FORM ONE HISTORIA TERMINAL EXAMS

OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SEREKALI ZA MITAA

MTIHANI WA MUHULA HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI

KIDATO CHA KWANZA

MUDA: 2:30 MEI 2026

Maelekezo;

  • Mtihani huu una sehemu A, B na C
  • Jibu maswali yote
  • Pangilia insha yako vizuri 

SEHEMU A. (Alama 15)

1. Kutoka kipengele i- x chagua herufi ya jibu sahihi. Kisha andika jibu kwenye sehemu ya kujibia.

i. Somo la Historia ya Tanzania na Maadili limeundwa na dhana kuu mbili, dhana hizo ni pamoja na

  1. Historia ya Tanzania na afrika mashariki
  2. Historia ya Tanzania na jamii zake za makabila
  3. Historia ya Tanzania na maadili yake
  4. Historia ya Tanzania na mila zetu za asili

ii. Historia kuhusu mambo au matukio yaliyopita yenye athari kiuchumi,kisiasa,na kiutamaduni katika jamii imesababishwa na matukio kadhaa yakiwemo;

  1. Biashara,siasana mwingiliano
  2. Biashara ya watumwa,,ukoloni, na vita
  3. Biashara ya watumwa,ukoloni mambo leo,na utandawazi
  4. Biashara ya watumwa, vita ya wenyewe kwa wenyewewe na ukabila

iii. Lengo la somo la Historia ya Tanzania na Maadili ni pamoja na

  1. Kuelewa tulipo na kutafakari tunapokwenda
  2. Kuelewa dhana ya maadili ya mtanzania
  3. Kujua asili yetu kimakabila
  4. Kuelewa tulipotoka, kujua tulipo na kutafakari tunapoelekea

iv. Kwanini ni muhimu kujua historia yetu

  1. Ili tusijisahau kama taifa juu ya makabila yetu
  2. Ili kujitambua kama mtanzania halisi na mzalendo
  3. Ili kujua tulipo toka tulipo na tunapoelekea kama taifa
  4. Ili taifa letu la Tanzania lisipoteze muelekeo kwa watu wake.

v. Ungepewa nafasi ya kusimamia maadili shuleni, je ungependa ujadili kuhusu ni niini?

  1. Historia yetu kama nchi na rasilimali zilizopo
  2. Nchi yetu ya Tanzania na watu wake
  3. Taifa letu la Tanzania na Imani zake
  4. Tabia na matendo yetu

vi. Wanazuoni na wanafalsafa mbalimbali wametoa fasili tofautitofauti juu za dhana ya jamii kati  ya hizi zifuatazo ni ipi fasili ya dhana ya jamii kwa mujibu wa mtaalam Margaret Thatcher?

  1. Ni mkusanyiko wa watu kwa ujumla wake  
  2. Ni jumla ya watu mmoja mmoja  
  3. Ni watu ambao ni wanawake na wanaume na familia zao
  4. Ni mkusanyiko wa watu ambao ni watanzania wenye akili timamu

vii. Makundi makuu yanayounda jamii ya watanzania ni pamoja na

  1. Wakichembe,wabantu na wamaasai
  2. Wakichembe,wanilo na wahadzabe
  3. Wakushito,wanilo na wasukuma
  4. Wakushito wakichembe na wabantu 

viii. . . . . . hawa shughuli zao ni uwindaji na ukusanyaji wa matunda ya porini.

  1. Wamaasai na wadatoga
  2. Wahadzabe na wasandawe
  3. Waha na wasukuma
  4. Wabantu na wazaramo

ix. Asili ya kabila la kibantu ni ..

  1. Waafroasiatiki kutoka bara la Asia
  2. Afrika magharibi
  3. Kutoka kwenye pembe ya Afrika
  4. Mashariki ya kati kupitia mto naili

x. Kwanini inasemekana taifa la Tanzania ni taifa la kipekee, hii ni kwa sababu ?

  1. Ukarimu wa watanzania
  2. Ni muunganiko wa makabilo yote yanayopatikana afrika na makabila hayo yanaishi kwa umoja na mshikamano
  3. Ni mkusanyiko wa makabila tofauti yasiyojua asili yao
  4. Ni watu bahili sana na wenye ubaguzi hasa ubaguzi wa kimakabila na kiukanda

Majibu

i ii iii iv v vi vii viii ix x









.

2. Oanisha maana ya dhana za kisarufi zilizo katika Orodha A na dhana zilizopo katika Orodha B kisha andika herufi ya jibu sahihi katika kisanduku ulichopewa.

ORODHA A

ORODHA B

  1. Wanilo 
  2. Wakushito 
  3. Wakichembe 
  4. Jamii ya visiwa vya Zanzibar.
  5. Wabantu
  1. asili yao ni Afrika magharibi katika maeneo ya kameruni na Nijeria na kutawanyika kupiyia misitu ya kongo
  2. inahusisha makabila ya Wairaki,Wagorowa na Waburungi.kiasili ni wakulima na wafugaji.
  3. hawa ndio wakazi wa mwanzo wa jamii ya watanzania, shughuli zao ni uwindaji na ukusanyji wa matunda.
  4. hawa ni washirazi, ambao wametokana na mwingiliano wa kibiashara baina ya waarabu na waajemi
  5. hawa ni jamii ya wafugaji ambao kwasasa ni wamasai,wajaluo na wadatoga

Majibu

i ii iii iv v





SEHEMU B (ALAMA 70)

JIBU KWA UFUPI

3. Maadili ya jamii za Kitanzania yamejengwa kupitia mila na desturi mbalimbali katika vipindi tofauti maadili hayo ni; (hoja 5)

4. Eleza umuhimu wa kujifunza historia yetu kama watanzania (hoja 5)

5. “Rushwa ni adui wa haki.” Kwa kutumia hoja 5 thibitisha kauli hii;

6. Kwa kutumia hoja tano bainisha ni kwanamna gani unaweza kutofautisha baina ya kabila moja na makabila mengine.

7. Taja sababu 5 za jamii ya asili ya Tanzania kuhama kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine

8. Jamii mbalimbali za kitanzania zilikuwa zinajihusisha na shughuli mbalimbali kabla ya ujio wa wakoloni.Taja shughuli kuu tano (5) zilizofanywa na makundi ya jamii za Kitanzania kabla ya uhuru.

9. Tanzania ina urithi wa asili ambao ni muhimu kwa maendeleo ya nchi. Ukiwa kama mwanafunzi wa kidato cha kwanza taja utajiri wa rasilimali za asili tulizonazo.

SEHEMU C (Alama 15)

Jibu swali hili kwa umakini, hakikisha unafuata kanuni zote za uandishi wa insha

10. Urithi wa kihistoria wa jamii za Kitanzania unajumuisha lugha, mila, desturi,muziki na ngoma za asili. Ukiwa kama mwananchi wa Tanzania eleza umuhimu wa urithi wa kihistoria. {hoja 6}.

FORM ONE HISTORIA EXAM SERIES 270  

FORM ONE HISTORIA EXAM SERIES 270  

JINA LA MWANAFUNZI: _______________________________

OFISI YA WAZIRI MKUU TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MTIHANI WA MUHULA KIDATO CHA KWANZA

HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI

MUDA: 2:30 MASAA MEI, 2026

MAELEKEZO.

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B, na C zenye jumla ya maswali kumi
  2. Jibu maswali yote kwenye nafasi ulizopewa
  3. Sehemu A ina alama, kumi na tano [15]  na sehemu B ina alama [10] kila moja na sehemu C ina alama kumi na tano [15]
KWA MATUMIZI YA MTAHINI
Namba ya swali Alama Saini ya Mtahini
1

2

3

4

5

6

7

8

9

10

Jumla

 Mhakiki

SEHEMU A [Alama 15]

1. Katika vipengele[i] hadi [x] chagua herufi ya jibu sahihi kisha andika herufi ya jibu hilo katika visanduku ulivyopewa.

i. Mvalingundi ni kiongozi wa taasisi binafsi anayetumi mali za taasisi na ofisi kwa maslahi binafsi kitendo hiki anachofanya mvulingundi kinaweza kutafsiriwa kama? 

  1. Uwajibikaji
  2. Rushwa
  3. Ujanja
  4. Wizi wa wazi 

ii. Katika hotuba yake juu ya ustawi wa maadili na maliasili za taifa waziri mkuu alizungumzia majukumu yanayohusiana na uhifadhi na ulinzi wa urithi wa taifa na maadili unadhani ni nani haswa anayehusika na ulinzi huo kwa maendeleo ya taifa letu?

  1. Raisi wa Tz
  2. Mkuu wa majeshi
  3. Kila mtanzania
  4. Afisa maliasi 

iii. Wakati wa ufundishaji wa moja ya mada darasani, mwalimu sochora alisema ‘’ ni kikundi cha watu wenye uhusiano wa kidamu, ndoa au kuasili ‘’ maana hii inaendana na lipi kati ya vipengele vifuatavyo?

  1. Kabila
  2. Ukoo
  3. Jamii
  4. Familia 

iv. Sababu ya kujifunza historia ya Tanzania na maadili ni 

  1. Kujifurahisha
  2. Kulinda mipaka ya nchi
  3. Kuelewa tulipotoka na tulipo
  4. Kuvumja heshima

v. Katika jamii za kibantu, elimu ilikuwa inatolewa kwa njia kuu mbili nazo ni

  1. Kulazimishwa na kushauriwa
  2. Mapishi na ufugaji
  3. Jando na unyago
  4. Kuwinda na kurina asali 

vi. Ni kitendo cha wageni kukaribishwa kwa furaha na kupewa heshima kubwa

  1. Amani
  2. Chereko
  3. Maendeleo
  4. Ukarimu 

vii. Nchi ya Tanzania imebarikiwa kuwa na makundi yote ya makabila yanayopatikana barani Africa kati ya makundi hayo kundi moja linachukua asilimia kubwa zaidi ya makabila ya watanzania wa leo lipi kati ya makundi hayo linathibitiwa ukweli huu wa kihostoria.

  1. Wanilo
  2. Wabantu
  3. Wakushito
  4. Wakichembe 

viii. Amani anajivunia kuwa miongoni mwa wanafunzi wanaosoma somo la historia ya Tanzania na maadili kwa kuwa limuwezesha kuwa na mapenzi na nchi yake kitendo hiki cha amani kuipenda nchi yake kinajulikana kuwa ni.

  1. Mapenzi ya kweli
  2. Utu
  3. Uzalendo
  4. Ukarimu 

ix. Tanganyika ilipata uhuru wake mwaka 1961. Je ni nani alikuwa waziri mkuu wa kwanza wa Tanganyika. 

  1. Rashidi kawawa
  2. Julius k.nyerere
  3. Bibi titi Mohamed
  4. Abed amani karume

x. Mwanafunzi anaposwa kufanya matendo yanayoendana na taratibu kanuni na sheria za shule kwani ni wajibu wake kati ya matendo yafuatayo lipi si wajibu wa mwanafunzi

  1. Kuwa shuleni
  2. Kusoma kwa bidii
  3. Kutii sheria za shule
  4. Kuwa mtukutu

MAJIBU

i ii iii iv v vi vii viii ix x










2. Oanisha vinavyohusu jamii ya wamasai vilivyopo katika Orodha A na kundi husika kutoka Orodha B kisha andika herufu ya jibu sahihi katika kuzanduku ulichopewa;

Orodha A

Orodha B

  1. Kundi rika la vijana wa kimasai wenye wajibu wa kuhakikisha ulinzi na usalama wa jamii zao.
  2. Kiongozi wa juu zaida wa kisiasa wa kabila la wamasai.
  3. Kundi muhimu katika jamii ya kimasai lenye watu wenye umri kuanzia miaka 40 na kuendelea lenye majukumu ya kufanya maamuzi na kusuluhisha migogoro.
  4. Uhusika zaidi na shughuli za nyumbani ukamuaji wa maziwa na ujenzi wa nyumba.
  5. Majukumu yao karibu na yalipo makazi ya jamii zao.
  1. Ol aiguanani
  2. Wazee
  3. Wabarabaigi
  4. Laibon
  5. Watoto wa miaka 0-8
  6. Marani
  7. Watoto wa miaka 8-18
  8. Wanilo
  9. Wanawake

MAJIBU

Orodha A i ii iii iv v
Orodha B




SEHEMU B [Alama 10 ]

Jibu maswali yote katika sehemu hii

3. Wanafunzi wa mkondo wa biashara wa shule ya secondari mikengo walitakiwa kufanya utafiti kwa njia ya mtandao ili kubaini shughuli mbalimbali zilizofanywa na makundi ya jamii ya asili ya kitanzania unadhani ni shughuli zipi walizibaini na kuzinukuu katika madaftari yao [taja nukta 5]

4. Arianna na lan wamekuwa wakichanganya dhana ya matendo yasiyofaa katika jamii waeleweshe arrianna na alan matendo yasiyofaa katika jamii kwa kuwapa mifano mitano ya matendo yasiyofaa katika jamii kwa kuwapa mifano mitano ya matendo hayo yasiofaa

5. Kuanzishwa kwa somo la histori ya Tanzania na maadili kumeibua mijadala mbalimbali miongoni mwa watu wapo baadhi yao wanaona kuwa hakukuwa na tija ya kuanzishwa kwa somo hili ukiwa kama mwanafunzi wa somo hili wape sababu tano zitakazofanya wabadili mtazamo walionao juu ya somo hii

6. Mashamu ni mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule ya secondari mazebe ameshindwa kuelewa baadhi ya vipengele vya mada ya pili katika somo la historia ya Tz na maadili msaidie aelewe kwa kumueleza maana ya vipengele

  1. Maadili 
  2. Jamii 
  3. Familia 
  4. Ukoo
  5. Kabila

7. Jamii yoyote isiyo na maadili inakuwa ni jamii mfuu . Maaadili katika jamii zetu yanachangia sehemu kubwa ya maendeleo ya watu na taifa zetu [taja nukta tano]

8. Taja sababu tano [5] za jamii ya asili ya Tanzania kuhama kutoka sehemu moja kwenda sehemu myingine

9. Bainisha matendo matano [5] ya kimaadili unayotenda au kutendewa na wenzako shuleni.

SEHEMU C [alama 15]

 Jibu swali la kumi[10]

10. Eleza kwa hoja tano matarajio yako ya kujifunza somo la historia ya Tanzania na maadili

FORM ONE HISTORIA EXAM SERIES 262  

FORM ONE HISTORIA EXAM SERIES 262  

OFISI YA WAZIRI MKUU TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MTIHANI WA MUHULA KIDATO CHA KWANZA

HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI

MUDA SAA 2:30 MEI,2026

MAELEKEZO

  • Karatasi hii ina sehemu A na B zenye jumla ya maswali sita (06)
  • Jibu maswali kufuatana na melekezo.

SEHEMU A ( Alama 20)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1. Chagua jibu sahihi kutoka kwenye majibu yaliyotolewa na andika herufi yake katika nafasi uliyopewa.

(i) Historia ya Tanzania inahusu nini?

  1. Wanyama na mimea 
  2. Watu, matukio na maendeleo yao
  3. Sayansi naTeknolojia 
  4. Michezo na burudani

(ii) Jamii za kwanza za Watanzania zilihamia toka wapi?

  1. Asia 
  2. Ulaya 
  3. Afrika ya kati naMagharibi 
  4. Amerika Kusini

(iii) Lugha inayotumiwa naWabantu wengi wa Tanzania ni ipi?

  1. Kiarabu 
  2. Kichina 
  3. Kifaransa 
  4. Kiswahili

(iv) Kundi lipi la jamii lilikuwa mahiri katika uwindaji?

  1. Wabantu 
  2. Wakichemba 
  3. Wanilo 
  4. Wakushito

(v) Miongoni mwa hizi ni ipi njia moja ya kutunza historia ya Tanzania?.

  1. Kupuuza mila na desturi 
  2. Kuchora maandiko ya kale
  3. Kufanya utafiti wa kihistoria 
  4. Kuiga tamaduni zakigeni

(vi) Historia ya Tanzania inaweza kuhifadhiwa kwanjia gani?

  1. Kuandika vitabu vya historia ya Tanzania
  2. Kusimulia hadithi zisizo na ukweli
  3. Kuacha kuandika historia
  4. Kuharibu kumbukumbu za kihistoria

(vii) Moja ya sifa ya jamii za asili za kibantu ni ipi?

  1. Ushirikiano 
  2. Ufisadi 
  3. Ubaguzi wa kijamii 
  4. Kutegemea misaada

(viii) Nini maana ya urithi wa Taifa?

  1. Mali ya viongozi waserikali
  2. Historia, tamaduni na rasilimali za nchi
  3. Bidhaa zinazouzwa nje ya nchi
  4. Elimu inayo tolewa shuleni

(ix) Moja ya tamaduni za asili zinazotumiwa kulinda maadili katika jamii ni?.

  1. Kunyanyasa wengine 
  2. Ukaidi na kiburi 
  3. Uonevu na ubaguzi 
  4. Upendo na mshikamano

(x) Kundi lipi kati ya haya lilihusika zaidi katika ufugaji wa asili?

  1. Wanilo 
  2. Wabantu 
  3. Wakihemba 
  4. Wakushito

MAJIBU

i ii iii iv v vi vii viii ix x









.

2. Oanisha maudhui ya Kundi A na yale ya Kundi B kwa kuandika herufi ya jibu sahihi.

Kundi A Kundi B

(i) Wabantu walihamiaTanzaia kutoka.

(ii) Lugha inayozungumzwa zaidi naWabantu.

(iii) Wakushito wanapatikana zaidi.

(iv) Moja ya shughuli za Wanito.

(v) Moja ya nia ya kuhifadhi historia.

  1. Kuandika kumbukumbu
  2. Ufugaji
  3. Kusini mwa Tanzania
  4. Kiswahili
  5. Afrika Magharibi na kati

Majibu

i ii iii iv v




.

SEHEMU B (Alama 80)

Jibu maswali yote katika sehemu hii

3. (a) Eleza maana ya Historia ya Tanzani. (alama 4)

(b) Taja matukio sita(06) kihistoria unayo yafahamu. (alama 6)

4. a) Taja jamii kuu nne (04) za asili za Kitanzania.(alama 4)

b) Eleza asili ya jamii za wabantu na shughuli zao za kiuchumi (alama 6)

5. a) Jamii ni nini?( alama 4)

b) Kuna umuhimu gani watu kuishi katika jamii? (alama 6)

6.(a) Maadili ni nini? (alama 4)

(b) Umuhimu wa maadili kwa taifa unaweza kutazamwa katika mambo mbalimbali .Taja mambo manne (alama 6)

7. (a) Unadhani ni vitu gani vina changia tabia njema? Eleza vinne(4) (alama 4)

(b) Bainisha matendo manne ya kimaadili unayotenda au kutendewa na wenzako shuleni (alama 6)

8. (a) Eleza maana ya urithi ( alama 04)

(b) Taja matendo manne yanayokuza na kulinda maadili na urithi wa Tanzania (alama 6)

SEHEMU C(Alama 15) 

Jibu swali moja(1) tu.

9.Eleza umuhimu wa somo la historia ya Tanzania na maadili kwa kutumia hoja tano (05)

10.Fafanua sababu tano za kuhama hama kwa Watanzania

FORM ONE HISTORIA EXAM SERIES 258  

FORM ONE HISTORIA EXAM SERIES 258  

JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, OFISI YA RAIS – TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MTIHANI WA KUMALIZA MUHULA

HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI

KIDATO CHA KWANZA

MUDA: SAA 2:30  2025

MAELEKEZO

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi (10).
  2. Jibu maswali yote kwenye sehemu ulizopewa.
  3. Sehemu A na C zina alama kumi na tano (15) kila moja na sehemu C alama sabini (70).
  4. Zingatia maelekezo ya kila sehemu na kila swali
  5. Andika namba yako sahihi uliyosajiliwa nayo

SEHEMU A (Alama 15)

Jibu maswali yote katika sehemu hii

1. Katika vipengele (i) – (x), chagua herufi ya jibu sahihi kisha andika herufi ya jibu hilo katika visanduku ulivyopewa.

(i) Bibi Halima alishuhudia baadhi ya wanakijiji wa kijiji cha madongo wakitupa taka katika vyanzo vya maji. Katika kutimiza wajibu wake aliwaeleza kuwa wanaharibu urithi wa taifa. Urithi uliokusudiwa na bibi Halima unaingia katika kipengele kipi kati ya vifuatavyo?

  1. Urithi usioshikika
  2. Urithi wa asili
  3. Urithi unaoshikika
  4. Urithi wa kale.

(ii) Ulinzi wa Historia ya Tanzania ni jukumu la kila Mtanzania mwenye mapenzi mema na Taifa hili la Tanzania. Ipi ni njia bora na sahihi ya kulinda historia ya Tanzania?

  1. Kufuta mila za jadi
  2. Kurekodi kumbukumbu
  3. Kuharibu maeneo ya kihistoria
  4. Kuiga tamaduni za kigeni.

(iii) Nyimbo na ngoma za jadi huimbwa na kupigwa kwa makusudi makubwa kabisa. Ni kipi kati ya yafuatayo huimarishwa pale ngoma na nyimbo zinapohusishwa?

  1. Teknolojia
  2. Maadili ya jamii
  3. Ubaguzi wa kijamii
  4. Mazoea ya kigeni

(iv) Michoro inayochorwa maeneo mbalimbali ya kuhistoria ina makusudi makubwa katika nchi yetu ya Tanzania. Nini nia kubwa ya kuchora picha maeneo ya kihistoria?

  1. Kujitafutia umaarufu 
  2. Kukuza maadili 
  3. Kuhifadhi urithi
  4. Kujaribu uchoraji

(v) Nyimbo za jadi huimbwa na makabila mbalimbali hapa nchini Tanzania. Je! Ni wakati gani unaofaa kuimba nyimbo hizi za jadi?

  1. Skukuu za kidini tu
  2. Tamasha la kisiasa
  3. Shughuli za kijadi kama harusi
  4. Maonesho ya magari

(vi) Katika hotuba yake juuya ustawi wa maadili na maliasili za taifa, waziri mkuu alizungumzia majukumu yanayohusiana na uhifadhi na ulinzi wa urithi wa taifa na maadili. Unadhani ni nani hasa anahusika na ulinzi huo wa maendeleo ya taifa letu?

  1. Rais wa Tanzania
  2. Mkuu wa majeshi
  3. Kila mtanzani
  4. Afisa maliasili

(vii) Mabadiliko gani yamekuwa yakizingatiwa katika historia ya Tanzania?

  1. Mabadiliko ya hali ya hewa
  2. Mabadiliko ya teknolojia pekee
  3. Mabadiliko ya kijamii, kisiasa na kiuchumi
  4. Mabadiliko ya michezo

(viii) Makundi katika jamii za Kitanzania hujishughulisha na shughuli mbalimbali ambazo huwapatia kipato. Ipi si shughuli ya wanilo kati ya hizi zifuatazo?

  1. Ufugaji 
  2. Uwindaji 
  3. Kilimo
  4. Uvuvi 

(ix) “Kupokea au kutoa mali isiyo halali au kutumia mali ya umma isivyo halali kwa manufaa binafsi.” Maelezo haya yanahitimishwa na neno lipi kati ya haya yafuatayo?

  1. Ukoloni
  2. Takrima 
  3. Rushwa
  4. Udhalimu 

(x) Watanzania wote bila kujali kabila, imani, rangi na dini hatunabudi kuzingatia miongozo, kanuni na sheria zinazoongoza mienendo ya mtu mmoja mmoja katika nchi yetu. Lipi ni jina moja linalojumuisha miongozo hiyo?

  1. Mila 
  2. Desturi
  3. Utamaduni
  4. Maadili

MAJIBU

i

ii

iii

iv

v

vi

vii

viii

ix

x











2. Oanisha sentensi kutoka kundi A na zile za kundi B, kisha andika herufi ya jibu sahihi katika kisanduku ulichopewa hapo chini.

KUNDI A

KUNDI B

(i) Njia ya kuhifadhi historia ya jamii

(ii) Mfano wa maadili ya kitanzania

(iii) Michezo ya jadi

(iv) Namna ya kuhifadhi urithi wa taifa

(v) Umuhimu wa kulinda na kutunza historia ya taifa

  1. Kuchora alama za urithi
  2. Kusaidiana na kuheshimu wengine
  3. Bao na rede
  4. Kuandika kumbukumbu
  5.    Kuweka kumbukumbu kwa vizazi
  6.    Kusoma na kuandika
  7. Kujifunza mara kwa mara

KUNDI A

i

ii

iii

iv

v

KUNDI B






SEHEMU B (Alama 70)

Jibu maswali yote katika sehemu hii

3. Taja shughuli tano (5) za kijamii na kiuchumi zinazofanywa na jamii ya wakichembe katika maisha yao ya kila siku.

  1. __________________________________________________________________
  2. __________________________________________________________________
  3. __________________________________________________________________
  4. __________________________________________________________________
  5. __________________________________________________________________

4. (a) Eleza maana ya urithi wa Taifa

________________________________________________________________________________________________________________________________________________

(b) Taja njia nne (4) zinazotumika kuhifadhi urithi wa taifa:-

i) ______________________________________________________________________

ii) ______________________________________________________________________

iii) _____________________________________________________________________

iv) _____________________________________________________________________

5. (a) Taja michezo miwili ya jadi inayotumika kuendeleza maadili

  1. _________________________________________________________________
  2. _________________________________________________________________

(b) Eleza namna michezo hiyo inavyosaidia watoto kujifunza maadili.

i) ______________________________________________________________________

ii) ______________________________________________________________________

iii)______________________________________________________________________

6. Bainisha mifano mitano ya maadili mbalimbali katika jamii za Kitanzania ambayo ingefaa kuigwa na kudumishwa kwa vizazi vijavyo.

  1. __________________________________________________________________
  2. __________________________________________________________________
  3. __________________________________________________________________
  4. __________________________________________________________________
  5. __________________________________________________________________

7. (a) Bainisha makabila mawili (2) ambayo yanatokana na jamii za wakichembe.

  1. __________________________________________________________________
  2. __________________________________________________________________

(b) Taja zana tatu (3) zilizotumika katika uwindaji katika jamii ya Wakichembe.

i)  __________________________________________________________________

ii)  __________________________________________________________________

iii) __________________________________________________________________

8. Jamii za watu wa visiwa vya Zanzibar walinunua na kuuza bidhaa kupitia biashara walizofanya na waajemi, waarabu na watu wa mashariki ya mbali. Taja bidhaa tano (5) zilizohusika katika biashara hiyo.

  1. __________________________________________________________________
  2. __________________________________________________________________
  3. __________________________________________________________________
  4. __________________________________________________________________
  5. __________________________________________________________________

9. Kwa nini jamii za asili ya Kitanzania zilihama kutoka eneo moja kwenda eneo lingine? Toa hoja tano (5).

  1. __________________________________________________________________
  2. __________________________________________________________________
  3. __________________________________________________________________
  4. __________________________________________________________________
  5. __________________________________________________________________

SEHEMU C (Alama 15)

Jibu swali hili kwa insha

10. Eleza hoja sita (6) ukionesha matarajio yako ya kujifunza somo la Historia ya Tanzania na  Maadili.

FORM ONE HISTORIA EXAM SERIES 203  

FORM ONE HISTORIA EXAM SERIES 203  

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256