KISWAHILI 2011
SEHEMU A
SARUFI
Katika swali la (1 - 20) andika herufi ya jibu sahihi katika karatasi yako ya kujibia.
1. Neno "jenga" likinyumbulishwa katika kauli ya kutendeka litakuwa neno lipi?
2. Neno "wamewalisha" linadokeza hali gani ya kitenzi?
3. "Yeye hupenda sana kusoma Kiswahili". Katika sentensi hii ni neno lipi limetumika kama kiwakilishi?
4. Katika sentensi zifuatazo ni ipi ipo katika hali ya mazoea
3. Sara alimwambia Heri kwamba hakusafiri bali alikuwepo pale pale. Kauli halisi itakuwa ipi?
6. "Alikuwa anajibu kihuni". Neno "kihuni" limetumika kama aina gani ya neno?
7. "Mtu anayetaka msaada wa aina nitampa". Neno linalofaa kukamilisha tungo hiyo ni lipi?
8. "Wanafunzi wanaendelea kusoma Kiswahili ingawa hawana mwalimu". Neno "wanaendelea" limetumika kama aina gani ya kitenzi?
9. Mahali pale panatisha. Neno "pale" ni aina gani ya neno
10. "Kinyonga anatembea". Ukanushi wa sentensi hii ni upi?
11. "Mama anapika lakini baba abapangamawe". Neno lakini limetumika kama aina gani ya neno?
12. "Kiburi si maungwana". Neno "si" limetumika kama aina gani ya kitenzi
13. "Baba yangu ni mwenyekiti wa lopp". Neno "mwenyekiti ni nomino ya aina gani?
14. Wingi wa neno chuma ni upi kati ya maneno yafuatayo?
15. "Wanafunzi walitumiana salamu". Sentensi hii ipo katika kauli gani?
16. Kinyume cha neno "elea" ni kipi?
17. "Huyu mwanangu mpendwa". Neno lipi ni sahihi iii kukamilisha sentensi hiyo.
18. "Mbwa ameonekana". Neno lipi ni sahihi kukamilisha tungo hiyo?
19. Hall ya kuwa na fedha au mall nyingi huitwaje?
20. Ni sentensi ipi inawakilisha kauli ya kutendwa?
SEHEMU B
LUGHA VA KIFASIH1
21. "Uzi mwembamba unafunga dume kubwa". Kitendawili hiki kina maana gani?
22. "Usisahau ubaharia kwa sababu ya unahodha". Methali ambayo ina uhusiano na hii ni ipi kati ya hizi zifuatazo?
23. "Watoto wangu wote wamevaa hirizi nyeupe" Kitendawili hiki kina maana gani
24. Hali ya kumfanya mtu atii kila analoambiwa ina maana sawa na nahau ipi kati ya zifuatazo?
25. Ni muhimu kwa kila mtu kuwa mwangalifu kwa wanaojitangazia kutibu kisukari. Ni usemi upi kati ya ifuatayo ina maana sawa na "kuwa mwangalifu"?
26. "Mambo mema na mabaya hayafungamani", kifungu hiki cha maneno kinatoa maana ya methali ipi kati ya zifuatazo?
27. Tegua kitendawili kisemacho "Gari langu halitumii mafuta ya waarabu"
28. "Umejuaje kuwa mimi ni mgeni hapa?" methali ipi kati ya zifuatazo inawajibu swali hilo?
29. Juma alipumzika chini ya mti, alipoulizwa anafanya nini pale alijibu kuwa, "Navinjari to mwalimu". Jibu sahihi alilotakiwa kutoa ni lipi?
30. "Babu kafa kaniachia pete". Kitendawili hiki kina maana gani?
SEHEMU C
UFAHAMU
Soma kwa makini habari ifuatayo kisha jibu maswali 31 - 40 kwa kuchagua herufi ya jibu lililo sahihi na kuandika katika karatasiyakoya kujibia.
Umewahi kusikia viumbe wanaoitwa dinozo? Hawa ni wanyama ambao walikuwepo duniani zaidi ya miaka milioni 65 iliyopita. Wanasayansi wamegundua mabaki ya mafuvu na mifupa yao ardhini. Wanasayansi wamechunguza sana sababu za kutokomea kwa dinozo. Mpaka leo hii haijapatikana sababu rasmi ya tukio hilo. Hata hivyo, bado uchunguzi unaendelea kufanywa katika kutafuta sababu za kupotea kwa wanyama hao.
Tanzania ni miongoni mwa nchi chache duniani zenye wanyama wa aina nyingi. Watalii wengi kutoka kila pembe ya dunia huja kuwaangalia wanyama hawa. Hali hiyo huongeza pato Ia taifa.
Aidha, vitendo mbalimbali vinahatarisha usalama wa viumbe hao; kwa mfano makazi ya wanyama yanaharibiwa kwa kuchomwa misitu na kukata miti ovyo. Hali hii husababisha misitu kubaki vichaka tu, hivyo wanyama hukosa makazi na mwishowe hupotea. Vile vile binadamu huwinda wanyama kama tembo kwa ajili ya pembe zao.
Sasa umefika wakati kwa kila mmoja wetu kukemea vitendo hivi. Wanyama na mimea ni urithi wa taifa letu. Ni fahari iliyoje kwetu kuwa navyo. Tusipokuwa waangalifu wanyama hao na mimea adimu kama mianzi vitatoweka kabisa. Vizazi vijavyo vitabaki kusimuliwa kama tunavyosikia kuhusu dinozo.
MASWALI
31. Dinozo ni wanyama wenye sifa ipi kati ya hizi zifuatazo?
32. Kwa kuzingatia habari uliyosoma mambo mawili yanayoathiri ustawi wa wanyama ni yepi?
33. Sababu kubwa ya watu kuwinda na kuwaua ndovu ni ipi?
34. Kutokana na habari hii ni sababu ipi inayowafanya watalii kuja Tanzania?
35. Tanzania hupata faida gani kubwa kutokana na sekta ya utalii?
36. Mwandishi anatoa wito gani kwa jamii kuhusiana na usalama wa viumbe hai?
37. Athari zipi zinapatikana kutokana na kuchoma misitu?
38. Mwandishi anadai kuwa fahari ya taifa letu bi kuwa na vitu gani?
39. Kuna tofauti gani kati ya msitu na kichaka?
40. Kwa ujumla habari hii inahusu nini?
SEHEMU D
USHAIRI
Soma shairi lifuatalo kisha jibu maswali 41 - 46 kwa kuandika herufi ya jibu lililo sahihi katika karatasi ya kujibia.
Kasimama kizimbani, popo anatetemeka,
Kuitwa mahakamani, popo kujibu shitaka,
Atakiwa abaini, kwa ulimi kutamka,
Ajitetee bayana, ni mnyama au ndege.
Hakimu nashukuru, shitaka kunisomea,
Sina jadi na kunguru, ila na Pundamilia,
Mimi ni mnyama huru, amini ninakwambia,
Tukidaiwa ushuru, kwa wanyama nalipia.
Ni kweli popo napaa, na mabawa nimepata,
Lakini mimi nazaa, hilo halina utata
Kuwa ndege nakataa, sina undugu na bata
Nakataa katakata, mimi si ndege nasema.
Hakimu nathibitisha, kwa moyo wangu thabiti,
Nazaa na kunyonyesha, vipi niwe msaliti,
Wale wanaopotosha, niwaonyeshe matiti,
Hakimu simama kati, nipatie kaki.
MASWALI
41. Popo anakataa kuwa si ndege kwa sababu gani?
42. Katika ubeti wa pill popo anasema "sina jadi na kunguru", usemi "sina jadi" una maana gani?
43. Popo alitakiwa kujitetea bayana. Usemi "Kujitetea bayana" una maana gani?
44. Mstari wa mwisho katika kila ubeti wa shairi hill huitwaje?
45. "Kitendo cha kuzaa na kunyonyesha hufanywa na viumbe ambao ni " Neno linalokamilisha sentensi hiyo ni lipi?
46. Kichwa cha shairi hill chafaa kiwe kipi?
SEHEMU E
UTUNGAJI
Umepewa habari yenye sentensi nne (4) zilizoaandikwa bila mtiririko sahihi wa mawazo katika swali la 47 - 50. Zipange sentensi hizo iii ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi A, B, C, na D.
47. Alipomaliza kusema hayo Mzee komba akauliza, "Tupande miti wakati inaota kwa uwezo wa Mungu?"
Chagua Jibu48. Mkutano ulipomalizika kila mtu alirejea nyumbani kwake akiwa na dhamira ya kupanda miti.
Chagua Jibu49. Bwana miti akasema "Yapasa kupanda miti kwa sababu matumizi yake yameongezeka sana siku hizi".
Chagua Jibu50. "Tusipopanda miti mipya tutaishiwa miti kabisa". Bwana miti alijibu.
Chagua Jibu