STD VII KISWAHILI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2005

KISWAHILI 2005

SEHEMU A

SARUFI

Katika swali 1 - 15 andika herufiyajibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia

1. Sudi na Celina "wanapigana". Neno lililopigiwa mstari liko katika kauli ipi?

  1. Kutendwa 
  2. Kutendana 
  3. Kutendewa
  4. Kutendea 
  5. Kutendeana
Chagua Jibu


2. Kamilisha sentensi ifuatayo kwa kutumia neno moja kati ya uliyopewa: "Ingawa walipata shida nyingi njiani . walifika salama

  1. hatimaye 
  2. ingawa
  3. ingawaje
  4. hivyo 
  5. hatima
Chagua Jibu


3. Sentensi isemayo, . Jumatatu tulipoanza mtihani" inakamilishwa kwa usahihi na neno lipi kati ya yafuatayo?

  1. Itakuwa 
  2. Ilikuwa
  3. Ifikapo
  4. Ifikiapo 
  5. Ilikuwepo
Chagua Jibu


4. Neno haiba lina maana sawa na neno lipi kati ya haya yafuatayo?

  1. Urembo wa mavazi 
  2. Urembo wa sura
  3. Mwenendo mwema 
  4. Amani na utulivu
  5. Uzuri na majivuno
Chagua Jibu


5. Tumia neno mojawapo kati ya haya yafuatayo ili ukamilishe sentensi isemayo "Tukitaka kupata mazao mengi ......... tutumie mbolea".

  1. ni budi 
  2. si budi 
  3. tuna budi
  4. budi. 
  5. hatuna budi
Chagua Jibu


6. Ni neno lipi linalokamilisha sentensi isemayo "Kiranja wetu wa darasa alikwenda dukani  . . . . . . . alikatazwa na mwalimu"?

  1. ila
  2. lakini 
  3. ingawa
  4. iwapo 
  5. isipokuwa
Chagua Jibu


7. "Kitabu ulichonipa kina kurasa chache". Katika sentensi hii maneno yaliyokolezwa wino yanawakilisha nini?

  1. Kishazi kitegemezi
  2. Kishazi huru
  3. Kishazi ambatano
  4. Kirai
  5. Kielezi
Chagua Jibu


8. "Kobe anatembea taratibu". Neno "taratibu" ni aina ipi ya maneno?

  1. Kivumishi 
  2. Nomino
  3. Kishazi ambatano 
  4. Kielezi
  5. Kihusishi
Chagua Jibu


9. Neno "vibaya" katika sentensi isemayo "vibaya pia vimenunuliwa" limetumika kama aina ipi ya maneno?

  1. Kivumishi 
  2. Nomino 
  3. Kiwakilishi
  4. Kielezi 
  5. Kisifa
Chagua Jibu


10. Katika sentensi: "Mama anaendesha gari," herufi a-katika neno anaendesha inawakilisha kiambishi cha aina ipi?

  1. Tendo 
  2. Rejeshi 
  3. Tamati
  4. Wakati 
  5. Nafsi
Chagua Jibu


11. Neno shule limetolewa kutoka katika lugha ipi?

  1. Kijerumani 
  2. Kihindi
  3. Kireno
  4. Kiingereza 
  5. Kiarabu
Chagua Jibu


12. Sentensi isemayo "Shangazi mkubwa alikuwa analima shambani" ni aina ipi ya sentensi?

  1. Ambatano 
  2. Sahili 
  3. Shurutia 
  4. Changamano 
  5. Ambatano — sahili
Chagua Jibu


13. Kinyume cha neno adimu ni kipi?

  1. haba 
  2. ghali 
  3. tele 
  4. rahisi 
  5. potea
Chagua Jibu


14. Sentensi isemayo "Ukinisaidia nitakusadia" ni aina ipi ya sentesi?

  1. Changamano
  2. Sahili
  3. Ambatano
  4. Shurutia
  5. Mseto
Chagua Jibu


15. "Huyu si ndugu yangu". Katika sentensi hii, neno si ni aina ipi ya maneno?

  1. Kitenzi kikuu 
  2. Kielezi jinsi 
  3. Kitenzi kisaidizi
  4. Kitenzi jina 
  5. Kielezi kivumishi
Chagua Jibu


SEHEMU B

MSAMIATI

Katika swali 16 — 25 andika herufi yajibu lililo sahihi katika karatasi yakoya kujibia.

16. Mahali panapochimbwa madini panaitwaje?

  1. Mgodini 
  2. Shimoni 
  3. Mererani
  4. Porini 
  5. Madinini
Chagua Jibu


17. "Furaha alishikwa na fadhaa alipobaini ameuziwa mali ya wizi" Neno ' fadhaa" katika sentensi hii lina maana ipi?

  1. Aibu 
  2. Mshangao 
  3. Hofu
  4. Ghadhabu 
  5. Chuki
Chagua Jibu


18. Ni kiumbe kipi kisichokuwa na uhusiano baina ya hivi vifuatavyo?

  1. Ngamia 
  2. Ng'ombe 
  3. Punda
  4. Mbuzi 
  5. Nyumbu
Chagua Jibu


19. Neno "tamati" lina maana sawa na neno lipi?

  1. Pembeni
  2. Katikati
  3. Mwisho
  4. Mwanzo
  5. Chanzo
Chagua Jibu


20. Kinyume cha neno tapanya ni kipi?

  1. Sambaza
  2. Tawanya
  3. Kusanya
  4. Eneza 
  5. Ongeza
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256