EDK FORM TWO REGIONAL EXAMS (MOCK, PRE-NATIONAL, etc.)

Namba ya upimaji ya Mwanafunzi. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

Bismillaahir rahmaanir rahiim 

OFISI YA RAIS OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUFIJI

image

 MTIHANI WA UMAHIRI KIDATO CHA PILI

015 ELIMU YA DINI YA KIISLAMU

 MUDA: SAA 2:30 MWAKA: 2025

 Maelekezo

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi (10).
  2. Jibu maswali yote kwenye nafasi ullizopewa
  3. Sehemu A na C zina alama kumi na tano (15) kila moja na sehemu B ina alam,a sabini (70)
  4. Zingatia maelekezo ya kila sehemu na ya kila swali
  5. Majibu yote yaandikwe kwa kalamu yenye wino wa bluu au mweusi
  6. Vifaa vyote vya mawasiliano visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba cha upimaji
  7. Andinka Namba yako ya upimaji katika kila ukurasa sehemu ya juu upande wa kulia.

KWA MATUMIZI YA MTAHINI TU

NAMBA YA MASWALI


ALAMA

SAHIHI YA MSAHIHISHAJI
1.

2.

3.

4.

5.

6.

7.

8.

9.

10.

TOTAL

SAHIHI YA MHAKIKI

SEHEMU ‘A’ (Alama 15 %)

Jibu maswali yote katika sehemu hii

1. Katika kipengele (i) – (x) Chagua jibu sahihi kisha andika herufi yake katika sehemu iliyowazi.

(i) Je utawezaje kumtambua muislamu aliyeelimika?

  1. Kwa kuwa na fani nyingi za kielimu
  2. Kwa kuwa elimu nyingi za fiq-hi
  3. Kwa kuwa na ufanisi katika utendaji
  4. Kwa kuwa na ujuzi mwingi wa kihistoria.

(ii) Wana wa chuoni wanatuambia Tawhid maana yake ni kumpwekesha Allh (sw). ni Tawhid ipi inaohusika na kumpwekesha Allah katika uungu wake?

  1. Tawhidul-asmaa was sifaat.
  2. Tawhidur-rubuiah 
  3. Tawhidul-uluhiyah
  4. Tawhidul-ibada.

(iii) Muandaaji wa Sanda anapaswa kuzingatia mambo gani katika uandaaji wa Sanda ya Mwanamke?

  1. Mapande matatu
  2. Uzito na aina ya kitambaa
  3. Kuwa na mapande matano
  4. Cheo cha aliyefariki

(iv) Pamoja na kutoonekana Allah wala kudirikika katika milango mikuu ya fahamu ila huwasiliana na waja wake kupitia njia zifuatazo:

  1. Ilham, maandishi, ndoto za kweli, na qur-an 
  2. Ilham, maandishi, ndoto za kweli na hadithi.
  3. Ilham, maandishi, ndoto za kweli na sunnah
  4. Ilham, maandishi, ndoto za kweli na malaika.

(v) Fafanua sunnah katika elimu ya hadithi lina maana gani? 

  1. Thawabu za ziada.
  2. Mwenendo au millah ya Mtume (saw)
  3. Swala isiyo ya faradhi.
  4. Jambo la khiyari kulifanya.

(vi) Jozi ipi klati yua zifuatazo inawakilisha nguzo za funga?

  1. Kusaidia wagonjwa na yatima
  2. Kutia nia na kujizuia na vifunguzi
  3. Kutokula na kunywa
  4. Kutotenda maovu na machafu

(vii) Kwa mujibu wa uislamu kuna aina kuu mbili za Dini “dini ya Allah na Dini za watu, fafanua aina tatu za Dini za watu.

  1. Utawa, ushirikina na ukristo.
  2. Ukristo, utawa na uyahuni.
  3. Uislamu, uyahudi na ukafiri.
  4. Utawa, ushirikina na ukafiri.

(viii) Changanua mkanganyiko ufuatao;

  1. Qur-an ina juzuu 30, sura 114 na ina aya 6326.
  2. Qur-an ina juzuu 30, sura 114 na ina aya 6236.
  3. Qur-an ina juzuu 30, sura 114 na ina aya 6336.
  4. Qur-an ina juzuu 30, sura 114 na ina aya 6366.

(ix) Allah (sw) alishawahi kuangamiza baadhi ya familia za mitume wake, ni mtume gani aliyeangamiziwa mke na mtoto wake.

  1. Nabii Mussa (as)
  2. Nabii Luti (as)
  3. Nabii Nuhu (as)
  4. Nabii Shuaibu (as)

(x) Mambo ya lazima kufanyiwa maiti wa kiislam bainisha ni katika faradhi gani?

  1. Faradhi a`ini.
  2. Faradhi mustahabu.
  3. Faradhi mutlaq.
  4. Faradhi kifaya.

2. Oanisha maneno kutoka orodha “B” na sentensi kutoka orodha “A” kisha jaza herufi yake kwenye jedwali hapo chini.

A

B

(i) Huswaliwa qabla na baada ya swala za faradhi.

(ii) Huswaliwa kwaajili ya kuomba mvua.

(iii) Huswaliwa muda wowote mara tu uingiapo msikitini.

(iv) Huswaliwa pindi lipatwapo jua au mwezi.

(v) Huswaliwa rakaa mbilimbili hadi nane usiku wa manane.

  1. At-tahajud
  2. Swalatul-khusufu au Al- kusufu
  3. At-tawba
  4. Tahiyatul-masjidi
  5. Al-istisqaai
  6. Istikhara
  7. Qabliyyah au Baadiyyah.

i

I

iii

iv

V





.

SEHEMU “B” (ALAMA 70)

Jibu maswali yote kwa ufupi katika sehemu hii

3. Fafanua njia kuu tano zinazomuwezesha mwanadamu kumtambua Mola wake

4. Makafiri hawaamini kama kuna maisha baada ya kufa. Fafanua hatua tano(5) anazopitia mwanaadamu kuyaendea maisha hayo.

5. a) Waislamu wengi na hata wasiokuwa waislamu(makafiri) hawaelewi maana halisi ya neno dini, wewe ukiwa kama mjuzi katika masuala haya, toa maana yake halisi kwa mitazamo yote miwili.

5 b) Ainisha sababu tatu za kwanini mwanadamu hawezi kusibi bila ya Dini.

6. (a) Waislamu wangi wanadhani kuwa Ibada ni kuswali, kufunga, kutoa zaka na kuhiji, wakati si sahihi. Wewe ukiwa mwana wa zuoni ifafanulie jamii maana yake halisi kilugha na kisheria;

(i) Kilugha

(ii) Kisheria

(b) Kuna mlevi mmoja maeneo ya Tandale alikuwa akiropoka kuwa hakuna lengo lolote la kuumbwa mwanaadamu ulimwenguni na vilivyomo. Wewe kama muislamu unayejitambua hebu fafanua lengo la kuumbwa kila kimoja

7. (a) Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayo katiba ya kuendeshea nchi, na uislamu una sheria zake. Ni ipi misingi inayotumika kuendeshea sheria mbalimbali za kiislamu

(b) Kuna mkanganyiko mkubwa kati ya Sharia na Fiq-hi, toa maelezo yatakayoondoa mkanganyiko huo.

  1. Sharia
  2. Fiq-hi

8. Mtume (saw) na maswahaba wake walitumia njia madhubuti na makini katika kuilinda na kuihifadhi Qur-an, na ndio maana makafiri wanajaribu kuikejeli na kuichafua lakini wanashindwa, toa njia tano (5) zilizotumika kuilinda na kuihifadhi Qur-an.

9. Kuna waislamu wanadai kuwa sunnah hazina umuhimu na nafasi yoyote katika uislamu, kwa kutumia nukta tano (5), fafanua umuhimu na nafasi yake katika uislamu.

SEHEMU “C” (ALAMA 15)

Jibu swali lifuatalo katika mfumo wa insha.

10. Wanafunzi wa kidato cha kwanza hawana elimu juu ya mambo ambayo wakiyafanya swaumu zao zitakuwa zimeharibika. Wewe kama mjuzi wa somo la Elimu ya Dini ya Kiislamu waelimishe wanafunzi hao juu ya mambo yanayobatilisha funga (Hoja tano)

FORM TWO EDK EXAM SERIES 128  

FORM TWO EDK EXAM SERIES 128  

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256