URAIA STANDARD FOUR REGIONAL EXAMS (MOCK, PRE-NATIONAL, etc.)

JINA LA MWANAFUNZI: . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

NAMBA: . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS- TAMISEMI

MTIHANI WA UJIRANI MWEMA WILAYA NKASI, SEI'TEMBA 2024

SOMO: URAIA NA MAADILI

MUDA: SAA 2:00

SEHEMU A (Mama 28)

1.Jibu vipengele (i — v) kwa kuchagua herufi ya jibu sahihi na uandike katika nafasi ulizopewa.

i.Ni nani kati ya viongozi wafuatao shuleni ambaye si mwanachama wa serikali ya wanafunzi?

  1. kaka mkuu
  2. Dada mkuu
  3. Mwalimu Mkuu
  4. Kiranja wa taaluma

ii.Kagembe ni Afisa Mtendaji wa kijiji cha Inonelwa.Kagembe alipata nafasi hiyo kwa njia gani?

  1. Aliteuliwa na rais.
  2. Alichaguliwa na wanakijui.
  3. Aliteuliwa na mwenyekiti wa kujip
  4. Aliteuliwa na mkurugenzi mtendaji wa wilaya.

iii.Moja ya alama zetu za kitaifa hutumika kama maombi. Ni ipi hiyo?

  1. Fedha ya Taifa
  2. Wimbo wa Taifa
  3. Nembo ya Taifa
  4. DMwenge wa Uhuru

iv. Ni nani kati ya wanafunzi wafuatao anafanya kitendo cha kutisha ambacho kinaweza kuathiri afya yake?

  1. Salama akicheza karibu na shimo la kutupa taka.
  2. Diana akiangalia alama na kanuni za barabarani
  3. Rashida akioga mara mbili kwa siku
  4. Petro akikwepa kucheza barabarani wakati wa kwenda shule

v.Pulupu anapendwa na kuheshimiwa na wanafunzi wote darasani kwake. Unafikiri ni kwasababu gani?

  1. Anafanya vyema katika masomo yake lakini ni mkorofi.
  2. Ni mbinafsi na anaheshimu watu wote.
  3. Ana adabu na anafanya vyema katika masomo yake.
  4. Anaiba mali ya wanafunzi wengine na kusema uwongo

2. Jibu swali la 2(i) — (iv) kwa kuoanisha maswali yaliyo katika sehemu A na majibu sahihi yaliyo katika sehemu B Andika herufi ya jibu kwenye mabano

SAFU A

SAFU B

  1. Huonesha utajiri wa mali asili ya nchi yetu
  2. Hutumika katika barua za kiofisi na machapisho ya serikali
  3. Huashiria uhuru wa nchi yetu
  4. Huwakilisha vifaa vinavyotumika kuendeleza Taifa.

  1. Bendera ya Taifa.
  2. Jembe na nyundo.
  3. Wimbo wa Taifa.
  4. Nembo ya Taifa.
  5. Fedha za Tanzania.
  6. Pembe za ndovu

3. Jibu vipengee (i) - (iv) kwa kuchagua jibu sahihi kwenye mabano na liandike katika nafasi zilizoachwa wazi.

  1. je matokeo ya kutokubali kukosolewa ni lipi? (Kupoteza umaarufu, kubaki na shida, kuangalia busara)
  2. Mtu anaweza kujijengea nidhamu kwa kuwa na mojawapo ya vitendo vifuatavyo, isipokuwa. (Kupenda kusoma, kuwa siri, kujitolea)
  3. Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulifanyika lini? (Aprili 26, 1961, 9 Desemba 1961, Aprili 26, 1964)
  4. Kitendo cha kuvumiliana na kukubali watu wengine wa jinsia na mawazo tofauti huonyesha (Uwajibikaji, uthabiti, uadilifu)

SEHEMU B: (Alama 22)

4.Jibu swali katika vipengele (i-v) kwa kuonyesha tabia zinazowakilishwa kwa kuweka tiki (✓) kwenye eneo linalosadifu tabia husika(i) inafanywa kama mfano.

Vitendo vinavyofanywa na watoto Tabia salama Tabia hatarishi

Tabia hatarishi

(i) Watoto wanaokunywa pombe na kuvuta sigara
(ii) Kuheshimu na kusaidia wazee na walemavu
(iii) Kucheza na chupa zilizovunjika na mbwa hatari
(iv) Kusoma kwa bidii na kufanya kazi ya shule
(v) Mwanafunzi anayetoka nje ya eneo la shule kwa kuruka ukuta

5.Chunguza alama za taifa zinazooneshwa na picha zifuatazo kisha jibu maswali yanayofuata

  1. Alama ya taifa inayooneshwa na picha A inaitwaje?
  2. Kitendo cha kuzungusha alama ya taifa iliyooneshwa kwa picha A hapo juu katika maeneo mbali mbali ya nchi yetu hujulikana kama
  3. Alama ya taifa inayooneshwa kwa picha C inaitwaje?
  4. Ni alama ipi ya taifa kati ya hizo zinazooneshwa na picha hapo juu inaonesha kwamba Tanzania ni nchi huru?

6. Soma kwa makini kifungu kilicho hapa chini, lcisha ujibu vipengele (i) - (iv)

Ajali nyingi za barabarani zinazosababishwa na kutozingatia sheria za barabarani. Sheria hizi ni pamoja na matumizi sahihi ya alama za barabarani na taa za barabarani. Alama za barabarani ni muhimu kwa sababu zinasaidia madereva na watumiaji wengine wa barabara kujua matumizi bora ya barabara. Jeshi la polisi na taasisi mbalimbali zimekuwa zikitoa elimu kuhusu sheria za barabarani ikiwa ni njia nzuri ya kuwasaidia watumiaji wa barabara kuelewa na kuzingatia matumizi sahihi ya barabara.Ni wajibu wa kila mtu kuheshimu na kuzingatia sheria za usalama barabarani.

Hii itasaidia kupunguza au kuondokana na ajali za barabarani. Ajali za barabarani zimekuwa zikisababisha vifo vya maelfu ya watu, uharibifu wa mali na usumbufu usio wa lazima kwa wananchi.

MASWALI:

  1. Nini chanzo kikuu cha ajali za barabarani?
  2. Alama za barabarani zinawasaidia vipi madereva na watumiaji wengine wa barabara?
  3. Taja athari mbili za ajali za barabarani. (i)........... (ii) .............................
  4. Je, ni njia gani kuu ya kumsaidia mtumiaji wa barabara kujua matumizi sahihi ya barabara?

STANDARD FOUR URAIA EXAM SERIES 46  

STANDARD FOUR URAIA EXAM SERIES 46  

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU

MTIHANI WA UPIMAJI DARASA LA IV TAREHE 23 NA 24 AGOST 2023

URAIA NA MAADILI

MUDA: SAA 1:30 AGOST 2023

MAELEKEZO

  1. Mtihani huu una maswali sita yenye vipengele vya namba za kirumi
  2. Jibu maswali yote
  3. Andika majina yako kwa usahihi kwenye kila ukurasa

SEHEMU A (Alama 26)

1. Chagua herufi ya jibu sahihi

(i) Katika sarafu zifuatazo ipi ina picha ya Hayati Abeid Amani Karume?

A. Shilingi 5000 B. Shilingi 100 C. Shiling 1000 D. Shilingi 200 [     ]

(ii) Kiongozi mkuu wa serikali ya kijiji niimage

A. Mkurugenzi wa Wilaya B. Mwenyekiti wa Kijiji C. Diwani D. Mwenyekiti wa Kitongoji [     ]

(iii) Uoto wa asili kwenye bendera ya taifa huwakilishwa na rangi ya

A. Bluu B. Njano C. Nyeusi D. Kijani [     ]

(iv) Ni alama gani hupatikana katika ya bendera ya Rais?

A. Fedha ya taifa B. Bendera ya taifa C. Ngao ya taifa D. Sikukuu za taifa [     ]

(vv) Waziri mkuu wa Tanzania anaitwa nani?

A. Tulia Ackson. B. Ummy Mwalimu C. Dr. Philipo Mpango D. Majaliwa Kassim [     ]

2. Oanisha maneno kutoka Kifungu A na Kifungu B ili kuleta maana sahihi

KIFUNGU A

JIBU

KIFUNGU B

i. Demokrasia


A. Muungano wa Tanganyika na Zanzibar

B. Uhuru wa Tanganyika

C. Ni eneo la mjini

D. Ni haki ya watu kuchagua viongozi wao

E. Muungano wa Tanzania na Zanzibar

F. Kuzaliwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere

ii. 1922


iii. 1964


iv. Serikali za mitaa


3. Jibu maswali yafuatayo kwa kuchagua jibu sahihi kutoka kwenye mabano

(i) imageKatibu wa vikao vya kamati ya shule huitwa (Mwalimu mkuu, Mtendaji wa kijiji, Diwani, Mzazi)

(ii) imageKitendo cha uvunjifu wa sheria za nchi huitwa. (uhalifu, uovu, katiba, haki)

(iii) imageMazao yanayopatikana katika nembo ya taifa ni ( karafuu na pamba, mtama na mahindi, ndizi)

(iv) Mambo ambayo mtu anastahili kuyapata yanaitwaimage (wajibu, sheria, malazi, haki)

SEHEMU B (Alama 24)

4. Jedwali hili linaonesha makabila mbalimbali na mikoa yanakopatikana Tanzania. Jaza nafasi zilizoachwa wazi.

KABILA

MKOA

i. image

Tabora

ii. image

Dodoma

Makonde

iii. image

iv. image

Singida

5. Soma picha ifuatayo kwa makini kisha jibu maswali yafuatayo namba (i) – (iv)

image

MASWALI

(i) Jina la sehemu inayooneshwa kwenye picha inaitwaimage

(ii) Ni nembo ipi ya taifa inaonekana mbele ya wanafunzi?image

(iii)Kiongozi mkuu wa jamii inayooneshwa kwenye picha ni image

(iv) Kutokana na uelewa wako, ni muda gani bendera ya taifa hupandishwa? image

6. Soma habari ifuatayo kisha jibu maswali yafuatayo

Ukatili wa watoto ni tabia ambayo hufanywa na watu wazima makusudi kuwaumiza watoto kwa njia ya ukatili na kuwafanyia vurugu. Ukatili wa watoto unahuusisha kuwapuuza watoto, ngono au unyanyasaji wakijinsia. Ukatili wa watoto pia hujulikana kama Ukiukwaji wa haki za watoto. Ni ukiukwaji kufanya kitendo ambacho kipo kinyume na haki za watoto. Ukiukwaji wa haki ni ukosefu wa haki na usawa. Ukiukwaji wa haki za watoto ni kutokuwatendea haki watoto. Ni uvunjifu wa haki za watoto.

Ukiukwaji wa haki za watoto ni kitendo cha kuwanyima haki zao watoto. Jamii inapaswa kufanya kila njia kulinda haki za watoto.

MASWALI

(i) Ukatili wa watoto ni tabia ambayo image

(ii) Ukatili wa watoto kama ilivyoelezwa katika habari unahusisha ngono, ukatili wa kijinsia na image

(iii) Mwandishi amesema ukiukwaji wa haki ni kitendo kisichokubalika dhidi yaimage

(iv) Jina jingine la Ukiukwaji wa haki za watoto kutokana na habari uliyosoma niimage

STANDARD FOUR URAIA EXAM SERIES 36  

STANDARD FOUR URAIA EXAM SERIES 36  

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

UPIMAJI WA UTAMILIFU DARASA LA NNE

MKOA WA NJOMBE

06 URAIA NA MAADILI

Muda: Saa 1:30 Mwaka :2023

MAELEKEZO

  1. Karatasi hii ina sehemu A na B zenye jumla ya maswali Matano (5).
  2. Jibu maswali yote.
  3. Majibu yote yaandikwe katika nafasi zilizotolewa katika kila swali.
  4. Andika majibu yote kwa kutumia kalamu ya wino wa bluu au mweusi.
  5. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba cha upimaji.
  6. Andika Jina na Namba yako ya Upimaji katika sehemu ya juu kulia ya kila ukurasa.
KWA MATUMIZI YA UPIMAJI TU
 NAMBA YA SWALI   ALAMA   SAINI YA MPIMAJI
1

2

3

4

5

JUMLA

SAINI YA MHAKIKI


SEHEMU : A Chagua herufi ya jibu sahihi

1. i. Kuwahi shuleni ni moja ya ____________________

  1. kumuogopa mwalimu mkuu
  2. kutii sheria
  3. kumtii mwalimu
  4. kuvunja sheria [       ]

ii. Baadhi ya matendo ya kujijali ni pamoja na_________________

  1. Kuvuta sigara
  2. Kula upendacho
  3. Kuwa msafi
  4. Kuwapenda wenzako [       ]

iii. Watoto waliokosa adabu wanaweza kuwa _________________

  1. msaada kwa wazazi wao
  2. uwajibikaji
  3. hatari katika familia
  4. wajinga [       ]

iv. Ni rangi gani katika bendera ya Taifa inawakilisha mali asili Tanzania? 

  1. Kijani
  2. Bluu
  3. Njano
  4. Nyeusi [       ]

v. Kufanya kazi kwa pamoja humaanisha ___________________

  1. ushirikiano
  2. utengano
  3. kutawanyika
  4. kunyanyaswa [       ]

2. Oanisha kifungu A na B:ili kupata maana sahihi.

Na

 Kifungu A 

 Kifungu B

Jawabu

i.

Kundi la watu wanaoishi katika eneo moja

A: Mazingira


ii.

Matendo ya uaminifu

B: Kufichua Uovu


iii.

Moja ya haki ya watoto

C: Kupata elimu bora


iv.

Ni jumla ya vitu vyote vinavyotuzunguka

D: Ukoo


v.

Kuhakikisha wanakijiji wanapata huduma za Kijamii kama vile maji, umeme na barabara

E: Kazi mojawapo ya serikali ya kijiji


SEHEMU : B

3. Andika neno HAKI au WAJIBU mbele ya kila sentensi.

i. Kujifunza kutokana na makosa__________________________________

ii. Kupata elimu bora____________________________________________

iii. Kuthamini watu wenye ulemavu_________________________________

iv. Mtoto kucheza_______________________________________________

v. Kusoma kwa bidii_____________________________________________

4. Jaza nafasi zilizo wazi

i. Makazi ya Rais huitwa ________________________________________

ii. Alama inayotambulisha shule au Taifa huitwa ______________________

iii. Mtu mwenye mapenzi na nchi yake huitwa________________________

iv. Bendera ya Taifa hupandishwa saa ngapi?_________________________

v. Katibu wa kamati ya shule anaitwa ______________________________

5. Soma kifungu cha habari kisha jibu maswali yanayofuata.

Maria na Tina ni wanafunzi wa darasa la IV katika shule ya msingi Chambalo. Marafiki hawa walifanya vibaya katika masomo yao.Walisoma kwa bidii lakini hawakufaulu mitihani yao.

Maria hakukata tamaa aliamini kuwa atafikia malengo aliyojiwekea ya kufaulu mitihani yake. Aliwashawishi wenzake kwenda kuunda kikundi cha kujisomea. Siku ya Jumamosi waliamka mapema kufanya shughuli za nyumbani na kila ilipotimu saa 5 asubuhi walikutana nyumbani na kujisomea. Baada ya Miezi sita tu. Maria alikuwa wa kwanza katika masomo, Maria aliongoza darasani.

Maswali

i. Maria hakukata tamaa kwa kuwa aliamini _______________________________________

ii. Maria na rafiki yake waliweza kufanya vizuri baada ya kuamua kufanya nini? __________________________________________

iii. Siku ya Jumamosi Maria na rafiki zake waliamka ___________________ ili wafanye majukumu yao ya nyumbani.

iv. Baada ya miezi sita maria alikuwa wa_____________________________ katika masomo yake.

v. Maria aliwashawishi wenzake kuunda kikundi cha _________________________________________


STANDARD FOUR URAIA EXAM SERIES 26  

STANDARD FOUR URAIA EXAM SERIES 26  

 OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

HALMASHAURI YA WILAYA YA MBARALI

MTIHANI WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE

URAIA NA MAADILI

SEHEMU A

1.Chagua   herufi ya jibu   sahihi   na kisha andika katika kisanduku

(i)Ni alama ipi kati ya zifuatazo inapatikana katikati ya bendera ya raisi wa Tanzania?

(A)Bendera ya taifa (B)Wimbo wa taifa (C)Nembo ya taifa(D)Katiba ya taifa (     )

( ii)Ni sarafu ipi kati ya zifuatazo ina picha ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere?

(A)Shilingi 100(B) Shilingi 50(C)Shilingi 200(D)Shilingi 500 (      )

(iii)Mojawapo ya vitu ambavyo vinaanza vinaonyesha upendo miongoni mwa wanajamii ni;

(A)Kusema uongo (B)Kupigana (C)Kuiba vitu vya wengine (D)Kuheshimiana (      )

(iv)Ni tarehe gani tunasherehekea muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar?

(A)9 disemba (B)12 Januari (C) 14 Oktoba (D) 26 Aprili (      )

(v)Wimbo wa Taifa unapoimbwa tunatakiwa

(A) Tulale (B) Tupige magoti (C)Tusimame wima (D) Tutembee (      )

SEHEMU B

Oanisha fungu A na Fungu B ili kupata maana kamili kutoka fingu A


FUNGU A

JIBU


FUNGU B

i

Rangi nyeusi katika bendera ya tanzania


A

Ardhi maji na mifugo

ii

Lugha,mavazi na chakula


B

Uaswa wa kijinsia

iii

Kutunga sheria


C

Utamadauni

iv

Mwanamke na mwanaume katika nembo ya Taifa


D

Watu wa Tanzania

v

Maliasili


E

Bunge

SEHEMU C 

 3.Jaza nafasi zilizoachwa wazi kwa kuchagua kuchagua jibu sahihi kutoka kwenye kisanduku 

Nne,Tano, Mazingira, J.K Nyerere, Kipaji, Utamaduni

i.Rais wa kwanza wa Tanzania …………………………………….

ii…………………….ni jumla ya vitu vyote vinavyomzunguka mwanadamu

iii.Uwezo wa kutenda jambo kwa ustadi ……………………………………………………………..

iv.Uchaguzi mkuu wa Tanzania hufanyika kila baada ya miaka …………………………

v.Bendera ya Taifa ina jumla ya rangi …………………………………………………………………

 4.Kamilisha kifungu cha hapo chini kwa kutumia maneno sahihi na uyaandike kwenye nafasi zilizoahwa wazi.Kipengere namba moja (i) imetolewa kama mfano

Tanganyika ilipata uhuru wake (i) 9 disemba 1961.Tarehe (ii)……………………………..ikawa jamhuri .Raisi wa kwanza wa Tanganyika alikuwa anaitwa (iii)………………………………….Alihudumu kama raisi wa Tanganyika kuanzia mwaka 1962 mpaka mwaka 1964 na amekuwa raisi wa jamhuri ya muungao wa Tanzania kuanzia mwaka 1964 mpaka (iv)……………………………Raisi wa awamu ya pili wa Tanzania alikuwa anaitwa(v)…………………………………………………….

5.Soma kifungu cha habari kwa makini kisha jibu maswali yafuatayo

Mtu mtiifu mwaminifu na mkweli katika jamii yake kila wakati hufanya vitu kwa usahihi hata kama hakuna mtu anayemwongoza kuwa mtiifu.Inamaana unakuwa mkweli na mwaminifu hata kwako wewe mwenyewe. Kama mtu mtu akitaka kufanikiwa katika maisha yake anatakiwa awe mwaminifu na mkweli.

MASWALI

i………………ni mtu anayefanya vitu kwa usahihi wakati wote

ii.Kichwa cha habari chafaa kiwe ……………………………………………………….

iii.Umejfunza nini kutokana na habari hii…………………………………………..?

iv.Ili uweze kufanikiwa katika jamii unatakaiwa kuwa ………………………

v.Kuwa mtiifu inamaana unakuwa ……………………………………………………..


STANDARD FOUR URAIA EXAM SERIES 12  

STANDARD FOUR URAIA EXAM SERIES 12  

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256