STD VII KISWAHILI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2006

KISWAHILI 2006

SEHEMU A

SARUFI

Katika swali la 1-15 andika herufi yajibu lililo sahihi katika karatasiya kujibia.

1. Huyu ......... mtoto aliyekuwa amepotea.

  1. ndio 
  2. ndiyo 
  3. ndiye
  4. ndiyo
  5. ndivyo
Chagua Jibu


2. Neno lipi ni kinyume cha neno 'Adili"? .

  1. wema 
  2. uovu 
  3. ujasiri
  4. ujanja
  5. ujinga
Chagua Jibu


3. "Ala kumbe! Ameondoka leo asubuhi”. Kihisishi ni kipi kati ya maneno haya?

  1. Ala kumbe
  2. leo
  3. Ala
  4. kumbe
  5. ameondoka
Chagua Jibu


4. Kisawe cha neno shaibu ni .

  1. barabara
  2. baneti
  3. buda 
  4. ajuza 
  5. kigori
Chagua Jibu


5. Neno "MBWA” lina silabi ngapi?

  1. nne
  2. mbili
  3. moja 
  4. tatu 
  5. sifuri
Chagua Jibu


6. Kipi kinyume cha neno aghalabu? ......

  1. mara nyingi
  2. mara kwa mara
  3. nadra
  4. muda wote
  5. kila wakati
Chagua Jibu


7. Kitoto hiki kinacheza kitQtQ. Neno lililopigiwa mstari limetumika kama ...

  1. Nomino 
  2. Kitenzi 
  3. Kielezi 
  4. Kivumishi 
  5. Kielelezi
Chagua Jibu


8. Shule ile imeendelea ingawa haina umeme. Sentensi hii iko katika aina ipi ya tungo?

  1. Tungo tegemezi 
  2. Tungo sahihi
  3. Tungo shurutia 
  4. Tungo ambatano 
  5. Tungo huria
Chagua Jibu


9. Sikuweza kutambua ni nani amelala kitandani kwa sababu alijifunika shuka  . . . . . . .

  1. Lote 
  2. Gubigubi
  3. Zima
  4. Nzima 
  5. Zama
Chagua Jibu


10.Neno "Vibaya” katika sentensi isemayo "Vibaya pia vinanunuliwa” limetumika kama aina ipi ya maneno?

  1. Kivumishi 
  2. Kiwakilishi 
  3. Kielezi
  4. Kisifa 
  5. Nomino
Chagua Jibu


11. Mkutano kati ya Viongozi wa DECI na Serikali ulikuwa haujapatiwaNeno lipi linalokamilisha sentensi hii?

  1. Uchunguzi 
  2. Ufumbuzi 
  3. Ufunguzi
  4. Kutendwa
  5. Kutendea
Chagua Jibu


12. 'Salama na Samina wanapendana sana". Sentensi hii ipo katika kauli ipi?

  1. Kutendwa 
  2. Kutendana 
  3. Kutenda
  4. Kutendwa 
  5. Kutendea
Chagua Jibu


13. Katika neno "tutakuja” kiambishi cha wakati ni .........

  1. tu- 
  2. -ku 
  3. -ja-
  4. u
  5. -ta-
Chagua Jibu


14. Neno ”MWALIMU” lipo katika upatanisho wa ngeli ya aina gani?

  1. A-WA
  2. I-ZI
  3. LI-YA 
  4. U-YA
  5. U-ZI
Chagua Jibu


15. Wingi wa sentensi ifuatayo ni ipi? mti huu unaharibu mazingira

  1. Miti hizi zinaharibu mazingira
  2. Miti hiyo inaharibu mazingira
  3. Miti hii itaharibu mazingira
  4. Miti hii inaharibu mazingira
  5. Miti hii imeharibu mazingira
Chagua Jibu


SEHEMU B

MSAMIATI

16. Mzee Mwendapole aliwapa wanaemawaidha juu ya maisha ya baadaye. Neno lililopigiwa mstari lina maana gani?

  1. Hotuba 
  2. Maonyo 
  3. Urithi
  4. Mawazo 
  5. Mahubiri
Chagua Jibu


17. Neno lenye maana sawa na "mawio” ni lipi kati ya yafuatayo?

  1. Asubuhi 
  2. Maonyo
  3. Mawazo
  4. Urithi
  5. Mahubiri
Chagua Jibu


18. Mwl. Juma alinunua shati dukani. Neno lililopigiwa mstari lilmetumika kama aina gani ya maneno?

  1. Kivumishi 
  2. Kiwakilishi
  3. Kielezi 
  4. Kihisishi
Chagua Jibu


19. Mtu anayesimamia kazi za shambani anaitwaje?

  1. Kiongozi 
  2. Msimamizi
  3. Mkuu
  4. Nokoa 
  5. Mnyapara
Chagua Jibu


20. Jina analotumia mjomba kumwita mtoto wa dada yake ni:

  1. Mtoto 
  2. Mjomba
  3. Binamu
  4. Shangazi 
  5. Mpwa
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256