FORM THREE KISWAHILI EXAMS SERIES

JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAISI, TAWALA ZA MIKOA NA SEREKALI ZA MITAA

MTIHANI WA KISWAHILI KIDATO CHA TATU.

MAELELKEZO

  1.         Mtihani huu una sehemu A,B, na C .
  2.         Jibu maswali yote kutoka A, B na Maswali 2 kutoka C.

 

SEHEMU A.

  1.         Chagua herufi ya jibu sahihi katika vipengele i-x andika herufi ya jibu sahihi katika jedwali.
  1.             Huyu ni mwanafunzi hodari sana. Je neno ni ni aina gani ya neno?
  1.         Kitenzi kishirikishi
  2.          Kiunganishi
  3.         Kitenzi kisaidizi
  4.         Kielezi cha wakati
  1.           Njia ipi ya uhifadhi wa fasihi simulizi inayoweza kupokea mabadiliko kwa haraka kati ya hizi?
  1.         Maandishi
  2.          Vinasa sauti
  3.         Kichwa
  4.         Kanda za video
  1.         Tofauti ndogondogo zinazojitokeza katika lugha moja huitwa....
  1.         Kimtang’ata
  2.          Lugha za kikanda
  3.         Lahaja
  4.         Kiimbo
  1.         Wazo kuu la mtunzi katka faihi huitwa
  1.         Ujumbe
  2.          Dhamira
  3.         Falsafa
  4.         Mtazamo
  1.           .... ni maneneno yasiyo sanifu yanayozuka na kutoweka
  1.         Misimu
  2.          Rejesta
  3.         Misamiati
  4.         Kishazi tegemezi
  1.         Kisawe cha neno masikini ni ...
  1.         Ukwasi
  2.          Ubahili
  3.         Ijima
  4.         Ukata
  1.       Neno pamoja na taarifa zake kwenye kamusi huitwa
  1.         Kidahizo
  2.          Kitomeo
  3.         Msamiati
  4.         Muundo
  1.     Utofauti wa kazi za kifasihi toka muandishi mmoja dhidi ya mwingine husababishwa na
  1.         Mtindo wa kazi
  2.          Dhamira za kazi ya fasihi
  3.         Migogoro ya kazi husika
  4.         Muundo wa kazi ya fasihi
  1.         Moj a ya sifa kuu ya kirai ni:
  1.         Kukaa sehemu yoyote katika sentensi
  2.          Hakina muundo wa kiima na kiarifu
  3.         Hutoa maana kamili
  4.         Huwa na muundo wa kiima na kiarifu
  1.           Neno lipi kati ya maneno haya linaweza kudikeza mtenda au mtendwa wa jambo?
  1.         Kiunganishi
  2.          Kihisishi
  3.         Kuelezi
  4.         kivumishi
  1.         oanisha dhana katika Orodha A Kuchagua herufi ya dhana husika kutoka Orodha B, kisha andika jibu katika jedwali.

ORODHA A

ORODHA B 

(i)     Neno pamoja na taarifa zake zote zilizo ndani ya kamusi  

  1. Utata
  2. Rejesta
  3. Simo
  4. Mofimu
  5. Kitomeo
  6. Kiimbo
  7. Kidahizo
  8. Kiima
  9. mkazo

(ii)   Hali ya neno au senensi kuwa na maana zaidi ya moja

(iii) Ni maneno yasiyo sanifu yaliyoanzishwa na kikundi cha watu wenye utamaduni mmoja 

(iv) Ni neno linaloingizwa katika kamusi ili lifafsanuliwe

(v)   Ni matumizi ya lugha kulingana na muktadha maalumu

(vi) Ni sehemu ya sentensi inayokaliwa na mtenda au mtendwa wa jambo

SEHEMU B

  1.         a) Dhana ya uainishaji wa ngeli za nomino kwa kigezi cha kisintaksia ina umuhimu wa ke katika lugha ya kiswahili. Ta hoja nne zinazoonesha umuhimu huu katika lugha ya kiswahili

b) Taja ngeli husika kutokana na sifa zifuatazo:

  1.      maneno yanayotokana na kunominishwa kwa vitenzi
  2.    nomino ambazo zina kiambishi awali “u” katika Umoja na “ma” katika wingi
  3.  majina ya baadhi ya vitu vinavyopatikana katika jozi na baadhi ya majina ya miti
  4.  majina ambayo hayabadiliki umbo katika Umoja ma wingi
  5.    ngeli inayotaja mahali au sehemu
  1.         Changanua sentensi zifuatazo kwa njia ya jedwali
  1.      yule alikataa mawazo yetu kabisa
  2.    nguo zilizofuliwa zimekauka vizuri
  3.  wanafunzi wa kidato cha kwanza wanachexza mpira wakati wengine wanaimba nyimbo.

 

  1.         Kipindi cha hivi karibuni tumekua tukishuhudia manenom mapya ya kiswahili yakizungumzwa na baadhi ya watanzania kama vile ughaighai, unyama mwingi n.k. wewe kama mwanafunzi wa kidato cha tatu eleza njia zinazotumika kuunda maneno jayo yanayonguka katika jamii.
  2.         Orodhesha misamiati miwili ambayo unadhani imeingia katika ludha ya kiswahili kutokana na :
  1.      Mabadiliko ya sanyansi na teknolojia
  2.    Mabadiliko ya kiuchumi
  3.  Muingiliano wa kiutamaduni
  4.  Mabadiliko ya kisiasa
  5.    Mabadiliko ya tabia ya nchi
  1.         “ Hahuna mgeni aliyekuwa na nia ya kukuza lugha ya kiswahili hapa nchini.” Kwa kutumia mifano tumia kiswahili kuthibitisha usemi huu kwa kutoa hoja tano. Kupitia utawala wa Mjerumani.
  2.         Ezeza maana ya istilahi zifuatazo
  1.             Sarufi
  2.             Kitomeo
  3.             Lugha
  4.             Kielezi

 

SEHEMU C

Jibu maswali mawili kutika sehemu hii

  1.         Lugha ya kiswahili ni lugha iliyokuuwepo kabla ya kuja kwa mwarabu. Kwa kutumi mifano eleza shughuli tano zilizofanywa naozikachangia kukuza na kueneza kiswahili.
  2.    Kiswahili ni kibantu kwa asili yake. Fafanua kwa kutumia ushahidi wa kimsamiatu na kimuundo.
  3.    Methali zinafunza na zinaweza kupotosha jamii zisipotumika kwa ukamilifu. Kwa kutumia methali nne, eleza namna kila moja inaweza kupotosha jamii.

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 167  

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 167  

JAMHURI YA MUNGANO WA TANZANIA

BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA

MTIHANI WA UPIMAJI – KISWAHILI

KIDATO CHA TATU- MARCHI 2024

Muda : Saa 3

Maelekezo 

  1.         Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi na moja (11).
  2.         Jibu maswali yote katika sehemu A na B, na maswali mawili (2) ktutoka sehemu C ambapo swali la tisa (9) ni la lazima.
  3.         Sehemu A ina alama kumi na sita (16), sehemu B alama hamsini na nne (54) na sehemu C ina alama thelathini (30)
  4.         Zingatia maelekezo ya kila sehemu na ya kila swali.
  5.         Vifaa vya mawasiliano na vitu visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba cha mtihani.
  6.         Andika namba ya yako ya mtihani katika kila ukurasa wa kujitabu  chako cha kujibia 

SEHEMU A (ALAMA 16)

  1.         Chagua jibu sahihi katika maswali yafuatayo;
  1.  Mende anapenda kula uchafu . neno Mende lipo katika ngeli ipi;
  1.    Ki-vi
  2.    U –i
  3.    A- wa
  4.    Ku
  5.    Li-ya
  1.  ......................... mna watu wengi
  1.    Aliingia
  2.    Alipoingia
  3.    Alikoingia
  4.    Alivyoingia
  5.    Alimoingia
  1.   Neno papai linaingia katika ngeli ya
  1.    Li-ya
  2.    Yu-a-wa
  3.    Pa- mu- ku
  4.    Ki-vi
  5.    U-i

 

  1.                         “Shangazi yupo shambani mwake “ kifungu hili kipo katika ngeli gani:-
  1.    Pa-mu-ku
  2.    Yu-a-wa
  3.    U-zi
  4.    U-ya
  5.    Li-ya
  1.   Ni ipi sababbu miojawapo ya kutumia kugha kulingana na muktadha?
  1.    Kusuka kwa matukio mbalimbali
  2.    Kuendana na Sayansi na technologia
  3.    Kumudu shughuli inayofanyika
  4.    Kupamba mazungumzo
  5.    Kuwezesha mawasiliano
  1.               Katika neno wanakula mzizi wa neno ni:
  1.    Kul
  2.    Kula
  3.    –l-
  4.    Nak
  5.    Ku
  1.                      Visasili ni mojawapoya vipera vya hadithi ambavyo hueleza kuhusu:
  1.    Matukio ya kihistoria
  2.    Makosa na uovu wa watu
  3.    Kuonya kuhusu maisha
  4.    Asili ya vitu kama vile milima, mito, wanyana n.k
  1.  Neno linaloingizwa katika kamusi kwa wino uliokolezwa, fasili, matamshi na aina ya neno kwa pamoja huitwa
  1.    Kidahizo
  2.    Kitomeo
  3.    Istilahi
  4.    Fasihi
  1.                         Neno lipi kati ya yafuatayo ni mofimu honi?
  1.    Chai
  2.    Kula
  3.    Imba
  4.    Ruka
  5.     Lala
  1.   Katika sababu zifuatazo ni ipi si sahihi kuhusu kamusi?
  1.    Kujifunza lugha ya kigeni
  2.    Kujua maana ya neno
  3.    Kujua tahajia ya neno
  4.    Kusanifisha maneno mapya

 

  1.         Oanisha dhana zlizopo katika Orodha A na zilizopo katika orodha B , kukamilisha mana kamili

ORODHA A

ORODHA B

(i)    Mwanafunzi aliyepewa zawadi jana asimame

  1. Kirai
  2. Kishazi tegemezi
  3. Shamirisho
  4. Kirai kielezi
  5. Chagizo
  6. Sentensi changamano
  7. Kirai nomino
  8. Prediketa

(ii) Huundwa na vitenzi vyenye O-rejeshi

(iii)                       Sehemu ya kiarifu ilyokaliwa na nomino

(iv)                        Neno au mpangilio wa neno wenye neno kuu moja

(v)  “Mwenye duka” ni muundo wa

(vi)                        Sehemu ya kiarifu inayokaliwa na kienzi

 

 

SEHEMU B

ALAMA 54

  1.         (a) Kwa kutumia mifano, fafanua taarifa nne za kisarufi zilizopo katika viambishi awali na vitrnzi vya kiswahili

(b) Nominisha vitenzi vifuatavyo

  1.     Pata
  2.  Jenga
  3.                        Fundisha
  4.                         Panda
  5.   Chuja
  1.         (a) Fafanua njia tatu (3) za uundaji wa misimu kwa kutumia mifano.

(b) Taja misimu minne iliyozuka kipindi cha serikalli ya awamu ya tano

  1.         Katika sentensi zifuatazo, onesha matumizi ya mofimu “ki”
  1.     Ukimwona atakueleza
  2.  Alikua akilia  gari lilipogonga mti
  3.                        Amevaa kifalme
  4.                         Mtoto anakimbia
  5.   Kikombe kimevunjika
  6.                         Amechukua kimoja tuu
  1.         Bainisha O- rejejeshi katika sentensi zifuatazo.
  1.     Mtu anayekunon’goneza aje apa
  2.  Mti ukioanguka umevunja nyumba lakini hakuna watu waliojeruhiwa
  3.                        Panga lililopotea limepatikana
  4.                         Kitabu alichookota ni cha kwangu
  5.   Vitabu vilivyosomwa ni vile vilivyotolewa na waziri wa Elimu
  6.                         Mahali alipolala mbuzi pamevamiwa na siafu
  1.         Andika simu ya maneno kwa mjomba wako kuhusu kuomba pesa ya safari ya kwenda hifadhi ya wanyama Tarangire . Jina lako liwe Mitomingi wa S.L.P. 37, huko Kibaha ,Mkoa wa Dar-es-Salaam . ( maneno tisa 9)
  2.         Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali.

         Ili kuondoa utat wa maneno sanaa na fasihi, inafaa kuyaeleza maneno hayo kwa uwazi zaidi. Sanaa imeelezwa kuwa ni uzuri ulio katika umbo lililosanifiwa. Fasihi ni sehemu ya uzuri huo. Katika fasihi kuna uzuri wa kifasihi, huitwa  fani na jambo lisemwalo huitwa maudhui. Fasihi lazima iwe na sehemu hizi mbili. Ikikosekana moja wapo, kazi haiwi ya kifasihi.

           Mtunzi wa kazi ya fasihi huwa na jambo kusema na namna ya kulisema. Kwa hiyo,ana dhamira na anatumia ufundi wa maneno mbalimbali kufikisha dhamira yake.

           Kazi ya fasihi inaweza kuwa na upungufu kutokana na upotofu wa fani au maudhui. Maudhui yanajengwa na dhamira, ujumbe, maadili, falsafa, na maranyingine suluhisho. Dhamira ya mtunzi ikiwa potofu au haikubaliki katika jamii, inapunguza uzuri wa kazi yake.

 

Maswali 

  1.     Kwa mujibu wa habari hii nini maana ya fasihi
  2.  Eleza tofauti kati ya sanaa na fasihi
  3.                        Mtunzi anaposema kazi ya fasihi inaweza kua na upungufu kutokana na upotofu wa fani na maudhui, ana maana gani?
  4.                         Eleza umuhimu wa sanaa katika fasihi
  5.   Fafanua imuhimu wa  fani na maudhui katika fasihi.

 

SEHEMU E

ALAMA  30

 

Jibu maswali mawili kutoka sehemu hii

 

  1.         “Fasihi ni chombo cha kufundishia maisha”. Jadili ukweli wa kauli hii kwa kutumia hoja sita.
  2.    Fasihi simulizi ndio fasihi ya awali iliyoanza wakati binadamu alipoanza kutumia lugha. Mara kwa mara inapowasilishwa ka hadhira huchukua sifa muhimu kadhaa ambazo si rahisi kuzipata katika fasihi andishi. Thibitisha iweli huu kwa hoja sita.
  3.    (a) Unaelewa nini kuhusu mashairi ya kimapokeo ?

(b) Kwa kutumia mifano kuntu, fafanua vipengele saba vya kuzingatia wakati wa kutunga shairi la kimapokeo.

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 164  

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 164  

OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

JAMUHURI YA MUUNGANO YA TANZANIA

MTIHANI WA MWISHO MWAKA

KIDATO CHA TATU

KISWAHILI NOVEMBA 2023

Muda 2:30

MAELEKEZO

  1. Jibu maswali yote
  2. Mtihani huu una sehemu A. B na C (Jumla ya maswali 9)
  3. Simu za mkononi haziruhusiwi

SEHEMU A (16)

  1. Chagua jibu sahihi katika maswali yafuatayo
  1. Neno lipi kati ya haya ni mofimu huru
  1. Uji
  2. Uzuri
  3. Uchache
  4. Ufa
  5. Upweke
  1. Ni kauli inayotumia maneno ya kawaida lakini hutoa maana tofauti na iliyopo kwenye maneno yale.
  1. Mafumbo
  2. Nahau
  3. Misemo
  4. Semi
  5. Hadithi
  1. Utokeji wa misimu katika jamii hutegemea na
  1. Uchaguzi wa viongozi
  2. Mabadiliko ya Kijamii
  1. Shughuli itendekayo
  2. Utani uliopo miongoni mwa wanajamii
  3. Kutumia na kudumu kwa muda mrefu
  1. Nyenzo kuu za lugha ya Mazungumzo ni
  1. Usimuliaji
  2. Mdomo
  3. Maandishi
  4. Vitendo
  5. Ishara
  1. Kipi kipengele kinachohusu mjengeko wa kazi za fasihi?
  1. Muundo
  2. Wahusika
  3. Mtindo
  4. Mandhari
  5. Lugha
  1. Kikundi cha maneno kinachoonesha jambo lililotendwa na mtenda katika sentensi hujulikanaje?
  1. Kikundi kivumishi
  2. Kikundi kitenzi
  3. Nomino
  4. Chagizo
  5. Shamirisho
  1. ni kauli ipi iliyotumika katika uundaji wa neno “Nitamfitinisha”
  1. Kutendeana
  2. Kutendesha
  3. Kutenda
  4. Kutendea
  5. Kutendewa
  1. Dhima Kuu ya Misima katika lugha ni ipi?
  1. Kuficha jambo kwa wasiohusika
  1. Kuongeza ukali wa maneno
  2. Kupatanisha maneno
  1. Kutambulisha aina za maneno
  2. Kuhimiza shughuli za maendeleo
  1. Ipi ni jozi sahihi ya vipera vya semi?
  1. Soga, nyimbo na nahau
  2. Methal mizungu na vitendawili
  3. Mafumbo, soga, maghani
  4. Misemo, mafumbo na vigano
  5. Mashairi mafumbo na mizungu
  1. Shule zetu zimeweka mikakati kabambe ya kutokomeza daraja la pili ili zibaki na daraja la kwanza pekee. Neno ‘ili’ katika tungo hii ni aina gani ya neno?
  1. Kiunganishi
  2. Kivumishi
  3. Kielezi
  4. Kitenzi
  5. Kihusishi
  1. Oanisha maelezo yaliyo katika Orodha A na dhana husika katika Orodha B. Kisha andika herufi husika katika karatasi ya majibu.

ORODHA A

ORODHA B

  1. Mada, Uhusiano, Malengo na Muktadha
  2. Umeupiga mwingi
  3. Nani Ugali mbuzi choma
  4. Baba Juma amefariki
  5. Hupokea mabadiliko ya papo hapo
  6. Kutumia lugha kulingana na kaida za jamii
  1. Tungo tata
  2. Utumizi wa lugha
  3. Lugha ya mazungumzo
  4. Simo
  5. Rejesta
  6. Humsaidia mzungumzaji kuteua lugha kwa usahihi
  7. Sababu ya utata
  8. Lahaja
  9. Lugha ya maandishi

SEHEMU B (ALAMA 54)

  1. (a)Unaelewa nini dhana ya misimu

(b) Onesha vyanzo viwili vya Msimu

(c) Misimu huweza kuundwa kwa njia tofauti tofauti

  1. Demu
  2. Kumzimikia
  3. Disco
  4. Ferouz ni twiga
  5. Mataputapu
  1. Batuli alitaka kuhifadhi methali na vitendawili kwa njia ya Kichwa tu kwa ajili ya kizazi kijacho. Lakini Kibutu alimkataza asifanye hivyo badala yake atumie njia nyingine
  1. Toa hoja nne (4) kama sababu ya katazo hilo
  2. Taja njia tano (5) sahihi ambazo unahisi kibuyu angemshawishi batuli atumie.
  1. Eleza kinagaubaga tofauti zilizopo kati ya lugha ya mazungumzo na lugha ya maandishi kwa kuzingatia vipengele vifuatavyo.
  1. Uwasilishaji
  2. Uhifadhi
  3. Manadiliko
  1. Lugha ina tabia ya kujiongeza msamiati wake kwa njia kadha wa kadha; kwa kuthibitisha dai hilo, tambulisha njia zilizotumika kuunda maneno yafuatayo.
  1. Kuku
  2. Mpangaji
  3. Kifaurongo
  1. TATAKI
  2. Fedha
  3. Msikwao
  1. Kitivo
  2. Pilipili

ix. Imla, mali, mila, lami

  1. Maendeleo ya Sayansi na Teknologia ni ndumi la kuwili kwa fasihi simulizi. Kwa hoja sita thibitisha ukweli wa kauli hii kwa kutoa hoja mbili.

8. Soma kifungu habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata:

"Ndugu wazazi, kumbe safari yenu inahusu harusi ya Maria ?".Mkuu wa shule aliwauliza wazazi."Ndiyo," wazazi walijibu kwa Pamoja bila aibu."inategemewa kufugwa lini ."Mkuu aliendelea kuhoji. Harusi hii ilikuwa ifanyike wakati Maria anapofika kidato cha nne, Lakini Maria huyu ametufanyia uhuni na vituko visivyoelezeka. Nasi sasa tunachukiwa kijiji kizima na kudharauliwa na kila mtu.Hii imetuudhi sana, tumetungiwa nyimbo na kufanyiwa kila shutuma. Hatuna raha ;hivyo tumeonelea bora tuje kukuomba umfukuze shule ili kiburi kimwishie .Nasi tupo tayari kukulipa kiasi chochote cha fedha ukitimiza haja yetu hii,"Mzee Abdallah alieleza." Muda wote mkuu wa shule alikuwa akimtazama Mzee kwa chati sana .Kisha akauliza swali la kuchochea zaidi: Maria ana kiburi kumbe?"

Mama Maria hakutaka hilo limpite ,hima hima akatoa maelezo yake ."Mama wewe ,Maria usimuone hivi. Maria mwanangu hataki kufuata utamaduni wetu wa kuolewa. Maria ati achague mchumba mwenyewe, ati mahari haiyoni kama ni kitu cha msingi. Kiburi hicho kinatokana na elimu mliyompa.

Mtoto sasa ameharibika .Anafanya apendavyo elimu gani isiyojali adabu.wala utii?" Mama Maria alimaliza huku jasho na machozi yanamtoka".

Hapa mkuu wa shule aliona kwanza awaelimishe kabla hajawatolea kauli ya mwisho.Alikwishatambua kwamba wazazi wa Maria walikuwa wameachwa nyuma na wakati .Kila upya wa mawazo waliuita kiburi.

Maswali

(i)Bainisha dhima nne (04) zilizotokana na habari uliyosoma.

Fupisha habari hiyo kwa maneno yasiyopungua 70 na kuzidi 80.

SEHEMU C: (ALAMA 30)

Jibu maswali mawili katika sehemu hii swali la 11 ni lazima

ORODHA YA VITABU

ORODHA YA VITABU.

USHAIRI.

  • Wasakatonge - M.S. Khatibu (DUP).
  • Malenga wapya -TAKILUKI (DUP)
  • Mashairi ya Chekacheka - T.A.Mvungi(EP&D.LTD)

RIWAYA.

  • Takadini -Ben J.Hanson (MBS)
  • Watoto wa Mama N'tilie - E.Mbogo(HP)
  • Joka la Mdimu - A.J.SaiTari (HP)

TAMTHILIYA

  • Orodha - Steve Reynolds(MA)
  • Ngoswe Penzi Kitovu Cha uzembe - E. Semzaba (ESC)
  • Kilio chetu - Medical Aid Foundation (TPH)
  1. Fasihi ya Kiswahili imemuweka mwanamke katika hadhi tofauti tofauti. Thibitisha Usemi huu kwa kutumia hoja tatu kwa kila riwaya
  2. Lugha ni mhimili katika kazi yoyote ya fasihi. Watunzi hutumia lugha kiufundi ili kufikisha ujumbe kwa jamii husika. Kwa kutumia jazanda au taswira tatu kutoka katika diwani mbili ulizosoma na uonyeshe namna zinavyofikisha ujumbe kwa jamii.
  3. “Ukiona mtu mzima analia ujue kuna jambo au mambo hayapo sawa. Kauli hii inaweza kuwiana na waandishi wa riwaya Juu ya jamii inavyowazunguka, kwa kutoa hoja tatu kutoka kila riwaya katika riwaya mbili ulizosoma, jadili kwa nini wasanii hao hulia?

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 152  

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 152  

OFISI YA RAIS

TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MITIHANI YA KUJIPIMA KWA SEKONDARI 

                           MTIHANI WA NUSU MUHULA WA PILI

KISWAHILI KIDATO CHA TATU

 

MUDA: MASAA 3                                                                         AUG 2023

 

MAELEKEZO

1.      Karatasi hii ina sehemu A, B na C

2.      Jibu maswali yote sehemu A na B na maswali 2 sehemu C

3.      Zingatia maelekezo ya kila swali

 

SEHEMU A (ALAMA 16) JIBU MASWALI YOTE.

1. Chagua jibu sahihi katika vipengele (i-x) kisha andika herufi ya jibu sahihi katika karatasi ya kujibia.

i.      Huyu ni mwanafunzi hodari sana. Je “ni” ni aina gani ya neon.

a)      Kitenzi shirikishi

b)      Kiunganisha

c)      Kitenzi kisaidizi

d)      Kielezi cha wakati

 

ii.      Njia ipi ni ya uhifadhi wa fasihi simulizi inayoweza kupokea mabadiliko kwa haraka kati ya hizi

a)      Maandishi

b)      Vinasa sauti

c)      Kichwa                                     (d)Kanda za video

 

iii.      Tofauti ndogondogo zinazojitokeza katika lugha moja huitwa

a)   Kimtang’ata

b)  Lugha za kikanda

c)   Lahaja

d)  Kiimbo

 iv.      Wazo kuu la mtunzi katika kazi ya fasihi huitwa

a)      Ujumbe

b)      Dhamira

c)      Falsafa

d)      Mtazamo

v.      -------------- ni maneno yasiyo sanifu yayozuka na kutoweka

a)      Misimu

b)      Rejesta

c)      Msamiati

d)      Kishazi tegemezi

vi.      Kisawe cha neno umaskini

a)      Ukwasi

b)     Ubahili

c)      Ujima

d)     Ukata vii. Ni neno pamoja na taarifa zake kwenye kamusi huitwa

a)      Kidahizo

b)      Kitomeo

c)      Msamiati

d)      Muundo

viii.      Utofauti wa kazi za kifasihi toka muandishi mmoja dhidi ya mwingine husababishwa na 

a)      Mtindo wa kazi

b)      Dhamira za kazi za fasihi

c)      Migogoro ya kazi husika

d)      Muundo wa kazi ya fasihi

 ix.      Moja ya sifa kuu ya kirai ni 

a)      Kukaa sehemu yeyote katika sentensi 

b)      Hakina muundo wa kiima na kiarifu

c)      Hutoa maana kamili

d)      Huwa na muundo wa kiima na kiarifu

x.      Neon lipi kati ya maneno haya linaweza kudokeza mtenda au mtendwa wa jambo

a)      Kiunganishi

b)      Kihisishi

c)      Kielezi

d)      Kivumishi

2.      (a) Oanisha dhana katika orodha A kwa kuchagua herufi ya dhana husika kutoka orodha B kisha andika herufi ya jibu sahihi katika karatasi ya kujibia. 

 

ORODHA A

ORODHA B

I.   Tungo shurutia

II.   Kosa la mpangilio mbaya wa viambishi

III.   Maneno yasiyo sanifu yanayozungumzwa na kikundi kidogo cha watu

IV.  Viambajengo vya sentensi

V.    Sehemu ya nchi kavu iliyochongoka na kuingia baharini

VI.  siataimba

A.    Ghubu

B.     Mpegani

C.     Ukanushi

D.    Anampigia pasi

E.     Rasi

F.      Ukimwonw ndani ya gari utamlipia nauli

G.    Kiima na kiarifu

H.    Simo

I.        Misemo

J.       jakabu

 

 

 

SEHEMU B (ALAMA 54)

 

3.      Wewe ni mwanafunzi wa shule ya sekondari Mazinyungu iliyopo Morogoro.

Umepokea barua kutoka kaka yako aitwaye Amani Furaha anayeishi Tabora S.L.P 300  pamoja na kukujulia hali amekueleza vipi wanavyoendelea huko kwenu Tabora. Pia ametaka uwajulishe ni lini utakwenda huko Tabora. Kutokanaa na ratiba ya shule kukubana unatarajia kwenda utakapofunga shule mwezi Septemba mjulishe kwa kutumia simu ya maandishi jina lako liwe Tusekele Amani.

4.      Kw kutoa hoja nne na mifano eleze jinsi matumizi ya picha na michoro yanavyosaidia matumizi ya kamusi.

5.      (a) toa dhana ya sentensi

(b)  sentensi za Kiswahili hujipambaua kwa sifa zake (taja 3).

(c)   changanua sentensi zifuatazo kwa mkabala wa kimuundo na kimapokeo

(i)     watu wote walimsikilza Rais (kwa njia ya matawi)

(ii)  wao wanaimba lakini sis tuanacheza ngoma (kwa njia ya jedwali)

6.      (a) nini maana ya mzizi wa neon

(b)  Onesha mizizi ya maneno yafatayo 

(i)       Salisha

(ii)    Onesha

(iii)  Onyana 

(iv)   Mpiganaji

(c)   Eleza maana ya istilahi zifuatazo

(i)       Sarufi

(ii)    Kitomeo

(iii)  Lugha

(iv)   Kielezi

7.      Kwa kutumia mifano toshelezi toa uthibitisho wa kiisimu wa Kiswahili ni kibantu.

8.      Kwa kuzingatia maumbo ya umoja na wingi tunga sentensi mbili kwa kila ngeli zifuatazo 

(a)                YU-A-WA

(b)               KI-VI

(c)                U-ZI

(d)               I-ZI                                 

(e)LI-YA. 

 

SEHEMU C (ALAMA 30)

JIBU MASWALI MAWILI KUTOKA SEHEMU HII

9.      Ujio wa waarabu ulisaidia sana kukuza lugha ya Kiswahili. Thibitisha kauli hii kwa hoja zisizopungua nne (4).

10.  Wanaisimu huona kuwa fasihi simulizi ni bora kuliko fasihi andishi. Kwa kutumia hoja tano (5) thibitisha ukweli huu.

11.  Methali zinafunza na zinaweza kupotosha jamii zisipotumika kwa ukamilifu kwwa kutumia methali tano (5) thibitisha kila moja inayoweza kufunza na kupotosha.

 

 

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 148  

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 148  

OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA

NA SERIKALI ZA MITAA

JAMUHURI YA MUUNGANO YA TANZANIA

MTIHANI WA MWISHO MUHULA

KIDATO CHA TATU

KISWAHILI 2023

Muda 2:30 

MAELEKEZO 

  1. Jibu maswali yote
  2. Mtihani huu una sehemu A. B na C (Jumla ya maswali 9)
  3. Simu za mkononi haziruhusiwi

SEHEMU A (15)

  1. Chagua herufi ya jibu sahihi kisha andika herufi ya jibu hilo katika sentensi (i) – (x)
  1. Pauka .............. Pakawa dhana hii hujihusisha katika aina gani ya vipera vya tanzu za fasihi simulizi?
  1. Tarihi
  2. Hadithi
  3. Vigano
  4. Ngano
  5. Masimulizi
  1. Maumbo ya mo, po, ye yanajulikana kama maumbo ya
  1. Mofimu
  2. Mofu
  3. O-rejeshi
  4. Fonimu
  5. Mofu huru
  1. Wataalamu wa simu ya lugha ya kiswahili wamekubaliana kwa dhana ya lugha imetoa fasili za kuzingatia isipokuwa
  1. Lugha ni kwa ajili ya binadamu
  2. Lugha ni sauti za nasibu
  3. Lugha ni mfumo maalumu
  4. Lugha hubadilika
  1. Nadharia gani? Yenye mashiko inayo chagua kunda asili y lugha ya kiswahili ni nini?
  1. Nadharia ya kibantu
  2. Nadharia ya kiarabu
  3. Nadharia ya kiajemi
  4. Nadharia ya kipijini na kikrio
  5. Nadharia ya kikongo
  1. Kipengele gani kinachohusu mjengo wa kazi za fasihi?
  1. Fani
  2. Maudhui
  3. Muundo
  4. Mtindo
  5. Fanani
  1. Mtoto wa muhammed Hussein alidondoka karibu na ukuta wa nyumba yao iliyojengwa kando ya barabara ya kuelekea kisutu. Maneno yaliyopigiwa mistari ni aina gani ya maneno
  1. Kihusishi
  2. Viunganishi
  3. Vielezi
  4. Vivumishi
  5. Vitenzi
  1. Shangazi yangu anapenda sana kurudia nomino katika muundo wa kiarifu anapokuwa akizungumza na wenzake, muundo huu hujulikana kama.
  1. Chagizo
  2. Yambua
  3. Kiyeyusho
  4. Hoponimu
  5. Shamilisho
  1. Neno nchi limeundwa na mfumo gani wa sauti?
  1. K + K + K + I
  2. I + I + I + K
  3. K + I + K + I
  4. K + K + K + K
  5. K + I
  1. Shamilisho katika uchanganuzi wa sentensi hutumia
  1. Kimapokeo
  2. Kimtindo
  3. Kisasa
  4. Kupatanisha
  5. Kisinteksia
  1. Mkazo katika mazungumzo ya kiswahili hutokea upande wa katika herufi ya?
  1. Upande wa kushoto herufi ya pili
  2. Upande wa kulia herufi ya kwanza
  3. Uoande wa juu herufi ya nne
  4. Upande wa chini herufi ya tano
  5. Upande wa kulia herufi ya tatu
  1.  

Kifungu A

Kifungu B

  1. Hadithi za kukejeli na kuchekesha
  2. Hadhithi za kuonya na maadili
  3. Hadithi za asili ya kitu (Umbo)
  4. Hadithi za matukio ya kihistoria
  5. Hadhithi za kuwaasa watoto juu ya maadili
  1. Ngano
  2. Visasili
  3. Soga
  4. Tarihi
  5.  
  6. Mizungu
  7. Vigano
  8. Lekebu
  9. Maghari
  10. Majigambo

 

SEHEMU B (ALAMA 55)

  1. Ni taarifa zipi zinazopatikana katika kiarifu hoja; kwa mfano
  2. Mtumiaji wa lugha ni bendera fuata upepo thibitisha kwa hoja nne (4)
  3. Bainisha mazingira manne ambapo O-rejeshi huweza kujipambania na kwa kila hoja tunga sentensi Moja
  4. Ondoa utata katika sentensi zifuatazo, kwa kutoa hoja mbili kwa kila sentensi
  1. Mtoto amelala na njaa
  2. Ana ametumwa na meshack
  3. Mwanafunzi amenunua mbuzi
  4. Kaka amekufa
  5. Ua limechanua
  1. (a)Wataalamu wa lugha ya kiswahili wanakubaliana kuwa kuna hatua za kuzifuata katika uchanganuzi wa sentensi ainishi hatua hizo hoja tano.

(b)Changanua sentensi zifuatazo kwa njia ya ngoe kwa 

  1. Mwalimu mkorofi amefika darasa
  2. Mama anapika chakula na baba analima shamba

SEHEMU C (30)

  1. Jifanye wewe ni muhitimu wa kidato cha nne mwaka 2022 umeliona na kusoma tangazo katika gazeti la mambo leo andika barua kwa mkurugenzi wa kampuni faidika limited SLP 111 Mwanza ya kuomba nafasi SLP 100 Mtwara.
  2. Kwa mifano kumi anishi tofauti kati ya barua kirafiki na barua ya kikazi.

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 133  

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 133  

 

WIZARA YA ELIMU SAYASI NA TEKNOLOJIA

SHULE YA SEKONDARI KIZUKA

MTIHANI WA MUHULA WA KWANZA

KISWAHILI - KIDATO CHA TATU

Muda: Saa 2:30                    

 

MAELEKEZO

  1.                   Karatasi hii ina sehemu A, B, na C jumla ya maswali kumi na mbili (12).
  2.                   Jibu maswali yote kutoka sehemu A na B na maswali matatu kutoka sehemu C.
  3.                   Sehemu A ina alama kumi na tano (15),  sehemu B ina alama arobaini (40) na sehemu C ina alama arobaini na tano.
  4.                   Zingatia maagizo ya sehemu na ya kila swali.
  5.                   Andika majina yako yote matatu kwa usahihi katika karatasi ya kujibia.
  6.                   Udanganyifu wa aina yoyote hautakiwi kwenye chumba cha mtihani.

 

SEHEMU A (Alama 15) 

Jibu maswali yote kutoka sehemu hii

  1.                   Chagua herufi ya jibu sahihi katika kipengele (i) hadi (x) kisha andika herufi ya jibu hilo katika karatasi yako ya kujibia.
  1. Neno linaloingizwa katika kamusi kwa wino ulio kolezwa, fasili, matamshi na aina ya neno kwa pamoja huitwa?
  1.              Kidalizo
  2.               Kitomeo
  3.              Istilahi
  4.             Kategoria
  5.               Fasili

 

  1. Ni sehemu ya neno isiyobadilika baada ya kuondolewa viambishi awali na tamati.
  1.              Shina
  2.               Kitenzi
  3.              Mzizi
  4.             Kiambishi tamati
  5.               Nomino

 

  1. Jambo gani muhimu huzingatiwa na mtunzi wa insha ya hoja?
  1.              Lugha yenye ukinzani
  2.               Lugha ya kisanaa
  3.              Lugha inayosifia
  4.             Lugha ya kufukirisha
  5.               Lugha isiyo na mvuto

 

 

  1. Zifuatzo ni njia za uundaji wa maneno isipokuwa moja wapo.
  1.              Ufupisho wa maneno
  2.               Ukatizaji
  3.              Kupachika maneno
  4.             Urudufishaji
  5.               Kuambatanisha katika mzizi wa neno

 

  1. Yafuatayo ni matumizi ya simu za maandishi isipokuwa moja wapo.
  1.              Kutoa taarifa juu ya vifo
  2.               Taarifa juu ya ugonjwa
  3.              Kutumia salamu
  4.             Taarifa juu ya kujiunga na shule
  5.               Taarifa ya kufaulu mtihani

 

  1. Ni namna ambavyo msanii hutunga kazi ya fasihi na kuipa sura ambayo kifani na maudhui na kutofautiana na mwandishi mwingine.
  1.              Mtindo
  2.               Muundo
  3.              Mandhari
  4.             Matumizi ya lugha
  5.               Fani

 

  1. Ni aina ya ngeli ambayo huchukuwa upatanisho wa umoja na wingi wa sentesi na kujumuisha viumbe kama wanyama, binadamu, ndege na wadudu.
  1.              Ki-vi
  2.               Yu-A –WA
  3.              Li-YA
  4.             U-I
  5.               I-ZI

 

  1. Ni neno au mapangilio wa maneno ambao hudokeza taarifa fulani ambayo inaweza kuwa kamili au isiyo kamili.
  1.              Kishazi
  2.               Tungo
  3.              Sentensi
  4.             Neno
  5.               Kirai

 

  1. Ni aina ya sentensi inayoundwa na kishanzi tegemezi kimoja au zaidi au kishazi huru kimoja au zaidi
  1.              Sentensi huru
  2.               Sentensi changamano
  3.              Sentensi ambatano
  4.             Sentensi shurutia
  5.               Sentensi sahili

 

  1.             Ni mwana ushahidi wa kihistoria juu ya chimbuko la lugha ya kiswahili na alipata kuandika kuwa Zanzibar ni kivutio chenye ukubwa wa mzunguko wa maili 200 za mraba na wana utawala wao wa kifalme na watu hawalipi kodi.
  1.              Marco-polo
  2.               Al Idris
  3.              Al- Masoud
  4.             Morce
  5.               Historia ya mji wa Kilwa

 

 

  1.               Orodhesha maana za tamathali za semi na maneno mbalimbali katika Orodha A na B kisha andika herufi ya jibu sahihi.

ORODHA  A

ORODHA B

  1. Uhaishwaji wa kitu kisicho binadamu kupewa uwezo wa kutenda kama binadamu.
  2. Nihadithi zinazosimulia matukio ya kihistoria yaliyopita yanaweza kuwa ya kweli au ya kubuni.
  3. Ni aina ya lahaja iliyozungumzwa Tanga.
  4. Ni kipashio kidogo cha sarufi chenye kutoa taarifa kamili au isiyo kamili.
  5. Ushangaaji wa jambo fulani aghalabu huambatana na alama ya mshangao.
  6.  
  1.              Tashihisi
  2.               Kimtang’ata
  3.              Tarihi
  4.             Kingozi
  5.               Tashititi
  6.               Mofimu
  7.              Viambishi
  8.             Nidaa

 

 

 

SEHEMU B (Alama 40)

SARUFI, UTUMIZI WA LUGHA, MAENDELEO YA KISWAHILI

Jibu maswali yote katika sehemu hii

 

  1.               Andika tofauti nne (4) kati ya fasihi simulizi na fasihi andishi.

 

  1.               Tunga sentensi au tungo moja kwa kila kipengele (i) – (iv) ukizingatia viambajengo vya kila kipengele.

 

  1.               Kisha tegemezi + kishazi huru
  2.             Kishazi huru
  3.          Kishazi tegemezi
  4.          Kishazi huru + kishazi huru

 

 

  1.               (a) Toa maana mbili za maneno yafuatayo:-
  1.               Paa             (ii) Mbuzi  (iii) Kanga   (iv)  Tai     (v) Kata

 

 

  1.               Kwa kutumia nomino zifuatazo tunga sentensi zenye upatanisho wa kisarufi na ukionyesha O-rejeshi kwa kupigia mstari chini yake.
  1.               Kalamu   (ii) Kiti     (iii) Ukuta (iv) Sufuria.

 

  1.               Kiswahili ni kibantu “thibitisha kwa kutumia vigezo vya kiisimu na kwa mifano

 

  1.               Soma shairi lifuatalo kisha jibu maswali yafuatayo:-

 

Huwezi kuwazuaia, waliokubaliana

Mimi wananitumia, wapate kuelewana,

Kanuni wazingatia, ili kuwasiliana,

Sauti zangu nasibu, hakuna wa kukanusha

 

Mfumo wangu makini, Sauiti kupangilia,

Maneno kuyatumia, yenye mpangilio sawa,

Sentensi kuzitumia, mawazo kupangilia,

Sauti zangu nasibu, hakuna wa kukanusha

 

 

 

 

MASWALI

  1.               Mwandishi anazungumzia nini katika shairi ulilosoma?
  2.             Ni nini walikubalina kuwasiliana kwa hicho alichokizungumzia mwandishi katika ubeti wa pili?
  3.          Ni mambo gani matatu yaliyojumuishwa na mwandishi katika mfumo wa jambo analolizungumzia?
  4.          Unafikiri kwa nini mstari wa mwisho wa kila beti umerudiwa na mwandishi?

 

 

SEHEMU C (Alama 45)

Jibu maswali matatu (3) tu katika sehemu hii, swali la kumi (10) ni la lazima

  1.               Bi. Hilda alimweleza Bw. Agustino kuwa insha za kisanaa na insha za kiada ni sawa na ndugu wa tumbo moja, Japo kuwa Bw. Agustino hakukubaliana na maoni yake Bi. Hilda. Je wewe kama mwanafunzi mzuri ungetumia hoja gani kumuunga mkono Bw. Agustino? Toa hoja sita (6) zinazothibitisha kama kweli umemuunga mkono Bw. Agustino.

 

  1.          Bw. Lugusi alimweleza Bw. Asheri kuwa waandishi wa kazi za kifasihi hawajafanikiwa kuonesha ufaafu wowote ule wa kimaudhui katika kazi zao, ingawa Bw. Asheri alimkatalia kata kata Bw. Lugusi kutokana na uneni wake alionena. Je wewe kama mwanafunzi uliyefundishwa darasani na ulielewa ungetumia hoja zipi ili umuunge mkono Bw. Asheri. Toa hoja tatu (3) kwa kila diwani.

 

  1.          Bi. Isabela alimweza Bi Theresia Mushi kuwa mapenzi hayana upofu wowote ule miongoni mwa wanajamii. Ingawa Bi. Theresia Mushi hakukubalina na usemi alionena Bi. Isabela. Je wewe kama msomi mzuri wa kazi za fasihi andishi ungetumia hoja zipi ili uweze kumuunga mkono Bi. Theresia Mushi? Toa hoja tatu (3) kwa kila riwaya.

 

  1.          Bw. Mbuya alimfahamisha Bw. Mkway kuwa uwepo wa misigano katika kazi za kifasihi hakuwezi kung’amua malengo makuu ya waandishi asilia. Ingawa Bw. Mkway hakumkubalia Bw. Mbuya kutokana na usemi wake, je wewe kama mwanafunzi uliyemesoma tasnia hii ya fasihi kwa muda mrefu ungetumia hoja zipi ili umuunge mkono Bw. Mkway? Toa hoja tatu (3) kwa kila tamthilia.

 

 

 

 

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 131  

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 131  

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

KISWAHILI KIDATO CHA TATU

MUDA: SAA 3:00        MAY  2022

 

MAELEKEZO

  1.                Karatasi hii ina sehemu A, B, na C, zenye jumla ya maswali kumi na mbili (12)
  2.                Jibu maswali yote kama ilivyoelekezwa katika kila sehemu. A na B maswali matatu kutoka sehemu C
  3.                Sehemu A ina alama kumi natano (15), sehemu B alama arobaini (40) na sehemu C ina alama arobaini na tano (45)
  4.                Zingatia mwandiko mzuri, Mpangilio na usahihi wa majibu yako.
  5.                Majibu yote yaandikwe kwenye karatasi za kujibia.

 

 

SEHEMU A

Jibu maswali yote katika sehemu hii

  1.                Chagua herufi ya jibu sahihi katika kipengtele cha (i) hadi (x) kisha andika herufi ya jibu sahihi katika karatasi ya kujibia
  1. Lugha huweza kuchukua maneno kutoka katika lugha za asili, baini maneno hayo katika orodha ifuatayo;
  1.              Bendera na meza
  2.               Bunge na shule
  3.               Hela na mtutu
  4.              Godoro na sharubati
  5.               Kitivo na ngeli
  1. Ipi ni aina ya tungo ambayo muudo wake una kitenzi ndani yake? Kitenzi hiko huweza kutoa taarifa kamili au isiyo kamili.
  1.              Kishazi
  2.               Kirai
  3.               Shamirisho
  4.              Yambwa
  5.               Sentensi
  1. Katika neon wanaimba, kuna viambishi vingapi?
  1.              4
  2.               8
  3.               3
  4.              5
  5.               6
  1. Ni mchakato wa uundaji wa maneno kwa kupachika viambishi kabla na baada ya mzizi wa neno.
  1.              Utohoaji
  2.               Uambishaji
  3.               Mnyambuliko
  4.              Uambatishaji
  5.               Urudufishaji
  1. Kitomeo huweza kuwa na taarifa kadha wa kadha. Je ipi kati ya zifuatazo si taarifa sahihi inayopatikana katika kitomeo?
  1.              Wingi wa neon
  2.               Aina ya neno
  3.               Mfano wa matumizi
  4.              Asili ya neno
  5.               Mnyumbuliko wa maneno
  1. Katika maneno choka na chako ni mbinu gani imetumika katika kuunda maneni hayo?
  1.              Uradidi
  2.               Uambishaji
  3.               Uhulutishaji
  4.              Mpangilio tofauti wa vitamkwa
  5.               unyumbulishaji
  1. Vipashio vya lugha hupangwa kidarajia kuanzia kidogo kwenda kikubwa katika mpangilio huo ni kipashio kipi kikubwa cha lugha?
  1.              Kirai
  2.               Neno
  3.               Sentensi
  4.              Kishazi
  5.               Sauti
  1. Kutokana na kigezo cha tabia muhusika JOTI ni aina gani ya mhusika?
  1.              Mhusika shida
  2.               Mhusika bapa
  3.               Mhusika foili
  4.              Mhusika mkuu
  5.               Mhusika duara
  1. Waingereza wanakumbukwa kwa mchango wao mkubwa kwa kufanya jambo moja la pekee tofauti na Waarabu na Waingereza katika kukuza na kueneza lugha ya Kiswahili enzi za utawala wao, jambo gani hilo.
  1.              Kutoa elimu kwa lugha ya Kiswahili
  2.               Kusafirisha manamba kutoka sehemu mbalimbali na kuwa fundisha Kiswahili
  3.               Kuteua lahaja ya kiunguja na kuisanifisha
  4.              kuhimizA matumizi ya lugha ya Kiswahili katika ofisi zao
  5.               kuchapisha kamusi mbalimbali za lugha ya kiswahili
  1. Ipi ni maana ya nahau “Uso mkavu”
  1.              Uso usio na mafuta
  2.               Uso usio na nuru
  3.               Uso usio na haya
  4.              Uso usio na shukurani
  5.               Uso wenye mabaka mabaka
  1.                Oanisha maana ya dhana zilizo katika ORODHA A kwa kuchangua herufi ya dhana husika katika ORODHA B

ORODHA A

ORODHA B

  1.                  Ngeli
  2.                Sentensi
  3.             Nomino za pekee
  4.              Neno lenye mofimu nne
  5.                Kiambishi cha nafsi ya pili wingi
  1.              Pangani, Asha, Usingizi na John
  2.               Anayesinzia ni mvivu
  3.               Chaki
  4.              PAMUKU
  5.               Wanaimba
  6.                Mnaimba
  7.              Mtoto
  8.              Chai
  9.                 Kariakoo, Tanga, Iringa na Ali
  10.                 Wewe ni mvivu

 

SEHEMU B (Alama 40)

Jibu maswali yote ya sehemu hii kwa kuzingatia maelekezo ya kila swali.

 

  1.                Taja mambo manne (4) yakuzingatia katika uandishi wa kumbukumbu za mikutano
  2.                Badili vishazi tegemezi vifuatavyo kuwa vishazi huru
  1.                  Mtoto aliyelia jana usiku
  2.                Kazi zinazofanywa
  3.             Jambo litakalomsumbua
  4.              Kitabu kinachosomwa
  1.                Kwa mwanafunzi anayeijua vizuri sarufi ya lugha ya Kiswahili ni rahisi kutambua makossa yanayotokea katika lugha. Kwa hoja nne (4) na mifano fafanua makossa ya kisarifi yanayojitokeza katika utumiaji wa lugha kwa mwanafunzi wa kitanzania.
  2.                Ainisha sentensi zifuatazo, kisha toa sababu moja (1) yaa uainishaji huo kwa kila sentensi.
  1.                  Mkate uliotupatia umeharibika
  2.                Sanga alikuwa amelala
  3.             Aliadhibiwa kwa kuwa alifanya makossa
  4.              Mwalimu akirudi tutaendelea na somo
  1.                “Licha ya lugha ya Kiswahili kuteuliwa kuwa lugha ya Taifa la Tanzania, bado inakabiliwa na changamoto mbalimbali kwa sasa” Onesha ukweli wa kauli hiyo kwa hoja nne (4)
  2.                Vifuatavyo ni vipera vya tanzu za fasi simulizi. Onesha tofauti iliyopo baina ya jozi za vipera hivyo
  1.                  Visakale na visasili
  2.                Ngonjera na majingambo
  3.             Mizungu na misemo
  4.              Wimbo na utenzi

 

SEHEMU C (Alama 45)

Jibu maswali matatu (3) kutoka sehemu hii

 

  1.                Anna ni mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari Kibo. Alikutwa na simu licha ya katazo la serekali na shule kuwa hairuhusiwi mwanafunzi kumiliki simu akiwa shuleni. Baada ya kukutwa na simu hiyo alihojiwa na mwalimu wa nidhamu. Kwa kutumia ukurasa mmoja na nusu (11/2) andika namna mazungumzo yao yalivyokuwa. 

 

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 90  

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 90  

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS

TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

KIDATO CHA TATU 2021

MSIMBO: 021 KISWAHILI

MUDA: SAA 3:00                                                             AUG 2021

 

MAELEKEZO

  1.                Karatasi hii ina sehemu A, B and C zenye jumla ya maswali kumi na mbili (12)
  2.                Jibu maswali yote katika sehmu A na B na maswali matatu (03) kutoka sehemu C
  3.                Zingatia maagizo ya kila sehemu na kila swali
  4.                Andika namba yako ya mtihani katika kila ukurasa wa karatasi

SEHEMU A {Alama 15 }

Jibu maswali yote

  1.                Chagua herufi ya jibu sahihi katika vipengele (i) hadi (x) kisha andika herufi ya jibu hilo katika karatasi yako ya kujibia.
  1. Tuimbe sote ni


  1.                 Wingi nafsi ya kwanza
  2.                Wingi nafsi ya pili
  3.                 Umoja nafsi ya kwanza
  4.                Umoja nafsi ya pili
  5.                 Wing nafsi ya tatu


 

  1. Kusoma kwake kwa bidii kumempatia mafanikio, Neno lililopigiwa mstari ni:


  1.                 Kitenzi
  2.                Kitenzzi kisaidizi
  3.                 Kitenzi jina
  4.                Kitenzi kikurupushi
  5.                 Nomino


 

  1. Jozi ipi ina vipengele sahihi vinavyounda umbo la ndani la kazi ya fasihi simulizi
  1.                 Falsafa, muundo, ujumbe, wahusika
  2.                Mandhari, msimamo, ujumbe, dhamira
  3.                 Ujumbe, mtizamo, migogoro, dhamira
  4.                Ujumbe, msimamo, dhamira, wahusika
  5.                 Lugha, migogoro, falsafa, mtindo

 

  1. Mpangilio sahihi wa vipashio vinavyounda lugha ya kiswahili ni upi
  1.                 Mofimu, kishazi, kirai, neno na sentensi
  2.                Mofimu, neno, kirai, sentensi na kishazi
  3.                 Neno, kirai, kishazi,  sentensi na mofimu
  4.                Neno, mofimu, kirai, kishazi na sentensi
  5.                 Mofimu, neno, kirai, kishazi na sentensi
  1. Ni jambo gani linalodhihirisha upekee wa kazi Fulani ya kifasihi


  1.                 Muundo wa kazi husika
  2.                Wahusika wa kazi husika
  3.                 Jina la kazi husika
  4.                Jina la mtunzi husika
  5.                 Mtindo wa kazi husika


  1. Ipi ni sehemu Ndogo sana ya lugha?


  1.                 Mofimu
  2.                Neno
  3.                 Herufi
  4.                Silabi
  5.                 Mofoloji


 

  1. Ni taratibu zipi zinazofuatwa na lugha fasaha:
  1.                 Kimaana, kimatamshi, kilafudhi, kimuundo
  2.                Kimatamshi, kimofolojia, kiufundi, kimaana
  3.                 Kimatamshi, kimaana, kimuundo, kimantiki
  4.                Kimantiki, kifonolojia, kimaana, kilafudhi
  5.                 Kilafudhi, kimuundo, kiufundi, kimaana

 

  1. Kwa nini lugha ni sauti za nasibu____________
  1.                 Kwa sababu inatumia ishara
  2.                Kwa sababu intumia sauti
  3.                 Kwa sababu inabeba maana
  4.                Kwa sababu inatumiwa na wanyama
  5.                 Kwa sababu inatumiwa na binadamu

 

  1. Ni sifa ipi hutofautisha fasihi simulizi na fasihi andishi?


  1.                 Ukubwa
  2.                Ueneaji
  3.                 Uwasilishaji
  4.                Uhifadhi
  5.                 Utamkaji


 

  1. Mhakiki wa kwanza katika kazi ya fasihi simulizi mfano wa igizo ni:


  1.                 Mtunzi
  2.                Mtazamaji
  3.                 Msomaji
  4.                Mwigizaji
  5.                 Mfasili


 

 

  1.                Oanisha maana za dhana za uandishi zilizo katika orodha A kwa kuchagua herufi ya dhana husika katika Orodha B, Kisha andika herufi husika katika karatasi yako ya kujibia:

ORODHA A

ORODHA B

  1. Irabu
  2. Sarufi
  3. Sentensi sahili
  4. Kidahizo
  5. Chagizo
  1.              Kiwakilishi cha a – unganifu
  2.               Tanzu ya lugha
  3.               Maana ya msingi
  4.              Inaotamkwa huwa hakuna kizuizi chochote kwenye mkondo wa hewa
  5.               Ina hadhi ya kishazi huru
  6.                Kitomeo na taarifa zake
  7.              Ni maneno yanayotokea baada ya kitenzi na kufanya kazi kama kielezi.

 

 

 

SEHEMU B (Alama 40)

 

  1.                Kwa kutumia mifano dhabiti fafanua dhana zifuatazo
  1.                 Urudufishaji
  2.                Uambishaji
  3.                 Kutohoa maneno
  4.                Ngeli

 

  1.                Maneno huweza kubadilika kutoka aina moja na kuwa aina nyingine “Dhihirisha kaulli hii kwa kubadili maneno yafuatayo kwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika mabano
  1.                 Kwenda (Badili kuwa nomino)
  2.                Ogopa (Badili kuwa kivumishi)
  3.                 Mzazi (Badili kuwa kitenzi)
  4.                Linda (Badili kuwa nomino)
  5.                 Bisha (Badili kuwa kivumishi)
  6.                 Bora (Badili kuwa kitenzi)
  7.                Refu (Badili kuwa kitenzi
  8.                Kabati (Badili kuwa kielezi)

 

  1.                Kwa kutumia mifano kuntu fafanua tabia zisizopungau nne (4) za vitenzi vya kiswahili

 

  1.                Wewe na msaidizi wako mmehudhruria kikao cha kupanga mahafali ya kidato cha nne.  Andika kumbukumbu ya kikao kilichofanyika katika shule yenu.

 

  1.                Baada ya kiswahili kuteuliwa kuwa lugha ya Taifa vyombo mbalimbali viliundwa kwa lengo la kukuza na kueneza kiswahili dhibitisha dai hilo kwa kutumia asasi tatu (03)

 

  1.                Soma shairi lifuatalo kisha jibu maswali yanayofuata

 

  1.                Korona ugonjwa gani umezua taharuki;

Chanjo haipatikani Ulaya hakukaliki,

Tiba haijulikani, Dunia haifurukutu,

Korona ni maafa kujikinga lazima,

 

  1.                Hofu kubwa imetanda, wakubwa kwa wadogo;

Mafua, homa kupanda utaona uki”gugo”,

China mpaka mpanda, korona haina vigo,

Korona ina maafa kujikinga lazima

 

  1.                Walakini juu ya yote, mapenzi yameoteshwa,

Karantini kwa wotee, makapera wameoa,

Mabinti wasiopenzini, huu msimu wa ndoa

Korona ina maafa kujinginga lazima

 

 

 

  1.                Hakika baniani mbaya Kiatu chake dawa,

Wanandoa walishane penzi bila taabu,

Nao wapenzi wachanga, wasubiri janga lipite

Korona ina maafa kujikinga lazima

 

  1.                Mungu atasaidia Korona itaisha,

Elimu tazingatia Wizara wanakumbushia,

Tunawe yetu mikono, epuka msongamano

Koroana ina maafa kujikinga lazima

MASWALI

  1.                 Pendekeza kichwa cha habari kisichozidi maneno matatu
  2.                Unafikiri kwa nini mshairi anatuasa kuwa Korona ina maafa kujikinga lazima?
  3.                 Mashairi wa shairi hili anawashauri nini wanafunzi kuhusiana na suala la mapenzi?
  4.                Kutokana na shairi ulilosoma eleza njia tano unazozijua utakazotumia kuepukana na ugonjwa wa Korona

 

SEHEMU C (Alama 45)

Jibu maswali matatu (3) kutoka katika sehemu hii

  1.                Fasihi simulizi ndio fashihi ya awali iliyoanza wakati binadamu alipoanza kutumia lugha mara kwa mara inapowasilishwa kwa hadhira huchukua sifa muhimu ambazo sirahisi kuziona katika fasihi Andishi.  Dhibitisha ukweli huu kwa kutumia hoja tano.

 

  1.            Nyimbo ni mbinu ya kifasihi ambayo wasanii wengi hutumia ili kufikisha ujumbe uliokusudiwa kwa hadhira.  Dhibitisha usemi huu kwa kutumia waandishi wawili wa riwaya ulizosoma.

 

  1.            Taswira ni kibebeo cha ujumbe wa mwandishi katika jamii.  Jadili kauli hii kwa kutumia thamthiliya mbili ulizosoma.

 

  1.            “Mshairi siku zote hukemea uonevu katika jamii “dhibitisha kauli hii wa kutoa hoja tatu kutoka katika kila diwani kati ya Diwani mbili (2) ulizosoma.

 

ORODHA YA VITABU

USHAURI

Wasakatonge    - M.s Khatibu (DUP)

Malenga wapya  - Takiluki (DUP)

Mashairi ya chekacheka - T. A Mvungi (EP & D. LTD)

RIWAYA

Takadini   - Benj. Hanson (MBS)

Watoto wa mama ntiliye - E. Mbogo (H.P)

Joka la mdimu   - A.J Safari  (H.P)

TAMTHILIYA

Orodha Steven Reynolds (MA)

Ngoswe penzi kitovu cha uzembe -E. semzaba

Kilio chetu     -Medical Aid foundation 

Page 1 of 4

 

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 65  

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 65  

  OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA KWANZA

KIDATO CHA TATU

021KISWAHILI

(Kwa watahiniwa Walioko na Wasiokuwa Shuleni)

MUDA: SAA 3 MEI 2021


Maelekezo

1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi na mbili (12).

2. Jibu maswali yote kutoka sehemu A, Bna chagua maswali matatu (03)kutoka sehemu C.

3. Zingatia maagizo ya kila sehemu na kila swali.

4.Andika kwa kutumia kalamu ya wino wa bluu au nyeusi

5. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa haziruhusiwikatika chumba cha mtihani.

6. Andika namba yako ya mtihani katika kila karatasi yako ya kujibia.

  1. Chagua herufi ya jibu sahihi katika vipengele i-x kisha andika herufi ya jibu sahih katika kisanduku.
  1.  Ni neno lipi linalotoa taarifa kuhusu Nomino?

A: Kitenzi  B: Kielezi  C: Kivumishi

D: Kiwakilishi  E: Kiunganishi

(ii) Katika lugha ya Kiswahili kuna aina ngapi za Vitenzi.

 A: Mbili  B: Tano  C: Sita

 D: Tatu  E: Nne

(iii) Maneno yapi kati ya haya yafuatayo yametokana na lugha ya Kibantu.

  A: Kitindamimba ba bendera   B: Hela za mtoto

  C: Kitivo na ngeli    D: Godoro na sharubati

  E: Bunge na Shule

(iv) Ni mambo gani muhimu ya kuzingatia katika kuteua maneno na miundo 

    ya tungo wakati wa mazungumzo.

   A: Mada, muktadhia wa mazungumzo ya aina kwa nia

    B: Mada, mazungumzo na uhusiano wa wazungumzaji

   C: Mada, mzungumzaji na muktadha wa mazungumzo 

   D: Mada, mzungumzaji na uhusiano wa wazungumzaji

   E: Mada, muktadha na uhusiano wa wazungumzaji.

(v)  Bainisha kauli unayoonyesha dhima muhimu za vitendawili katika jamii za 

    vitendawili katika jamii.

     A. Kuhimiza umoja na mshikamano.

    B. Kupanga watu katika marika yao.

    C. Kuchochea udadisi wa mambo

  D. Kuchochea uwongo wa mambo.

  E. Kukosoa wadadisi wa mambo.

(vi) Njia mojawapo ya kuzuia utata katika lugha ya mazungumzo ni ipi kati ya zifuatazo?

 A. Kuepuka makosa ya kisarufi na kimantiki

 B. Kutumia neno lenye maana zaidi ya moja 

 C. Kutumia kiwakilishi kiambata katika neno 

 D. Kuweka msisitizo au ufafanuzi zaidi

 E. Kutumia misimu sahihi za wakati.

(vii) ‘’Wanafasihi hutumia wahusika wenye mienendo hiyo’’ katika tamthiliya ulizosoma, ni wahusika wapi kati ya wafuatao wana mienendo isiyokubalika?

 A. Joti, Ngoswe na Mama Furaha

 B. Padri James, Ngoswe na Baba Anna.

 C. Mazoea, Mama Furaha na Joti

 D. Ngoswe, Baba Anna na Suzi

 E. Ngoswe, Joti na Padri Jamaes

(viii) Kati ya sababu zifuatazo ni ipi si sahihi kuhusu matumizi ya Kamusi?

 A. Kujifunza Lugha ya Kigeni

 B. Kusanifisha maneno mapya

 C. Kubaini kategoria ya neno

 D. Kujua maana za maneno

 E. Kujua tahajia za maneno.

(ix) Ni methali ipi inayokinzana na methali ‘’Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu.’’

 A. Manahodha wengi, chombo huenda mrama.

 B. Palipo na wengi, hapaharibiki neno

 C. Haba na haba, hujaza kibaba.

 D. Kidole kimoja, hakivunji chawa

 E. Fimbo ya mnyonge, ni umoja 

(x) Upachikaji wa Viambishi katika mzizi wa neno huitwaje?

 A. Mnyambuliko  B. Utohoaji  C. Uambishaji

 D. Viambishi   E. Kukopa maneno  

  1. Oanisha maana za maneno kutoka orodha A kwa kubainisha dhama zilizoko katika

Orodha B na uandike herufi ya jibu sahihi pembeni na swali.

ORODHAA

ORODHAB

(i) Tungo shurutia ukwasi

A. Rejesta ya Tanga

(ii) Kimtang’ata

B. Angeliniita ningeitika

(iii) Malaika, Shetani, Mzimu

C. Lahaja ya Kiswahili

(iv) Juzi asubuhi

D. Nomino za mguso


E. Njeo ya ya wakati wa mazoea


F. Nomino za dhahania


G. Kirai kielezi


H. Utajiri

SEHEMU B: (ALAMA 40)

Jibu maswali yote kutoka sehemu hii

  1. Bainisha mzizi asilia kwa kila neno katika maneno yafuatayo.

(a) Anawaandikisha

(b) Mkimbizi

(c) Mlaji

(d) Muumbaji

(e) Nisingelipenda

(f) Kuburudika

(g) Sadifu

(h) Aliokota

(i) Walichopoka

(j) Kipambanuliwe.

  1. Bainisha matumizi mbalimbali ya ‘’KWA’’ katika sentensi zifuatazo

(a) Amejificha kwa kuwa hapendi anione

(b) Kukataa kwa Mwajuma kumesababisha matatizo mengi.

(c) Amelima shamba kwa jembe

(d) Ameenda kwa Mwalimu

(e) Amesafiri kwa ndege

  1. Kwa kutumia mfano taja njia tano za uundaji wa maneno.
  2. Toa maana mbili katika tungo tata zifuatazo?

(a) Pili alimwandikia barua Asha

(b) Wizi wa Silaha umeongezeka

(c) Mwalimu ameijia fedha yake

(d) Mtoto amelalia uji

(e) Mama amenuena Mbuzi

  1. Taja mambo matano ya kuzingatia wakati wa utunzi wa Insha na ueleze umuhimu wa kila jambo.
  2. Eleza tofauti za msingi tano, zilizopo baina ya varua ya kikazi na barua za kindugu.

SEHEMU C: (ALAMA 45)

Jibu maswali matatu tu toka sehemu hii

  1. Eleza sababu tano zilizosaidia kuenezza Kiswahili wakati wa utawala wa Wajerumani.
  2. Fasihi ni Chuo chenye kufundisha kila mwanajamii husika. Thibitisha hoja hiyo kwa kutumia vitabu viwili vya riwaya ulivyosoma. Toa hoja tatu kwa kila Kitabu.
  3. Mashairi huburudisha na kuliwaza pale yanapoimbwa au kusomwa lakini nayatoa mafunzo mazuri sana kwa jamii husika. Jadili kauli hii kwa kutumia Diwani mbili ulizosoma. Toa hoja nne kutoka kila diwani.
  4. Siku zote katika jamii, migogoro ndiyo inayoibua dhamira mbalimbali. Thibitisha dai hili kwa kutumia tamthiliya mbili ulizozisoma ukitoa hoja tano kwa kila kitabu.

1

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 55  

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 55  

OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MTIHANI WA MWISHO WA MWAKA 2020

021KISWAHILI

(Kwa watahiniwa Walioko na Wasiokuwa Shuleni)

MUDA: SAA 3 DECEMBER 2020


Maelekezo

1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi na mbili (12).

2. Jibu maswali yote kutoka sehemu A, B na chagua maswali matatu (03) kutoka sehemu C.

3. Zingatia maagizo ya kila sehemu na kila swali.

4Andika kwa kutumia kalamu ya wino wa bluu au nyeusi

5. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa haziruhusiwi katika chumba cha mtihani.

6. Andika namba yako ya mtihani katika kila karatasi yako ya kujibia.

SEHEMU A, (Alama 15)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1. Chagua herufi ya jibu sahihi katika vipengele (i) hadi (x), kisha andika herufi ya jibu hilo katika karatasi yako ya kujibia.

(i) Ni kanuni, sheria na taratibu zipi zinazozingatiwa na wazungumzaji wa lugha fulani?

A Mofimu, Neno, Kirai, Kishazi na Sentensi

B Herufi, Sauti, Mofimu,Silabi na neno.

C Sarufi Maana, Sarufi Miundo, Sarufi Maumbo na Sarufi Matamshi.

 Sarufi maana, Mofimu, Neno na Kirai

E Silabi, Neno, Kirai na Sentensi.

(ii)………………. Ni sauti zinazotamkwa mara moja na kwa pamoja kama fungu moja la sauti.

 A Sauti B Herufi

 C irabu D  Silabi

 E Konsonanti

(iii)  Zipi ni nyenzo za lugha yoyote duniani?

A Sarufi na Fasihi B Irabu na Konsonanti

C Sarufi, Irabu na KonsonantiD Fasihi, Irabu na Konsonanti

E Sarufi, Fasihi, Irabu na Konsonanti

(iv) Mpangilio sahihi wa ngeli za kisintaksia ni upi?

A YU/A-WA, I-ZI,LI-YA,U-I,KI-VI,U-ZI,U-YA, KU,PA-MU-KU

B U-ZI, I-ZI,LI-YA,U-I, KU, YU/A-WA,U-YA, KI-VI, PA-MU-KU

C YU/A-WA, I-ZI, LI-YA,U-YA, KI-VI,U-ZI,U-I, KU,PA-MU-KU

D YU/A-WA,I-ZI, LI-YA,U-I,KI-VI, U-ZI,U-YA, PA-MU-KU, KU

E YU/A-WA, I-ZI,LI-YA, U-I, KI-VI,U-ZI, U-YA,KU, PA-MU-KU

(v)  Ni upi mpangilio sahihi wa mjengo wa Tungo?

A Kirai, Neno, Sentensi na Kishazi

B Neno, Kirai, Kishazi na Sentensi

 Kishazi, Kirai, Sentensi na Neno

E Sentensi, Neno. Kishazi na Kirai

(vi)  Ni lugha mseto ya muda inayozuka pindi makundi mawili yenye lugha mbili tofauti yakutanapo.

 Lugha ya vizalia B Pijini

C Kibantu D Kiswahili

E Kiunguja

(vii)Mambo muhimu yanayopatikana katika maana ya lugha ni kama yafuatayo, isipokuwa;

A Ni sauti za nasibu B Ni mfumo

C Lugha hufurahisha na kufundisha D Lugha inamuhusu binadamu

E Lugha ni chombo cha mawasiliano

(viii)  Ni sentensi ipi sio sentensi huru?

A Juma anacheza mpira B Anaimba vizuri

C Mtoto aliyepotea jana amepatikana. D Asha ni mtoto mzuri

EYule alikuwa anataka kucheza mpira.

(ix)  ……………. Ni kipashio kidogo kabisa cha lugha chenye maana. Maana hiyo yaweza kuwa ya kisarufi au kileksika;

 Isimu B Shina

C Mzizi D Kiimbo

E Mofimu

(x) Ni seti ipi inawakilisha kikamilifu wahusika wa fasihi simulizi?

A Vitu, mahali, wanyama, binadamu, fanani na maleba.

B Hadhira, wanyama, maleba, binadamu na fanani.

C Fanani, vitu, mahali, binadamu, maleba na wanyama.

 Wanyama, manju, binadamu, vitu, mahali na maleba

E Hadhira, binadamu, wanyama, vitu, mahali na fanani.

2. Oanisha maelezo yaliyo katika orodha ‘’A’’ ambayo ni aina ya tungo na orodha ‘’B’’ ambazo ni aina za maneno yanayounda tungo hizo kwa kuandika herufi ya jibu sahihi katika karatasi yako ya kujibia.

ORODHA “A”

ORODHA “B”

i.Wale waliamini maneno yangu

 ii. Salama alikuwa mwanafunzi wangu

 iii. Walikuwa wanataka kwenda kulima

 iv.Alikuwa anajisomea darasani polepole

 v. Loo! Yule anapenda ugomvi

A. N + t +N +V

B. H + w +T + N

C. W + T + N + V

D. Ts + T + E +E

E. Ts + Ts + Ts + T

F. N + V + t +E

G. N + U+ N+ T

SEHEMU B (Alama 40)

Jibu maswaliyote katika sehemu hii

3.Tunga sentensi moja kwa kila alama kuonesha matumizi ya alama zifuatazo.F4

i. Mkato

ii. Mabano

iii. Alama za mtajo

iv. Nukta pacha

4.Andika maana ya methali zifuatazo;

  1. Kikulacho ki nguoni mwako.
  2. Mtaka cha uvunguni sharti ainame.
  3. Mchumia juani hulia kivulini.

5.(a) Tenga kiima na kiarifu katika sentensi zifuatazo. Tumia alama ya mkwaju (/) na kuweka herufi “K” juu ya kiima na herufi “A” juu ya kiarifu.

i. Mdogo wangu anaongea sana

ii. Yule kijana aliyekuja hapa juzi amefariki dunia

iii. Frank ni kijana mpole sana

iv. Mama amelala sakafuni

(b) Changanua sentensi zifuatazo kwa njia yamatawi kwa kutumia mkabala wa kimapokeo

i. Fisi mkubwa ameuawa kichakani jana alfajiri.

ii. Mtoto aliyekuwa anacheza uwanjani amevunjika mguu.

6.(a) Kwa kutumia mifano miwili kwa kila kipengele, fafanua kwa ufupi jinsi vipengele vifuatavyo vinavyoonesha kuwa vitenzi vya Kiswahili na lugha za kibantu vina asili moja.

  1. Mpangilio wa viambishi katika vitenzi
  2. Kiambishi tamati katika vitenzi

b) Eleza kwa ufupi juu ya nadharia zifuatazo kwa jinsi zinavyoelezea asili ya Kiswahili

a)Kiswahili ni pijini au krioli

b)Kiswahili ni kiarabu

7. Kwa kutumia mifano, fafanua dhana zifuatazo kama zinavyotumika katika fasihi

a)Tashibiha

b)Takriri

c)Sitiari

d)Tashihisi

e)Mubaalagha

8. Soma kifungu cha habari kifuatacho, kisha jibu maswali yanayofuata;

Wanangu, toka zamani bara letu la Afrika lilikuwa na mambo yaliyohitilafiana na haya tunayoyaona sasa. Hadithi, vitimbi, na visa vilivyotokea zamani katika bara letu vinatofautiana sana na mabara yoyote mengine. Vyetu ni vitamu na bora kuliko vyote vile vilivyotokea katika mabara hayo.

Miujiza ya mambo yaliyotokea ina mizizi ambayo viini vyake hubenua waziwazi mila na desturi za asili tangu zamani, hivyo, hadithi hizo zina tija ya makumbusho ya daima milele. Kwa hiyo, katika hali yoyote yatupasa kuhifadhi hazina za mila zetu. Mila zetu zidumishwe; kwa mfano watu kuzunguka moto huku kizee kikongwe au ajuza akisimulia hadithi za mambo ya kale liwe ni jambo la kawaida kabisa. Katika dunia ya leo simulizi hizo za ujasirina uzalendo zimeenea kutoka vizazi hadi vizazi. Mambo mengi yamebadilika kutoka mitindo aina aina, hivyo mabadiliko hayo yasitufanye sisi kusahau simulizi zetu katika mitindo yetu. Ni wajibu utupasao kuendeleza tabia hizi ili tubenue mbinu za masimulizi hata kwa vitabu.

Maswali

  1. Pendekeza kichwa cha habari hii kisichozidi maneno matatu.
  2. Bara la Afrika lina mambo gani mawili mazuri.
  3. Mwandishi anatuhimiza tudumishe mila ipi?
  4. Fupisha habari uliyosoma kwa maneno yasiyopungua 50 na yasiyozidi 60.

SEHEMU C (Alama 45)

Jibu maswali matatu(3) kutoka katika sehemu hii.

9.Wewe kama afisa Manunuzi wa kiwanda cha mbao cha Mshikamao S. L. P 100 Chamwino, andika barua kwa mfanyabiashara yeyote mashuhuri wilayani kwenu kuhusu agizo la vifaa vifuatavyo; Misumeno 5, gundi ya mbao lita 20, misumari ya nchi sita Kg 25, na kofia ngumu 40. Jina lako liwe Shukrani Kazamoyo.

10. Kwa kutumia diwani mbili ulizosoma, eleza jinsi taswira tatu kutoka kila diwani zilivyotumiwa na msanii kuwasilisha ujumbe kwa jamii.

11. “Kazi ya fasihi ina radha kwa sababu inamzungumzia pia mwanamke kwa namna tofautitofauti” Thibitisha kauli hii kwa kutoa hoja tatu kwa kila kitabu katika riwaya mbili ulizosoma.

12. Chagua wahusika wawili katika tamthiliya teule mbili ulizosoma na uoneshe ujumbe unaowasilishwa na waandishi kupitia matendo yao.

ORODHA YA VITABU 

USHAIRI

Wasakatonge ---------------------------- M. S Khatibu (DUP)

Malenga wapya-------------------------- TAKILUKI (DUPU)

Mashairi ya Chekacheka---------------- T. A. Mvungi (EPdD.LTD)

RIWAYA

Takadini ----------------------------------- Ben J. Hanson (MBS)

Watoto wa Mama Ntilie ----------------- E. Mbogo (H.P)

Joka la Mdimu ---------------------------- A. J. Safari ( H.P)

TAMTHILIYA

Orodha ------------------------------------ Steve Reynolds ( M. A)

Ngoswe Penzi Kitovu cha Uzembe ----- E. Semzaba (ESC)

Kilio Chetu --------------------------------- Medical Aid Foundation (TPH)

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 37  

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 37  

THE PRESIDENT'S OFFICE

MINISTRY OF REGIONAL GOVERNMENT AND LOCAL GOVERNMENT

AUGUST-SEPTEMBER   EXAMINATION SERIES

KISWAHILI  FORM-3

2020

TIME: 2:30 HRS

Maelekezo

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi na mbili (12).
  2. Jibu maswali yote katika sehemu A na B na maswali matatu (3) kutoka sehemu C.
  3. Zingatia maagizo ya kila sehemu na ya kila swali.
  4. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba cha mtihani.
  5. Andika Namba yako ya Mtihani katika kila ukurasa wa kijitabu chako cha kujibia.

SEHEMU A (Alama 15)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1. Chagua herufi ya jibu sahihi katika vipengele (i) hadi (x), kisha andika herufi ya jibu hilo katika kijitabu chako cha kujibia.

(i) Neno lipi kati ya maneno haya linaweza kudokeza mtenda au mtendwa?

  1. Kiunganishi   
  2. Kivumishi
  3. Kihisishi 
  4. Kiwakilishi 
  5. Kielezi

(ii) Shamba letu li kubwa neno “Li” ni aina gani ya neno? 

  1. Kiwakilishi 
  2. Kielezi 
  3. Kivumishi 
  4. Kiunganishi 
  5. Kitenzi kishirikishi

     (iii) Lugha fasaha hufuata taratibu za lugha, taratibu hizo ni pamoja na 

A       fonolojia, mofolojia, semantiki na sintaksia

B        maana, matamshi, muundo na maumbo

C        maana, matamshi, muundo na mantiki

D        kiimbo, shada, mkazo na toni

E.       fonolojia, mkazo, shada na semantiki

(iv) Kamati ya lugha ya Afrika ya Mashariki (the interteritorial Swahili language committee) iliteua lahaja moja na kuisanifisha, lahaja hiyo ilikuwa ni

A         kimvita             

 B       kiunguja

C         kimtang’ata       

D        kisiu

E         kivumba

(v). Watoto hawa wanacheza vizuri neno “Vizuri” ni aina gani ya neno? 

  1. Kivumishi 
  2. Kielezi 
  3. Kiwakilishi 
  4. Kivumishi cha sifa 
  5. Kihisishi 

 

(vi) Kiswahili ni kibantu kwa kuwa:- 

  1. Kinaongewa na wabantu wengi 
  2. Ni lugha ya Taifa 
  3. Kina maneno mengi ya kibantu 
  4. Kimethibitishwa kiisimu na kihistoria 
  5. Wasomi wengi wamethibitisha hivyo.  


(vii) Ni jambo gani linalodhihirisha upekee wa kazi fulani ya kifasihi? 

  1. Muundo 
  2. Mtindo 
  3. Wahusika 
  4. Jina la mtunzi  
  5. Jina la kazi husika 


(vii) Ipi ni fasili sahihi kuhusu tungo? 

  1. Maneno yanayoonesha uhusiano baina ya neno moja na jingine. 
  2. Kipashio kidogo katika lugha kinachotumika kama dhana ya kuchambulia lugha Fulani. 
  3. Matokeo ya kuweka na kupanga pamoja vipashio sahili ili kujenga vipashio vikubwa zaidi. 
  4. Kipashi cha kimuundo chenye neno moja na kuendelea 
  5. Maneno yenye kutoa maana kamili


(viii) Nini maana ya sentensi sahili. 

  1. Ni sentensi yenye kishazi kuu kimoja au zaidi pamoja na kishazi tegemezi.
  2. Ni sentensi yenye kishazi huru 
  3. Ni sentensi yenye kuonesha masharti 
  4. Ni sentensi yenye maana nyingi 
  5. Ni sentensi yenye vishazi vingi 


(ix) Zifuatazo ni sifa za pijini isipokuwa 

A.      Pijini huwa na maneno kutoka lugha mbili au zaidi

B.      Pijini hutokea kurahisisha mawasiliano baina ya watu ambao kila mmoja 

         ana lugha yake

C.      Miundo ya maneno na tungo katika pijini imerahisishwa ili kukidhi 

         mawasiliano

   D.     Pijini haina msamiati mwa kutosha, hivyo wazungumzaji hutumia sana 

        ishara

  E.    Pijini ina watu ambao kwao hiyo ni lugha yao ya kwanza


2. Katika kila sentensi uliyopewa, orodhesha vishazi huru katika Safu A na vishazi tegemezi katika safu B.
(a) Ngoma hailii vizuri kwa kuwa imepasuka.
(b) Watoto walioandikishwa watakuja kesho.
(c) Kiongozi atakayefunga mkutano amepelekewa taarifa.
(d) Mtawatambua walio wasikivu.
 (e)       Kitabu ulichopewa kina kurasa nyingi. 

 

3. Taja aina za sentensi zifuatazo kisha eleza muundo ujengao kila sentensi.

  1. Maisha ni safari ndefu.
  2. Ukisoma kwa bidii utafaulu kwa kiwango cha juu.
  3. Mtoto aliyelazwa hospitalini ameruhusiwa kwenda nyumbani.
  4. Nitakuja leo ingawa nitachelewa sana.
  5. Alinunua madaftari lakini kitabu cha Kiswahili alipewa na mwalimu.

4. Andika maneno matano ambayo yameundwa kutokana na kufananisha sauti. Kwa kila neno tunga sentensi moja.

5. Eleza dhima za mofimu "li" kama ilivyotumika katika sentensi zifuatazo:

  1. Shamba letu li kubwa sana.
  2. Wlishelewa kurudi.
  3. Tunalifuatilia.
  4. Limeharibika.
  5. Shikilia.

6. Andika sentensi zifuatazo katika hali ya ukanushi:

  1. Ameshiba sana.
  2. Watoto wengi wanaogelea.
  3. Mvua ilinyesha kwa wingi sana.
  4. Kijana anakula chakula kingi.
  5. Mimi nasoma polepole.

7. Bainisha mzizi wa asili kwa kila neno katika maneno yafuatayo:

  1. Anawaandikisha
  2. Mkimbizi
  3. Mlaji
  4. Muumbaji
  5. Nisingelipenda
  6. Kuburudika
  7. Sadifu
  8. Aliokota
  9. Walichopoka
  10. Kipambanuliwe

1. Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata:

Karibu masikio ya watu wa mahali pengi yalijaa habari za Karama na mashtaka yake. Umaarufu wake wa ghafla ulizungumzwa karibu na mbali. Mtu yeyote wa desturi anapozuka katika umaarufu, huyavuta masikio na macho ya watu wengi kwa sababu jambo kama hili hutokea nadra sana kwa watu ambao bahati mbaya imeshughulika kuwaweka nyuma. Kwa hiyo, siku ya tatu ya baraza ilihudhuriwa na mfalme, watu wenye vyeo mbalimbali, pamoja na nusu moja ya umati mkubwa wa Kusadikika. Fikra zilizochanganyika ziliushika umati huu. Baadhi ya watu walimwajabia Karama wakamhesabu kama mtu bora wa karne yao. Hawa walitumaini ataokoka lakini wengine waliwaza kuwa Karama alikuwa kama mjinga aliyekuwa akicheza na hatari kubwa iliyofunua taya mbele yake.

Waliokuwa wakimtazamia kuokoka walikuwa na wasiwasi wao; na wale waliokuwa wakimtazamia kuanguka walikuwa na fadhaa yao. Walakini hapana mtu hata mmoja aliyepata kulisema wazo lake.

Bila ya kujua alivyoajabiwa Karama aliendelea kusema mbele ya baraza, “Watu wanaoteswa ndio wanaoyajua mateso yao.” Kusadikika ilikuwa chini ya mateso makubwa sana. Maisha yao yalizungukwa na maradhi na mauti, uadui usiokwisha, nchi iliyokaribia kugeuka jangwa na mwamba na madhila mengine mazito yaliyowakabili watu. Wanakusadikika walitaka faraja katika mateso haya. Kila jitihada ilijaribiwa ili kuirekebisha saa ya maendeleo ya nchi, lakini mara kwa mara majira yake yalirudishwa nyuma. Kama hili lilifanywa kwa makosa ama kwa makusudi ni siri iliyo ng’ambo ya fahamu zangu hata sasa. Lakini kama siri njema hufichika, ile iliyo mbaya haifichiki hata kidogo. Uchaguzi wa wajumbe ulikuwako lakini hathibitisho ya matokeo ya ujumbe hayakupatikana.

Kusadikika iliishi kuona mjumbe baada ya mjumbe kuadhiriwa na kuadhibiwa vibaya. Kama washauri hawakudhuriwa na hili lakini watu wengine walidhuriwa sana. Kazi njema za wajumbe wawili zilipotea bure. Manung’uniko ya lawama hii yalikuwa katika hewa yote ya Kusadikika.

Hili lilipotokea serikali iliombwa ima faima kufanya ujumbe mwingine. Basi mjumbe wa tatu alitakikana ajitolee mwenyewe kwa ujumbe wa Kusini. Wito wa mjumbe wa tatu uliitikiwa na Kabuli; mtu mwenye busara, haya na mcheshi. Yeye alipatikana upesi kabisa kuliko ilivyokuwa kwa mara ya pili na ya kwanza. Misiba ya Buruhani na Fadhili ilikuwa mikubwa ya kutosha kuikongoa mioyo ya bidii katika bawaba zake. Kabuli aliyajua haya yote lakini alikuwa mtu wa moyo wa namna nyingine kabisa. Alikuwa na bidii kubwa kama ile ya siafu athubutiye kukivuka kijito kwa daraja iliyofanywa kwa maiti ya siafu wengine walioelea majini huko na huko. Maji yalijulikana kuwa na asili ya rutuba, mvuke na umeme. Nguvu nyingine za namna mbalimbali zipo pia katika maji. Kama siafu mdudu mdogo na kipofu wakati mwingine haogopi kuzikabili nguvu hizo pamoja na hatari zake kwa sababu njema, basi ni dhahiri kuwa viongozi wa wanadamu wanapoteswa bure bidii za wafuasi wao hutanuka ajabu.

Hapana tishio liwezalo kuukomesha mwendo huu. Kwa hakika utafululiza kuwako duniani mpaka mateso yakome kabisa, na labda wakati huo dunia hii itakuwa njema kama itamaniwavyo kuwa.

Buruhani na Fadhili walitoa sadaka zao bora ili kuyahimiza majilio ya wakati uliotakikana sana. Kabuli aliwaona watu wawili hawa kama wafadhili wakubwa wa ulimwengu. Alitaka kuwa mshirika wao kwa thamani yoyote ya maisha yake.

Kama ilijulikanavyo, Kusini na upande wa dunia yatokako matufani makubwa na baridi kali sana. Kabuli aliyakabili mashaka haya bila ya kigeugeu. Naam, alikuwa kama mtu aliyekuwa akinywa uchungu bila ya kigegezi. Mara mbili alikamatwa akafanywa mahabusu.

Maswali

(a) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika kifungu cha habari:

  1. Fadhaa
  2. Madhila
  3. Kuadhiriwa
  4. Ima faima
  5. Kigeugeu
  6.  Kigegezi.

(b) Eleza mchanganyiko wa fikira walizonazo wana wa Kusadikika kuhusu Karama.

(c) Kwanini bidii ya mjumbe wa Kusini imelinganishwa na bidii ya siafu? Toa sababu mbili.

(d) Ujumbe wa mwandishi wa kifungu hiki unahusu nini?

SEHEMU C (Alama 45)

Jibu maswali matatu (3) kutoka katika sehemu hii.

8. Andika insha isiyozidi maneno mia tatu (300) na isiyopungua mia mbili na hamsini (250) kuhusu faida za televisheni kwa jamii.

ORODHA YA VITABU USHAIRI

Wasakatonge - M.S. Khatibu (DUP)

Malenga   Wapya - TAKILUKI (DUP)

Mashairi   ya   Chekacheka - T.A. Mvungi (EP & D.LTD)

RIWAYA

Takadini - Ben J. Hanson (MBS)

Watoto   wa   Maman’tilie - E. Mbogo (H.P)

Joka   la   Mdimu - A.J. Safari (H.P)

TAMTHILIYA

Orodha - Steve Reynolds (MA)

Ngoswe Penzi Kitovu   cha   Uzembe - E. Semzaba (ESC)

Kilio   Chetu - Medical Aid Foundation (TPH)

10. "Fasihi ya Kiswahili imemweka mwanamke katika hadhi tofauti tofauti." Thibitisha usemi huu kwa kutumia hoja tatu kwa kila riwaya kutoka katika riwaya mbili ulizosoma.

11. (a) Vigano ni nini?

(b) Tunga vigano kwa kutumia methali isemayo "Umdhaniaye siye kumbe ndiye!"

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 28  

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 28  

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256