KISWAHILI STANDARD SEVEN REGIONAL EXAMS (MOCK, PRE-NATIONAL, etc.)

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA - MKOA WA DODOMA

KISWAHILI - DARASA LA VII JANUARI, 2025

MUDA: SAA 1:30

MAELEKEZO KWA MTAHINIWA:

  1. Mtihani huu una sehemu A, B, na C zenye jumla ya maswali SITA (6).
  2. Soma maelekezo na ujibu maswali YOTE katika kila sehemu.
  3. Tumia kalamu ya wino wa BLUU au MWEUSI kujibu maswali.
  4. Simu za mkononi pamoja na vitu visivyoruhusiwa HAVITAKIWI

SEHEMU A: UFAHAMU

1. Sikiliza kwa makini hadithi utakayosomewa kisha jibu swali la 1 mpaka la 5

i. Wanakijiji walipata mafunzo kuhusu nini? 

  1. Upishi wa vyakula
  2. usafi wa mazingira
  3. kutengeneza mafya
  4. kupika mikate
  5. kulima mazao

ii. Walijifunza njia bora za kupika na kuhifadhi chakula ili ____

  1. Kuepuka magonjwa
  2. chakula kisiharibike
  3. kupata chakula kitamu
  4. kitumike mwaka mzima
  5. kuwa wasafi

iii. Kwa nini mwendesha mafunzo alisisitiza usafi wa vyakula na jiko?

  1. Ili kupata chakula kitamu
  2. ili kuwa naanuani za vyakula
  3. ili chakula kisiharibike
  4. ili kuepuka magonjwa
  5. kulamboga za majani

iv. Chakula kilipikwa na kina nani? 

  1. Sankwaleto
  2. wanakijiji
  3. wakina mama
  4. mafya
  5. waendesha mafunzo

v. Andika umoja wa neno mafya kama lilivyotumika katika kifungu cha habari. 

  1. Majifya
  2. mawematatu
  3. mafiga
  4. jifya
  5. jivu

2. Chagua herufi ya jibu sahihi

i. Katika sentensi “Juma alikuwa anaandika darasani” neno alikuwa limesimama kama aina gani ya neno? 

  1. Kitenzi kikuu
  2. kitenzi kisaidizi
  3. kitenzi kishirikishi
  4. kielezi cha nomino
  5. kivumishi

ii. “Tunafundisha wanafunzi masomo yote ya biashara.sentensi hiyo ipo katika wakati gani? 

  1. Ujao
  2. uliopita
  3. timilifu
  4. uliopo
  5. mazoea

iii. Mjomba anauza kiwanja kilichoko mjini.neno lipi limetumika kama kielezi katika sentensi hiyo? 

  1. Mjomba
  2. kiwanja
  3. anauza
  4. kilichoko
  5. mjini

iv. Ukulima wa kisasa ________ kutiliwa mkazo ili kuinua uchumi wa nchi yetu. 

  1. Una budi
  2. hauna budi
  3. ni budi
  4. si budi
  5. hatuna budi

v. Kisawe cha neno adimu ni kipi? 

  1. Patikana
  2. changa
  3. chache
  4. chenga
  5. julikana

vi. Tulikuwa tukimshauri rafiki yetu asome kwa bidii ili aweze kufanikiwa maishani. Yeye hakutusikia kwani alitamani kupata utajiri kwa njia isiyo halali. Hivi sasa amekamatwa kwa kosa la wizi na anajuta kwa kusema?

  1. Elimu haina mwisho
  2. akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki
  3. tamaa mbele mauti nyuma
  4. sikio la kufa- halisikii dawa nyingi
  5. usiache mbachao kwa msala upitao

vii. Chakula chote kimemwagika sakafuni. Wingi wa neno chote ni upi? 

  1. Yote
  2. zote
  3. wote
  4. pote
  5. vyote

viii. Chombo maalumu cha majini kinachotumika kuvusha watu na mizigo kwenda ng’ambo ya pili huitwa _______ 

  1. Daladala
  2. pikipiki
  3. basi
  4. kivuko
  5. baiskeli

ix. Mtu mwenye taaluma ya ujuzi wa kubuni,kutengeneza au kurekebisha majengo, barabara au mitambo anaitwaje?

  1. Rubani
  2. dereva
  3. mkutubi
  4. mhandisi
  5. mhunzi

x. Malizia methali ifuatayo; mwanzo wa ngoma ni _______

  1. Mdundo
  2. lele
  3. nyumbani
  4. kucheza
  5. kuimba

3. Oanisha maneno yaliyopo katika orodha A na yale ya orodha B kwa kuandika herufi ya jibu sahihi

ORODHA A

ORODHA B

  1. Ukumbi maalumu wa kulia chakula [     ]
  2. Jengo au chumba maalumu kinachotumika kwa ajili ya majaribio na utafiti wa kisayansi. [     ]
  3. Jengo lenye maonyesho ya vitu vya kale kazi za sanaa au sampuli za malighali. [     ]
  4. Enda mahali Fulani kwa madhumuni ya kutembelea nakujifunza jambo. [     ]
  5. Elimu au ujuzi aupatao mtu kutokana nakusoma, kusikia au kutenda. [     ]
  1. Maarifa
  2. Zuru
  3. Bwalo
  4. Makumbusho
  5. Maabara
  6. Kituo

 SEHEMU B

4. Panga sentensi zifuatazo katika mtiririko mzuri wa mawazo unaoleta mantiki kwa kuzipa herufi A, B, C, D na E

  1. Matokeo yalipotoka Mariam alibahatika kuchaguliwa miongoni mwa watahiniwa waliofaulu. [     ]
  2. Hivyo alimwandikia barua baba yake aliyeko Mwanza. [     ]
  3. Watahiniwa wote walifanya mtihani siku hiyo. [     ]
  4. Barua hiyo ilikuwa mambo muhimu yanayohitajika shuleni. [     ]
  5. Mariamu alikuwa miongoni mwa watahiniwa hao. [     ]

 5. Jaza nafasi zilizoachwa wazi

  1. Andika neno lenye maana sawa na bakora _______________
  2. Mtoto wa mwisho kuzaliwa huitwa __________________
  3. Andika neno linalojumuisha maneno yafuatayo Almasi, dhahabu, shaba na ulanga___________
  4. Andika kirefu chaneno BAKITA__________________________________________
  5. Pigia mstari neno lililotofauti. kodi, rushwa, ushuru, ada .

6. Soma kwa makini shairi lifuatalo kisha ujibu maswali yafuatayo

Ndugu watanzania, shime tujitokezeni.
Kuhesabiwa muhimu, mipango kukadiria
Wala tusibabaike, kusikiliza majungu
Sensa kwa maendeleo,kuhesabiwa muhimu

Mipango kukadiria, kwa kila mtanzania,
Elimu nayo afya,kila raia apate,
Barabara nayo maji, kila sehemu sawa
Sensa kwa maendeleo, kuhesabiwa muhimu,  

Muhamasishe na ndugu, hata na Yule jirani.
Wote wakajitokeze, mapema kuhesabiwa,
Wasihusishe sihiri, imani zisizofaa.
Sensa kwa maendeleo, kuhesabiwa muhimu.

Maswali

  1. Shairi hii limeundwa na mishororo mingapi katika kila ubeti?_______________________
  2. Mshororo wa pili katika ubeti wa kwanza una jumla ya mizani mingapi?_______________
  3. Andika kibwagizo cha shairi hili ________________
  4. Andika vina vya kati na vya mwisho katika ubeti wa tatu mstari wa tatu ___________na_____
  5. Pendekeza kichwa cha habari kinachofaa katika shairi hili.__________________

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 72  

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 72  

Namba Ya Mtahiniwa ________________________________

Jina La Shule__________________________________

Wilaya__________________________________

JAMUHURI YA MUUNGANO VA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA MKOA WA DAR ES SALAAM

MTIHANI (PRE-NATIONAL) KWA DARASA LA VII

01 KISWAHILI

Muda: Saa 1:40 Mwaka: 2024 

Maelekezo 

  1. Karatasi hii ina schemu A, B na C zenye jumla ya maswali sita (6)
  2. Jibu maswali yote katika nafasi ulizopewa. 
  3. Sehemu A na B zina alama ishirini (20) kila moja na sehemu C ina alama kumi (10)
  4. Maandishi yote yaandikwe kwa kalamu yenye wino wa bluu au mweusi, isipokuwa katika michoro ambapo ni lazima kutumia pensili.
  5. Vifaa vya mawasiliano na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi ndani ya chumba cha mtihani.
  6. Andika Namba yako ya Mtihani na taarifa nyingine zote muhimu katika kila ukurasa sehemu ya juu upande wa kulia.
KWA MATUMIZI YA MATAHINI TUU
NAMBA YA SWALI ALAMA SAHIHI YA MTAHINI
1.

2.

3.

4.

5.

6.

JUMLA

SAHIHI YA MHAKIKI

SEHEMU A: (Alama 20)

Jibu maswali yote katika sehemu hii

1. Sikiliza kwa makini hadithi utakayosomewa na msimamizi kisha jibu kipengele cha (i) - (v) kwa kuchagua heruti ya jibu sahihi na kuandika katika kisanduku.

i/  Nani alikuwa na miguu hapo zamani?  [    ]

  1.  Ngoma
  2. Jongoo
  3. Kale
  4. Nyoka
  5. Macho

ii/ Nani alikuwa na macho hapo zamani? [    ]

  1. Miguu
  2. Jongoo
  3.  Nyoka
  4. Ngoma
  5. Kale

iii/ Nyoka alimwomba Jongoo amuazime macho ili aende wapi?  [    ]

  1. Zamani
  2. Ngomani
  3. Kwenye sherehe
  4.  Kwenye kale
  5.  Michezoni

iv/  Kwanini Jongoo hana macho hadi leo?  [    ]

  1. Alimuazima Nyoka
  2. Aliyapeleka kwenye sherehe
  3. Aliyarudisha ngomani
  4. Aliyapeleka kale
  5. Amrudishie macho

v/ Nani alikuwa msaliti kwa mwenzie?  [    ]

  1. Miguu
  2. Macho
  3. Jongoo
  4.  Kale
  5.  Nyoka

2. Katika kipengele cha (i) - (x) chagua jibu sahihi kisha andika herufi yake katika kisanduku ulichopewa. 

i/ Matata alisema kuwa hawezi kuja kwetu. Kauli halisi ya sentensi hii ni ipi?  [    ]

  1. Matata alisema, "Siwezi kuja kwenu"
  2. "Siwezi kuja kwao". Matata alisema
  3. "Siji kwenu". Matata aliongea sana
  4. "Sitawahi kuja kwenu tena" Matata alisema
  5. Matata alisema kuwa, "Sitakuja tena walahi!"

ii/ "Kulwa na Doto hawaimbiani wimbo" Katika sentensi hii kiambishi cha ukanushi ni kipi?  [    ]

  1.  -wa-
  2.  -1mb-
  3. -Ha -
  4.  -ni
  5.  - ha-

iii/  Panya huyu anakula unga wangu. Wingi wa sentensi hii ni upi?  [    ]

  1.  Panya hawa wanakula unga wangu
  2. Mapanya hawa wanakula unga wetu
  3. Panya hizi zinakula unga wangu
  4.  Panya hizi zinakula unga wetu
  5. Panya hawa wanakula unga wetu

iv/ Mtu anayefundisha chuo kikuu huitwa nani?  [    ]

  1.  Mwalimu
  2. Mhadhiri
  3. Mhariri
  4. Mkalili
  5. Mkufunzi

 v/ Kisawe cha pipi ni peremende. Je, kisawe cha "Munyu" ni kipi kati ya maneno yafuatayo?  [    ]

  1. Kocho
  2. Sukari
  3. Sharubati
  4.  Chumvi
  5. Sima

vi. Hapo . . . . aliposimama kiongozi wa mbio za mwenge siku ya ufunguzi wa jengo jipya  Ia shule yetu.  [    ]

  1. ndiye
  2. ndipo
  3. ndiko
  4. ndimo
  5. ndio

vii. " Fumole hufuma huku na huko" 3ibu Ia kitendawili hiki ni lipi kati ya maneno yafuatayo  [    ]

  1. Sindano
  2. Mchi
  3. Mwiba
  4. Mkuki
  5. Moto

viii. Mwambinga hapendi kushirikiana na wenzake. Yeye hupenda kusema kuwa  [    ]

  1. Wengi wape
  2. Wema hauozi
  3. Wingi si hoja
  4. Akiba haiozi
  5. Elimu ni baharl

ix. Ainisha aina za maneno katika sentensi ifuatayo kimuundo"Gari lao linatembea polepole"  [    ]

  1. N+t + T + E
  2. N + V + Ts + V
  3. W+Vi-T+E
  4. N+ Ts + E H
  5. N + T E

x. Nahau "fyata mkia" ina maana gani?  [    ]

  1. Nyamaza
  2. Tembea nyuma Kama mkia
  3. Legeza moyo wako
  4. Ondoa mkia
  5. Ongea kwa sauti

3. Oanisha maneno ya kifungu A na aina za maneno ya kifungu B ili kuleta maana kamili, kwa kuandika herufi ya jibu sahihi katika nafasi ya majibu.

KIFUNGU A

MAIIBU

KIFUNGU B

(i) Mpole, Mweusi, mdogo

[    ]

  1.     Viunganishi
  2.     Vihisishi
  3.     Vielezi
  4.     Vivumishi
  5.      Nomino
  6.   Viwakilishi
  7.  Vitenzi

(ii) Sisi, mimi, wewe

[    ]

(iii) Mungu, Rime, Kiti

[    ]

(iv) Ingawa, lakini, hatimaye

[    ]

(v) Polepole, shuleni, upandeupande

[    ]    

 SEHEMU B: (Alama 20)

Jibu maswali yote katika sehemu hii

 4. Panga sentensi zifuatazo katika mtiririko unaoleta mantiki kwa kuzipa herufi A, B, C, D na E

  1. Mama yake Daudi hakumpenda Bakari,
  2. Napo zamani za kale waliishl vijana wawili waliokuwa marafiki.
  3. Bakari alichukua panga kuelekea porini.
  4. Siku moja mama yake Daudi alimtuma Bakari kwenda porini kutafuta kuni.
  5. Marafiki hao walikuwa Daudi na Bakari.

5. Soma habari ifuatayo kwa umakini, kisha jibu maswali yanayofuata

Hamisi ni mwanafunzi wa darasa la saba katika shule ya"Msingi Upendo. Anaishi na bibi yake katika kijiji cha Muungano. Kijiji hicho kipo karibu na Hifadhi ya wanyama ya Ruaha.

Siku moja Jumamosi, Hamisi na bibi yake walijihimu kuelekea shambani. Wakiwa wanakaribia kufika shambani, Hamisi aliwaona wanyama wawili kwa mbali wakitembea kuelekea upande waliokuwa wakielekea wao.

Maswali . 

  1. Hifadhi ya wanyama ya Ruaha ipo jiranl na MAI gani?
  2. Hamisi anaishi na nani kijijini kwao?
  3. Ni kitu gani walikiona Hamisi na bibi yake wakiwa wanakaribia kufika shambani?
  4. Hamisi ni mwanafunzi wa darasa la ngapi?
  5. Shule aliyosoma Hamisi ililtwaje?

6. Andika vipengele vinavyokosekana katika kadi ye mwaliko ifuatayo:

MWALIKO WA SHEREHE .

YA MAHAFALI

Wanafunzi wa Darasa la Saba

wa Shule ya Msingi Tumaini

Wanayo furaha kukualika

(i) . . . . . . . . . . . . . . . . . .

(ii) . . . . . . . . . . . . . . . . . ..

Itakayofanyika

(iii)   . . . . . . . . . . . . . . . . . . . ..

Kwenye viwanja vya mpira vya shule yetu

Kuanzia (iv) . . . . . . . . . . . . . . . . . . . ..

(v) . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 74  

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 74  

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS  TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

HALMASHAURI YA MANISPAA YA KINONDONI

MTIHANI WA UTAMILIFU DARASA LA VII

01. KISWAHILI

Muda: Saa 1:40 Agosti, 2024

MAELEKEZO

1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali sita (6).

2. Jibu maswali yote kwenye nafasi ulizopewa.

3. Sehemu A na B zina alama ishirini (20) kila moja na sehemu C ina alama kumi (10).

4. Majibu yote yaandikwe kwa kalamu yenye wino wa bluu au mweusi, isipokuwa katika michoro ni lazima kutumia penseli.

5. Vifaa vya mawasiliano havitakiwi katika chumba cha mtihani.

6. Andika Namba yako ya Mtihani na Jina la Shule yako katika kila ukurasa sehemu ya juu upande wa kulia.

KWA MATUMIZI YA MTAHINI TU
NAMBA YA SWALI ALAMA SAHIHI YA MTAHINI
1

2

3

4

5

6

JUMLA

SAHIHI YA MHAKIKI



SEHEMU A: (Alama 20)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1. Sikiliza kwa makini hadithi utakayosomewa na msimamizi, kisha jibu kipengele cha (I – V) kwa kuchagua herufi ya jibu sahihi na kuiandika katika kisanduku ulichopewa.

I. Mvua alijigamba ana faida gani? _______________

  1. husababisha vifo vya watu na mifugo
  2. huweza kusababisha ukame 
  3. huipa maji mimea na mifugo
  4. husababisha madhara 
  5. huweza kusababisha madaraja kujengwa

II. Mvua isiponyesha kwa wakati husababisha nini? _______________

  1. mafuriko 
  2. ukame 
  3. vifo vya watu na mifugo
  4. kilimo kuendelea vizuri 
  5. pato la taifa kuongezeka

III. ______________ ni matone ya maji ambayo hudondoka kutoka kwenye mawingu.

  1. Mito 
  2. Chemchemi
  3. Mvua 
  4. Maporomoko 
  5. Ukame

IV. Madhara gani ambayo yanaweza kutokea endapo mvua itanyesha sana? ______

  1. ukosefu wa maji 
  2. vita vya mara kwa mara 
  3. kilimo kuendelea vizuri 
  4. kuharibu mimea, nyumba, barabara na madaraja
  5.  uzalishaji kuongezeka 

V. Kutokana na hadithi uliyosomewa, ni kitu gani kimetajwa kuongeza pato la taifa?

  1. kilimo 
  2.  mifugo 
  3. uvuvi 
  4. ujenzi wa barabara na madaraja 
  5. mvua

2. Katika kipengele (I – X) chagua jibu sahihi kisha andika herufi yake katika kisanduku ulichopewa.

I. Azizi alisafiri siku nzima kutoka Arusha kwenda Musoma. Silabi iliyopigiwa mstari inawakilisha nini? ____________

  1. nafsi 
  2. wakati 
  3. hali 
  4. awali 
  5. mzizi wa neno

II. Walimu wanafundisha masomo yote kwa bidii. Mwaka jana walimu wamefanya nini?

  1. Walimu watafundisha masomo yote kwa bidii
  2. Walimu wamefundisha masomo yote kwa bidi
  3. Walimu walifundisha masomo yote kwa bidii 
  4. Walimu hufundisha masomo yote kwa bidii
  5. Walimu wanafundisha masomo yote kwa bidii

III. Neno lipi ni tofauti na mengine kati ya haya yafuatayo? ______________

  1. Gauni 
  2. Baibui 
  3. Shati 
  4. Buibui 
  5. Suruali

IV. Upi ni muundo sahihi wa sentensi hii? “Mjomba wangu ameuza gari lake” _____

  1. N+V+T+E 
  2.  N+W+T+N+V
  3.  N+V+T+W+V 
  4.  T+V+T+W+V
  5.   N+V+T+N+V

V. Mwanafunzi alisema “Kitabu hiki ni changu” Ipi ni kauli taarifa ya sentensi hii?

  1. Mwanafunzi alisema kwamba kitabu kile ni chake
  2. Mwanafunzi alisema kwamba kitabu hiki ni chake
  3. Mwanafunza alisema kitabu hiki ni changu
  4. Mwanafunzi alisema kitabu changu hiki
  5. Mwanafunzi alisema kuwa nipe kitabu changu

VI. Usimdharau mtu mwingine; ni vema kuchukua tahadhari kwa kila jambo. Methali ipi inasadifu maelezo haya? _______________

  1. Kikulacho ki nguoni mwako
  2. Baya lako si jema la mwenzako
  3. Usichezee maji yaliyotuama
  4.  Usiache mbachao kwa msaada upitao 
  5. Heri nusu shari kuliko shari kamili

VII. Chasambi ameingizwa mjini kwa mara ya kwanza. Nini maana ya nahau “ingizwa mjini?” ______________

  1. aliingizwa mjini kwa pupa 
  2. alilazimishwa kuingia mjini
  3. alitapeliwa 
  4. aliuona mji kwa mara ya kwanza 
  5. aliletwa mjini

VIII. Ukanushi wa sentensi, “Jua liliwaka sana” ni upi? _______________

  1. Jua halikuwaka sana 
  2. Jua halijawaka sana
  3. Jua haliwaki sana 
  4. Jua halitawaka sana 
  5. Jua huwaka sana

IX. “Kibatari” ni jibu la kitendawili kipi? _______________

  1. Amefika kabla ya mjumbe
  2. Jini mnywa damu haangazi bila damu 
  3. Anaangaza dunia nzima
  4. Gari langu halitumii mafuta ya mwarabu 
  5. Nakipenda lakini sikioni

X. Katika maneno yafuatayo ni neno lipi lina maana zaidi ya moja? ___________

  1. Nanasi 
  2. Jeshi 
  3. Hema 
  4. Majani
  5.  Nyekundu

3. Oanisha misemo Kifungu A na maana zake katika Kifungu B kwa kuandika herufi ya jibu sahihi.

Kifungu A

Majibu

Kifungu B

I. Maisha ya utusitusi

[    ]

A. Mpaka asubuhi

B. Maisha yasiyo kuwa na matumaini

C. Ugomvi mkali

D. Arusi kubwa

E. Zawadi na sherehe

F. Shida, dhiki na taabu za maisha

G. Baridi kali

H. Neema na zawadi kubwa

II. Baridi yenye mzizimo

[    ]

III. Mpaka liamba

[    ]

IV. Ukali wa maisha

[    ]

V. Arusi ya ndovu kumia mwanawe

[    ]

SEHEMU B: (Alama 20)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

4. Chunguza muundo huu wa barua kisha Jaza sehemu zilizoachwa wazi katika kipengele I – V

I. _____________________

Tarehe

II. _______________________________

III. _______________________________

Barua yenyewe

IV. _______________________________

V. __________________________

5. Soma kwa makini shairi kisha jibu maswali katika kipengele cha I – V kwa kundika jibu sahihi katika nafasi iliyoachwa wazi.

SHAIRI

1. Vipo vya kupuuzia, si elimu kwa mtoto,
Elimu kutupatia, ndio ngao yetu nzito,
Viongozi kukazia, sera zilizo mvuto,
Elimu izingatiwe, haki ya sisi watoto.

2 Haki yetu tupatie, shuleni tupelekeni,
Shuleni tujiendee, tusibaki mtaani,
Urithi tufurahie, hizo siku za usoni,
Elimu izingatiwe, haki ya sisi watoto.

3. Haki yetu ni elimu, wazazi zingatieni,
Ni suala la muhimu, walezi changamkeni,  
Bure msingi elimu, walezi tusikieni,
Elimu izingatiwe, haki ya sisi watoto.

Maswali

I. Shairi hili linahusu nini? __________________________________________

II. Shairi hili limetumia aina gani ya kituo? _____________________________________

III. Vina vya kati na vya mwisho katika ubeti wa tatu ni vipi? _______________________

IV. Ubeti wa pili una jumla ya mizani ngapi? _____________________________________

V. Shairi hili ni la aina gani? _________________________________________________

SEHEMU C: (Alama 10)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

6. Soma sentensi zifuatazo kisha uzipange kwenye mtiririko ulio sahihi kwa kutumia herufi A, B, C, D na E.

I. Siku moja Jumamosi, Busara na bibi yake walijihimu kuelekea shambani. [    ]

II. Busara ni mwanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Ving’awe [    ]

III. Wakiwa wanakaribia shambani, Busara aliwaona wanyama wawili kwa mbali

wakitembea kuelekea upande waliokuwa wakielekea wao. [    ]

IV. Anaishi na bibi yake katika kijiji cha Nakauga [    ]

V. Kijiji hicho kipo karibu na hifadhi ya wanyama ya Mkomazi [    ]

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 59  

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 59  

Namba Ya Mtahiniwa . . . . . . . . . . . . . . . . .

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA 

HALMASHAURI YA MANISPAA YA TEMEKE 

MTIHANI WA UTAMILIFU KWA DARASA LA VII 

SOMO : KISWAHILI

MUDA SAA 1:30 MWAKA 2024

MAELEKEZO

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C Zenye jumla ya maswali 6.
  2. Jibu maswali yote 
  3. Majibu yote yaandikwe kwenye nafasi ulizopewa katika karatasi ya maswali 
  4. Majibu yote yaandikwe kwa kutumia Kalamu ya wino wa bluu au nyeusi 
  5. Simu za mkononi haziruhusiwi katika chumba cha mtihani 
  6. Andika namba yako ya mtihani sehemu ya juu upande wa kulia kwenye kila kurasa
KWA MATUMIZI YA MTAHINI TU
NAMBA YA SWALI ALAMA SAHIHI YA MTAHILI
1.

2.

3.

4.

5.

6.

JUMLA

SAHIHI YA MHAKIKI

SEHEMU A( ALAMA 20)

1. SIKILIZA KWA MAKINI HABARI UTAKAYO SOMEWA NA MSIMAMIZI KISHA JIBU SWALI (i) - (v) KWA KUCHAGUA HERUFI YA JIBU SAHIHI

(i) Uharibifu wa mazingira husababisha upungufu, wa rasilimali. Kama vile . . . . . . . . . . . . . . . [    ]

  1. Mbao
  2. chakula
  3. Maji
  4. Nafaka
  5. Binaadamu

(ii) Ongezeko la joto duniani husababisha  . . . . . . . . . . . . . . . [    ]

  1. Magonjwa
  2. ukataji miti
  3. Miundombinu mibovu
  4. harufu mbaya
  5. ukame.

(iii) Kutokana na habari uliyosikiliza uharibifu wa mazingira husababishwa na vitendo vya  . . . . . . . . . . . . . . . [    ]

  1. binadamu
  2. Wanyama
  3. Mimea
  4. Ndege
  5. Ongezeko la joto.

(iv) Utiririshaji wa maji machafu kwenye vyanzo vya maji husababisha magonja kwa binadamu Kama vile . . . . . . . . . . . . . . . [    ]

  1. Kichomi
  2. dondakoo
  3. Kipindupindu
  4. Kiriba tumbo
  5. ukichaa.

(V) Kichwa cha habari uliyosomewa Kinawezakuwa . . . . . . . . . . . . . . . [    ]

  1. Matokeo ya joto
  2. Uharibifu wa Mazingia
  3. Kukauka kwa nyasi
  4. Kukata miti
  5. utiririshaji wa maji.

2 CHAGUA HERUFI YA JIBU LILILO SAHIHI

 (i) utungo wa kifasihi unaotumia lugha ya mkato kuwasilisha ujumbe kwa hadhira huitwa.

  1. Sanaa
  2. Fasihi
  3. Shairi
  4. lnsha
  5. Methali.

 (ii) Katika kitabu cha Shaban Robert mashairi yake yana mishororo minne minne. kisawe cha nen mshororo ni  . . . . . . . . . . . .

  1. beti
  2. Mistari
  3. Silabi
  4. Mizani
  5. Sauti

(iii) Maendeleo yetu yanakuwa kwa Kasi. Ni neno gani limetumika kama kivumishi kati ya yafuatayo?

  1. kasi
  2. Yanakua
  3. Maendeleo
  4. Kwa
  5. yetu.

(iv) Emao alinitembelea jana kwa . . . . . . . . . . . . kunijulia hali. Ni neno gani linakamilisha sentensi hii kati yafuatayo?

  1. dhumuni la
  2. Mathumuni ya
  3. thumuni La
  4. Madhumuni ya
  5. Udhumuni wa

(v) Nimefika shuleni mapema. Pendo alimwambia bosi wake, Ukanushi wa Sentensi hii ni upi?

  1. Sikufika shuleni mapema
  2. sijafika Shuleni mapema
  3. hatujafika shuleni
  4. Nimefika shuleni kwa kuchelewa
  5. tumefika shuleni kwa kuchelewa

(vi) Neno lipi ni jumuishi kwa maneno haya " mshale, panga, kisu na upinde"?

  1. zana
  2. Nyenzo
  3. Vyuma
  4. Pembejeo
  5. Nyara

(vii)Yeye alisema "siwezi kuja kwenu." Kauli taarifa ya sentensi hii ni ipi kati ya zifuatazo?

  1. Yeye alisema kwamba haji kwenu
  2. yeye alisema kwamba sitakuja Kwenu
  3. yeye alisema hataweza kuja kwenu
  4. yeye alisema kuwa hawezi kuja kwenu
  5. yeye alisema kwamba hawezi kuja kwetu.

(viii) Neno lipi kati ya yafuatayo Tina maana sawa na neno "koroboi?

  1. Taa
  2. Kibatari
  3. chemli
  4. Karabai
  5. Mshumaa.

(ix) Babu alikuwa anakula ugali jana jioni. Katika sentensi hii neno lipi kati ya yafuatayo limetumika kama Kitenzi Kisaidizi?

  1. anakula
  2. baba
  3. alikuwa
  4. jana
  5. jioni

(x) Katika neno "wanasherehekea" kiambishi gani huonesha njeo?

  1. -na-
  2. -ashe-
  3. -ana-
  4. Shereh
  5. -wan-

3. OANISHA SENTENSI ZA KIFUNGU 'A' NA KIFUNGU 'B' ILI  KULETA MAANA ILIYOKUSUDIWA KWA KUANDIKA HERUFI YA JIBU SAHIHI  KWENYE KISANDUKU

KIFUNGU A:

KIFUNGU B

i/ Upepo unaovuma kwa kishindo na kuleta madhara huitwa  [     ]

ii/kitu chenye thamani na heshima kubwa anachopewa mtu baada ya kufanya Kazi nzuri au jambe Fulani.  [     ]

iii/ Mahali ambapo wavulana waliopevuka hufundishwa mambo ya utuuzima.  [     ]

iv/ Mtu wa kale.  [     ]

v/ Tamko la kumtakia mtu heri wakati wa kuagana usiku, usiku mwema.  [     ]

  1. MKONGEKWA
  2. ALAMSIKI
  3. KIMBUNGA
  4. TUZO
  5. DHAHABU
  6. MHENGA
  7. JANDONI

 

SEHEMU B (ALAMA 20)

Jibu Maswali Yote Katika Sehemu Hii

4. KAMILISHA SENTENSI ZIFUATAZO KWA KUJAZA NAFASI ZILIZOACHWA WAZI

i............................... ni mtu anayefanya uamuzi katika mchezo wa soka

ii. Mtu mwenye ujuzi wa kutunga mashairi huitwa ...................................

iii................................... hutumika kuhifadhi mshale

iv. Andika neno lenye maana sawa jimbi .............................................................  

v. Kanusha sentensi ifuatayo. "Kiranja amewahi Shute".........................................  

5. SOMA SHAIRI! LIFUATALO KISHA JIBU KIPENGELE CHA i -v

SHAIRI

Tukiwa ndugu watatu, Modi, Iddi na Waziri
Pamoja na dada zetu Mima na Hindu, Mazuri
Na Momo mkubwa wetu, kwa painoja twakariri
Tuwaheshimu wazazi, Pamoja na waalimu.

Tukiwa sisi watoto, Sote tuwe na adabu
Ukichapwa kwa kikoto, baba akikuadhibu
Usilitilete utoto, utakuja pata tabu
Tuwaheshimu wazazi, Pamoja na waalimu

MASWALI

  1. Shairi hili lina beti ngapi  . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
  2. Vina Vya mwisho vya ubeti wa kwanza ni . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
  3. Kibwagizo katika shairi hili ni kipi . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
  4. shairi hili lina mizani ngapi  . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
  5. Shairi hili ni la muundo wa  . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

SEHEMU C (Alama 10)

Jibu Swali La 6

6. Soma Kwa makini habari ifuatayo kisha jibu swali la (i-v) Kwa Kuweka herufi ya jibu sahihi

Zamani za kale sehemu nyingi duniani zilikuwa na misitu. Maji na ardhi nzuri kwa kilimo.Mfano wa Sehemu hizo ni pori la Geita mkoani Geita. Watu wa jamii ile walilima mashamba madogo lakini walipata mavuno mazuri. Ilikuwepo misitu mikubwa iliyokuwa na miti ya mitundu, mipodo na mibanga. Miti ilikuwa ikitikia hatua ya kukomaa bila kuharibiwa licha ya kutoa mazao mengi Misitu iliwaletea watu wa jamii ile mvua ya kutosha kila mwaka. Wanyama na ndege walizaliana kwa wingi katika misitu hiyo. Wakati huo watu walikuwa wachache na mahitaji yao ya misitu yalikuwa machache pia, kwa hiyo kila kitu cha asili kilijitosheleza mahitaji ya kila mtu kwa kila siku. Je, baada ya mfumo wa soko huria na mfumo wa mawasiliano kwa teknolojia ya kisasa kuna nini?

MASWALI

  1. Mtu anaposema kila kitu cha asili kilijitosheleza mahitaji ana maana gani    . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .  . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
  2. Katika msitu ulizungumziwa miti gani ili kuwepo kwa wingi   . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .  . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
  3. Kichwa cha habari hii kinafaa kiwe  . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .  . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
  4. Misitu iliwaletea nini watu wa jamii ile  . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .  . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
  5. Katika nchi yetu ya Tanzania kuna aina ngapi za misitu . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .  . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 54  

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 54  

JINA LA MTAHINIWA . . . . . . . . . . . . 

NAMBA YA MTAHINIWA . . . . . . . . . . . . . . 

OFISI YA RAIS-TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, HALMASHAURI YA WILAYA YA MPWAPWA 

MTIHANI WA UTAMILIFU DARASA LA SABA APRIL 2024

SOMO: 01 - KISWAHILI

Muda: Saa 1:40

Maelekezo: 

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye maswali sita (06)
  2. Jibu maswali yote katika kila sehemu. 
  3. Soma maelekezo yote yaliyoko katika kila swali iii kujibu vipengele husika kwa usahihi. 
  4. Jaza taarifa zako (jina, shule nk) katika nafasi uliyopewa hapo juu. na kwenye nafasi uliyopewa katika kila ukurasa. 
  5. Tumia penseli kuchora kama kutakua na swali la kuchora, na kalamu ya wino wa bluu au mweusi kwa maj ibu yote ya kuandika. 
  6. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi ndani ya chumba cha upimaji.

SEHEMU A (Alama 20 )

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1. Sikiliza kwa makini habari utakayosomewa na msimamizi wako kisha jibu kipengele cha i-v kwa kuchagua herufi ya jibu sahihi

(i) Msimuliaji alipokuwa juu ya mti aliona nini? 

A. Mbwamwitu B. Majani C. Matawi D. Nyoka E. Mto [     ]

(ii) Msimuliaji alipotupa jicho pembeni mwa mti aliona nini? 

A. Kibanda B. Nyumba C. Mto D. Mtu E. Simba [     ]

(iii) Msimuliaji alikuwa anaelekea kijiji gani? 

A. Mtini B. Kibandani C. Nyumbani D. Mkoka E. Shambani [     ]

(iv) Mnyama gani alikaa karibu na kibanda chakavu? A. Nyoka B. Mbwamwitu C. Mamba D. Kima E. Simba [     ]

(v) Nahau “tupa jicho” maana yake ni nini? A. Sikia B. Angalia C. toa jicho D. Kodoa macho E. Kimbia [     ]

2. Chagua jibu sahihi kisha uandike herufi ya jibu hilo katika visanduku ulivyopewa ili kukamilisha kipengele cha (i )-(x)

(i) Mama alipanga vyombo kabatini. Kinyume cha neno panga ni ipi kati yafuatayo? 

A. Pangisha B. Pangusa C. Pangua D. Panua E. Pango [     ]

(ii) Nomino ipi inatokana na kubadilishwa kwa kitenzi lima? 

A. Limisha B. Limiana C. Limika D. Mkulima E. Kalime [     ]

(iii) Mama amekwenda safari atafika kesho jioni . Neno lililopigiwa mstari ni aina gani ya neno? 

A. Nomino B. Kielezi C. Kiwakilishi D. Kitenzi E. Kiunganishi [     ]

(iv) Mtoto alinunuliwa zawadi. Kitenzi alinunuliwa kipo katika kauli gani? 

A. Kutendana B. Kutendwa C. Kutenda D. Kutendwa E. Kutendesha [     ]

(v) Yupi kati ya wafuatao anafanya kazi ya kuazimisha vitabu katika maktaba? 

A. Mkutubi B. Muhtasi C. Mhandisi D. Nahodha E. Mhadhiri [     ]

(vi) Pale . . . . . . panapofuka moshi. 

A. Ndio B. Ndiyo C. Ndivyo D. Ndimo E. Ndipo [     ]

(vii) Katika neno “ Shanga” Mzizi wa neno ni upi? 

A. shanga B. sha C. sha D. shang E. a [     ]

(viii) Sisi ni wanafunzi wa darasa la saba. Neno sisi linawakilisha nafsi ya na ngapi? 

A.Nafsi ya kwanza umoja B. Nafsi ya tatu wingi C. Nafsi ya tatu umoja D. Nafsi ya kwanza wingi E. Nafsi ya pili wingi [    ]

(ix) Baba alimwagiza Juma, “ Nenda kanunue mbuzi sokoni”. Sentensi hii ipo katika kauli gani? 

A. Tata B. Taarifa C. Mazoea D. Halisi E. Desturi [    ]

(x) Katika maneno yafuatayo neno lipi halilandani na mengine ? 

A. Ndovu B. Mbogo C. Faru D. Korongo E. Nyumbu [     ]

3. Oanisha Sehemu A na sehemu B ili kukamilisha kazi ya fasihi kwa kuandika herufi ya jibu sahihi katika kipengele cha (i )- (v)

NA

SEHEMU A

JIBU

SEHEMU B

i .

Piga maji

A. Anajua

ii .

Methali inayotumika kuonya mtu asiyesikiliza ushauri wa wakubwa

B. Maji na Maziwa

iii .

Kiti cha dhahabu akikaliwi na watu

C. Maziwa na tui la nazi

iv .

Asiyeuliza

D.Kunywa maji

V .

Ukiona njigi utadhani njege, ukiona njege utadhani njigi.

E .Jua

F. Hana ajifunzalo

G. Moto

H. Kunywa Pombe

I. Asiyesikia la mkuu huvunjika guu.

J. Kunywa chai

SEHEMU B: ( Alama 20)

4. Panga sentensi zifuatazo kwa mtiririko sahihi ili zilete maana kamili iliyokusudiwa kwa kuzipa herufi A,B,C,D na E.

  1. Kijiji hicho kipo karibu na hifadhi ya wanyama ya Mkomanzi.
  2. Siku moja, Busara na bibi yake walijihimu kuelekea shambani.
  3. Anaishi na bibi yake katika kijiji cha Mwendokasi
  4. Wakiwa wanakaribia kufika shambani, waliona wanyama wawili wakitembea kuelekea upande waliokuwa wanaelekea wao.
  5. Busara ni mwanafunzi wa darasa la saba katika Shule ya msingi Tumaini.

5. Soma Shairi lifuatalokisha jibu maswali kipengele cha i -- v.

 Shairi

1. La mgambo likilia, ujue kuna jambo,

Ndugu kwenye familia, hutakiwi kenda kombo, 

Vijana wazee pia, lisikilize hili jambo,

Ni hatari kutumia dawa hizi za kulevya.


2. Dawa tukizitumia, haifai asilani, 

Jamii inakataa, hata vitabu vya dini,

Madhara yameshajaa, Kila pembe duniani, 

Ni hatari kutumia dawa hizi za kulevya.

MASWALI

  1. Taja vina vya kati na vina vya mwisho katika ubeti wa pili . . . . . . . . . . . .
  2. Mtu anayetunga mashairi anaitwa malenga. Je mwalimu wa malenga anaitwaje? . . . . . . . . . . .
  3. Shairi hili lina jumlaya beti ngapi? . . . . . . . . . . . .
  4. Kituo cha shairi ni kipi? . . . . . . . . . . . . . . . . .
  5. Pendekeza kichwa cha shairi hili . . . . . . . . . . . . . .

SEHEMU C: UTUNGAJI (Alama 10)

6. Andika simu ya maandishi kwa Kaka yako anayeitwa Juma Sioni S.L.P 2015 Shinyanga, ukimtaarifu kuwa Mama yenu mgonjwa amelazwa. Wewe tumia jina la Chausiku Sioni

JUMA SIONI, S.L.P 2015, SHINYANGA

i. .. . . . . . . . . . . . . . . . . .

ii. .. . . . . . . . . . . . . . . . . .

iii. .. . . . . . . . . . . . . . . . .

iv. .. . . . . . . . . . . . . . . . .

v. .. . . . . . . . . . . . . . . .

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 46  

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 46  

OFISI YA RAIS-TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

MTIHANI WA UPIMAJI DARASA LA SABA MACHI 2024 

SOMO: 01 - KISWAHILI

Muda: Saa 1:40

Maelekezo: 

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye maswali sita (06)
  2. Jibu maswali yote katika kila sehemu. 
  3. Soma maelekezo yote yaliyoko katika kila swali iii kujibu vipengele husika kwa usahihi. 
  4. Jaza taarifa zako (jina, shule nk) katika nafasi uliyopewa hapo juu. na kwenye nafasi uliyopewa katika kila ukurasa. 
  5. Tumia penseli kuchora kama kutakua na swali la kuchora, na kalamu ya wino wa bluu au mweusi kwa maj ibu yote ya kuandika. 
  6. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi ndani ya chumba cha upimaji.

SEHEMU A (Alama 20 )

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1. Sikiliza kwa makini habari utakayosomewa na msimamizi wako kisha jibu kipengele cha i-v kwa kuchagua herufi ya jibu sahihi

(i) Kwa mujibu wa habari uliyosikiliza nini maana ya maisha? A. Maisha ni silaha B. Maisha ni vita C. Maisha ni uhai D. Maisha ni kuishi E. Maisha ni kusoma [     ]

(ii) Kwanini mwanafunzi upo shuleni? A. ili kupambana B. ili kunoa silaha C. ili ukue vyema D. ili uweze kujua maana ya maisha E. ili kucheza na wenzako [     ]

(iii) Ni wapi mtu huweza kujifunza maana ya maisha? A. shuleni B. chuoni C. hakuna sehemu yoyote D. chuoni na shuleni E. kanisani [     ]

(iv) Ikiwa mtu anatamani kuwa na nyumba,gari au mali yampasa kufanya nini? A. kuishi B. kwenda shule C. kuhamia mjini D. kuanzisha biashara E. kupambana [     ]

(v) Kwanini mnasisitizwa kutumia vyema muda wenu muwapo shuleni? A. ili kufaulu vyema B. ili kuepuka maisha C. ili kuyashinda maisha D. ili kutojuta baadaye E. ili kukua vyema

2. Chagua jibu sahihi na kisha uandike herufi ya jibu sahihi hilo katika sehemu ya kujibia.

(i) Walifanya kazi ile bega kwa bega hadi ilipokamilika. Nahau “bega kwa bega” inafafanuliwa na kifungu kipi cha maneno? A. kujituma sana B. walishirikiana kwa pamoja C. walitumia nguvu nyingi D. walifanya kwa uzalendo E. walitumia maarifa sana [     ]

(ii) Nahau ipi yenye maana ya “kuzama au kuogelea majini?” A. piga maji B. zama maji C. piga mbizi  D. piga kumbo E. piga zengwe [     ]

(iii) “Utakapowasili hapa utahutubia wananchi”. Mzungumzaji ametumia nafsi gani kati ya hizi? A. nafsi ya pili umoja B. nafsi ya kwanza wingi C. nafsi ya kwanza umoja D. nafsi ya tatu umoja E. nafsi ya tatu wingi [     ]

(iv) “Yanga wamefuzu katika hatua ya mtoano”. Kauli hiyo inawakilisha nafsi ipi kati ya hizi zifuatazo? A. nafsi ya kwanza wingi B. nafsi ya pili wingi C. nafsi ya kwanza umoja D. nafsi ya tatu umoja E. nafsi ya tatu wingi [     ]

(v) “Aminata amefaulu mtihani”, mwalimu alisema. Hiyo ni aina gani ya kauli kati ya hizi zifuatazo? A. mazoezi B. halisi C. tata D. taarifa E. tendwa [     ]

(vi) “Juma anasoma ingawa Neema anacheza”. Neno “ingawa” ni aina gani ya neno? A. kitenzi B. kihisishi C. kiiunganishi D. kielezi E. kiwakilishi [     ]

(vii) Rehema mama yake Mary. Neno linalokamilisha sentensi hii ni lipi? A. siyo B. sio C. sie D. siye E. si [     ]

(viii) Hapa alipozikwa hayati Ali Hassan Mwinyi. A. ndiko B. ndimo C. nipo D. ndipo E. ndicho [     ]

(ix) “Sitakubali kuondoka”. Neno “sitakubali” liko katika hali gani? A. ukanushi B. mazoea C. timilifu D. endelevu E. halisi [     ]

(x) “Damu ni nzito kuliko maji”. Methali hii inahusiana na ipi kati ya hizi zifuatazo? A. mchumia juani hulia kivulini B. penye nia pana njia C. mla nawe hafi nawe ila mzaliwa nawe D. mbio za sakafuni huishia ukingoni E. baada ya dhiki faraja [     ]

3. Katika sehemu hii oanisha methali zinazofanana kutoka sehemu A na B kwa kuandika herufi ya jibu sahihi

Sehemu A

Sehemu B

  1. Usipoziba ufa, utajenga ukuta [     ]
  2. Mchumia juani, hulia kivulini [     ]
  3. Mvumilivu hula mbivu [     ]
  4. Mtoto umleavyo, ndivyo akuavyo [     ]
  5. Mchagua nazi huambulia koroma [     ]
  1. Mdharau mwiba, mguu huota tende
  2. Mchagua jembe, si mkulima
  3. Samaki mkunje, angali mbichi
  4. Polepole ndio, mwendo
  5. Jembe halimtupi, mkulima
  6. Kidole kimoja hakivunji, chawa
  7. Umoja ni nguvu, utengano ni dhaifu

SEHEMU B (ALAMA 20)

4. Katika sehemu hii kamilisha sentensi kadri ulivyoulizwa kwenye kipengele husika

(i) Meza, kabati, kiti na kitanda kwa neno moja huitwaje?                                                

(ii) Abdalah alitapanya mali za urithi. Kinyume cha neno tapanya ni nini?                                                

(iii) “Kazi ya Halima ni ya kijungujiko”. Kazi ya kijungujiko ni kazi ya aina ipi?                                                

(iv) Kitoto hiki kinacheza kitoto. Neno lililopigiwa mstari limetumika kama aina ipi ya maneno?                                                    

(v) Nashon hufanya kazi ya kuhifadhi na kuazimisha vitabu kwa wasomaji katika maktaba ya mkoa. Je, Nashon ni nani?                                               

5. Soma shairi lifuatalo kisha jibu maswali yanayofuata

Kaitwa mahakamani, popo kujibu shitaka, 

Hakimu naye makini, hadhira shauku tua, Atakiwa abaini, 

kwa ulimi kutamka, 

Ajitetee bayana, ni mnyama au ndege

Hakimu nashukuru, shitaka kunisomea, 

Hakimu nashukuru, shitaka kunisomea, 

Sina jadi na kunguru, ila na pundamilia,

Mimi ni mnyama huru, amini ninakwambia,

Tukidaiwa ushuru, kwa Wanyama nalipia.

Ni kweli popo napaa, na mabawa nimepata, 

Lakini mimi nazaa, hilo halina utata,

Nazaa na kunyonyesha, sina undugu na bata

Wale wanaopotosha , niwaonyeshe matiti.

 Maswali

(i) Ni sababu ipi inayomfanya popo akatae ya kuwa yeye si ndege?                                      

(ii) Mstari wa mwisho katika kila ubeti wa shairi huitwaje?                                   

(iii) Katika ubeti wa pili popo anasema, “sina jadi na kunguru”, usemi “sina jadi” una maana gani?                                          

(iv) Kutokana na shairi hili, unadhani ni tuhuma gani zilikua zinamkabili popo?                                                    

(v) “Hakimu makini, hadhira shauku tua”. Unaelewa nini kuhusiana na neno hadhira?                                             

SEHEMU C : UTUNGAJI (ALAMA 10)

6. Ichunguze barua rasmi ifuatayo kisha jibu maswali yanayofuata;-

Tafadhali husika na barua hii.


Shule ya Msingi Ugele,

S.L.P. 165,

RINGO

Mimi ni mwanafunzi wa darasa la saba katika shule yako. Ninaomba ruhusa ya kushiriki mashindano ya kanda ambayo yatafanyikia katika uwanja wa Samora siku ya Alhamis. Mashindano hayo yataanza mnamo saa 2:00 asubuhi na kuhitimishwa saa 8:30 mchana.

Ahsante

Baada ya kukamilisha kuiandika barua hiyo Lashack aliambiwa na mwalimu wake kuwa barua yake ina mapungufu mengi na kuifanya ikose sifa za kuitwa barua rasmi. Taja vipengele vitano vinavyokosekana katika barua hii.

  1.                                                    
  2.                                                    
  3.                                                    
  4.                                                    
  5.                                                    

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 43  

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 43  

OFISI YA RAIS - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKAKI ZA MITAA, HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA

MTIHANI WA UPIMAJI DARASA LA SABA APRIL 2024 

SOMO: 01 - KISWAHILI

Muda: Saa 1:40

Maelekezo: 

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye maswali saba (06). 
  2. Jibu maswali yote katika kila sehemu. 
  3. Soma maelekezo yote yaliyoko katika kila swali iii kujibu vipengele husika kwa usahihi. 
  4. Jaza taarifa zako (jina, shule nk) katika nafasi uliyopewa hapo juu. na kwenye nafasi uliyopewa katika kila ukurasa. 
  5. Tumia penseli kuchora kama kutakua na swali la kuchora, na kalamu ya wino wa bluu au mweusi kwa maj ibu yote ya kuandika. 
  6. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi ndani ya chumba cha upimaji.

SEHEMU A (Alama 20 )

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1. Sikiliza kwa makini hadithi utakayosomewa na msimamizi, kisha jibu kipengele cha (i)- (v), kwa kuchagua herufi ya jibu sahihi na uiandike katika parandesi.

i) Mutalemwa ni kijana mwenye umri wa miaka mingapi?

A: Miaka kumi B: Miaka nane C: Miaka tisa D: Miaka saba E: Miezi kenda [     ]

ii) Nini maana ya msemo “aghalabu” kama ulivyotumika katika habari?

A: Mara nyingi B: Mara chache C: Mara moja D: Angalau E: Kwa hasira [     ]

ii) Nani alimuokoa Mutalemwa alipokuwa akiraruliwa na mbwa?

A: Mama yake B: Mutashobya C: Mutahaba D: Kokubanza E: Kyaruzi [     ]

iv) Mutalemwa alitibiwa kwa muda gani?

A: Siku sita B: Siku mbili C: Wiki tatu D: miezi mitatu E: Siku tatu [     ]

v) Mbwa alimrarua Mutalemwa maeneo gani ya mwili wake?

A: Miguuni na usoni B: Miguuni na mikononi C: Miguuni na shingoni D: Mikononi na kichwani E: Miguuni na kiunoni [     ]

2. Katika kipengele cha (i) – (x), chagua herufi ya jibu sahihi kisha iandike katika parandesi.

i) Hapo kabla Fatuma na Musa walikuwa ni marafiki wakubwa. Ila ilitokea siku moja Musa alimnyima peremende Fatuma. Tangu siku hiyo Fatuma alimkasirikia sana Musa wakawa hawapikiki chungu kimoja. Msemo wenye ukolezo una maana gani?

A: Hawaishi pamoja B: Hawatembei pamoja C: Hawali pamoja D: Hawaelewani E: Hawazungumzi pamoja [     ]

ii) Wenyewe wangeweza kwenda hata ninyi pia mngekwenda. Katika sentensi hii maneno wenyewe na ninyi yametumika kama aina ipi za maneno?

A: Nomino B: Viunganishi C: Viwakilishi D: Vivumishi E: Vielezi [     ]

iii) Watoto wanaopenda kukimbizana barabarani wanaweza kugongwa na magari. Kiarifu cha sentensi hii kipo katika kauli gani?

A: Kutendana B: Kutendwa C: Kendewa D: Kutenda E: Kutendea [     ]

iv) Viongozi wengi walikuwa wakila mlungula ili kutoa huduma ambayo wananchi walipaswa kuipata bure. Lakini tunamshukuru Mhe. Rais kwa kuwatumbua. Nini maana ya nahau kula mlungula?[     ]

A: Kula pesa B: Kula fadhila C: Kutoa huduma bora D: Kupokea rushwa E: Kutoza hela

v) Watoto wanapenda kutazama vikaragosi kwenye runinga. Tungo hiyo ipo katika nafsi gani?

A: Nafsi ya I umoja B: Nafsi ya II umoja C: Nafsi ya III umoja D: Nafsi ya II wingi E: Nafsi ya III wingi [     ]

vi) Methali ipi kati ya zifuatazo ina maana sawa na isemayo;- “Mchakacho ujao haulengwi jiwe”

A: Jiwe moja moja hujenga nyumba ya mawe. B: Jiwe la kutupa ngomani humpiga wako

C: Jina jema hung’aa gizani D: Jino la pembe si dawa ya pengo E: Jina jema ni hazina [     ]

vii) “Teketeke huzaa gumugumu na gumugumu huzaa teketeke.” Mwalimu Manjia aliwataka wanafunzi wategue kitendawili hicho kwa kutumia picha. Ungekuwepo darasani ungechagua picha gani kati ya hizi?

[     ]

viii) Mchomoeni nyoka shimoni. Kuna silabu ngapi katika neno lililopigiwa mstari?

A: Tisa B: Tano C: Sita D: Nane E: Nne [     ]

(ix) Uliponifanyia ubaya ulifurahia sana na kunicheka, sasa na mimi nimekufanyia ubaya huo huo kama ulionifanyia unaona nimekuonea. Ama kweli wahenga walituambia;- . . ...

A: Shukurani ya punda ni mateke B: Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki C: Hakuna masika yasiyokuwa na mbu D: Mtaka cha uvunguni sharti ainame E: Mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu [     ]

x) “Lala chini la sivyo nitakupasua kichwa chako.” Badili kauli hiyo kuwa taarifa.

A: Aliambiwa kuwa lala chini la sivyo angepasuliwa kichwa chake.
B: Aliambiwa kwamba alale chini la sivyo atapasuliwa kichwa chake.
C: Aliambiwa kuwa alale chini vinginevyo angepasuliwa kichwa.
D: Aliambiwa kuwa alale chini vinginevyo angepasuliwa kichwa chake.
E: Aliambiwa kwamba lala chini vinginenvyo nitalipasua kichwa chako. [     ]

3. Oanisha msamiati uliopo katika Orodha A na maana yake iliyopo kutoka Orodha B, kwa kuandika herufi ya jibu sahihi katika nafasi ya majibu.

Na. Orodha A Majibu Orodha B
(i) Mtu anayefanya biashara ya kuuza vitu rejareja
A. Kuli
(ii) Mtu anayetangaza bei na kuuza vitu wakati wa mnada
B. Utingo
(iii) Mtu anayefanya kazi ya kupakia na kupakua mizigo bandarini au forodhani
C. Kondakta
(iv) Chete ifanywayo mara moja kwa juma au mwezi
D. Mpagazi
(v) Mtu anayefanya kazi ya kupakia na kupakua mizigo
kwenye gari.

E. Mchuuzi



F. Mnadi



G. Mnuni



H. Gulio

SEHEMU B (Alama 20)

4. Chunguza picha zifuatazo kisha jibu maswali yote katika kipengele cha (i) – (v) kwa kuandika jibu sahihi katika nafasi zilizoachwa wazi.


i) Jina la tunda linalowakiliswa na herufi A limeundwa na konsonanti ngapi? . . . . . . .
ii) Kuna silabi ngapi katika jina la tunda linalowakilishwa na herufi C? . . . . . . . . .
iii) Zipo irabu ngapi katika jina la tunda linalowakilishwa na herufi B? . . . . . . . . . .
iv) Kuna aina ngapi za irabu katika jina la mnyama anayewakilishwa na herufi D? . . . . . . ...
v) Ukidondosha silabi moja ya jina la samaki anayewakilishwa na herufi E, utapata jina la aina gani ya kifaa? . . . . . . . . . . . . .

5. Soma kwa makini habari ifuatayo kisha jibu maswali katika kipengele cha (i) - (v) kwa kuandika jibu sahihi katika nafasi iliyoachwa wazi.

Omari na Sara wanasoma katika shule ya msingi Kiloleni. Siku moja Omari aliona makala kwenye gazeti la Mwananchi. Akamwita rafiki yake Sara ili waisome pamoja. Makala yenyewe ilihusu utunzaji wa mazingira. Kwa pamoja walisoma vizuri na kujionea umuhimu wa utunzaji wa mazingira. Pia waliona madhara yanayoweza kuwapata ikiwa hawatatunza mazingira kama vile kukumbwa na magonjwa ya mlipuko.

Katika Makala hiyo, kulikuwa na tangazo la mashindano ya uandishi wa insha kuhusu mazingira kwa wanafunzi wote wa shule za msingi. Na mshindi atapewa zawadi ya kutembelea Zanzibar kwenda kujionea mazingira ya mji mkongwe. Omari na Sara kwa pamoja walikata shauri kushiriki shindano hilo ili ndoto yao ya kutembelea Zanzibar itimie. Walishauriana kwenda kwenye maktaba ya shule yao ili wakatafute vitabu vinavyoeleza zaidi kuhusu mazingira. Sara alipata kitabu kilichoitwa “Tutunze tukutunze” Alimuita rafiki yake, “Omari njoo uone hiki kitabu, inaonekana kitakuwa ni jibu la kile tunachokitafuta” Baada ya Omari kukitazama akasema “Swadakta! Hapa sasa ndio penyewe.” Haraka walikwenda chini ya mti kivulini walijisomea hadi pale waliporidhika kwamba wameelewa vizuri. Baada ya kumaliza kusoma kila mmoja aliandika Insha kivyake na kuipeleka kwenye mashindano. Wote waliandika vizuri lakini Sara alijiongeza kwa kuandika hitimisho zuri. Alishauri serikali kuweka sheria kali ili kuwakomesha wachafuzi wa mazingira. Kipengele hicho ndicho kilimfanya Sara aibuke kidedea kwenye shindano.

Maswali

(i) Kwa unavyofahamu wewe, nini maana ya Mazingira? . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
(ii) Omari aliona makala kwenye nini? . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . ... . . . .
(iii) Madhara ya kutotunza mazingira ni pamoja na nini? . . . . . . . . . . . . . . . ... . . . .
(iv) Sara alipata kitabu gani kule maktaba? . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
(v) Unadhani ni kwa nini Sara aliibuka kidedea kwenye shindano hilo? . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

SEHEMU C: (Alama 10)

Umepewa insha yenye sentensi (5) zilizoandikwa bila kufuata mpangilio maalum, zipange sentensi hizo ili zilete mtiririko mzuri wa mawazo kwa kuzipa herufi A-E katika kujibu kipengele cha (i) – (v)

(i) Maendeleo hayo hayakuja kama ndoto bali ni kwa maarifa na juhudi kubwa.
(ii) Katika nchi ya Tanzania, kuna vijiji vingi sana na vingi kati ya hivyo vimepiga maendeleo.
(iii) Hata hivyo bado ipo haja ya kusukuma maendeleo zaidi katika vijiji ambavyo bado vipo nyuma.
(iv) Kwa kufanya hivyo kutasaidia kumwezesha kila mwananchi kufikiwa na huduma za jamii kwa karibu.
(v) Juhudi hizo zilitokana na msukumo wa viongozi wa serikali na kufanya kazi kwa kikoa.

Kisanduku cha majibu

(i) (ii) (iii) (iv) (v)




.

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 36  

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 36  

OFISI YA RAIS - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKAKI ZA MITAA, HALMASHAURI YA MJI WA BARIADI


MTIHANI WA UPIMAJI DARASA LA SABA FEBRUARI 2024 

SOMO: KISWAHILI

Muda: Saa 1:40

Maelekezo

  1. Karatasi hii ina sehemu mbili: A na B zenye jumla ya maswali arobaini na tano
  2. Jibu maswali yote katika kila sehemu. 
  3. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi ndani ya chumba cha mtihani.

SEHEMU A (Alama 35)

Sikiliza kwa makini hadithi utakayosomewa na msimamizi, kisha jibu swali la 1 - 5, kwa kuweka kivuli katika herufi ya jibu lililo sahihi katika karatasi ya kujibia.

1. Kwa mujibu wa habari uliyosomewa, unadhani kina Juju walijuaje kuwa mahali mashua yao ilipogota kuna karibia kukucha?

A: Walisikia sauti za watu B: Walisikia sauti za ndege C: Walisikia sauti za wanyama D: Walisikia jogoo akiwika E: Walisikia jogoo akilia [     ]

2. Imeelezwa kuwa dhoruba ilitokea katika kisiwa gani?

A: Wete B: Pemba C: Nungwi D: Zanzibar E: Unguja [     ]

3. Kama umesikiliza kwa makini habari uliyosomewa, tuambie jina la mtu aliyekuwa wa kwanza kuhisi mahali mashua yao ilipogota palikuwa panakaribia kukucha.

A: Janja B: Jojo C: Jaja D: Juju E: Jeje [     ]

4. Baada ya dhoruba kutokea, vyombo vingi walivyosafiria wavuvi vilienda mrama. Nini maana ya msemo kwenda mrama?

A: Kupoteza nguvu B: Kwenda kasi C: Kupoteza mwelekeo D: Kwenda taratibu E: Kwenda ovyoovyo [     ]

5. Kwa mujibu wa habari hiyo, unadhani Juju na wenzake walikuwa ni akina nani?

A: Walinzi wa bahari B: Wavuvi C: Wafanyakazi wa melini D: Wafanyabiashara E: Wakulima [     ]

Katika swali la 6 - 35, weka kivuli katika herufi ya jibu lilio sahihi katika karatasi ya kujibia.

6. Mwalimu Masumbuko ana utaratibu wa kuandikiwa majina ya wasumbufu darasani. Bainisha kauli ya utendaji ya sentensi hiyo.

A: Kutendewa B: Kutendwa C: Kutendeka D: Kutendana E: Kutendeana [     ]

7. Ningekuwa na hela ningelima shamba lote. Badili sentensi hiyo kuwa katika kauli ya kutendesha?

A: Nikiwa na hela nitalimisha shamba lote B: Ningekuwa na hela ningelimia shamba lote C: Ningekuwa na hela ningelimisha shamba lote D: Ningekuwa na hela ningelimiana shamba lote
E: Ningekuwa na hela shamba lote lingelimika [     ]

8. Tulikwenda kumsalimia mwanafunzi mwenzetu aliyefiwa na wazazi wake na tukampa . . . ..Tumia moja ya nahau zifuatazo kukamilisha sentensi hiyo.

A: mkono wa heri B: mkono wa Idi C: mkono wa buriani D: mkono wa ihsani E: mkono wa pongezi [     ]

9. Wachezaji wa timu ya Mtibwa Sugar walikula kiapo ili wasitoe siri ya kambini. Ni nahau ipi inasadifu msemo kula kiapo cha siri?

A: Kata tamaa B: Pata ahueni C: Tia hatiani D: Kaza kamba E: Kula yamini [     ]

10. Utatumia nahau gani kati ya zifuatazo kumuelezea mtu mwenye tabia ya kukasirika kila wakati?

A: Timua mbio B: Kunja ndita C: Chanja mbuga D: Kaa chonjo E: Piga ishara [     ]

11. “Mzee Kondo amekuwa na tabia ya kujisomea magazeti kila siku.” Tambua nafsi ya sentensi hiyo.

A: Kwanza umoja B: Pili umoja C: Tatu umoja D: Pili wingi E: Tatu wingi [     ]

12. Ipi kati ya sentensi zifuatazo ipo katika nafsi ya pili wingi?

A: Tumekunywa maziwa yote. B: Amekunywa maziwa yote. C: Wamekunywa maziwa yote D: Mmekunywa maziwa yote. E: Umekunywa maziwa yote [     ]

13. Bainisha kauli taarifa ya sentensi hii;- “Nitaimba wimbo wangu kesho”

A: Alisema kuwa ataimba wimbo wake kesho B: Alisema kuwa angeimba wimbo wake kesho C: “Alisema kuwa angeimba wimbo wake siku inayofuata” D: Alisema kesho ataimba wimbo wake
E: Alisema kuwa angeimba wimbo wake siku inayofuata

14. Walikuwa wameanzisha bustani yao. Kama ungeambiwa uibadili sentensi hiyo kuwa katika kauli taarifa, lipi lingekuwa ni jibu lako?

A: “Tutaanzisha bustani yetu B: “Tumeanzisha bustani yetu” C: Tumeanzisha bustani yetu D: “Tulianzisha bustani yetu” E: “Tunaanzisha bustani yetu” [     ]

15. Kama ujuavyo methali huwa na pande mbili zinazokamilishana. Katika muktadha huo, upi ni ukamilisho wa methali ifuatayo? “Mkono uliotia jiwe majini . . . . . . . . . . . ..

A: ndio utakaotia jiwe kichwani B: ndio utakaokatwa C: ule ule utaepua D: ule ule utaopoa E: ndio huo utakaolipasua [     ]

16. Unaye rafiki anayependa kufanya mambo bila kuyajua undani wake na mara zote mambo hayo huishia kumdhuru mwenyewe. Utatumia methali gani kumuonya mtu huyo?

A: Usiibe kabla giza halijaingia B: Usichokula usikichachishe C: Usifunue kinywa kama hukijui ulacho D: Usile na kipofu ukamshika mkono E: Usiache mbachao kwa msala upitao [     ]

17. Methali zifuatazo zinalandana kimaana isipokuwa moja tu. Tumia ujuzi wako kuitambua.

A: Panya wengi hawachimbi shimo B: Kidole kimoja hakiui chawa C: Jifya moja haliinjiki chungu D: Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu E: Mkono mmoja haulei mwana [     ]

18. Chuguza methali zifuatazo kisha ubaini moja unayoweza kuitumia kumuonya mtu mnyimi asiyependa kutoa akiogopa ataishiwa.

A: Mkono usioweza kuukata ubusu B: Mkono utoao ndio upatao C: Mpata radhi hupata hadhi D: Mpanda hila huvuna ufukara E: Mpiga ngumi ukuta huumiza mkonowe [     ]

19. Tumia ujuzi wako wa lugha za kifasihi, kubaini kitendawili ambacho jibu lake ni kibatari.

A: Tatu tatu hadi Ulaya B: Napigwa faini kosa silijui C: Natumia nne, mbili, tatu D: Jini mnywa damu, haangazi bila damu E: Mwavuli wa mwitu una nguzo moja [     ]

20. Kwa mfano umepita karibu na shamba la minazi na katika moja ya mnazi ukamuona mtu akichuma na kudondosha nazi chini. Ni kitendawili kipi kitakujia kichwani kutokana na ulichokiona?

A: Amchukuapo hamrudishi B: Amekula ncha mbili C: Ajihami bila silaha D: Ana mali lakini nguo havai E: Aliyefuatwa amekuja bali aliyefuata hajaja [     ]

21. Ni kundi lipi la maneno ambalo limebeba nomino za dhahania pekee?

A: Utukufu, Upole, Ungo, Ukarimu B: Uzuri, Shibe, Upendo, Hasira C: Upepo, Njaa, Kima, Kiu D: Mapenzi, Uchungu, Chuma, Chuki E: Ubaya, Zuri, Ukingo, Unyenyekevu [     ]

22. Laiti ningejua kuwa yeye hapendi mayai nisingempikia. Neno yeye limetumika kama aina gani ya neno?

A: Kivumishi B: Nomino C: Kiwakilishi D: Kielezi E: Kiunganishi [     ]

23. Wanafunzi wa shule ya Mapambano wamekwenda ziara ya mafunzo. Maneno yenye ukolezo na mstari yanasifa gani inayofanana?

A: Yote ni nomino B: Yote ni viunganishi C: Yote ni vihisishi D: Yote ni vielezi E: Yote ni vihusishi [     ]

24. Kama ukidondosha silabi ya mwisho katika neno sakafuni, utapata aina gani ya neno?

A: E B: N C: T D: U E: V [     ]

25. Kalulu, mwanafunzi wa darasa la tano alisema “Nimekwenda nyumbani nimemkuta baba hayupo” Unadhani Kalulu alikosea wapi?

A: Kusema alimkuta wakati hakumkuta B: Kusema alimkuta kumbe yupo C: Kusema nilimkuta badala ya nilifika D: Kusema nilimkuta wakati hakwenda E: Kusema hakumkuta wakati hayupo [     ]

26. Mwalimu angalifundisha vizuri . . . . . . ..Kifungu kipi kinakamilisha kwa usahihi sentensi hiyo?

A: tungelifaulu B: tungafaulu C: tungefaulu D: tutafaulu E: tungalifaulu [     ]

27. Mama amenituma mkate uliotengenezwa kwa unga wa nafaka kwa ajili ya kunywea na chai asubuhi. Kwa neno moja unadhani mama amenituma nini?

A: Andazi B: Mofa C: Bumunda D: Chapati E: Kababu [     ]

28. Daktari alitupa ufafanuzi wa ugonjwa uliokuwa unamsumbua babu. Kipi ni kisawe cha neno lenye mstari?

A: Matibabu B: Hotuba C: Fasili D: Chanzo E: Sababu [     ]

29. Garimoshi . . . . .tutaanza safari yetu. Ni muundo upi unafaa kukamilisha sentensi hiyo?

A: ikija B: akija C: vikija D: likija E: kikija [     ]

30. Chunguza maneno yafuatayo kisha ubaini neno lililotofauti na mengine.

A: Kicheko B: Ucheshi C: Kichekesho D: Cheka E: Mchekeshaji [     ]

31. Unaitambuaje Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa hapa nchini Tanzania kati ya taasisi zifuatazo?

A: BAKITA B: MKUKUTA C: MKURABITA D: TAKUKURU E: KIUTA [     ]

32. Shangazi Mage ni mfanyabiashara wa nafaka pale katika soko la Tandika. Unafikiri Shangazi Mage anauza bidhaa gani?

A: Shuka, Vitenge na Khanga B: Viazi, Mihogo na Magimbi C: Mchele, Ulezi na Mahindi D: Mabegi, Mikanda na Viatu E: Machungwa, Maembe na Maparachichi [     ]

33. Mwazani, mwanafunzi wa darasa la sita ameshindwa kuyapanga maneno yafuatayo kialfabeti. Ukiwa kama mjuzi wa matumizi ya kamusi lipi litakuwa ni jibu lako utakalomsaidia Mwazani? [buza, bubu, bunga, bunge, buti]

A: Bubu, Bunga, Bunge, Buza, Buti B: Bubu, Bunge, Buti, Buza, Bunga C: Bunga, Bubu, Bunge, Buti, Buza D: Bubu, Bunga, Bunge, Buti, Buza E: Bunga, Bunge, Bubu, Buti, Buza [     ]

34. Kwa mujibu wa elimu ya viambishi, unafikiri katika neno hili “amemjengea” vipi ni viambishi awali?

A: ame- B: amem- C: a- D: -jeng- E: -ea [     ]

35. Kabla ya uhuru wa nchi yetu, babu zetu walinyanyasika sana chini ya utawala wa kikoloni. Neno lenye mstari lina silabi ngapi?

A: Saba B: Nane C: Tano D: Kumi na nne E: Sita [     ]

SEHEMU B: (Alama 5)

Umepewa insha yenye sentensi (5) zilizoandikwa bila kufuata mpangilio maalum, zipange sentensi hizo ili zilete mtiririko mzuri wa mawazo kwa kuzipa herufi A, B, C, D na E. Siliba herufi ya jibu sahihi.

36. Bundala aliwaona wanyama wawili kwa mbali wakitembea kuelekea upande wao. [     ]

37. Bibi alinyanyua shingo ili awatazame vizuri, akasema, “Wale sio ng’ombe ni tembo. [     ]

38. Wakiwa wanakaribia kufika shambani, [     ]

39. Bundala aliuliza, “Umejuaje kuwa wale ni tembo?” Bibi akajibu nimeona masikio na mikonga [     ]

40. Alimshika bibi yake kwa woga, huku akisema, “Bibi! bibi! Unawaona wale ng’ombe?” [     ]

SEHEMU C: (Alama 10)

Soma kwa makini utenzi ufuatao kisha jibu swali la 41 - 45 kwa kuandika jibu katika fomu ya kujibia.

Kuwajuza natamani,
Na ukweli ujueni,
Somo kuwapatieni,
Faida yake mjue.

Dunia kama Kijiji,
Ni TEHAMA usihoji,
Marekani Msumbiji,
Ni mafupi masafae.

Utandawazi hakika,
Dunia kuunganika,
Kotekote kwafikika,
Hili ulizingatie.
Teknolojia hizi,
Faidaze kwa vizazi,
Ubunifu ugunduzi,
Himahima twendelee.

Palipo mwanya wa rushwa,
TEHAMA huteremshwa,
Kodi nyingi huzalishwa,
Mapato yasipotee.

Utenzi mwisho mefika,
Chini kalamu naweka,
Somo limekamilika,
Tijaye mzingatie.

Maswali.

41. Ukiusoma vizuri utenzi huo unagundua kuwa malenga alitaka kutoa ujumbe gani kwa hadhira? . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . ..
42. Utenzi huu una jumla ya beti ngapi? . . . . . . . . . . . ...
43. Kila mshororo wa utenzi huu una jumla ya mizani mingapi? . . . ... . . . . . . .
44. Andika kina cha kiishio cha utenzi huu . . . . . . . .
45. Kipi ni kirefu cha neno lililoandikwa kwa herufi kubwa katika beti za utenzi huu? . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . ... . . . . . . . . . .. . .

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 30  

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 30  

OFISI YA RAIS - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKAKI ZA MITAA, HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

 

MTIHANI WA KUJIANDAA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI - 2023

SOMO: KISWAHILI DARASA: VII MUDA: SAA 1:40 

MAELEKEZO:

  • Mtihani huu una maswali 45
  • Jibu maswali yote kama ulivyoelekezwa  

SEHEMU A

Sikiliza habari itakayosomwa na msimamizi kisha jibu maswali yanayofuata kwa kuchagua herufi ya jibu sahihi

1. Habari hii inahusu nini? _______

A. umoja B. Tanzania C. utamaduni D. wageni E. ulaya [       ]

2. Nchi gani inasifika kuwa na ukarimu?

A. Asia B. Ulaya C. Amerika D. Tanzania E. India [       ]

3. Ni vipengele vipi vya utamaduni vimetajwa katika habari hii? _______

A. amani na desturi B. upendo na mila C. amani na upendo D. upendo E. mila na desturi [       ]

4. Wageni wanaotoka Tanzania hutoka katika jamii za nchi gani? ______ 

A. Ulaya tu B. wenyeji wa Tanzania C. Umerika asia na Ulaya D. Uganda na Ulaya E. Asia tu [       ]

5. Kichwa cha habari hii cha faa kiwe ______

A. Mila B. Desturi C. Utamaduni D. Umoja E. Amani [       ]

 Katika swali la 6 – 35 chagua herufi ya jibu sahihi kisha iandike kwenye mabano uliyopewa.

6. Katika maneno yafuatayo ipi ni nomino ya dhahani? ________

A. unakuja B. umeenia C. utalima D. uelewe E. ulisoma

7. Neno lipi ni tofauti na mengine?_____ 

A. embe B. chungwa C. ndizi D. ng’ombe E. papai [       ]

8. “Nitatetema kama Mayele” Kiambishi cha njeo katika neno nitatetema ni kipi? _____

A. nita B. -ta C. te D. –a- E. tema [       ]

9. Walimu walifundisha masomo vizuri. Sentensi hii ipo katika wakati gani? ____ 

A. uliopita B. ujao C. uliopo D. mazoea E. usiodhihirika [       ]

10. Neno “paka” lina silabi ngapi? _____ 

A. mbili B. nne C. tano D. moja E. sita [       ]

11. Umoja wa neno nyaraka ni _________

A. waraka B. nyaraka C. miwaraka D. wawaraka E. kanyaraka [       ]

12. Hadi sasa hakuna mtu_________ aliyekamatwa kuhusika na wizi. 

A. yoyote B. wowote C. yeyote D. yote E. vyovyote [       ]

13. Mahali ambapo anaishi Rais wa nchi huitwa? _______

A. nyunbani B. makao ya Rais C. ikulu D. ngome E. banda [       ]

14. Neno “kitongoji” lina konsonati ngapi? _______ 

A. moja B. mbili C. tano D. tatu E. kumi [       ]

15. Wahenga walisema “hakuna marefu yasiyokuwa na ncha” nini maana ya methali hii? ______

A. hakuna kitu kisicho kirefu B. hakuna kitu kisicho na ncha C. hakuna jambo lenye mwanzo mrefu

D. hakuna jambo lisilokuwa na mwisho E. hakuna marefu yasiyokuwa na mafupi [       ]

16. “Angeliamka” mapema asingeliachwa na ndege. Kipi ni kiambishi cha masharti katika sentensi hii? _______

A. –a- B. –nge- C. –ngeli- D. angel E. –ili- [       ]

17. Mzee Juma ameishi Morogoro ____miaka kumi. 

A. toka B. kwa C. tangu D. kipindi E. tangia [       ]

18. Ni neno lipi kati ya haya yafuatayo lipo katika kundi la majina?_______ 

A. mlimani B. peponi C. mweusi D. utoto E. kwaya [       ]

19. Kama ungeliimba vizuri _____ zawadi.

A. ungelipewa B. ungepewa C. ungalipewa D. ungapewa E. ukipewa [       ]

20. Kitabu chako ni kizuri ukienda dukani nami ninunulie ________. Ni kifungu kipi cha maneno kinakamilisha sentensi hiyo? ___ 

A. kama hivyo B. kama hiko C. kama hicho D. kama iko E. kama icho [       ]

21. John husafisha eneo lake mpaka muda wa kuingia darasani unapowadia. Neno wadia lina maana gani? ___

A. kuwasili B. kuisha C. kufika D. kusogea E. rejea [       ]

22. Kila mtu atalipitia darasa hili apende asipende. Darasa hili ni lipi ? ________ 

A. kifo B. elimu ya msingi C. elimu ya awali D. dini E. semina [       ]

23. Mzee Mpili alizunguka mbuyu, nini maana ya nahau zunguka mbuyu? _______ 

A. kutoa rushwa B. kupiga rushwa C. kupokea rushwa D. kuleta rushwa E. kula rushwa [       ]

24. Mihogo iliyotoka Kidahwe haipikiki, imekaa sana. Neno lililopigiwa mstari liko katika kauli gani ya utendaji?__

A. Kutendeana B. Kutendewa C. Kutenda D. Kutendana E. Kutendeka [       ]

25. Asha anapia uvivu maana yake maneno yaliyopigiwa mstari ni ______ 

A. kutabili kazi B. kula uvivu C. kukaa raha  D. kuamka na uvivu E. kukaa huku ukifanya kazi [       ] 

26. __________________ mbele kiza. Methali hii inakamilishwa na maneno yapi kati ya haya yafuatayo?

A. Usiku B. Ujinga mwingi C. Werevu mwingi D. Ubishi mwingi E. Upendo [       ]

27. Malizia methali hii. “Mwenda tezi na omo ________” 

A. ni mnafiki B. marejeo ngamani C. hafai kwenye raha D. uakufa naye E. hufaidi siku ya iddi [       ]

28. “Gari lile liliendeshwa na mdogo wangu.” Hii ni kauli ya ______ 

A. kutendeka B. kutendewa C. kutenda D. kutendwa E. kutendana [       ]

29. Tegua kitendawili kisemacho Kondoo wetu ana nyama nje ngozi ndani. ________ 

A. Nywele na kichwa B. Katani C. Uyoga D. Chungwa E. Filigisi [       ]

30. Siwema ni msichana mzuri lakini ana mkono wa birika. Maana ya nahau iliyokolezwa ni ipi? _____

A. Mchoyo B. Mwizi C. Muongo D. Kusengenya E. Msahaulifu [       ]

31. Tegua kitendawili hiki “bomu la machozi baridi” _______

A. nywele B. moshi C. miguu D. ngozi E. gesi [       ]

32. Maana ya nahau “kufa moyo” ni ipi ? _______

A. kufariki B. kuugua sana C. kuchoka sana D. fia ndani ya moyo E. kukata tama [       ]

33. Samaki mkunje angali mbichi. Methali ipi kati ya hizi ina maana sawa na hii ? ______ 

A. samaki huanza kuoza kichwani B. ukitaka riba ziba C. jino la pembe si dawa ya pengo D. sikio la kufa halisikii dawa E. ngozi ivute ingali maji [       ]

34. Methali ipi haifanani na zingine kati ya hizi? ________

A. sikio la kufa halisikii dawa B. chombo cha kuzama hakina usukani C. siku ya kufa nyani miti yote huteleza D. maji yakimwagika hayazoleki [       ]

35. Maana ya “fuja mali” ni ________

A. kuiba mali B. kutumia mali ovyo C. kuhifadhi mali D. kutumia mali kibali E. kuitumia mali [       ]

 SEHEMU B: UTUNGAJI

 Panga sentensi zifuatazo katika mfuatano sahihi kwa kizipa herufi A, B, C, D na E.

36. Zima taa ulale, kuna radi sana. [       ]

37. Nilikuwa chumbani kwangu nikisoma kitabu cha hadithi. [       ]

38. Ilikuwa ni wakati wa usiku. [       ]

39. Mara nilimsikia baba akiniita, Bura! Bura! [       ]

40. Siku hiyo kulikuwa na mvuya kubwa iliyoambatana na radi. [       ]

SEHEMU C: USHAIRI - Soma shairi lifuatalo kisha jibu maswali yafuatayo Ukiwepo darasani, mwalimu msikilize,

Kisichotiwa mizani, angalia usimeze, 

Kilopita kipimoni, ndicho ukitekeleze, 

Elimu ni ufunguo, kila mtoto sikia.

Mazoezi darasani, yatakufanya uweze,

La kufanya akilini, kuchagua ipendeze, 

Uzio ubaini, jamii usipumbaze,

Elimu ni ufunguo, kila mtoto sikia.

MASAWALI

41. Shairi hili lina jumla ya beti ngapi? ......................................................................

42. Taja vina vya mwisho katika ubeti wa kwanza . . . . . . . . . . . . . . . . . . ...

43. Kila ubeti wa shairi hili una mishororo mingapi? ....................................................

44. Ubeti wa pili una mizani mingapi? . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

45. Mstari unaojirudiarudia katika kila ubeti unaitwaje? . . . . . . .. ... . . . . . . . .




HABARI YA KUSOMA

Utamaduni ni mfumo wa maisha ya watu na jinsi wanavyoishi na taratibu zao za kijamii, kiuchumi na kisiasa. Tanzania ni moja ta kati ya nchi zinazosifika duniani kwa ukarimu, amani na upendo kwa wageni, licha ya kuwa na makabila zaidi ya mia moja na ishirini ambayo yote hutunza mila na desturi zao, watanzania wanaishi kwa umoja, upendo na mshikamano. Hali hiihuwavutia watu wa mataifa mengine na wengine na wengine hupenda kuishi Tanzania.

Wageni hawa hutoka katika jamii za nchi tofauti zikiwemo zile za Asia, Ulaya na Amerika.

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 21  

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 21  

 JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA  OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

 HALMASHAURI YA MANISPAA YA UBUNGO

 MTIHANI WA UTAMILIFU KATA 
 KISWAHILI DARASA LA SABA – MACHI, 2023

 MUDA: SAA 1:30

 MAELEKEZO 

  1. Mtihani huu una maswali arobaini na tano (45) tu.
  2. Jibu maswali yote
  3. Soma maelekezo kwa kila kurasa uliyopewa
  4. Kumbuka kuandika Jina lako, Namba yako ya mtihani na Jina la shule yako katika karatasi ya kujibia.
  5. Tumia penseli ya HB tu.
  6. Simu hazihitajiki katika chumba cha mtihani.

SEHEMU A: UFAHAMU WA KUSIKILIZA

Sikiliza kwa makini habari utakayosomewa na msimamizi kisha jibu swali 1- 5 kwa kuweka kivuli katika herufi ya jibu sahihi katika fomu yako ya kujibia. 

1. Kutokana na habari uliyoisikiliza, ni nani aliyezungumziwa?

(A) Amani (B) Bibi (C) Wananchi (D) Bibi na Amani (E) Kilole [     ]

2. Amani alimuuliza swali gani bibi yake? 

(A) kama unajua kusoma na kuandika (B) kama unajua kuandika (C) kama unajua kusoma (D) kama unajua kuimba na kuandika (E) kama unajua kuimba [     ]

3. Amani anaishi katika kijiji cha Kilole. Je, Amani anaishi na nani?

(A) Bibi (B) Babu (C) Shangazi (D) Mjomba (E) Babu na bibi [     ]

4. Kwa mujibu wa habari uliyoisikiliza. Amani ana tabia gani?

(A) mvivu (B) mdadisi (C) mkarimu (D) mchapakazi na mdadisi (E) mpole [     ]

5. Kichwa cha habari hii kinafaa kiwe kipi miongoni mwa hivi?

(A) kijiji cha Kilole (B) Amani (C) Amani na bibi yake (D) Kilole (E) Bibi [     ]

Katika Swali la 6 – 35 weka kivuli katika herufi ya jibu sahihi 

6. Neno machweo lina maana ipi kati ya hizi zifuatazo?

(A) wakati jua linapozama (B) wakati jua linapochomoza (C) wakati jua linapokuwa la utosi

(D) wakati jua linapokuwa kati (E) wakati jua linapokuwa pembeni [     ]

7. “Kazi mbaya si mchezo mwema” methali inayofanana na methali hii ni ipi kati ya hizi zifuatazo?

(A) hewala haigombi (B) mchezea tope humrukia (C) mcheka kivu asiyefikwa na jeraha (D) lila na fila havitengamani (E) mcheza kwao hutunzwa [     ]

8. Wanafunzi wale wanapenda kucheza mpira. Katika sentensi hii neno lipi limetumika kama kivumishi? 

(A) wanafunzi (B) wale (C) wanapenda (D) mpira (E) kucheza [     ]

9. Katika lugha ya Kiswahili neno “staftahi” lina silabi ngapi?

(A) sita (B) tano (C) nne (D) tatu (E) saba [     ]

10. “Ukitaka kuruka agana na nyonga”. Sentensi hii iko katika aina gani ya sentensi kati ya hizi?

(A) sahihi (B) ambatano (C) changamano (D) tegemezi (E) shurutia [     ]

11. Ipi ni maana ya kitedawili “nyumba yangu imeungua mwamba wake umebaki”

(A) mfupa (B) njia (C) kaburi (D) kisima (E) mlima [     ]

12. Kuwa na nyota ya jaha maana yake ni___________ 

(A) jua la mchana (B) nyota ya asubuhi (C) bahati nzuri (D) bahati mbaya (E) bahati nasibu [     ]

13. Wewe ni mtoto mdogo sana. Sentensi hii iko katika nafsi gani?

(A) ya kwanza umoja (B) ya pili umoja (C) ya tatu wingi (D) ya pili wingi (E) ya kwanza umoja na wingi [     ]

14. Watu hufanya kazi mbalimbali ili kuweza kujipatia kipato. Mtu anayefanya kazi ya kutunza na kuazima vitabu maktaba anaitwa Mkutubi. Je! mtu anayefanya kazi ya kuzibua vyoo anaitwa nani? 

(A) kuli (B) topasi (C) toinyo (D) chepe (E) zubaifu [     ]

15. Bwana Afya aliuliza, kuna umuhimu gani wa kuchemsha maji ya kunywa? Je! sentensi hii iko katika kauli ipi kati ya zifuatazo? 

(A) taarifa (B) halisi (C) tata (D) tungo huru (E) kutenda [     ]

16. Asha ana gari. Neno “ana” ni aina gani ya neno?

(A) kitenzi (B) nomino (C) kiunganishi (D) kielezi (E) kihusishi [     ]

17. Baba amelima shamba kubwa sana. Silabi inayoonesha nafsi ni ipi?[     ]

(A) –li– (B) –a– (C) –me– (D) –i– (E) –lim–[     ]

18. Ngumi  zilipigika vilivyo, Neno lililopigiwa mstari lipo katika kauli gani?

(A) kutenda (B) kutendewa (C) kutendwa (D) kutendeka (E) kutendesha [     ]

19. __________ Kamilisha methali ifuatayo. Akikalia Kigoda

(A) huanguka (B) usimtukane (C) mtii (D) mfukuze (E) harudi [     ]

20. _______________ Ali anakula wali maharage.

(A) na (B) kwa (C) ni (D) ya (E) pamoja [     ]

21. Simba mkali amepita shuleni kwetu. Mchanganuo wa sentensi hii ni upi kati ya michanganuo ifuatayo? 

(A) T+N+V+W+E (B) N+E+V+T+W (C) V+E+T+W+N (D) N+V+T+E+V (E) N+V+E+T+V [     ]

22. ________ Kinyume cha methali isemayo; “Ngoja ngoja yaumiza matumbo” ni

(A) bendera hufuata upepo (B) mtu hujikuna hajipatiapo (C) mwisha hadhuru maiti (D) haraka haraka haina Baraka (E) asiyesikia la mkuu huvunjika guu [     ]

23. ______ Wakoloni walitunyanyasa lakini hatimaye unyanyasaji huo ulifika ukingoni kwani Ni methali ipi kati ya zifuatazo inamalizia sentensi hii?

(A) hakuna marefu yasiyokuwa na ncha (B) mchumia juani hulia kivulini (C) ukiona vyaelea ujue vimeundwa (D) umoja ni nguvu utengano ni udhaifu (E) bandubandu humalia gogo [     ]

24. Kazi ya Daudi ni kazi ya kijungujiko. Je! kazi ya kijungujiko ni kazi ya aina gani?

(A) kazi ya kuchimba vyoo (B) kazi ya kujitolea (C) kazi ya kufundisha wanafunzi (D) kazi isiyo rasmi au inayotosha mahitaji ya mlo tu (E) kazi ya kikoa [     ]

25. Ikiwa mzizi wa neno “PIK” tukiunda neno litakalokuwa katika wakati uliopita nafsi ya kwanza
umoja hali ya kutenda tunapata neno.

(A) alipika (B) nilipika (C) walipika (D) tulipika (E) nimepika [     ]

26. Akikosekana maana inakosekana. Jibu la kitendawili hiki ni lipi?

(A) kitabu (B) kamusi (C) magazeti (D) shairi (E) vipeperushi [     ]

27. Mashairi ya kimapokeo yamegawanyika katika aina mbalimbali. Je ubeti wa shairi wenye mistari minne huitwaje?

(A) mshororo (B) tarbia (C) kituo (D) kibwagizo (E) mizani [     ]

28. _______ Mnyama ambaye amekuwa laini bado hajazaa anaitwa

(A) mtamba (B) mbuguma (C) maksai (D) fahali (E) beberu [     ]

29. Nenda ukawasikilize watakachokueleza uniletee mrejesho. Katika sentensi hii mtenda ni nafsi ya ngapi? 

(A) ya kwanza umoja (B) ya pili umoja (C) ya tatu wingi (D) ya kwanza wingi (E) ya pili wingi [     ]

30. _______________________ Ali ni askari kanzu. Ali ni 

(A) trafiki (B) kanga (C) bunduki (D) mpelelezi (E) askari mwenye cheo cha juu [     ]

31. Jambazi alihukumiwa kwa kuua mfanyabiashara. Sentensi hii iko katika hali gani?

(A) hali timilifu (B) hali ya kuendelea (C) hali isiyodhihirika (D) hali ya mazoea (E) hali tata [     ]

32. Tungo changamano ni tungo yenye vishazi vingapi?

(A) vitatu (B) viwili (C) vinne (D) vitano (E) kimoja [     ]

33. _______ Kisawe cha jogoo ni jimbi, kisawe cha beseni ni karai. Je kisawe cha kinyonga ni

(A) bombo (B) hua (C) lumbwi (D) kelbu (E) baghala [     ]

34. Katika neno anacheza. Kipi ni kiambishi njeo?

(A) –a– (B) –na– (C) –chez– (D) –a– (E) –cheza– [     ]

35. Lipi kati ya maneno yafuatayo si kivumishi likiambatanishwa na nomino?

(A) Yule (B) nzuri (C) polepole (D) huyo (E) hawa [     ]

 SEHEMU B:

 Panga sentensi zifuatazo kwa kuzipa herufi A – E ili zilete maana kamili kwa kujibu swali la 36 – 40 kwa kuweka kivuli katika herufi ya jibu lililo sahihi

36. Niliogopa lakini nilipiga moyo konde  [    ]

37. Nilirudi nyuma kidogo nikaokota fimbo na kumpiga   [    ]

38. Jumamosi iliyopita mama alinituma sokoni   [    ]

39. Nilipokuwa njiani nilimwona nyoka   [    ] 

40. Aliniambia ninunue nyanya, vitunguu, sukari na mafuta   [    ]


 SEHEMU C: 

 Soma habari ifuatayo kisha jibu maswali yafuatayo 

Masebo ni mwalimu anayefundisha katika shule ya Msingi Maendeleo iliyoko wilaya ya Masasi. Anakaa katika kitongoji cha usafi kilichopo umbali wa kilometa tano kutoka shuleni. Siku moja mwalimu Masebo alikuwa anakwenda shuleni. Pembezoni mwa msitu wa kijiji aliwaona vijana watatu, vijana hao walikuwa wakikata miti kwa kutumia mapanga na mashoka na kuivundika pembeni. Aliwatambua vijana hao kuwa ni Juma, Sadiki na Joseph. Mwalimu Masebo alisikitika sana. Alisimamisha pikipiki yake haraka na kwenda katika eneo lile. Alianza kuwafokea vijana wale kwa kukata miti mingi kiasi kile. Vijana wale walishangaa sana.

 Maswali 

41. Juma, Sadiki na Joseph walikuwa wanafanya nini msituni?

42. Mwalimu Masebo aliona nini pembezoni mwa msitu wa kijiji?

43. Je! ukikuta watu wanaoharibu mazingira utafanya nini?

44. Kwa nini mwalimu Masebo alisikitika sana?

45. Kwa nini tunashauriwa kutokata miti ovyo?



UFAHAMU WA KUSIKILIZA

Amani anaishi na bibi yake katika kijiji cha Kilole. Anamsaidia bibi yake shughuli za nyumbani. Anamsaidia kusafisha nyumba, kupika, kuosha vyombo na kufua. Juzi Amani alimuuliza bibi yake; bibi unajua kusoma? Bibi akajibu ninajua kusoma na kuandika. Amani akasema sawa bibi, kesho nitaleta kitabu changu ili tusome pamoja.



STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 3  

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 3  

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256