani
- Kuongeza mafuriko katika ziwa Victoria
- kuongezeka kwa maji ya mto Nile unaoanzia ziwa Victoria
- kuongezeka kwa wanyama wakali maeneo ya jirani na ziwa
Chagua Jibu
40. Moja ya matatizo yanayovikabili viwanda na biashara Tanzania ni
- uhaba wa wateja wa bidhaa zinazozalishwa
- upungufu wa gharama kubwa ya nishati
- uhaba wa wafanyabiashara
- hall mbaya ya hewa
- uhaba wa wafanyakazi.
Chagua Jibu
41. Kwanini usafirishaji wa malighafi na bidhaa za viwanda hutumia zaidi njia ya maji?
- Ni njia ya haraka ya usafirishaji wa bidhaa
- Gharama nafuu na husafirisha mizigo mingi
- Sehemu kubwa ya dunia imezungukwa na maji
- Ni njia salama zaidi kuliko nyingine
- lnapunguza uchafuzi wa mazingira
Chagua Jibu
42. Ardhi, misitu, mito, bahari na madini kwa ujumla tunaviita
- bidhaa muhimu
- Dunia
- uoto wa asili
- maliasili
- mahitaji muhimu
Chagua Jibu
43. Ipi kati ya zifuatazo sio miongoni mwa sababu za uchafuzi wa mazingira?
- Teknolojia duni
- Kuwepo kwa watu wengi
- Kutokuwa na Elimu
- Kutumia mbolea za asili zaidi katika kilimo
- Utaratibu mbaya wa kutupa takataka
Chagua Jibu
44. Nchi zilizopo Mashariki mwa Afrika ni
- Zambia, Malawi, Tanzania na Kenya
- Sudan, Zambia, Tanzania na Uganda
- Rwanda, Burundi, Tanzania na Malawi
- Kenya, Tanzania, Uganda na Malawi
- Kenya, Uganda, Tanzania na Somalia
Chagua Jibu
45. Zama za mawe zimegawanyika katika sehemu ngapi?
- Tatu
- Mbili
- Nne
- Tana
- Moja
Chagua Jibu
SEHEMU B
Soma kwa makini ramani ifuatayo (Kielelezo Namba 1) kisha jibu maswali 46 - 50 kwa kuandika en o moja to katika karatasi ya kujibia.

46. Hifadhi ya Taifa inayooneshwa kwa herufi A inaitwa........
Chagua Jibu
47. Taja aina ya madini yanayopatikana katika eneo lililooneshwa kwa herufi B . . . . . . . . .
Chagua Jibu
48. Zao gani la biashara linastawi kwenye mteremko wa mlima uliooneshwa kwa herufi C?
Chagua Jibu
49. Kisiwa kilichooneshwa kwa herufi D kinaitwaje?
Chagua Jibu
50. Reli iliyooneshwa kwa herufi EF inaitwa . .....
Chagua Jibu
Try Another Test |