?> KISWAHILI STANDARD SIX EXAMS SERIES
KISWAHILI STANDARD SIX EXAMS SERIES

OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

KISWAHILI- MTIHANI WA MWISHO WA MWAKA-2023

DARASA LA SITA

MUDA: 1.30      

MAELEKEZO

  1. Karatasi hii ina kurasa nne zenye maandishi yenye sehemu A,B, C,D na E zenye maswali arobaini na tano (45).
  1. Jibu maswali yote katika kila sehemu ya mtihani huu.
  2. Kumbuka kuandika majina yako, na shule yako kwenye karatasi ya kujibia.
  3. Hakikisha kazi yako ni nadhifu sana.
  4. Tumia kalamu ya wino wa bluu au nyeusi kwa maswali yote uliyopewa.

SEHEMU A

Sikiliza kwa makini kifungu cha habari. Kisha jibu swali la 1 – 5

Umaskini hauwezi kuondolewa kwa maneno matupu kama vile kuukemea au kuutangaza katika vyombo vya habari. Tunaweza kuondoa umaskini kwa kufanya kazi kwa bidii na maarifa.

Ni kazi bure kwa Mkulima, kwa mfano kuendelea kufyeka mashamba mapya kila mara kwa matarajio ya mavuno mengi. Kilimo kinahitaji mkulima awe na juhudi ya kufanya kazi yake. Kilimo cha jembe la mkono hakitamwondolea mkulima umaskini, kutaendelea kumchosha, kumzeesha na kumfanya maskini maisha yake yote. Mkulima lazima abadili fikra zake kuhusu kilimo ili aitumie ardhi kwa usahihi. Hivyo hana budi alime kwa kutumia jembe la kukokotwa na wanyama kazi ambao tunao wengi, kwa kufanya hivyo ataweza kulima shamba kubwa kwa muda mfupi.

Mkulima wa sasa ashauriwe kupanda mbegu zilizochaguliwa vizuri, yaan mbegu bora. Akipanda mbegu zisizokuwa bora, asitarajie kuvuna mazao bor na mengi hata kama mvua zitakuwa nyingi. Mbegu bora hutoa mazao bora. Ni muhimu sana mkulima azingatie kanuni za kilimo bora apande kwa nafasi, apalilie kwa wakati, atumie dawa kuua wadudu waharibifu wa mazao shambani vilevile mkulima atumie mbolea hasa aina ya samadi.

MASWALI

  1. Neno “Umaskini” tunaweza kulifananisha na neno lipi kati ya maneno yafuatayo? (A)ukwasi (B)Utajiri (C)ufukara (D)upungufu (E)Uzee
  2. Mwandishi anasema umaskini hautaondolewa kwa maneno bali utaondolewa kwa kufanya nini? (A)kwa kufuata kanuni za kilimo, kutumia jembe la kukokotwa na wanyama na kutumia mbegu bora (B)kutumia mbegu za asili zilizokakamaa (C)kwa kukopa fedha nyingi benki kwa ajili ya kilimo (D)kwa kutegemea kilimo cha mvua (E)kwa kulima kilimo mseto bil utaratibu.
  3. Wanyama gani wanaotumika katika kurahisisha kazi ya kilimo hapa Tanzania. (A)nguruwe (B)swala (C)ng’ombena punda (D)Twiga na nyati (E)simba na ngiri
  4. Nini maana ya neno “fikra” kama lilivyotumika kwenye habari uliyosoma (A)fariji (B)wazo (C)uelewa (D)ubongo (E)akili
  5. Kutokana na habari uliyoisikia samadi ni mbolea inayotokana na nini? (A)mimea (B)gesi vunde(C)viwanda (D)kinyesi cha wanyama (E)Mabaki ya vyakula.

Chagua jibu sahihi

  1. Neno lipi kati ya maneno yafuatayo ni jumuishi kwa maneno haya “nyanya, vitunguu, pilipili na tangawizi. (A)nafaka (B)matunda (C)vinywaji (D)vitoweo (E)viungo
  2. Sote tunacheza mpira uwanjani neno uwanjani limetumika kama aina gani ya maneno. (A)kivumishi (B)kielezi (C)kitenzi (D)Kiwakilishi (E)nomino
  3. Nomino inayotokana na kitenzi “Cheza” ni ______ (A)chezeka (B)mpira (C)anacheza (D)mchezo (E)chezea
  4. Maneno yenye maana sawa katika lugha ya kiswahili hujulikana kama _____ (A)visawe (B)vitawe (C)vitenzi (D)vidahizo (E)vitate
  5. Kitenzi kinachotokana na nomino uvuvi ni _(A)vuna (B)vua (C)samaki (D)nyavu (E)vuta
  6. Katika neno “sikujua” kiambishi kipi kinaonesha ukanushi (A)siku (B)jua (C)a (D)-ku- (E)si-
  7. Neno “kindumbwendumbwe” lina silabi ngapi? (A) 7(B)4 (C)5 (D) 9 (E)6
  8. Nini kinyume cha neno duni (A)thamani (B)kidogo (C)dhaifu (D)kikubwa (E)Imara
  9. Wote tulimpokea mgeni rasmi. Sentensi hi ipo katika kauli ya (A)kutenda (B)kutendwa (C)kutendea (D)kutendeana (E)kutendwa
  10. Mtaalamu wa Elimu ya Nyota huitwa _________ (A)mtabiri (B)dazeni (C)mnajimu (D)mkalimani (E)mwanang’aa
  11. Mwana wetu ameenda shuleni _________ afya yake si nzuri (A)Ikiwa (B)pamoja na hayo (C)ili (D)kama (E)ingawa
  12. “Wimbo huu hauimbiki” sentensi hii iko katika kauli __________ (A)kutendana (B)kutendeka (C)kutendwa (D)kutendeana (E)kutenda
  13. Alikaa kimya __________ alisikia tukimwita (A)kwa kuwa (B)japokuwa (C)kwa vile (D)pia (E)vile vile
  14. Alimsihi asimwadhibu. Sentensi hii ipo katika kauli ipi? (A)halisi (B)kutendewa (C)taarifa (D)pevu (E)kutendeana
  15. “Huyu unaemuona hapa ni mama yangu na yule pale ni baba yangu” “huyu” na “yule” ni aina gani ya maneno? (A)vivumishi (B)vielezi (C)vitenzi (D)viwakilishi (E)nomino
  16. Nini kinyume cha neno “huzuni”? (A)masifu (B)farakana (C)sifia (D)chukia (E)Furaha
  17. Kivumishi ni neno linalotoa taarifa zaidi kuhusu nomino au kiwakilishi, katika sentensi hii “wanafunzi wale wanapenda kucheza mpira” neno lipi limetumika kama kivumishi (A)wanafunzi (B)mpira (C)wanapenda (D)wale (E)kucheza
  18. “Nyumba imeezuliwa kwa upepo mkali” sentensi hii ipo katika kauli gani_____ (A)kutendwa (B)taarifa (C)halisi (D)kutendewa (E)kutenda
  19. Ili tuvune mazao bora na mengi ______ tulime kwa juhudi na maarifa (A)ni budi (B)hatuna budi (C)budi (D)hawana budi (E)hamna budi
  20. Baba atamkanya mjomba ili aache ulevi. Sentensi hii ipo katika wakati gani? (A)timilifu (B)ujao (C)uliopo (D)mazoea (E)uliopita
  21. Neno lipi kati ya haya yafuatayo lina maana sawa na neno shehena? (A)Robota (B)bidhaa (C)mzigo (D)roda (E)furushi
  22. Baada ya Ali kuasi Ukapera wazazi wake walimpongeza. Kuasi ukapera maana yake ni _ (A)kuacha kazi ya kutumikisha (B)kuacha kucheza mpira (C)kuacha wizi (D)kupata kazi (E)Kuoa
  23. Mpenda chongo huona _____ (A)marumaru (B)kengeza (C)karibu (D)vizuri (E)mbali
  24. Walimu walipigwa na butwaa baada ya kuona matokeo ya darasa la saba. Nahau “kupigwa butwaa” maana yake ni (A)kushangaa (B)kustuka (C)kukimbia (D)kulia (E)kufurahi
  25. Methali isemayo “mdharau mwiba mguu huota tende” ina maana sawa na methali ipi ___ (A)maji ukiyavulia nguo sharti uyaoge (B)usipoziba ufa utajenga ukuta (C)mwenda pole hajikwai (D)fuata nyuki ule asali (E)penye miti hapana wajenzi
  26. Nini maana ya nahau “ana mkono wa birika” (A)mwizi (B)mfupi (C)mkarimu (D)umepinda (E)mchoyo
  27. Maana ya nahau “piga jeki” ni ipi? (A)kumweka mtu (B)kumuumiza mtu (C)kumwonea mtu (D)kumwadhibu mtu (E)kumsaidia mtu
  28. Tulitia nanga salama kwani ______ wetu alikuwa mzoefu (A)Rubani (B)utingo (C)mwendeshaji (D)nahodha (E)dereva
  29. Neno “Mwangwi” ni jibu la kitendawili kipi kati ya vifuatavyo (A)huku ng’o na huko ng’o (B)jinamizi laniita lakini silioni (C)huku pili na huko pili (D)kila niendapo ananifuata (E)sirudi tena kwa mjomba
  30. Ipi maana sahihi ya neno “aghalabu” (A)Mara nyingi (B)mara moja (C)mara chache (D)mara dufu (E)mara nyingine

SEHEMU B: Utungaji

Panga sentensi zifuatazo ili ziletee habari yenye mtiririko mzuri kwa kuzipa herufi A B C D E

  1. Vile vile matunda huongeza damu mwilini
  2. Kula matunda kuna saidia kuponyesha magonjwa na vidonda haraka
  3. Hivyo matunda yana umuhimu mkubwa katika miili yetu
  4. Pia husaidia macho kuona vizuri katika mwanga hafifu
  5. Lakini watu wasiokula matunda hupata maradhi kama vile ugonjwa wa fizi macho na ngozi.

 

SEHEMU C: Ufahamu

Baraka alizaliwa huko mkoani Mbeya mwaka 1978. Alizaliwa katika mwaka ambao nchi ya Tanzania iliingia vitnai na nchi ya Uganda. Baba yake Baraka alitamani kumwita mwanaye jina “Vita” kwa sababu alizaliwa mwaka wa vita. Mama yake Baraka hakuafiki kumwita mtoto wa jina la “Vita” kwani aliamini jina la mtu ndiyo mtu mwenyewe. Hivyo kumwita mtoto vita ingeweza kumfanya mtoto huyo kuwa ni mwenye kupenda vita au vurugu za aina nyingine. Kwa hiyo baada ya malumbano na mjadala wa muda mrefu, wakafikia muafaka wa kumwita mtoto wao Baraka. Jina lenye maana na tafsiri vizuri na isiyokuwa na mashaka

 

MASWALI

  1. Baraka alizaliwa lini
  2. Nani alitamani jina “Vita”
  3. Kwa nini mama yake Baraka alikataa kumwita mtoto wake vita
  4. Neno “malumbano”katika habari hii lina maana gani
  5. Baba alitaka mtoto wake aitwe “Vita” kwa sababu gani?

LEARNINGHUBTZ.CO.TZKISWAHILI STANDARD SIX EXAM SERIES 84

OFISI YA RAIS, TAWALA ZAMIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MTIHANI WA NUSU MUHULA WA PILI

DARASA LA SITA

KISWAHILI

 

JINA : __________________________TAREHE________________________DRS -6

SEHEMU A: UFAHAMU WA KUSIKILIZA

Sikiliza kwa makini habari inayosomwa na msimamizi kisha ujibu maswali kwa usahihi.

  1. Taja aina mbili ya simu zilizotajwa kwenye habari hii
    1. Simutamba na telegram C. Kiswaswadu na simutamba E. Simuya mkononi na simuhuru
    2. Simuhuru na simutamba D. Simutamba na Rununu                                                                        [        ]
  2. Kitendo cha watu kupashana habari huitwaje?
    1. Kusikilizana   B. Maongezi  C. Mawasiliano D. Simulizi E. Kupashana habari  [        ]
  3. Simu ya mkononi kwa jina lake huitwaje?
    1. Rununu    B. Redio C. Runinga D. Kiswanswadu E. Simutamba                [        ]
  4. Taja faida mbili za simu ya mkononi.
    1. Mawasiliano na kupata elimu D. Kupata elimu na michezo mbalimbali ya kisasa
    2. Mawasiliano na kupata picha za utupu E. Kupashana habari za ugaidi na uhuni                        [       ]
    3. Mawasiliano na kupata habari za matukio mbalimbali ya wizi, biashara na siasa
  5. Ni simu ya aina gani hutumia gharama kubwa sana kufikisha ujumbe wake?
    1. Simutamba B. Runinga C. Simu ya mkononi D. Telegram   E. Simu ya mfukoni   [        ]
  6. Neno lipi kati ya haya yafuatayo ni kinyume na neno „Adili‟
    1. Wema B. Uovu C. Ujasiri D. Ujanja E. Ujinga          [         ]
  7. Maneno matamu yaliwafanya watu washawishike haraka. Neno „Matamu‟ limetumika kama aina ipi ya maneno?
    1. Nomino B. Kivumishi C. Kielezi D. Kiwakilishi E. Kihisishi   [        ]
  8. Kiti kimepotea. Sentensi hii ipo kwenye ngeli ya _           
    1. LI - YA B. A - WA C. KI - VI D. U - I E. U  ZI    [       ]
  9. Walifika salama. Hii sentensi ni nafsi ya           
    1. kwanza wingi B. pili umoja C. tatu wingi      D. kwanza umoja     E. pili wingi     [       ]
  10. Mtu anayesimamia kazi shambani anaitwaje?
    1. Kiongozi     B. Msimamizi        C. Mkuu D. Nokoa E. Mnyampala                         [       ]
  11. Mzee Mwendapole aliwapa mawaidha juu ya maisha ya baadaye. Neno lililopigiwa mstari lina maana gani?
    1. Hotuba B. Maonyo             C. Urithi        D. Mawazo E. Mahubiri                            [        ]
  12. Ipi maana sahihi ya neno „ANGALABU‟
    1. mara chache B. mara nyingi   C. maradufu   D. mara moja E. mara mbili                           [       ]
  13. Lipi kati ya maneno yafuatayo haliandamani na mengine.
    1. weusi B. hudhurungi C. tipwatipwa  D. kijani     E. samawati                   [       ]
  14. Neno shule limetobolewa kutoka katika lugha ipi?
    1. Kibantu    B. Kiswahili     C. Kireno   D. Kiunguja    E. Kijerumani                                                          [        ]
  15. Magari mawili yaligongana jana usiku. Sentensi hii ni kauli             
    1. Kutenda   B. Kutendewa        C. Kutendeka D. Kutendana E. Kutendwa                             [        ]
  16. Kaka alikata         alipoona hajaridhishwa na uamuzi wa hukumu aliyotoa Hakimu.
    1. Rufaa B. Dhamana C. Mahabusu D. Kizimba E. Fidia  [        ]
  17. Hali ya kuwa maskini zaidi huitwa           
    1. mashaka B. uchumi C. ufukara D. ukosefu E. ukwasi [       ]
  18. Yule bibi ameishi miaka mia moja. Miaka mia moja ni            
    1. Karne B. Muongo C. Milenia D. Daima E. Milele   [       ]
  19. Mtakuja sasa hivi kwa kuwa baadaye sitakuwa na           wa kuja.
    1. saa B. wasaa C. milenia D. daima E. milele     [       ]
  20. Masalale! Nyumba yetu imeanguka. Neno lililopigiwa mstari limetumika kama:
    1. kielezi B. nomino C. kihisishi D. kivumishi E. kitenzi    [      ]
  21. Mtoto aliyevunjika mguu amepelekwa hospitali. Hii ni aina ipi ya sentensi?
    1. changamano B. ambatano C. shurutia D. sahili E. tegemezi  [      ]
  22. Katika neno „Wataimba‟ kiambishi kinachoonesha wakati ni?
    1. -ta B. -wa C. -ba D. -imba E. –mba     [       ]
  23. Mgeni akifika nitakuwa nimeandaa risala. Sentensi hii ipo katika wakati ujao hali              
    1. ya kuendelea B. timilifu C. isiyodhihirika D. nyepesi E. iliyopo  [       ]
  24. Neno „Waraka‟ lina maana sawa na neno lipi kati ya yafuatayo:
    1. Barua   B. risala     C. hotuba  D. katiba   E. muhtasari                                                                                    [       ]

           


  1. „Jinamizi laniita lakini silioni‟. Maana ya kitendawili hiki ni ipi?
    1. Jini B. mwangwi C. mchafu D. umeme   E. shetani      [        ]
  2. „Watoto hawa ni hirimu yako‟, Mzee alimwambia Ramadhani. Neno hirimu lina maana gani?
    1. Makamo B. manaibu C. makamu D. nasaba   E. wasaidizi     [        ]
  3. Maana ya nahau „Kufa Moyo‟ ni ipi?
    1. Kuchoka   B. kuugua C. kufariki   D. kuchoka sana   E. kukata tamaa                                                      [       ]                                                           
  4. Ipi kati ya methali zifuatazo ina maana sawa na ile isemayo “Udongo upate ungali maji”
    1. Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo D. Tamaa mbele mauti nyuma
    2. Samaki mkunje angali mbichi E. Hakuna marefu yasiyo na ncha                       [       ]
    3. Dau la mnyonge haliendi joshi
  5. Tegua kitendawili hiki. „Nina kitanda changu cha Mkangashele mwana wa halali aende akalale”
    1. Mvua B. Maji        C. Bahari D. Nyumba E. Jua                              [      ]
  6. Ng‟ombe ambaye hajazaa huitwa           
    1. mbogoma B. lagoli        C. mtamba D. beberu                         E. ndama                       [       ]
  7. Neno lenye maana sawa na „motisha‟ ni            
    1. Bidii B. marupurupu   C. nyongeza D. kichocheo E. dukuduku                     [        ]
  8. Umoja wa neno „vikuku‟ ni upi?
    1. Kuku B. kikuku        C. kakuku D. mkuu                    E. kakukuu                          [        ]
  9. Kitendawili: “Askari tele Mzungu katikati”
    1. Macho na pua                                                         C. Pua na masikio
    2. Meno na ulimi D. Kichwa na kidevu   E. Kidevu na masikio        [       ]
  10. “Siku za mwizi ni arobaini” ina maana ipi?
    1. Mfanya mabaya huishia siku arobaini
    2. Hakuna marefu yasiyo na ncha D. Mwizi hukamatwa baada ya siku arobaini   [        ]
    3. Mchoyo maisha yake ni mafupi E. Mwizi ana marafiki arobaini tu
  11. Kutokana na maradhi yaliyokuwa yanamsumbua Mwanahawa hakuweza hata kumeza              la uji.

A.Fundo                B. Lepe C. Funda D. Tonge E. Pozi                  [         ]

                                   SEHEMU B: UTUNGAJI

TUMIA MANENO HAYA KUJAZA NAFASI ZILIZO ACHWA WAZI (andika herufi ya jibu sahihi)

A.  NAKUSANYA B.   JINA C. MTIHANI        D. MAELEKEZO       E. MAREKEBISHO

Kila ifikapo wakati wa mtihani ninajiandaa kikamilifu. Mtihani uletwapo kwenye chumba
cha mtihani mimi husali. Nikiruhusiwa kuanza kufanya mtihani hatua zangu ni kama ifuatavyo:
Hatua ya kwanza  36.  __________. Hatua ya pili husoma  37. _____________________ya
mtihani. Baada ya hapo huaanza kufanya 38. _________________________. Nifikapo swali
la mwisho hukagua karatasi ya maswali na kufanya  39. ____________________. Baada ya
hatua zote huwa nimeridhika , hivyo 40.  _____________________mtihani nikiwa na

uhakika wa kufaulu.

 Soma kwa makini shairi lifuatalo na kisha jibu maswali 41-45 majibu mafupi

Kasimama kizimbani, popo anatetemeka,
Kaitwa mahakamani, popo kujibu shitaka,
Atakiwa abaini, kwa ulimi kutamka,
Ajitetee bayana, ni mnyama au ndege.

Hakimu nashukuru, shitaka kunisomea,

Sinajadinakunguru, ikiwapundamilia,

Mimi ni mnyama huru, amini ninakuambia,
Tukidaiwa ushuru, kwa wanyama nalipia.

Ni kweli popo napaa, na mabawa ninayo,
Lakini mimi nazaa, hili halina utata,
Kuwa ndege nakataa, sina undugu na bata,
Nakataa katakata, mimi si ndege nasema.

                   Maswali

41. Popo anakataa kuwa Si ndege kwa sababu gani?__________________________________________________

42. Katika ubeti wa pili popo anasema “sina jadi na kunguru”. Usemi. “sina jadi” una maana gani?____________

___________________________________________________________________________________________

43. Kichwa cha shairi hili chafaa kiwe?__________________________________________________________

44. Mstari wa mwisho katika kila ubeti wa shairi hili huitwaje?_______________________________________

45. Popo alitakiwa kujitetea bayana. Usemi “kujitetea bayana’’ una maana gani?___________________________

_____________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________


SEHEMU A: UFAHAMU WA KUSIKILIZA

Sikiliza kwa makini habari inayosomwa na msimamizi kisha ujibu maswali kwa usahihi.

 

Simu ni chombo kinachotumika kupelekea na kupokelea mawimbi ya sauti baina ya mtu na mtu papo kwa hapo. Zipo aina mbalimbali za simu kama vile simutamba na telegram n.k ambazo mtu huweza kupata mawasiliano anayotaka. Simutamba ni simu ambayo watu wengi huwa nazo kwa mawasiliano na ni tofauti na telegram ambayo huandikwa kwa kutumia gharama kubwa.

Hivyo basi simu ni chombo muhimu sana cha mawasiliano ambacho hutupa utandawazi wa mambo mengi yanayoendelea dunia nzima hasa katika masuala ya biashara, uchumi na siasa. Vile vile simu ikitumiwa vizuri inaweza kuleta faida kubwa kwa mtumiaji yaani kupata elimu na maarifa mapya,

pia simu ikitumiwa vibaya inaweza kumletea mtumiaji madhara makubwa katika jamii kwa kuiga tabia fulani ya mtu au kujifunza mambo yasiyoendana na jamii yake.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

LEARNINGHUBTZ.CO.TZKISWAHILI STANDARD SIX EXAM SERIES 76

OFISI YA RAIS

TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MITIHANI YA KUJIPIMA KWA SHULE ZA MSINGI

MTIHANI MWA MWISHO WA MUHULA-MEI-2023

DARASA LA SITA

KISWAHILI

MUDA: SAA 1:30

MAELEKEZO

  1. Mtihani huu una maswali arobaini na tano (45) tu
  2. Jibu maswali yote
  3. Soma maelekezo kwa kila kurasa uliyopewa
  4. Tumia penseli ya HB tu
  5. Simu hazihitajiki katika chumba cha mtihani

SEHEMU A: UFAHAMU WA KUSIKILIZA

Sikiliza kwa makini habari utakayosomewa na msimamizi kisha jibu swali 1 – 5 kwa kuweka kivuli katika herufi ya jibu sahihi katika fomu yako ya kujibia.

  1. Kutokana na habari uliyosikiliza, ni nani aliyezungumziwa?

(a) Amani   (b) Bibi   (c)Wananchi   (d) Bibi na Amani    (e) Kilole

  1. Amani alimuuliza swali gani bibi yake? (a)Kama unajua kusoma na kuandika (b)Kama unajua kuandika (c)Kama unajua kusoma  (d)Kama unajua kuimba na kuandika  (e) kama unajua kuimba
  2. Amani anaishi katika kijiji cha Kilole. Je, Amani anaishi na nani?

(a)Bibi  (b)Babu (c)Shangazi (d)Mjomba (e)Babu na Bibi

  1. Kwa mujibu wa habari uliyosikiliza. Amani ana tabia gani?

(a)Mvivu (b)Mdadasi (c)Mkarimu (d)Mchapakazi na mdadisi (e)Mpole

  1. Kichwa cha habari hii kinafaa kiwe kipi miongoni mwa hivi?

(a)Kijiji cha Kilole (b) Amani  (c)Amani na bibi yake  (d)Kilole (e)Bibi 

Katika swali la 6 – 35 weka kivuli katika herufi ya jibu sahihi

  1. Neno machweo lina maana ipi kati ya hizi zifuatazo?

(a)Wakati jua linapozama   (b)wakati jua linapochomoza    (c)wakati jua linapokuwa la utosi   (d)wakati jua linapokuwa kati    (e)wakati jua linapokuwa pembeni.

  1. “Kazi mbaya si mchezo mwema” methali inayofanana na methali hii ni ipi kati ya hizi zifuatazo? (a)hewala haigombi   (b)mchezea tope humrukia   (c) mcheka kivu asiyefikwa na jeraha (d)lila na fila havitengamani  (e)mcheza kwao hutunzwa
  2. Wanafunzi wale wanapenda kucheza mpira. Katika sentensi hii neno lipi limetumika kama kivumishi? (a)wanafunzi   (b)wale  (c)wanapenda  (d)mpira  (e) kucheza
  3. Katika lugha ya kiswahili neno “staftahi” lina silabi ngapi?

(a)sita   (b)tano  (c)nne  (d)tatu  (e)saba

  1.                      “Ukitaka kuruka agana na nyonga”. Sentensi hii iko katika aina gani ya sentensi kati ya hizi? (a)sahihi  (b)ambatano  (c)changamano  (d)tegemezi  (e)shurutia
  2.                      Ipi ni maana ya kitendawili “nyumba yangu imeungua mwamba wake umebaki”

(a)mfupa  (b)njia  (c)kaburi (d)kisima (e)mlima 

  1.                      Kuwa na Nyota ya jaha maana yake ni ______ (a)jua la mchana  (b)Nyota ya asubuhi

(c) Bahati nzuri  (d)Bahati mbaya  (e)Bahati nasibu

  1.                      Wewe ni mtoto mdogo sana. Sentensi hii iko katika nafsi gani? (a)ya kwanza umoja

(b)ya pili umoja  (c)ya tatu wingi  (d)ya pili wingi  (e)ya kwanza umoja na wingi.

  1.                      Watu hufanya kazi mbalimbali ili kuweza kujipatia kipato. Mtu anayefanya kazi ya kutunza na kuazima vitabu anaitwa Mkutubi. Je! Mtu anayefanya kazi ya kuzibua vyoo anaitwa nani? (a) kuli              (b)topasi              (c) toinyo              (d)chepe              (e)zubaifu
  2.                      Bwana Afya aliuliza, kuna umuhimu gani wa kuchemsha maji ya kunywa? Je sentensi hii iko katika kauli ipi kati ya zifuatazo? (a)taarifa  (b)halisi  (c)tata (d)tungo huru (e)kutenda
  3.                      Asha ana gari. Neno “ana” ni aina gani ya neno?

(a)kitenzi (b)nomino (c)kiunganishi  (d)kielezi  (e)kihusishi

  1.                      Baba amelima shamba kubwa sana. Silabi inayoonesha nafsi ni ipi?

(a) –li-  (b) –a-  (c) –me- (d) – i-  (e) – lim-

  1.                      Ngumi zilipigika vilivyo, Neno lililopigiwa mstari lipo katika kauli gani?

(a)Kutenda  (b)Kutendewa  (c)Kutendwa (d)Kutendeka              (e)Kutendesha 

  1.                      Kamilisha methali ifuatayo. Akikalia Kigoda ____ (a)huanguka   (b) usimtukane

(c) mtii   (d) mfukuze   (e)harudi

  1.                      Ali anakula wali ____ maharage. (a)na  (b)kwa  (c)ni   (d)ya  (e)pamoja
  2.                      Simba mkali amepita shuleni kwetu. Mchanganuo wa sentensi hii ni upi kati ya michanganuo ifuatayo? (a)T+N+V+W+E   (b)N+E+V+T+W  (c)V+E+T+W+N (d)N+V+T+E+V   (e)N+V+E+T+V
  3.                      Kinyume cha methali isemayo; “Ngoja ngoja yaumiza matumbo” ni ______ (a)bendera hufuata upepo. (b)mtu hujikuna hajipatiapo (c) mwisho hadhuru maiti (d)haraka haraka haina Baraka               (e) asiyesikia la mkuu huvunjika guu
  4.                      Wakoloni walitunyanyasa lakini hatimaye unyanyasaji huo ulifika ukingoni kwani ___Ni methali ipi kati ya zifuatazo inamalizia sentensi hii? (a)hakuna marefu yasiokuwa na ncha (b)mchumia juani hulia kivulini (c)ukiona vyaelea ujue vimeundwa (d)umoja ni nguvu utengano ni udhaifu               (e)bandubandu humaliza gogo.
  5.                      Kazi ya Daudi ni kazi ya kijungujiko. Je! Kazi ya kijungujiko ni kazi ya aina gani? (a)Kazi ya kuchimba vyoo              (b)kazi ya kujitolea              (c)Kazi ya kufundisha wanafunzi   (d)kazi isiyo rasmi au inayotosha mahitaji yam lo tu.              (e) kazi ya kikoa
  6.                      Ikiwa mzizi wa neno “PIK” tukiunda neno litakalokuwa katika wakati uliopita nafsi ya kwanza umoja hali ya kutenda tunapata neno.              (a)alipika               (b)nilipika (c)walipika               (d)tulipika               (e)nimepika
  7.                      Akikosekana maana inakosekana. Jibu la kitendawili hiki ni lipi? (a)kitabu

(b)Kamusi (c)magazeti (d)shairi (e)Vipeperushi

  1.                      Mashairi ya kimapokeo yamegawanyika katika aina mbalimbali. Je ubeti wa shairi wenye mistari minne huitwaje?(a)mshororo               (b)tarbia               (c)Kituo (d)Kibwagizo (e)mizani
  2.                      Mnyama ambaye amekuwa laini bado hajazaa anaitwa _____

(a)mtamba (b)Mbuguma (c)Maksai (d)fahali (e)beberu

  1.                      Nenda ukawasikilize watakachokueleza uniletee mrejesho. Katika sentensi hii mtenda ni nafsi ya ngapi?               (a)ya kwanza umoja               (b) ya pili umoja               (c)ya tatu wingi

(d) ya kwanza wingi   (e)askari mwenye cheo cha juu

  1.                      Ali ni askari kazu. Ali ni _____ (a) trafiki  (b)kanga   (c)bunduki   (d)mpelelezi

 (e) askari mwenye cheo cha juu

  1.                      Jambazi alihukumiwa kwa kuua mfanyabiashara. Sentensi hii iko katika hali gani?

(a)hali timilifu  (b)hali ya kuendelea  (c) hali isiyodhihirika (d)hali ya mazoea (e)hali tata

  1.                      Tungo changamano ni tungo yenye vishazi vingapi? (a)viatu (b)viwili

(c)vinne (d)vitano (e) kimoja 

  1.                      Kisawe cha jogoo ni jimbi, kisawe cha beseni ni karai. Je kisawe cha kinyonga ni ____

(a)bomba (b)hua  (c)lumbwi (d)kelbu (e)baghala

  1.                      Katika neno anacheza. Kipi ni kiambishi njeo? (a)-a- (b)-na-               (c)-chez-

(d)-a-  (e)-cheza-

  1.                      Lipi kati ya maneno yafuatayo si kivumishi likiambatanishwa na nomino?              (a)Yule

(b)nzuri (c)polepole (d)huyo (e)hawa

SEHEMU B:

Panga sentensi zifuatazo kwa kuzipa herufi A – E ili zilete maana kamili kwa mujibu swali la 36 – 40 kwa kuweka kivuli katika herufi ya jibu lililo sahihi

  1.                      Niliogopa lakini nilipiga moyo konde
  2.                      Nilirudi nyuma kidogo nikaokota fimbo na kumpiga
  3.                      Jumamosi iliyopita mama alinituma sokoni
  4.                      Nilipokuwa njiani nilimwona nyoka
  5.                      Aliniambia ninunue nyanya, vitunguu, sukari na mafuta

SEHEMU C:

Soma habari ifuatayo kisha jibu maswali yafuatayo

Masebo ni mwalimu anayefundisha katika shule ya Msingi Maendeleo iliyoko wilaya ya Masasi. Anakaa katika kitongoji cha usafi kilichopo umbali wa kilometa tano kutoka shuleni. Siku moja mwalimu Masebo alikuwa anakwenda shuleni. Pembezoni mwa msitu wa kijiji aliwaona vijana watatu, vijana hao walikuwa wakikata miti kwa kutumia mapanga na mashoka na kuivundika pembeni. Aliwatambua vijana hao kuwa ni Juma, sadiki na Joseph. Mwalimu Masebo alisikitika sana. Alisimamisha pikipiki yake haraka na kwenda katika eneo lile. Alianza kuwafokea vijana wale kwa kukata miti mingi kiasi kile. Vijana wale walishangaa sana.

Maswali:

  1.                      Juma, Sadiki na Joseph walikuwa wanafanya nini msituni?
  2.                      Mwalimu Masebo aliona nini pembezoni mwa msitu wa kijiji?
  3.                      Je! Ukikuta watu wanaoharibu mazingira utafanya nini?
  4.                      Kwa nini mwalimu Masebo alisikitika sana?
  5.                      Kwa nini tunashauriwa kutokata miti ovyo?

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

UFAHAMU WA KUSIKILIZA 

Amani anaishi na bibi yake katika kijiji cha Kilole. Anamsaidia bibi yake shughuli za nyumbani. Anamsaidia kusafisha nyumba, kupika, kuosha vyombo na kufua. Juzi Amani alimuuliza bibi yake; bibi unajua kusoma? Bibi akajibu ninajua kusoma na kuandika. Amani akasema sawa bibi, kesho nitaleta kitabu changu ili tusome pamoja.

LEARNINGHUBTZ.CO.TZKISWAHILI STANDARD SIX EXAM SERIES 70

OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOGIA

MTIHANI WA MWIGO DARASA LA SITA

KISWAHILI

MUDA:1:30                                                             

JINA_____________________________________SHULE_________________________

MAELEKEZO:

  1. Jibu maswali yote katika kila sehemu ya mtihani huu.
  2. Kumbuka kuandika majina yako.
  3. Hakikisha kazi yako ni nadhifu sana.

SEHEMU A: FASIHI NA MSAMIATI

1   Hali ya kuwa na mali nyingi au fedha huitwa  

  1.    Ubahili b. ukwasi c. ukapa d. ukata e. ukachero
  1.    Mtoto mpole hupendwa na wanafunzi wenzake darasani. Neno ‘mpole’ limetumika kama
    1.    Kiwakilishi b. nomino c. kivumishi d. kielezi e. kiungo
  2.    “Ili tuendelee          kufanya kazi kwa bidii”. Neno lipi limekosekana ili kukamilisha sentensi
    1.    Ni budi b. hatuna budi c. tuna budi d. kuna budi e. hapana budi
  3.    “Maandishi yanasomeka vizuri”. Sentensi hii ipo katika wakati gani?
    1.    Ujao b. uliopita c. mazoea d. uliopo e. timilifu
  4.    Hamza alikuwa anaimba tangu ujana wake. Neno ‘alikuwa’ ni aina gani ya kitenzi?
    1.    Kisaidizi b. jina c. kishirikishi d. kitegemezi e. sana
  5.    Mahindi, maharage, ufuta, michungwa, migomba na mihogo kwa neno moja huitwa
    1.    Mimea b. vyakula c. matunda d. mboga e. miche
  6.    Wale wanakimbia polepole. Neno ‘wale’ limetumika kama aina ipi ya maneno?
    1.    Nomino b. nafsi c. kiwakilishi d. kielezi e. kitenzi
  7.    Neno lipi kati ya maneno yafuatayo ni kinyume cha neno ‘hobelahobela’?
    1.    Faragha b. ovyo ovyo c. vizuri d. mpangilio e. ubaya
  8.    Neno moja linalojumuisha herufi a, e, i, o na u ni lipi?
    1.    Silabi b. konsonanti c. mwambatano d. irabu e. kiambishi
  9. Mzizi wa neno “amenichora” ni          
    1.    –achor- b. –nichor- c. –chorea- d. –amenich- e. –chor-
  10. Mabomba ya kupitisha moshi toka jikoni kwenda nje huitwa
    1.    Bahari b. dohari c. ghala d. hosteli e. boya
  11. Wingi wa sentensi “Yule mwali hali wali” ni      
    1.    Wale wali hali wali
    2.    Wale wali hawakuli wali
    3.     Wale wanawali hawali wali
    4.    Wale wali hawali wali
    5.    Wale wali hajala
  12. Kama angelilima shamba kubwa           
    1.    Angevuna mazao mengi
    2.    Angelivuna mazao mengi
    3.     Angalelivuna mazao mengi
    4.    Angalivuna mazao mengi
    5.    Atavuna mazao mengi
  13. Kalamu zako ni nzuri. Ukienda dukani uninunulie         . Kifungu kipi cha maneno hukamilisha sentensi hiyo?
    1.    Kama hivyo
    2.    Kama hicho
    3.     Kama hizo
    4.    Kama hiko
    5.    Mfano wa hicho
  14. Ni sentensi ipi kati ya hizi zifuatazo ipo katika kauli taarifa?
    1.    Tafadhali nichunie ng’ombe wangu
    2.    Nichunie ng’ombe wangu
    3.     Aliniomba nikamchunie ng’ombe wake
    4.    Nichunie ng’ombe tafadhali
    5.    Kwanini unanichunia ng’ombe wangu
  15. Neno ‘kuku’ liko katika ngeli ya aina gani?
    1.    KI – VI
    2.    A – WA
    3.     YU-A-WA
    4.    I-ZI
    5.    LI-YA
  16. “Ukitaka kuja unijulishe mapema”. Usemi huu ni aina gani ya sentensi?
    1.    Ambatano b. shurutia c. sahihi d. changamano e. sentensi fupi
  17. Penina huimba kila siku. Hii ni hali gani ya kitenzi?
    1.    Timilifu b. isiyodhihirika c. mazoea d. kuendelea e. kupita
  18. Kipi ni kisawe cha neno ‘tembo’?
    1.    Faru  b. ndovu c. nyati d. twiga e. mbogo
  19. Tulicheza ngoma na kuimba usiku kucha. Katika sentensi hii watenda ni nafsi ipi?
    1.    Ya tatu wingi b. ya pili wingi c. ya kwanza wingi d. ya pili Umoja  e. ya tatu Umoja SEHEMU B: LUGHA YA KIFASIHI

Andika herufi ya jibu sahihi

  1. Siku hizi siri za mafisadi zimeanikwa juani. Usemi ‘kuanikwa juani’ una maana ipi kati ya hizi zifuatazo?
    1.    Kuelezwa waziwazi
    2.    Kusemwa hadharani
    3.     Kusemwa jukwaani
    4.    Kusemwa nje ya kikao
    5.    Kuelezwa hadharani
  2. “Kidagaa kimemuozea”. Msemo huu una maana gani?
    1.    Kukwepa kulipa deni


  1.    Kutowajibika kulipa
  2.     Kuelemewa na jambo
  3.    Kupoteza Tumaini
  4.    Kulipa deni maradufu
  1. Tegua kitendawili kisemacho “bibi kafa kaniachia pete”.
    1.    Konokono b. jongoo c. tandu d. nyoka e. mende
  2. Methali isemayo “Mgaagaa na upwa hali wali mkavu” inatoa funzo gani?
    1.    Bidii huleta mafanikio
    2.    Mafanikio ni matokeo ya kazi
    3.     Bidii huleta faraja
    4.    Bidii ni kazi ya kuhangaika
    5.    Mafanikio ni ya lazima
  3. Nazi yangu yafurahisha ulimwengu pia. Jibu la kitendawili hiki ni
    1.    Moto b. mwezi c. nyota d. jua e. mbingu
  4. Kuwa na ulimi wa upanga maana yake ni
    1.    Kutoa maneno makali
    2.    Kupayuka
    3.     Kutoa maneno ovyo
    4.    Kukata maneno
    5.    Kukataa katakata
  5. Maisha ya Abunuasi yalivyo ni sawa na kukalia kuti kavu. Maana ya kukalia kuti kavu ni ipi?
    1.    Kuwa mzee sana b. kuwa na maisha ya kimwinyi c. kuwa na maisha ya kipwani

d. kuwa na maisha ya kutegemea urithi e. maisha ya kutojishughulisha

  1. Mama ameandaa meza. Maana ya Nahau kuandaa meza ni
    1.    Kusafisha na kupamba meza b. kununua meza c. kuandaa chakula mezani

d. kusafisha meza e. kupamba maua meza

  1. Wana wa mfalme ni wepesi kujificha. Maana ya kitendawili hiki ni
    1.    Masikio b. macho c. pua d. ulimi e. ini
  2. Haraka haraka haina Baraka. Kinyume cha Methali hii ni
    1.    Polepole ndio mwendo
    2.    Mpanda ovyo hula ovyo
    3.     Mtoto umeleavyo ndivyo akuavyo
    4.    Asiyekuwepo na lake halipo
    5.    Ahadi ni deni

SEHEMU C: UTUNGAJI

Zipange sentensi zifuatazo zilizochanganywa ili zilete mtiririko mzuri wa mawazo kwa kuzipa herufi A, B, C na D

  1. Dakika chache baadaye tuliona msafara wa magari ukiingia
  2. Gari hilo lilifuatwa na gari lingine lillilojaa askari wa kuzuia fujo kisha lilifuata gari la Rais


  1. Mnano saa saba hivi tuliona pikipiki ya askari wa usalama barabarani ikija mbio kama mshale
  2. Mbele ya msafara huo kulikuwa na pikipiki nne zilizofuatwa na gari la polisi lenye

king’ora

 

SEHEMU D: UFAHAMU

Soma kwa makini habari ifuatayo kisha jibu swali la 31 – 40 kwa kuandika herufi ya jibu sahihi

Umma ulipozinduka na wakawauliza wafalme walivyotajirika kinyume na matarajio ya umma, kulikuwa na vita……”watu wetu wanatuonea”. Watu hawakuwaelewa….hawakurudi nyuma, walichukua kilicho chao. Hii ndio hadithi ya kisiwa cha wafalme! Kijiji hicho kilikuwa na viwanda mbalimbali vilivyosaidia kujenga na kuinua uchumi wake.

Waliteuliwa wakurugenzi wa aina aina waliosaidiwa na watumishi wengi kukamilisha sera yao ya kazi lakini shetani mbaya – pesa! Alikuwa sehemu hii. Wakurugenzi walikula, wahasibu walikula, watumishi pia walikla. Kwa ufupi kila mtu alikula. Walipoona wanataka kushikwa kwa makosa ya kula kilicho cha umma, wakachoma moto kiwanda chao ili kupoteza ushahidi. Hasara ilibaki kwa umma. Wao wakaanzisha miradi iliyowalisha kwa kutumia pesa za umma.

Wengine nao walipoona hayo nao wakaiga. Matokeo yake vikajengwa vijiji kama vile vya wafalme. Umma pia ukashtuka, ukawauliza na kisha kuchukua haki zao kwa nguvu. Hivyo hadithi iliyotamba mwanzo ikawarudia tena watu hawa na ukweli ukabaki kuwa jamii isiyojua kiini cha matatizo yake haiwezi kuyatatua.

MASWALI

  1. Neno ‘kuzinduka’ kama lilivyotumika katika habari hii lina maana ipi?
  2. Umma ulivyoshtuka kwa mara ya pili uliamua             
  3. Shetani mbaya aliyetajwa katika habari hii ni              
  4. Shetani mbaya alikumba sehemu hii pia. Neno ‘shetani’ limetumika kama nomino ya aina

gani

  1. Katika habari hii hapa juu, Methali ipi inaweza kuwa na mafunzo sawa na habari hii hapo juu?
  2. Kisawe cha neno ‘utajiri’ ni                 

SEHEMU E: USHAIRI

Soma kwa makini shairi lifuatalo kisha jibu swali la 41 hadi 46 kwa kuandika herufi ya jibu sahihi

Nami nashika kalamu, maana menilazimu. Nawataka mfahamu, kuhusu mambo muhimu, Maana mekuwa ngumu, kuachwa na wahujumu, Rushwa ni adui wa haki, wananchi tupingeni.

 

Mepewa majina mengi, lukuki yaso idadi, Maana walafi ni wengi, kila siku wanazidi, Waheshimiwa na wengi, wamekuwa wakaidi, Rushwa ni adui wa haki, wananchi tupingeni.

 

Inaitwa takrima, au chai ya mgeni, Mnapotaka huduma, basi mikono nyosheni, Na mkijiweka nyuma, huduma isahauni, Rushwa ni adui wa haki, wananchi tupingeni.

 

MASWALI

  1. Kichwa cha shairi hili chafaa kuwa

 

  1. Shairi hili lina jumla ya beti ngapi?
  2. Neno ‘takrima’ kama lilivyotumiwa na mshairi lina maana gani?
  3. Vina vya kati vya shairi hili ni
  4. Kila ubeti wa shairi hili una jumla ya mizani

 

LEARNINGHUBTZ.CO.TZKISWAHILI STANDARD SIX EXAM SERIES 65

OFISI YA RAIS

TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MITIHANI WA MWISHO WA MWAKA

KISWAHILI

DARASA LA SITA

2022

JIBU MASWALI YOTE

SEHEMU A

Sikiliza kwa makini habari inayosomwa na msimamizi kisha jibu maswali 1 – 5 kwa kuchagua herufi ya jibu sahihi na kuandika katika karatasi ya kujibia.

Fisi na sungura walialikwa kwenye karamu moja. Basi wakajiandaa kwa safari. Kabla ya kuondoka Sungura akamwambia fisi, “Bwana huko tunakokwenda nimesikia ni kwa watu waungwana. Hivyo inabidi tubadilishane majina yetu”. Fisi akadakia, “Wasema kweli?” Sungura akamwambia Fisi, “Ndivyo. Hivyo mimi nitakuwa ‘cha wageni’ na wewe utakuwa ‘cha wote’. Fisi akakubali. Walipofika huko wakakaribishwa. Muda wa chakula ulipofika, mtoto mmoja akawa analilia chakula cha wageni. Mama yake akamwambia, “Hicho ni chakula cha wageni” Sungura aliposikia hivyo akamwambia Fisi, “Umesikia? Chakula hicho ni changu mimi cha wageni. Wewe subiri cha wote”. Basi ikabidi sungura ale chakula chote na kumwacha Fisi na njaa.

  1. Fisi na sungura walialikwa wapi?


  1. Shambani
  2. Kwenye karamu
  3. Mwituni
  4. Ugenini
  5. Cha wote


  1. Nani alililia chakula?


  1. Fisi
  2. Sungura
  3. Mtoto
  4. Wageni
  5. Mama


  1. kwa nini fisi hakula chakula?
  1. Chakula kilikuwa kibaya
  2. Alikuwa ameshiba
  3. Wenyeji walimkataza
  4. Hakupendezwa nacho
  5. Sungura alimdanganya kuwa chakula kilikuwa ni chake.
  1. Sungura ana tabia gani?


  1. Watoto
  2. Wanyama
  3. Sungura na fisi
  4. Huruma
  5. Uchoyo


  1. Nani walialikwa kwenye sherehe?


  1. Watoto
  2. Wanyama
  3. Sunguru na fisi
  4. Mama na mtoto
  5. Dhihaka


Chagua herufi ya jibu na kisha andika katika karatasi ya kujibia.

  1. “Wapiganaji wetu walipowasili visiwa vya Comoro walishangiliwa kwa …… “Ni neno lipi linakamilisha sentensi hiyo?


  1. Hofu
  2. Mzaha
  3. Shangwe
  4. Mayowe
  5. Dhihaka


  1. Mawaziri wote wa Baraza la Mapinduzi waliapishwa. Neno “Wote” limetumika kama aina gani ya neno?


  1. Nomino
  2. Kiwakilishi
  3. Kitenzi
  4. Kivumishi
  5. Kiunganishi


  1. Babu amemhamishia yule mbuguma kwenye zizi kubwa . Neno “Mbuguma” lina maana ipi?
  1. Mbuzi dume anayelima
  2. Ng’ombe dume anayelima
  3. Kondoo jike aliyezaa
  4. Ng’ombe jike anayelima
  5. Ng’ombe jike anayeendelea kuzaa
  1. “Chama kimeteka nyara sera ya serikali.” Wingi wa sentensi hiyo ni upi?
  1. Vyama vimeteka nyara masera ya serikali
  2. Vyama vimeteka nyara sera ya serikali
  3. Vyama vimeteka nyara serikali
  4. Vyama vimeteka nyara sera za serikali
  5. Vyama vimeteka nyara visera vya serikali
  1. Nyumba ya ndege huitwaje?


  1. Mzinga
  2. Kiota
  3. Korongo
  4. Banda
  5. Shimo


  1. “Wanafunzi hodari watapewa zawadi”. Sentensi hiyo ipo katika wakati gani?


  1. Ujao
  2. Timilifu
  3. Uliopita
  4. Mazoea
  5. Uliopo


  1. Maji yamejaa “Pomoni”. Neno “pomoni” ni aina ipi ya neno?


  1. Nomino
  2. Kiwakilishi
  3. Kielezi
  4. Kihisishi
  5. Kivumishi


  1. Kati ya maneno “Sherehi, Sherehe, Shamrashamra, Halfa, Tafrija” neno lipi halihusiani na mengine?


  1. Sherehi
  2. Sherehe
  3. Shamrashamra
  4. Hafla
  5. Tafrija


  1. Neno lipi kati ya maneno yafuatayo lina maana sawa na “thubutu”?


  1. Ufidhuli
  2. Ujasiri
  3. Umahiri
  4. Ukakamavu
  5. Utashi


  1. “Kuzua kizaazaa” ni msemo wenye maana gani?


  1. Ushabiki
  2. Upendeleo
  3. Malumbano
  4. Masikikitiko
  5. Majungu


  1. Mtu anayetafuta kujua jambo Fulani kwa kuuliza maswali huitwaje


  1. Mawazo
  2. Mbeya
  3. Mfitini
  4. Mdadisi
  5. Mjuaji


  1. Neno “Mchakato” lina maana ya mfululizo wa ……..


  1. Mawazo
  2. Maoni
  3. Shughuli
  4. Safari
  5. Fikra


  1. Neno lipi kati ya yafuatayo lina maana sawa na neno “shehena”?


  1. Roda
  2. Furushi
  3. Mizigo
  4. Bidhaa
  5. Robota


  1. Mtu aliezaliwa na wazazi wa rangi mbalimbali huitwaje?


  1. Albino
  2. Mkimbizi
  3. Mhamiaji
  4. Chotara
  5. Mzawa


  1. Baada ya miaka minne kalunde ……. Mafunzo yake ya udaktari. Ni neno lipi linakamilisha sentensi hiyo?


  1. Aliitimu
  2. Alihimidi
  3. Aliitimisha
  4. Alihitimu
  5. Halihitimu


  1. Methali isemayo “katika msafara wa mamba na kenge wamo” Iko sawa na methali ipi kati ya zifuatazo.
  1. Akutukanaye hakuchagulii tusi
  2. Kila kiboko na kivuko chake
  3. Amulikaye nyoka huanzia miguuni mwake
  4. Tajiri na mali yake maskini na mwanawe
  5. Hakuna masika yasiyo na mbu.
  1. Diengi anapenda kuwarairai watu. “Kurairai watu” ni msemo wenye maana ipi?
  1. Kuwasihi watu ilia pate cheo anachokipenda
  2. Kusema na watu kwa maneno mazuri
  3. Kusema na watu ili uwape chochote
  4. Kusema watu kwa ajili ya kuwatapeli
  5. Kuwabembeleza watu ili wasimpangie kazi.
  1. Msemo “kubarizi” maana yake ni kukusanyika kwa ajili ya ………..


  1. Sherehe
  2. Mkutano
  3. Mazungumzo ya kawaida
  4. Burudani
  5. Chakula cha pamoja


  1. Methali isemayo “Kila mtoto na Koja lake” ina maana gani?
  1. Kila binadamu ana mapungufu yake
  2. Kila mtoto ana mapungufu yake
  3. Kila mtoto ana wazazi wake
  4. Kupewa sifa mbaya
  5. Kupewa sifa chache
  1. Nahau isemayo “Kuvishwa kilemba cha ukoka” ina maana gani?


  1. Kupewa sifa unazostahili
  2. Kupewa sifa mbaya
  3. Kupewa sifa nyingi
  4. Kupewa sifa chache
  5. Kupewa sifa usizostahili


  1. Tegua kitendwali kifuatacho; “Nyumbani kwangu kuna jinni mnywa maji”


  1. Kikombe
  2. Kata
  3. Kinywa
  4. Kibatari
  5. Mtungi


  1. “Wakulima wa kahawa wa wilaya ya mbinga wamepewa heko kwa kuzalishana kahawa bora”


  1. Kupewa tunzo
  2. Kupewa pongezi
  3. Kupewa heri
  4. Kupewa zawadi
  5. Kupewa hawala


  1. Methali isemayo, “Mwenda pole hajikwai” inafanana na methali ipi kati ya zifuatazo?
  1. Haba na haba hujaza kibaba
  2. Fuata nyuki ule asali
  3. Awali ni awali hakuna awali mbovu
  4. Mchumia juani hulia kivulini
  5. Baada ya dhiki faraja
  1. Methali ipi kati ya hizi zifuatazo haifanani na zingine?
  1. Mtegemea nundu haachi kunona
  2. Nazi haishindani na jiwe
  3. Mlinzi wa kisima hafi kiu
  4. Mchumia juani hulia kivulini
  5. Baada ya dhiki faraja
  1. Mwamba ngoma …….. kifungu kipi cha maneno kinakamilisha methali hiyo?


  1. Hualika watu wengi
  2. Hufanya maandalizi mengi
  3. Huimba nyimbo nyingi
  4. Ngozi huvutia kwake
  5. Hucheza na jamaa zake


Soma kwa makini shairi lifuatalo kisha jibu maswali 31 – 35 kwa kuandika herufi ya jibu sahihi katika karatasi ya majibu.

Nimekwisha peleleza , karibu kila mahali,

Mule wanamotangaza, matangazo lugha mbili,

Juu kuwa kingereza, chini kuwa Kiswahili,

Juu kiwe Kiswahili, chini kiwe kingereza.

Kitangazwe kingereza, baada ya Kiswahili 

Hivi tutapotimiza, lugha itakuwa ghali,

Hivi mnayofanyiza, sana mnaidhalili,

Juu kiwe Kiswahili, chini kiwe kingereza

Serikali bembelezwa, tafakari tafadhali,

Jambo hili kueleza, kwa zingine serikalini

Kiswahili kutangaza, kuwa chini twakidhili 

Juu kiwe Kiswahili, chini kiwe kingereza

Tuache kukipumbaza, kwa andiko au kauli,

Kwa nyuma kukisogeza, kukipa kisulisuli,

Lazima kuyafukuza, yawezayo kikatili,

Juu kiwe Kiswahili, chini kiwe kingereza 

Na wenyewe kujikaza, kwa bidi za kimwili

Kiswahili kutukuza, tukivalie bangi,

Ngomani kutumbuiza, waume kwa wanawali

Juu kiwe Kiswahili, chini kiwe Kingereza

MASWALI

  1. Katika shairi hilo mstari wa pili katika ubeti wa pili una mizani mingapi?


  1. Tano
  2. Mbili
  3. Kumi na sita
  4. Nane
  5. Thelathini na tatu


  1. Katika ubeti wa nne vina ni vipi?


  1. Za na li
  2. La na li
  3. La na ya
  4. Ju na za
  5. Tu na li


  1. Kituo ni kipi katika shaiti hili?
  1. Nimekwisha peleleza, karibu kila mahali.
  2. Kitangazwe kingereza, badala ya Kiswahili
  3. Serikali bembeleza, tafakari tafadhali.
  4. Tuache kukipumbaza, kwa andiko na kauli
  5. Juu kiwe Kiswahili, chini kiwe kingereza.
  1. Shairi hili linahimiza kuhusu nini?
  1. Kudumisha na kuendeleza mila
  2. Kudumisha na kuendeleza jadi zetu
  3. Kudumisha lugha ya kingereza
  4. Kudumisha na kuendeleza Kiswahili
  5. Kudumisha na kuendeleza lugha
  1. Ujumbe unaopatikana katika shairi hili unafanana na methali ipi?
  1. Asiesikia la mkuu huvunjika guu.
  2. Umoja ni nguvu utengano ni dhaifu
  3. Mkono usioweza kuukata ubusu
  4. Ukitaka cha uvunguni sharti uiname
  5. Ukipata chungu kipya usitupe cha zamani

SEHEMU B

UTUNGAJI

Umepewa habari yenye sentensi tano (5) zilizoandikwa bili mtiririko sahihi wa mawazo katika maswali 36 – 40. Zipange sentensi hizo ili ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi A, B, C, D na E. weka kivuli katika hefuri ya jibu sahihi.

  1. Hivyo mazoezi huleta afya, kwa hiyo ni muhimu kwa kila mmoja wetu kufanya mazoezi.
  2. Lakini mtu asiyefanya mazoezi anapata maradhi ya moyo; atanenepa kupita kiasi, kwa hiyo atapata ugonjwa wa kuumwa mgongo na magoti.
  3. Mazoezi ya viungo yanachangamsha misuli ya mwili, mifupa na ubongo.
  4. Mtu anaefanya mazoezi anaepuka magonjwa ya moyo na msukumo wa damu.
  5. Watu wengi hupenda kufanya mazoezi.

SEHEMU C

UFAHAMU

Soma kwa makini habari ifuatayo kisha jibu maswali 41 – 45 kwa kuandika lililo sahihi.

Mpendwa kaka Yohana,

Natumaini hujambo na unaendelea vizuri na masomo yako. Nimefurahi kusikia kwamba umechaguliwa kujiunga na masomo ya sekondari. Ndugu wote wanakupongeza na kukutakia kila la kheri katika masomo yako. Soma kwa bidii Zaidi kwani elimu ni bahari na haina mwisho.

Baba na mama walifurahi sana baada ya taarifa za kuchaguliw kwkao kwa njia ya simu kutoka kwa shangazi. Wanamshukuru sana shangazi kwa kukuwezesha na misaada yake mingi kwako ya hali na mali. Baba ameahidi kumtembelea shangazi tarehe ishirini mwezi wa kumi na moja mwaka huu ili kumkabidhi zawadi aliyomuandalia kutokana na ukarimu wake kwak.

Rafiki yake Juma alifika hapa nyumbni akisema kwamba picha nikutumie. Hamisi amekuandalia zawadi ambayo atakukabidhi utakapokuja nyumbani wakati wa likizo yako ya mwisho wa muhula tunu amesema atakutembelea, lakini uwe mwangalifu unapoongea naye asije akakuchezea katika masomo yako.

Akupendae daima,

Mdogo wako Tumaini

MASWALI

  1. Neno “ukarimu” lina maana ipi:
  2. Mwandishi wa barua hii ametumia msemo “Kuchezea shere” Misemo huo una maana ipi?
  3. Katika barua hii mwandishi anafananisha elimu na nini?
  4. Lengo la Tumaini kumwandikia kaka yake barua lilikuwa lipi?
  5. Kifungu hiki cha habari ni aina gani ya barua.

LEARNINGHUBTZ.CO.TZKISWAHILI STANDARD SIX EXAM SERIES 59

OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOGIA

MTIHANI WA MWISHO WA MWAKA DARASA LA SABA

KISWAHILI

MUDA:1:30                                                             

JINA_____________________________________SHULE_________________________

MAELEZO

1. Jaza taarifa zako muhimu katika karatasi ya kujibia uliyopewa

2. Jibu maswali yote kulingana na maelekezo ya kila sehemu

3. Zingatia unadhifu wa kazi yako

4. Katika swali la 1-40 andika herufi ya jibu sahihi

5. Kwa swali la 41-45 andika majibu katika nafasi iliyoachwa wazi

 

Chagua jibu sahihi kuanzia swali la 1-40, kisha andika kwenye nafasi zilizo wazi

SEHEMU A: SARAFU

1.Neno lipilinakamilishasentensiisemayo “Humu __________ alimoingia yule nyoka”

(A) ndiye (B)ndio (C) ndiyo (D)ndimo

2.Ala kumbe! Ameondokaleomchana. Kihisishinikipikatiyayafuatayo? 

(A)Ameondoka (B)Leo (C) Ala kumbe (D)Ala

3.Kisawe cha neno “faraghani” nikipikatiyayafuatayo? 

(A)hadharani (B)mafichoni (C)pembezoni (D)waziwazi

4.Mtoto aliyepoteaamepatikana. Hiiniainaipiyasentensi. 

(A)sahihi (B)Tegemezi (C)changamoto (D)shurutia. 

5.Yule “msichana”anaimbavizuri. NenolililopigiwaMstarilimetumikakamaainaipiyamaneno?

(A)Nomino (B)kielezi (C)kitenzi (D)kivumishi

6.Sentensi ipikatiyazifuatazoipokatikakaulihalisi? (A)mimisiendi (B)alisemahaendi (C)ameenda (D)alisemahataenda(E)alisemaanaenda.

7.Neno lipilinakamilishasentensiisemayo, TimuyaTaifaingalichezavizuri __________

(A)ingelishinda (B)ingeshinda (C)ingashinda (D)ingalishinda (E)itashinda

8.Siku ya Mei Mosiwafanyakaziwalipitambeleya Waziri mkuuwakishikilia __________ yenyemanenoyakuhimizakazi. (A)mabango (B)libango (C)kibango (D)vibango (E)bango

9.Mwalimu aliandika maneno yafuatayo ubaoni , Ni nenolipihalinauhusianonamengine? 

(A)Ng’ombe (B)Mbuzi (C)Simba (D)Chiriku (E)Nyani

10.Mama alinunua, Samaki, dagaananyamakwanenomojahuitwaje? __________

(A)kitoweo (B)mboga (C)Mchuzi (D)Mlo (E)chakula

11.Kinyume cha neno “duni” nikipi? (A)Thamani (B)Kidogo (C)Hafifu (D)Kikubwa (E)Imara

12.Mzee jumbealiwapawanaemawaidhajuuya Maisha yao. Nenolililopigiwamstarilinamaanagani? (A)mawazo (B)urithi (C)maonyo (D)mahubiri (E)hotuba.

13.Juma anafanyakazi za kusimamiawatushambani, hivyoJumaninani ?______________

(A)Nokoa (B)Mnyapara (C)Msimamizi (D)Kiongozi (E)Kiranja

14.Pandamali nikijanamwenye hila sana. Kisawe cha neno “hila” nikipi?

(A)Hasira (B)Ulafi (C)Udanganyifu (D)Ukorofi (E)ukabila

15. “Jionibahariilikuwa __________ kwahiyowavuviwalivua Samaki bilawasiwasi. Nenolipilinakamilishasentensikwausahili. (A)kupwa (B)Shwari (C)kavu (D)baridi (E)joto

16.Mama alijifunzakuendesha gari lakinibadohajafuzu. Neno “Hajafuzu”linamaanagani

(A)Hajajuakuendesha (B)Hajamalizamafunzohayo (C)Hajapataleseni

(D)Hajahitimumafunzohayo (D)Hatamalizamafunzohaya.

17.Kijana yule anafanyakazizakekwamakini. Badalayakutumianeno “makini” ungewezakutumianenolipi. (A)Busara (B)Hekima (C)ujasiri (D)wasiwasi (E)uangalifu.

18.Neno “jenga” likinyambulishwakatikakauliyakutendekalitakuwa _________ (A)jengwa (B)jengea (C)jengeka (D)jengesha (E)jengewa.

19. “Baba yangunimwenyekitiwa Kijiji. Neno “Mwenyekiti”ninominoyaainagani?

(A)Dhahania (B)kawaida (C)pekee (D)jumla (E)mguso

20. “Mama anapikalakini baba anapangamawe” Nenolakinilimetumikakamaainaganiyaneno

(A)kivumishi (B)Kiwakilishi (C)Kielezi (D)kitenzi (Kiunganishi.

 

SEHEMU B: LUGHA YA KIFASIHI

21. “Kidolekimojahakivunjichawa” methalihiiinamaana saw ana methaliipikatikayazifuatazo. (A)Mchaguajembesimkulima (B)kilemasiugonjwa (C)umojaninguvuutenganoniudhaifu (D)kuvujakwapakachanafuukwamchukuzi (E)kuliakwakenikichekokwetu.

22.Kifungu kipi cha manenohukamilishakitendawilikifuatachokwausahihi? “Watoto wabinadamu

(A)huondokanakurudi (B)wakiondokahawarudi (C)hutanguliakuondoka (D)huchelewakuondoka (E)huondoka Pamoja nabinadamu

 

23. “Udongouwahiungalimaji” methalihiiinamaanagani? (A)udongoukikaukaunakuwamgumu

(B)kuchukuatahatharikablayahatari (C)usitatuetatizokablayahatari

(D)udongowenyemajiusiuwahi (E)kukimbiliatatizosikulitatua.

24.Tatizo la ufisadilimeotamzizikatikanchiyetu“kuotamizizi”niusemiwenyemaanagani? 

(A)kuibuka (B)kutoweka (C)kufifia (D)kuanza (E)kushamiri

25. “Mgonjwaaendapohospitalininakutopatamatibabuhadiatoechochotekwamuhudumuwaafya “Nahauipiinasaididahalihiyo”? (A)kutiamkonokazini (B)kuzungukambuyu. (C)kuuatembokwaubua (D)kujikazakisabuni (E)kutoanimoyo.

26.Kiangazi chotehulalausingizi, yakija Maisha Nakesha, maanayakitendawilihikini

(A)Nyote (B)kaa (C)samaki (D)Ndege (E)Chura

27. “Samaki mkunjeangalimbichi” methaliipikatiyazifuatazoinamaanasawa ana hii

  1. Samaki huanzakuozakichwa
  2. Ukitakaribasikioziba
  3. Jino la pembenisidawayapengo
  4. Sikio la kufahalisikiidawa
  5. Ngozi ivuteilimaji

28. “Hamadi kibindoni” katiyatafsirizifuatazoniipiinayotoamaanasahihiyamsemohuo.

  1. Akiba niileiliyonyingi
  2. Weka akibayakovizuri
  3. Kizurihakinabudikuhifadhiwa
  4. Kikulachonikileulicho nacho
  5. Akiba iliyohifadhiwahunusurika

29. “Kaachonjo” Nahauhiimaanayakeniipi. (A)Kaapembeni (B)Kuwamwangalifu

(C)kuwamwaminifu (D)kuwamcheshi (E)kuwamjanja

30. “Wakulimawakahawawa wilaya yambingawamepewahekokwakuzalishakahawa bora”

(A)kupewatuzo (B)kupewapongezi (C)kupewaheri (D)kupewazawadi (E)kupewa hawala.

 

SEHEMU C UTUNGAJI

UmepewaInshayenyesentensitano (5) zilizoandikwabilamtiririkosahihiwamawazo. Zipangesentensihizoiliziwenamtiririkowenyemantikikwakuzipa A, B, C, D na E ilikujibumaswali 31 – 35 

 

31.Tutaendelea kusaidiananakushirikianakatika mambo mbalimbalihasa katikashughuli za kiuchumi, kielimunakijamii

32.Kumekuwa namwingilianowatamaduni za kigenikatikanchizetumfanomavazi, lugha, ngoma, nyimbo, milanadesturi

33.lakini katika Kijiji chetu cha Tupendanetumeamuakudumishaupendonaushirikianomiongonimwetu.

34.Baadhi yamisingimizuriya Maisha imevurugwa .

35.Mambo mengiyaliyotokeanayanayoendeleakutokeayameathirisehemuyautamaduniwetu.

 

SEHEMU D: USHAIRI

Soma kwamakinishairilifuatalokishajibumaswaliyanayofuata.

Nawaulizawahenga, wa bara wanavisiwani

Na nduguzanguwaganga, nitoenimashakani,

Hizibetinazitunga, ilinipateamani,

Ni kipikilicho bora, Mchana au Usiku.

 

Mchanaunatufaa, kazinikujiendea,

Tusijetukafanjaa, Watoto tuweze lea,

Usikunao Wafaa, tuwezekusinzia,

Ni kipikilicho bora, Mchana au Usiku.

 

 

36.Shairi hililinabeti ngapi? (A)nane (B)nne (C)sita (D)mbili (E)tatu

37.Neno wahengakamalilivyotumikakatikaubejiwa kwanza washairihililinamaanagani? (A)watuwapwani (B)watuwa bara (C)Watoto (D)waganga (E)watuwazamani

38.Mstari uliopigiwamstarichinikatikakilaubetiwashairihilihujulikanakama

(A)mshororo (B)vina (C)ubeti (D)Mkarara (E)mizani

39.Vina vyakatinamwishokatikaubetiwa pili washairihilini ________ 

(A)a na a (B)aa nae a (C)aa naia (D) a nae a (E)nganani

40. Mshairianasemamchanaunatufaakwasababu. (A)ndiyomudawakufanyakazi

(B)ndiyomudawakupumzika (C)ndiyomudawakulea Watoto (D)ndiyomudawakusinzia (E) ndiyomudawakushindanjaa

 

SEHEMU E UFAHAMU

Soma kwamakinikifungu cha habarikifuatachokishajibumaswaliyanayofuata

 MiongonimwamashujaaambaohawawezikusahaulikakatikahistoriayanchiyetuniMtwaMkwawa. Huyualikuwakiongoziwakabila la waheheMkoani Iringa. Baba yakeMkwawaalitwaMunyigumba. Mkwawaaliongozamapambanomakalidhidhiyawajerumanikuanziamwaka 1891 hadimwaka 1898. Alifanikiwakuwauawajerumaniwengiakiwemoaliyekuwakamandawakikosi cha kijerumanialiyejulikanakwajina la Emili Zelwski. Mara baadayakuuawakwakamandaZelwiskiMnamomwaka 1891, Gavanawaujerumanialiwamuruwanajeshi wake wamtafuteMkwawakwanguvuzotehadiwamkamate. BaadayaMkwawakugunduakuwaamezidiwasananawajerumaniakaamuakujiuakwakujipigarisasiyeyenamlinzi wake kwakuhofiaasikamatwenawajerumani.

 

41.kwa mujibuwakifunghiki cha habari, nishujaaganihawezikusahaulikakirahisikatikahistoriayanchiyetu?

42.Mkwawa alipambananawajerumanikwamudawamiakamingapi? __________

43.Kiongozi wakijerumanialiyeuliwanajeshila Mkwawamwaka 1891 alikuwanani ____________

44.Baba yakeMkwawaaliitwanani ____________________________________

45. Kwa ninimkwawaaliamuakujiuamweneyewe? ___________

 

LEARNINGHUBTZ.CO.TZKISWAHILI STANDARD SIX EXAM SERIES 52

OFISI YA RAIS

TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

KISWAHILI DARASA LA SITA

MTIHANI WA NUSU MUHULA WA KWANZA

SEHEMU A: CHAGUA HERUFI YA JIBU SAHIHI KUTOKANA NA HABRI ULIOSOMEWA

  1. Mwandishi anasema mwezi huangaza kwa sababu
  1. Unaakisi mwanga wa jua
  2. Unatoka usiku
  3. Uko angani,
  4. Unatoa nuru yake
  5. Huangaza
  1. Kwenye mwezi hakuna kimbuga kwa sababu, (a) kuna mawe tu (b) hakuna upepo (c) pako kimya (d) hakuna maji  (e) hakuna miti
  2. Mtu akiwa kwenye mwezi kisha akaongea hawezi kusikika  kwa vile, (a) hakuna upepo (b) kuna joto kali (c) hakuna maji (d) hakuna hewa (d) kuna kila kitu
  3. Ardhi ya kwenye mwezi ina……………(a) vumbi na majani (b) mawe na miti (c) mawe na vumbi (d) majani na miti (e) maji tu
  4. Binadamu hawezi kuishi kwenye mwezi kwa sababu (a) hakuna miti wala hewa (b) hakuna nuru wala maji (c) kuna baridi na vumbi (d) hakuna maji na hewa (e) kuna unyevu

SARUFI: Chagua herufi ya jibu sahii

  1. Sote tunacheza mpira uwanjani. Neno uwanjani limetumika kama aina ya neno gani?
  1. Kivumishi
  2. Kielezi
  3. Kitenzi
  4. Kiwakilishi
  5. Nomino
  1. Nomino inayotokana na kitenzi “cheza “ ni…………………….(a) chezeka (b) mpira (c) anacheza (d) mchezo (e) chezea
  2. Maneno yenye maana sawa katika lugha ya Kiswahili hujulikana kama….(a) visawe (b) vitawe (c) vitenzi (d) vidahizo (e) vitate
  3. Kitenzi kinachotakana na nomino uvuvi ni………….(a) vuna (b) vua (c) Samaki (d) nyavu (e) vuta
  4. Katika Neno “Sikujua” kiambishi kipi kinaonyesha ukanushi (a)  siku (b) jua (c) a (d) -ku- (e) si-
  5. Neno “kindumbwendumbwe” lina silabi ngapi? (a) 7 (b) 4 (c) 5 (d) (e) 6
  6. Nini kinyume cha neno Dunia? (a) thamani (b) kidogo (c) dhaifa (d)kikubwa (e) imara
  7. Wote tulimpokea mgeni rasmi. Sentensi hii ipo katika kauli ya (a) kutenda (b) kutendewa (c) kutendea (b) kutendeana (e) kutendwa
  8. Mtaalamu wa elimu ya nyota huitwa……(a) mtabiri (b) dazeni (c) mnajimu (d) mkalimani (e) mwanaanga
  9. Kuwa na shingo ngumu ni…………………………(a) kuwa na shingo isiyogeuka (b) kuwa mkaidi (c) kuwa mvumilivu (d) kubeba mzigo (e) kubeba mzigo mzito
  10. Neno lipi linakamilisha methali ifuatayo? ……..mpishe (a) mwenye nguvu (b) mkimbizi (c) mwanafunzi (d) mwenye busara (e) usimpige
  11. Mtu anayetenda kinyume  na asemavyo kwa wenzake huitwa……….(a) mnafiki (b) mwongo (c) mhuni (d) mkweli (e) longolongo
  12. Maana ya Nahau “Tia nanga” ni (a) kuondoka kwa meli (b) kusimama kwa meli (c) kuogelea majini (d) kuzama (e) kuibuka
  13. Kamilisha methali ifuatayo. “Jino la pembe……………….” (a) si jino (b) husaidia jina (c) dawa ya pengo (d) husaidia kutafuna (e) sio dawa ya pengo
  14. Nyumbani kwangu kuna jinni mnywa maji…..(a) kikombe (b) kibatari (c) maji (d) mtungi (e) pipa
  15. Neno “kubarizi” maana yake ni…………………(a) kupunga hewa (b) sherehe (c) mkutano (d) chakula ( e) kubanika
  16. Baada ya Edson kuasi ukapera, wazazi wake walimpongeza. Kuasi ukapera maana yake ni……

(a) kuacha kazi ya kutumikisha (b) kuacha kucheza mpira (c) kuacha wizi (d) kupata kazi (e) kuoa

  1. Mama anauza vitumbua, baba anafanya kazi ya ulinzi. Sentensi hii ni………..(a) ghangamano (b) tegemezi (c) sahihi (d) shurutia (e) ambatana
  2. Maimu ni mtoto wa kitukuu change, hivyo maimu ni (a) mpwa wangu (b) kiningina (c) kilembekezi (d) kilembwe (e) kijukuu
  3. Mpenda chongo huona…………..(a) marumaru (b) kengeza (c) karibu (d) vizuri (e) mbali
  4. Walimu walipigwa na butwaa baada ya kuona matokeo ya darasa la saba. Nahau “kupigwa na butwaa maana yake ni? (a) kushangaa (b) kushtuka (c) kukimbia (d) kulia (e) kufurahi
  5. Methali isemayo;  “Mdharau mwiba mguu huota tende” ina maana saw ana methali ipi? (a) maji ukiyavulia nguo shart uyaoge (b) usipoziba ufa utajenga ukuta (c) Mwenda pole hajikwai (d) fuata nyuki ule asali (e) penye miti hapana wajenzi
  6. Nini maana ya nahau’” Ana mkono wa birika” (a) mwizi, (b) mfupi (c) mkarimu (d) umepinda (e) mchoyo
  7. Maana ya kitendawili “ Nyumba yangu imeungua umebaki mwamba wake “ ni (a) njia (b) kaburi (c) mfupa (d) mti (e) kisima
  8. Neno lipi kati ya haya yafuatayo lina maana saw ana neno shehena? (a) robota (b) bidhaa (c) mzigo (d) roda (e) furushi
  9. Maana nyingine ya neno mafichoni ni; (a) waziwazi (b) kivulini (c) faraghani (d) pembezoni (e) hadharani
  10. Mwanamke huyu alikaa………………….baada ya kufiwa na mme wake. Ni neno lipi linakamilisha sentensi hii? (a) eda (b) head (c) arobaini (d) fungate (e) edaha
  11. Tulitia nanga salama kwani……………..wetu alikuwa mzoefu (a) rubani (b) utingo (c) mwendeshaji (d) nahodha (e) dereva
  12. Neno “mwangwi” ni jibu la kitendawili kipi kati ya vifuatavyo? (a) huku ng’o na huko ng’o (b) jinamizi laniita lakini silioni (c) huku pili na huko pili (d) kila niendapo ananifuata (e) sirudi tena kwa mjomba.
  13. Ipi maana sahihi ya neno “aghalabu” (a) mara nyingi (b) mara moja (c) mara chache (d) mara dufu (e) mara nyingine

SEHEMU B: UTUNGAJI: Panga sentensi zifuatazo ili zilete habari yenye mtiririko mzuri kwa kuzipa herufi A, B, C, D, na E

  1. Vile vile matunda huongeza damu mwilini
  2. Kula matunda kuna saidia kuponyesha magonjwa na vidonda haraka
  3. Hivyo matunda yana umuhimu mkubwa katika miili yetu
  4. Pia husaidia macho kuona vizuri katika mwanga hafifu
  5. Lakini watu wasiokula matunda huapata maradhi kama vile uonjwa wa fizi, macho na ngozi

SEHEMU C. UFAHAMU: Soma kwa makini shairi lifuatalo kisha jibu swali la 41-45

1. Twakushukuru karima, kwa zawadi ulotupa

Ingawa umeichuma, sifa kwako tunakupa

Jemedari kama chuma, mpenda yalotukuka

Buriani Magufuli, kwa mola twakuombea

 

2. yote ulitotufanyia, Daima twakukumbuka

Kaziyo ilitukuka, samia kuendeleza

Tanzania ya viwanda, hakika yawezekana

Buriani Magufuli, kwa Mola twakuombea

Jibu Maswali yafuatayo

  1. Kichwa kinachofaa shairi hili ni……………………………….
  2. Vina vya kati katika ubeti wa kwanza mshororo wa pili ni ………………………….na………………………
  3. Shairi hili lina beti ngapi?...............................
  4. Neno Buriani lilivyotumika linamaana gani?
  5. Shairi hili lina mizani ngapi kwa kila mshororo?

 

 

KISWAHILI DARASA LA SITA

MAELEKEZO KWA MSIMAMIZI

Zingatia yafuatayo kabla ya kusoma maelekezo kwa watahiniwa.

  1. Hakikisha unasoma hadithi kwa sauti na taratibu kwa mara ya kwanza huku ukizingatia alama zote za uandishi zilizopo katika hadithi hiyo. Unaposoma kwa mara ya pili ongeza kidogo kasi ya usomaji
  2. Muda utakaotumia kuwasomea watahiniwa hadithi ni dakika tano (05) na muda utakaotumika kwa watahiniwa kujibu maswali ni dakika tano (05). Sehemu hii itafanyika kwa dakika kumi (10)
  3. Wasomee watahiniwa kwa sauti maelekezo (1 hadi 3)

 

MAELEKEZO KWA WATAHINIWA

 

 

  1. Nitasoma kwa sauti hadithi mara mbili, hivyo kila mmoja asikilizie kwa makini.
  2. Nikisoma hadithi kwa mara ya kwanza, sikiliza bila kujibu maswali na nikimaliza kusoma kwa mara ya pili, jibu swali la 1 hadi 5 kisha endelea kujibu maswali mengine (6 hadi 45)
  3. Ninaanza kusoma kifungu cha habari/hadithi sasa hivyo sikiliza kwa umakini.

 

 

KIFUNGU CHA HABARI

 Mara kadhaa nyakati za usiku tunaona mwezi ukiangaza angani. Mwezi hauna nuru yake yenyewe, bali huangaza kwa sababu unaakisi mwanga kutoka kwenye jua.

 Mwezi hauna mimea kwa vile hauna maji. Ardhi yake imejaa mawe na vumbi tu. Ijapokuwa kuna vumbi hakuna kimbunga. Hii ni kwa sababu kwenye mwezi hakuna upepo; vile vile hakuna hewa. Hewa ndiyo hufanya sauti isikike.

 

LEARNINGHUBTZ.CO.TZKISWAHILI STANDARD SIX EXAM SERIES 44

OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOGIA

MTIHANI WA MWISHO WA MWAKA DARASA LA SITA

KISWAHILI

MUDA:1:30                                                             

JINA_____________________________________SHULE_________________________

MAELEKEZO:

  1. Jibu maswali yote katika kila sehemu ya mtihani huu.
  2. Kumbuka kuandika majina yako.
  3. Hakikisha kazi yako ni nadhifu sana.

SEHEMU A: SARUFI NA FASIHI

Chagua jibu sahihi kisha andika herufi yake kwenye mabano

  1. Watoto ................chakula kitamu
  1. Wanapenda
  2. Watalia
  3. Wanaimba
  4. Walitenda
  1. Baba yake Eliza ...........................Akida
  1. Anaita
  2. Anaitwa
  3. Ameitwa
  4. Anaitika
  1. Leo mwalimu.....................elimu kwa vitendo
  1. Himiza
  2. Alihimiza
  3. Huhimiza
  4. Anahimiza
  1. Mwanaidi atakapokuwa mkubwa , ....ghorofa
  1. Anajenga
  2. Hujenga
  3. Atajenga
  4. Akijenga
  1. Jana.......................kitabu kinachoelezea utii wa watoto kwa wazazi na walimu
  1. Nimesoma
  2. Nilisoma
  3. Nitasoma
  4. Anasoma
  1. Jiwe lilitumbukia mtoni..................
  1. Chumbwi
  2. Kacha!
  3. Pruu!
  4. Chubwi!
  1. Maneno yafuatayo ni mwanzo wa hadithi isipokuwa
  1. Kitendawili
  2. Paukwa
  3. Hapo kale
  4. Siku moja
  1. Kazi ya fundi mwashi ni
  1. Kupiga deki
  2. Kujenga
  3. Kulima bustani
  4. Kumwagilia
  1. Rafiki yake Juma aliitwa Madege. Neno rafiki lina maana sawa na neno liitwalo?
  1. Jirani
  2. Ndugu
  3. Adui
  4. Mpendwa
  1. Hapa dukani wanauza sahani, masufuria, vikombe na mabirika
  1. Chakula
  2. Vyombo
  3. Chai
  4. Vyakula
  1. Dada alifua (shati, suruali sketi kanga na kitenge,) Dada alifua........................
  1. Sare
  2. Nguo
  3. Mavazi
  4. Urembo
  1. Baba alileta(maembe, machungwa, mananasi na matikiti) Baba alileta?
  1. Utamu
  2. Zawadi
  3. Mimea
  4. Matunda
  1. Sikujua alibeba( sato, sangara, perege na change) Sikujua amebeba................
  1. Ndege
  2. Nyama
  3. Chakula
  4. Samaki
  1. Wanakijiji walitengeneza (viti, meza, madawati na makabati) Wanakijiji walitengeneza..............
  1. Sanaa
  2. Zamani
  3. Samani
  4. Vitu
  1. Mama alipika( ndizi, wali, kande, biriani, na ugali). Mama alipika....................
  1. Sherehe
  2. Sikukuu
  3. Chakula
  4. Mapochopocho
  1. Scola .................kiswahili fasaha
  1. Kanazungumza
  2. Kinazungumza
  3. Anazungumza
  4. Atazungumza
  1. Mke wa Rajabu ......................kupiga simu
  1. Kanajua
  2. Anajua
  3. Watajua
  4. Hujua
  1. Kaka......................kesho kutwa
  1. Alikuja
  2. Amekuja
  3. Atakuja
  4. Aja
  1. Doni......................aliyepiga simu kwa shangazi yake
  1. Ndicho
  2. Ni
  3. Ndiye
  4. Ndio
  1. Jana mwalimu ................jinsi ya kupiga simu
  1. Alitufundisha
  2. Anajifundisha
  3. Anafundisha
  4. Amelifundisha
  1. Maharage ..................chakula kitamu
  1. Ni
  2. Kama
  3. Ndimi
  4. Ndicho
  1. Ufupi.........................ugonjwa
  1. Ndio
  2. Si
  3. Sio
  4. Ndiyo
  1. Kuwa na hofu na wasiwasi.......................
  1. Gwaya moyo
  2. Kaa ange
  3. Guu kwa guu
  4. Kutetemeka
  1. Kasirika sana
  1. Iva miguu
  2. Iva macho
  3. Lainika moyo
  4. Iva nyonga
  1. Kucheka sana
  1. Furaha sana
  2. Cheka mno
  3. Kufa mbavu
  4. Kufa kifua
  1. Kuwa na sifa ya kufanya mambo pole pole
  1. Kuwa na mkono mrefu
  2. Kuwa na mkono mzuri
  3. Kuwa na mkono mfupi
  4. Kuwa na mkono mzito
  1. Macho yasioonesha haya............
  1. Macho mabichi
  2. Macho makavu
  3. Macho bila miwani
  4. Macho yenye utandu
  1. Watoto wakorofi wamelala. Neno wakorofi ni;
  1. Kitenzi
  2. Nomino
  3. Kivumishi
  4. Kiwakilishi
  1. Mtoto wa ng’ombe anaitwa?
  1. Maksai
  2. Mtamba
  3. Mdoli
  4. Ndama
  1. Yule ni mzee hamisi. Neno yule ni la aina ipi ya maneno?
  1. Kielezi
  2. Kiunganishi
  3. Nomino
  4. Kiwakilishi

SEHEMU B. FASIHI, METHALI, NAHAU NA VITENDAWILI

Kamilisha Methali

  1. Zimwi likujualo............................................
  2. Usipoziba ufa.................................................
  3. Mwanzo wa ngoma.................................................
  4. Ari ya mjinga ni.......................................................

Tegua vitendawili

  1. Huuawa na uzazi wake...............................................
  2. Bibi hupigwa virungu kila siku na hatoroki....................................
  3. Askari wangu akiniona hutikisa au kuficha mkia..............................

Toa maana ya nahau zifuatazao

  1. Unga mkono
  2. Bega kwa bega
  3. Fanya juu chini

SEHEMU C. UTUNGAJI

        Tunga habari yenye maneno mia moja kuhusu biashara unayoipenda ukizingatia yafuatayo

  1. Jina la biashara
  2. Inahusu nini
  3.                     Faida uzipatazo kwenye biashara yako
  4.                      Changamoto zake
  5. Namna ya kukabiliana na changamoto hizo

 

SEHEMU D. USHAIRI

Jibu Maswali yafuatayo kuhusu ushairi

  1. Shairi huweza kuimbwa au?
  1. Kughaniwa
  2. Kuchezwa
  3. Kutambwa
  4. Kutegwa
  1. Nini maana ya kughani shairi?
  1. Kusoma shairi
  2. Kuimba shairi
  3. Kueleza shairi
  4. Kuandika shairi
  1. Idadi ya silabi katika mshororo huitwa?
  1. Beti
  2. Vina
  3. Mizani
  4. Silabi
  1. Ubeti wa ushairi wenye mistari minne huitwa?
  1. Kibwagizo
  2. Kituo
  3. Mshororo
  4. Tarbia.
  1. Katika shairi la kimapokeo, ..............................vya kati na vya mwisho katika ubeti hufanana
  1. Beti
  2. Vina
  3. Mizani
  4. Silabi.

LEARNINGHUBTZ.CO.TZKISWAHILI STANDARD SIX EXAM SERIES 33

MINISTRY OF EDUCATION, REGIONAL ADMINISTRATION AND LOCAL GOVERNMENT

STANDARD SIX EXAMINATION SERIES

KISWAHILI, MID TERM SEPTEMBER 2021

ANSWER ALL QUESTIONS

SEHEMU A: SARUFI

  1. Ili nifaulu mtihani wangu.........nijifunze kwa bidii.
  1. Budi
  2. Ni budi
  3. Sina budi
  4. Sio budi
  5. Si budi
  1. Viongozi wanatuhimiza tufanye “utundu” wa kisayansi. Neno “utundu” limetumika kama aina ipi ya maneno?
  1. Nomino
  2. Sifa
  3. Kivumishi
  4. Kiwakilishi
  5. Kiunganishi
  1. Neno lipi linakamilisha sentensi hii? “waziri aliwataka wananchi waudhibiti uchumi wao ili..........na mabadiliko yaliyopo.
  1. Usiasiliwe
  2. Usiadhiriwe
  3. Usiashiriwe
  4. Usiathiliwe
  5. Usiathiriwe
  1. Sentensi ifuatayo iko katika kauli ipi? “ shule yetu imeharbiwa na upepo”
  1. Kutenda
  2. Kutendana
  3. Kutendeana
  4. Kutendewa
  5. Kutendea
  1. Sikumkuta mtu........nyumbani.
  1. Yoyote
  2. Yeyote
  3. Wowote
  4. Awaye
  5. Yote
  1. “Alisema yeye hatakwenda”. Sentensi ipi kati ya hizi zifuatazo imebadilisha kauli hii taarifa kuwa kauli halisi?
  1. Alisema haendi
  2. Alisema yeye ataenda
  3. Mimi sitaenda
  4. Kuwa sitaenda
  5. Alisema mimi nitaenda
  1. Katika sentensi ifuatayo ni neno lipi limetumika kama kivumishi? “Jana mwalimu alivaa shati nadhifu”
  1. Nadhifu
  2. Jana
  3. Alivaa
  4. Mwalimu
  5. Shati
  1. Ipi maana sahihi ya neno “aghalabu”
  1. Mara nyingine
  2. Mara chache
  3. Mara nyingi
  4. Mara dufu
  5. Mara kwa mara
  1. Nani amesema kwamba mwalimu mkuu amehamishwa? Neno lipi katika sentensi hiyo ni kiwakilishi?
  1. Nani
  2. Amesema
  3. Mwalimu
  4. Mkuu
  5. Amehamishwa
  1. Jana waziri alitoa hotuba nzuri. Katika sentensi hii neno lipi limetumika kama kivumishi?
  1. Jana
  2. Alitoa
  3. Waziri
  4. Hotuba
  5. Nzuri
  1. Katika sentesi ifuatayo, neno linalokosekana ni lipi? Ni lazima tuwe waangalifu kwani..........wengi.
  1. Hasidi
  2. Husuda
  3. Mahasidi
  4. Aside
  5. Maasidi
  1. Katika neno “wananifuata” kiambishi kinachoonesha wakati ni kipi?
  1. Fua
  2. Ata
  3. Na
  4. Ni
  5. Fuata
  1. Neno lipi kati ya haya lina maana sawa na neno “suriama”
  1. Zeruzeru
  2. Chotara
  3. Mzuri
  4. Mlimbwende
  5. Msichana
  1. Kama ungaliniomba mapema.........
  1. Nitakusaidia
  2. Ningelikusaidia
  3. Ningekusaidia
  4. Ningalikusaidia
  5. Nikusaidie
  1. Ng’ombe walifugwa zizini. Sentensi hii ipo katika hali ya
  1. Kutenda
  2. Kutendwa
  3. Kutendea
  4. Kutendewa
  5. Kutendana
  1. Anapenda kukaa bure............ana nguvu za kufanya kazi.
  1. Angalau
  2. Iwapo
  3. Sipokuwa
  4. Pamoja
  5. Japokuwa
  1. “Wizi wa mali za shule umetokea jana usiku”. Katika sentensi hii neno lipi limetumika kama kitenzi?
  1. Mali
  2. Shule
  3. Wa
  4. Ya
  5. Umetokea

SECTION B: MSAMIATI

  1. Jeni alikuwa na..........aliposikia habari za ajali ile.
  1. Dukuduku
  2. Tama
  3. Shauku
  4. Njozi
  5. Fikira
  1. Neno lenye maana sawa na “ufukara” ni lipi?
  1. Ukwasi
  2. Usawa
  3. Mkukuta
  4. Ukata
  5. Utemi
  1. Mahindi, ngano, nazi, machungwa, mihogo, viazi na mtama. Andika kwa neno moja
  1. Nafaka
  2. Matunda
  3. Mizizi
  4. Mazao
  5. Mimea
  1. Fundi atengenezaye herein, pete na mikufu huitwaje?
  1. Sofara
  2. Mfuaji
  3. Sonara
  4. Mnajimu
  5. Fundi
  1. Neno la kiswahili lenye maana sawa na mwisho ni
  1. Mwanzo
  2. Kifo
  3. Tamati
  4. Utangulizi
  5. Pembezoni
  1. Kumwonea mtu kijicho ni
  1. Kumwona mtu kwa jicho dogo
  2. Kumnyanyasa
  3. Kumwonea wivu
  4. Kumsakama
  5. Kumtuliza
  1. Tembo aliweza kuvunja tawi la mti kwa kutumia..........wake.
  1. Mkungu
  2. Mkonga
  3. Mkia
  4. Ulimi
  5. Pembe
  1. Mtu anayenadi na kuuza vitu mnadini anaitwa
  1. Dalali
  2. Mzabuni
  3. Muuzaji
  4. Mbinguzi
  5. Mchuuzi
  1. Jumanne alikimbia..........ya farasi
  1. Kawaida
  2. Mithili
  3. Kama
  4. Mfano
  5. Mbio
  1. Kinyume cha “aghalabu” ni
  1. Abadani
  2. Kamwe
  3. Mara nyingi
  4. Nadra
  5. Mara chache
  1. Neno lipi kati ya maneno yafuatayo lina maana sawa na neno “shaghalabagala”
  1. Mpangilio
  2. Ovyo ovyo
  3. Vizuri
  4. Faragha
  5. Mafichoni
  1. Mtu anayeacha kazi ya ajira baada ya kutimiza umri wake kutokana na kanuni anaitwa?
  1. Mzee
  2. Mchapakazi
  3. Mstaafu
  4. Mstaarabu
  5. Muhitimu
  1. “Urafiki wetu ni kama pete na kidole” Maneno ambayo ni viunganishi ni
  1. Kama” na “ni”
  2. “urafiki” na “wetu”
  3. “wetu” na “pete”
  4. “kama” na “na”
  5. “pete” na “kidole”

SEHEMU C: METHALI, NAHAU NA VITENDAWILI

  1. Maana ya nahau “kupiga chuku” ni
  1. Kusema kweli daima
  2. Kutoa maelezo ya uongo
  3. Kutia maneno chumvi
  4. Kukataa katakata
  5. Kuona mengi
  1. Kindendawili kisemacho “wana wa mfalme ni epesi sana kujificha” maana yake ni
  1. Ulimi
  2. Masikio
  3. Pua
  4. Macho
  5. Kope
  1. Methali yenye maana sawa na methali “upele humwota asiye na kucha”
  1. Usimwage mchele penye kuku wengi
  2. Penye nia pana njia
  3. Akili nyingi huondoa maarifa
  4. Penye miti mingi hakuna wajenzi
  5. Mwenda pole hajikwai
  1. Mbwa mwitu wamemzunguka kumlinda. Maana ya kitendawili hiki ni
  1. Ulimi na meno
  2. Nywele kichwani
  3. Mate na meno
  4. Mti na miiba
  5. Pua na mdomo
  1. Nini maana ya nahau “ashakumu si matusi”
  1. Samahani kwa haya nitakayosema
  2. Tafadhali usitamke matusi
  3. Tafadhali sikiliza
  4. Sikiliza kwa makini
  5. Kata kauli

SECTION D: UTUNGAJI

Umepewa insha yenye sentensi 5 zilizoandikwa bila mpangilio sahihi zipange sentensi hizo ili zililete mtiririko mzuri wa mawazo kwa kuzipa herufi A, B, C, D na E.

  1. Aliposhuka nikamlaki kwa furaha na kuelekea nyumbani pamoja
  2. Kumbe basi hilo ndilo alilosafiria rafiki yangu
  3. Ingawaje sikuchelewa lakini nilijawa na wasiwasi pale kituoni
  4. Baada ya kuangaza macho upende wa magharibi nikaona basi la kwanza likijitoma pale kituoni
  5. Kulipopambazuka nilioga haraka nikavaa upesi kuelekea kituo cha mabasi

SEHEMU E: USHAIRI

Soma shairi kwa makini, kisha jibu maswali 41-45 kwa kuchagua jibu sahihi

Kusahau ni kubaya, kwani kwaleta majuto,

Kwamtia mtu haya, achekwe kama mtoto,

Kunapoteza hedaya, yeye kuleta kipato

Mtu atafuta jembe, kumbe lipo mabegani.

Ataivunja safari, awaulize jirani,

Moyoni atafakari, ameliacha kwa nani,

Yafaa uwe jasiri, tenda mambo kimakini,

Mtu atafuta jembe, kumbe lipo mabegani.

Maswali

  1. Katika ubeti wa kwanza mtunzi ametumia neno “hedaya” kama
  1. Mkufu
  2. Zawadi au tuzo
  3. Mazao
  4. Heshima na adabu
  5. Mawazo
  1. Vina vya kati katika ubeti wa pili ni
  1. ya
  2. ri
  3. ni
  4. ze
  5. wa
  1. shairi lina mizani......
  1. 16
  2. 14
  3. 18
  4. 36
  5. 8
  1. Kibwagizo au kituo katika shairi hili ni
  1. Kutafuta jembe
  2. Mtu atafuta jembe, kumbe lipo mabegani
  3. Kuvunja safari
  4. Kusahau
  5. Hakipo
  1. Kichwa chwa habari kifaacho kwa shairi hili ni
  1. Jembe
  2. Kusahau
  3. Kutafuta kitu
  4. Tuwe makini
  5. Tukumbatiane

LEARNINGHUBTZ.CO.TZKISWAHILI STANDARD SIX EXAM SERIES 31

OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOGIA

MTIHANI WA MWISHO WA MWAKA DARASA LA NNE

KISWAHILI

MUDA:1:30

JINA_____________________________________SHULE_________________________

MAELEKEZO

1. Karatasi hii ina sehernu A,B,C,D na E zenye jumla ya maswali 45

2. Jibu maswali yote katika kila sehemu

SEHEMUA (Mama 20)

SARUFI

Katika swali is 1-20, weka kivuli katika herufi ya jibu iililosahihi katika fomu yako ya kujibia.

  1. Neno lipi kati ya haya halilandani na mengine? 
  1. Tembe 
  2. Kibanda 
  3. Msonge 
  4. Ghorofa 
  5. Daraja
  1. Katika sentensi ifuatayo neno lipi limetumika kama kiwakilishi? "hicho ulichotaka sikupata".
  1. Ulichotaka
  2. Hicho
  3. Sitapata
  4. Nitapata
  5. .Lichochukuwa
  1. Mtu anayesimamia kazi za shambani anaitwaje? 
  1. Msimamizi 
  2. Mkuu 
  3. Nokoa 
  4. Mnyapara 
  5. Kiongozi
  1. Ni sentensi ipi iliyo sahihi kimuundo kati ya zifuatazo?
  1. Amenunua redio Juma
  2. Juma redio amenunua 
  3. Amenunua juma redio 
  4. Juma amenunua redio 
  5. Redio amenunua juma

5. Kisawe cha neno "bahati" ni kipi kati ya haya yafuatayo

  1. Tunu
  2. Hidaya
  3. Shani
  4. Sudi
  5. Hiba

6. "Nguo yangu imechafuka sana" wingi wa sentensi hiyo ni upi?

  1. Nguo yangu imechafuka sana
  2.  Nguo yetu zimechafuka sana
  3.  Nguo zetu zimechafuka sana 
  4. Nguo zao zimechafuka sana 
  5. Nguo yetu imechafuka sana

7. Lima na Omani wanatembea kivivu. Neno ‘kivivu" limetumika kama aina gani ya neno? 
A. KieleziB)KivumishiC)NominoD) KiwakilishiE) Kionyeshi

8. Mgeni aliondoka alipofika……….kuaga

  1. Licha ya
  2. Pasi ya
  3. Bila kwa
  4. Bila na
  5. Bila ya

9. Unaponyumbulisha neno "apiza"unapata nomino ipi?

  1. Kiapo
  2. Pizo
  3. Apizika
  4. Waapizo
  5. Apizana

10. Sikuweza kutambua ni nani amelala kitandani kwa sababu alijifunika shuka

  1. Lote
  2. Zima
  3. Zama
  4. Gubigubi
  5. Tororo

11. Alisema hajisikii vizuri. Kauli halisi ya sentensi hii ni ipi?

  1. "hajisikii vizuri"
  2. "anajisikia vizuri"
  3. "najisikia vizuri"
  4. "nilijisikia vizuri"
  5. "sijisikii vizuri"

12. Neno lipi linakamilisha sentensi ifuatayo? Kama kazi ingalifanywa na mtu mmoja.................kumaliza.

  1. Asingeweza
  2. Asingaliweza
  3. Angailweza
  4. Asingeliweza 
  5. Angeliweza

13. Katika neno "hatukukamilisha" kiambishi kinachoonyesha nafsi ni kipi?

  1. ka- 
  2. a. ta- -
  3. ha- 
  4. – sha- 
  5. -tu-

14. Alfajiri na mapema tuliondoka ukumbini. Mzizi katika neno lilllopigiwa mstari ni upi?

  1. Undo 
  2. Ondok 
  3. Ondoka 
  4. londok 
  5. Uondoka

15. Umoja wa sentensi "ndege hawa wanakunywa maji ni

  1. Ndege hii inakunywa maji
  2. Dege hill inakunywa may
  3. Ndege yule__anakunwa maji
  4. Ndege huyu hakunywa maji
  5. Ndege huyu anakunywa maji

16. Neno lipi ni tofauti na maneno mengine kati ya yafuatayo?

  1. Seng'enge
  2. Wigo
  3. Barabara
  4. Ukuta
  5.  Ukingo

17. Neno "MWANAFUNZI" lipo katika upatanisho wa ngeli aina gani?

  1. I-ZI
  2. LI-YA
  3. U-YA
  4. A-WA
  5. U-ZI

18. "Ala kumbe! Aliondoka jana jioni?" Kihisishi ni kipi katika maneno yafuatayo? 

  1. Ala kumbe! 
  2. Aliondoka 
  3. Kumbe 
  4. Ala 
  5. Jana

19. Ili tuvune mazao bora…………. tulime kwa juhudi na maarifa.

  1. Ni budi
  2. Budi 
  3. Hatuna budi
  4. Tuna budi 
  5. Kura budi

20. Katika vitenzi "sitafyeka" na "hupendi" ni silabi zipi zinazoonesha ukanushi? 
A. Ta na hu B) Ta na peC) Ka na ndi D) Fye na pe E) Si na hu

SEHEMU B (alama 10)

LUGHA YA KIFASIHI

21. Ntandi alikuwa na kichwa cha panzi. Msemo kichwa cha panzi una maana gani?

  1. Msikivu sana
  2. Mtiifu sana
  3.  Mtambuzi
  4. Msahaulifu
  5. Ana kumbukumbu

22. Methali ipi kati ya hizi zifuatazo haifanani na nyingine?

  1. Mgagaa na upwa hall wall rnkavu
  2. Anayekaa karibu na waridi hunukia waridi
  3. Mlinzi wa kisima hafi kiu 
  4. Nazi haishindani na jiwe 
  5. Mtegemea nundu haachi kunona
  1. Kukubali kwa ulimi ni msemo wenye maana ipi?
  1. Kukubali kwa dhati
  2. Kukubali kwa maneno
  3. Kukubaii bila kusema neno
  4. Kukubali kimoyomoyo 
  5. Kukubali kwa moyo mmoja
  1. Jamilaana ulimi wa upanga Nahau "ulimi wa upanga" ina maana gani?
  1. Kusema ovyo
  2. Kupayuka
  3. Kutoa maneno makali
  4. Kusema ukweli
  5. Kusema uongo
  1. Tegua kitendawili kifuatacho" nyumbani kwangu kuna jini mnywa maji".
  1. Mtungi
  2. Kibatari
  3. Kinywa
  4. Kata
  5. Kikombe
  1. Methali isemayo "chanda chema huvikwa pete" inatoa funzo gani?
  1. Mshindi hupokea Baraka
  2. Dhahabu hupewa aliyeshinda
  3. Jambo zuri huzawadiwa 
  4. Inapobidi jamii hupewa zawadi 
  5. Mtu mzuri husifiwa.
  1. "Meno ya mbwa hayaumani "ni methali ipi inaweza kufanana na hii?
  1. Mwana kidonda mjukuuu kovu
  2. Akipenda chongo huita kengeza
  3. Maneno matupu hayavunji mfupa 
  4. Damu nzito kuliko maji 
  5. Heri mrama kuliko kuzama
  1. Jinamizi laniita lakini silioni. Maana ya kitendawili hiki ni
  1. Jua
  2. Mwangwi
  3. Radi
  4. Popo
  5. Mwezi
  1. Uzururaji umepigwa marufuku .nahau" umepigwa marufuku ina mana gani? 
  1. Umezoeleka 
  2. Umepigwa winda 
  3. Umekithiri 
  4. Umekatazwa 
  5. Umepigwa konde
  1. " Mwenye nguvu ---" neno lipi linakamilisa methali hii?
  1. Mfunge
  2. Usimkamate
  3. Mkimbie
  4. Usimpige
  5. Mpishe

SEHEMU C (Alama 6)

USHAIRI

Soma kwa makini shairi lifuatalo kisha jibu maswali 3136 kwa kuweka katika herufi ya jibu sahihi katika fomu ya kujibia.

Wanafunzi siklliza, nawapa huu wosia Nataka kuwaeleza, mambo muhimu Kwanza ninawapongeza, hapa mlipofikia Hongereni, hongereni, hongereni kuhitimu

Hapa mlipolikia, kamwe msije bweteka, Malengo kuyafikia, huu ni mwanzo hakika, Usije kuvisikia, vitabuvyo kamwe taka, Hongereni hongereni, hongereni kuhitimu

Shuleni mmejifunza, masomo kwa hakika, ICiswahili ni cha kwanza, lugha hamkuichoka, Kwa ari mkijifunza, mbele kita wapeleka, Hongereni hongereni, hongereni kwa kuhitimu

Safari miaka saba, yenye raha na karaha, Mlichopataisi haba, mwende nacho kwa furaha, hicho kidogo kihaba, kisilete majeraha,

Hongereni hongereni, hongereni kwa kuhitimu

  1. Mshairi anaposema " mlichokipata si haba"ana alaana gani?
  1. Mlichokipata si kelele
  2. Mlichokipata si kidogo
  3. Mlichokipata si duni
  4. Mlichokipata si dhaifu 
  5. Mlichokipata si kibaya
  1. Vina katika ubeti wa pili ni vipi?
  1. Ha na ka
  2. A na ka
  3. Ho na ho
  4. Hi na mu
  5. U na vi
  1. Wazo kuu katika shairi hill ni lipi?
  1. Kuhitimu ni jambo muhimu
  2. Elimu ya msingi ni bora zaidi
  3. Kujiendeleza kielimu ni muhimu 
  4. Kiswahili ni somo la muhimu 
  5. Kuhitimu ni lazima
  1. Kichwa kinachofaa kwa shairi hill ni kipi?
  1. Ushauri kwa wahitimu
  2. Kuhitimu si fahari
  3. Elimu ya Msingi
  4. Wanafunzi wahitimu
  5. Fahari ya kuhitimu
  1. Kinyume cha neno " karaha" ni kipi?
  1. Amani
  2. Kero
  3. Furaha
  4. Adhabu
  5. Adabu
  1. Neno "bweteka" kama lilivyotumika kwenye shairi hilo lina maana ipi?
  1. Kudhihaki
  2. Kudhalilika
  3. Kudhoofika
  4. Kuridhika
  5. Kudhihirika

SEHEMU D (ALAMA 4)

UTUNGAJI

Umepewa habari yenye sentensi nne (4) zilizoandikwa bila mtiririko sahihi wa mawazo katika swali la 37-40. Zipange sentensi hizo ill ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi A,B,-C. na D

  1. Ili mpate kuyajua ni lazima mjifunze kwa bidii na maarifa ill muweze kufaulu mitihani yenu.
  2. Ninyi ni vijana wadogo wenye matumaini ya kupata maendeleo katika maisha yenu ya baadaye.
  3. Endeleeni kusoma na kujifunza kwa bidii kwani elimu ni bahari haina mwisho.
  4. Elimu ndiyo itakayoweza kuwafungulia njia za kupata maendeleo hayo katika safari hii ya kuelimika zaidi.

SEHEMU (Alama 10)

UFAHAMU

Soma kwa makini habari ifuatayo kisha jibu swali 41-45 .c va kuandika jibu sahihi katika nafasi iliyoachwa wazi.

Zamani babu zetu walitabiri mvua wao wenyewe bila kuwa na vyombo vya kisasa. Suala linalozungumziwa sasa ni mabadiliko ya hali ya hewa na athari zake kwa jamii nzima, mabadiliko haya yamekuwa makubwa kiasi cha'kutisha.

Kila mtu ana wasiwasi kuhusu mvua ambazo huchukua muda mrefu bila kunyesha. Ukosefu wa mvua huleta ukame na njaa ambayo umechangiwa na bianadamu kwa kiasi kikubwa na shughuli za kibinadamu ambazo huongezeka kwa haraka siku hadi siku, kwa upande mwingine huonekana kama ni maendeleo.

Mifano inayoonyesha matumizi hayo ni ujenzi wa nyumba, nishati kwa ajili ya kupikia, mbao na magogo kwa wingi kwa matumizi ya ndani na nje ya nchi.

Hata hivyo ili maendeleo yawe chanya jamii inalazimika kupanda miti kwa wingi ilii kukidhi mahitaji yao. Aidha, ni vema kuzingatia kuwa ukataji wa miti kwa wingi ni chanzo kikubwa cha mito na vijito kuvva na maji haba au kukauka kabisa.

MASWALI

  1. Kichwa cha habari kinachofaa kwa habari hii ni ----
  2. Neno "haba" kama linavyotumika katika habari hii lina maana sawa na neno
  3. Ili maendeleo yawe chanya jamii inalazimika kufanya nini?
  4. Ukame na njaa husababishwa na ukosefu wa......
  5. Watu wa zamani waliweza kutabiri mvua kwa kutumia.....

LEARNINGHUBTZ.CO.TZKISWAHILI STANDARD SIX EXAM SERIES 21

OFISI YA RAIS WIZARA YA ELIMU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

KISWAHILI- MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA

DARASA LA SITA

MUDA: 1.30

MAELEKEZO

  1. Karatasi hii ina kurasa nne zenye maandishi yenye sehemu A,B, C,D na E zenye maswali arobaini na tano (45).
  2. Jibu maswali yote katika kila sehemu ya mtihani huu.
  3. Kumbuka kuandika majina yako, na shule yako kwenye karatasi ya kujibia.
  4. Hakikisha kazi yako ni nadhifu sana.
  5. Tumia kalamu ya wino wa bluu au nyeusi kwa maswali yote uliyopewa.

SEHEMU : A SARUFI

Chagua herufi ya jibu sahihi kisha uiandike kwenye karatasi ya kujibia uliyopewa

1. Gari langu ni bovu, lake ni zima. Neno lake limetumika kama aina ipi ya neno?

  1. Kielezi
  2. Kitenzi
  3. Kiwakilishi
  4. Nomino
  5. Kivumishi

2. Anakuja kufanya nini? Sentensi hii ipo katika nafsi ya ngapi?

  1. Kwanza umoja 
  2. Tatu wingi
  3. Tatu umoja
  4. Pili wingi
  5. Pili umoja

3. Neno mlimbwende lina silabi ngapi?

  1. Nne
  2. Tatu
  3. Sita
  4. Saba
  5. Kumi

4. Nitakula chakula changu chote. Ipi ni kauli taarifa ya sentensi hii?

  1. Alisema kuwa atakula chakula chake chote 
  2. Alisema kuwa nitakula chakula changu chote 
  3. Alisema kuwa nitakula chakula        
  4. Alisema nitakula chote
  5. Alisema kuwa chakula chake chote atakula

5. Kipi ni kiambishi cha wakati katika neno watamaliza?

  1. Ha
  2. Wa
  3. Ma
  4. Li
  5. ta

6. Kinyonga anatembea polepole. Neno polepole ni aina gani ya neno?

  1. Kielezi
  2. Kiwakilishi
  3. Kivumishi
  4. Kitenzi
  5. Nomino

7. Ipi ni ngeli ya neno embe?

  1. A-WA
  2. LI-YA
  3. U-YA
  4. I-ZI
  5. U-ZI

8. Kipi ni kinyume cha neno ezua?

  1. Ezeka
  2. Paa
  3. Paua
  4. Panua
  5. Panda

9. Hakuna mwalimu__________ darasani

  1. Yoyote
  2. Yeyote
  3. Lolote
  4. Wowote
  5. Kokote

10. Shangazi amejengewa nyumba na baba. Sentensi hii ipo katika kauli gani ? 

  1. Kutenda
  2. Kutendewa
  3. Kutendeka
  4. Kutendwa 
  5. kutendesha

11. Neno lipi halilandani na mengine?

  1. Bahasha
  2. Stempu
  3. Anwani
  4. Sahihi
  5. ukuta

12. Huko____ alikoelekea simba

  1. Ndimo
  2. Ndiko
  3. Ndipo
  4. Ndilo
  5. ndicho

13. Wamekuja wote isipokuwa Munira. Neno isipokuwa llimetumika kama aina ipi ya neno?

  1. Kitenzi
  2. Kiunganishi
  3. Kivumishi
  4. Kiwakilishi
  5. kihisishi

14. Kipindi cha mvua za rasha rasha hujulikana kama      

  1. Kifuku
  2. Kipupwe
  3. Vuli
  4. Kiangazi
  5. Masika

15. Upi ni mzizi wa neno fundisha

  1. fundi___
  2. fund___
  3. fundish____
  4. fundis___
  5. fundisha

16. Ipi ni nomino ya dhahania kati ya hizi?

  1. Iringa
  2. Usingizi
  3. Miti
  4. Ndege
  5. jozi

17. Pete ya dada imetengenezwa na  mzoefu sana.

  1. Mwashi
  2. Mhunzi
  3. Sonara
  4. Rubani
  5. Nahodha

18. Nilimsisitiza Aisha kuwa kusoma kwa bidii ili afaulu vizuri.

  1. Hatuna budi
  2. Hawana budi
  3. Hana budi
  4. Sina budi
  5. Hamna budi

19. Nomino ya kitenzi lia ni…………

  1. Kilio
  2. Somo
  3. Nakala
  4. Mafundisho
  5. Malio

20. Wingi wa sentensi paka anakunywa maziwa ni__ 

  1. Mapaka yanakunywa maziwa         
  2. Paka yanakunywa maziwa
  3. Mapaka yamekunywa maziwa         
  4. Paka wanakunywa maziwa
  5. Paka anakunywa ziwa

SEHEMU B: LUGHA YA KIFASIHI

Chagua herufi ya jibu sahihi.

21.    Methali ipi haisisitizi juu ya ushirikiano?

  1. Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu
  2. kidole kimoja hakivunji chawa
  3. figa moja haliinjiki chungu      
  4. kidole kimoja hakipigi kofi
  5. chelewa chelewa utakuta mwana si wako

22. Methali ipi inasisitiza juu ya umuhimu wa undugu?

  1. damu nzito kuliko maji  
  2. haba na haba hujaza kibaba
  3. upele humwota asiyekuwa na kucha
  4. penye miti hapana wajenzi
  5. siku za mwizi ni arobaini

23. Juma ana kichwa cha panzi. Hii ina maana kuwa Juma ni__________ 

  1. mwongo
  2. mzoefu
  3. msahaulifu
  4. mkweli
  5. kichwa kikubwa

24.    Malizia methali hii, ukila nyama ukumbuke………

  1. kuguguna mfupa wake 
  2. kula mfupa wake 
  3. kubeba
  4. kubakiza 
  5. kushukuru

25.  Fimbo ya mtemi haina fundo. Lipi ni jibu la kitendawili hiki?

  1. Moshi
  2. Njia
  3. Nyoka
  4. Mti
  5. kichwa

26.  Kinachokufaa ni kile ulichonacho, methali yenye kubeba maelezo haya ni.

  1. hamadi kibindoni
  2. wema hauozi
  3. ajali haina kinga
  4.  kiburi si maungwana
  5. mwenda pole hajikwai

27.   Tegua kitendawili hiki, kulia kwake ni kicheko kwetu____ 

  1. radi
  2. mvua
  3. upepo
  4. njia
  5. popo

28. Metahli ipi inalandana na ile isemayo meno ya mbwa hayaumani

  1. siku za mwizi ni arobaini
  2. zimwi likujualo halikuli likakwisha
  3. asiyeuliza hana hajifunzalo
  4. chembe na chembe mkate huwa
  5. sanda ya mbali haiziki maiti

29. Nahau ya kuwa popo ina maana gani?

  1. Kigeugeu
  2. kuwa mnyama
  3. kuwa msahaulifu 
  4. kuwa mwoga 
  5. kuwa tajiri

30.  Nyumbani kwangu kuna jini mnywa maji. Jibu la kitendawili hiki ni

  1. kikombe
  2. kibatari
  3. kitabu
  4. kisima
  5. shimo

SEHEMU C: USHAIRI

Soma shairi hili kisha jibu maswali yafuatayo

  1. Karudi baba mmoja, toka safari ya mbali, kavimba yote mapaja, na kutetemeka mwili, watoto wake wakaja , ili kumtaka hali, wakataka na kauli, iwafae maishani.
  2. Akatamka mgonjwa , ninaumwa kwelikweli, hata kama nikichanjwa, haitoki homa kali roho naona yachinjwa , kifo kinanikabili, kama wakata kauli , sema niseme nini?

MASWALI

Chagua herufi ya jibu sahihi kisha iandike kwenye karatasi ya kujibia.

31. Neno kauli kama lilivyotumika katika ubeti wa kwanza wa shairi lina      maana gani?

  1. Tamko
  2. Muhtasari
  3. Maradhi
  4. Ugonjwa
  5. Vina

32. Kuna mizani mingapi katika kila mstari

  1. Kumi
  2. Nane
  3. Kumi na sita
  4. Tisa
  5. Nne

33. Vina vya katikati ubeti wa pili ni?

  1. li
  2. wa
  3. njwa
  4. ja
  5. nj

33. shairi hili lina beti ngapi?

  1. Tatu
  2. Tano
  3. Nne
  4. Moja
  5. Mbili

34. wakakata na kauli, iwafae maishani lipi ni jina la mstari huu?

  1. Mizani
  2. Vina
  3. Mkarara
  4. Mshororo
  5. Mstari

35. Shairi hili lina majibizano ya pande ngapi?

  1. Nne
  2. Tatu 
  3. Nane
  4. Moja
  5. Mbili.

 SEHEMU D: UTUNGAJI

Panga sentensi zifuatazo kwa mtiririko unaofaa kwa kuzipa herufi A,B,C,na D

36. Ilikuwa ni usiku wa manane

[  ]

37. Asubuhi yake tulianza safari ya kuelekea kijijini Manga

[  ]

38. Baba alipigiwa simu na kupewa taarifa ya msiba wa bibi yetu

[  ]

39. Baba alituamsha   na kutupa taarifa zile na kutusihi tulale lakini

hatukupata hata lepe ya usingizi

[  ] 

 SEHEMU E: UFAHAMU

Soma vizuri habari ifuatayo kisha jibu maswali yafuatayo kwa usahihi.

Mfalme Bwanyenye wa nchi ya Ahadi hakupenda kuongoza kwa haki. Kila alichokisema yeye wapambe wake walikifanya kuwa sheria. Alivimba kichwa na kujiona yeye ndiye mwamba shupavu. Ulikuwa ni ufalme wa kimabavu. Haswa! Wanazuoni wengi walidai kuwa huo ni udiktekta. Kila mtu hakuwa salama, jela zilijaa watu wasio na hatia. Useme kipi uwe salama? Hilo lilikuwa ni fumbo kubwa, wengi kwa kuogopa walinyamaza kimya na kujifariji kwa kusema hakuna marefu yasiyokuwa na ncha. Walijiuliza yupo wapi Adolf Hilter, yule mtawala

wa Ujerumani aliyekuwa katili, yu wapi Mobutu wa Kongo aliyekuwa na nguvu tele? Naam, wote wamepita mithili  ya radi.

MASWALI

40. Neno wanazuoni kama lilivyotumika katika habari hiyo lina maana gani

41. Mfalme Bwanyenye alitawala nchi gani?____________ 

42. Eleza maana ya methali iliyotumika katika habari hii ? __ 

43. Neno mithili kama lilivyotumika katika aya ya mwisho lina maana gani ?

44. Kichwa cha habari hii chafaa kuwa

LEARNINGHUBTZ.CO.TZKISWAHILI STANDARD SIX EXAM SERIES 12

OFISI YA RAISI, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MTIHANI WA KUJIPIMA DARASA LA SITA

APRIL-2020  MUDA:SAA 2:00

KISWAHILI

MAELEZO KWA MTAHINIWA

  1. MTIHANI HUU UNAMASWALI JUMLA YA 50
  2. JIBU MASWALI YOTE
  3. ANDIKA MAJIBU KWA HERUFI KUBWA
  4. KAZI YAKO IWE SAFI.

SEHEMU A. Chagua jibu sahii katika uliopewa.

1.       "Mwajuma amemwibia Mwanahamisi kalamu yake". Katika sentensi hii. https://myfiles.space/user_files/30996_4958b541bbe404eb/1569855423_kiswahili-2017_files/image022.jpg"Mwajuma ni nani?

  1. Mtendewa 
  2.  Mtendana
  3.  Mtendeka 
  4.  Mtenda
  5. Mtendwa

2       "Uvumilivu ulimfanya Pendo apate zawadi. "Uvumilivu ni aina gani ya neno?

  1. Nomino
  2.  Kitenzi
  3. Kivumishi
  4. Kihisishi
  5. Kiwakilishi

3.         Kauli ipi inaonesha hali ya kutendewa?

  1. Tumechimba visima vyetu. 
  2.  Tunachimbisha kisima chetu. 
  3. Tulichimbiwa kisima chetu. 
  4. Tumechimba kisima chetu.
  5. Tutachimba kisima chetu.

4.         Katika vifungu vya maneno vifuatavyo, kifungu kipi kipo katika kauli taarifa?

  1. Unataka kuondoka lini? 
  2. Alitaka kukuuliza unaondoka lini. 
  3. Ni lini wewe utaondoka? 
  4.  Aliuliza, utaondoka lini?
  5. Aliuliza kuwa ataondoka lini?

5.         Mwenyekiti hakufika mkutanoni leo. Kitenzi "hakufika" kipo katika hali gani?

  1. Mazoea  
  2. Kuendelea  
  3. Timilifu
  4. Matarajio 
  5.  Kanushi

6.      Wingi wa sentensi "Mbuzi wamepotea" ni upi?

  1. Mbuzi zetu zimepotea
  2. Mbuzi yetu zimepotea
  3. Mbuzi wetu wamepotea 
  4.  Mbuzi zetu wamepotea
  5. Mbuzi yetu wamepotea.

7.      "Wanafunzi kenda walikwenda ziara nchini Kenya".neno wa ni aina gani ya neno?

  1.   https://myfiles.space/user_files/30996_4958b541bbe404eb/1569667722_kisw-2018_files/image019.jpgKivumishi https://myfiles.space/user_files/30996_4958b541bbe404eb/1569667722_kisw-2018_files/image020.jpg
  2.    Kiwakilishi
  3.    Kielezi 
  4.    Kitenzi
  5.     Nomino.

8.      Ashura anacheza mpira wa miguu vizuri.katika sentensi hii,neno lipi limetumika kama kielezi? https://myfiles.space/user_files/30996_4958b541bbe404eb/1569667722_kisw-2018_files/image022.jpg

  1. Anacheza
  2.  Mpira
  3. Vizuri
  4. Ashura
  5. Wa mguu.

9. Mtu anayetafsiri ana kwa ana katika lugha moja kwenda lungha https://myfiles.space/user_files/30996_4958b541bbe404eb/1569667722_kisw-2018_files/image023.jpghuitwaje?

  1. Msuluhishi
  2. Mpatanishi
  3. Mkalimani
  4.  Mfafanuzi
  5. Mhubiri

10. "Sote tunafanya mtihani darasani". "darasani" limetumika kama aina gani ya neno?

  1. Kielezi
  2. Kivumishi https://myfiles.space/user_files/30996_4958b541bbe404eb/1569667722_kisw-2018_files/image022.jpg
  3. Kitenzi
  4. Kiwakilishi 
  5.  Nomino

11.      "Tulicheza ngoma na kuimba usiku kucha.” Katika sentensi hii watenda ni nafsi ipi?

  1. Ya tatu wingi 
  2. Ya pili wingi
  3.  Yapili umoja
  4. Ya tatu umoja 
  5. Ya kwanza wingi.

12.      ”Utundu wake ulimfanya ajulikane shuleni.” Neno "Utundu” limetumika kama aina gani

neno? 

  1. Kivumishi  
  2.  Nomino
  3.  Kiwakilishi
  4.  Kitenzi  
  5. Kielezi.

13.      "Mwanamuziki hodari aliimba nyimbo vizuri.” Kielezi katika sentensi hii ni kipi? ........

  1. Hodari 
  2.  Aliimba 
  3. Mwanamuziki
  4. Nyimbo  
  5. Vizuri

14.      "Mgeni aliondoka alikofikia.............kuaga.” Kifungu kipi cha maneno kinachokamilishE sentensi hiyo kwa usahihi?

  1. licha ya 
  2. pasi ya 
  3. bila kwa 
  4.  bila ya   
  5.  bila na

15. "Shuleni kwetu kuna upungufuwa . ....Ni neno lipi hukamilisha tungo hiyo kwa usahihi?

  1.  thamani 
  2. thamini 
  3. dhamini
  4. zamani 
  5. samani

16. "Mtoto ametengeneza toroli Ia mti." Wingi wa sentensi hii ni upi?

  1.  Watoto wametengeneza toroli za miti
  2.  Watoto wametengeneza matoroli ya mti
  3.  Watoto ametengeneza matoroli ya miti
  4.  Watoto wametengeneza toroli za mti
  5.  Watoto wametengeneza matoroli ya miti

17. "Muda mfupi atakuwa anaingia uwanjani." Sentensi hii ipo katika wakati gani?

  1.  Uliopo
  2.  Uliopita
  3.  Wa mazoea
  4.  Ujao
  5.  Timilifu

18. Ni neno lipi kati ya haya yafuatayo halilandani na mengine?

  1. Fikiria
  2. Dodosa
  3. Uliza
  4. Hoji
  5. Saili

19. Tegua kitendawili kisemacho, " Atembeapo kila mara huringa hata kama kuna adui.”

  1.  Bata 
  2. Konokono 
  3.  Kobe
  4.  Kanga 
  5.  Kinyonga

20. "Siku hizi siri za mafisadi zimeanikwa juani.” Usemi "kuanikwa juani” una maana ipi kati ya hizi zifuatazo?

  1. Kuelezwa waziwazi
  2. Kusemwa hadharani
  3. Kusemwa nje ya kikao
  4. Kuelezwa hadharani
  5. Kusemwa jukwaani

MATUMIZI YA LUGHA

SEHEMU B.

21. Badilisha sentensi zifuatazo kuwa katika wakati timilifu.

  1. Wanafunzi wanapiga picha za ukumbusho
  2. Mboni anawasimulia wenzake ndoto alioiota
  3. Baba aliniambia nizime taa
  4. Ninasoma kitabu cha hadith
  5. Mama anatayarisha kifunguakinywa

25. oanisha nahau na maana zake

Nahau 

Maana

  1. Kalia kitako
  2. Shika tama
  3. Shingo upande
  4. Tia moyp
  5. Sina hali
  1. Sikitika
  2. Sijiwezi
  3. Sengenya
  4. Kutokuridhika
  5. Kalia kiti
  6. Kumpa mtu matumaini

SEHEMU C.

30. Andika NDIYO au HAPANA

  1. Hadithi ni masimulizi ya kubuni……… …
  2. Hadithi huburudisha na huelimisha…… …….
  3. Ukiandika hadithi sio lazima kuweka alama za uandishi………… ….
  4. Hadithi inaweza kusomwa au kusimuliwa……… ….
  5. Hadithi huwekwa kichwa cha habari………… …………..

35. Tengua vitendawili vifuatavyo

  1. Kuku wangu katagia mibani………… ……………..
  2. Watoto wa tajiri wangua hulala na kutembea uchi… ……….
  3. Mama hachoki kunibeba… …………..
  4. Shamba langu ni kubwa lakini mazao ni machache mno……… ………
  5. Wana wa mfalme ni wepesi sana kujificha……… ……………..

SEHEMU D.

SOMA KIFUNGU KIFUATACHO KISHA JIBU MASWALI

Matunda kama yalivyo mazao mengine ya kilimo yanatokana na mimea mbalimbali. Kwa mfano fenesi ni tunda litokanalo na mfenesi na chungwa hutokana na mchungwa. Maembe, mapapai, mananasi na mapera ni matunda matamu. Ubuyu, ukwaju na limau ni matunda machachu. Hata hivyo, karibu matunda mengi huwa machachu yakiwa mabichi, yakiiva huwa matamu.

Miaka ya hivi karibuni watu wengi wamepanda mimea ya matunda kwenye maeneo ya nyumba zao, hivyo kujipatia matunda kwa njia rahisi. Baadhi ya watu wanaoishi katika mikoa kama vile Tanga na Morogoro wamelima mashamba ya matunda na wameshaona faida ya kilimo hicho na kupanua mashamba yao. Licha ya watu hao kujipatia chakula bora, wameuza na kuwa na pato kubwa.

Matunda yana umuhimu mkubwa sana katika miili yetu. Matunda tunayokula yanaikinga miili yetu isipatwe na maradhi. Pia matunda yanaongeza damu mwilini, husaidia kuponyesha vidonda haraka na macho kuona vizuri katika mwanga hafifu. Watu wasiokula matunda hupata udhaifu wa fizi ambao husababisha fizi kutoa damu.

Aidha matunda ni kiburudisho wakati wa joto. Watu wengi wamekuwa wakisindika matunda ili kupata juisi kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na biashara.

MASWALI

41.      Kichwa cha habari hii kinachofaa zaidi ni kipi?

  1. Matunda kwa afya
  2. Umuhimu wa matunda
  3.  Matunda chanzo cha pato 
  4.  Matunda na ulinzi wa mwili 
  5. Matunda hujenga mwili.

42.      "Watu wanaokula matunda huepuka magonjwa mengi,” ni methali ipi inaendana na kauli hii?

  1. Heri kufa macho kuliko kufa moyo 
  2. Usiache mbachao kwa msala upitao 
  3.  Kinga ni bora kuliko tiba.
  4.  Lisemwalo lipo na kama halipo laja. 
  5.  Mwenye kovu usidhani kapoa.

43.      Maji ya matunda yaliyokamuliwa huitwaje? .

  1. Mvinyo
  2. Juisi
  3. Jusi
  4. Rozera
  5. Zabibu

44."Matunda yaliyoiva” ina maana sawa na ipi kati ya zifuatazo? ........

  1.            yenye ukakasi
  2.             machachu
  3.             matamu
  4.            mabichi
  5.             mabivu

45."Kilimo cha matunda kimekuwa cha faida kubwa kwao.” Methali ipi ambayo inaendana na maelezo hayo?

  1. Jembe halimtupi mtu
  2. Mla ni mla leo, mla jana kala nini?
  3. Jisaidie Mungu Akusaidie
  4. Mchumia juani hulia kivulini
  5. Kula nanasi kwahitaji nafasi

46. Ni kwanini wakulima wa matunda hupanua mashamba yao? 

  1. Kupata chakula  
  2. Kupata kiburudisho
  3. Kuongeza pato D. 
  4. Kupata sifa 
  5.  Kupata mikopo

47.      Matunda ya ubuyu na ukwaju yakiwa yameiva huwa na ladha gani? 

  1. Chumvi  
  2. Uchungu 
  3. Ukakasi 
  4.  Ukali 
  5. Uchachu

48.      Kazi kubwa ya matunda mwilini ni ipi? 

  1. Kuponyesha macho 
  2. Kuburudisha
  3.  Kujenga mwili 
  4.  Kuponyesha vidonda
  5.  Kulinda mwilli

49.      "Kusindika matunda” ina maana sawa na kifungu kipi kati ya vifuatavyo? 

  1. Kusaga na kukamua matunda
  2. Kukamua matunda na kuyahifadhi
  3. Kukamua na kuchuja matunda
  4.   Kuyasaga matunda yaliyoiva
  5. Kuyaivisha matunda na kuyasaga

50.      Umepata funzo gani kutokana na kifungu hiki cha habari?

  1. Matunda hukuza akili. 
  2.  Matunda huongeza unene.
  3.  Matunda hukuza akili na mwili.
  4. Matunda hulinda mwili na huongeza damu.
  5.  Matunda hujenga mwili na huongeza joto.

LEARNINGHUBTZ.CO.TZKISWAHILI STANDARD SIX EXAM SERIES 3

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256