FORM FOUR KISWAHILI NECTA 2017

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL

CERTIFICATE OF SECONDARY EDUCATION EXAMINATION

021             KISWAHILI

(Kwa watahiniwa Walioko na Wasiokuwa Shuleni)

Muda: Saa 3:00                                      Jumanne, 31 Oktoba 2017 mchana

Maelekezo

  1.  Karatasi hii ina sehemu A, B, C, D na E zenye jumla ya maswali kumi na tano (15).
  2. Jibu maswali yote katika sehemu A, B na D, swali moja (1)      kutoka sehemu C na maswali    matatu (3) kutoka sehemu E. Swali la 15 ni lazima.
  3. Zingatia maagizo ya kila sehemu na ya kila swali.
  4. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa haziruhusiwi katika chumba cha mtihani.
  5. Andika Namba yako ya Mtihani katika kila ukurasa wa kijitabu chako cha kujibia.

SEHEMU A (Alama 10) UFAHAMU

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1.    Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata.

Mipango ya elimu katika nchi mbalimbali duniani siku zote inahitilafiana, kimuundo na elimu itolewayo. Mipango hiyo huhitilafiana kwa sababu nchi zenyewe zinazotoa elimu huhitalifiana, kwa sababu elimu yoyote iwe ya darasani au si ya darasani, ina shababa yake. Shabaha yenyewe ni kurithishana maarifa na mila za taifa kutoka kizazi kimoja hadi kizazi kingine na kuwaandaa vijana wawe tayari kuchukua nafasi zao katika kulitumikia na kuliendeleza taifa. Hivi ndivyo ilivyo katika nchi zote yaani nchi za kikabaila za Magharibi, nchi za kikomunist za Mashariki na hata zilivyokuwa nchi za kiafrika kabla ya ukoloni.

Kwa hiyo, sio kweli kusema kwamba kabla ya ukoloni waafirka hawakuwa na elimu, eti kwa sababu tu hawakuwa na shule, na kwamba makabila machache yalitoa mafunzo kwa muda mfupi tu kambini. Watoto na vijana walijifunza kwa kuishi na kutenda. Nyumbani au shambani walijifunza ufundi wa kazi zilizopaswa kufanywa, pamoja na tabia wanayopaswa kuwa nayo watu wa jamii ile. Vile vile walifijunza aina za majani na mizizi ya miti ya porini, na kazi zake; walijifunza namna ya kushughulikia mavuno na jinsi ya kuangalia mifungo. Haya yote waliyafanya kwa kushirikiana na wale waliowazidi umri au wakubwa kuliko wao.

HIvyo jamii zilijifunza historia za makabila yao, na uhusiano baina ya kabila moja na makabila mengine, uhusiano baina ya makabila yao na mizimu kwa kusikiliza tu hadithi zilizokuwa zikitolewa na wazee. Kwa njia hii na kwa desturi za kushirikiana walizofunzwa vijana, tamaduni za nchi ziliendelezwa. Kwa hiyo elimu waliyopata haikuwa y kukosekana kwa madarasa hakumaanishi kwamba hakukuwako elimu, wala hakukupunguza umuhimu wa elimu katika Taifa. Kwa msingi hiyo inawezekana kabisa kwamba elimu aliyokuwa akiipata kijana wa enzi zile ilikuwa elimu inayomfaa kuishi katika jamii yake.

Huko Ulaya elimu ya darasani ilianza siku nyingi. Lengo la elimu hiyo ya Ulaya ilikuwa sawa na ile iliyotolewa kwa mtindo wa asili wa Kiafrika, yaani, kwa kuishi na kutenda. Madhumuni makubwa yalikuwa ni kuimarisha mila zilizokuwa zikitumika katika nchi, na kuwanadaa awatoto na vijana kutimiza wajibu wao katika nchi hiyo. Na hivyo ndivyo ilivyo katika nchi za kikomunisti siku hizi. mafunzo yanayotolewa ni tofauti na yale yanayotolewa katika nchi za Magharibi, lakini lengo likiwa ni moja; kuwaandaa vijana kuishi katika taifa na kulitumikia taifa hilo, na kuendeleza busara, ujuzi na mila za taifa katika kizazi kijacho. Mahali popote ambapo elimu inashindwa kutimiza malengo hayo, basi maendeleo ya nchi hiyo yatalegalega, vinginevyo kutatokeo malalamiko watu watakapogundua kwamba elimu yao imewaandalia kuishi maisha ambayo kwa kweli hayapo.

 Maswali

  1. Eleza sababu mbili zinazosababisha nchi mbali mbali kuhitilafiana katika muundo wake wa elimu.
  2. View Ans


  3.  (i)      Fafanua namna jamii za kiafrika zilivyokuwa zinatoa elimu kwa watu wake.View Ans


     (ii)    Ni nami waliohusika kutoa elimu katika jamii za kiafrika?

    View Ans


  4. Elimu iliyotolewa katika jamii za kiafrika na ile iliyotolewa huko Ulaya zilikuwa na malengo gani?
  5. View Ans


  6. Andika kichwa cha habari kinachofaa kwa habari uliyosoma.
  7. View Ans


2. Fupisha habari uliyosoma kwa maneno yasipungua mia moja (100) na yasiyozidi mia moja na arobaini (140).
View Ans



3. Katika kila sentensi uliyopewa, orodhesha vishazi huru katika Safu A na vishazi tegemezi katika safu B.

3. Katika kila sentensi uliyopewa, orodhesha vishazi huru katika Safu A na vishazi tegemezi katika safu B.
(a)       Ngoma hailii vizuri kwa kuwa imepasuka.
(b)       Watoto walioandikishwa watakuja kesho.
(c)       Kiongozi atakayefunga mkutano amepelekewa taarifa.
(d)       Mtawatambua walio wasikivu.
(e)       Kitabu ulichopewa kina kurasa nyingi.
View Ans



4.   (a) Eleza maana ya kielezi kwa kutoa mfano wa sentensi moja.View Ans



(b) Kwa kila tungo uliyopewa pigia mstari kielezi na kisha taja ni cha aina gani.
(i) Darasani kuna utulivu mkubwa 
(ii) Wanafunzi wanaimba kimasihara.
(iii)  Mwalimu amerudi tena.
(iv)  Nitaondoka wiki inayokuja.
View Ans



5.  Toa maana tano tofauti za neno “kibao” kisha tunga sentensi moja kwa kila maana uliyotoa.
View Ans



6. Moja ya faida ya misimu ni kuhifadhi historia ya jamii. Toa mfano mmoja wa misimu zagao iliyovuma Tanzania katika vipindi vifuatavyo:
(a) Muda mfupi baada ya kupata uhuru.
(b)  Miaka ya Azimio la Arusha.
(c)  Njaa ya mwaka 1974/1975.
(d)  Miaka ya vita vya Kagera.
(e)   Kipindi cha hali ngumu ya maisha baada ya vita vya Kagera.
View Ans



7.   (a) Eleza maana ya kiarifu.View Ans



      (b) Kwa kutumia mifano, taja miundo minne ya kiarifu.
View Ans



SEHEMU C (Alama 10) UANDISHI
Jibu swali moja (1) kutoka sehemu hii.

8.Andika barua kwa rafiki yako kuhusu mipango yako ya baadaye utakapoaliza Kidato cha Nne. Jina la rifiki yako liwe Dito Jito wa S.L.P 300 Longido na jina lako liwe Kijito Bahari wa Shule ya Sekondari Mtaweza, S.L.P 200 Dar-es-Salaam.
View Ans



9.   Andika insha ya hoja isiyopungua maneno mia mbili na hamsini (250) na isiyozidi maneno mia tatu (300) kuhusu ‘Madhara ya Madawa ya Kulevya nchini Tanzania’.View Ans



SEHEMU D (Alama 10) MAENDELEO YA KISWAHILI
Jibu swali la kumi (10)

10. “Lugha ya Kiswahili imetokana na lahaja za Kibantu.” Thibitisha kauli hii kwa kutoa hoja mbili kuelezea chanzo cha lahaja na hoja tatu kuhusu matumizi ya lahaja katika Kiswahili sanifu.
View Ans



SEHEMU E (Alama 45) FASIHI KWA UJUMLA
Jibu maswali matatu (3) kutoka katika sehemu hii. Swali la 15 ni la lazima.

ORODHA YA VITABU

USHAIRI
Wasakatonge                                              - M.S. Khatibu (DUP)
Malenga Wapya                                         - TAKILUKI (DUP)
Mashairi ya Chekacheka                          - T.A. Mvungi (EP & D.LTD)

RIWAYA
Takadini                                                       - Ben J. Hanson (MBS)
Watoto wa Maman’tilie                              - E. Mbogo (H.P)
Joka la Mdimu                                             - A.J. Safari (H.P)

TAMTHILIYA
Orodha                                                        - Steve Reynolds (MA)
          Ngoswe Penzi Kitovu cha Uzembe              - E. Semzaba (ESC)
Kilio Chetu                                         - Medical Aid Foundation (TPH)

11.Fasihi simulizi ikihifadhiwa katika maandishi hupoteza uhai na uhalisia wake. Fafanua changamoto nne zinazoweza kujitokeza kwa kuhifadhi fasihi simulizi katika maandishi.
View Ans




12.“Msanii ni kinda la jamii husika hivyo anayoandika huihusu jamii hiyo.” Jadili kauli hii kwa kutumia hoja tatu kutoka katika kila diwani kati ya diwani mbili ulizosoma.
View Ans



13. “Elimu ni ufunguo wa maisha.” Fafanua kauli hii kwa kutoa hoja tatu kwa kila kitabu kati ya vitabu viwili vya riwaya vilivyoorodheshwa.
View Ans



14. “Wahusika katika kazi za fasihi ni mfano wa kuigwa na jamii kwa tabia na matendo yao.” Thibitisha kauli hii kwa kutumia hoja tatu kwa kila mhusika kutoka katika tamthiliya mbili ulizosoma.
View Ans



15.Tunga shairi la kimapokeo lenye beti nne kuhusu “Rafiki yako anayechamia shule nyingine.”

View Ans


Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256