HISABATI STANDARD SEVEN REGIONAL EXAMS (MOCK, PRE-NATIONAL, etc.)

JINA LA MTAHINIWA . . . . . . . . . . . . . . . . . Na. YA MTAHINIWA . . . . . . . . . . . . .

JINA LA SHULE : . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .. WILAYA: . . . . . . . . . . . . . . .

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

image 

MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) – DARASA LA VII – 2024 MKOA WA KILIMANJARO 

 04 HISABATI

Muda: Saa 2:00 Mei 2024

MAELEKEZO

  1. Karatasi hii inasehemu A, na C, jibumaswali yote.
  2. Fuata maelekezo kama yalivyo tolewakwenyekilaswali.
  3. Kumbuka kuandika namba yako ya mtihani na jina lako kwenye sehemu iliyotengwa apojuu.
  4. Tumia kalamu ya wino wabluuau mweusi
  5. Simu yamkononi au vifaavingine visivyoruhusiwa kwenye chumba cha mtihani haviruhusiwi
KWA WATAHINI TU
NAMBA YA SWALI ALAMA KIFUPISHO CHA JINA LA MTAHINI
1

2

3

4

5

6

7

8

9

MJUMLISHAJI

MHAKIKI


SEHEMU A: MATENDO YA KIHISABATI (Alama 10)
Na. Swali Kazi Jibu
1. (i) 663548 + 8500452 =


(ii)  111111222 – 19999999 =


(iii) 4146 X 512 =


(iv) 586432 ÷ 98 =


(v) 3 ⅗ + 12 4/7 =


(vi) 23 ¼ - 8 ⅘


(vii) 6 ¼ ÷ 1 ¼ =


(viii) image x 2 image


(ix) 10.967 + 0.876 =


(x) 3.978 x 6.7 =


SEHEMU B: MAFUMBO YA KIHISABATI (Alama 30)

2. (i) Shuleya Uhuru hutumia theluthi ya gunia la unga wamahindi kwa siku 3 kwa chakula. Je, nusugunia litaliwa kwa siku ngapi?


(ii) Mwamtumu alipotaka kusafiri km 320 aliambiwa nauli yake itakuwa ni shilingi 24,000, ikiwa alikuwa na shilingi 9000/= alisafiri umbali gani? (Jibu katika meta).


(iii) Uzito wa Dobini kg.5 zaidi ya uzitowa Paulo. Uzitowa Joseph ni mara mbili ya uzito wa Paulo. Ikiwa jumla ya uzitowao ni kg.65, tafuta uzito wa Paulo.


(iv) Basi liliondoka Babati saa 2030 siku ya Jumatano na kufika Arusha saa 0315 siku yaAlhamisi. Ikiwa umbali ni km 189, Basi hilo lilisafiri kwamwendo kasi gani?


(v) Umri wa Jiko ni mara mbili ya umri wa Sufuria wasasa.  Miakami tano iliyopita umri wa Jiko ulikuwa ni mara tatu ya umri wa Sufuria. Tafuta umri wa Jiko wasasa.


(vi) Chausiku alipewa noti kumi za shilingi elfu kumi kila moja kwenda kununua mchele kg 10@3000, mafuta lita 5 @ 4000, nyama kg 5 @ 9000, na nazi 5. Ninibei ya nazi moja ikiwa hakuwana fedha yoyote mkononi ?

3. (i) Amina alipanga namba kuanzia kubwa hadi ndogo, je ni namba ipi inafuata katika mfululizo ufuatao? 16, 10, 5, 1, __________


(ii) Mwanaharusi ana shilingi 16,500/=. Amepungukiwa na asilimia ngapi ya fedha ili kununua dazani 3 za daftari, iwapo bei ya daftari moja ni shilingi 500?


(iii) Athuman alifik ashuleni saa 2:30 asubuhi akiwa amechelewa kwa dakika 55. Je, alitakiw akufika shuleni saa ngapi?

4. (i) Kengele tatu zilianza kupigwa kwa pamoja mara ya kwanza saa 4:30 asubuhi. Ikiwa zinagongwa kwa kupishana kwa dakika 4, 5, 6. Ni baada ya muda gani zitagongwa tena pamoja?


(ii) Mwalimu John alipokuwaanafundishavipimo, aliwaelekezamatendokatikavipimo.  Mwanafunzi alipogawanya km16 meta 24 sm 5 kwa 3 alipatajibugani?


(iii) Mpima ardhi alipima ardhi ya hekta 896.5891 kwaajiliyaupanuziwabarabara.Kadiria idadi ya ardhi kwa sehemu mbili (2) za desimali.

5. (i) Gharama za kilogramu 8 za maharagweni shilingi 19,200. Tafutagharama za kilogramu 6 za maharagweyaainahiyohiyo.


(ii) Mwalimu alipokuwa anakagua daftari la mahudhurio aligundua kuwa  wastani wa umri wa watoto 4 ni miaka 10 na miezi 10. Ikiwa watoto watatu ni miaka 16 namiezi 9, miaka 9 na mwezi mmoja na miaka 10 namiezi 11. Tafuta umri wa mtoto wanne.


(iii) Upana wa bustani ya mboga iliyona umbo la mstatilini m.4 pungufu ya urefu wake. Ikiwaurefu wake ni m 15. Tafut aeneo lake.

6. (i) Katika ujenzi wa banda la kuku Chidi aligundua kona mbili mkabala za msambamba ni (3x + 100) na (2x + 200), akaamua kwanza kutafuta thamani ya pembe ndogo zaidi. Nini jibu alilolipata?


(ii) Eneo la nyuso za mcheduara uliozibwa pande zote ni sm24239 na nusu kipenyo chake ni sm.15. Tafuta ujazo wake katika lita. Tumia π = 22/(sm31000 = lita 1)


(iii) Urefu wa mezaya Mussa ni dm. 46.134 na urefu wa meza ya Ally ni dm. 66.995.  Andika tofauti ya urefu wa meza hizo katika kiwango kimoja cha desimali.

SEHEMU C: TAKWIMU NA MAUMBO  (Alama 10 kila swali alama 2)
7. TAKWIMU(Alama 4)



(i) Kijiji kilipata jumla ya Tshs 2,880,000, kwakuuzamazaombalimbali.Jewalipatakiasigani cha fedhakutokananamahindi?

image




(ii) Ifuatayo ni jedwali linalo onesha miche ya miti iliyooteshwa kwa miaka mitano mfululizo. Nini wastani wa miti iliyooteshwa kwa miaka hiyo.

Miaka

Idadi ya miti

2019

1946

2020

2065

2021

3344

2022

1688

2023

2008



8. MAUMBO (Alama 6)



(i) Tafutaeneo la sehemuiliyotiwakivulikatika umbo lifuatalo.

image





(ii) Umbo lifuatalo ni mstatili na mstariAB ni kiegama ambao umepandwa miti. Je, ni miti mingapi imeoteshwa ikiwa nafasi ya mti na mti ni meta 2?

image





(iii) Jitujeusi aliamua kutafuta thamani ya b katika umbo lifuatalo. Ukiwa wewe kama mtaalamu wa Hisabati utamwonesha njia ipi na kupata jibu sahihi.

image




STANDARD SEVEN HISABATI EXAM SERIES 66  

STANDARD SEVEN HISABATI EXAM SERIES 66  

Namba Ya Mtahiniwa ________________________________

Jina La Shule__________________________________

Mkoa__________________________________

Wilaya_________________________________

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS  TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA  

MTIHANI WA UTAMILIFU DARASA LA VII 

SOMO : HISABATI

TIME: 1:30 HOURS YEAR: 2024

Maelekezo

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye maswali nane (08)
  2. Jibu maswali yote katika kila sehemu. 
  3. Soma maelekezo yote yaliyoko katika kila swali kujibu vipengele husika kwa usahihi.
  4. Jaza taarifa zako (jina, shule nk) katika nafasi uliyopewa hapo juu. na kwenye nafasi uliyopewa katika kila ukurasa. 
  5. Tumia penseli kuchora kama kutakua na swali la kuchora, na kalamu ya wino wa bluu au mweusi kwa majibu yote ya kuandika. 
  6. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi ndani ya chumba cha upimaji.

SEHEMU A: (Alama 10) 

Matendo ya kihisabati

Na

 SWALI

KAZI

JIBU

1.

i. 183256 + 347684 =







ii. 982650 – 81152 =







iii. 289 × 163 =







iv. 21035 ÷ 35=







v. 3 ½ – 1 ¼ =







vi. 5 ⅘ ÷ 2 ¾ =







vii. 345 – 9.456 =







viii. 132 ÷ 8.25 =








ix. 4 3/7 + 3 ⅖







x. 8 - (+ 5) + 9 =






SEHEMU: B (Alama 30) Mafumbo

2.

i. Andika nafasi ya thamani ya 5 kwenye namba ifuatayo 456789?






ii. Tafuta jumla ya 67 na 543 (Andika jibu kwa namba za KIRUMI )







iii. Panga sehemu zifuatazo kutoka sehemu ndogo kwenda kubwa 1/7 , 5/6 , 1/2 na 4/5







iv. Shamba la bwana Nguzu lina jumla ya miche ya ndizi mia mbili na saba elfu mia tatu na moja. Andika miche ya ndizi ya bwana Nguzu kwa Tarakimu.







iv. Kadiria 78564 katika maelfu yaliyo karibu.







v. Janeth ana watoto saba ambao wanatofautiana kwa miaka saba. Ikiwa mtoto wa mwisho ana umri wa miaka 12, tafuta umri wa Mtoto wa kwanza.





3.

i. Badilisha 56.7% kuwa desimali.







ii. Tafuta jumla ya K.K.S na K.D.S ya 12, 16 na 20






iii. Husna na juma waligawana maembe kwenye uwiano wa 4:6. ikiwa juma alipata maembe 300, je Husna alipata maembe mangapi?





4.

i. Mariamu alianza kufanya kazi saa 4:45 asubuhi na kumaliza saa 3:10 jioni. Je alitumia muda gani kumaliza kazi?







ii. Fundi seremala alitengeneza mlango kwa gharama ya shilingi 250,000 na kuiuza kwa faida ya asilimia 10. Tafuta kiasi alichouzia mlango?







iii. Amina aliweka benki kiasi cha shilingi 200,000 . Ikiwa benki inalipa riba ya . Je, ni kwa muda gani alipata riba ya 7 ½ shilingi 45,000?





5.

i. Tafuta jumla ya miaka 12 na miezi 10 pamoja na miaka 18 na miezi 9.







ii. Mwalimu alihifadhi kg26 na g450 za mchele kwenye mifuko 25 inayobeba uzito sawa. Tafuta uzito ambao utabebwa na kila mfuko.







iii. Ndege ilitoka Mwanza kwenda Morogoro kwa muda wa saa 4. Ikiwa umbali ulikuwa ni kilomita 2456. Tafuta mwendokasi wa ndege hiyo.






6.

i. Shule ina jumla ya wanafunzi 465 ambao ni wavulana. Ikiwa namba ya wavulana ni ⅓ ya wanafunzi wote, je kuna wasichana wangapi katika shule hiyo?







ii. Ikiwa a=1, b=2 na c=3, tafuta thamani ya mlinganyo ufuatao 5a + 2b – c







iii. Ikiwa jumla ya namba shufwa tatu zinazofuatana ni 108. Tafuta nusu ya namba ndogo.





SEHEMU:C ( Alama 10) Dhana ya takwimu na maumbo

7.

i. Charles alitumia mshahara wake wa shilingi 540,000 kama inavooneshwa katika grafu kwa duara lifuatalo. Je ni kiasi gani alikitumia kwenye usafiri?

image














ii. Ikiwa wastani wa urefu wa wanafunzi 3 ni sm158 na wastani wa urefu wa wanafunzi 2 ni sm153. Tafuta wastani wa wanafunzi wote watano.





8.

i. Kipenyo cha mcheduara ni sm 28. Ikiwa kimo chake ni sm 50, tafuta ujazo wa mcheduara huo katika sentimita za ujazo
image







ii. Mzunguko wa duara ni sm 88. Tafuta eneo la duara hilo.








iii. Tafuta thamani ya ‘x’ kwenye umbo lifuatalo.

image






STANDARD SEVEN HISABATI EXAM SERIES 56  

STANDARD SEVEN HISABATI EXAM SERIES 56  

JINA LA MTAHINIWA . . . . . . . . . . . . 

NAMBA YA MTAHINIWA . . . . . . . . . . . . . . 

OFISI YA RAIS-TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI  YA WILAYA YA MPWAPWA 

MTIHANI WA UTAMILIFU WA DARASA LA SABA,APRIL, 2024

SOMO : HISABATI

Muda: Saa 2:00

Maelekezo: 

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye maswali nane (08)
  2. Jibu maswali yote katika kila sehemu. 
  3. Soma maelekezo yote yaliyoko katika kila swali iii kujibu vipengele husika kwa usahihi. 
  4. Jaza taarifa zako (jina, shule nk) katika nafasi uliyopewa hapo juu. na kwenye nafasi uliyopewa katika kila ukurasa. 
  5. Tumia penseli kuchora kama kutakua na swali la kuchora, na kalamu ya wino wa bluu au mweusi kwa maj ibu yote ya kuandika. 
  6. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi ndani ya chumba cha upimaji.

SEHEMU A: MATENDO YA KIHISABATI (ALAMA 10)

Katika kila kipengele, jibu maswali yote katika sehemu hii

SWALI LA 1

i. 4021 + 7929=

ii. 30045-869=

iii. 792 × 48=

iv. 8888÷88=

v. 7 1/7+4 ½ =

vi. 4 5/8+1 4/5 

vii. 7.263+6.96=

viii. 0.00075÷0.03=

(ix) Tafuta kipeuo cha pili cha 7921

(x) Zidisha km 6 m 350 kwa 25

SEHEMU B: MAFUMBO ( ALAMA30)

Jibu maswali yote katika sehemu hii

SWALI LA 2

(i) Eneo la la shamba la shule ya lupeta lina ukubwa wa hekari 89738. Kadiria hekari hizo katika maelfu yaliyo karibu

(ii) Katiak namba 983084 tarakimu 8 huwakilisha kiwango gani cha namba

(iii) Ng`ombe wa mwajuma hutoa maziwa lita 14 ¾ za maziwa kila siku. Je kwa siku 16 ngombe huyo atatoa lita ngapi za maziwa?

(iv) Wastani wa vimo vya wavuala 6 na sm 143. Wastani wa vimo vya wavulana watano kati ya hao n ism 142. Nini uregu wa kimo cha mvulana wa sita?

(v) Umeagizwa na mwalimu wa Hisabati kutafuta namba kubwa ambayo inaweza kuzigwa 12,18,na 24 kwa wakati mmoja.Wewe kama Mtaalam wa Hisabati, Je namba hiyo ni ipi?

(vi) Punguza miaka 3 na miezi 9 kwenye miaka 12 na miezi 4

SWALI LA 3

(i) Majira ya nukta A(1,-3) B(1,-1) C4,-1) ukiunganisha A ,B, na C utapata umbo gani?

(ii) Umri wa mtoto na 1/5 ya umri wa mama yake . ikiwa jumla ya umri wao ni miaka 40,tafuta umri wa mama,.

(iii) John aliuza magunia sita ya mtama akapata wastani wa shilingi 56,000/= kwa gunia moja . Ikiwa alipata sh 282000/=kwa magunia matano . Gunia la sita aliuza kwa bei gani?

SWALI LA 4.

(i) Mfanayabiashara alipata faida sh 25000/=kwa siku kwa kuuza mayai Je atapata sh ngapi kwa mwezi Februari 2025?

(ii) Kijiji cha chunyu kina jumla ya wakazi 3000 ikiwa kuna wanaume 1700. Je sehemu gani ya wakazi ni wanawake?

(iii) Bei ya simu ni shilingi 96000/= baada ya kutolewa punguzo la 20% je simu hiyo ilikuwa inauzwa sh. Ngapi kabla ya punguzo?

SWALI LA 5.

(i) Kigomba aliweka fedha benki sh 400,000/= benki hiyo hutoa faida ya 10% kwa mwaka mmoja. Tafuta jumla ya fedha baada ya mwaka mmoja na miezi sita.

(ii) Umbali wa kutoka arusha hadi tanga ni km 455 iwapo basi liliondoka tanga saa 1530 na kufika arusha saa 2200 siku hiyo hiyo nini wastani wa mwendokasi wa basi hilo.

(iii) Said aliuza vitenge kw ash. 42000 na akapata hasara ya 16% tafuta thamani ya vitenge hivyo.

SWALI LA 6.

(i) Swaumu aliwagawia watoto wake watatu Ali,Juma na Amin ash 6000/= katika uwiano wa 4:6:2 kwa mfuatano huo. Tafuta kiasi cha fedha alichopata Amina?

(ii) Mwaluko alitumia 0.25 ya fedha zake kununua chakula 1/6 ya fedha zilizobaki alinunua nguo. Iwapo alibakiwa n ash 10,000/= je mwanzoni Mwaluko alikuwa ni sh ngapi?

(iii) Salama alikwenda dukani kununua vitu vifuatavyo:- maharage kg 1 ½ @sh 3500/= sukari kg 2 @ sh 2800/=, nyama kg 1 ½ @ sh 9000/=na mafuta lita 2 @ sh 3000/= . Iwapo alimpatia mwenye duka note 4 za sh 10000/= alirudishiwa kiasi gani cha fedha?

SEHEMU C: MAUMBO NA TAKWIMU( ALAMA 10)

Jibu maswali yote katika sehemu hii

SWALI LA 7

(i) Mchoro kwa njia ya pai ufuatao unaonyesha idadi ya wafugaji na wakulima katika kijiji cha Godegode iwapo kijiji kina wafugaji 800 tafuta idadi ya wakulima katika kijiji cha Godegoge.

(ii) Grafu ifuatayo inaonyesha kiasi cha mvua kilichonyesha katika kijiji cha Kyamba kwa mwezi January hadi Machi. Tafuta wastani wa mvua iliyonyesha kwa miezi yote mitatu.

SWALI LA 8.

(i) Tafuta eneo la umbo hili (Tumia pai 22/7)

(ii) Eneo la mstatili ABCD ni sm2 120. Tafuta mzingo wake.

(iii) Tafuta ukubwa wa pembe q

STANDARD SEVEN HISABATI EXAM SERIES 44  

STANDARD SEVEN HISABATI EXAM SERIES 44  

MKOA WA SIMIYU HALMASHAURI YA MJI WA BARIADI 

MTIHANI WA KWANZA WA UTAMILIFU KATA - FEBRUARI 2023 

DARASA LA SABA HISABATI

Muda : Saa 2:00 

Maelekezo 

  1.  Maelekezo Karatasi hii ina sehemu A na B zenye jumla ya maswali arobaini na tano (45).
  2. Jibu maswali yote.
  3. Soma maelekezo yote yaliyoko katika fomu maalum ya kujibia (OMR).
  4.  Jaza taarifa zote katika fomu ya OMR.
  5.  Weka kivuli katika kila tarakimu ya Namba yako ya Mtihani kwenye nafasi husika katika fomu ya OMR.
  6. Weka kivuli katika herufi ya jibu lililo sahihi kwa swali la 1 hadi 40 katika fomu yako ya kujibia uliyopewa. Kwa mfano, kama jibu sahihi ni A weka kivuli kama ifuatavyo:
  1.  Ukigundua kuwa herufi uliyowekea kivuli si jibu sahihi, futa kivuli hiclto kwa umakini kwa kutumia kifutio sail kabla ya kuweka kivuli katika herufi mpya.
  2. Tumia penseli ya HR to katika kujibu swali la 1 hadi 40, na kalamu ya wino wa bluu au mweusi kwa swali Ia 41 hadi 45.
  3.  Onesha wazi njia iliyotumika katika kujibu swali Ia 41 hadi 45 katika nafasi iliyotolewa kwenyc fomu ya OMR.
  4. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi ndani ya chumba cha mtihani.

SEHEMU A: MATENDO YA HISABATI, MAUMBO NA MAFUMBO

Kwa swali la 1-40, kokotoa majibu, kisha chagua jibu sahihi na usilibe herufi yake kwenye karatasi maalumu ya kujibia (OMR) uliyopewa.

1. Ni lipi kati ya majibu yafuatayo linalandana na Mia tisa sabini elfu mia nne arobaini na moja?

A: 9070441 B. 900000+400+70000+1+40

C. 700000+90000+400+40+1+40 D. 9000000+70000+0+400+40+1 E. 900000+70000+0+4000+1+40

2. John alibeba mzigo wenye uzani wa tani 0.75. Je, ni kilogram ngapi alizobeba John?

A: kg 750 B. kg 7500 C. kg 0.7500 D. kg 725 E. kg 705

3. Uzani wa ng’ombe 200 ni kilogramu 250.763. Ni tarakimu ipi katika uzito ulio rekodiwa iko katika nafasi ya thamani iliyo juu ya mia moja?

A: 0 B. 2 C. 7 D. 6 E. 3

4. Sadala alitembea umbali wa hektomita 50. Umbali huu ni sawa na umbali upi kati ya vizio vifuatavyo?

A: km 0.5 B. dam 5000 C. m 5000 D. dg 50500 E. sm 30000

5.Yafuatayo ni makundi yenye fedha za noti 100 za shilingi elfu kumi kama zilivyo hesabiwa na Salome. Je, ni kiasi gani cha fedha hizi zote kwa ujumla katika tarakimu?

  1. 100,000,000/=
  2. 1,000,000/=
  3. 10,000,000/=
  4. Shilingi milioni 200
  5. 1,000.000,000/=

6. Ng’ombe mmoja anaweza kutoa lita 5 na mililita 500 za maziwa kwa siku. Je, ng’ombe huyo atatumia siku ngapi kutoa lita 22 za maziwa ?

A: Siku 8 B. Siku 2 C. Siku 4 D. Siku 5 E. Siku 3

7. Idadi ya mbegu za ngano zilikusanywa na wanafunzi saba katika makundi ya mbegu; 7000000, 6000, 500000, 10, 30000, 100, 600000000 kwa kila mmoja. Je, ni jumla ya mbegu ngapi zilikusanywa kama namba moja?

A: 6007536110 B. 607536110 C.760536110 D. 670536110 E. 670563110

8. Sarafina hulipwa kiasi cha shilingi 204000 zaidi ya rafiki yake Ulimwengu. Ikiwa Ulimwengu hulipwa na kampuni kiasi cha shilingi 500500, ni kiasi gani cha fedha Sarafina hulipwa na kampuni?

A: 745000/= B. 704500/= C. 296500/= D. 296000/= E. 754000/=

9. Philemon alitakiwa aandike namba ndogo kuliko zote inayoweza kugawanywa kwa 6,9 na 12 bila baki. Unafikiri ni namba ipi aliyoiandika ni sahihi kati ya zifuatazo?

A: 3 B. 36 C. 48 D. 24 E. 120

10. Bosco ni mwanafumzi wa darasa la sita katika shule ya msingi Mkanyageni. Alipewa na mwalimu wake jumla ya shilingi 3055000 kwa ajili ya kununulia ng’ombe. Ikiwa Bosco alinunua ng’ombe wanne(4) kwa jumla ya shilingi 2700500, Je ni kiasi gani cha fedha alibakiwa nacho?

A: 354500/= B. 435000/= C. 543500/= D. 435500/= E. 345500/=

11. Douglas alirekodi jumla ya uzito wa watoto wawili wenye jumla ya kilogram 57.8563. Ni kwa namna gani namba hii inaweza kuandikwa katika nafasi mbili za desimali?

A: Kg 58.00 B. Kg 50.85 C. Kg 578.56 D. Kg 75.86 E. Kg 57.86

12. Shule imesajili wanafunzi 200 katika mwaka wa masomo 2023. Ikiwa 35% ya wanafunzi waliosajiliwa wamesha wasili shuleni, Je ni wanafunzi wangapi bado hawajawasili shuleni?

A: 70 B. 230 C. 130 D. 103 E. 170

13. Odhiambo aliandika orodha ya namba tasa tano zinazofuatana. Kama mtaalamu wa Hisabati, orodha ipi ni sahihi kati ya hizi zifuatazo?

A: 1,2,3,5,7 B. 2,5,7,11,13 C. 7,11,13,15,17 D. 5,7,9,11,13 E. 3,5,7,11,13

14. Shulala alipanda miti katika mistari mitatu, ambapo kila mstari una mashimo 21. Ikiwa kila shimo alipanda miti minne, je alipanda jumla ya miti mingapi kwa pamoja?

A: 252 B. 84 C. 63 D. 225 E. 522

15. Baraka alikuwa na noti za shilingi 1000. Noti ya kwanza ilikua na namba 136700201 wakati noti ya mwisho ilikuwa na namba 136700300. Ikiwa noti hizo zilikuwa zimepangwa kwa namba zenye mtiririko mzuri, je Baraka alikua na jumla ya noti ngapi?

A: 99 B. 89 C. 100 D. 98 E. 101

16. Umbali wa barabara ni kilometa 270.007. Serikali ina tarajia kujenga umbali wa kilometa 198.13 kwa kiwango cha lami. Ni kilometa ngapi za barabara zitabaki bila lami baada ya ujenzi huo?

A: Km 70.807 B. Km 71.87 C. Km 877.71 D. Km 71.877 E. Km 7.1877

17. Kalunde aliambiwa na mwalimu wake aandike namba ndogo kuliko zote ambayo hutokana na tarakimu sita. Lipi unafikiri ni jibu lililokusudiwa na mwalimu kati ya majibu yafuatayo?

A: 210010 B. 102345 C. 110100 D. 012345 E. 1012345

18. Shule inamiliki theluthi ya ardhi ya kijiji. Ikiwa shule inamiliki kilomita za mraba 60, ni kiasi gani cha eneo la kilomita za mraba za ardhi linamilikiwa na Peter ikiwa anamiliki moja ya tisa ya eneo la kijiji?

A: 40 B. 80 C. 90 D. 20 E. 180

19. Watu watano walihudhuria mkutano wa kijiji. Walikaa kwenye viti vilivyokuwa vimewekwa namba kwa mpangilio wa 5, 7, 11, 13, _____ Je, ni namba ipi ya kiti iliwekwa kwenye kiti cha mtu wa tano?

A: 15 B. 14 C. 19 D. 23 E. 17

20. Jedwali lifuatalo linaonesha idadi ya vitabu kwa masomo matano yanayofundishwa darasa la tano. Tafuta wastani wa idadi ya vitabu katika shule hiyo.

Jina la kitabu

Sayansi

Kiswahili

English

M/Jamii

Idadi

35

30

40

15

A: 82 B. 104 C. 20 D. 28 E. 140

21. Mkulima alipanda mbegu katika mashimo matano ya bustani yake. Ikiwa katika mashimo manne ya kwanza, kila moja lilikua na mbegu 4, 9, 16 na 25 kwa mpangilio huo. Je ni ipi ilikua jumla ya mbegu zilizopandwa katika mashimo yote matano?

A: 90 B. 360 C. 36 D. 63 E. 49

22. Bw. Kidulo alichora pembe nyuma ya kitabu chake ambayo ukubwa wake ulikua ni 63°. Kama mtaalamu wa Hisabati, ni lipi ni jina la pembe hiyo iliyochorwa na Bw. Kidulo?

A: Pembe butu B. Pembe kuu C. Pembe kali D. Pembe mraba E. Pembe nyoofu

23. Wakati wa mchezo wa mpira wa miguu kati ya Singida United dhidi ya Mwadui FC, magoli yalikua yakifungwa kila baada ya dakika 18 ya mchezo. Ikiwa mchezo uliendeshwa kwa dakika 90 bila ya mapumziko, ni magoli mangapi yalifungwa kwa muda wote wa mchezo?

A: 10 B. 6 C. 19 D. 8 E. 5

24. Katika umbo, ukubwa wa pembe ya nje ni mara mbili ya ukubwa wa pembe ya ndani. Ni ipi kati ya pembe zifuatazo itakua ni ukubwa wa pembe ya nje?

A: 45° B. 120° C. 90° D. 60° E. 240°

25. Hidaya alijaribu kupanga namba katika machaguo yafuatayo kutoka ndogo kwenda kubwa. Kati ya namba hizi ni ipi alipaswa aanzie?

A: 2001 B. CMXCIX C. 1526 D. MCXIX E. MDCCCLXXXIII

26. Upande mmoja wa kasha la mche mraba ni sm 10. Ikiwa Bwana Heri atatumia kasha hilo kununulia maziwa, ni kiasi cha lita ngapi Bwana Heri atabeba?

A: L 10 B. L1.2 C. L 2.0 D. L 1000 E. L 1

27. Ngombola alikwenda sokoni na jumla ya shilingi 1,000,000 kwa ajili ya kununulia bidhaa zifuatazo;-

  • Kilogramu 4 za sukari @ shilingi 5,000
  • Mifuko10 ya saruji @ shilingi 20,000
  • Dazani 5 za daftar @ shilingi 40,000 na
  • Simu 2 za mkononi @ shilingi 90,000.

Ni kiasi gani cha fedha alibakiwa nacho katika asilimia?

A: 60% B. 20% C. 75% D. 40% E. 30%

28. Umbo lifuatalo linalandana na umbo la nyumba ya Bw. Msemakweli. Ni kwa namna gani tunaweza kulitaja jina la umbo hili kuhusianisha na elimu ya maumbo (jiometri)?


A: Pentagon B. Hexagon C. Heptagon D. Octagon E. Decagon

29. Baba yangu alilima shamba kwa siku 2 na saa tano. Je, baba alitumia dakika ngapi?

A: 3180 B. 3420 C. 3080 D. 1440 E. 1280

30.

Gaucho alifunga magoli 240 pungufu ya rafiki yake Neymar ambaye alifunga magoli 890 katika kipindi cha maisha yake ya soka. Ni magoli mangapi walifunga wote kwa pamoja?

A: 650 B. 560 C. 1540 D. 1130 E. 1450

31.

Garimoshi liliondoka Kilosa majira ya saa 1945. Dakika 25 baadae, basi ambalo lilikuwa njiani likitokea Dumila likawasili Kilosa. Ni muda gani basi hilo liliwasili Kilosa katika mtindo wa saa 12?

A: 2:10 mchana B. 2010 hrs C. 8:45 usiku D. 8:10 asubuhi E. 2:10 usiku

32. Endapo Monica atatembea mara moja kuzunguka uwanja uliochorwa hapo chini, ni umbali gani atakuwa ametembea? (Tumia pai = 3.14)


A: m 741 B. m 614 C. m 740 D. m 714 E. m 7140

33. Kama Halima angeuza gauni lake kwa shilingi 1,200,000 angepata hasara ya shilingi 240,000. Ipi ilikuwa ni thamani halisi ya gauni hilo?

A: 2400000/= B. 960000/= C. 1440000/= D. 1040000/= E. 1240000/=

34. Zinduna alitumia jumla ya shilingi 25,500 kama matumizi yake ya kila siku katika mwezi Februari mwaka 2016. Ni kiasi gani cha fedha alikitumia kwa mwezi mzima?

A: 714000/= B. 741000/= C. 739500/= D. 765000/= E. 756000/=

35. Kitabu chenye kurasa mia moja kinaweza kusomwa na Ashura kwa saa 2 na dakika 12. Ashura atatumia muda gani kusoma vitabu 9 vya aina hiyo?

A: saa 19 dk 40 B. dk 1188 C. saa 18 dk 48 D. saa 19 dk 108 E. dk 1088

36. Kwenye uchaguzi wa kata mwaka 2014, Zidane alipata kura 378, Shumbana kura MXIX wakati Suzan akapata kura 608. Ni kura ngapi zilipigwa na wajumbe wa kata wakati wa uchaguzi huo?

A: MCV B. MCMXCV C. MMV D. MCIV E. MCV

37. Mfanyabiashara alikuwa na gunia moja la mahindi na akaliuza kwa faida ya 20%. Ikiwa aliliuza kwa kiasi cha shilingi 240,000, ni kiasi gani cha fedha alitumia kununulia hilo gunia la mahindi?

A: 200000/= B. 140000/= C. 40000/= D. 220000/= E. 20000/=

38. Galaga alikuwa na kamba yenye urefu wa mita 8 2/3 . Ikiwa aliamua kumpatia rafiki yake Mrope kipande chenye urefu wa mita 4 1/24 , ni mita ngapi ambazo Galaga alibakiwa nazo?

A: m 4 B. m 6 3/8 C. m 4 3/8 D. m 5 3/8 E. m 4 5/8

39. Bukuru alinunua kg 46 na dag 5 za unga wa mahindi. Akataka kuwapatia watu watano (5) ambao aliwaahidi kama zawadi ya kufanya kazi kwa bidii.

Je, kila mtu alipata kiasi gani?

A: kg 21 dag 9 B. kg9 dag 105 C. g9 dg 21 D. kg9 dag 21 E. dag 12 kg 9

40. David alirahisisha mtajo ufuatao hapo chini kama ilivyokua inahitajika urahisishwe. Lipi ni jibu sahihi kati ya yafuatayo ikiwa mtajo wenyewe ulikuwa 16x – x + 13 ?

A: 3x B. 2x C. 15x-13 D. 15x+13 E. 13x-x

SEHEMU B: MATENDO YA HISABATI, MAUMBO NA MAFUMBO

Kwa swali la 41-45, Tumia kalamu ya wino wa buluu au mweusi kukokotoa majibu katika nafasi ya karatasi maalumu ya kujibia (OMR) uliyopewa kwa kuonyesha kazi yako kwa usahihi.

41.  75% ya wanafunzi wa darasa la nne katika shule ya msingi Kibondo wanajua kusoma kwa ufasaha. Idadi ya wanafunzi iliyobaki hawawezi kusoma kwa ufasaha. Je, darasa hilo lina wanafunzi wangapi ikiwa idadi ya wanafunzi ambao hawawezi kusoma vizuri ni wanafunzi 40 ?

42.  Kwenye mzani wa uzito barabarani tani 250 na kg 750 zilirekodiwa kwa kipindi cha siku moja. Je, ni kiasi gani cha uzani wa magari kitarekodiwa kwa kipindi cha siku nne (4) ikiwa uzani wa siku hautobadilika?

43.  Fundi Saudi alianza kujenga kona ya nyumba ya Mwashamba katika majira ya nukta yaliyowakilishwa na herufi C. Andika majira ya nukta ya herufi ambapo fundi Saudi alianzia kujenga nyumba hiyo.


44.  Mchoro ufuatao unaonesha mgawanyo wa tani za zao la tumbaku zilizokusanywa mkoani Tabora kutoka wilaya mbalimbali. Ikiwa idadi ya tani zote zilizo kusanywa kutoka wilaya zote ni tani 720, Je ni tani ngapi zilikusanywa kutoka katika wilaya ya Sikonge?


45.  Katika mgawanyo fulani, Gatuka alipata 4080 pungufu ya rafiki yake Mponjoli ambaye alipata 19008. Ni kiasi gani Gatuka alipatiwa?

STANDARD SEVEN HISABATI EXAM SERIES 17  

STANDARD SEVEN HISABATI EXAM SERIES 17  

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

HALMASHAURI YA MANISPAA YA UBUNGO

MTIHANI WA UTAMILIFU KATA

HISABATI DARASA LA SABA – MACHI, 2023

MUDA: MASAA 2

MAELEKEZO

  1. Mtihani huu una maswali arobaini na tano (45) tu.
  2. Jibu maswali yote
  3. Soma maelekezo kwa kila kurasa uliyopewa
  4. Kumbuka kuandika Jina lako, Namba yako ya mtihani na Jina la shule yako katika karatasi ya kujibia.
  5. Tumia penseli ya HB tu.
  6. Simu hazihitajiki katika chumba cha mtihani.

SEHEMU A: MASWALI YA KUCHAGUA

1. Mika alivuna magunia 56 ya mahindi. Kama aliuza magunia yote kwa shilingi 140,000/=, je! kila gunia moja la mahindi aliliuza kwa shilingi ngapi?

(A) sh. 140,000 (B) 25,000 (C) 40,000 (D) 15,000 (E) 78,400 [     ]

2. Andika “milioni saba laki tisa na mia nane” kwa tarakimu

(A) 79,000,800 (B) 7,009,800 (C) 7,900,800 (D) 7,090,800 (E) 700,900,800 [     ]

3. Darasa la saba katika shule ya msingi Ndala ina wavulana 16 na wasichana 28. Je! uwiano wa wavulana kwa idadi ya wasichana ni upi?

(A) 16:28 (B) 28:16 (C) 4:7 (D) 4:11 (E) 11:16 [     ]

4. Kama Jerry alikula 5/7 ya mkate na Tonny akala 1/8 ya mkate huohuo. Je! sehemu ya mkate uliobakia ni ipi? 

(A) 9/56 (B) 33/56 (C) 1/13 (D) 23/56 (E) 13/15 [     ]

5. Wanafunzi wa darasa la saba waliulizwa na mwalimu wao kurahisisha algebra ifuatayo;


 Je! walipata jibu gani?

(A) 4a2b (B) 4a2b2 (C) 4a3b2 (D) a2b2 (E) 4ab2 [     ]

6. Ali anasoma darasa la tano, rafiki yake mmoja alimuuliza jina la umbo hilo hapo chini. Je! jina sahihi ni lipi?


(A) pembetatu mraba (B) pembe tatu gunia (C) pembetatu sawa (D) pembetatu msambamba (E) pembetatu pacha [     ]

7. Tafuta eneo la kabati hili ikiwa juu lipo wazi


(A) 1670m(B) 217m(C) 1150m(D) 2170cm(E) 1670cm2 [     ]

8. Bei ya gari imeongezeka kutoka shilingi 3,000,000 hadi shilingi 4,500,000. Tafuta asilimia ya bei iliyoongezeka. (A) 33.3% (B) 30% (C) 25% (D) 66.6% (E) 50% [     ]

9. Ni mchoro upi unaoweza kuunganisha majira ya nukta yafuatayo? A (5,3) B(4,5) C(0,3) D (1,1)

(A) mstatili (B) trapeza (C) duara (D) msambamba (E) mraba [     ]

10. Upi kati ya michoro ifuatayo sio pembe nne?

(A) trapeza (B) mraba (C) pembe tatu (D) msambamba (E) mstatili [     ]

11. Mwalimu Beni ametuambia tutafute K.K.S cha 56,117 na 6 kwa kutumia njia yoyote. Je! lipi ni jibu sahihi? 

(A) 9 (B) 1 (C) 13 (D) 11 (E) 17 [     ]

12. Sheila alichelewa kulala na kuamka saa 05:45. Andika muda huo kwa masaa kumi na mbili. 

(A) 5:45 asbh (B) 5:45 mchana (C) 17:45 asbh (D) 17:45 jioni (E) 5:17 [     ]

13. Mwalimu wako wa hesabu amekuuliza jibu la swali hili, (x-y) toa (x+y). Je! lipi ni jibu sahihi?

(A) -2y (B) +2y (C) 2x (D) 0 (E) 2xy [     ]

14. Taja namba shufwa zote zinazogawanyika kwa 6 zilizopo kati 20 – 40

(A) 24, 30, 36 (B) 32, 34, 36 (C) 22, 24, 28, 30 (D) 24, 30, 36, 40 (E) 30,24, 36, 38 [     ]

15. Babu alivuna matikiti maji 8 kwenye shamba lake na kuwagawia yatima. Siku moja alikula 31/2 na kuwapa yatima 17/8. Je! alibakiwa na matikiti maji mangapi?

(A) 23/8 (B) 2 (C) 25/8 (D) 45/8 (D) 5/8 [     ]

16. Darasa la sita walipewa mfululizo wa namba 1, 8, 27, 64, ____. Je! namba inayofuata ni ipi?

(A) 81 (B) 101 (C) 125 (D) 119 (E) 72 [     ]

17. Tafuta eneo la shamba lifuatalo


(A) 36m(B) 112m(C) 768m(D) 112m (E) 36m2 [     ]

18. Andika majira ya nukta X


(A) x (-2,-1) (B) x (0,2) (C) x (2,0) (D) x (2,1) (E) x (-0, +0) [     ]

19. Kuna mistari mingapi linganifu katika umbo hili la pembe tatu?


(A) 1 (B) 2 (C) 3 (D) 4 (E) 5 [     ]

20. Tafuta ujazo wa lita uliojaza chombo hapo chini (Lita 1 – 1000cm3)


(A) 8L (B) 8cm3 (C) 80L (D) 8000L (E) 800 cm[     ]

21. Badilisha 60% kuwa katika sehemu (a/b)

(A) 6/10 (B) 3/2 (C) 6/100 (D) 12/(E) 3/[     ]

22. Kuna lita 2/5 ngapi kwenye lita 10 za mafuta ya kupikia?

(A) 25 (B) 100 (C) 4 (D) 8 (E) 1/25 [     ]

23. Kipi ni kipeuo cha pili cha 9 kati ya namba zifuatazo?

(A) 1 (B) 3 (C) 81 (D) 29 (E) 9 [     ]

24. Katika takwimu 345.97 namba ipi inaonyesha makumi?

(A) 3 (B) 4 (C) 5 (D) 9 (E) 7 [     ]

25. Badili 608,864 kwenda kwenye maelfu

(A) 609,00 (B) 608,900 (C) 608,860 (D) 618,000 (E) 600,000 [     ]

26. Wakulima watatu wamechanga shilingi 80,000/= katika uwiano wa 2:5:9. Je! mkulima wa kwanza alipata kiasi gani? (A) 45,000 (B) 5000 (C) 25000 (D) 2000 (E) 10,000 [     ]

27. Wafanyakazi 12 walivuna heka 8 kwa siku 8. Wafanyakazi 18 wakaongezeka. Je! watavunakwa siku ngapi katika heka hizo? (A) siku 1 (B) siku 3 (C) siku 4 (D) siku 5 (E) siku 2 [     ]

28. Tafuta thamani ya “y” katika swali hili 3y+3 = 2y-2

3 (A) 5/2 (B) -3 (C) 3 (D) -5 (E) 4/3 [     ]

29. Jenereta lina uwezo wa kubeba lita 80 za dizeli. Ikiwa 40% ya dizeli yametumika, Je! sehemu ya ujazo wa dizeli uliobakia kwenye tanki ni kiasi gani?

(A) 32 (B) 48 (C) 2/5 (D) ½ (E) 3/5 [     ]

30. Benard ana pipi 24 na Ally ana pipi 72. Je! ni kiasi gai cha pipi Benard anatakiwa kukipata toka kwa Ally ili wawe na idadi sawa ya pipi? 

(A) 27 (B) 18 (C) 24 (D) 16 (E) 20 [     ]

31. Ikiwa 7/8 ya namba iliyofichwa ni 21, Je! ¾ ya namba hiyo ni ipi?

(A) 24 (B) 18 (C) 12 (D) 28 (E) 14 [     ]

32. Darasa la tano njano walipewa kazi ya kutafuta jumla ya namba zilizopo kati ya 12 na 20. Lipi ni

jibu sahihi? (A) 49 (B) 32 (C) 30 (D) 64 (E) 45 [     ]

33. Andika 3.0695 katika nafasi mbili ya desimali. (A) 0.36 (B) 3.68 (C) 3.16 (D) 3.07 (E) 3.67[     ]

34. Namba fulani ukiizidisha yenyewe unapata 6561. Tafuta kipauo cha pili cha namba hiyo.

(A) 9 (B) 81 (C) 3 (D) 39 (E) 33 [     ]

35. Baba yake na Hadija alizaliwa mwaka 1944. Andika mwaka aliozaliwa kwa kirumi.

(A) MCMXCIV (B) MMXMLV (C) MCMXLIV (D) MCDXLIV (E) MCMXCIX [     ]

36. Wastani wa uzito wa wanafunzi watano ni kilogram 42. Kama uzito wa wanafunzi wane ni 54kg, 18kg, 48kg na 60kg. Tafuta uzito wa mwanafunzi wa tano kwa gramu.

(A) 35000g (B) 30000g (C) 50000kg (C) 40000g (E) 29000g [     ]

37. Gari lina viti 50. Kama 15 ni rangi nyekundu, tafuta sehemu inayowakilisha viti visivyo na rangi nyekundu. (A) ¾ (B) 5/7 (C) 3/5 (D) 7/10 (E) 3/10 [     ]

38. Ikiwa jumla ya mfululizo wa namba tatu witirini 57. Tafuta zao la namba hizo tatu.

(A) 21 (B) 14 (C) 784 (D) 6873 (E) 6783 [     ]

39. Badili 11/2% kuwa desimali 

(A) 0.015 (B) 1.15 (C) 0.15 (D) 0.05 (E) 1.5 [     ]

40. Tafuta jumla ya 121/2 na 33/4 

(A) 154/6 (B) 161/4 (C) 151/4 (D) 11/4 (E) 134/6 [     ]

 SEHEMU B: MATENDO YA HISABATI, MAUMBO NA MAFUMBO

Kokotoa kwa makini kisha andika jibu sahihi

41. Grafu ifuatayo inaonyesha idadi ya wanafunzi waliohudhuria shuleni Jumanne hadi Ijumaa. Tafuta wastani wa siku tatu za mwanzo kisha kadiria jibu lako katika namba kamili.


42. Kama mzunguko wa mstatili ABCD hapo chini ni 26cm. Tafuta eneo la sentimita za mraba


43. Jumla ya pembe za ndani za umbo mraba ni 2x. Pembe nyingine mbili ni 70o na 80o. Tafuta thamani ya “X”

44. Siku moja mwalimu Yusufu aliwapa kazi wavulana wa darasa la saba wachimbe shimo, walipokuwa wanachimba na kufika urefu fulani walikutana na mwamba mgumu kama umbo la eneo lililotiwa kivuli katika mchoro hapo chini. Tafuta eneo lililotiwa kivuli katika mchoro hapo chini.


45. Kielelezo kifuatacho kinaonyesha namna Mzee Mbwiga alivyoutumia mashahara wake wa mwezi. Kama alipokea shilingi 720,000 baada ya makato ya kodi, je! alitumia kiasi gani kwa chakula?


STANDARD SEVEN HISABATI EXAM SERIES 9  

STANDARD SEVEN HISABATI EXAM SERIES 9  

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256