SAYANSI 2005
 Chaguajibu sahihi na andika herufi inayohusika mbeleya nambaya kila swali katika karatasiya kujibia.
 1. Zilizoorodheshwa hapa chini ni sehemu za jicho la binadamu isipokuwa
  - siliari
  - retina 
  - mboni 
  - shata 
  - irisi
  
Chagua Jibu    
2. Usambazaji wa chakula mwilini hufanywa na:
  - damu 
  - maji 
  - hewa
  - misuli
  - neva
  
Chagua Jibu    
3. Kemikali inayotumika kutambua iwapo chakula Fulani ni cha aina ya wanga ni:
  - besi 
  - alkoholi 
  - aside 
  - alkali
  - ayodini
  
Chagua Jibu    
4. Ombwe katika chupa ya chai (kielelezo namba 1) huzuia upotevu wa joto kwa njia ya:
      |  
  | Kielelezo Na. 1 |  
  
  - kuakisi
  - mpitisho
  - msafara na mpitisho
  - mnururisho
  - msafara na mnururisho
  
Chagua Jibu    
5. Taswira halisi hufanywa na vitu vyenye tabia ya:
  - kutupa mwanga kwenye kiwambo
  - kukusanya mwanga 
  - kutawanya mwanga
  - kuruhusu mwanga kupenya
  - kuzuia kupinda kwa mwanga
  
Chagua Jibu    
6. Mbung'o husababisha ugonjwa uitwao
  - matende
  - surua
  - kipindupindu 
  - malale
  - malaria
  
Chagua Jibu    
7. Maji magumu aushi yanaweza kubadilishwa kuwa maji laini kwa
  - kuyachemsha
  - kuyachuja 
  - kuyatonesha
  - kuyagandisha 
  - kuyapasha joto
  
Fungua Jibu 
8. Kiini cha ugonjwa kinachooneshwa katika kielelezo namba 2 kinaitwa
      |  
  | Kielelezo Na. 2 |  
  
  - bacteria
  - plasmodiamu
  - kirusi
  - amiba
  - fungi
  
Chagua Jibu    
9. Uga wa sumaku ni eneo
  - lililoko kwenye sumaku
  - ambalo unga wa chuma huonekana
  - ambalo nguvu ya sumaku hupatikana
  - linaloonesha sehemu za kaskazini na kusini za sumaku
  
Chagua Jibu    
10. Wakati wa kiangazi mimea hupukutisha majani kwa sababu ya:
  - kuruhusu majani mapya yaote
  - kukomaa sana
  - kuongeza rutuba ardhini
  - kuruhusu maua yaote 
  - kupunguza upotevu wa maji
  
Chagua Jibu    
11. Shinikizo la damu hutokana na:
  - mafuta 
  - ateri kuwa kubwa
  - kupasu a kwa vena 
  - mgandamizo wa mishipa
  - vena ku kubwa
  
Chagua Jibu    
12. Ni muhimu kuchukua tahadhari zifuatazo wakati wa vita isipokuwa:
  - kusafisha mazingira kwa kukata miti
  - kujenga nyumba imara 
  - kuhifadhi chakula
  - kuchimba mahandaki 
  - kuhamia mahali pengine
  
Chagua Jibu    
13. Mlo kamili ni ule wenye mchanganyiko ufuatao:
  - muhogo, maharage, mayai, maziwa na tunda
  - tunda, mayai, wali, karanga na nyama
  - mkate, mchicha, kunde, karanga na tunda 
  - ugali, mayai, samaki, wali na tunda
  - mchicha, karanga, mayai, maharage na tunda.
  
Chagua Jibu    
14. Sayari hutofautiana na nyota kwasababu sayari:
  - ni kubwa kuliko nyota 
  - zina mwanga wa asili
  - zipo katika hali ya gesi 
  - hazizunguki jua
  - huzungukwa na mwezi au miezi
  
Chagua Jibu    
15. Ulinganifu wa rula inayooneshwa katika kelelezo namba 3 utapatikana tu iwapo uzito wa P utakuwa gm .
      |  
  | Kielelezo 3 |  
  
  - 46
  - 16
  - 10 
  - 40 
  - 24
  
Chagua Jibu    
16. Watu wanaofanya mazoezi ya viungo wanapaswa kula chakula chenye wingi wa:
  - protini
  - kabohaidreti
  - vitamin D 
  - vitamini C 
  - madini
  
Chagua Jibu    
17. Herufi J katika kielelezo namba 4 inawakilisha mshipa unaotoa damu kutoka kwenye moyo unaoitwa:
      |  
  | Kielelezo Na. 4 |  
  
  - venakava
  - auriko
  - ventriko
  - vena
  - aorta
  
Chagua Jibu    
18. Roda aina ya abedari na kamba husahilisha kazi zaidi kwasababu:
  - nguvu nyingi hutokana na mashine yenyewe
  - huongeza nusu ya nguvu ya kubebea mzigo
  - husaidia kubadili uelekeo wa nguvu
  - wingi wa kamba huongeza msuguano
  -  mzigo hufungwa mwisho
  
Fungua Jibu 
19. Nyakati za joto kali, si vema kuvaa nguo nyeusi kwasababu nguo hizo:
  - huakisi mwanga 
  - hukinga joto
  - huakisi joto
  - husharabu joto 
  - hupindisha nuru.
  
Chagua Jibu    
20. Kitumi cha umeme kinachobadili mkondogeu wa umeme kuwa mkondo mnyofu huitwa:
  - rektifaya 
  - transista
  - amplifaya
  - resista. 
  - transfoma
  
Chagua Jibu    
        BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB  
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA   
Try Another Test |