STD VII MAARIFA_JAMII ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2016

2016 - MAARIFA YA JAMII

SEHEMU A

Chagua jibu herufiyake kwenye karatariya

1.         Katibu kata anachaguliwa na:

  1.  Wanachama wa chama tawala
  2.   Mkutano mkuu wa kata
  3.  Wananchi wa kata ile
  4.   Mkutano wa kijiji wa mwaka 
  5.  Kamati ya kijiji
Chagua Jibu


2.         Kamati ya maendeleo ya kata inaundwa na wafuatao isipokuwa:

  1.   Katibu kata
  2.   Afisa mtendaji wa Kata
  3.   Katibu Kata wa viti maalumu
  4.   Afisa mtendaji wa Mkoa
  5.   Kamanda wa Polisi wa Mkoa
Chagua Jibu


3.         Mwakilishi wa Rais katika ngazi ya mkoa ni:

  1.  Katibu tawala wa Mkoa
  2.  Mkurugenzi mtendaji wa manispaa
  3.  Mkuu wa Mkoa
  4.  Afisa mtendaji wa Mkoa
  5.  kamanda wa Polisi wa mkoa
Chagua Jibu


4.         Kauli mbiu ya Tanzania iliyopo kwenye nembo ya taifa ni:

  1.  uhuru na maendeleo
  2.  uhuru na kazi
  3. uhuru na umoja 
  4.  uhuru na amani
  5. umoja na amani
Chagua Jibu


5.          Wimbo wa taifa una beti ngapi?

  1.  Tatu 
  2.  Mbili  
  3.  Nne   
  4.  Tano 
  5.  Sita
Chagua Jibu


6.   Mambo yote ambayo watu wote wanastahili bila ya kujali kabila, utaifa au jinsia ya huitwa:

  1. utawala bora
  2. haki za binadamu
  3. utawala wa sheria
  4. demokrasia
  5. usawa wa kijinsia
Chagua Jibu


7.   Ushiriki wa wanafunzi kwenye kuchagua viongozi wao shuleni huimarisha:

  1.  uongozi wa kikatiba shuleni
  2.  kiongozi mkuu wa uongozi wa shule
  3.  ukiritimba shuleni
  4.  usalama shuleni
  5.  uongozi bora shuleni
Chagua Jibu


8.    Tume ya Haki za Binadamu na utawala bora ilianzishwa Tanzania mwaka:

  1.   2005        
  2.  1995 
  3.  1992    
  4. 2001 
  5.  1977
Chagua Jibu


9.    Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa ni:

  1.  Kamanda wa Polisi wa Mkoa
  2.  Katibu Tawala wa mkoa
  3.  Afisa Usalama wa Mkoa
  4.  Afisa Upelelezi wa makosa ya jinai wa Mkoa
  5.  Mkuu wa Mkoa
Chagua Jibu


10.  Umuhimu wa kivuko cha pundamilia ni:

  1.  kupunguza msongamano wa magari barabarani
  2.  kuwezesha walemavu kuvuka barabara kwa usalama
  3.  kuwezesha watembea kwa miguu kuvuka barabara kwa usalama
  4.  kutoa ishara ya kuwepo kwa mifugo karibu na barabara 
  5.  kuashiria uwepo wa reli karibu na barabara
Chagua Jibu


11. Uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania ni:

  1.   kilimo
  2.   ujasiriamali 
  3.  biashara
  4.  utandawazi 
  5.  madini
Chagua Jibu


12.  Ujumla wa taratibu za maisha ya kila siku ya mwanadamu huitwa:

  1.    mila 
  2.  desturi
  3.  sanaa
  4.  utamaduni
  5. kazi za mikono
Chagua Jibu


13. Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania huchaguliwa na:

  1.  wananchi 
  2.  wabunge
  3.  mawaziri 
  4.  madiwani 
  5.  Jaji Mkuu
Chagua Jibu


14.  Wajumbe wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ni:

  1.  Marekani, Uingereza, Ufaransa, Urusi na China
  2.  Marekani, Uingereza, Ujerumani, Urusi na China
  3.  Marekani, Uingereza, Ufaransa, Urusi na Italia
  4.  Marekani, Uingereza, Urusi, Kanada na Ujerumani
  5.  Marekani, Uingereza, Urusi, Japani na Ujerumani
Chagua Jibu


SEHEMU B

HISTORIA

Chagua jibu herufi yake kwenye karatariya

15. Chimbuko la familia ni:

  1. babu na bibi
  2. baba na mama
  3.  shangazi na mjomba
  4. watoto na wazazi
  5. kaka na dada
Chagua Jibu


16.  Kiongozi mkuu wa shule ni:

  1. mwalimu mkuu msaidizi
  2. mwalimu wa taaluma
  3. kiranja mkuu
  4. mwalimu mkuu
  5. mwalimu wa nidhamu 
Chagua Jibu


17. Nini faida ya mgawanyo wa kazi katika familia?

  1. Hudhoofisha familia
  2. Huchochea utengano
  3. Huleta udikteta
  4. Huleta maendeleo
  5. Huleta mitafaruku
Chagua Jibu


18. Moto uligunduliwa katika:

  1. Zama za Mawe za Kale 
  2. Zama za Mawe za Kati
  3. Zama za Chuma
  4. Zama za Mawe za Mwisho
  5. Zama za Viwanda 
Chagua Jibu


19. Uchoraji wa wanyama katika mapango ulianza kufanywa na binadamu katika:

  1. Zama za Chuma  
  2. Zama za Mawe za Kati
  3. Zama za Mawe za Kale  
  4. Zama za Mawe za Mwisho
  5. Zama za Mavve za Mwanzo
Chagua Jibu


20.     Mabaki ya Zinjanthropus yaliyopatikana katika bonde la Olduvai mwaka 1959 yaligunduliwa na:

  1. David Livingstone    
  2. Fredrick Lugard
  3.  Louis Leakey
  4. Carl Peters
  5. Charles Darwin
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256