THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL
CERTIFICATE OF SECONDARY EDUCATION EXAMINATION
021 KISWAHILI
(Kwa watahiniwa Walioko na Wasiokuwa Shuleni)
Muda: Saa 3:00 Jumanne, 31 Oktoba 2017 mchana
Maelekezo
SEHEMU A (Alama 10) UFAHAMU
Jibu maswali yote katika sehemu hii.
1. Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata.
Mipango ya elimu katika nchi mbalimbali duniani siku zote inahitilafiana, kimuundo na elimu itolewayo. Mipango hiyo huhitilafiana kwa sababu nchi zenyewe zinazotoa elimu huhitalifiana, kwa sababu elimu yoyote iwe ya darasani au si ya darasani, ina shababa yake. Shabaha yenyewe ni kurithishana maarifa na mila za taifa kutoka kizazi kimoja hadi kizazi kingine na kuwaandaa vijana wawe tayari kuchukua nafasi zao katika kulitumikia na kuliendeleza taifa. Hivi ndivyo ilivyo katika nchi zote yaani nchi za kikabaila za Magharibi, nchi za kikomunist za Mashariki na hata zilivyokuwa nchi za kiafrika kabla ya ukoloni.
Kwa hiyo, sio kweli kusema kwamba kabla ya ukoloni waafirka hawakuwa na elimu, eti kwa sababu tu hawakuwa na shule, na kwamba makabila machache yalitoa mafunzo kwa muda mfupi tu kambini. Watoto na vijana walijifunza kwa kuishi na kutenda. Nyumbani au shambani walijifunza ufundi wa kazi zilizopaswa kufanywa, pamoja na tabia wanayopaswa kuwa nayo watu wa jamii ile. Vile vile walifijunza aina za majani na mizizi ya miti ya porini, na kazi zake; walijifunza namna ya kushughulikia mavuno na jinsi ya kuangalia mifungo. Haya yote waliyafanya kwa kushirikiana na wale waliowazidi umri au wakubwa kuliko wao.
HIvyo jamii zilijifunza historia za makabila yao, na uhusiano baina ya kabila moja na makabila mengine, uhusiano baina ya makabila yao na mizimu kwa kusikiliza tu hadithi zilizokuwa zikitolewa na wazee. Kwa njia hii na kwa desturi za kushirikiana walizofunzwa vijana, tamaduni za nchi ziliendelezwa. Kwa hiyo elimu waliyopata haikuwa y kukosekana kwa madarasa hakumaanishi kwamba hakukuwako elimu, wala hakukupunguza umuhimu wa elimu katika Taifa. Kwa msingi hiyo inawezekana kabisa kwamba elimu aliyokuwa akiipata kijana wa enzi zile ilikuwa elimu inayomfaa kuishi katika jamii yake.
Huko Ulaya elimu ya darasani ilianza siku nyingi. Lengo la elimu hiyo ya Ulaya ilikuwa sawa na ile iliyotolewa kwa mtindo wa asili wa Kiafrika, yaani, kwa kuishi na kutenda. Madhumuni makubwa yalikuwa ni kuimarisha mila zilizokuwa zikitumika katika nchi, na kuwanadaa awatoto na vijana kutimiza wajibu wao katika nchi hiyo. Na hivyo ndivyo ilivyo katika nchi za kikomunisti siku hizi. mafunzo yanayotolewa ni tofauti na yale yanayotolewa katika nchi za Magharibi, lakini lengo likiwa ni moja; kuwaandaa vijana kuishi katika taifa na kulitumikia taifa hilo, na kuendeleza busara, ujuzi na mila za taifa katika kizazi kijacho. Mahali popote ambapo elimu inashindwa kutimiza malengo hayo, basi maendeleo ya nchi hiyo yatalegalega, vinginevyo kutatokeo malalamiko watu watakapogundua kwamba elimu yao imewaandalia kuishi maisha ambayo kwa kweli hayapo.
Maswali
(ii) Ni nami waliohusika kutoa elimu katika jamii za kiafrika?
View AnsORODHA YA VITABU
USHAIRI
Wasakatonge - M.S. Khatibu (DUP)
Malenga Wapya - TAKILUKI (DUP)
Mashairi ya Chekacheka - T.A. Mvungi (EP & D.LTD)
RIWAYA
Takadini - Ben J. Hanson (MBS)
Watoto wa Maman’tilie - E. Mbogo (H.P)
Joka la Mdimu - A.J. Safari (H.P)
TAMTHILIYA
Orodha - Steve Reynolds (MA)
Ngoswe Penzi Kitovu cha Uzembe - E. Semzaba (ESC)
Kilio Chetu - Medical Aid Foundation (TPH)
11.Fasihi simulizi ikihifadhiwa katika maandishi hupoteza uhai na uhalisia wake. Fafanua changamoto nne zinazoweza kujitokeza kwa kuhifadhi fasihi simulizi katika maandishi.
View Ans
12.“Msanii ni kinda la jamii husika hivyo anayoandika huihusu jamii hiyo.” Jadili kauli hii kwa kutumia hoja tatu kutoka katika kila diwani kati ya diwani mbili ulizosoma.
View Ans
13. “Elimu ni ufunguo wa maisha.” Fafanua kauli hii kwa kutoa hoja tatu kwa kila kitabu kati ya vitabu viwili vya riwaya vilivyoorodheshwa.
View Ans
14. “Wahusika katika kazi za fasihi ni mfano wa kuigwa na jamii kwa tabia na matendo yao.” Thibitisha kauli hii kwa kutumia hoja tatu kwa kila mhusika kutoka katika tamthiliya mbili ulizosoma.
View Ans
15.Tunga shairi la kimapokeo lenye beti nne kuhusu “Rafiki yako anayechamia shule nyingine.”