STD IV MAARIFA_JAMII ONLINE NECTA EXAM REVIEW FOR YEAR 2014

 MAARIFA YA JAMII DARASA LA IV 2014

SEHEMU A : HISTORIA

Jibu swali la 1 - 4 kwa kuchagua herufi sahihi na kuandika katika kisanduku

1. Sifa kubwa ya Ukabaila ni ....

  1. Kumiliki ardhi
  2. Kugawana ardhi
  3. Kukusanya kodi
  4. Kuwa na watumwa
Chagua Jibu


2. jamii za siku hizi hazibadilishani bidhaa kwa bidhaa kwa sababu .......

  1. hakuna bidhaa za kubadilishana
  2. watu wamechoka kufanya biashara hiyo
  3. bidhaa zilizopo ni nzito kuzibeba
  4. fedha hutumika kununua bidhaa
Chagua Jibu


3. Mojawapo ya mila na desturi za zamani ni

  1. kuogopa kazi za shambani
  2. kuwafunza watoto maadili mema
  3. kuchoma misitu ovyo
  4. kuchafua nyumba na mazingira
Chagua Jibu


4. Nasaba ni hali ya kuwa na...........

  1. uhusiano wa karibu sana
  2. watoto wa karibu sana
  3. uhusiano baina ya watu katika familia
  4. urafiki mzuri baina ya watu
Chagua Jibu


Jibu swali la 5 kwa kuandika neno "Kweli"au "si kwelf:

5. Umasikini wakati wa ujima ulisababishwa na vitendea kazi duni..................

Fungua Jibu


6. Kumwaga takataka za viwandani katika bahari na mito huongeza mazalia ya samaki . . . .

Fungua Jibu


7. Kabila linalodumisha vazi lake la asili ni Wamakonde . . . . .

Fungua Jibu


SEHEMU B : URAIA

Jibu swali la 8 - 9 kwa kuchagua herufi ya jibu sahihi na kuandika katika karatariya kujibia.

8. Katika muundo wa serikali ngazi amhayo raia wote wanaweza kushiriki ni katika mkutano mkuu wa 

  1. Mtaa au kijip
  2. Mkoa
  3. Wilaya
  4. Taifa
Chagua Jibu


9. Taja maeneo ambayo huwekwa nembo ya Taifa 

  1. Shuleni na mahakamani
  2. Mahakamani na uwanja wa Taifa
  3. Gari la Rais na kwenye fedha
  4. Kofia ya polisi na fulana za shule
Chagua Jibu


Chagua jibu sahihi kutoka kwenye mabano na liandike kwenye karatasi ya kujibia

10. Sikukuu ya wafanyakazi ni .......... 

(Sikukuu ya kitaifa, sikukuu ya kidini, sikukuu ya kisiasa).

Fungua Jibu


11. Tarehe ambayo Tanzania ilipata uhuru wake ilikuwa  . . . . . . .

(12/01/1964,  09/12/1961, 26/04/1964)

Fungua Jibu


12. Wajibu wa mtoto ni .......... 

(kucheza, kuwa na tabia njema, kufanya kazi)

Fungua Jibu


13. Mambo yanayoathiri utawala bora ni...... 

(ushirikishwaji, rushwa, maslahi bora)

Fungua Jibu


14. Jukumu la ulinzi ni la...

(watu wote, watoto peke yao, walezi peke yao

Fungua Jibu


SEHEMU C : JOGRAFIA

Jibu swali la 15 - 18 kwa kujaza jibu sahihi :

15 ..... ni tabaka la gesi linaloikinga dunia dhidi ya mionzi hatati ya jua.

Fungua Jibu


16. Kuna aina kuu ..... za uoto

Fungua Jibu


17. Madini aina ya .. . . . . . hupatikana Mererani mkoani Arusha.

Fungua Jibu


18  . . . . . . . . hupenda kutembelea mbuga wanyama, milima mirefu na makumbusho ya kihistoria

Fungua Jibu


Jibu swali 19 - 23 kwa kuoanisha maneno yaliyo katika "Fungu A" no yaliyo katika "Fungu

FUNGU A

19. Haigrometa

20. Uoto wa asili

21. Ufunguo

22. Majira ya mwaka

23. Ramani

FUNGU B

  1. Miti mirefu na mifupi
  2. Huwakilisha sura ya kitu au eneo linavyoonekana tokea juu.
  3. Huonesha alama zinazotumika katika ramani
  4. Kifaa cha kupimia unyevu
  5. Hufafanua alama zote zilizotumika katika ramani
  6. Misitu, nyasi na vichaka
  7. Usiku na mchana
  8. Masika, kipupwe, kiangazi na vuli

24. Andika majina ya pande za dunia

  1. . . . . . . . . . .
  2. . . . . . . . . . .
  3. . . . . . . . . . .
  4. . . . . . . . . . .
Fungua Jibu


24. Andika majina ya pande za dunia

  1. . . . . . . . . . .
  2. . . . . . . . . . .
  3. . . . . . . . . . .
  4. . . . . . . . . . .
Fungua Jibu


25. Toa maana ya alama hii

Fungua Jibu


Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256