JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI
060 HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI
(MKONDO WA AMALI)
(Kwa wanafunzi Walioko na Wasiokuwa Shuleni)
Muda: Saa 2:30 Mwaka: 2025
Maelekezo
Upimaji huu una sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi (10).
Jibu maswali yote kwenye nafasi ulizopewa.
Sehemu A ina alama kumi na tano (15), sehemu B sabini (70) na sehemu C ina alama kumi na tano (15).
Andika majibu yote kwa kutumia kalamu yenye wino wa bluu au mweusi.
Vifaa vyote vya mawasiliano na vitu vingine visivyonuhusiwa havitakiwi katika chumba cha upimaji.
Andika Namba yako ya Upimaji katika kila ukurasa sehemu ya juu upande wa kulia.
KWA MATUMIZI YA MPIMAJI TU
NAMBA YA SWALI
ALAMA
SAHIHI YA MPIMAJI
1.
2.
3.
4.
5.
6.
7.
8.
9.
10.
JUMLA
SAHIHI YA MHAKIKI
SEHEMU A (Alama 15)
Jibu maswali yote katika sehemu hii.
1. Katika kipengele (i) – (x), chagua jibu sahihi kutoka kwenye machaguo uliyopewa na kuandika herufi yake katika kisanduku ulichopewa.
(i) Wakati wa somo la Historia ya Tanzania na Maadili mwalimu aliwaonesha wanafunzi picha za majengo ya kale na sanaa za jadi. Vitu hivyo hutambulika kama:
maeneo muhimu kwa ajili ya utalii.
historia na utambulisho.
urithi wa kihistoria na kiutamaduni.
visaidizi vya kuelewa historia yetu.
Choose Answer :
(ii) Kabla ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya mwaka 1964, Zanzibar ilikuwa imepata uhuru uliojulikana kama “Uhuru wa bendera”. Uhuru huo ulipatikana mwaka gani?
1957
1963
1961
1962
Choose Answer :
(iii) Serikali ya Tanganyika iliongozwa na kiongozi gani kabla ya kuwa Jamhuri mwaka 1962?
Gavana Mkuu
Waziri Mkuu
Rais
Malkia
Choose Answer :
(iv) Ni ipi kati ya orodha zifuatazo inabainisha nguzo ya kujenga maadili katika mfumo wa elimu ya jadi?
Mila na desturi za jamii, ujuzi wa kazi, lugha, jando na unyago
Jando na unyago, mavazi na mafunzo ya kusaidia vijana
Vyakula, mila na desturi, ujuzi wa kazi za jamii na umoja
Mila na desturi za jamii, lugha, muziki na vyakula vya jamii
Choose Answer :
(v) Ni kwa namna gani unaweza kumaliza mgogoro kati ya wanafunzi wawili wanaopigana darasani kwa kutumia maarifa ya mifumo ya haki ya jadi?
Kumuadhibu aliyesababisha ugomvi
Kuwatenganisha wasichdelee kupigana
Kuwapatanisha na kumaliza ugomvi kati yao
Kuwashitaki kwa mujibu wa sheria za shule
Choose Answer :
(vi) Wanafunzi wa shule yako walipata fursa ya kutembelea mbuga za wanyama za Serengeti na Ngorongoro. Yapi kati ya maelezo yafuatayo yanatoa maana sahihi ya shughuli hiyo?
Kusafiri na kukaa nje ya shule kwa muda
Kwenda nje ya shule kwa ajili ya burudani
Kutoka shuleni kwenda mbugani kwa wanyama
Kutoka nje ya shule yako kwa lengo la kujifunza
Choose Answer :
(vii) Ni mbinu ipi ilitumiwa na wakoloni kudhoofisha matumizi ya tiba za jadi?
Kuziondoa kwenye maala wa shule zao
Kutowazajiri wakunga na matabibu wa jadi
Kutowapa mafunzo ya kisasa waganga wa jadi
Kuzihusianisha na uchawi na ushirikina
Choose Answer :
(viii) Maelezo yapi yanathibitisha ukweli kuhusu jamii zilizoamua kuungana na wavamizi wa kikoloni ili kuweza kuwashinda maadui zao wa muda mrefu?
Zilitawaliwa kirahisi na wakoloni
Ziliimarika kisiasa na kiuongozi
Zilifanikiwa kiuchumi na kiusalama
Zilipata misaada ya silaha za kivita
Choose Answer :
(ix) Ni kwa namna gani udhibiti wa rasilimali kwa watu binafsi na vikundi katika mfumo wa kikabaila ulikuza siasa za jamii husika?
Ulisababisha kufutwa kwa mfumo wa koo
Ulipunguza vitendo vya rushwa katika jamii
Ulichangia kuendesha uchaguzi huru na haki
Uliwapa watu nguvu na ushawishi mkubwa katika jamii
Choose Answer :
(x) Ni kwa namna gani matumizi ya lugha ya Kiswahili katika utengenezaji wa filamu za Kitanzania yanaweza kusaidia kukuza uchumi na ushirikiano wa kimataifa?
Kufikia watazamaji wengi zaidi Afrika Mashariki
Kuifanya iwe lugha ya kufundishia ili kuongeza wataalamu
Kurahisisha mawasiliano katika biashara na sanaa
Kuzuia matumizi ya lugha nyingine nchini
Choose Answer :
2. Oanisha maelezo kuhusu uhusika wa viongozi wa makabila ya jamii za Kitanzania katika harakati za kuupinga uvamizi wa kikoloni katika Orodha A na majina ya viongozi husika katika Orodha B kwa kuandika herufi ya jibu sahihi katika jedwali ulilopewa.
Orodha A
Orodha B
(i) Kiongozi wa kabila la Wahehe aliyepambana na Wajerumani.
(ii) Kiongozi aliyeungana na Wajerumani kupigana dhidi ya Wahehe.
(iii) Kiongozi aliyeshirikiana na Wajerumani kuuangusha utawala wa Wakibosho.
(iv) Kiongozi wa Wanyamwezi aliyepinga kuenea kwa ukoloni wa Kijerumani Tanganyika.
(v) Kiongozi wa Wayao aliyekataa kusaini mikataba ya kilaghai ya Wajerumani.
5. Kwa kutumia hoja tano, eleza jinsi maarifa ya mifumo ya kisiasa na kiuchumi kabla ya ukoloni yanavyoweza kutumika kuimarisha uwajibikaji katika jamii za sasa.