OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SEREKALI ZA MITAA
MTIHANI WA MUHULA HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI
KIDATO CHA KWANZA
MUDA: 2:30 MEI 2026
Maelekezo;
SEHEMU A. (Alama 15)
1. Kutoka kipengele i- x chagua herufi ya jibu sahihi. Kisha andika jibu kwenye sehemu ya kujibia.
i. Somo la Historia ya Tanzania na Maadili limeundwa na dhana kuu mbili, dhana hizo ni pamoja na
ii. Historia kuhusu mambo au matukio yaliyopita yenye athari kiuchumi,kisiasa,na kiutamaduni katika jamii imesababishwa na matukio kadhaa yakiwemo;
iii. Lengo la somo la Historia ya Tanzania na Maadili ni pamoja na
iv. Kwanini ni muhimu kujua historia yetu
v. Ungepewa nafasi ya kusimamia maadili shuleni, je ungependa ujadili kuhusu ni niini?
vi. Wanazuoni na wanafalsafa mbalimbali wametoa fasili tofautitofauti juu za dhana ya jamii kati ya hizi zifuatazo ni ipi fasili ya dhana ya jamii kwa mujibu wa mtaalam Margaret Thatcher?
vii. Makundi makuu yanayounda jamii ya watanzania ni pamoja na
viii. . . . . . hawa shughuli zao ni uwindaji na ukusanyaji wa matunda ya porini.
ix. Asili ya kabila la kibantu ni ..
x. Kwanini inasemekana taifa la Tanzania ni taifa la kipekee, hii ni kwa sababu ?
Majibu
| i | ii | iii | iv | v | vi | vii | viii | ix | x |
| . |
2. Oanisha maana ya dhana za kisarufi zilizo katika Orodha A na dhana zilizopo katika Orodha B kisha andika herufi ya jibu sahihi katika kisanduku ulichopewa.
| ORODHA A | ORODHA B |
|
|
Majibu
| i | ii | iii | iv | v |
SEHEMU B (ALAMA 70)
JIBU KWA UFUPI
3. Maadili ya jamii za Kitanzania yamejengwa kupitia mila na desturi mbalimbali katika vipindi tofauti maadili hayo ni; (hoja 5)
4. Eleza umuhimu wa kujifunza historia yetu kama watanzania (hoja 5)
5. “Rushwa ni adui wa haki.” Kwa kutumia hoja 5 thibitisha kauli hii;
6. Kwa kutumia hoja tano bainisha ni kwanamna gani unaweza kutofautisha baina ya kabila moja na makabila mengine.
7. Taja sababu 5 za jamii ya asili ya Tanzania kuhama kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine
8. Jamii mbalimbali za kitanzania zilikuwa zinajihusisha na shughuli mbalimbali kabla ya ujio wa wakoloni.Taja shughuli kuu tano (5) zilizofanywa na makundi ya jamii za Kitanzania kabla ya uhuru.
9. Tanzania ina urithi wa asili ambao ni muhimu kwa maendeleo ya nchi. Ukiwa kama mwanafunzi wa kidato cha kwanza taja utajiri wa rasilimali za asili tulizonazo.
SEHEMU C (Alama 15)
Jibu swali hili kwa umakini, hakikisha unafuata kanuni zote za uandishi wa insha
10. Urithi wa kihistoria wa jamii za Kitanzania unajumuisha lugha, mila, desturi,muziki na ngoma za asili. Ukiwa kama mwananchi wa Tanzania eleza umuhimu wa urithi wa kihistoria. {hoja 6}.
FORM ONE HISTORIA EXAM SERIES 270
FORM ONE HISTORIA EXAM SERIES 270
JINA LA MWANAFUNZI: _______________________________
OFISI YA WAZIRI MKUU TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
MTIHANI WA MUHULA KIDATO CHA KWANZA
HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI
MUDA: 2:30 MASAA MEI, 2026
MAELEKEZO.
| KWA MATUMIZI YA MTAHINI | ||
| Namba ya swali | Alama | Saini ya Mtahini |
| 1 | ||
| 2 | ||
| 3 | ||
| 4 | ||
| 5 | ||
| 6 | ||
| 7 | ||
| 8 | ||
| 9 | ||
| 10 | ||
| Jumla | ||
| Mhakiki | ||
SEHEMU A [Alama 15]
1. Katika vipengele[i] hadi [x] chagua herufi ya jibu sahihi kisha andika herufi ya jibu hilo katika visanduku ulivyopewa.
i. Mvalingundi ni kiongozi wa taasisi binafsi anayetumi mali za taasisi na ofisi kwa maslahi binafsi kitendo hiki anachofanya mvulingundi kinaweza kutafsiriwa kama?
ii. Katika hotuba yake juu ya ustawi wa maadili na maliasili za taifa waziri mkuu alizungumzia majukumu yanayohusiana na uhifadhi na ulinzi wa urithi wa taifa na maadili unadhani ni nani haswa anayehusika na ulinzi huo kwa maendeleo ya taifa letu?
iii. Wakati wa ufundishaji wa moja ya mada darasani, mwalimu sochora alisema ‘’ ni kikundi cha watu wenye uhusiano wa kidamu, ndoa au kuasili ‘’ maana hii inaendana na lipi kati ya vipengele vifuatavyo?
iv. Sababu ya kujifunza historia ya Tanzania na maadili ni
v. Katika jamii za kibantu, elimu ilikuwa inatolewa kwa njia kuu mbili nazo ni
vi. Ni kitendo cha wageni kukaribishwa kwa furaha na kupewa heshima kubwa
vii. Nchi ya Tanzania imebarikiwa kuwa na makundi yote ya makabila yanayopatikana barani Africa kati ya makundi hayo kundi moja linachukua asilimia kubwa zaidi ya makabila ya watanzania wa leo lipi kati ya makundi hayo linathibitiwa ukweli huu wa kihostoria.
viii. Amani anajivunia kuwa miongoni mwa wanafunzi wanaosoma somo la historia ya Tanzania na maadili kwa kuwa limuwezesha kuwa na mapenzi na nchi yake kitendo hiki cha amani kuipenda nchi yake kinajulikana kuwa ni.
ix. Tanganyika ilipata uhuru wake mwaka 1961. Je ni nani alikuwa waziri mkuu wa kwanza wa Tanganyika.
x. Mwanafunzi anaposwa kufanya matendo yanayoendana na taratibu kanuni na sheria za shule kwani ni wajibu wake kati ya matendo yafuatayo lipi si wajibu wa mwanafunzi
MAJIBU
| i | ii | iii | iv | v | vi | vii | viii | ix | x |
2. Oanisha vinavyohusu jamii ya wamasai vilivyopo katika Orodha A na kundi husika kutoka Orodha B kisha andika herufu ya jibu sahihi katika kuzanduku ulichopewa;
| Orodha A | Orodha B |
|
|
MAJIBU
| Orodha A | i | ii | iii | iv | v |
| Orodha B |
SEHEMU B [Alama 10 ]
Jibu maswali yote katika sehemu hii
3. Wanafunzi wa mkondo wa biashara wa shule ya secondari mikengo walitakiwa kufanya utafiti kwa njia ya mtandao ili kubaini shughuli mbalimbali zilizofanywa na makundi ya jamii ya asili ya kitanzania unadhani ni shughuli zipi walizibaini na kuzinukuu katika madaftari yao [taja nukta 5]
4. Arianna na lan wamekuwa wakichanganya dhana ya matendo yasiyofaa katika jamii waeleweshe arrianna na alan matendo yasiyofaa katika jamii kwa kuwapa mifano mitano ya matendo yasiyofaa katika jamii kwa kuwapa mifano mitano ya matendo hayo yasiofaa
5. Kuanzishwa kwa somo la histori ya Tanzania na maadili kumeibua mijadala mbalimbali miongoni mwa watu wapo baadhi yao wanaona kuwa hakukuwa na tija ya kuanzishwa kwa somo hili ukiwa kama mwanafunzi wa somo hili wape sababu tano zitakazofanya wabadili mtazamo walionao juu ya somo hii
6. Mashamu ni mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule ya secondari mazebe ameshindwa kuelewa baadhi ya vipengele vya mada ya pili katika somo la historia ya Tz na maadili msaidie aelewe kwa kumueleza maana ya vipengele
7. Jamii yoyote isiyo na maadili inakuwa ni jamii mfuu . Maaadili katika jamii zetu yanachangia sehemu kubwa ya maendeleo ya watu na taifa zetu [taja nukta tano]
8. Taja sababu tano [5] za jamii ya asili ya Tanzania kuhama kutoka sehemu moja kwenda sehemu myingine
9. Bainisha matendo matano [5] ya kimaadili unayotenda au kutendewa na wenzako shuleni.
SEHEMU C [alama 15]
Jibu swali la kumi[10]
10. Eleza kwa hoja tano matarajio yako ya kujifunza somo la historia ya Tanzania na maadili
FORM ONE HISTORIA EXAM SERIES 262
FORM ONE HISTORIA EXAM SERIES 262
OFISI YA WAZIRI MKUU TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
MTIHANI WA MUHULA KIDATO CHA KWANZA
HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI
MUDA SAA 2:30 MEI,2026
MAELEKEZO
SEHEMU A ( Alama 20)
Jibu maswali yote katika sehemu hii.
1. Chagua jibu sahihi kutoka kwenye majibu yaliyotolewa na andika herufi yake katika nafasi uliyopewa.
(i) Historia ya Tanzania inahusu nini?
(ii) Jamii za kwanza za Watanzania zilihamia toka wapi?
(iii) Lugha inayotumiwa naWabantu wengi wa Tanzania ni ipi?
(iv) Kundi lipi la jamii lilikuwa mahiri katika uwindaji?
(v) Miongoni mwa hizi ni ipi njia moja ya kutunza historia ya Tanzania?.
(vi) Historia ya Tanzania inaweza kuhifadhiwa kwanjia gani?
(vii) Moja ya sifa ya jamii za asili za kibantu ni ipi?
(viii) Nini maana ya urithi wa Taifa?
(ix) Moja ya tamaduni za asili zinazotumiwa kulinda maadili katika jamii ni?.
(x) Kundi lipi kati ya haya lilihusika zaidi katika ufugaji wa asili?
MAJIBU
| i | ii | iii | iv | v | vi | vii | viii | ix | x |
| . |
2. Oanisha maudhui ya Kundi A na yale ya Kundi B kwa kuandika herufi ya jibu sahihi.
| Kundi A | Kundi B |
| (i) Wabantu walihamiaTanzaia kutoka. (ii) Lugha inayozungumzwa zaidi naWabantu. (iii) Wakushito wanapatikana zaidi. (iv) Moja ya shughuli za Wanito. (v) Moja ya nia ya kuhifadhi historia. |
|
Majibu
| i | ii | iii | iv | v |
| . |
SEHEMU B (Alama 80)
Jibu maswali yote katika sehemu hii
3. (a) Eleza maana ya Historia ya Tanzani. (alama 4)
(b) Taja matukio sita(06) kihistoria unayo yafahamu. (alama 6)
4. a) Taja jamii kuu nne (04) za asili za Kitanzania.(alama 4)
b) Eleza asili ya jamii za wabantu na shughuli zao za kiuchumi (alama 6)
5. a) Jamii ni nini?( alama 4)
b) Kuna umuhimu gani watu kuishi katika jamii? (alama 6)
6.(a) Maadili ni nini? (alama 4)
(b) Umuhimu wa maadili kwa taifa unaweza kutazamwa katika mambo mbalimbali .Taja mambo manne (alama 6)
7. (a) Unadhani ni vitu gani vina changia tabia njema? Eleza vinne(4) (alama 4)
(b) Bainisha matendo manne ya kimaadili unayotenda au kutendewa na wenzako shuleni (alama 6)
8. (a) Eleza maana ya urithi ( alama 04)
(b) Taja matendo manne yanayokuza na kulinda maadili na urithi wa Tanzania (alama 6)
SEHEMU C(Alama 15)
Jibu swali moja(1) tu.
9.Eleza umuhimu wa somo la historia ya Tanzania na maadili kwa kutumia hoja tano (05)
10.Fafanua sababu tano za kuhama hama kwa Watanzania
FORM ONE HISTORIA EXAM SERIES 258
FORM ONE HISTORIA EXAM SERIES 258
JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, OFISI YA RAIS – TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
MTIHANI WA KUMALIZA MUHULA
HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI
KIDATO CHA KWANZA
MUDA: SAA 2:30 2025
MAELEKEZO
SEHEMU A (Alama 15)
Jibu maswali yote katika sehemu hii
1. Katika vipengele (i) – (x), chagua herufi ya jibu sahihi kisha andika herufi ya jibu hilo katika visanduku ulivyopewa.
(i) Bibi Halima alishuhudia baadhi ya wanakijiji wa kijiji cha madongo wakitupa taka katika vyanzo vya maji. Katika kutimiza wajibu wake aliwaeleza kuwa wanaharibu urithi wa taifa. Urithi uliokusudiwa na bibi Halima unaingia katika kipengele kipi kati ya vifuatavyo?
(ii) Ulinzi wa Historia ya Tanzania ni jukumu la kila Mtanzania mwenye mapenzi mema na Taifa hili la Tanzania. Ipi ni njia bora na sahihi ya kulinda historia ya Tanzania?
(iii) Nyimbo na ngoma za jadi huimbwa na kupigwa kwa makusudi makubwa kabisa. Ni kipi kati ya yafuatayo huimarishwa pale ngoma na nyimbo zinapohusishwa?
(iv) Michoro inayochorwa maeneo mbalimbali ya kuhistoria ina makusudi makubwa katika nchi yetu ya Tanzania. Nini nia kubwa ya kuchora picha maeneo ya kihistoria?
(v) Nyimbo za jadi huimbwa na makabila mbalimbali hapa nchini Tanzania. Je! Ni wakati gani unaofaa kuimba nyimbo hizi za jadi?
(vi) Katika hotuba yake juuya ustawi wa maadili na maliasili za taifa, waziri mkuu alizungumzia majukumu yanayohusiana na uhifadhi na ulinzi wa urithi wa taifa na maadili. Unadhani ni nani hasa anahusika na ulinzi huo wa maendeleo ya taifa letu?
(vii) Mabadiliko gani yamekuwa yakizingatiwa katika historia ya Tanzania?
(viii) Makundi katika jamii za Kitanzania hujishughulisha na shughuli mbalimbali ambazo huwapatia kipato. Ipi si shughuli ya wanilo kati ya hizi zifuatazo?
(ix) “Kupokea au kutoa mali isiyo halali au kutumia mali ya umma isivyo halali kwa manufaa binafsi.” Maelezo haya yanahitimishwa na neno lipi kati ya haya yafuatayo?
(x) Watanzania wote bila kujali kabila, imani, rangi na dini hatunabudi kuzingatia miongozo, kanuni na sheria zinazoongoza mienendo ya mtu mmoja mmoja katika nchi yetu. Lipi ni jina moja linalojumuisha miongozo hiyo?
MAJIBU
| i | ii | iii | iv | v | vi | vii | viii | ix | x |
2. Oanisha sentensi kutoka kundi A na zile za kundi B, kisha andika herufi ya jibu sahihi katika kisanduku ulichopewa hapo chini.
| KUNDI A | KUNDI B | ||||
| (i) Njia ya kuhifadhi historia ya jamii (ii) Mfano wa maadili ya kitanzania (iii) Michezo ya jadi (iv) Namna ya kuhifadhi urithi wa taifa (v) Umuhimu wa kulinda na kutunza historia ya taifa |
| ||||
| KUNDI A | i | ii | iii | iv | v |
| KUNDI B | |||||
SEHEMU B (Alama 70)
Jibu maswali yote katika sehemu hii
3. Taja shughuli tano (5) za kijamii na kiuchumi zinazofanywa na jamii ya wakichembe katika maisha yao ya kila siku.
4. (a) Eleza maana ya urithi wa Taifa
________________________________________________________________________________________________________________________________________________
(b) Taja njia nne (4) zinazotumika kuhifadhi urithi wa taifa:-
i) ______________________________________________________________________
ii) ______________________________________________________________________
iii) _____________________________________________________________________
iv) _____________________________________________________________________
5. (a) Taja michezo miwili ya jadi inayotumika kuendeleza maadili
(b) Eleza namna michezo hiyo inavyosaidia watoto kujifunza maadili.
i) ______________________________________________________________________
ii) ______________________________________________________________________
iii)______________________________________________________________________
6. Bainisha mifano mitano ya maadili mbalimbali katika jamii za Kitanzania ambayo ingefaa kuigwa na kudumishwa kwa vizazi vijavyo.
7. (a) Bainisha makabila mawili (2) ambayo yanatokana na jamii za wakichembe.
(b) Taja zana tatu (3) zilizotumika katika uwindaji katika jamii ya Wakichembe.
i) __________________________________________________________________
ii) __________________________________________________________________
iii) __________________________________________________________________
8. Jamii za watu wa visiwa vya Zanzibar walinunua na kuuza bidhaa kupitia biashara walizofanya na waajemi, waarabu na watu wa mashariki ya mbali. Taja bidhaa tano (5) zilizohusika katika biashara hiyo.
9. Kwa nini jamii za asili ya Kitanzania zilihama kutoka eneo moja kwenda eneo lingine? Toa hoja tano (5).
SEHEMU C (Alama 15)
Jibu swali hili kwa insha
10. Eleza hoja sita (6) ukionesha matarajio yako ya kujifunza somo la Historia ya Tanzania na Maadili.
FORM ONE HISTORIA EXAM SERIES 203
FORM ONE HISTORIA EXAM SERIES 203