KISWAHILI 2010
SEHEMU A
SARUFI
Katika swali la 1-5 andika herufiya jibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia.
1. "Ukitaka cha mvunguni inama". Hii ni sentensi ya aina gani?
2. Katika neno "hatutakamilisha", kiambishi kinachoonesha nafsi ni kipi?
3. "Kampeni ya upandaji miti wilayani Kishapu ilifanikiwa sana na wananchi." Sentensi hii ipo katika kauli gani?
4. Kisawe cha neno "beseni" ni kipi?
5. Wingi wa sentensi isemayo, "Ubao umetumika" ni ipi?
6. Katika sentensi ifuatayo, ni neno lipi limetumika kama kiwakilishi? "Huu ni wa maziwa."
7. Ubegete ameshinda kondeni akiamia ndege. Kielezi katika sentensi hii ni kipi?
8. Mwalimu alikuwa anatunga mtihani. N eno "anatunga" limetumika kama aina ipi ya kitenzi?
9. Alfajiri na mapema tuliondoka ukumbini. Mzizi katika neno lililopigiwa mstari ni upi?
10. Kinyume cha neno "Tandika" ni kipi?
11. Umoja wa sentensi "Machungwa mabichi yana ladha ya uchachu” ni...
12. Fundi atengenezaye herein, pete an mikufu huitwaje?
13. "Zena amemnunulia mwanae kizibao” limetumika kwa maana ipi?
14. Neno "kindumbwendumbwe” lina silabi ngapi?
15. Watalii wengi hufika Tanzania ili .mlima Kilimanjaro. Ni neno lipi linalokosekana kukamilisha sentensi hiyo?
SEHEMU B
MSAMIATI
Katika swali la 16 - 25 andika herufiyajibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia.
16. Baada ya mshenga kutoa wageni waliondoka na kurudi makwao. Chagua neno sahihi kati ya maneno yafuatayo ili ukamilishe sentensi hiyo.
17. Neno "msimu” lina maana gani?
18. Yule bwana amelima kwa bidii na amevuna . . mwingi sana.
19. Kisawe cha neno ”hitimisho” ni kipi?
20. Katika vifungu vya maneno vifuatavyo ni kifungu kipi chenye maneno yanayoshabihiana?
21. Kinyume cha neno "shaibu" ni kipi?
22. Ng'ombe dume aliyeachishwa ambaye hutumika kwa kufanya kazi kama vile kuvuta mkokoteni au plau huitwaje?
23. "Mfanyabiashara alipatwa na nuksi kubwa baada ya bidhaa zake kuungua moto". Ni neno lipi linalandana na neno "nuksi" kati ya yafuatayo?
24. Kisawe cha neno "runinga" ni kipi?
25. Kinyume cha neno "kunyanyapaa" ni kipi?
SEHEMU C
METHALI, NAHAU NA VITENDAWILI
Katika swali la 26 - 30 Andika herufiyajibu lililo sahihi katika karatasi yakoya kujibia.
26. Wanafunzi wa darasa la tano wanafanya kazi zote bega kwa bega. Neno lililopigiwa mstari lina maana gani?
27. Kifungu cha maneno kisemacho, "Anayefanya juhudi katika masomo au jambo Iolote hufanikiwa" kinashabihiana na methali ipi kati ya zifuatazo?
28. Baada ya John kupanda cheo, alimtilia Sara kitumbua chake mchanga. Maana ya msemo "kutilia kitumbua mchanga" ni upi?
29. Wanafunzi wa darasa Ia saba wamesoma kwa makini hadi wamehitimu masomo yao. Ni methali ipi kati ya zifuatazo inasadifu sentensi hiyo?
30. "Mwana wa ndugu kirungu, mjukuu mwanangwa." Methali ambayo haifanani na mehtali hii kati ya hizi zifuatazo ni ipi?
31. Kifungu kipi cha maneno kinakamilisha methali ifuatayo? "Ikiwa kilemba kimelowa..."
32. Aisatu hujulikana sana kwa "majina ya lakabu". "Majina ya lakabu" maana yake ni ipi?
33. Binetuu anawachukua wazazi wake. "Kuwachukua" lina maana gani?
34. Mama Chakupewa alipotokeza tu sebuleni, wapangaji wenzake wote yyaliangua-kichelo Msemo uliopigiwa mstari una maana gani?
35. Kasanga alitegewa kitendawili na babu yake na akakitegua kwa kusema "Mwangwi". Kitendawili hicho ni kipi?
SEHEMU D
UFAHAMU
Soma kwa makini kifungu cha habari kifuatacho kashajibu swali la 36 - 45 kwa kuandika herufi yajibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia.
Hapo kale watu walikuwa wakila vyakula vibichi. Kadri miaka ilivyokwenda mbele watu igundua matumizi ya moto kwa njia ya kupekecha vijiti. Ugunduzi huu uliwasaidia kuanza kuchoma nyama na kupika vyakula.
Kadri miaka ilivyoendelea ndivyo maendeleo yalivyopatikana. Baada ya watu kupata moto kwa kupekecha vijiti, waligundua pia njia nyingine. Njia iliyotumiwa na watu wengi ni ile ya kutumia viberiti. Hivyo waliweza kutumia majiko ya aina mbalimbali kama jiko la mafuta ya taa, jiko la mkaa, jiko la gesi na waliweza kupika kwa kutumia kuni.
Kazi ya kupika ilikuwa rahisi baada ya ugunduzi huu, walianza kula vyakula vya mchanganyiko. Walitambua kwamba vyakula vinavyopikwa kwa mchanganyiko kama mseto na vinginevyo vina manufaa makubwa. Vyakula hivi hujulikana kama mlo kamili. MIO kamili huimarisha siha ya mlaji.
Matumizi ya viberiti hayakuishia katika kuwasha majiko. Viberiti hadi leo vinatumika kuwashia kandili, karabai, vibatari na mishumaa ili kuweza kupata mwanga katika nyumba zetu. Tunatumia viberiti kupata moto tunaoutumia kuchoma mabiwi na takataka nyingine ili kuondoa uchafu katika mazingira yetu.
Moto pia huweza kupatikana kwa njia ya umeme ambao aghalabu hutumika katika sehemu za miji. Ugunduzi wa umeme umesaidia katika shughuli za upishi. Huwawezesha akina mama kupika vyakula kwa kutumia majiko ya umeme. Hupika vyakula vingi kwa urahisi na kwa haraka zaidi. Hali hii imeleta uwezekano wa kupika vyakula vya mchanganyiko yaani mlo kamili. Vyakula hivi huwa na mchanganyiko wote, yaani vyakula vinavyotia nguvu na joto mwilini, vyakula vya kulinda mwili na kujenga mwili. Watu walao mlo kamili kwa nadra huwa goigoi.
Moto pia huweza kupatikana kwa kutumia lensi, kwani lensi ikielekezwa kwenye mwanga wa jua kwa muda mrefu basi karatasi itakayowekwa chini yake hushika moto.
Faida za moto ni nyingi. Hutupa mwanga wakati wa usiku, hutumika katika kuendesha mashine na mitambo mbalimbali. Kama moto usingegunduliwa, maisha ya watu yangekuwa duni.
Aidha, moto una madhara mbalimbali usipotumika vema. Madhara haya hutukumbusha kwamba "uzuri wa mkakasi, ndani kipande cha mti". Athari zake ni kama kuunguza majengo na mitambo, majengo yanapoungua wakati mwingine husababisha maafa ya watu kuungulia ndani ya majengo na mali zao.
Kuepuka madhara na hasara zitokanazo na moto hatuna budi kuwa waangalifu. Tuweke viberiti, mishumaa na taa mbali na watoto; tuunganishe nyaya za umeme kwa kutumia wataalamu, warina asali kufuata njia za kisasa kwa kutumia mavazi ya kitaalamu, kulima kwa kuepuka kuchoma mapori na mashamba. Tusipochukua tahadhari hiyo tutajuta, kwani "Hamna! Hamna! Ndimo mliwamo".
MASWALI
36. Kichwa cha habari hapo juu ni kipi?
37. Neno "Mseto" lina maana sawa na kifungu kipi cha maneno kati ya vifuatavyo?
38. "Watu walao mlo kamili kwa nadra huwa goigoi". Sentensi hii ina maana ipi?
39. "Hamna! Hamna! Ndimo mliwamo". Methali hii ina maana gani?
40. Neno "siha" kama lilivyotumika katika kifungu cha habari Ilina maana gani?
41. Kwanini watu wa kale walikula vyakula vibichi?
42. MIO kamili huwa na mchanganyiko wa vyakula vyenye virutubisho mwilini. Vyakula hivyo ni vipi?
43. Moto una faida nyingi katika maisha ya kila siku. Taja faida tatu za moto.
44. kama ilivyotumiwa na mwandishi, methali inayosema "Uzuri wa mkakasi ndani kipande cha mti" ina maana gani?
45. Madhara yasababishwayo na moto kama yalivyoelezwa kwenye kifungu cha habari ni yapi?
SEHEMU E
UTUNGAJI
Umepewa insha yenye sentesi tano (5) zilizoandikwa bila mtiririko sahihi wa mawazo. Zipange sentensi hizi ili ziwe na mtiririko wenye mantiki kwa kuzipa herufi A, B, C, D na E ili ujibu maswali 46 - 50.
46. Ili mpate kuyajua ni lazima mjifunze kwa bidii na maarifa muweze kufaulu mitihani yenu.
Chagua Jibu47. Ninyi ni vijana wadogo bado wenye matumaini ya kupata maendeleo katika maisha yenu ya baadaye.
Chagua Jibu48. Endeleeni kusoma na kujifunza kwa bidii kwani Elimu ni bahari, haina mwisho.
Chagua Jibu49. Elimu ndiyo itakayoweza kuwafungulia njia za kupata maendeleo hayo, katika safari hii ya kuelimika zaidi.
Chagua Jibu50. Katika safari hiyo ya kuelimika zaidi, utagundua kuwa yapo mambo mengi muhimu ambayo hamyajui.
Chagua Jibu